JOHANESmedia

JOHANESmedia Johanes Media,ni media itayokuhabarisha habari mbalimbali za NENO LA MUNGU, na Matangazo ya Moja kwa � � � � � � � � � � � � � � � � � �

KARIBU KWENYE SEMINA YA KUPANDA NA KUVUNA TAREHE 17 JAN 2021 KUANZIA SAA SABA KAMILI MCHANA MPAKA SAA KUMI NA MBILI JION...
12/01/2021

KARIBU KWENYE SEMINA YA KUPANDA NA KUVUNA TAREHE 17 JAN 2021 KUANZIA SAA SABA KAMILI MCHANA MPAKA SAA KUMI NA MBILI JIONI.

MWALIMU ATAFUNDISHA

USISAHAU MAHALI NI DIAMOND JUBILEE, UPANGA JIJIJI DAR ES SALAAM.

12/01/2021
Wana wa Israel walipokuwa katika Safari ya kuelekea Kaanani kikwazo cha kwanza kilichokuwa mbele yao ilikuwa ni Bahari y...
12/01/2021

Wana wa Israel walipokuwa katika Safari ya kuelekea Kaanani kikwazo cha kwanza kilichokuwa mbele yao ilikuwa ni Bahari ya Shamu. Watu wengi wanapoendelea na Safari hii ya Wokovu kikwazo cha kwanza wanachokutana nacho ni Bahari ya Shamu ambayo inasababisha wengi kuahirisha Safari zao na hatimaye adui zao kuweza kuwapata kwa urahisi. Unapaswa kutambua kuwa hakuna njia ya mkato wala njia ya kuzunguka bali unatakiwa upite katikati kwenye hiyo Bahari ya Shamu ili uweze kufika Kaanani yako yaani kule ambapo Mungu amekuandalia Baraka zako.

Kwa nini unatakiwa kuivuka hiyo bahari? Kwa sababu Mungu anataka amalizane na adui zako ndani ya hayo maji ili usiwaone tena.

Mwaka huu wa 2021 ni wa KUENDELEA MBELE Mwanangu usiruhusu chochote kikuzuilie, anza kutembea sasa; Usiruhusu chochote kikurudishe nyuma.

© MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA – KANISA LA EFATHA.

JUMATATU YAKO IMEBARIKIWA. Furahi Mwanangu, Mambo yaliyokuwa yanakuvuta Nyuma hayatakuwepo tena.MUNGU Anakupenda na Mimi...
11/01/2021

JUMATATU YAKO IMEBARIKIWA.

Furahi Mwanangu, Mambo yaliyokuwa yanakuvuta Nyuma hayatakuwepo tena.

MUNGU Anakupenda na Mimi Nakupenda, uko Mahali SALAMA.

#🇪 🇫 🇦 🇹 🇭 🇦 🇨 🇭 🇺 🇷 🇨 🇭
#🇯 🇴 🇭 🇦 🇳 🇪 🇸 𝕞𝕖𝕕𝕚𝕒

SOMO:ONDOA VIZUIZI2) Mipaka ya kibinadamu (udhaifu)Kutoka 4:10 " Musa akamwambia Bwana Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea ...
10/01/2021

SOMO:ONDOA VIZUIZI

2) Mipaka ya kibinadamu (udhaifu)
Kutoka 4:10 " Musa akamwambia Bwana Ee Bwana, mimi si msemaji, tokea zamani, wala tokea hapo uliposema na mtumishi wako; maana mimi si mwepesi wa kusema, na ulimi wangu ni mzito. "

Udhaifu unaoujua na usioujua unaweza kuwa kizuizi kwako, na kizuizi kinakunyima uwezo wa kujua na namna ya wewe kumuamini Mungu.
Neno la Mungu likiwa taa/nuru ndani yako linakuonyesha udhaifu ulionao. Tambua kwanza udhaifu ulionao na kisha utambue nguvu ya Mungu ndipo Mungu ataweza kuuondoa udhaifu huo.
Kulijua neno sio kujua mistari ya biblia bali ni kuliishi neno.

Unapokuwa katika kizuizi hiki cha mipaka ya kibinadamu muda wote unawaza ni nani atakuletea. K**a unapenda sana kulala ujue kuwa wewe ni mvivu.

3) Mambo yaliyopita (mambo ya nyuma)
Mwanzo 11:26-32 " Tera akaishi miaka sabini, akamzaa Abramu, na Nahori, na Harani."

