
10/09/2025
Chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Vunjo kinatarajia kuzindua kampeni zake rasmi Jumamosi, Septemba 13, 2025, katika Kata ya Makuyuni kwenye uwanja wa Polisi Himo.
Katika uzinduzi huo, mgombea ubunge wa jimbo hilo, Enock Koola (.koola ), atapanda jukwaani kuwasilisha sera na mikakati yake ya maendeleo kwa wananchi wa Vunjo, akieleza vipaumbele vya chama hicho katika kipindi kijacho cha uongozi.
Uzinduzi huo unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa chama, wafuasi pamoja na wananchi mbalimbali wa jimbo hilo.
βοΈ
πππππππ πππππ
πππππππ ππππππ ππππππππ ππππ ππ πππππππ
Kilimanjarorevivalfm
π» SIKILIZA KILIMANJARO REVIVAL RADIO
95.9 KILIMANJARO, ARUSHA, TANGA, MANYARA