Safari Media

Safari Media Safari Media is a News/Media Company
Subscribe youtube channel now
www.youtube.com/channel/UCGml3vag_bwtdS_o7lp3YpA?sub_confirmation=1

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeishauri Serikali kutafuta fedha za kuwalipa fidia wananchi waliopitiwa...
17/03/2025

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Nishati na Madini imeishauri Serikali kutafuta fedha za kuwalipa fidia wananchi waliopitiwa na Miradi ya kufua Umeme ya Ruhudji na Rumakali, ili wananchi hao wapishe maeneo hayo na waweze kuendelea na shughuli zao za kila siku wakati miradi hiyo ikisubiri kutekelezwa.

Kauli hiyo imetolewa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, ambaye ni Mbunge wa Same Mhe. David Mathayo baada ya kupokea taarifa ya utekelezaji wa miradi ya umeme katika Mkoa wa Njombe, tarehe 16 Machi 2025.

Mhe. Mathayo amesema, Serikali itafute fedha za kuwalipa fidia wananchi walioathiriwa na miradi hiyo ili wananchi hao wapishe na meneo hayo na waendelee na shughuli zao zingine wakati serikali ikiendelea kutafuta fedha za kutekeleza miradi hiyo.

“ Tayari tathmini imeshafanyika kwa wananchi watakaopitiwa na mradi huo na gharama za kuwalipa zimefahamika,na wananchi wanayo hiyo taarifa, ni vyema sasa serikali ikatafuta fedha za kuwalipa fidia wananchi hao ili wakaendelee na Maisha yao mengine wakati juhudi za kutekeleza mradi hiyo zikiendelea kufanyika”, alisisitiza Mhe. Mathayo.

Kwa upande wake Naibu Waziri wa Nishati, Mhe. Judith Kapinga, akizungumza kwa niaba ya Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko, amesema Wizara ya Nishati pamoja na Taasisi zilizo chini yake wamepokea maelekezo ya kamati hiyo pamoja na shukrani kwa niaba ya serikali, katika kutekeleza miradi ya umeme.

Kuhusu suala la fidia amesema kuwa Serikali imekuwa ikilipa fidia kwa wananchi wote wanaopisha miradi mbalimbali inayoanzishwa nchini, ikiwemo hiyo ya Ruhudji na Rumakali yenye thamani ya shilingi Bilioni 63.

Kwa upande wake Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa Wakala wa Nishati Vijijini REA, Mhandisi Jones Olotu amesema kuwa mwambao wa Ziwa Nyasa una maeneo korofi ambayo hayafikiki kirahisi katika utekelezaji wa mradi wa usambazaji umeme vijijini kwa kuwa hakuna miundombinu ya Barabara na kuahidi kutafuta utaratibu maalum wa kumpata mkandarasi mahsusi wa kutekeleza kazi hiyo ambapo sasa kazi kufanya upembuzi yakinifu inaendelea .

Viongozi wa dini mkoani Mtwara wametakiwa kuendelea kuwaambia waumini wao juu ya kuchagua viongozi bora watakaoleta maen...
15/03/2025

Viongozi wa dini mkoani Mtwara wametakiwa kuendelea kuwaambia waumini wao juu ya kuchagua viongozi bora watakaoleta maendeleo ndani ya mkoa na taifa kwa ujumka utakapofika uchaguzi mkuu mwaka huu 2025.

Hayo yameelezwa na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala wakati wa ghafla fupi ya Iftar iliyoandaliwa kwa lengo la kuwafuturisha waumini wa dini ya kiislamu na kikristo kwakua ni kipindi cha Mwezi Mtukufu wa Ramadhani na Kwarezma.

RC Sawala amesema tunapoelekea katika uchaguzi viongozi hao wadini ni vyema kuendelea kuuombea mkoa na Taifa kwa ujumla ili ukawe uchaguzi wa amani na utulivu.

Aidha amewashukuru viongozi hao wa dini kwa namna wanavyoendelea kuwaongoza kiroho,kimwili kwa kuwafundisha yaliyokuwa mema na kuchukia mabaya lakini kudumisha utulivu katika mkoa.

