LikuNews

LikuNews

KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO AMPA KICHEKO BWANA YOHANA YUSUPH MKAZI WA KOROGWE MJIN...
03/02/2024

KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO AMPA KICHEKO BWANA YOHANA YUSUPH MKAZI WA KOROGWE MJINI KWA KUMPATIA KITI MWENDO CHA UMEME.

Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu Paul Makonda ametimiza Ahadi yake kwa Kumpatia Kiti Mwendo cha Umeme Bwana Yohana Yusuph ambaye ni Mkazi wa Korogwe Mjini Mkoani Tanga .

Ahadi hiyo kutoka kwa Ndugu Paul Makonda aliitoa tarehe 21 Januari 2024 alipokuwa kwenye Mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Mpira Sokoni Manundu .

26/11/2023

MBUNGE AWESO AANZA MCHAKATO WA KUJENGWA KWA ZAHANATI KATIKA KATA YA UBANGAA

26/11/2023

KUTOKA JIMBONI

Mbunge wa Jimbo la Pangani, Mhe. Jumaa Aweso wakiimba kwa pamoja na Wananchi wa Jimboni kwake wakati wa Ziara yake ya kusikiliza na kutatua kero .

26/07/2023

ZIARA YA MBUNGE WA JIMBO LA LUPEMBE WILAYANI NJOMBE YAWAAMISHA MWENYEKITI WA CHADEMA JIMBO LA LUPEMBE NA KATIBU WA CHADEMA KATA YA IKUNA WAJIUNGA NA CHAMA CHA MAPINDUZI (CCM) MARA BAADA YA KURIDHISHWA NA UTEKELEZAJI WA ILANI YA CCM.

Habari na Abdallah Athumani Liku (Njombe )

Mbunge wa Jimbo la Lupembe ,Mhe. Edwin Enosy Swalle pamoja na Viongozi wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Kata wameshudia kurejea kwa Mwenyekiti wa Chama cha CHADEMA katika Jimbo la Lupembe Ndugu .AHAZI KIHOMBO na Katibu wa CHADEMA Kata ya Ikuna Ndugu JAPHET NGIMBUDZI wamejiunga rasmi na Chama cha Mapinduzi mara baada ya kuridhishwa na utendaji Bora Serikali ya Chama cha Mapinduzi katika kusimamia vyema wa ILANI ya Chama hicho .

Tunayofuraha kuwataarifu kuwa tumeingia mkataba wa miaka mitatu na nyota wa kimataifa wa Tanzania, Feisal Salum ().Kiung...
09/06/2023

Tunayofuraha kuwataarifu kuwa tumeingia mkataba wa miaka mitatu na nyota wa kimataifa wa Tanzania, Feisal Salum ().

Kiungo huyo fundi maarufu k**a Fei Toto, anakuwa mchezaji wetu wa kwanza kumsajili kuelekea msimu ujao.

Tunamshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. na uongozi wa klabu ya kwa kuweka wepesi na kufanikisha usajili huu.

.amin

Liverpool wamekamilisha usajili wa Alexis Mac Allister kutoka Brighton kwa kitita cha pauni milioni 35 (ambazo zinaweza ...
09/06/2023

Liverpool wamekamilisha usajili wa Alexis Mac Allister kutoka Brighton kwa kitita cha pauni milioni 35 (ambazo zinaweza kufika hadi pauni milioni 55). Nyota huyu wa Argentina atavaa jezi namba 10 iliyokuwa ikivaliwa na Sadio Mane.

08/06/2023


SHIRIKA LA AGRI-CONNECT KWA KUSHIRIKIANA CEFA YATOA ELIMU YA LISHE NJOMBE DC.

Katika kutokomeza hali ya udumavu na ukondevu Kwa Watoto, leo June 8, 2023 Shirika la Agri-Connect kwa kushirikiana na Shirika la CEFA wametoa elimu ya lishe na malezi ya watoto kwa wananchi wa kijiji cha Havanga kata ya Kidegembye Halmashauri ya Wilaya ya Njombe.

Akizungumza na Wananchi hao Kaimu Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Njombe Ndugu, Augustino Nyenza amewaeleza kwamba dhumuni kubwa la serikali ni kuhakikisha Watoto wote wanakuwa na afya bora ya mwili na akili.

