Kilimanjaro Revival Fm

Kilimanjaro Revival Fm Most Credible Christian Radio broadcast from Moshi-Kilimanjaro."Power Of Revival"

Chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Vunjo kinatarajia kuzindua kampeni zake rasmi Jumamosi, Septemba 13, 2025, katika Kat...
10/09/2025

Chama cha Mapinduzi (CCM) Jimbo la Vunjo kinatarajia kuzindua kampeni zake rasmi Jumamosi, Septemba 13, 2025, katika Kata ya Makuyuni kwenye uwanja wa Polisi Himo.

Katika uzinduzi huo, mgombea ubunge wa jimbo hilo, Enock Koola (.koola ), atapanda jukwaani kuwasilisha sera na mikakati yake ya maendeleo kwa wananchi wa Vunjo, akieleza vipaumbele vya chama hicho katika kipindi kijacho cha uongozi.

Uzinduzi huo unatarajiwa kuhudhuriwa na viongozi wa chama, wafuasi pamoja na wananchi mbalimbali wa jimbo hilo.

✍️

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

Kilimanjarorevivalfm

πŸ“» SIKILIZA KILIMANJARO REVIVAL RADIO
95.9 KILIMANJARO, ARUSHA, TANGA, MANYARA


Mgombea Ubunge Jimbo la Moshi Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ibrahim Shayo  amesema kuwa Jimbo hilo bado linach...
09/09/2025

Mgombea Ubunge Jimbo la Moshi Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Ibrahim Shayo amesema kuwa Jimbo hilo bado linachangamoto kadhaa zinazotakiwa kutatuliwa haraka ili kuchochea uchumi wa Wananchi.

Ametoa kauli hiyo Septemba 8,2025 Katika hotuba yake wakati akizundua kampeni zake katika Viwanja vya Mandela Kata ya Bomambuzi,Mjini Moshi Mkoani Kilimanjaro ulioongozwa na Mgeni rasmi Mjumbe wa Kamati Kuu ya Halmashauri ya CCM Taifa,Namelock Sokoine pamoja na viongozi wengine wa chama.

Katika ahadi zake amesema kuwa Jimbo la Moshi Mjini linahitaji kuwa na magari ya kisasa ya kuzoa taka, miundombinu mizuri ya barabara za lami ikiwemo taa za barabarani maeneo yenye msongamano wa magari akitolea mfano eneo la Mbuyuni,ukamilishaji wa kiwanja cha ndege Moshi ili kuchochea Utalii, viwanda vya kuchakata mazao hasa matunda pamoja na Mji wa Moshi kuwa Jiji.

"Mkimpa Mgombea Urais Dkt.Samia Suluhu Hassan kura za kutosha pamoja na mimi na Madiwani wangu wa CCM niwahakikishie tutaondoa changamoto zote kutokana na kuwa na uwezo wa kupenyeza juu hadi matokeo yatokee" alisema Shayo

Aidha aligusia suala la Stendi ya mabasi Ngangamfumuni ambayo haijakamilika kwa muda mrefu, akiahidi kushirikiana na Madiwani, Mkurugenzi wa Manispaa pamoja na Mamlaka husika kuhakikisha ujenzi wa standi hiyo unakamilika kwa wakati.
Cc ✍️

Aliyekuwa mtia nia wa nafasi ya ubunge Jimbo la Moshi Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Izack Ngowi, ameshiriki k...
08/09/2025

Aliyekuwa mtia nia wa nafasi ya ubunge Jimbo la Moshi Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Izack Ngowi, ameshiriki katika uzinduzi wa kampeni za mgombea ubunge wa jimbo hilo, Ibrahim Mohammed Shayo maarufu k**a (Ibraline)

Uzinduzi huo umefanyika Septemba 8, 2025, katika uwanja wa mpira wa Mandela, uliopo Kata ya Bomambuzi, Manispaa ya Moshi mkoani Kilimanjaro.

Ushiriki wa Izack Ngowi kwenye tukio hilo umeonyesha mshik**ano na umoja ndani ya CCM baada ya mchakato wa ndani ya chama kukamilika kwa mafanikio.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

Kilimanjarorevivalfm

πŸ“» SIKILIZA KILIMANJARO REVIVAL RADIO
95.9 KILIMANJARO, ARUSHA, TANGA, MANYARA


Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Clatous Chota Chama ameanza kazi rasmi na Singida Black Stars baada ya kusaji...
05/09/2025

Aliyekuwa kiungo mshambuliaji wa Yanga SC, Clatous Chota Chama ameanza kazi rasmi na Singida Black Stars baada ya kusajiliwa siku za hivi karibuni.

