Kilimanjaro Revival Fm

Kilimanjaro Revival Fm Most Credible Christian Radio broadcast from Moshi-Kilimanjaro."Power Of Revival"

 : Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamsaka mtu mmoja aitwaye John Anselim Filipi kwa kosa la kumjeruhi Thomas Fili...
12/05/2026

:
Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linamsaka mtu mmoja aitwaye John Anselim Filipi kwa kosa la kumjeruhi Thomas Filipi Silayo (75), mkazi wa Mbomai Tarakea kwa kumkata na kitu chenye ncha kali miguuni, tumboni na mkononi.

Akizungumza na vyombo vya habari Mjini Moshi,Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kilimanjaro (SACP) Simon Maigwa amesema kuwa tukio hilo lilitokea Mei 8, 2026 majira ya mchana huko kijiji cha Wama, Kata ya Ubetu Kahe, Tarafa ya Usseri, Wilaya ya Rombo, Mkoa wa Kilimanjaro ambapo mtuhumiwa huyo alimshambulia kwa kumkata na kitu chenye ncha kali baba yake mkubwa aitwaye Thomas Filipi Silayo wakati akishugulikia mgogoro wa mipaka ya shamba la familia na kupelekea majeraha makubwa kisha mhalifu huyo kukimbia kusikojulikana.

Amesema kuwa Majeruhi huyo alipatiwa huduma ya kwanza hospitali ya Wilaya ya Rombo Huruma na baadaye alikimbizwa Hospitali ya Rufaa KCMC Moshi ambako alifariki dunia akiwa anapatiwa matibabu Mei 9, 2026.

"Jeshi la Polisi Mkoa wa Kilimanjaro linawasihi Wananchi kutoa taarifa zitakazosaidia kumpata mtuhumiwa huyo ili achukuliwe hatua za kisheria" alisema Kamanda Maigwa.

05/05/2026

Katika simulizi za mafanikio zinazobadili mtazamo wa jamii, jina la Deogratius Chami linaingia kwa uzito wake akiwa na ulemavu wa miguu, ameandika historia kwa kupanda Mlima Kilimanjaro, mlima mrefu zaidi barani Afrika wenye urefu wa mita 5,895 kwa kutumia kiti mwendo na kufanikiwa kufika kilele cha Uhuru.

Hii si mara ya kwanza, alifanya jaribio hilo mwaka 2014, lakini safari yake ya Machi 10, 2026 imebeba ujumbe mpana zaidi kwa taifa na dunia ambapo hakuweka mkazo kwenye ushindi wake binafsi pekee, bali alielekeza macho kwa jamii akisisitiza kuwa watu wenye ulemavu si kundi la kuonewa huruma bali ni watu wenye uwezo, ndoto, na mchango halisi kwa maendeleo ya jamii.

Hatua yake pia inafungua mjadala mpana kuhusu utalii jumuishi nchini Tanzania katika Sekta ya utalii, ambayo ni mhimili muhimu wa uchumi, ambapo kupitia safari hiyo, Chami ameweka wazi kuwa kuna fursa ya kupanua wigo wa utalii ili ujumuishwe zaidi kwa Watanzania na wageni kutoka nje ya nchi kwa kutoa wito wa mabadiliko kuanzia sera, miundombinu, hadi mtazamo wa kijamii.

Aida Mbilinyi Afisa mwandamizi wa biashara na masoko Benki ya Tawi la Moshi walioshiriki kufanikisha safari hiyo ameeleza kuwa Chami amevunja dhana potofu kuwa wenye ulemavu hawawezi kufanya utalii Mlima Kilimanjaro kwa kundi hilo kuwa na mawazo chanya pamoja na jamii.

Kwa upande wake Daktari Saimon Mallya kutoka Hospitali ya Rufaa ya Kanda ya Kaskazini walioshiriki kufanya maandalizi ya uhakiki wa afya ya Chami kabla ya kupanda Mlima ameeleza kuwa tukio hilo ni ushuhuda kwa walemavu wengine kuonesha uthubuti wao.

Guinness World Records
Utalii Plus Tanzania

28/04/2026

Ila CMF 😂😂😂

Usipange kukosa Tarehe 03,Mei 2026 Kilele cha sikukuuu ya Wanaume CMF katika Kanisa la Kilimanjaro Revival Temple

Actors & Imma masai

🎥









28/04/2026

Ukweli wa mambo upo hapa katika kumjua Mungu,wale watafutaji wote na wale walalamikaji wa hali ngumu ya maisha mnaweza jitafakari upya na ujumbe huu.




𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 𝐊𝐔𝐓𝐔𝐅𝐔𝐀𝐓𝐈𝐋𝐈𝐀 𝐊𝐀𝐓𝐈𝐊𝐀 𝐌𝐈𝐓𝐀𝐍𝐃𝐀𝐎 𝐘𝐄𝐓𝐔 𝐘𝐀 𝐊𝐈𝐉𝐀𝐌𝐈𝐈

@ Kilimanjaro revival fm
Youtube Kilimanjaro Revival Tv

26/04/2026
25/04/2026

Sherehe za miaka 2000's ilikuwa ni ngumu wakwena vikundi vingine vya wageni kusogea mbele pasipo burudani ya Mtumishi YESU NI BWANA Moja kati ya wimbo uliowabariki wengi hadi leo hii umebeba mafuta yake yasiyo isha.

