Kilimanjaro Revival Fm

Kilimanjaro Revival Fm Most Credible Christian Radio broadcast from Moshi-Kilimanjaro."Power Of Revival"

12/12/2025

Msemaji wa M23 Lawrence Kanyuka, ametoa wito kwa wakaazi hao kurejea nyumbani bila hofu yoyote.

Waasi hao wanaodaiwa kuungwa mkono na Rwanda, wamethibitisha kuuteka kikamilifu mji huo wa kimkakati wa Uvira, Mashariki mwa Kongo, baada ya mapambano makali kati ya vikosi vyake na wanajeshi wa serikali.

Mapambano hayo mapya yalianza tangu mwanzoni mwa mwezi huu huku Marekani ikijaribu kutuliza hali katika mgogoro huo.

Cc

11/12/2025

Mamlaka ya Hali ya Hewa Tanzania (TMA), imetangaza kuanza kwa mvua zitakazoambata na radi mikoa mbalimbali nchini kuanzia leo Desemba 11 hadi 20, 2025.

Katika taarifa yake TMA inaonesha kuwepo kwa vipindi vya mvua zilizoambatana na ngurumo za radi katika maeneo ya Ziwa Victoria, Magharibi mwa nchi na nyanda za juu Kusini-Magharibi huku maeneo machache ya pwani na nyanda za juu Kaskazini-Mashariki kupata mvua kwa kiwango kidogo.

Maeneo hayo ni Kanda ya Ziwa Victoria ambapo mikoa ya Kagera, Geita, Shinyanga, Mwanza, Simiyu na Mara, kutakuwa na mvua zinazoambatana na ngurumo za radi zikitarajiwa katika maeneo machache.

Nyanda za juu Kaskazini- Mashariki (Mikoa ya Arusha, Manyara na Kilimanjaro) mvua zinatarajiwa katika maeneo machache.

Pwani ya Kaskazini (Mikoa ya Tanga, maeneo ya kaskazini mwa Morogoro, Pwani na Dar es Salaam pamoja na visiwa vya Unguja na Pemba) mvua zinatarajiwa katika maeneo machache.

11/12/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. M***a Azzan Zungu (Mb), ametangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho, Mhe. Jenista Joakim Mhagama, kilichotokea leo tarehe 11 Desemba 2025 Jijini Dodoma.

Katika taarifa hiyo, Spika Zungu amesema:
“Kwa masikitiko makubwa, naomba kutangaza kifo cha Mbunge wa Peramiho Mhe. Jenista Joakim Mhagama kilichotokea leo 11 Desemba, 2025 Jijini Dodoma. Natoa pole kwa Waheshimiwa Wabunge wote, familia ya marehemu, ndugu, jamaa na Wananchi wa Jimbo la Peramiho. Mwenyezi Mungu awape moyo wa uvumilivu na subira katika kipindi hiki kigumu.”

Aidha, Ofisi ya Bunge ikishirikiana na familia ya marehemu imesema inaendelea kuandaa mipango ya mazishi na taarifa zaidi zitatolewa mara zitakapokamilika.

Mhe. Jenista Mhagama, aliyewahi kushika nyadhifa mbalimbali serikalini, amekumbukwa k**a kiongozi mahiri, mchapakazi na mwenye kujitolea kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

“Mwenyezi Mungu ailaze roho ya marehemu mahali pema peponi. Amina,” imehitimisha taarifa hiyo.

10/12/2025

Shirika la Kimataifa la Wanahabari (IFJ), limechapisha ripoti yake ya 2025 Jumanne, likisema Waandishi wa habari 111 waliuawa walipokuwa katika majukumu yako kote ulimwenguni mwaka huu wa 2025.

Kati ya idadi hiyo, vifo 51 vilirekodiwa huko Gaza.

Wafanyakazi tisa wa vyombo vya habari waliuawa barani Afrika mwaka 2025. Kwa mara nyingine tena, Sudan ilikuwa kitovu cha mauaji ya Waandishi wa habari katika eneo hilo, na kusababisha vifo sita kati ya vifo hivyo.

Tangu mzozo nchini Sudan uanze tarehe 15 Aprili 2023, Waandishi wa habari wanaoripoti juu ya vita vya wenyewe kwa wenyewe wamekuwa wakilengwa haswa na pande zinazopigana, haswa na vikosi vya msaada wa Haraka (RSF).

Kwingineko, IFJ pia ilirekodi mauaji ya mtu mmoja nchini Msumbiji, Somalia na Zimbabwe.

Cc Voice

09/12/2025

Nini maoni yako kuhusiana na hili?

HOST &

🎥 Cc

Unaweza kupata Muendelezo kupitia Youtube Channel yetu ya Kilimanjaro Revival Tv usisahau kusubcribe kulike na kucomment

09/12/2025

Wakati Jamhuri ya Benin ikiwa chini ya mvutano baada ya jaribio la mapinduzi lilisababisha kifo cha raia mmoja, wasiwasi umeongezeka Afrika Magharibi baada ya wanajeshi kumi na mmoja wa Nigeria kuk**atwa nchini Burkina Faso.

Wanajeshi hao walikuwa ndani ya ndege ya Jeshi ya Nigeria C-130 ambayo ilitua kwa dharura huko Bobo-Dioulasso, jiji la pili kwa ukubwa nchini Burkina Faso.