Nae Shekhe Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Jamaldin Chamwi ametumia nafasi hiyo kuwataka waumini wa dini wa dini zote mbili kuendeleza hali ya mani wakati wote ili kudumisha mshikamano waliokuwa nao.

Muinjilisti Matayo Masaka amewaomba waumini kumuombea dua Rais Samia Suluhu Hassan ambae ndie amemteua RC Sawala kuuongoza mkoa wa Mtwara kwakua amekuwa kiongozi sahihi kwa wananchi wa Mtwara.

Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli Nchini na Wadau kutoka Taasisi mbalimbali za ELIMU, wamefanya ziara Mkoani ...
15/03/2025

Mamlaka ya Udhibiti Mkondo wa Juu wa Petroli Nchini na Wadau kutoka Taasisi mbalimbali za ELIMU, wamefanya ziara Mkoani Mtwara katika visima vya gesi asilia vya Mnazi bay,Madimba na Chuo cha Ualimu TTC ambacho kinachonufaika na nishati ya gesi ya kupikia majumbani.

Ziara hiyo yenye lengo la kupata elimu ya utafutaji,uendelezaji na uzalishaji wa gesi asilia kwa wadau wa elimu ya vyuo vya juu na vyuo vya kati nchini Tanzania.

Akizungumzia lengo la ziara hiyo Mjiolojia Mwandamizi wa PURA M***a Itumbo,amesema lengo kubwa ni kuwaongezea uwelewa wadau wa elimu hasa kwa wakufunzi wa vyuo mbalimbali ambao wameambatana nao ili na wao waweze kuwajengea wanafunzi wao maarifa sahihi kuhusu sekta hiyo ya gesi asilia.

Ameongeza kuwa baadhi ya wanazuoni wanaohitimu kwenye vyuo hivyo wanatarajiwa kufanya kazi kwenye sekta ya mafuta na gesi hivyo kupitia elimu hiyo itakwenda kuwasaidia kujiandaa kwaajili ya ushindani kwenye soko la ajira.

Kwa upande wake Mdhibiti Ubora Mkuu kutoka Tume ya Vyuo Vikuu Tanzania Dkt. Malehe Setta amesema ziara hiyo ya kuongeza uwelewa wa uzalishaji na uchakataji wa gesi asilia inakizi mahitaji ya sera mpya ya elimu kwasababu sera hiyo inahitaji kutoa elimu ambayo itawafanya wahitimu kuwa na ujuzi kuliko kutoa elimu ya nadharia tu.

"Ukiangalia katika kutimiza majukumu ya sera mpya iliyoanzishwa vyuo vimeambiwa vitengeneze programu ambazo zitalenga kuwapa ujuzi wahitimu badae hivyo kwakufika hapa itatusaidia hasa kwa walimu kuongeza uwelewa wa namna gesi inavyozalishwa na uchakataji ambayo itaongeza thamani katika programu zao kule vyuoni ." Amesema Setta

Wadau hao walioshiriki katika ziara hiyo ni kutoka Chuo Kikuu cha Dar es salaam (UDSM),Chuo Kikuu cha Dodoma (UDOM),Chuo cha Bahari (DMI),Chuo cha Teknolojia Dar es Salaam(DIT), Chuo cha Teknolojia ya Ardhi (ATC),VETA MRI na wadhibiti ubora upande wa elimu ya juu na kati NACTVET na TCU.




Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Barbados...
15/03/2025

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Waziri Mkuu wa Barbados, Mhe. Mia Mottley ambapo wamekubaliana kuendelea kuimarisha ushirikiano baina ya nchi hizo mbili.

Mazungumzo hayo yamefanyika katika makazi rasmi ya Waziri Mkuu, Mhe. Mia Mottley, Jijini Bridgestone, nchini Barbados.

Waziri Mkuu Mia amesema, kuna umuhimu wa kuwa na mkakati wa pamoja na kushirikiana kwa lengo la kukuza utalii kati ya Barbados na Tanzania na nchi za Afrika Mashariki kwa ujumla. Amesema kuna maeneo mengi ya vivutio vya utalii ambavyo vinaweza kuzinufaisha pande hizo mbili yakiwemo masuala ya ukarimu.