Chama mwenye umri wa miaka 34, ameungana na Khalid Aucho na Nickson Kibabage ambao kwa pamoja msimu uliopita walikuwa Yanga.

Chama anatarajiwa kucheza mchezo wa kwanza akiwa na klabu hiyo hii leo saa 10:00 jioni, ambapo Singida BS itachuana na Kenya Police kwenye michuano ya CECAFA Kagame Cup 2025.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

Kilimanjarorevivalfm

πŸ“» SIKILIZA KILIMANJARO REVIVAL RADIO
95.9 KILIMANJARO, ARUSHA, TANGA, MANYARA


Simba SC imetangaza rasmi kunasa saini ya golikipa wa timu ya taifa ya Tanzania Yakoub Suleiman kutoka klabu ya JKT Tanz...
03/09/2025

Simba SC imetangaza rasmi kunasa saini ya golikipa wa timu ya taifa ya Tanzania Yakoub Suleiman kutoka klabu ya JKT Tanzania.

Kipa huyo wa zamani wa JKU ya Zanzibar amejiunga na Simba baada ya kuitumikia JKT Tanzania kwa mwaka mmoja.

Alionesha kiwango bora akiwa na klabu hiyo na pia katika michuano ya CHAN 2024 iliyofanyika mwaka huu na kumalizika siku za hivi karibuni.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

Kilimanjarorevivalfm

πŸ“» SIKILIZA KILIMANJARO REVIVAL RADIO
95.9 KILIMANJARO, ARUSHA, TANGA, MANYARA


Simba SC imethibitisha kumsajili wa beki wa kati, Wilson Nangu (23) kutoka JKT Tanzania kwa mkataba wa miaka mitatu.Pia,...
03/09/2025

Simba SC imethibitisha kumsajili wa beki wa kati, Wilson Nangu (23) kutoka JKT Tanzania kwa mkataba wa miaka mitatu.

Pia, Nangu anamudu kucheza k**a mlinzi wa kushoto.

𝐄𝐍𝐃𝐄𝐋𝐄𝐀 πŠπ”π“π”π…π”π€π“πˆπ‹πˆπ€ πŠπ€π“πˆπŠπ€ πŒπˆπ“π€ππƒπ€πŽ π˜π„π“π” π˜π€ πŠπˆπ‰π€πŒπˆπˆ

Kilimanjarorevivalfm

πŸ“» SIKILIZA KILIMANJARO REVIVAL RADIO
95.9 KILIMANJARO, ARUSHA, TANGA, MANYARA


Serikali ya kijeshi nchini Burkina Faso imepitisha sheria inayopiga marufuku uhusiano wa kimapenzi wa jinsi moja na kuwe...
02/09/2025

Serikali ya kijeshi nchini Burkina Faso imepitisha sheria inayopiga marufuku uhusiano wa kimapenzi wa jinsi moja na kuweka adhabu ya kifungo cha hadi miaka mitano jela, hatua ambayo inaiweka nchi hiyo miongoni mwa mataifa ya Afrika yaliyoanzisha sheria kali dhidi ya uhusiano huo unaohusisha ushoga.

Kabla ya hatua hii, uhusiano huu haukuwa umeharamishwa nchini Burkina Faso, lakini hali hiyo imebadilika tangu jeshi lilipochukua madaraka miaka mitatu iliyopita kufuatia mapinduzi ya mara mbili mwaka 2022.

Kulingana na tovuti ya Africainsider, muswada huo wa sheria ulipitishwa kwa kauli moja na wabunge 71 wa bunge la mpito lisilochaguliwa na wananchi.

β€œSheria hii inaweka adhabu ya kifungo cha kati ya miaka miwili hadi mitano pamoja na faini,” amesema Waziri wa Sheria wa Burkina Faso, Edasso Rodrigue Bayala, kupitia televisheni ya taifa RTB.

