Safari Media

Safari Media Safari Media is a News/Media Company
Subscribe youtube channel now
www.youtube.com/channel/UCGml3vag_bwtdS_o7lp3YpA?sub_confirmation=1

EWURA, TRA KUIMARISHA USHIRIKIANOWatendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na wenzao wa Maml...
23/12/2025

EWURA, TRA KUIMARISHA USHIRIKIANO

Watendaji wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji (EWURA) na wenzao wa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), leo 23 Desemba 2025, wamekutana na kujadili namna ya kuimarisha ushirikiano wa utendaji hususani katika usimamizi wa masuala ya kikodi yanayotokana na huduma zinazodhibitiwa na EWURA.

Kaimu Mkurugenzi Mkuu wa EWURA, Bwana Gerald Maganga, amesema EWURA ni mshirika mzuri katika kuisaidia TRA kutekeleza wajibu wake wa usimamizi wa kodi nchini.

“Ushirikiano uliopo kati ya taasisi hizi mbili, utatupeleka mbele, tuudumishe na tusimamie utekelezaji wa makubaliano yetu,” alisema.

Meneja wa TRA mkoa wa Dodoma, Bwana Pendolake Elinisafi, ameishukuru EWURA kwa kuipatia TRA ushirikiano mzuri, na kuahidi kuuendeleza ili kuweka msingi imara wa mafanikio ya taasisi hizo mbili na taifa kwa ujumla.

MABARAZA YA BIASHARA NI NGUZO YA KUBORESHA UWEKEZAJI Mabaraza ya biashara yameelezwa kuwa nguzo muhimu katika kuboresha ...
23/12/2025

MABARAZA YA BIASHARA NI NGUZO YA KUBORESHA UWEKEZAJI

Mabaraza ya biashara yameelezwa kuwa nguzo muhimu katika kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji mkoani Mtwara, huku viongozi wakihimizwa kuyatumia k**a jukwaa rasmi la kusikiliza na kutatua changamoto za wafanyabiashara.

Hayo yamesemwa leo Disemba 23,2025 na Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Kanali Patrick Sawala, wakati wa kikao cha tisa cha Baraza la Biashara la Mkoa wa Mtwara kilichofanyika katika Manispaa ya Mtwara Mikindani.

Kanali Sawala amesisitiza umuhimu wa viongozi wa ngazi zote kutumia mabaraza ya biashara kupokea kero za wafanyabiashara na kuzifanyia kazi kwa lengo la kuzipatia ufumbuzi, akihimiza sekta binafsi kuwa na utamaduni wa kuwasilisha changamoto zao kupitia mabaraza hayo kwa ajili ya majadiliano ya pamoja.

“Niendelee kuwasihi sekta binafsi kuwa na utamaduni wa kuwasilisha kwenye mabaraza hayo kero na changamoto mbalimbali zinazojitokeza katika biashara kwa ajili ya majadiliano na kuzipatia ufumbuzi kero hizo,” amesisitiza Sawala.

Kikao hicho pia kimejadili namna ya kuimarisha ushiriki wa wazawa katika miradi mbalimbali ya kimkakati inayotekelezwa ndani ya mkoa huo, ikiwamo miradi ya barabara, kwa lengo la kuhakikisha manufaa yanawanufaisha wananchi na taifa kwa ujumla.

Kwa upande wao washiriki wa kikao hicho, akiwamo Mwenyekiti wa Chemba ya Taifa ya Biashara,Viwanda na Kilimo (TNCC) mkoani Mtwara Kizito Galinoma, wamesema uwepo wa miradi mikubwa na ya kimkakati mkoani humo ikiwamo ya barabara k**a Mingoyo–Masasi ni fursa kubwa kwa wafanyabiashara.

23/12/2025

MRADI WA TACTIC KUONGEZA MTANDAO WA BARABARA ZA LAMI MTWARA

Mamlaka ya Barabara za Vijijini na Mijini (TARURA) inatarajia kunufaika na mradi wa Uboreshaji wa Miundombinu ya Miji ya Tanzania (TACTIC) inayofadhiliwa na Serikali Kuu kupitia mkopo wa Benki ya Dunia,katika kukarabati na kujenga barabara pamoja na mifereji ya maji katika baadhi ya maeneo ya Manispaa ya Mtwara Mikindani mkoani Mtwara.