Maeneo mengine ya ushirikiano ni katika utoaji wa mafunzo maeneo ya ufundi kati ya nchi za Carib (Caribbean) na nchi mbalimbali za kiafrika huku akisisitiza kuwa umuhimu wa uboreshaji wa masoko na kubadilishana wataalam katika sekta mbalimbali kwa makubaliano maalum.

Aidha, amesema upo uhitaji wa wataalam katika sekta ya maji na miundombinu na hivyo kuna uwezekano wa kubadilishana wataalam ili kujengeana uzoefu katika sekta mbalimbali kulingana na makubaliano yatakayofikiwa.

Kwa upande wake, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Biteko amesema mapendekezo hayo ni mazuri na yanaweza kuwa matokeo chanya baada ya kuchambuliwa na watalaam katika sekta husika kupitia Wizara zinazohusika na masuala ya kidiplomasia.

Dkt. Biteko amesema Serikali ya Tanzania chini ya uongozi wa Rais, Mheshimiwa Dkt. Samia Suluhu Hassan inaendeleza kampeni ya Nishati Safi ya Kupikia ambayo inalenga kuwawezesha asilimia 80 ya watumiaji wa nishati kuondokana na matumizi ya nishati isiyokuwa safi ifikapo mwaka 2034.

Katika utekelezaji wa mpango huo, amesema Tanzania inatembea kifua mbele kunadi mkakati huo wa miaka 10 ambao pamoja na mambo mengine unakusudia kupunguza madhara kwa watumiaji wa nishati isiyokuwa safi inayopelekea uchafuzi wa mazingira, magonjwa ya kupumua pamoja na vifo.

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Zainab Katimba, amesema tayari Serikali imetoa Sh.Bilioni 1.8 kwa ajili kuende...
14/03/2025

Naibu Waziri wa Ofisi ya Rais – TAMISEMI, Zainab Katimba, amesema tayari Serikali imetoa Sh.Bilioni 1.8 kwa ajili kuendelea na ujenzi wa Hospitali ya Halmashauri ya Muleba, mkoani Kagera baada ya kukamilisha hatua za kimkataba.

Mhe. Katimba ameeleza kuwa ujenzi wa hospitali hiyo ni mwendelezo wa juhudi za serikali katika kuboresha huduma za afya, ambapo awali halmashauri hiyo ilipokea sh.milioni 500 zilizotumika kujenga jengo la wagonjwa wa nje (OPD) na sasa, serikali imeongeza sh.bilioni 1.8 kwa ajili ya ujenzi wa majengo mengine ya hospitali.

Akiwa katika ziara ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya TAMISEMI wilayani Muleba leo, Machi 14, 2025 ilihusisha pia ukaguzi wa mradi wa ujenzi wa shule ya sekondari ya Amali inayojengwa katika kata ya Mubunda, Mhe. Katimba ameeleza kuwa mkataba wa ujenzi wa hospitali hiyo umekamilika na mkandarasi anatarajiwa kukabidhiwa eneo la ujenzi ndani ya wiki hii ili kuanza kazi.

"Ujenzi wa hospitali hii ni sehemu ya mpango wa serikali kuhakikisha huduma za afya zinawafikia wananchi kwa karibu zaidi. Mpaka sasa, hospitali mpya 129 zimejengwa katika halmashauri mbalimbali kupitia Ofisi ya Rais – TAMISEMI," amesema Mhe. Katimba.

Aidha, amewataka wananchi wa Muleba kuendelea kuunga mkono juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika kuwaletea maendeleo na kuboresha huduma za kijamii.

DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDSNaibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto B...
14/03/2025

DKT. BITEKO AKUTANA NA MTENDAJI MKUU WA CLIMATE INVESTMENT FUNDS

Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amekutana na kufanya mazungumzo na Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Climate Investment Funds (CIF) Bi. Tariye Gbadegesin Mjini Bridgetown, Barbados.

