Safari Media

Safari Media Safari Media is a News/Media Company
Subscribe youtube channel now
www.youtube.com/channel/UCGml3vag_bwtdS_o7lp3YpA?sub_confirmation=1

Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Francis Alfred amewaomba waendesha maghala waache kufanya kazi kwa mazoea n...
15/09/2025

Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho Tanzania (CBT) Francis Alfred amewaomba waendesha maghala waache kufanya kazi kwa mazoea na badala yake wafanye kazi kwa kuzingatia maadili na uadilifu.

Amesema hayo Septemba 12,2025 kwenye mafunzo ya usimamizi na udhibiti wa ubora wa korosho ghafi yaliyowakutanisha wadau mbalimbali wa zao hilo, kwa lengo la kuzidi kulipa thamani ambapo amewasisitiza waendesha maghala wasifanye kazi kwa mazoea.

Ameongeza kuwa ili kuendelea kubaki vinara kwenye sekta ya zao la korosho ni wajibu wa kila mtu katika kitengo chake kuhakikisha anasimamia ubora wa zao hilo, ikiwemo wasimamizi wa maghala kupokea korosho zenye ubora.

“Tunachopigania sisi hapa ni nchi, hatupiganii mtu mmoja bali maslahi ya taifa. Tukipeleka korosho yenye ubora wa hali ya juu, inamaanisha tutaendelea kupata wanunuzi wengi kupitia Tanzania, kuimarisha ushindani, bei zitapanda na wakulima watanufaika.” Amesema Alfred.

Kwa upande wake Katibu Tawala wa Wilaya ya Mtwara Wakili Richard Mwalingo, amesema serikali haitaweza kumvumilia mtu yeyote atakayehusika na kuhujumu ubora wa korosho.

Ameongeza kuwa korosho ni moja ya mazao ya kimkakati nchini Tanzania hivyo amewataka washiriki wa mafunzo hayo kuweka uzalendo mbele kwa kusimamia kanuni na maelekezo wanayopewa katika kutekeleza majukumu yao.

Aidha, ametoa maelekezo kwa washiriki kuhakikisha wanawafikishia wakulima elimu waliyoipata huku akiiahidi Bodi ya Korosho kuwa mamlaka za mkoa na wilaya ziko tayari kushirikiana ili kuhakikisha miongozo inatekelezwa kwa lengo la kufikia malengo ya uzalishaji wa tani milioni 1 ifikapo mwaka 2030.

Kwa upande wa washiriki wa mafunzo hayo ikiwemo Nyaburuma Wanjara, wamesema mafunzo hayo yamewakumbusha kusimamia kanuni ili kuhakikisha ubora wa korosho unakuwa juu na kufanya pato la taifa kuzidi kukuwa.

Mgombea Ubunge Jimbo la Songea Mjini na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema utekelezaji wa Ilani ya...
15/09/2025

Mgombea Ubunge Jimbo la Songea Mjini na Waziri wa Katiba na Sheria, Dkt. Damas Ndumbaro, amesema utekelezaji wa Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya mwaka 2020–2025 umetekelezwa kwa mafanikio makubwa katika sekta muhimu za kilimo, elimu, afya, maji na miundombinu.

Ameeleza kuwa upatikanaji wa mbolea ya ruzuku, soko la mahindi kupitia NFRA, pamoja na ukarabati wa uwanja wa ndege wa Songea ni miongoni mwa hatua zilizoboresha maisha ya wananchi na kuchochea maendeleo ya mji huo.

Akizungumza kwenye mkutano wa uzinduzi wa kampeni 14 Septemba 2025 ulifanyika katika Kata ya Lizaboni, Dkt. Ndumbaro alibainisha kuwa katika Ilani ya 2025–2030, CCM imejipanga kupeleka umeme katika kila nyumba, kuendeleza ruzuku ya mbolea, kuhakikisha ardhi yote inapimwa na wananchi wanajenga kwenye viwanja vilivyopimwa.

Vilevile, ameahidi ujenzi wa vyuo vikuu, masoko mapya ikiwemo Manzese A na B, pamoja na maghala ya kisasa ya kuhifadhia nafaka ili kuongeza thamani ya kilimo.