Akizungumza na waandishi wa habari Meneja wa TARURA Wilaya ya Mtwara Mhandisi Hatibu Nunu, amesema kuwa kupitia mradi wa TACTIC, TARURA itanufaika na ujenzi wa barabara mbalimbali zenye kiwango cha lami ambapo miongoni mwa barabara hizo ni barabara ya kutoka Pacha ya Mbae hadi Chuo cha Ualimu yenye urefu wa kilomita 2.4, barabara ya Stendi ya Chipuputa yenye urefu wa kilomita 2.4 pamoja na barabara za kuzunguka Soko la Chuno zenye jumla ya kilomita 3.

Mhandisi Nunu ameongeza kuwa ujenzi wa barabara hizo utaongeza mtandao wa barabara za lami ndani ya Manispaa ya Mtwara Mikindani kutoka kilomita 54 hadi kufikia kilomita 60, kutokana na ongezeko la kilomita 6 kupitia mradi huo.

Aidha, amesema kuwa kila mwaka serikali hutenga kiasi cha shilingi bilioni 3.8 kwa ajili ya ukarabati wa barabara ndani ya manispaa, na kwa mwaka huu tayari TARURA imeshasaini mikataba yenye thamani ya shilingi bilioni 1.5 kwa ajili ya ukarabati wa barabara na usafishaji wa mifereji ya maji.

Kwa upande wake, Mhandisi Mshauri Mkazi wa miradi ya TACTIC katika Manispaa ya Mtwara Mikindani, Henry Moshi amesema kuwa mojawapo ya faida za mradi huo ni uwepo wa maabara ya kupima ubora wa vifaa vya ujenzi (materials testing laboratory) ambayo haitasaidia TARURA pekee bali pia kampuni nyingine zinazotekeleza miradi ya ujenzi.

Ameongeza kuwa amependekeza kuajiri vibarua kutoka maeneo ya karibu na miradi hiyo ili kuongeza ajira kwa wananchi wa eneo husika.

Naye mmoja wa wanufaika wa mradi huo, Yohana Peter, amesema kuwa mradi wa TACTIC umekuwa ukiwasaidia wananchi kujipatia kipato, na amewahamasisha vijana kujitokeza kufanya kazi kwa bidii ili kunufaika na fursa zilizopo.

UONGOZI WA APRM WAKUTANA NA VIONGOZI WA WANAFUNZI WA VYUO VIKUUKatibu Mtendaji wa Mpango wa Hiari wa Nchi za Umoja wa Af...
23/12/2025

UONGOZI WA APRM WAKUTANA NA VIONGOZI WA WANAFUNZI WA VYUO VIKUU

Katibu Mtendaji wa Mpango wa Hiari wa Nchi za Umoja wa Afrika wa Kujitathmini kwa Vigezo vya Utawala Bora (APRM) Tanzania, Bw. Lamau Mpolo, amekutana na kufanya mazungumzo na viongozi wa wanafunzi kutoka vyuo vikuu mbalimbali nchini.

Lengo la kikao hicho lilikuwa kujadili nafasi ya vijana katika kukuza dhana ya Utawala Bora k**a nguzo muhimu ya kuimarisha amani na usalama nchini Tanzania.

Katika kikao hicho, Bw. Mpolo alisisitiza umuhimu wa ushiriki wa vijana katika masuala ya utawala, akieleza kuwa vijana ni rasilimali muhimu katika kujenga jamii yenye uwajibikaji, uwazi na maamuzi jumuishi.

Kikao hicho cha siku moja kilifanyika Desemba 22, 2025, katika Ofisi za APRM zilizopo katika jengo la Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, jijini Dar es Salaam.

KATAMBI AAGIZA KULINDWA USHINDANI WA HAKI, AKEMEA UKIRITIMBA WA BEINaibu  Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas K...
23/12/2025

KATAMBI AAGIZA KULINDWA USHINDANI WA HAKI, AKEMEA UKIRITIMBA WA BEI

Naibu Waziri wa Viwanda na Biashara, Mhe. Patrobas Katambi (Mb), ameliagiza Baraza la Ushindani (FCT) kuendelea kusimamia na kulinda ushindani wa haki ili kuondoa vitendo vya ukiritimba, hususan katika suala la kupandisha bei za bidhaa na huduma.

Ameyasema hayo wakati wa ziara yake katika Baraza la Ushindani Desemba 22, 2025 Jijini Dar es Salaam akisisitiza kuwa ushindani wa haki ni msingi muhimu wa ukuaji wa biashara, kwani vitendo vya ukiritimba vimekuwa vikiathiri biashara nyingi na walaji.