"Baba na mama ndiyo watu sahihi wanaotakiwa kuhakikisha kwamba mtoto anakuwa na afya bora hivyo tunatakiwa kuwapa Watoto mchanganyiko wa vyakula mbalimbali ili kuondoa hali ya udumavu" Alisema Ndugu. Nyenza

Mratibu wa Shirika la Agri-connect ameeleza kwamba lengo kubwa la kampuni hiyo ni kuhakikisha kwamba vijiji vyote vinafikiwa na kupatiwa elimu kusiana na Lishe bora.

Ndugu Lusiana Mwalongo ni miongoni mwa Wananchi walioshiriki mavunzovhayo hivyo ameushukuru Uongozi wa Halmashauri kwa jitihada za kufikisha elimu hiyo vijijini.

"Elimu tuliyopewa itakuwa na msaada mkubwa sana kwetu sisi wote pia tutahakikusha tunakuwa mabalozi kwa wale walioshindwa kufika".Alisema Bi.Lusiana

Kaulimbiu ilikuwa ni " Lishe bora Kwa afya imara na kilimo chenye tija.

06/05/2023

MBIO ZA MWENGE WA UHURU 2023

KIONGOZI WA MBIO ZA MWENGE WA UHURU ARIDHISHWA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA KITUO CHA AFYA KICHIWA KILICHOPO HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE

*DC JOKATE  AFANYA ZIARA BANDARI YA TANGA, AMEWATAKA WAFANYABIASHARA KUTUMIA BANDARI HIYO KUSAFIRISHA BIDHAA ZAO.*Mkuu w...
06/05/2023

*DC JOKATE AFANYA ZIARA BANDARI YA TANGA, AMEWATAKA WAFANYABIASHARA KUTUMIA BANDARI HIYO KUSAFIRISHA BIDHAA ZAO.*

Mkuu wa Wilaya ya Korogwe Mkoani Tanga, Mhe. Jokate Mwegelo amefanya ziara katika Bandari ya Tanga akiwa na Wafanyabiashara, Viongozi wa Chama na Serikali, Wakulima na Wadau wengine wa Korogwe ambapo amesema lengo ni kujionea maboresho ya Bandari hiyo yaliyotumia zaidi ya Tsh. Bilioni 400 na kuwapa chachu Wana Korogwe kusafirisha bidhaa zote Tanga badala ya kutegemea Bandari ya Dar es salaam pekee.

Akiongea na Waandishi wa Habari Bandarini hapo DC Jokate amesema “Uwekezaji mkubwa umefanyika hapa na Serikali ya awamu ya sita chini ya Dkt. Samia Suluhu Hassan zaidi ya Bilioni 400 katika maboresho ya Bandari ya Tanga , mnaona Meli hii kubwa huko nyuma ilikuwa haiwezi kufika, tumekuja Wafanyabiashara na lazima tukubaliane tani tunazozalisha wote tusafirishe hapa”

“Tukubaliane na Wakala wa Meli ili wapunguze tozo zao lakini ili apunguze lazima awe na uhakika wa kuondoa kontena kadhaa, malengo yetu ni kwamba bidhaa zote zinazozalishwa Wilayani Korogwe tutumie Bandari ya Tanga, ili fedha nyingi zilizowekezwa hapa ziwe na tija”

Kwa upande wake Meneja wa Bandari ya Tanga, Masoud Mrisha amesema “Kwa harakaharaka kuanzia January hadi Machi,2023 tumekusanya zaidi ya Tsh Bilioni 7, baada ya uwekezaji wa Bilioni 429.1 maendeleo ni makubwa, kwa mwaka tulikuwa tunazalisha tani Laki 7.5 lakini baada ya maboresho tunazalisha mpaka tani Mil 3, meli kubwa sasa zinaingia moja kwa moja katika bandari yetu ya Tanga”

TANGAZO KWA UMMA KUHUSU MAPOKEZI YA MRADI WA BOOST KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE .
06/05/2023

TANGAZO KWA UMMA

KUHUSU MAPOKEZI YA MRADI WA BOOST KATIKA HALMASHAURI YA WILAYA YA NJOMBE .

06/05/2023

NJOMBE DC YAADHIMISHA WIKI YA CHANJO KITAIFA KATIKA KIJIJI CHA ITUNDUMA.