Katika sekta ya miundombinu, alieleza kuwa barabara za mjini Songea zitaendelezwa kwa kiwango cha lami, ikiwemo barabara za Londoni–Subira, Msamala–Mwengemshindo na Mtwara Korido, huku uwanja wa ndege ukiboreshwa kwa taa za kisasa ili kuruhusu ndege kutua usiku. Aidha, serikali itawekeza katika michezo kwa kuimarisha timu ya Songea United, hatua ambayo itakuza vipaji na kuongeza hamasa kwa vijana.

Dkt. Ndumbaro alisisitiza kuwa utekelezaji wa miradi hiyo utachochea ukuaji wa uchumi na kuipandisha hadhi Songea kuwa Jiji ndani ya kipindi cha miaka mitano ijayo. Amewaomba wananchi wa Songea Mjini kumpa ridhaa ya kuendelea kuwa Mbunge wao, akibainisha kuwa kura kwa CCM ni kura ya maendeleo, mshik**ano na mustakabali bora wa Taifa.

MTAMBO  WA GESI ASILIA WASAFIRISHWA KWENDA MTWARA KUONGEZA NGUVU YA UZALISHAJI WA UMEMEShirika la Umeme Tanzania (TANESC...
15/09/2025

MTAMBO WA GESI ASILIA WASAFIRISHWA KWENDA MTWARA KUONGEZA NGUVU YA UZALISHAJI WA UMEME

Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) limeendelea kuchukua hatua madhubuti kuhakikisha upatikanaji wa huduma ya umeme wa uhakika katika mikoa ya Mtwara na Lindi, ili kukidhi ongezeko la mahitaji ya matumizi ya umeme kutokana na ukuaji wa shughuli za kiuchumi na kijamii.

Hayo yanathibitishwa na hatua zilizochukuliwa na Shirika hilo Kusafirisha mtambo wa Kuzalisha Umeme kwa Gesi Asilia megawati 20 unaojulikana kitaalamu kwa jina la TM 2500 kutoka kituo cha Ubungo III jijini Dar es Salaam kwenda Mtwara.

Akizungumza Septemba 11, 2025 wakati wa zoezi la usafirishaji, Mhandisi wa Kituo cha Kuzalisha Umeme Mtwara II, Godfrey Matiko, alisema mtambo huo una uwezo wa kuzalisha Megawati 20, na utaunganishwa na mtambo mwingine uliopo ambao tayari unazalisha Megawati 20 na hivyo kuongeza jumla ya uzalishaji kufikia Megawati 40 kwenye Kituo cha Uzalishaji Umeme kwa Gesi Asilia kilichopo eneo la Hiyari mkoani humo.

Amesema, Umeme huo utasambazwa Mikoa ya Lindi na Mtwara ili kukidhi mahitaji ya matumizi ya umeme yanayoongezeka.

“Usafirishwaji wa mtambo huu unalenga kuongeza nguvu katika kituo cha Mtwara II, hivyo kuimarisha hali ya upatikanaji wa umeme wa uhakika kwa wananchi na wawekezaji,” alieleza Mhandisi Matiko.

Aidha, alitoa wito kwa wananchi wa mikoa ya Mtwara na Lindi kujipanga kunufaika na fursa za uwekezaji zitakazochochewa na upatikanaji wa umeme wa kutosha na wa uhakika.

Itakumbukwa kuwa mpaka sasa Mkoa wa Mtwara unauwezo wa kuzalisha umeme jumla ya megawati 50 kwa gesi asilia na uwepo wa mtambo huu mpya wa megawati 20 kutafanya uwezo wa uzalishaji umeme mkoani humo kufikia megawati 70.

✍️ Bryson Mshana

OFISI YA AG MTWARA YAFANYA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI WA KISHERIAOfisi ya Mwanasheria mkuu wa Serikali Mkoa wa Mtwara, ...
12/09/2025

OFISI YA AG MTWARA YAFANYA KIKAO CHA KAMATI YA USHAURI WA KISHERIA

Ofisi ya Mwanasheria mkuu wa Serikali Mkoa wa Mtwara, imefanya kikao cha kwanza cha Kamati ya ushauri wa kisheria, chenye lengo la kupeana majukumu na namna ya utekelezaji wake ikiwa ni pamoja na ushauri na uangalizi katika utekelezaji wa huduma za ushauri wa kisheria na Elimu ya Sheria kwa wananchi.