Mazungumzo hayo yamefanyika leo Machi 14, 2025 kando ya Mkutano wa Kimataifa wa kuhusu upatikanaji wa Nishati endelevu kwa wote (Energy ForAll)

Dkt. Biteko amesema kuwa, Wizara ya Nishati iko tayari kukuza ushirikiano na Taasisi hiyo ili kuunganisha juhudi za pamoja kuhakikisha matumizi ya nishati safi ya kupikia hususan maeneo ya Vijijini.

Aidha, Katika mazungumzo hayo yamehudhuriwa na Mshauri wa Rais Masuala ya Nishati Safi na Maendeleo ya Jamii, Angellah Kairuki, Katibu Mkuu Wizara ya Nishati, Mha. Felchesmi Mramba pamoja na Balozi wa Tanzania nchini Cuba na mwakilishi katika eneo la Caribean, Mhe. Humphrey Polepole.

MBUNGE AMSHUKURU DKT.SAMIA KWA UHARAKISHAJI WA MAENDELEO RUVUMAMbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma, Jacqueline Msongozi...
09/03/2025

MBUNGE AMSHUKURU DKT.SAMIA KWA UHARAKISHAJI WA MAENDELEO RUVUMA

Mbunge wa Viti Maalum Mkoa wa Ruvuma, Jacqueline Msongozi, amemshukuru Rais Samia Suluhu Hassan kwa juhudi zake katika kuleta maendeleo mkoani Ruvuma kupitia utoaji wa fedha kws ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali.

Akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani yaliyofanyika kwenye Uwanja wa Majimaji mjini Songea march 8 2025, Msongozi amesema mchango wa wanawake katika uchumi wa taifa ni mkubwa, kwani wanachangia asilimia 75 ya pato la taifa, hasa kupitia shughuli za kilimo na ujasiriamali.

Ameeleza kuwa moja ya changamoto kubwa inayowakabili wanawake wa Ruvuma ni upatikanaji wa masoko ya mazao wanayozalisha, jambo linalokwamisha juhudi zao za kujikwamua kiuchumi.

Ameiomba serikali kuhakikisha kunakuwepo na masoko ya uhakika kwa mazao ya wakulima ili kuongeza kipato cha wanawake na kuinua uchumi wa mkoa huo.

Aidha, ameizungumzia changamoto ya barabara ya mchepuko (bypass) katika Manispaa ya Songea, akieleza kuwa msongamano wa magari makubwa yanayobeba makaa ya mawe unaleta usumbufu kwa wafanyabiashara wadogo hususan wanawake.

Ameiomba serikali kuharakisha ujenzi wa barabara hiyo ili kupunguza ajali na kuboresha mazingira ya biashara kwa wanawake wajasiriamali wa Songea.

DKT.SAMIA AZINDUA MRADI WA MAJI WA SAME-MWANGA-KOROGWERais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Ha...
09/03/2025

DKT.SAMIA AZINDUA MRADI WA MAJI WA SAME-MWANGA-KOROGWE

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan akizindua mradi wa maji wa Same-Mwanga-Korogwe kwenye hafla iliyofanyika Mwanga mkoani Kilimanjaro tarehe 09 Machi, 2025.

Uzinduzi wa mradi huu wa kihistoria umehudhuriwa pia na Waziri Mkuu Mstaafu ambaye pia aliwahi kuwa Mbunge wa Jimbo la Mwanga Mkoani Kilimanjaro Mzee Cleopa David Msuya.

✍️

📸



WAFANYAKAZI MSD KANDA YA MTWARA WATEMBELEA WAFUNGWA WANAWAKE GEREZA LA LILUNGUKatika kuadhimisha Siku ya Wanawake Dunian...
07/03/2025

WAFANYAKAZI MSD KANDA YA MTWARA WATEMBELEA WAFUNGWA WANAWAKE GEREZA LA LILUNGU

Katika kuadhimisha Siku ya Wanawake Duniani, Wanawake wafanyakazi wa Bohari ya Dawa (MSD) Kanda ya Mtwara, wamefanya ziara maalum katika Gereza la Lilungu kuwatembelea Wafungwa wanawake.

