Safari Media

Safari Media Safari Media is a News/Media Company
Subscribe youtube channel now
www.youtube.com/channel/UCGml3vag_bwtdS_o7lp3YpA?sub_confirmation=1

24/01/2026

MAELEKEZO YA DKT.SAMIA KATIKA KUMUENZI MZEE MTEI

Maelekezo hayo yamesomwa na Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt Mwigulu Nchemba wakati akizungumza kwa niaba ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, jijini Arusha leo, Jumamosi Januari 24, 2026 alipotoa salamu za Serikali katika maziko ya Gavana wa kwanza wa Tanzania, Edwin Mtei.

24/01/2026

DKT.SAMIA: TANZANIA ITAVUKA SALAMA

Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt Mwigulu Nchemba amesema Serikali haitakuwa kikwazo cha kuhakikisha nchi inakuwa moja na inasonga mbele, baada ya kupita katika changamoto.

Akizungumza kwa niaba ya Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, mtendaji mkuu huyo wa Serikali, amesisitiza tayari kuna utashi wa kisiasa wa kujenga umoja nchini na kwamba jukumu hilo amekabidhiwa yeye.

Dkt Nchemba ametoa kauli hiyo jijini Arusha leo, Jumamosi Januari 24, 2026 alipotoa salamu za Serikali kwa Rais Dkt Samia, aliyemwakilisha katika maziko ya Gavana wa kwanza wa Tanzania, Edwin Mtei.

“Serikali haitakuwa kikwazo cha kuhakikisha kwamba nchi inakuwa moja na tunasonga mbele na mimi niwahakikishie tutavuka na tutasonga mbele na heshima ya Tanzania ya mara zote tutakuwa nayo,” amesema.

Amesema Rais Dkt Samia angependa kushiriki maziko hayo, lakini wingi wa majukumu umemfanya amtume yeye kumwakilisha na kwamba yaliyozungumzwa na wadau mbalimbali wakiwemo viongozi wa dini ameyachukua.

24/01/2026

MBOWE ASHAURI UPINZANI KUSHIRIKIANA NA SERIKALI KUJENGA UMOJA WA KITAIFA

Mwenyekiti wa mstaafu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Freeman Mbowe amewataka viongozi wa chama hicho na vyama vingine vya upinzani kushirikiana na Serikali kuleta umoja wa kitaifa.

Katika kulitekeleza hilo, Mbowe amevitaka vyama vya upinzani kuweka utaratibu wa kufanya kazi kwa pamoja ili kuwa katika njia moja ya kuliunganisha Taifa.

Kauli hiyo ya Mbowe inakuja wakati ambao Rais Dkt Samia ameshafanya juhudi mbalimbali zinazolenga kuleta maridhiano ili kujenga mshik**ano na umoja wa kitaifa.

Mbowe ametoa kauli hiyo leo, Jumamosi Januari 24, 2026 alipotoa salamu kwa niaba ya familia ya Mzee wakati wa maziko ya Gavana wa kwanza wa Tanzania, Edwin Mtei yanayofanyika mkoani Arusha.

“Tafuteni namna ya kufanya kazi kwa pamoja ili katika utaratibu wa kuliunganisha Taifa, kusiwe na taifa la vipande vipande vya vyama vya siasa,” amesema Mbowe na kuongeza kuwa

“Tunataka Taifa moja lenye misingi ya maendeleo, lenye upendo, lenye utengamano ili kuwezesha wale watakaokuwa na kwenye uongozi katika maeneo mbalimbali kufanya kazi zao kwa furaha na amani,” ameeleza Mbowe.

24/01/2026

NISHATI SAFI YA RAFIKI BRIQUETTES IWAFIKIE WATANZANIA WOTE - BALOZI KINGU






23/01/2026

SIO AHADI TENA, BIMA YA AFYA KWA WOTE KUANZA JANUARI 26

Ilianza ahadi, ikafuata mipango na mikakati, hatimaye Watanzania kwa mara ya kwanza katika historia, watanufaika na mpango wa Bima ya Afya kwa Wote (BAW), utakaoanza kutekelezwa Jumatatu Januari 26, 2026 kwa awamu ya kwanza.

