NLGCC TV

NLGCC TV Arch Bishop & Founder
Of (NLGCC) New Life Gospel Community Church - TZ
Through The Word Of God

26/01/2025
07/11/2024

Tunaomba radhi kwa kukatika matangazo jana katika ibada ya Jumapili.Tunajitahidi kuhakikisha kuwa utaweza kujiunga nasi moja kwa moja wiki ijayo katika ibada zetu.
Tunakupenda na kukusherehekea.






04/11/2024

Don't miss next Sunday, April 14, 2024 for another time to meet in God's presence.

Invite your loved ones to join us and continue
with us for faith-building content throughout the week, on our social media platforms.
God bless you!

See you next week!

April 2024 Holy Ghost Service

KIRI PAMOJA NAMI MAOMBI HAYA KWA IMANI • Baba Mungu katika jina la Yesu; nakwenda kinyume na mapepo yote ambayo shetani ...
08/09/2024

KIRI PAMOJA NAMI MAOMBI HAYA KWA IMANI

• Baba Mungu katika jina la Yesu; nakwenda kinyume na mapepo yote ambayo shetani ameyatuma kusababisha matatizo katika maisha yangu. Mapepo yoyote yaliyotumwa kusababisha kutokuelewana kati yangu na jirani yangu, kati yangu na mke au mme wangu, kati yangu na rafiki zangu, mimi na familiya yangu, ninao wajua au nisiowajua.

• Nawakemea na kuwafunga mapepo hao popote mlipojificha. Naachilia moto wa Roho Mtakatifu kuyaharibu katika nguvu ya jina la Yesu.

• Nashambulia kila nguvu ya mapepo yaliyotumwa kusababisha magonjwa maishani mwangu mwaka huu. Imaandikwa katika kitabu cha kutoka 23:25-26 “Nanyi mtamtumikia Bwana, Mungu wenu, naye atakibarikia chakula chako, na maji yako; nami nitakuondolea ugonjwa kati yako. Hapatakuwa na mwenye kuharibu mimba, wala aliye tasa, katika nchi yako; na hesabu ya siku zako nitaitimiza.”

• Nakemea na kuvunja mapepo yote ambayo yametumwa kusababisha magonjwa maishani mwangu na katika familia yangu. Nawaamuru ninyi mapepo wote makauke na magonjwa yenu mbalimbali. Naachilia moto wa Mungu na waharibu wote katika jina la Yesu. Amina.

Tunamshukuru Mungu kwa Ibada ya leo, Mungu akubariki uliyefika na wewe uliyeungana pamoja nasi kupitia YouTube channel y...
08/09/2024

Tunamshukuru Mungu kwa Ibada ya leo, Mungu akubariki uliyefika na wewe uliyeungana pamoja nasi kupitia YouTube channel yetu BISHOP DANIEL OUMA.

Waalike wapendwa wako wajiunge nasi na kuendelea pamoja nasi kwa maudhui ya kujenga imani wiki nzima, kwenye majukwaa yetu ya mitandao ya kijamii.

Hesabu 6:25 Bwana akuangazie nuru za uso wake, na kukufadhili.

Tutaonana wiki ijayo Mungu akubariki!!

Tune in and join me and thousands of people in learning the word of God live from NLGCC TV,Musoma.Unaweza ungana nami kw...
08/09/2024

Tune in and join me and thousands of people in learning the word of God live from NLGCC TV,
Musoma.

Unaweza ungana nami kwenye ibada yetu ya Jumapili.
Ubarikiwe na Bwana na

KARIBU UABUDU NASI KATIKA IBADA YA JUMAPILI HII || SEPT 08, 2024 || NLGCC-MUSOMA, MARA.Nuru mpya iangaze juu yako jioni ...
07/09/2024

KARIBU UABUDU NASI KATIKA IBADA YA JUMAPILI HII || SEPT 08, 2024 || NLGCC-MUSOMA, MARA.

Nuru mpya iangaze juu yako jioni ya leo, uone kila ambacho Mungu amekuandalia.