Ziara hiyo imefanyika leo tarehe 7 Februari 2025 ikiwa na lengo kuwafariji, na kuwapa misaada mbalimbali kwa ajili ya kuboresha hali ya maisha yao , pamoja na kuwakumbusha kuwa jamii inawajali.

Wafanyakazi hao wamekabidhi vifaa mbalimbali ikiwa ni pamoja na taulo za k**e, mifuko ya Sukari, Sabuni, Vyakula mafuta na dawa za meno.

Kilele cha siku ya wanawake Duniani kitaifa kinafanyika Jijini Arusha, ambapo mgeni rasmi anatarajiwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt.Samia Suluhu Hassan.

✍️ Bryson Mshana

REA YAENDELEA KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFIWakala wa Nishati Vijijini (REA), leo Machi 6, 2025 umeendelea kutoa e...
06/03/2025

REA YAENDELEA KUHAMASISHA MATUMIZI YA NISHATI SAFI

Wakala wa Nishati Vijijini (REA), leo Machi 6, 2025 umeendelea kutoa elimu ya matumizi ya nishati safi ya kupikia katika siku ya pili ya Kongamano na Maonesho ya Petroli ya Nchi Wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAPCE’25) yanayofanyika katika ukumbi wa Kimataifa wa JNICC jijini Dar es Salaam.

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amesema kukamilika kwa Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la ...
05/03/2025

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Kassim Majaliwa amesema kukamilika kwa Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kidunda kutahakikisha upatikanaji wa huduma ya uhakika ya majisafi kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, baadhi ya maneo ya Mkoa wa Morogoro na Pwani.

Waziri Mkuu Majaliwa ametoa kauli hiyo mara baada ya kuweka jiwe la msingi la Mradi wa Ujenzi wa Bwawa la Kidunda, wenye thamani ya zaidi ya Sh. bilioni 335 ambazo ni fedha za ndani za Serikali.

Katika hotuba yake, Mhe. Majaliwa amesema kuwa bwawa hilo ni mradi wa kimkakati wenye lengo la kuhakikisha upatikanaji wa majisafi na salama kwa Jiji la Dar es Salaam, pamoja na baadhi ya maeneo ya mikoa ya Morogoro na Pwani.

“Fedha za utekelezaji wa miradi ya maji zipo, ila uharibifu wa vyanzo vya maji ni changamoto kubwa katika adhma ya Serikali kufikisha huduma ya maji kwa wananchi, Hivyo, hatuna budi kulinda na kutunza vyanzo vya maji.” Waziri Mkuu ametoa rai.

Katika hatua nyingine, Waziri Mkuu amezindua rasmi Wiki ya Maji Kitaifa mwaka 2025 kuanzia leo yenye Kaulimbiu “Utunzaji wa Uoto wa Asili kwa Uhakika wa Maji’ sanjari na uzinduzi na uwekaji wa mawe ya msingi wa miradi ya maji na shughuli za kijamii katika maeneo mbalimbali nchini.

Naye, Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amesema mradi huo unagharamiwa kwa fedha za ndani za Serikali, ambapo mpaka sasa mkandarasi anayetekeleza mradi huo Sinohydro Corporation Ltd kutoka China ameshalipwa Sh. Bilioni 85 kwa awamu ya kwanza na mradi umefikia asilimia 28 ya ujenzi na unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Novemba, 2026.

Ujenzi wa Bwawa la Kidunda ni hatua muhimu kuelekea utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo ya mwaka 2025, inayolenga kuhakikisha kila Mtanzania anapata majisafi, salama, na ya kutosha.

Wazazi na walezi katika Manispaa ya Mtwara Mikindani Mkoani Mtwara wamehamasika kujitolea kuchimba msingi katika ujenzi ...
05/03/2025

Wazazi na walezi katika Manispaa ya Mtwara Mikindani Mkoani Mtwara wamehamasika kujitolea kuchimba msingi katika ujenzi wa uzio shule ya sekondari chuno ili kudhibiti wanafunzi kuingia na kutoka shuleni kiholela.

Kukamilika kwa uzio katika shule hiyo ya Sekondari Chuno kutasaidia wanafunzi kuhudhulia vipindi vyote vya masomo.