Kuanza kwa mpango huo wa bima ya afya kwa wote, ni utekelezaji wa ahadi ya Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan aliyoitoa wakati wa kampeni za Uchaguzi Mkuu, aliposema ndani ya siku 100 baada ya kuapishwa atalitekeleza jambo hilo.

Hatua ya kuanza utekelezaji wa bima hiyo, inatarajiwa kuwaondolea mzigo wa gharama za matibabu wananchi wasio na uwezo wakiwemo wazee, watoto, wajawazito na watu wenye ulemavu, ambao gharama zao zitabebwa na Serikali.

Taarifa kuhusu kuanza kwa utekelezwaji wa bima hiyo, imetolewa jijini Dodoma leo, Ijumaa Januari 23, 2026 na Waziri wa Afya, Mohamed Mchengerwa, wakati wa kikao kazi cha kitaifa cha utekelezaji wa bima ya afya kwa wote.

Amesema awamu ya kwanza ya utekelezaji itaambatana na kuanza kutumika kwa kitita cha huduma muhimu, kitakachotolewa na skimu za bima ya afya, wakilenga makundi yaliyohatarini ili kupata huduma za afya bila kikwazo cha fedha.

"Bei ya kitita hicho ni Sh150,000 kwa kaya isiyozidi watu sita, kikiwa kinazingatia utaratibu wa rufaa katika vituo vya afya vilivyoingia mkataba na Skimu za Bima ya Afya.

"Nasisitiza kuwa Bima ya Afya kwa Wote si mradi wa wizara moja bali ni ahadi ya Taifa kwa wananchi wake. Mafanikio ya mpango huo yatapimwa si kwa hotuba wala maagizo, bali kwa idadi ya wananchi wanaolindwa dhidi ya gharama za matibabu na wanaopata huduma kwa heshima," amesema.

Amewataka wakuu wa mikoa yote nchini, kubeba dhamana ya moja kwa moja, binafsi na isiyohamishwa ya utekelezaji wa Bima ya Afya kwa Wote katika mikoa yao.

23/01/2026

MTWARA-MIKINDANI KUNUNUA BASI ILIKUWA MUHIMI LAKINI SIO LAZIMA

Hivi karibuni Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara-Mikindani MKOANI MTWARA, ilitangaza kununua basi aina ya TATA lililogharimu Shilingi Milioni 178, kutoka katika mapato ya ndani ya Halmashauri hiyo.

Uamuzi huo umeibua hisia na maoni mseto kutoka kwa wananchi na wadau mbalimbali wa maendeleo mkoani Mtwara, huku baadhi yao wakisema kuwa hatua hiyo iliyofanywa na Halmashauri ni nzuri lakini imekuwa ya mapema wakati ambapo bado kuna changamoto zingine zinazowakabili wananchi katika maeneo yao.

Tazama maoni ya mwanahabari Bryson Mshana, kupitia kipindi cha Safari Nasi kinachoruka kupitia Safari Radio Mtwara.



Mtwara 89.9 Fm
Lindi 88.9 Fm
Ruvuma 88.5

23/01/2026

RAIS SAMIA AMETIMIZA AHADI AJIRA 12,000 ZA WAALIMU, MADAKTARI

Waziri Mkuu wa Tanzania, Dkt Mwigulu Nchemba amesema Rais Samia Suluhu Hassan ametimiza ahadi ya ajira za walimu 7,000 aliyoahidi wakati wa kampeni za uchaguzi mkuu wa Oktoba 29, 2025.

Katika mikutano yake ya kampeni za mikoa mbalimbali Dkt Samia aliahidi ndani ya siku 100 kutoa ajira 12,000 za elimu na kada ya afya.

