Nyaka Data

Nyaka Data pata habari mbalimbali na motomoto za bongo uswahilini apa tz

Esther wa UMISSETA na mwandishi wa TBCEsther Seme ni mmoja wa wanafunzi wanaoonyesha vipaji katika mashindano ya Umoja w...
22/06/2024

Esther wa UMISSETA na mwandishi wa TBC

Esther Seme ni mmoja wa wanafunzi wanaoonyesha vipaji katika mashindano ya Umoja wa Shule za Sekondari Tanzania (UMISSETA) yanayoendelea mkoani Tabora, yakizikutanisha timu kutoka mikoa 28 nchini.

Esther mwenye umri wa miaka 14, ni mwanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya Sekondari ya Kutwa Mbeya na anashiriki mchezo wa netiboli katika mashindano hayo.

Mwanafunzi Esther ana urefu wa futi 6.3 akiwa ni mwanafunzi wa netiboli mrefu zaidi katika mashindano hayo ya UMISSETA kwa mwaka huu.

Picha: Ni mwanafunzi Esther akifanya mahojiano na mwandishi wa Shirika la Utangazaji Tanzania (TBC), Steven Kigora.

Baada ya vijembe vizito kuendelea Mitandaoni kati ya Harmonize na Aliyekuwa Bossi wake  Basi Diamond Ameamua kumvulia ko...
29/04/2024

Baada ya vijembe vizito kuendelea Mitandaoni kati ya Harmonize na Aliyekuwa Bossi wake

Basi Diamond Ameamua kumvulia kofia baada ya Kujibiwa kuwa Hawezi kumlipa Mil 600 ya kumfanya aje kwenye Event ya Kutimiza miaka 15 kwenye Industry ya muziki

Pia mbali na hivyo Harmonize alimempa onyo Ya Kuacha kumzungumzia kwani tayari alishalipwa pesa zake ..

Basi Diamond naye amemjibu kuwa,

" Ooh..! Kumbe una dhamira ya kubishana... Mie mnyonge siwezi kubishana na wewe mtu mzito.. 😥Mataji yote nakupa chukua ushindi " ameandika Diamond platnumz

Unakipi cha kumshauri Diamond..? Dondosha comment..!


 : Inadaiwa kuwa tabia ya kuoga kila siku haina manufaa yoyote kwa afya ya binadamu, bali watu hufanya hivyo, wakihofia ...
28/04/2024

: Inadaiwa kuwa tabia ya kuoga kila siku haina manufaa yoyote kwa afya ya binadamu, bali watu hufanya hivyo, wakihofia kutengwa na jamii, kwa sababu ya kunuka.
Hoja hiyo imetetewa na wataalamu mbalimbali akiwemo Julie Russak, ambaye ni Daktari wa Ngozi, huko Manhattan, nchini Marekani ambapo ameeleza kuwa tabia ya kuoga mara kwa mara, inaweza kuondoa bakteria wa ulinzi wanaokaa kwenye ngozi ya mwanadamu.
Hoja hiyo pia iliwahi kutetewa na mtaalamu wa masuala ya Kemia Bw.David Whitlock, ambaye aliacha kuoga kwa muda wa miaka 12 na kuchagua kujipulizia marashi yenye mchanganyiko wa bakteria wa ulinzi wa ngozi, ambapo aliwaasa watu kuacha kuoga ili kuwalinda bakteria hao muhimu kwa afya ya binadamu.
Tuambie unafikiri unaweza kuishi bila kuoga na kutegemea marashi pekee k**a mbadala wa kuoga?

Kampuni ya simu za mkononi ya Infinix Mobile Tanzania imezindua rasmi toleo jipya la simu za NOTE 40 series na kutangaza...
10/04/2024

Kampuni ya simu za mkononi ya Infinix Mobile Tanzania imezindua rasmi toleo jipya la simu za NOTE 40 series na kutangaza kuwa sasa ni rasmi simu hizo zimeanza kuuzwa Nchini Tanzania.

Moja ya sifa kuu za simu hizo imetajwa kuwa ni teknolojia ya kuchaji wa haraka iitwayo All Round Fast Charge 2.0, watt 70 ambayo ina uwezo wa kuchaji kwa haraka na kufikisha asilimia 50 ndani ya muda wa dakika 16 tu ambapo pia toleo la NOTE 40 pro limekuja na teknolojia ya wireless charge yenye Watt 20 ambayo inampa Mtumiaji urahisi wa kuchaji anapokuwa mihangaikoni pasipo kutumia wire k**a kauli mbiu yao inavyosema

Infinix NOTE 40 Series imetengenezwa kwa umahiri na chip cheetax X1, chip ambayo imetengenezwa na Infinix wenyewe ili kuongeza ufanisi katika teknolojia hii ya fast charge ambapo kwa upande wa picha camera yake ni ya megapixel 108 pamoja na kuzoom kwa usaidizi wa OIS na umbo lenye muundo wa kisasa wa 3D Curved, AMOLED Display na refresh rate 120Hz.

