04/07/2020
"BIRD STRIKE"
Ndege kugongana na Ndege.
{Tafsiri Nyepesi}
Katika usafiri wa anga neno " " lina maana ya ndege (kiumbe) kugongana na ndege (chombo).
Hali hii inaweza kutokea wakati wa ndege kupaa, kuwa angani au kutua.
Muda mwingine hali hiyo ikitokea inaweza kupelekea ndege (chombo) kupata ajali (ingawa ni mara chache), kuharibika sehemu husika k**a pua, kupasua kioo na kujeruhi rubani, kuharibu injini, mbawa n.k
Kiwango wa uharibifu huo kinategemea kasi, ugumu wa ndege (kiumbe) na ndege (chombo), uzito wa ndege kiumbe, pembe inayokutana wakati wa kugongana n.k
Wanahisabati na fizikia wanakokotoa hali hilo kwa njia ifuatayo;
F=MA
= ร
Au kiswahili chepesi
ni sawasawa na wa kitu zidisha na yake..
(shukrani kwake kwa kujaribu kufafanua kwenye "comments")
Ndege nyingi zinaundwa na malighafi za au mchanganyiko wa maplastiki , (epoxy) ili kuifanya kuwa nyepesi.
Wepesi wa ndege ndiyo pesa yenyewe katika usafiri wa anga maana itabeba abiria wengi zaidi, mafuta, mizigo ya ziada na kwenda mbali zaidi pasipo kutumia nguvu kubwa ya injini hivyo kutumia mafuta kidogo.
Kwahiyo kitu chochote kikiwa na kasi na uzito huwa kinasababisha uharibifu pale kinapogongana na kitu kingine.
K**a risasi ingekuwa inarushwa na mkono isingeleta madhara tunayoyaona leo kwakukosa kasi, lakini inaporushwa na bunduki kasi inakuwa kubwa na madhara yake inapogongana na kitu inafanya uharibifu mkubwa.
Ikiwa kasi ya ndege k**a ni kilomita 400-900 kwa saa jumlisha na kasi ya ndege kiumbe madhara au uharibifu hutokea pale vinapokutana na kishindo/nguvu ya mgongano huo unaweza kufikia tani au zaidi kutegemea kasi na uzito.
Ndege nyingi zinaundwa kwa viwango maalumu vya kukabiliana na hali hiyo lakini si mara zote zinaweza kuhimili kishindo hasa pale kasi inapokuwa kubwa na ndege kiumbe kuwa na uzito mkubwa na ugumu.
Mfano mdogo,
Mbegu ya ubuyu inaweza kupasua kichwa vizuri tu endapo itarushwa kwa kasi inayozidi 900km/h.