Dk Mwigulu ameeleza hayo leo Ijumaa, Januari 23,2026 wakati wa ziara yake ya kikazi mkoani Mwanza ambapo alipata fursa ya kuweka jiwe la msingi mradi wa ujenzi vituo vya kusukuma maji jijini humo.

“Mheshimiwa Rais (Dkt Samia) alisema ndani ya siku 100 wataajiriwa walimu 7,000 tayari wameshaajiriwa na wanakwenda katika shule za sekondari mpya zaidi ya 1,300,” ameeleza Dkt Mwigulu na kuongeza kuwa

“Wanakwenda pia katika shule za msingi mpya zaidi ya 2,700. Tayari walimu hao wapya wameshapangiwa maeneo yao ya kazi,” amesisitiza Dkt Mwigulu.

Dkt Mwigulu amesisitiza hakuna ahadi hata moja iliyoahidiwa na Dkt Samia ambayo haijatekelezwa, akifafanua kuwa hata ile ya watalaamu wa afya 5,000 imeshatekelezwa.

“Hivi tunavyoongea watalaamu hao 5,000 wameshaajiriwa ili kuwatibu Watanzania katika hospitali mbalimbali. Walisema kutakuwa na Bima ya Afya kwa Wote, leo hii shughuli inaendelea,” amefafanua Dkt Mwigulu.

23/01/2026

MTUHUMIWA WA UCHOCHEZI MTANDAONI AACHIWA KWA DHAMANA MTWARA

Jeshi la Polisi mkoani Mtwara limemwachia kwa dhamana muuguzi wa Hospitali ya Rufaa ya Ligula, Kulwa Kosmasi, ambaye alikuwa akishikiliwa kwa tuhuma za uchochezi mtandaoni.

Kamanda wa Polisi mkoani hapa Issa J. Suleimani, amethibitisha kuwa muuguzi huyo alihojiwa na kupewa dhamana huku upelelezi wa shauri lake ukiendelea.

Kamanda amesisitiza kuwa mtuhumiwa huyo hakutekwa bali alik**atwa kwa kufuata taratibu zote za kisheria za jeshi hilo.

Aidha, Kamanda Suleimani amewasihi wananchi wa Mkoa wa Mtwara kutumia mitandao ya kijamii kwa faida na kuepuka kuitumia kwa nia ovu au kusambaza ujumbe wa uchochezi unaoweza kuhatarisha amani.

Hatua hiyo imekuja kufuatia kuenea kwa uvumi kuhusu mazingira ya kuk**atwa kwa muuguzi huyo, ambapo Jeshi la Polisi limeweka wazi kuwa litaendelea kusimamia sheria kwa yeyote atakayebainika kukiuka miongozo ya matumizi ya mitandao.

22/01/2026

WAZIRI NDEJEMBI AFUNGUA KIKAO CHA 55 CHA BARAZA KUU LA WAFANYAKAZI WA TANESCO DODOMA

Waziri wa Nishati Mhe. Deogratius Ndejembi, leo tarehe 22 Januari, 2026 amefungua rasmi Kikao cha 55 cha Baraza Kuu la Wafanyakazi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO) kinachofanyika mkoani Dodoma.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho, Waziri Ndejembi amemshukuru Mhe. Rais Dkt Samia kwa kuboresha maslahi na stahiki za wafanyakazi wa TANESCO, huku akisisitiza usimamizi madhubuti wa masuala ya haki za wafanyakazi na kuimarisha ushirikiano mahali pa kazi, pamoja na kuendeleza utoaji wa elimu kwa umma kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu huduma ya umeme.

"Natambua mmekutana hapa kujadili kwa kina mambo yanayowahusu wafanyakazi naomba mhakikishe mnazungumza yote na kukubaliana ili kuendelea kuboresha utendaji wa shirika na maslahi ya wafanyakazi''.