Kikao hicho kimefanyika katika ofisi za Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mkoa wa Mtwara, leo tarehe 12 Septemba 2025, na kufunguliwa na Wakili wa serikali Mkoa, Ofisi ya mwanasheria Mkuu wa Serikali Nunu Mangu.

Kwa mujibu wa wakili Nunu Mangu, k**ati hiyo imeundwa kwa mujibu wa Sheria ya Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali (Utekelezaji wa Majukumu, Huduma ya Ushauri wa Kisheria za Mikaoa na Wilaya, vidokezo vya Mwaka, 2024).

“Lengo kuu la k**ati hii ni kuwezesha Mawakili wa Serikali kuhakikisha utawala wa sheria unafuatwa na kutekelezwa katika Mikoa na Wilaya kwa minajili ya kupunguza migogoro ya kisheria dhidi ya serikali”

Kikao hiki cha kwanza kina umuhimu wa kipekee, kwani pamoja na kujitambulisha tunatarajia kujadili majukumu ya k**ati, kupanga mikakati ya utekelezaji, na kujenga msingi thabiti wa ushirikiano kati ya k**ati na viongozi wa serikali na wadau wengine katika kutoa ushauri, msaada wa kisheria, elimu na uelewa kwa viongozi, watumishi wa umma na umma kwa ujumla juu ya umuhimu wa kufuata sharia” ameeleza Wakili Nunu.

Amewakumbusha wajumbe wa k**ati hiyo kutimiza wajibu wao kwa kuzingatia Weledi, Uadilifu na Uzalendo mkubwa huku wakitanguliza mbele maslahi ya Mkoa na Taifa kwa ujumla kwa kuzingatia kuwa haki ni msingi wa mani, maendeleo na mshik**ano wa kijamii.

Mjumbe wa k**ati hiyo wakili wa serikali Naftal Mzava ameeleza kuwa wamejipanga vema kwenda kuwatumikia wananchi, kwa kuhakikisha kuwa wanapata msaada, ushauri na elimu ya masuala ya kisheria ili kujenga jamii iliyostawi.

“Kama ambavyo mmesikia, hiki ni kikao cha kwanza na k**ati hii inalenga kutoa usaidizi katika ofisi za serikali ili kutatua migogoro ambayo ilikuwa inawawia vigumu watendaji mbalimbali kuitatua na kupata suluhisho” amesema Mzava.

✍️ Bryson Mshana

WATUHUMIWA 13 WAKAMATWA KWA WIZI WA PEMBEJEO ZA KOROSHO Jeshi la Polisi mkoa wa Mtwara linawashikilia watuhumiwa 13 kwa ...
11/09/2025

WATUHUMIWA 13 WAKAMATWA KWA WIZI WA PEMBEJEO ZA KOROSHO

Jeshi la Polisi mkoa wa Mtwara linawashikilia watuhumiwa 13 kwa tuhuma za wizi wa pembejeo za wakulima wa korosho msimu wa 2024/2025.

Kamanda wa Polisi mkoa huo SACP Issa Sulemani amesema mnamo Agosti 29, 2025 polisi kwa kushirikiana na vyombo vingine vya dola na Bodi ya Korosho (CBT) walifanikiwa kuwanasa watuhumiwa hao wakiwemo viongozi wa vyama vya msingi (AMCOS) katika Halmashauri ya Mji Nanyamba na baadhi ya watumishi wa serikali.

Watuhumiwa wanadaiwa kugawa pembejeo kwa “wakulima hewa” na kusababisha upotevu wa pembejeo za maji lita 308 na mifuko 12 ya sulphur aina ya simba zenye thamani ya zaidi ya milioni 15.8.

Kamanda Issa amesema uchunguzi bado unaendelea na pindi utakapokamilika wote watafikishwa mahak**ani na amewaonya wananchi kutojihusisha na wizi wa pembejeo kwa kuwa jeshi la polisi na vyombo vya usalama vitachukua hatua kali.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Bodi ya Korosho (CBT) Francis Alfred amesema udanganyifu wa baadhi ya viongo.