Ameeleza kuwa biashara zinapaswa kufanyika kwa kuzingatia ulinzi wa walaji, ambapo bei za bidhaa na huduma ziwe za haki, bidhaa ziwe na ubora, na uchunguzi wowote ufanyike kwa haki na kwa kuzingatia misingi ya kisheria.

Mhe. Katambi amebainisha kuwa Serikali inaendelea kuhamasisha uwekezaji kwa kuboresha sera rafiki, kufanya marekebisho ya sheria na kuendelea na maboresho ya mazingira ya biashara ili kuhakikisha Tanzania inakuwa mahali salama na rafiki kwa kufanya biashara bila kuweka vikwazo kwa wafanyabiashara wa ndani na nje ya nchi.

Amesisitiza kuwa haki katika utatuzi wa migogoro ni kipaumbele, kwa kulinda muda, heshima na maslahi ya wawekezaji na kusimamia sheria za ushindani, ndani na nje ya nchi, kwa lengo la kumlinda mlaji ili awe mnufaika mkuu wa shughuli za kibiashara.

Kwa niaba ya Mwenyekiti wa Baraza la Ushindani Jaji Rose Ibrahim, Dkt. Onesmo Kyauke amesema Baraza la Ushindani lina nafasi ya kipekee katika kuhakikisha malengo ya sera ya ushindani nchini yanatekelezwa kwa ufanisi, hususan kupitia usikilizaji wa rufaa na mashauri yanayotokana na maamuzi ya Tume ya Ushindani pamoja na mamlaka za udhibiti wa soko.

Amesema hatua hiyo inasaidia kujenga mazingira bora ya biashara, kuvutia uwekezaji na kulinda maslahi ya walaji na washiriki wote wa soko.

UHARIBIFU WA MIUNDOMBINU YA BARABARA MANISPAA YA MTWARA KUTAFUTIWA UFUMBUZISiku mbili baada ya Wakazi wa Mtaa wa Mbae Ma...
22/12/2025

UHARIBIFU WA MIUNDOMBINU YA BARABARA MANISPAA YA MTWARA KUTAFUTIWA UFUMBUZI

Siku mbili baada ya Wakazi wa Mtaa wa Mbae Mashariki, Kata ya Ufukoni, Manispaa ya Mtwara- Mikindani mkoani Mtwara, kulalamikia ubovu wa miundombinu ya barabara katika baadhi ya maeneo ya mtaa huo, hatimaye hatua za awali zimeanza kuchukuliwa.

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na Ofisi ya Mbunge wa Jimbo la Mtwara Mjini leo tarehe 22 Desemba 2025, imesema kuwa tayari Mbunge amshafanya majadiliano na Meneja wa TARURA Mkoa wa Mtwara pamoja na Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani ili kuchukua hatua za haraka.

Taarifa hiyo imeeleza kuwa Mkurugenzi wa Manispaa ya Mtwara-Mikindani ameitisha kikao cha dharura Jumanne tarehe 23 Desemba 2025, kitakachohusisha wataalamu wa TARURA, Mstahiki Meya, na ofisi ya Mbunge ambacho kitatoa maamuzi na hatua za kuchukuliwa haraka.


HARRY KANE AMEFUNGA MWAKA 2025 NA MAGOLI 60Kane pia amekuwa mchezaji mwenye kasi zaidi katika historia ya Bundesliga aki...
22/12/2025

HARRY KANE AMEFUNGA MWAKA 2025 NA MAGOLI 60

Kane pia amekuwa mchezaji mwenye kasi zaidi katika historia ya Bundesliga akichangia jumla ya magoli 100.

Magoli 81 na Pasi 19 katika michezo 78.

Hii sio AI, ni Harry Edward Kane.




ASTON VILLA USHINDI WA 10 MFULULIZOUshidi wa 2-1 dhidi ya Manchester uliifanya Aston Villa kufikisha michezo 10 mfululiz...
22/12/2025

ASTON VILLA USHINDI WA 10 MFULULIZO

Ushidi wa 2-1 dhidi ya Manchester uliifanya Aston Villa kufikisha michezo 10 mfululizo bila kufungwa katika mashindano yote msimu huu wa 2025/26

Villa sasa iko nyuma ya vinara Arsenal wenye alama 39 na Manchester City 37 huku wenyewe wakiwa na 36 katika ligi ya Uingereza.