Unakumbuka wimbo huu ukiwa wapi na ilikuwaje

23/04/2026

Mwenyekiti Mstaafu wa Chama Cha Demokrasi na Maendeleo (CHADEMA) Freeman Mbowe ameeleza kuwa yapo maisha bila siasa huku akiwataka wenye nafasi za maamuzi na madaraka kusimama katika misingi ya kuhakikisha haki inatendeka katika Taifa.

Ametoa kauli hiyo Aprili 23,2026 Kijiji cha Uduru Kata ya Machame Kaskazini Wilayani Hai wakati aliposhiriki mazishi ya Nsarye Elinikyo Mafuwe ambaye ni Mama wa Mbunge wa Jimbo la Hai Saashisha Mafuwe na kutoa salamu za rambirambi ambapo alionesha kufurahishwa na kumuona aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya.

23/04/2026

Aliyewahi kuwa Mkuu wa Wilaya ya Hai Lengai Ole Sabaya ameibuka msibani kwa Mbunge wa Hai Saashisha Mafuwe na kukiri kubadilika baada ya kupitia changamoto ya kuwekwa gerezani wakati utumishi wake.

Akizungumza leo Aprili 23,2026 katika mazishi ya Nsarye Elinikyo Mafuwe ambaye ni mama wa Mbunge wa Jimbo la Hai Saashisha Mafuwe yaliyofanyika katika Kijiji cha Uduru Kata ya Machame Kaskazini wakati akitoa salamu za rambirambi amesema kuwa kitendo cha kuwekwa gerezani kimembadilisha maisha yake.

Mazishi hayo yamehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Serikali na Taasisi binafsi na kuongozwa na Naibu Waziri Mkuu Mstaafu Dkt.Doto Biteko

23/04/2026

Rais Samia Suluhu Hassan amesema serikali itaweka utaratibu maalum wa kugharamia matibabu kwa majeruhi wa vurugu za Oktoba 29, sambamba na kuchukua hatua za kuwafariji na kuwasaidia wafanyabiashara waliopata hasara wakati wa matukio hayo, ikiwa ni sehemu ya juhudi za kurejesha hali ya kawaida ya maisha na uchumi.

23/04/2026

Mamlaka za tume ya ushindani Jumuiya ya Afrika Mashariki (EACCA)zimekutana Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro na kuwaapisha makamishina wanne kutoka Nchi za Tanzania,Somalia,Uganda na DRC ambao wata simamia mazingira mazuri ya ushindani wa biashara na walaji kwa jumuiya hiyo.

Akizungumza leo Aprili 23,2026 mara baada ya kuapishwa Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa tume ya ushindani FCC kutoka Tanzania Khadija Ngasongwa amesema kuwa watahakikisha mazingira mazuri ya biashara yanakuwepo kwa wafanyabiashara wa jumuiya hiyo pamoja na kulinda walaji wa jumuiya na kuwa linda dhidi ya mbinu potofu sokoni.

Mwenyekiti wa Jumuiya ya ushindani ya Afrika Mashariki Devid Kimei amesema kuwa Makamishina wanne wapya walioapishwa wataungana na makamishina wengine watatu na kuwa saba ambao watasaidia kutetea Wananchi wasidhulumiwe na wafanyabiashara wengine kwa kufuata Sheria za Afrika Mashariki.

Kwa upande wake Naibu Katibu Mkuu wa Jumuiya ya Afrika (EAC) Mashariki Aneth Mutaawe Semuemba anaye shughulikia masuala ya sekta za uzalishaji na miundombinu ya uchumi amewakaribisha makamishina hayo katika jumuiya hiyo nakuwakata kusimamia ushindani mzuri wa biashara kwa Jumuiya hiyo ya Afrika Mashariki ili kuweka na tija.

EACCA ni taasisi ya kikanda chini ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC) inayosimamia ushindani wa haki wa biashara katika nchi wanachama, iliyo anzishwa ili kuhakikisha kuwa soko la pamoja la Afrika Mashariki linafanya kazi bila upendeleo, udanganyifu, au ubabe wa kampuni kubwa.

23/04/2026

Mwenyekiti wa Tume ya Uchunguzi, Jaji Othman Chande, amesema kuwa kulikuwa na viashiria vya mapema vilivyoashiria uwezekano wa kutokea kwa ghasia siku ya Uchaguzi Mkuu wa Oktoba 29, zikiwa na lengo la kuzuia na kuvuruga mchakato wa uchaguzi.

Jaji Chande ameeleza kuwa dalili hizo zilianza kujitokeza kupitia mitandao ya kijamii takriban miezi sita kabla ya uchaguzi kufanyika.

Aidha, alibainisha kuwa tume hiyo iligundua viashiria vingine vya moja kwa moja, ikiwemo uwepo wa makundi ya vijana wasiopungua 500 waliokuwa wakihifadhiwa katika maeneo mbalimbali nchini, yakiwemo majengo, misitu na makambi maalum.

Kwa mujibu wa uchunguzi huo, vijana hao walikaa katika maeneo hayo kwa muda wa takriban siku 28, ambapo walidaiwa kupatiwa mafunzo maalum kwa lengo la kushiriki katika vitendo vya ghasia siku ya uchaguzi.

Address

Moshi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilimanjaro Revival Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kilimanjaro Revival Fm:

Share