Kilimanjaro Revival Fm

Kilimanjaro Revival Fm Most Credible Christian Radio broadcast from Moshi-Kilimanjaro."Power Of Revival"

11/06/2026

Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro imefanikiwa kutatua zaidi ya migogoro mbalimbali 200 huku ya ardhi ikiwa ni migogoro 120.

Hayo yameelezwa leo Juni 11,2026 na Mkuu Wilaya ya Hai Hassan Bomboko wakati akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu katika Kiko cha kutoa maamuzi ya kumaliza mgogoro wa Chama Cha Ushirika Cha Lambo Estate pamoja na waliokuwa wafanyakazi wa Ushirika huo uliodumu kwa miaka ushirini na tatu.

Bomboko amesema kuwa Wilaya hiyo imekuwa na migogoro mingi na wakati anaripoti kazini mgogoro wa Lambo Estate aliukuta ukiwa na muda mrefu huku akiweka wazi kuwa mgogoro mwingine uliibuka eneo la Machine tools wakati wa ziara ya Waziri Mkuu ukihusisha watu 45 ambapo wamefanikiwa kuutafutia suluhisho.

Cc ✍️

11/06/2026

Serikali Mkoani Kilimanjaro imefanikiwa kumaliza mgogoro wa ardhi kati ya Chama Cha Ushirika Cha Lambo Estate Wilayani Hai na waliokuwa wafanyakazi wa Ushirika huo uliodumu kwa miaka ishirini na tatu.

Akizungumza Juni 11,2026 katika Kijiji Cha Lambo Estate Kata ya Machame Kaskazini kwenye kikao rasmi cha kueleza maafikiano ya mgogoro huo baada ya Mahak**a kuwapa muda wa maelewano kati ya Chama hicho Cha Ushirika pamoja na Kaya 65 za waliokuwa wafanyakazi wa Ushirika huo,Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu amewataka Wananchi hao kutoa ushirikiano wakati wa kugawiwa hekari mbili kila Kaya na kuwataka kuzitumia kujiletea maendeleo na siyo kuzalisha migogoro.

Kwa upande wake Afisa Ardhi Mkoa wa Kilimanjaro Rehema Mdee amesema kuwa Mahak**a ilitoa maelekezo ya namna ya kusimamia jambo hilo kwa kuhusisha pande zote mbili ambapo pande hizo zilikubaliana kumaliza mgogoro huo kwa kuridhia kupata hekari mbili na wao kuondoka katika eneo litakalo salia la Chama Cha Ushirika.

Hatua hiyo imefikiwa baada ya waliokuwa wafanyakazi wa Ushirika huo kumaliza muda wao na kulipwa stahiki zao ila walishindwa kurejea makwao kutokana na wengi wao kuwa ni vibarua (Manamba) kutoka sehemu mbalimbali ya Nchi,waliokuwa wanafanya kazi katika mashamba ya Mkonge wakati wa Ukoloni ambapo Serikali iliona ni busara kushrikiana na Chama hicho Cha Ushirika kuwapa hekari 2 kwa kila Kaya 65 waweze kufanya makazi.

Chama Cha Ushirika Cha Lambo Estate kilikuwa kina miliki shamba lenye ukubwa wa hekari 1308.5 ambapo aliyewahi kuwa Waziri wa Kilimo Hussein Bashe alishauri hekari 164 zigawiwe kwa Wananchi hao na zinazo baki kumilikiwa na Halmashauri ya Wilaya ya Hai ili kumaliza mgogoro huo.

10/06/2026

Katika harakati za kuhakikisha upatikanaji wa ajira unakuwepo kwa Wananchi wa Jimbo la Moshi Mjini,Mbunge wa Jimbo hilo Ibrahim Shayo amehoji Bungeni Jijini Dodoma wakati akiuliza swali la nyiongeza,kuwa ni lini Serikali itafufua viwanda vilivyokufa Mkoani Kilimanjaro ili wananchi wapate ajira.

Amesema kuwa Mji wa Moshi ulikuwa na viwanda vingi lakini kwa sasa viwanda hivyo vimekufa hali inayopelekea ukosefu wa ajira hivyo kutoaka Serikali kutoa kauli ya kufufua viwanda hivyo.

Akijibu swali hilo Waziri wa Viwanda na biashara Judith Kapinga amesema kuwa Serikali imeanza kufufua viwanda vilivyo kufa maeneo mengi ya nchi ikiwemo Moshi Mjini ambapo ni utekelezaji wa agizo la Rais Samia Suluhu Hassan .