22/12/2025

MASHABIKI WA SIMBA WAIBUKA NA USHINDI WA MAGOLI 2-0 DHIDI YA YANGA.

Timu ya Mashabiki wa Simba FC imeifunga timu ya mashabiki ww Yanga FC magoli 2-0 katika mchezo wa kirafii uliomalizika jioni ya ya tarehe 21 Desemba 2025 katika Uwanja wa KMC complex Dar es Salaam.

Ofisa habari wa klabu ya Yanga Ali kamwe ambaye alikuwa sehemu ya benchi la ufundi na mchezaji pia amesema mchezo huo haujaisha maana klabu ya Simba waliingiza mamluki na mwamuzi hakuwa upande wao huku akisisitiza lazima mechi hiyo irudiwe maana hawajazoea unyonge.

Kwa upande wa Simba Afisa habari wa klabu hiyo Ahmed Ally ambaye alikuwa sehemu ya benchi la ufundi na mchezaji pia alikuwa sehemu ya ushindi amesema walikuja kucheza mechi ya ushindi sio ya heshima na wao ndio wabingwa wa mechi ya leo.

Baada ya mechi timu zote zilikabiziwa kiasi cha fedha Milioni Ishirini (20,000,000) huku Simba akikabiziwa na ubingwa wa mechi hiyo.

Lengo la mchezo huo uliovuta hisia za mashabiki wa mpira nchini, ilikuwa ni kuwakutanisha pamoja mashabiki wa Simba na Yanga katika kudumisha umoja, upendo na mshik**ano wa makundi hayo licha ya tofauti zao za kisoka.





21/12/2025

BANDARI YA KISIWA MGAO KUFUNGUA FURSA ZA KIUCHUMI

Bandari ya Kisiwa Mgao inayojengwa mkoani Mtwara inatarajiwa kuongeza uwezo wa nchi ya Tanzania kuhudumia shehena ya mzigo mbalimbali.

Aidha kukamilika Kwa bandari hiyo kutaisaidia kupunguza msongamano wa shughuli za Bandari ya Mtwara, na kuimarisha biashara pamoja na usafirishaji wa bidhaa katika ukanda wa Kusini mwa Tanzania na nchi jirani.

Waziri wa uchukuzi Profesa Makame Mbarawa amefanya ziara ya kukagua maendeleo ya ujenzi wa bandari hiyo Disemba 20, 2025.

mradi huo unaogharimu zaidi ya Shilingi Bilioni 434 za Tanzania, ukiwa umefikia asilimia 25 ya Ujenzi na unatarajiwa kukamilika mwaka 2028.

Waziri Mbarawa ameeleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji pamoja na ubora wa kazi zinazoendelea kufanyika katika eneo la mradi.

Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa amesema mradi huo utakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi kwa mkoa wa Mtwara na maeneo ya jirani kwa kuongeza fursa za ajira, kuchochea shughuli za kibiashara, na kuboresha miundombinu ya usafirishaji wa bidhaa za kimkakati, hususan makaa ya mawe, saruji na mbolea.

Ziara ya Waziri Profesa Mbarawa ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha miradi mikubwa ya kimkakati inatekelezwa kwa ufanisi, uwajibikaji na kwa kuzingatia malengo ya kukuza uchumi wa Taifa na kuboresha ustawi wa wananchi.

KUKAMILIKA KWA BANDARI YA KISIWA MGAO NI FURSA KIUCHUMIWaziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema kukamilika kwa...
21/12/2025

KUKAMILIKA KWA BANDARI YA KISIWA MGAO NI FURSA KIUCHUMI

Waziri wa Uchukuzi, Profesa Makame Mbarawa amesema kukamilika kwa Bandari ya Kisiwa Mgao, mkoani Mtwara kutaongeza uwezo wa nchi kuhudumia shehena ya mzigo mchafu.

Aidha, kutaisaidia kupunguza msongamano wa shughuli za Bandari ya Mtwara, na kuimarisha biashara pamoja na usafirishaji wa bidhaa katika ukanda wa Kusini mwa Tanzania na nchi jirani.

Waziri Mbarawa aliyasema hayo Disemba 20, mwaka huu, wakati wa ziara yake kutembelea na kukagua mradi huo unaogharibi zaidi ya Shilingi Bilioni 434, ukiwa umefikia asilimia 25 ya Ujenzi na unatarajiwa kukamilika mwaka 2028.