Katika uzinduzi huo, Infinix imetangaza kuwa sasa NOTE 40 series zipo madukani Nchini Tanzania ambapo wamewaongezea Wateja wa simu hizo ofa ya GB 96 za internet kutoka Vodacom na nafasi ya kwenda nje au ndani ya Nchi kwa kutumia usafiri wa ndege ya Air Tanzania (ATCL) “tunawakaribisha Wateja wetu kutupigia simu kupitia 0656317737/ 0743558994 kwa maulizo mbalimbali”

𝐓𝐮𝐣𝐢𝐟𝐮𝐧𝐳𝐞Hapo ni Urambo Tabora na huyu ni Nyoka aina ya Koboko aliyeuliwa na wakulima. Koboko ndiyo nyoka hatari kuliko ...
31/03/2024

𝐓𝐮𝐣𝐢𝐟𝐮𝐧𝐳𝐞
Hapo ni Urambo Tabora na huyu ni Nyoka aina ya Koboko aliyeuliwa na wakulima. Koboko ndiyo nyoka hatari kuliko nyoka wote hapa duniani na hii ni kwa sababu ya mkusanyiko wa sumu kali alionao, nyoka huyu ana aina mbili za sumu ambazo hufanya kazi kwa pamoja na endapo mtu atang’wata basi ndani ya dakika 3 hadi 10 mtu huyu akikosa matibabu hupoteza maisha.

Nyoka hawa huwa na maeneo maalumu ya kung’ata ambayo ni kichwani, shingoni au kifuani kwani mara nyingi hukaa juu ya mti, na ukiwakuta chini urefu wao ni futi 16 na akiwa na hasira husimama nusu mwili wake ambapo ni sawa na futi 8.

Wataalamu wanashauri jinsi ya kumuua ni kuchemsha chungu cha maji ya moto au uji kisha kujitwika kichwani na kupita maeneo ambao wanapatikana nyoka hawa, wakitaka kung’ata katika maeneo yao huishia kudumbukia ndani ya chungu hiko chenye kimiminika cha moto, hufa.

Lakini pia nyoka huyu unaambiwa anauwezo wa kutembea mwendo kasi mkubwa sana ambapo anaweza kukimbia 23km hadi 25km ndani ya saa moja, huku binadamu wa kawaida ana uwezo wa kukimbia 12km ndani ya saa moja na endapo mnyama huyu ataamua kung’ata sehemu yenye kundi kubwa la watu basi anauwezo wa kung’ata kunzia watu/wanyama 70 nakuendelea bila kuchoka.

Hapa nchini kwetu nyoka aina hii hupatikana kwa wingi mkoani Tabora na sehemu zenye misitu mikubwa k**a vile, Iringa, Morogoro, Milima ya Udzungwa huko wapo wegi sana.

Pia nyoka aina hii hutajwa katika orodha ya wanyama wanaoongoza kuuwa watu wengi zaidi duniani.

Na unaambiwa nyoka huyu akiwa msituni hapendelei kusikia kelele au milio ya gari na mara nyingi endapo atasikia mlio wa gari hupendelea kuufuatilia mlio huo nakufanya shambulio hivyo inashauriwa kufunga vizuri vioo vya magari wakati wa kupita msituni.

Na wataalamu wanashauri kuwa endapo nyoka huyu atakuwa amejificha katika upenyo wa gari basi ni vyema dereva kukimbiza gari hilo kwa mwendo kasi usiopungua 80 na kuendelea kwa ndani ya dakika 10 hadi 15 ili kusaidia kummaliza nyoka huyo kutokana na joto kali au kumchosha nyoka huyo na kumpunguzia makali ya sumu yake ya kudhuru watu.

HATIMAYE TANZANIA YAANZA MAJARIBIO YA TRENI YA KWANZA YA UMEME AFRIKA MASHARIKI NA KATI Tanzania leo imeandika historia ...
27/02/2024

HATIMAYE TANZANIA YAANZA MAJARIBIO YA TRENI YA KWANZA YA UMEME AFRIKA MASHARIKI NA KATI

Tanzania leo imeandika historia kwa kufanya safari ya
kwanza ya majaribio ya treni ya umeme kutoka mji wa
kibiashara wa Dar es Salaam hadi mkoa jirani wa
Morogoro.

Majaribio hayo yanafuatia kukamilika kwa ujenzi wa reli ya kisasa ya kiwango cha 'Standard Gauge' kati ya
maeneo hayo mawili.

Hiyo ni treni ya kwanza inayoendeshwa kwa umeme kwenye kanda ya Afrika Mashariki na Kati.

Neno moja la pongezi kwa taifa hilo la Afrika
Mashariki.

📸: Kwa hisani ya Shirika la Reli Tanzania

Address

Morogoro

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Nyaka Data posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Nyaka Data:

Share