Bei ya petroli nchini imeshuka kwa Sh29 kwa lita katika jiji la Dar es Salaam na sasa itauzwa kwa Sh4,086 kutoka Sh4,115...
03/06/2026

Bei ya petroli nchini imeshuka kwa Sh29 kwa lita katika jiji la Dar es Salaam na sasa itauzwa kwa Sh4,086 kutoka Sh4,115 iliyokuwa mwezi Mei 2026, huku bei ya dizeli ikiongezeka kwa Sh85 kwa lita baada ya kuwekewa ruzuku ya Sh534 kwa lita.

Baada ya ruzuku hiyo, dizeli inayosafirishwa kupitia Bandari ya Dar es Salaam itauzwa kwa Sh4,333 kwa lita kutoka Sh4,248 iliyokuwapo mwezi Mei 2026.

Bei hizo zimetangazwa na Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (Ewura) na zimeanza kutumika leo, Jumatano Juni 3, 2026.

Katika taarifa iliyotolewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Ewura, Gerald Maganga, mamlaka hiyo imeeleza kuwa mabadiliko ya bei za mafuta kwa mwezi Juni 2026 yamechangiwa kwa kiasi kikubwa na vita vinavyoendelea katika eneo la Mashariki ya Kati tangu Februari 28, 2026, vikihusisha Marekani, Israeli na Iran.

Maganga amesema kuwa kutokana na Tanzania kuagiza sehemu kubwa ya mafuta yake kutoka nchi za Mashariki ya Kati, mabadiliko yanayotokea katika soko la kimataifa yameendelea kuathiri moja kwa moja bei za mafuta katika soko la ndani.

01/06/2026

Hali ya taharuki,vilio na majonzi vimetawala katika Mtaa wa Matindigani, Kata ya Pasua wilayani Moshi baada ya mtoto mwenye umri wa miaka sita, Idrisa Khatibu Ramadhani, aliyekuwa akitafutwa tangu jana, kukutwa amefariki ndani ya bwawa la kufugia samaki Mei 31, 2026.

Mkaguzi Msaidizi wa Jeshi la Zimamoto na Uokoaji Mkoa wa Kilimanjaro, Philbert Beda, amesema mtoto huyo alipatikana akiwa amefariki ndani ya bwawa hilo na kwamba uchunguzi wa chanzo cha tukio unaendelea.

Baba wa marehemu, Khatibu Ramadhani, amesema familia ilikesha ikimtafuta mtoto huyo baada ya kutoweka jana jioni kabla ya taarifa za kupatikana kwake kutolewa leo asubuhi.

Baadhi ya wananchi wa eneo hilo wameeleza kuwa bwawa hilo limekuwa hatari kwa muda mrefu kutokana na kukosa uzio imara, huku wakitaka lifukiwe ili kuzuia madhara zaidi kwa watoto.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

@ Kilimanjaro revival fm
Kilimanjaro Revival Tv

26/05/2026

KUMBUKUMBU YA AJALI YA KIKAFU NA URAFIKI WA TANZANIA NA JAPAN

Pengine umewahi kusafiri katika barabara ya Moshi-Arusha eneo la Mto Kikafu Wilayani Hai Mkoa Kilimanjaro na ukaona jiwe la ukumbusho lililosimama kimya pembeni ya barabara bila kufahamu limebeba historia gani au mpaka sasa hujawahi kuona jiwe hilo na unataka kufahamu kwa undani, imekuandalia simulizi ya eneo hilo.

Jiwe hili bado linasimama k**a ishara ya historia,majonzi na mshik**ano wa kimataifa, ni ukumbusho kwamba nyuma ya kila safari ya kawaida kuna simulizi ambazo hazipaswi kusahaulika.

Wakati mwingine historia huendelea kuishi si kwa kelele....bali kwa ukimya wa kumbukumbu.

🚨MUHIMU: Picha za ajali zilizotumika katika simulizi hii siyo halisi badala yake zimetumika ili kuleta uasilia wa tukio lenyewe kwani picha za ajali hiyo ya mwaka 1985 hazijawahi kuwekwa wazi na pengine mamlaka za pande mbili Tanzania na Japan zimehifadhi.

Mwandaaji na msimulizi Devis Minja
πŸ“Ή Nuhu Suleiman

Mama Mzazi wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, Suzana Mag...
25/05/2026

Mama Mzazi wa aliyekuwa Rais wa Awamu ya Tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Hayati John Pombe Magufuli, Suzana Magufuli amefariki dunia leo Mei 25, 2026, Chato Mkoani Geita baada ya kuugua kwa muda mrefu.

Kupitia ukurasa wa Instagram, Mtoto wa Hayati Magaufuli, Jesca Magufulia amethibitisha kutokea kwa msiba huo akieleza kuwa Bibi Suzana amefariki saa 1 usiku Nyumbani kwake Chato.