Welcome to NLGCC TV  Tune in andworship the Lord with us
01/09/2024

Welcome to NLGCC TV Tune in and
worship the Lord with us

KUELEKEA DPPJ 2024Ujumbe Toka Kwa AskofuNew Life Gospel Community ChurchSababu 12 zinazotupa jukumu la kuomba Kwa ajili ...
31/08/2024

KUELEKEA DPPJ 2024
Ujumbe Toka Kwa Askofu
New Life Gospel Community Church

Sababu 12 zinazotupa jukumu la kuomba Kwa ajili ya Amani ya Israeli

Kuna sababu nyingi, sababu zisizo na mashaka zipatikanazo katika Biblia. Kimsingi leo tutaona kwa nini tunapaswa kuombea amani ya Israeli na kwa watu waliochaguliwa na Mungu yaani Wayahudi. Sababu ambazo sisi k**a Wakristo hatuwezi kuzipuuza; kwani sababu nyingine zina maana ya unabii.

Sababu 12 zisizokuwa na shaka.

1. Mungu anatuamuru tufanye hivyo. Katika Zaburi 122: 6, Mungu kupitia Daudi anatuambia,"Utakieni Yerusalemu amani; Na wafanikiwe wakupendao." Yerusalemu haiko Kenya wala Saudi Arabia iko katika Israeli hata k**a kwa hila mtu akipinga.

2. Kwa kufuata mifano ya wengine ambao waliiombea. Zaburi 25:22 inasema, "Ee Mungu, umkomboe Israeli, Katika taabu zake zote/shida yake yote." (Soma pia 51: 18-19; 137: 6-7; Rom 10: 1.)

3. Kwa hiyo kwa maombi yako, watu wake watakuwa na amani na mafanikio. Zaburi 122: 8: "Kwa ajili ya ndugu zangu na rafiki zangu Niseme sasa, Amani ikae nawe.'"

4. Kwa ajili ya wokovu wao. "Ndugu zangu, nitakayo sana moyoni mwangu, na dua yangu nimwombayo Mungu, ni kwa ajili yao, ili waokolewe/kwa ajili ya wokovu wao" (Warumi 10: 1).

5. Kwa sababu wao (Wayahudi) ni watu maalum wa Mungu. Katika Kumbukumbu la Torati 32:10 inasema, Alimkuta katika nchi ya ukame, Na katika jangwa tupu litishalo; Alimzunguka, akamtunza; Akamhifadhi k**a mboni ya jicho;

Tena, katika Kumbukumbu la Torati 14: 2 Mungu anasema juu ya Wayahudi, "Kwa kuwa u taifa takatifu kwa Bwana, Mungu wako, na Bwana amekuchagua kuwa watu wake hasa, kuliko mataifa yote yaliyo juu ya uso wa nchi."

6. Kuleta agano la Mungu la amani. Ezekieli 37:26 "Tena nitafanya agano la amani pamoja nao; litakuwa agano la milele pamoja nao; nami nitawaweka na kuwazidisha, na patakatifu pangu nitapaweka katikati yao milele."

7. Ili kusudi serikali yake (hasa katika milenia) ipate kuwa serikali ya amani.
Isaya 9: 7 Maongeo ya enzi yake na amani Hayatakuwa na mwisho kamwe, Katika kiti cha enzi cha Daudi na ufalme wake; Kuuthibitisha na kuutegemeza Kwa hukumu na kwa haki, Tangu sasa na hata milele. Wivu wa Bwana wa majeshi ndio utakaotenda hayo.


8. Kwa sababu ni makazi/maskani ya Mungu wa amani hapa duniani.
Isaya 9: 6 Maana kwa ajili yetu mtoto amezaliwa, Tumepewa mtoto mwanamume; Na uweza wa kifalme utakuwa begani mwake; Naye ataitwa jina lake, Mshauri wa ajabu, Mungu mwenye nguvu, Baba wa milele, Mfalme wa amani.