08/01/2023

DC NJOMBE AKITAKA CHAMA CHA WAFAKANYAZI SERIKALI ZA MITAA( TALGWU) KUENDELEA KUTOA ELIMU KUHUSU NIDHAMU MAKAZINI.

Mkuu wa Wilaya ya Njombe ,Mhe. Kissa Gwakisa Kasongwa amemuwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Njombe ,Mhe. Anthony Mtaka katika uchaguzi mdogo wa Chama cha Wafanyakazi Serikali za Mitaa Mkoani Njombe kwa kumchagua Mjumbe wa k**ati ya Utendaji Taifa kwenda kuwakilisha Wafanyakazi Mkoani Njombe ,kabda ya kuzindua Uchuguzi huo ambao umeudhiliwa na baadhi ya viongozi ngazi ya Taifa katika chama cha Wafanyazi nchini ,amewataka viongozi kuendelea kusimamia maadili mema na kutanguliza uzalendo zaidi ndani ya Nchi ili kuakikisha kila kitu kinakuwa sawa katika utendaji wao ili kupunguza matukio mbalimbali ya uvunjaji nidhamu yanayoendelea kuzagaa mitandao ambayo yanaonyesha taswira mbaya kwa Serikali na Watumishi .Aidha kwa upande wa Watumishi Mkoani Njombe wamempongeza na Kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ,Mhe. Dkt .Samia Suluhu Hassan kwa Jitihada kubwa ambazo anazozifanya kwa kuwajali Watumishi kwa kuwapandisha Madaraja na kuwaongezea Mishahara ambapo hapo awali haikuwahi kutokea kwa Wafanyakazi Kupandishiwa mishahara na Madaraja ila kwa awamu ya sita imeweza kufuta kilio hicho. Hata hvyo kwa upande wa Serikali imewatoa hofu Wafanyakazi Mkoani Njombe kuendelea kuiamini Serikali ya awamu sita na kuendelea kuunga juhudi za Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe.Dkt. Samia Suluhu Hassan katika kuleta maendeleo katika utekelezaji wa Miradi mbalimbali ya Maendeleo nchini bila kusahau namna anavyowajali Watumishi kwa kuwaboreshea Mishahara na kuwawekea Miundo mbinu mizuri katika maeneo yao ya kazi .

04/10/2022

WAZIRI WA MAJI, MHE. JUMAA AWESO AMEKAGUA NA KUWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA OFISI NDOGO NJOMBE, UKARABATI NA UPANUZI MAABARA YA MAJI SONGEA ,TAREHE 4/10/2022 MKOANI NJOMBE.

03/10/2022

RAIS SAMIA AWATAKA VIONGOZI WALIOTEULIWA NA KUAPA WAENDE WAKATEKELEZE KWA KUKIHESHIMU KIAPO HICHO AMBACHO KIPO KWA AJILI YA THAMANA YA KULITUMIKIA TAIFA KIUDILIFU NA UAMINIFU KATIKA SAFARI ZAO ZA UONGOZI ILI WAKAYAFANYE YALIYOMEMA KWA KUWATUMIKIA WANANCHI WENYE IMANI YA UTENDAKJI NA NCHI YAO .

02/10/2022



WAJUMBE WAMUACHA MWENYEKITI WA ZAMANI WILAYANI NJOMBE WAENDA NA MWENYEKITI MPYA KATIKA UCHAGUZI MKUU WA CCM WILAYA 2022.

30/09/2022

RAIS SAMIA - "VIFAA HIVI VIKATUNZWE , ATANIELEZA ALIYEVINUNUA NA ALIYEVITUMIA KWANI NINI VIARIBIKE MAPEMA "

29/09/2022

JUMAA AWESO (WAZIRI WA MAJI) - " MSIJIITE TU MIMI MKURUGENZI WA MAJI HALAFU WATU MAJI HAWANA "

AMEYAZUNGUMZA HAYA WAKATI WA UZINDUZI WA BODI YA MAJI YA SITA BONDE LA RUVUMA NA PWANI YA KUSINI.

29/09/2022

RAIS SAMIA - " MIKATABA YOTE ITAKAYOINGIWA NA SERIKALI LAZIMA ISHIRIKISHE OFISI YA MWANASHERIA MKUU WA SERIKALI.

Address

Tanga
Muheza
8591

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when LikuNews posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share