Baadhi ya wananchi hao akiwemo Shakira Mustafa amesema baadhi ya wanafunzi wamekuwa wakitoroka na kwenda katika maeneo yasiyofaa huku baadhi yao wakijiingiza katika vitendo vya kihalifu.

Ameongeza kuwa kukamilika kwa uzio huo utasaidia kuondoa changamoto hiyo na kufanya wanafunzi kuhudhulia vipindi vyote vya masomo na hatimaye kuongeza ufauru .

Diwani wa kata ya Chuno Fanikio Chijinga amesema ujenzi huo ni azimio la kikao ambacho waliazimia kila mzazi kuchangia elfu 32000 ili waweze kukamilisha ujenzi wa uzio huo.

Katika kuunga mkono juhudi za wananchi hao Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara Mikindani Hassan Nyange ameahidi kugharamia malipo kwa mafundi ambao watajenga uzio huo na kwa upande wa Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini Hassan Mtenga ameahidi kutoa tofali 1,000

Mkuu wa shule ya sekondari Chuno Mwalimu Hamisi Kaoneka amesema pamoja na mambo mengine ujenzi huo unakwenda kuondoa adha ya watu kukatiza eneo la shule bila utaratibu maalumu,wanafunzi kufika shuleni kwa wakati pamoja na kulinda miundombinu ya shule.

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amewahimiza wanawake wa mkoa wa Ruvuma  kujitokeza na kugombea nafasi ...
05/03/2025

Mkuu wa Mkoa wa Ruvuma, Kanali Ahmed Abbas Ahmed, amewahimiza wanawake wa mkoa wa Ruvuma kujitokeza na kugombea nafasi mbalimbali za uongozi katika uchaguzi mkuu utakaofanyika mwaka huu.

Kanali Abbas ameeleza hayo wakati akizungumza na waandishi wa Habari March 4, 2025 Ofisini kwake kuelekea kilele cha siku ya wanawake duniani march 8 mwaka huu ambapo halmashauri zote 8 za mkoa wa Ruvuma zitaungana na kuadhimisha siku hiyo katika uwanja wa Majimaji Mjini Songea.

Amesema kuwa lengo la maadhimisho ya siku ya wanawake kwa mwaka 2025 ni kuihamasisha jamii kukuza usawa, haki na uwezeshaji wa wanawake, wasichana na wanaume kuelekea uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

Sambamba na hilo amewasisitiza viongozi wa dini watumie nyumba za ibada kutoa ujumbe kuhusu umhimu wa malezi ya Watoto katika kujenga familia na taifa imara.

Kwa upade wake siwazuri ally mwinyi ambaye ni mwenyekiti wa kamati ya maandalizi ya maadhiisho ya siku ya wanawake duniani katika mkoa wa Ruvuma amesema kamati imejipanga vizuri kuonesha vitu vingi vinavyofanywa na wanawake na kuonesha mchango wa wanawake katika sekta mbalimbali.

Afisa mendeleo ya jamii kutoka ofisi ya mkoa wa Ruvuma Exaveria mlimila amesema kuwa mpaka kufia sasa vikundi zaidi 456 vya wanawake ambavyo tayari vimeptiwa mikopo, ameongeza kuwa halmashauri zote zinapesa za kutosha kwahyo wanawake wajasiliamali wasisite Kwenda kuomba mikopo

MBUNGE ANASTAZIA WAMBURA ACHANGIA UJENZI WA NYUMBA ZA VIONGOZI UWT MASASI NA NANYUMBUMbunge wa viti Maalumu CCM Mkoa wa ...
27/02/2025

MBUNGE ANASTAZIA WAMBURA ACHANGIA UJENZI WA NYUMBA ZA VIONGOZI UWT MASASI NA NANYUMBU

Mbunge wa viti Maalumu CCM Mkoa wa Mtwara Anastazia Wambura amekabidhi mbao 650 na Bati 185 ikiwa ni mchango wake kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa nyumba za makatibu wa Umoja wa Wanawame wa Chama cha Mapinduzi Wilaya za Masasi na Nanyumbu Mkoani Mtwara.