9. Mungu anaahidi baraka kwa wale wanaowabariki Israeli. Mwanzo 12: 3 Nami nitawabariki wale wanaokubariki, Na mtu atakayekulaani nitamlaani. Na ndani yenu jamaa zote za dunia zitabarikiwa. "(Soma pia Hes. 24: 9; Zab 122: 6).

10. Tumeitwa kuwa watetezi. Mathayo 5: 9 inasema, "Heri wapatanishi; Maana hao wataitwa wana wa Mungu."

11.Tumeamriwa kuwa na amani na wote. Warumi 12:18 inasema, "Ikiwezekana, kwa kadiri inategemea wewe, kuwa na amani na watu wote."

12. Sisi kanisa tuna wajibu wa Israeli. Sisi kanisa tuna uhusiano wa kipekee na Israeli. Tumeunganishwa kwenye mzabibu wao na tunapata ahadi zao za kiroho. Kwa hakika tunawajibika kwao (Warumi 11).

KWA NINI LEO TUSIMAME NA ISRAELI?

Israeli ni nchi ambayo kwayo Mungu husema Ki-pekee, Ki-unabii, Ki-ukombozi, na kujirudia katika biblia akisema “Huyu ni Wangu.” Mungu anairejea Israeli kimaelezo tofauti na nchi yoyote duniani. Neno la Mungu lawaita Wayahudi kuwa “shina” na mataifa yanaitwa “Matawi.” Kwa muda tumekumbushwa vivyo “kwa sababu ya kutokuamini, wengine wao walivunjika na mkasimama mahala pao kwa Imani,” Hatustahili kujivunia hili bali tuogope: “Kwa maana ikiwa Mungu hakuyaachia matawi ya asili, wala hatakuachia wewe.” Patakapokamilika uaminifu wa Mataifa, “Hivyo Israeli wote wataokoka.” (mst. 11:16-27)

• Mungu aliwachagua kwa makusudi: “…ambao ni Waisraeli, wenye kule kufanywa wana, na ule utukufu, na maagano, na kupewa torati, na ibada ya Mungu, na ahadi zake; ambao mababu ni wao, na katika hao alitoka Kristo kwa jinsi ya mwili. Ndiye aliye juu ya mambo yote, Mungu, mwenye kuhimidiwa milele. Amina.” (Warumi 9:4)

Kimsingi, maandiko husema nasi wazi kabisa: twashughulika na mashina ya kila kitu kinachohusiana na ufunuo wa Mungu kwa binadamu. Uthibitisho wa hili uko katika ule uwepo wa Wayahudi k**a watu na ukweli kwamba wamepata kuponywa k**a taifa. Leo hii mapambano yako juu ya Yerusalemu, dhidi ya Israeli, na kinyume cha uwepo wa Wayahudi na haki yao k**a wengine kuwa na nchi. Yapo mataifa machache yaliyokubali kufanya mafungamano ya kujitoa kusimama na Wayahudi na Israeli, bali Mungu anaahidi kuwaheshimu watakaofanya hivyo.

• Maandiko yanaazimia kuwa, katika roho, unapompokea Bwana, unafanyika kuwa Myahudi (Warumi 2:28-29; Wagalatia 3:26-29).

• Ikiwa wewe ni mwenye kuamini, basi hautashupaza shingo dhidi ya jumla ya maandiko yawahusuyo Wayahudi na Israeli.

• Mambo ya Walawi 25:23 – Nchi ni ya Bwana, na imedhihirishwa kutokupotezwa wala kuuzwa pale asemapo: “Nayo nchi haitauzwa kabisa kabisa; kwani nchi ni yangu mimi;…”

• Kumbukumbu 32:43 – “Furahini, enyi mataifa, pamoja na watu wake;…atafanya kafara kwa nchi yake, na watu wake.”

• 2 Mambo ya Nyakati 7:20 – Mungu anasema kuwa wakiniasi Mimi “…Nitawang’oa katika nchi yangu niliyowapa…”

• Zaburi 85:1-2 – “Bwana umeiridhia (umependelea) nchi yako, umewarejeza mateka wa Yakobo (Israeli). Umeusahau uovu wa watu wako, umezisitiri hatia (Dhambi) zao zote.”