Uchunguzi ulioanzishwa haraka na AES umeripoti kuthibitisha ukiukaji huo.

Muungano huo umeonya kwamba "ndege yoyote itakayojaribu kuvuka anga lake bila kibali itashughulikiwa mara moja".

‎‎Baadhi ya wadadisi wa siasa, wanaelezea tukio hili wakilihusisha na jeshi la sasa Nigeria ECOMOG lililopelekwa Jamhuri ya Benin baada ya jaribio la mapinduzi, na kuongeza uhasama kati ya ECOWAS na serikali zinazoongozwa kijeshi ikiwemo Burkina Faso, Mali, na Niger.

09/12/2025

VIDEO : Mkuu wa Mkoa wa Mwanza Said Mtanda Akitoa ufafanuzi kuhusu Video inayosambaa kwenye Mitandao ya kijamii ikionesha kundi la watu wakiandamana na kutoa malalamiko.

09/12/2025

Wakati Tanzania Bara ikisherehekea miaka 64 ya uhuru wake, Rais Samia Suluhu Hassan ametangaza msamaha kwa wafungwa 1,036 baadhi akiwapunguzia adhabu na wengine kuachiwa huru.

Kati ya wafungwa hao waliopata msamaha huo wa Rais, 22 wameachiwa huru, huku 1,014 wakipunguziwa adhabu zao na watakabaki gerezani kutumikia sehemu ya vifungo vilivyobaki.

Idadi ya wafungwa walioachiwa huru leo, Desemba 9, 2025 inafanana na ile ya waliochiwa katika msamaha wa Rais wakati wa sherehe za uhuru za mwaka jana.

Msamaha huo wa Rais kwa wafungwa, hutolewa Desemba 9, kila mwaka. Mkuu wa nchi chini ya ibara ya 45(1)(a)-(d) ya Katiba ya Tanzania, amepewa mamlaka ya kutoa msamaha kwa wafungwa.

Taarifa ya msamaha huo, imetolewa leo Jumanne, Desemba 9, 2025 na Wizara ya Mambo ya Ndani na kutiwa saini na Waziri wa wizara hiyo, George Simbachawene.

Katika taarifa hiyo, Simbachawene amesema ni matarajio ya Serikali kuwa wafungwa walioachiwa huru watajiepusha kutenda makosa ili wasirejee gerezani.

Ukurasa mpya wa maisha ya kiongozi wetu mpendwa,  Meneja wa Kilimanjaro Revival Radio, anapoingia kwenye hatua ya upendo...
08/12/2025

Ukurasa mpya wa maisha ya kiongozi wetu mpendwa, Meneja wa Kilimanjaro Revival Radio, anapoingia kwenye hatua ya upendo iliyojaa heshima na baraka.

Ndoa ni safari ya mioyo miwili kuwa kitu kimoja— safari ya kusameheana, kuombeana mema, na kushik**ana katika kila hatua ya maisha.

Tunamtakia maisha marefu ya furaha, amani na upendo usiokoma.

08/12/2025

Ujumbe wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuhusu Maadhimisho ya Sikukuu ya Uhuru

05/12/2025

Mkurugenzi wa African Agency Sports Company Limited, Joseph Msele, ameelezea kwa kina dhamira, na upekee wa tukio jipya la Kilimanjaro Classic Car Show & Adventure Trip alipokuwa akizungumza katika kipindi cha Sunset cha Kilimanjaro Revival FM.

Tukio hilo, ambalo litarindima tarehe 29–30 Desemba 2025 katika Uwanja wa Mashujaa, Moshi, limeelezwa kuwa moja ya matukio yenye mwelekeo wa kipekee katika kuunganisha utalii, urithi wa magari ya zamani, ubunifu na burudani kwa kiwango ambacho hakijawahi kushuhudiwa nchini.

Mbali na maonesho ya magari ya kale, kutakuwepo na adventure trip itakayowapa washiriki fursa ya kutembelea vivutio vya mkoa wa Kilimanjaro, ikiwemo mashamba ya kahawa, maporomoko ya maji, mandhari ya Mlima Kilimanjaro na maeneo ya utamaduni wa asili.



HOST
🎥Cc

05/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Albert Chalamila amesema pamoja na mambo mengine yanayodaiwa kuongeza chuki kwenye jamii ni pamoja na utekaji, kukosekana kwa ajira kwa vijana, wananchi kutosikilizwa, viongozi kuishi maisha ya starehe, matumizi mabovu ya raslimali za umma, matumizi ya nguvu kupita kiasi nk

Akizungumza na Wahariri wa Vyombo vya Habari jijini Dar es Salaam leo, Ijumaa Desemba 05.2025, Chalamila amesema hata wao kwa upande wa serikali (Mkoa wa Dar es Salaam) wanalaani vikali matukio hayo

"Mtu akipanga kuwa na nia ovu katika Taifa anaweza kuangalia yeye mwenyewe akaangalia hivi ni mtu gani nikimlenga jamii moja kwa moja itasema ni huyu.., jambo hili linapotokea katika mikoa yetu, ninyi mnajuwa kuwa sio jambo jepesi, hata mimi kiongozi naweza kuwa na Vyombo vya Dola lakini sio kwamba muda wote niponao"

Address

Moshi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilimanjaro Revival Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kilimanjaro Revival Fm:

Share