Akizungumza tarehe 24 februari 2025, Wambura amesema nyumba hizo zimeaza kujengwa mwaka 2023 hivyo ameamua kuchukua jukumu la kuhakikisha kuwa zinakamilika ili viongozi hao waanze kuzitumia.

Kwaupande wao wajumbe wa kamati ya utekeleza ya UWT wilaya ya Masasi wamemshukuru Mhe. Wambura kwa uamuzi wake wa kumalizia ujenzi wa nyumba hizo.

UWT Mkoa wa Mtwara umeamua kuazisha ujenzi wa nyumba za watumishi wa jumuhiya hiyo katika Ngazi ya Mkoa na Wilaya kwa lengo la kuondoa changamoto ya makazi kwa watumishi wao.

Mabalozi wa serikali ya Tanzania na Msumbiji wamefanya kikao cha ujirani mwema juu ya kudumisha uhusiano wa kiuchumi kwa...
27/02/2025

Mabalozi wa serikali ya Tanzania na Msumbiji wamefanya kikao cha ujirani mwema juu ya kudumisha uhusiano wa kiuchumi kwa nchi hizo mbili ambazo Tanzania inapakana na Msumbiji katika mipaka yake iliyoko mkoani Mtwara.

Kikao hicho kimefanyika Leo Februari 27,2025 katika manispaa ya mtwara Mikindani mkoani Mtwara ambacho lengo lake kubwa ni namna ya kuimarisha vikao vya ujirani mwema kwa nchi hizo mbili na kudumisha uhusiano pamoja na kukuza uchumi kwa mkoa na wananchi kwa ujumla.

Balozi wa Tanzania nchini Msumbiji phaustine Kasike amesema licha ya nchi hizo kuwa na ushirikiano mkubwa wa kihistoria hasa kwenye upande wa siasa na kijamii lakini hali ni tofauti kwa upande wa kiuchumi bado haujafikia kiwango cha kulidhisha hivyo kupitia mikutano ya ujirani mwema itakuwa fursa ya kuwezesha nchi ya Tanzania kutangaza fursa zake za uchumi ambazo ziko katika maeneo ya kilimo,viwanda,utalii na biashara yatakayosaidia kupata masoko.

Nae Balozi wa Msumbiji nchini Tanzania Ricardo Ambroisio amesema manufaa ya kikao hicho ni kuona namna ya majimbo mawili kati ya Cabo Delgado na Mtwara yanaweza kunufaika nayo.

Hata hivyo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara Kanali Patrick Sawala ameyaomba mataifa hayo mawili kupitia mabalozi wake kuendeleza ujirani mwema katika nyanja mbalimbali ambapo nyanja ya kiuchumi kiwe kipaumbele.

Aidha ameweka wazi hatua ya mataifa hayo mawili ambayo tayari jitihada za kuunganisha mawasiliano baina ya watu wake zimeanza kuchukuliwa katika mipaka yake na tayari wamesharekebisha kivuko cha MV Kilambo.

Benki Kuu ya Tanzania – BOT imesema itaendelea kushirikiana na waandishi wa habari wanaofanya kazi katika vyombo mbalimb...
26/02/2025

Benki Kuu ya Tanzania – BOT imesema itaendelea kushirikiana na waandishi wa habari wanaofanya kazi katika vyombo mbalimbali ya habari nchini, ili kuwajengea uwezo wa kuwaelimisha wananchi kuhusu masuala mbalimbali yanayohusu biashara, uchumi na fedha.

Mkurugenzi wa Benki Kuu Tawi la Mtwara Nassoro Omary, ameeleza hayo tarehe 25 Februari 2025 wakati akifungua Semina ya Siku tatu inayoambatana na mafunzo kwa waandishi wa habari za Uchumi, Biashara na Fedha kutoka Zanzibar, Dar es salaam, Mtwara, Lindi na Ruvuma.

Amesema kuwa BOT inatambua mchango wa wanahabari katika kufikisha taarifa mbalimbali kwa jamii kupitia uandishi wa habari, ndio maana wamekuwa wakiandaa utaratibu wa kukutana nao kila mwaka kwa ajili ya kukumbushana mambo muhimu yanayohusu uchumi na fedha.