✍️ Husna Hassan

RUVUMA YAOMBEA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUUMkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, amewaongoza vion...
11/09/2025

RUVUMA YAOMBEA AMANI KUELEKEA UCHAGUZI MKUU

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Brigedia Jenerali Ahmed Abbas Ahmed, amewaongoza viongozi Wadini, Chama na Serikali,wazee na wananchi wa Mkoa wa Ruvuma katika maombi maalum ya kuliombea Taifa la Tanzania amani kuelekea Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kifanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Akizungumza katika maombi hayo maalum yaliyofanyika katika ukumbi wa Songea Club mjini Songea sep 8,2025, Brig. Jen. Ahmed amesema uchaguzi ni tukio la kidemokrasia lakini wakati mwingine unaweza kuwa ni chanzo cha changamoto nyingi ambazo zinaweza kuharibu Taifa.

"Uchaguzi ni tukio la kidemokrasia lakini pia linaweza kuwa chanzo cha changamoto nyingi ambazo zinaweza kulipalaganyisha Taifa letu, hivyo leo hii tumesimama k**a watu wa Mungu kuombea Uchaguzi huu uwe wa amani, haki nahuru, tuombe vyombo vya uchaguzi vifanye kazi kwa weledi na uadilifu, tuombe wagombea wawe na nia njema na moyo wa kushik**ana pamoja sio Kwa matusi au rushwa au uchochezi," alisema Mkuu hiyo wa Mkoa Brigedia Jenerali Ahmed.

Awali akisoma Dua Shekhee wa Wilaya ya Songea Ibrahim Issa alisema kuwa Katika kipindi hiki cha kuelekea kwenye uchaguzi Taifa linahitaji amani na utulivu k**a chaguzi zingine zote zilizowahi kufanyika nchini hivyo ametoa rai kwa watu wote walioshiriki katika maombi hayo maalum kuwa mabalozi wa kuendelea kuhamasisha mshik**ano, upendo na umoja na si vinginevyo.

WAFANYABIASHARA WA SOKO KUU MTWARA WAOMBA UKARABATI WA CHOO UHARAKISHWEWafanyabiashara wa Soko Kuu la Mtwara wameiomba M...
11/09/2025

WAFANYABIASHARA WA SOKO KUU MTWARA WAOMBA UKARABATI WA CHOO UHARAKISHWE

Wafanyabiashara wa Soko Kuu la Mtwara wameiomba Manispaa ya Mtwara Mikindani kukamilisha haraka ukarabati wa choo cha soko hilo ili waweze kupata huduma muhimu na kufanya biashara katika mazingira bora ya kiafya.

Wakizungumza na Safari Redio, baadhi ya wafanyabiashara akiwemo Mohamedi Nangamnyake wamesema kukosekana kwa choo kinachofanya kazi sokoni humo kumesababisha wao kutumia gharama kubwa kwa vyoo binafsi vilivyopo jirani, ambapo ada ya kutumia huduma hiyo imepanda hadi shilingi 500 kutokana na uhitaji mkubwa.

Kwa upande wake Diana Othumani ameeleza kuwa mara nyingi wanapobanwa na haja hasa nyakati za usiku hulazimika kujisaidia kwenye vichochoro baada ya wamiliki wa vyoo vya kulipia kufunga huduma zao, hali inayohatarisha afya na usalama wa wafanyabiashara.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa soko hilo, Mshamu Kaisi amekiri kuwepo kwa changamoto hiyo na kufafanua kuwa uongozi wa soko uliwahi kukubaliana na wamiliki wa vyoo vya jirani kuongeza muda wa huduma hadi saa 5 usiku na kuongeza wahudumu, lakini bado tatizo halijatatuliwa kikamilifu na kuongeza kuwa tatizo hilo limesababishwa na uchakavu wa choo cha awali kilichokuwepo sokoni.

Akitoa ufafanuzi, Afisa Habari wa Manispaa ya Mtwara Mikindani, Jamadi Omary amesema soko hilo lina vyoo viwili vya muda mrefu upande wa nafaka na upande wa mkunguni hivyo katika bajeti ya mwaka 2024/2025, Manispaa imetenga zaidi ya shilingi milioni 14.8 kwa ajili ya ukarabati huo, na kwenye bajeti ya 2025/2026 imetenga shilingi milioni 2 za kumalizia kazi hiyo.

Jamadi ameongeza kuwa ukarabati mkubwa umeshakamilika na kinachosubiriwa sasa ni ufungaji wa umeme na mifumo ya maji. Kwa mujibu wa msimamizi wa mradi, choo hicho kinatarajiwa kukamilika na kuanza kutumika ifikapo Septemba 20, 2025.