Amesema kuwa raia wa kigeni watakaopatikana na makosa hayo watarudishwa makwao. Sheria hiyo pia ni sehemu ya mabadiliko mapana ya sheria za familia na uraia, na serikali imetangaza kuwa itasambazwa kwa wananchi kupitia kampeni za uhamasishaji.

Mataifa jirani yamechukua hatua k**a hiyo; Mali, ambayo pia iko chini ya utawala wa kijeshi, ilipitisha sheria ya kuharamisha ushoga mnamo Novemba 2024. Ghana na Uganda pia zimeimarisha sheria zao dhidi ya ushoga katika miaka ya karibuni licha ya ukosoaji mkubwa wa kimataifa.

Nchini Uganda, sheria iliyopitishwa hivi karibuni imeweka kipengele cha β€œushoga uliokithiri” k**a kosa la adhabu ya kifo, huku makosa ya uhusiano wa ridhaa kati ya watu wa jinsi moja yakihusisha kifungo cha maisha jela.

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Agosti 30, 2025 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uzinduzi wa matumizi...
30/08/2025

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Agosti 30, 2025 amemwakilisha Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan katika uzinduzi wa matumizi ya Nishati Safi ya Kupikia katika Magereza 129 nchini.

Uzinduzi huo umefanyika katika gereza la Karanga lililopo Moshi Mkoani Kilimanjaro kwa niaba ya magereza yote nchini.

Mpaka sasa vyanzo vya nishati mbadala vinayotumika katika magereza ni Gesi Vunde (BIOGAS), Mkaa Mbadala (Briquettes), Kuni Poa na Gesi Asilia (NATURAL GAS) na umeme.

Mheshimiwa Majaliwa amesema hatua hiyo ni ya kupongeza kwa kuwa inaunga mkono maono ya Rais Dkt. Samia ya kuhakikisha jamii yote inatumia nishati hiyo na hivyo kwa kiasi kikubwa kuondoa madhara yatokanayo na matumizi ya nishati isiyo safi.

Akizungumza wakati akitoa taarifa ya mradi huo kwa Mheshimiwa Waziri Mkuu, Msimamizi wa Kitengo cha Kilimo, Mifugo na Utunzaji wa Mazingira kutoka Jeshi la Magereza SACP Daimu Mmolosha amesema lengo la jeshi hilo ni kuhakikisha kunakuwa na chanzo zaidi ya kimoja cha nishati ili kuepukana na matumizi ya kuni ma mkaa.

Jeshi la Polisi Nchini limeeleza kuwa limesha anza kushughulikia wamiliki wa magari walioweka usajili wa namba SSH 25 30...
29/08/2025

Jeshi la Polisi Nchini limeeleza kuwa limesha anza kushughulikia wamiliki wa magari walioweka usajili wa namba SSH 25 30 kwani hazitambuliki kisheria.

Kauli hiyo imetolewa Agosti 29,2025 Jijini Dar es salaam na Msemaji wa Jeshi la Polisi Nchini David Misime wakati akijibu swali la Katibu wa Kablu ya Wanahabari Mkoa wa Kilimanjaro (MECKI) Devis Minja aliyetaka kujuwa uhalali wa namba hizo na usalama wa wananchi,katika mdahalo wa Kitaifa wa Usalama wa Waandishi wa habari.

DCP Misime amesema kuwa tayari changamoto hiyo imeshafanyiwa kazi na hazionekani tena.

"Tumesha lifanyia kazi natumaini huzioni, kwasababu hazipo katika mfumo ambao umehalalishwa,kwahiyo ukiziona tena tupe taarifa tutazirukia mara moja na sheria itachukua mkondo wake" alisema Misime.

Uwepo wa namba hizo SSH 25 30 umekuwa ukizua mjadala na baadhi ya watu kuhoji uhalali wake kutokana na kuwa mmiliki wa chombo cha moto anaweza kufanya matukio ya uvunjifu wa amani au kusababisha ajali na chombo chake kisiweze kutambulika huku namba hizo zikichafua taswira ya mtu.

Mjadala huo wa Kitaifa kuhusu Usalama wa Waandishi wa Habari umeandaliwa na UTPC pamoja na wadau wengine, umefunguliwa na Inspekta Jenerali wa Polisi,IGP Camilius Wambura katika ukumbi wa Umoja wa Mataifa Jijini Dar es salaam

Address

Moshi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kilimanjaro Revival Fm posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kilimanjaro Revival Fm:

Share