Waziri Mbarawa ameeleza kuridhishwa na kasi ya utekelezaji pamoja na ubora wa kazi zinazoendelea kufanyika katika eneo la mradi wa usanifu na ujenzi wa Bandari mpya ya Kisiwa Mgao mkoani Mtwara.

Amesema Bandari mpya ya Kisiwa Mgao ni mradi wa kimkakati unaolenga kuimarisha sekta ya uchukuzi wa majini na kukuza uchumi wa Taifa, hususan kwa ukanda wa Kusini.

Naye Mkurugenzi Mkuu wa TPA, Plasduce Mbossa amesema mradi huo utakuwa chachu kubwa ya maendeleo ya kiuchumi kwa mkoa wa Mtwara na maeneo ya jirani kwa kuongeza fursa za ajira, kuchochea shughuli za kibiashara, na kuboresha miundombinu ya usafirishaji wa bidhaa za kimkakati, hususan makaa ya mawe, saruji na mbolea.

Amesema kukamilika kwa bandari hiyo mpya kutaongeza mapato ya serikali na kuiweka Tanzania katika nafasi nzuri zaidi ya ushindani wa kikanda katika sekta ya bandari na usafirishaji wa majini.

Ziara ya Waziri Profesa Mbarawa ni sehemu ya juhudi za serikali za kuhakikisha miradi mikubwa ya kimkakati inatekelezwa kwa ufanisi, uwajibikaji na kwa kuzingatia malengo ya kukuza uchumi wa Taifa na kuboresha ustawi wa wananchi.



WAZIRI MKUU APONGEZA TPDC KWA UJENZI WA SHULE YA MSINGI LIKONG'O KUPITIA MRADI WA LNG-LINDI Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Mu...
20/12/2025

WAZIRI MKUU APONGEZA TPDC KWA UJENZI WA SHULE YA MSINGI LIKONG'O KUPITIA MRADI WA LNG-LINDI

Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Mwigulu Nchemba amepongeza Wizara ya Nishati kupitia Shirika la Maendeleo ya Petroli Tanzania (TPDC) kwa ujenzi wa shule bora ya Awali na Msingi katika Kijiji cha Likong'o mkoani Lindi inayojengwa kupitia mradi wa uzalishaji na usindikaji wa Gesi Asilia kuwa kimiminika ( LNG). .

Waziri Mkuu ametoa pongezi hizo tarehe 20 Desemba 2025 wakati akikagua ujenzi wa shule hiyo itakayokuwa na uwezo wa kuhudumia wanafunzi 400 katika Kijiji cha Likong'o, Kata ya Mbanja, Halmashauri ya Manispaa ya Lindi.

" Nawapongeza TPDC kwa hatua hii ya kutekeleza shughuli za uwajibikaji kwa jamii (CSR) kupitia mradi huu wa LNG, shule hii ni bora ya kisasa na imezingatia mahitaji mbalimbali ikiwemo kuwa na miundombinu inayokidhi watu wenye mahitaji maalum na watoto wa k**e." Amesema Mhe. Nchemba

Kwa upande wake Salome Makamba ambaye ni Naibu Waziri wa Nishati, amesema mradi wa ujenzi wa Shule ya Msingi Likong'o unatekelezwa k**a sehemu ya kurudisha fadhila kwa wananchi waliotoa ardhi kwa ajili ya utekelezaji mradi wa LNG.

Ameeleza kuwa ujenzi wa Shule hiyo ambao umefikia asilimia 70 unaonesha jinsi kaulimbiu ya kazi na utu inavyotekelezwa kwa vitendo na Serikali ya Awamu ya Sita.

Naye, Mbunge wa Lindi, Mohamed Utaly amemshukuru Rais Samia kwa uwekezaji huo wa mradi wa LNG ambao amesema unaleta chachu ya elimu mkoani Lindi.

Awali, Mhandisi Msimamizi wa mradi wa shule ya Awali na Msingi Likong'o, Upendo Mahavanu kutoka TPDC alisema mradi huo unagharimu Sh .bilioni 1.27 ambapo shule itakuwa na Madarasa 9; saba yakiwa ni ya shule msingi na mawili ni ya awali, ofisi na nyumba za walimu.

Utekelezaji wa mradi wa LNG unatarajiwa kuwa na manufaa mbalimbali nchini ikiwemo mapato ya Serikali yatakayotokana na uuzaji wa LNG kwenye soko la kimataifa na fursa za ajira.

Address

Shangani Area, Kambarage Street, Plot No. 870
Mtwara
1121

Telephone

+255652462770

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Safari Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share