Aidha, amewaomba wafanyabiashara kuvumilia kipindi hiki cha mpito na kuwaomba kuwa choo kipya kitakapokamilika wakitunze ili kiweza kudumu na wasiwe wagumu kuchangia michango midogo midogo kwa ajili ya usafi wa mara kwa mara na ulinzi.

✍️ Husna Hassan

WANANCHI WA NAMAYANGA WAOMBA KUTOBOLEWA BARABARA KUPUNGUZA USUMBUFUWakazi wa Mtaa wa Namayanga Kata ya Mtawanya Manispaa...
11/09/2025

WANANCHI WA NAMAYANGA WAOMBA KUTOBOLEWA BARABARA KUPUNGUZA USUMBUFU

Wakazi wa Mtaa wa Namayanga Kata ya Mtawanya Manispaa ya Mtwara Mikindani, wameiomba Halmashauri ya Manispaa hiyo kuwajengea barabara itakayounganisha mtaa huo na maeneo mengine.

Wakizungumza na Safari Redio wakazi hao wamesema changamoto ya kukosa barabara inawalazimu kutumia barabara moja pekee kwa kuingia na kutoka hali inayolete usumbufu mkubwa ikiwalazimu kutembea umbali mrefu kufuata huduma mbalimbali.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Mtaa wa Namayanga M***a Bakari, amekiri changamoto hiyo na kueleza kuwa ukosefu wa barabara umekuwa kikwazo kwa maendeleo ya wananchi na unasababisha gharama kubwa za usafiri.

“Leo hii ukija kutoboa barabara hapa ukaunganisha Namayanga na Naliendele utakuwa umefanya jambo bora sana kwa wananchi."Amesema M***a.

Aidha wananchi tayari walishaanza kuchonga barabara kwa kutumia majembe na walikubaliana na wamiliki wa shamba la kilimo lililopo Naliendele ili kupitisha barabara hiyo wakiamini kuwa barabara ni maendeleo kwa jamii.

Akizungumzia suala hilo, Afisa Habari wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Jamadi Omary amesema kila mwaka Halmashauri hutenga bajeti kwa ajili ya kufungua barabara mpya katika maeneo mbalimbali.

Amewataka wakazi hao kuwasilisha rasmi maombi yao kuanzia ngazi ya mtaa, kata kisha kufikishwa katika ngazi ya Halmashauri ili yafanyiwe kazi.

✍️ Husna Hassan

MTWARA DC YAZINDUA KAMPENI YA UTOAJI WA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO. Katibu Tawala wa Wilaya ya Mtwara, Wakili. Richard...
11/09/2025

MTWARA DC YAZINDUA KAMPENI YA UTOAJI WA CHANJO NA UTAMBUZI WA MIFUGO.

Katibu Tawala wa Wilaya ya Mtwara, Wakili. Richard Jackson Mwalingo amezindua rasmi zoezi la utoaji wa chanjo za ruzuku na utambuzi wa mifugo katika Halmashauri ya Wilaya ya Mtwara.

Zoezi hilo limefanyika tarehe 10 Septemba 2025, kwa kuchanja moja kwa moja na kuwatambua kwa kuwavesha Hereni N'gombe wa Kata ya Naumbu, matarajio ya Halmashauri yakiwa ni kuchanja na kutambua Ng'ombe zaidi ya 3,700 na Mbuzi zaidi ya 27,600.

Akiongea mbele ya wananchi mgeni rasmi wa zoezi hilo Wakili. Mwalingo amepongeza Serikali kwa kuchangia Chanjo hiyo kwa Asilimia 75 na Asilimia 100 kwa upande wa Hereni, ikionesha ni namna gani Serikali inavyowathamini wafugaji.

Naye Kaimu Mkuu wa Divisheni ya Kilimo, Mifugo na Uvuvi Dkt. Innocent Masawe ametoa faida ya Chanjo hiyo kuwa ni kumkinga mnyama na magonjwa na kumpunguzia mfugaji gharama za matibabu.

Aidha mfugaji atachangia Sh. 300 kwa Mbuzi na Sh. 500 kwa Ng'ombe na kwa upande wa utambuzi Serikali tayari imeshagharamia.