Amehimiza pia umuhimu wa kuendelea kuboresha utoaji wa huduma bora na za uhakika za umeme kwa wateja wake nchini.

Akimkaribisha katika kikao hicho Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la umeme Bw. Lazaro Twange amemshukuru Mhe Waziri kwa kukubali wito wa kuja kufungua kikao hicho na kumuahidi kuwa wataendelea kusimamia haki za wafanyakazi na kuhakikisha wanakuwa na matokeo katika utendaji.

“Kipekee nikushukuru kwa kuitikia wito wa kuja kutufungulia kikao hiki, k**a Mwenyekiti wa baraza hili nikuahidi kuwa nitaenda kuyasimamia yote tutakayojadili hapa kwa ajili ya kuleta tija na maendeleo ya Shirika hili na kuongeza ufanisi katika kuhudumia wananchi”, alieleza Twange.

Kikao hicho kimewakutanisha viongozi wa TANESCO, wawakilishi wa Chama cha Wafanyakazi (TUICO), Wakurugenzi wa Kanda, pamoja na wawakilishi wa wafanyakazi kutoka kampuni tanzu na ofisi mbalimbali za mikoa nchini.

22/01/2026

BUTIKU ATAKA WATANZANIA KUJITATHMINI KWA UTULIVU BAADA YA VURUGU ZA OCTOBA 29

Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), imewataka Watanzania kuendelea kushik**ana na misingi ya Taifa, hususan katika kipindi hiki ambacho nchi inatafakari matukio ya vurugu za Oktoba 29, 2025 kupitia Tume iliyoundwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Hayo yameelezwa jijini Dar es Salaam leo, Alhamisi Januari 22, 2026 na Mwenyekiti wa MNF, Joseph Butiku, wakati wa kikao chake na wazee, kilichojadili masuala mbalimbali ikiwemo vurugu za Oktoba 29, mabadiliko ya Katiba, uzalendo, haki, amani na uwajibikaji.

Amesisitiza umuhimu wa kutafakari yaliyotokea kwa utulivu, busara na kwa kuzingatia misingi iliyoijenga Tanzania.

Butiku amesema matukio ya Oktoba 29 ni msiba ulioligusa Taifa zima na kwamba katika nyakati k**a hizo, ni muhimu jamii kuendelea kuzungumza kwa hekima.

Amefananishia hali hiyo na msiba ambao wakati mwingine maziko yanachelewa, lakini katika kusubiri, mazungumzo yanapaswa kuendelea kwa utulivu.

Amesema wakati Taifa linajiuliza nini kilitokea Oktoba 29, kwa nini kilitokea na nani aliyesababisha, ni muhimu Watanzania wasipoteze mwelekeo wala kujikuta wakitawaliwa na lugha za matusi na jazba, hususan katika mitandao ya kijamii.

22/01/2026

WANANCHI MTWARA KUNUFAIKA NA KAMATI ZA USHAURI WA KISHERIA


Kamati ya ushauri wa kisheria wilaya ya Mtwara, imekutana kwa ajili ya kupanga mikakati ya utelezaji na kujenga misingi ya ushirikiano kati ya k**ati na wadau wengine katika kutoa ushauri wa kisheria kwa wananchi.

Akizungumza wakati wa ufunguzi wa kikao hicho leo tarehe 22 Januri 2026, Mwenyekiti wa Kamati ya huduma za ushauri wa kisheria za mkoa, ambaye pia ni wakili wa Serikali kutoka Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali Mkoa wa Mtwara Nunu Mangu, amewakumbusha wajumbe wa k**ati hiyo kwenda kuwajibika kwa wananchi katika maeneo yao

Ameelezakuwa wajumbe hao wameaminiwa na kupewa jukumu la kipekee la kusaidia ushauri na uangalizi katika utekelezajiwa wa huduma za ushauri wa kisheria na elimu ya sharia kwa wanaanchi wa wilaya ya Mtwara.