• Isaya 8:8 – Nchi hii ni milki ya Baba Mungu na ni nchi ya Masihi wake: “…na kule kuyanyoosha mabawa yake kutaujaza upana wa nchi yako, Ee Imanueli.”

• Yeremia 2:7 – Bwana anawaambia watu kwa nini patatokea upotevu, kuangamia kwa mji wa Yerusalemu. “Nami nikawatia katika nchi ya shibe…lakini ninyi mlipoingia katika nchi ile, mliitia unajisi nchi yangu, na urithi wangu mliufanya kuwa chukizo.”

• Ezekieli 38:16 – Mungu anasema na watu wa nyakati za mwisho watakaoinuka kinyume na Israeli. Mungu anasema juu ya majibizano yatakayofanyika katika nchi yake. “Nawe utapanda juu uwajilie watu wangu, Israeli,….nitakuleta upigane na nchi yangu, ili mataifa wanijue, nitakapotakaswa kwako…”

• Yoeli 1:6, 2:18, 3:2 – Mara tatu katika kitabu hiki, nchi inarejewa k**a milki ya Bwana. “Maana taifa limepanda juu ya nchi yangu…” (1:6) “Hapo ndipo Bwana alipoona wivu kwa ajili ya nchi yake…” (2:18) “Nitakusanya mataifa yote, nami nitawaleta chini katika bonde la Yehoshafati, na huko nitawahukumu kwa ajili ya watu wangu, kwa ajili ya urithi wangu Israeli, ambao wamewatawanya kati ya mataifa, na kuigawanya nchi yangu.” (3:2)

• Hosea 9:3 – Hili linarejea katika kutawanyika kwa Israeli: “Hawatakaa katika nchi ya Bwana; lakini Efraimu atarudi Misri, nao watakula chakula kinajisi katika Ashuru.”

• Zekaria 9:16 – “Na Bwana, Mungu wao, atawaokoa siku hiyo, k**a kundi la watu wake; kwa maana watakuwa k**a vito vya taji, vikainuliwa k**a Bendera juu ya nchi yake…”

Tunapozungumzia kuihusu Israeli, tunakabiliana na: 1) Kipande cha mali ambacho Mungu amekifanyia agizo kukihusu 2) Watu wa Mungu waliopewa nchi.

Ni jambo kubwa kwake yeye aliye muumba wa vyote, hili halina mjadala. Mambo ambayo Mungu ameyasema, kipekee, kuihusu Israeli hayajawahi kubatilishwa.

• Siyo tu kwamba nchi ni milki ya Mungu, lakini pia Mungu amemkabidhi Abraham nchi, kupitia kwa uzao wa Isaka, siyo kwa muda, bali kapewa milele. (Mwanzo 17:7-8)

• “Kwa kitambo kidogo nimekuacha (nimekuficha uso wangu)…lakini, kwa fadhili za milele nitakurehemu, wala agano langu la Amani halitaondolewa…” (Isaya 54:8-10)

• Upotevu wa Israeli kutawaliwa kutokana na dhambi na kutawanyika kwao hakujauondolea mbali msimamo wa maagano ya Mungu ya milele (Ezekieli 37:1-28)

Bishop Daniel & Debra Ouma
Bonde la Baraka - Musoma

Utokapo kwenda vitani kupigana na adui zako, na kuona farasi, na magari, na watu wengi kuliko wewe, usiwaogope; kwa kuwa...
29/08/2024

Utokapo kwenda vitani kupigana na adui zako, na kuona farasi, na magari, na watu wengi kuliko wewe, usiwaogope; kwa kuwa Bwana Mungu wako, yu
pamoja nawe, aliyekukweza kutoka nchi ya Misri.
-Kumb 20:1
+

Address

Kigera
Musoma

Opening Hours

Wednesday 22:00 - 12:00
Sunday 09:00 - 20:00

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when NLGCC TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category