11/06/2026
Wilaya ya Hai Mkoani Kilimanjaro imefanikiwa kutatua zaidi ya migogoro mbalimbali 200 huku ya ardhi ikiwa ni migogoro 120.
Hayo yameelezwa leo Juni 11,2026 na Mkuu Wilaya ya Hai Hassan Bomboko wakati akitoa taarifa kwa Mkuu wa Mkoa wa Kilimanjaro Nurdin Babu katika Kiko cha kutoa maamuzi ya kumaliza mgogoro wa Chama Cha Ushirika Cha Lambo Estate pamoja na waliokuwa wafanyakazi wa Ushirika huo uliodumu kwa miaka ushirini na tatu.
Bomboko amesema kuwa Wilaya hiyo imekuwa na migogoro mingi na wakati anaripoti kazini mgogoro wa Lambo Estate aliukuta ukiwa na muda mrefu huku akiweka wazi kuwa mgogoro mwingine uliibuka eneo la Machine tools wakati wa ziara ya Waziri Mkuu ukihusisha watu 45 ambapo wamefanikiwa kuutafutia suluhisho.
Cc βοΈ