“Ni matumaini ya Benki Kuu kuwa kukutana huku kutakuwa na manufaa makubwa, kwa waandishi wa habari wanaoshiriki watapata fursa ya kukutana na wataalm mbalimbali na kujifunza kwa ajili ya kwenda kuwaelimisha wananchi wengine” amesema Nassoro Omary.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa semina hiyo Ndg. Bryson Mshana ameishukuru BOT kwa kuendeleza utaratibu wa kukutana na waandishi wa habari kila mwaka, kwa ajili ya kuwakumbusha masuala muhimu yanayohusu fedha, uchumi na biashara hali ambayo imewapa urahisi katika kuwaelimisha wananchi.

“Semina hizi zinazoambatana na mafunzo kutoka kwa wataalam wa Benki Kuu zimekuwa zikifanyika kwa miaka kadhaa sasa, na zimekuwa msaada mkubwa kwa wanahabari hawa na wengine sio katika kuandika tu lakini kuwa na mawasilaino ya moja kwa moja na watendaji wa benki kuu ambao wamekuwa wakitoa msaada wa kihabari wakato wowote”

Naye Dominick Mwita Mchumi kutoka BOT aliyewasilisha mada za Muundo na Majukumu ya BOT pamoja na Sera ya fedha inayotumia Riba ya Benki Kuu, amesema mfumko wa bei nchini uko chini ya lengo la5%, ambapo kwa January 2025 ilikuwa 3% sawa na ilivyokuwa Disemba 2024.

Noves Moses ambaye ni Meneja msaidizi Idara ya mawasilaino BOT, ameeleza umuhimu wa semina hiyo kwa waandishi wa habari na namna ambavyo imekuwa na faida kwa waandishi wa habari na wananchi kwa takribani miaka 17 tangu ianze kufanyika katika maeneo mbalimbali nchini.

TAARIFA KUTOKA BENKI KUU YA TANZANIA
24/02/2025

TAARIFA KUTOKA BENKI KUU YA TANZANIA

Naibu Waziri wa Nishati, Mhr.Judith Kapinga amewataka watendaji wa Sekta ya Nishati kuwajengea uwezo watoa huduma wanaot...
24/02/2025

Naibu Waziri wa Nishati, Mhr.Judith Kapinga amewataka watendaji wa Sekta ya Nishati kuwajengea uwezo watoa huduma wanaotekeleza miradi mbalimbali ya sekta ya nishati nchini.

Hayo ameyasema leo Februari 23, 2025 na Kapinga wakati akizungumza na wafanyakazi wa Shirika la Umeme nchini (TANESCO, na wakuu wa taasisi za wizara kabla ya kushiriki ziara ya Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Samia Suluhu Hassan inayotarajiwa kuanza leo mkoani Tanga.

"Tunataka hii miradi ikamilike kwa wakati na kwa ubora mkubwa, wakandarasi wajengewe uwezo wa utendaji kazi ili kazi ionekane inafanyika, " Ameongeza Mhe. Kapinga.

Aidha, ameipongeza REA kwa kumaliza kufikisha umeme kwenye vijiji vyote nchini na kusisitiza miradi inayoendelea na ile inatakayoanza mwaka huu wa fedha itekelezwe kwa wakati.

"Ni muhimu sana kuwasimamia wakandarasi kwa nguvu kuanzia mwanzo tuwe nao makini ili miradi hii ya kupeleka umeme kwenye vitongoji ikamilike kwa wakati, " Amesema Mhe. Kapinga

Katika hatua nyingine, Mhe. Kapinga amewataka watendaji wa taasisi za nishati kuwa na mahusiano mazuri na wananchi hususan wakati wa kupitisha miradi ya maendeleo kwenye maeneo yao.

"Imarisheni mahusiano na wananchi mnapopitisha miradi yetu na kuwaeleza kuwa Serikali italipa fidia kwa wote miradi hiyo ilipopita," Amesema Mhe. Kapinga

Address

Shangani Area, Kambarage Street, Plot No. 870
Mtwara
1121

Telephone

+255652462770

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Safari Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share