“lengo kuu la k**ati hii ni kuwawezesha Mawakili wa Serikali kuhakikisha utawala wa sharia unafuatwa na kutekelezwa katika Mikoa na Wilaya kwa minajili ya kupunguza migogoro ya kisheria dhidi ya serikali na kutoa hudumaza ushauri wa kisheria kwa viongozi katika ngazi ya wilaya na wananchi kwa ujumla” ameeleza Wakili nunu Mangu.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Kamati ya ushauri wa kisheria wilaya ya Mtwara, Wakili mfawadhi wa ofisi ya wakili mkuu wa Serikali Mtwara Thomas Mahushi, ameipongeza ofisi ya mwanasheria mkuu wa serikali kwa kuwezesha uanzishwaji wa k**ati hizo ambazo amesema zitaleta tija kubwa katika sekta ya sharia nchini.

Naye mjumbe wa k**ati hiyo ambaye pia ni Wakili wa Serikali Wakili kutoka Halmashauri ya Manispaa ya Mtwara Mikindani Vivian Swai, amesema kuwa uanzishwaji wa k**ati hiyo unaenda kusogeza huduma msaada wakisheria kwa wananchi.

“k**a alivyosema mwenyekiti k**ati hizi zinalenga kutoa msaada wa kisheria kwa wanachi bure, kwa hiyo tumejipanga kuhakikisha kuwa wananchi wote wenye uhitaji huo wanafikiwa na msaada huu bila kutoa malipo yoyote” amesema

FCC, ZFCC ZAJADILI UIMARISHAJI WA USHINDANI WA BIASHARA NA KUMLINDA MLAJIKaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC...
20/01/2026

FCC, ZFCC ZAJADILI UIMARISHAJI WA USHINDANI WA BIASHARA NA KUMLINDA MLAJI

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani (FCC), Bi. Khadija Ngasongwa, amefanya ziara ya kikazi katika Tume ya Ushindani Halali wa Biashara Zanzibar (ZFCC) ikiwa ni hatua ya kuimarisha mashirikiano kati ya taasisi hizo mbili katika masuala ya ushindani, ulinzi wa mlaji na udhibiti wa bidhaa bandia.

Bi. Ngasongwa alipokelewa na Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa ZFCC, Bi. Aliya Juma ambapo viongozi hao walifanya mazungumzo kuhusu kuendeleza ustawi wa taasisi hizo na kuongeza ufanisi katika utekelezaji wa majukumu yao.

Akizungumza katika ziara hiyo iliyofanyika tarehe 14 Januari, 2026 katika ofisi za ZFCC - Zanzibar, Bi. Ngasongwa alisema ushirikiano kati ya taasisi hizo unaendelea kuimarika kupitia utekelezaji wa Hati ya Makubaliano (MoU) yaliyokwisha sainiwa.

"FCC na ZFCC tayari zimeanza kutekeleza kwa vitendo maeneo ya ushirikiano ikiwemo kujengeana uwezo, kubadilishana uzoefu na kufanya ukaguzi wa pamoja ili kudhibiti bidhaa bandia na kulinda haki za watumiaji wa bidhaa au huduma."alisema Bi. Ngasongwa

Katika ziara hiyo, Bi. Ngasongwa pia alikutana na kuzungumza na menejimenti ya ZFCC ambapo walijadili namna ya kuendeleza mpango wa pamoja wa kuboresha mifumo ya utendaji kazi na kubadilishana taarifa.

Kikao hicho cha siku moja kilihitimishwa kwa pande zote mbili kuahidi kuendeleza juhudi za pamoja ili kuhakikisha mazingira ya biashara yanaendelea kuwa shindani, salama na rafiki kwa mlaji.

Address

Shangani Area, Kambarage Street, Plot No. 870
Mtwara
1121

Telephone

+255652462770

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Safari Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share