β€œSiku ya Leo siku ya Juma tatu tarehe 25 May kwa majonzi makubwa na simanzi iliyotanda mioyoni mwetu tunasikitika kuwajulisha ndugu, jamaa na marafiki, na Watanzania wote kwa ujumla kuwa aliyekuwa mama mzazi wa Rais wetu mpendwa Hayati Dkt. John Pombe Magufuli amefatiki Dunia”

β€œKumpoteza mama ni pigo ambalo halina mfano, Yeye alikuwa kimbilio la wengi, chemchemi ya busara, na mwanamke aliyesimama kwa maombi na malezi yaliyotupa viongozi na watu bora katika taifa hili”

β€œPengo lake halitazibika, lakini tunamshukuru Mungu kwa miaka yote aliyotujalia kuwa naye na kwa kazi kubwa ya malezi aliyoifanya kwetu, Bwana alitoa na Bwana ametwaa Jina la Bwana lihimidiwe β€œ ameandika Jesca Magufuli Mtoto wa Hayati Magufuli, Jesca Magufuli

18/05/2026

Mwenyekiti wa Umoja wa Vijana wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Moshi Vijijini Yuvenal Shirima ambaye pia ni mhasibu na mchumi ameeleza dhamira yake ya kuwasaidia waokaji mikate na keki walioandaa matembezi ya kilomita 5 kwaajili ya watoto wenye saratani katika hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini KCMC.

Shirima ameeleza kuwa Taasisi au vikundi vilivyo shiriki tukio hilo ambavyo vimeshafikia hatua ya ukaguzi wa mahesabu atasaidia kutoa huduma hiyo huku akiwa tayari kuwapa elimu ya uchumi ili wafanye biashara kisomi.

Cc βœοΈπŸ“Ή

15/05/2026

Wanafunzi wa shule ya Msingi Mawanda iliyopo Kata ya Mwika Kusini Wilayani Moshi Mkoani Kilimanjaro wameondokana na hatari ya kupata usumbufu wa funza baada ya wadau kukarabati shule hiyo kongwe.

Akizungumza wakati alipofanya ziara shuleni hapo Mei 14,2026 Diwani wa Kata ya Mwika Kusini John Tarimo amesema kuwa shule hiyo kongwe ilikuwa na changamoto ya uchakavu hali iliyopelekea Wanafunzi kusumbuliwa na funza kutokana na vumbi.

"Nilitafuta wadau mbalimbali walioungana na mimi ili kuanza ukarabati na kazi hii umefikia asilimia 65 kwa kuziba nyufa za kuta,kuweka sakafu,kuimarisha ofisi za walimu na Mwalimu Mkuu ambapo gharama ya ukarabati huo ni kutumia Milioni 40, mhandisi wa Halmashauri amesimamia kazi hii k**a mshauri pamoja na kutumia mafundi wa ndani" alisema Tarimo

Kwa upande wake Mkuu wa Shule ya Msingi Mawanda Evarest Shirima amesema kuwa changamoto ya uchakavu wa Shule hilo kulipelekea kuwa na Wanafunzi wachache 75 kutokana na wazazi kuwapeleka watoto shule jirani Wilayani Rombo.

 : Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamsaka mtu mmoja aitwaye John Anselim Filipi kwa kosa la kumjeruhi Thomas Fili...
12/05/2026

:
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamsaka mtu mmoja aitwaye John Anselim Filipi kwa kosa la kumjeruhi Thomas Filipi Silayo (75), mkazi wa Mbomai Tarakea kwa kumkata na kitu chenye ncha kali miguuni, tumboni na mkononi.

Akizungumza na vyombo vya habari Mjini Moshi,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro (SACP) Simon Maigwa amesema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 8, 2026 majira ya mchana huko kijiji cha Wama, Kata ya Ubetu Kahe, Tarafa ya Usseri, Wilaya ya Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro ambapo mtuhumiwa huyo alimshambulia kwa kumkata na kitu chenye ncha kali baba yake mkubwa aitwaye Thomas Filipi Silayo wakati akishugulikia mgogoro wa mipaka ya shamba la familia na kupelekea majeraha makubwa kisha mhalifu huyo kukimbia kusikojulikana.

Amesema kuwa Majeruhi huyo alipatiwa huduma ya kwanza hospitali ya Wilaya ya Rombo Huruma na baadaye alikimbizwa Hospitali ya Rufaa KCMC Moshi ambako alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu Mei 9, 2026.

"Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linawasihi Wananchi kutoa taarifa zitakazosaidia kumpata mtuhumiwa huyo ili achukuliwe hatua za kisheria" alisema Kamanda Maigwa.

Address

Moshi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilimanjaro Revival Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kilimanjaro Revival Fm:

Shortcuts

Share