03/02/2024
KATIBU WA HALMASHAURI KUU YA CCM TAIFA ITIKADI, UENEZI NA MAFUNZO AMPA KICHEKO BWANA YOHANA YUSUPH MKAZI WA KOROGWE MJINI KWA KUMPATIA KITI MWENDO CHA UMEME.
Katibu wa Halmashauri Kuu ya Chama cha Mapinduzi (CCM) Taifa Itikadi, Uenezi na Mafunzo Ndugu Paul Makonda ametimiza Ahadi yake kwa Kumpatia Kiti Mwendo cha Umeme Bwana Yohana Yusuph ambaye ni Mkazi wa Korogwe Mjini Mkoani Tanga .
Ahadi hiyo kutoka kwa Ndugu Paul Makonda aliitoa tarehe 21 Januari 2024 alipokuwa kwenye Mkutano wa hadhara katika Viwanja vya Mpira Sokoni Manundu .