Dkt. Innocent ameongeza kuwa pamoja na zoezi hilo tayari zoezi la uchanjaji wa kuku na Bata limeshafanyika ambapo zaidi ya kuku elfu Sabini na Tano wamepatiwa chanjo, Asilimia 15 hawakupatiwa chanjo kwa sababu chanjo zilizoletwa zilikuwa pungufu kutokana na changamoto ya takwimu, hivyo chanjo hizo zitakuja na kukamilisha Asilimia 15 zilizobaki.

Ikumbukwe kuwa zoezi hilo linaenda sambamba na uwekaji wa hereni za kielektroniki kwa ajili ya utambuzi wa mifugo, hatua inayolenga kuimarisha ulinzi wa mifugo na kusaidia wizara kuwa na takwimu sahihi za mifugo.

✍️ Bryson Mshana

BALOZI WA URUSI NCHINI TANZANIA AFANYA ZIARA MKOANI MTWARABalozi wa Urusi nchini Tanzania, Andrey Avetisyan, amefanya zi...
09/09/2025

BALOZI WA URUSI NCHINI TANZANIA AFANYA ZIARA MKOANI MTWARA

Balozi wa Urusi nchini Tanzania, Andrey Avetisyan, amefanya ziara rasmi katika Mkoa wa Mtwara ikilenga kuimarisha uhusiano wa kibiasbara.

Katika ziara yake iliyofanyika Septemba 8, 2025 Balozi Andrey ametembelea Bodi ya Korosho Tanzania na Bandari ya Mtwara

Balozi Andrey pia amifika eneo la ujenzi wa Viwanda vya kubangulia Korosho lililopo katika kijiji cha Maranje, Halmashauri ya Mji wa Nanyamba, ambapo alikutana na viongozi wa sekta ya korosho pamoja na viongozi wa serikali za mitaa.

Akizungumza wakati wa ziara hiyo, Mkurugenzi Mkuu wa Bodi ya Korosho Tanzania, Francis Alfred, amesema serikali inaendelea kufanya jitihada za kutafuta masoko mapya ya zao la korosho, likiwemo soko la Urusi, ili kukuza zaidi sekta hiyo muhimu ya kilimo nchini.

Francis ameongeza kuwa serikali imejiwekea lengo la kuhakikisha kuwa ifikapo mwaka 2030, korosho zote zinazozalishwa zibanguliwe hapa nchini jambo litakalosaidia kuongeza thamani ya zao hilo na kuongeza ajira.

Kwa upande wake, Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala, amesema uhusiano wa Tanzania na Urusi ni wa muda mrefu, hususan katika nyanja za uwekezaji, elimu na kilimo.

Amesema serikali ya awamu ya sita chini ya Rais Samia Suluhu Hassan imetoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa maghala ya kuhifadhi korosho, hatua itakayochochea uwekezaji mkubwa zaidi mkoani humo.

✍️ Abdul Lukanga




POLISI INAFUATILIA TUKIO LA MWANAMKE ALIYEONEKANA AKIMNYWESHA MTOTO POMBEJeshi la Polisi nchini limeeleza kuwa linafuati...
06/09/2025

POLISI INAFUATILIA TUKIO LA MWANAMKE ALIYEONEKANA AKIMNYWESHA MTOTO POMBE

Jeshi la Polisi nchini limeeleza kuwa linafuatilia tukioa la Mwanamke mmoja ambaye ameonekana kwenye picha yake ikisambaa akimnywesha mtoto mdogo pombe jambo ambalo ni ukatili kinyume cha sheria za nchi.

Taarifa iyotolewa leo tarehe 6 Septemba na Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini Naibu Kamishna wa Polisi(DCP) David Misime, imesema kuwa ufuatiliaji wa kina umeshaanza ili kujua k**a kujua k**a tukio hilo limetokea ndani ya nchi ili kuweza kumpata mtuhumiwa.

✍️ Bryson Mshana

MAPOKEZI YA MGOMBEA MWENZA MBOGWEMgombea Mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kupitia Chama Cha Mapinduzi ...
05/09/2025

MAPOKEZI YA MGOMBEA MWENZA MBOGWE

Mgombea Mwenza wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Mhe. Balozi. Dkt. Emmanuel Nchimbi akiteta jambo na Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko mara baada ya kuwasili katika Viwanja vya Shule ya Msingi Masumbwe, Wilayani Mbogwe Mkoa wa Geita leo Septemba 5, 2025.

Address

Shangani Area, Kambarage Street, Plot No. 870
Mtwara
1121

Telephone

+255652462770

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Safari Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share