Inawezekana kabisa mambo yaliyopita yakawa kizuizi kwako kwasababu ya mambo maovu. Acha mambo maovu na uamue kutembea na Mungu.
Unaweza kusema kuwa wewe haupo huko lakini ni mpaka uamue kutoka hapo na kweli ya Mungu iwe na wewe ndipo utaweza kusonga mbele.

4) Kizuizi cha mipaka unayojiwekea wewe mwenyewe.
Kizuizi hiki kina vipengele viwili
a) Mawazo yako
Zaburi 19:14 " Maneno ya kinywa changu, Na mawazo ya moyo wangu, Yapate kibali mbele zako, Ee Bwana, Mwamba wangu, na mwokozi wangu."
K**a wewe unajiwazia vibaya ndilo litakalopata kibali mbele za Mungu. Mfano unajiwazia kushindwa ndilo litakalopata kibali mbele za Mungu. Unapowaza mawazo mazuri panakuwepo na amani.
K**a kuna kitu cha kumwambia Mungu mwambie akili yake ikae na wewe maana akili yako ikiwa na akili ya Mungu mawazo yako yatakuwa ya kimungu na ukiwa na akili ya kibinadamu siku zote utawaza mambo mabaya tu.

b) Maneno ya kinywa chako
Ili maneno yako yasiwe na kizuizi wewe angalia neno la Mungu linasema nini na sio maneno yako.
Mwenye kuondoa kizuizi ni wewe mwenyewe, hivyo jitamkie vizuri, jiwazie vizuri juu ya alichosema Mungu kwenye neno lake.

SOMO:ONDOA VIZUIZIUnapokutana na kizuizi mbele yako usimnung’unikie kiongozi wako maana sio yeye aliyeweka hicho kizuizi...
10/01/2021

SOMO:ONDOA VIZUIZI

Unapokutana na kizuizi mbele yako usimnung’unikie kiongozi wako maana sio yeye aliyeweka hicho kizuizi bali muulize yeye awezaye kuondoa vizuizi.
Unachohitajika kufanya ni kuyaweka maisha yako mikononi mwa Mungu, usiweke maisha yako kwa mtu mwingine maana ni Mungu pekee ndo awezaye kuondoa hivyo vizuizi.

AINA ZA VIZUIZI
1) Kizuizi cha mazoea
K**a hutafahamu kuwa kina kizuizi cha mazoea kimesimama mbele yako, hutaweza kufika unapotakiwa kufika na hutamiliki unachotakiwa kumiliki.
Kizuizi cha mazoea kinatokana na muingiliano wa maisha yetu ya kila siku hivyo kitakufanya wewe ufanye mambo ya Mungu kwa mazoea. Badala ya kufanya jambo sawasawa na neno la Mungu unaanza kuwa na hoja.

Hiki ni kizuzizi ambacho shetani amekificha ndani yake hivyo k**a hutajua sio rahisi kutoka hapo. Na ili uweze kung’aa na ufike pale ulipokusudiwa kufika ni lazima ukiondoe hicho kizuizi.

Mwanzo 12:1 " Bwana akamwambia Abramu, Toka wewe katika nchi yako, na jamaa zako, na nyumba ya baba yako, uende mpaka nchi nitakayokuonyesha;"

Usipotoka kwenye hicho kizuizi cha mazoea laana ipo, na ukitoka kwenye hicho utaelekea kunako Baraka zako.
PRISCA .A. KILYA

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 10 JANUARY 2021, KANISA LA EFATHA KILOMBEROMCHUNGAJI PRISCA .A. KILYASOMO:ONDOA VIZUIZIKatika s...
10/01/2021

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 10 JANUARY 2021, KANISA LA EFATHA KILOMBERO
MCHUNGAJI PRISCA .A. KILYA

SOMO:ONDOA VIZUIZI
Katika safari hii ya imani, tunapotembea, kuna vizuizi vingi k**a ambavyo wana wa Israel walipokutana navyo lakini sisi tumetamkiwa neno kwamba pamoja na vizuizi lakini usilie, songa mbele, tumia fimbo yako kugawa bahari iliyop mbele yako ili upate kuvuka.

Isaya 54:1-4 “ Imba, wewe uliye tasa, wewe usiyezaa; paza sauti yako kwa kuimba, piga kelele, wewe usiyekuwa na utungu; maana watoto wake aliyeachwa ni wengi kuliko watoto wake yeye aliyeolewa, asema Bwana.
2 Panua mahali pa hema yako, na wayatandaze mapazia ya maskani yako; usiwakataze; ongeza urefu wa kamba zako; vikaze vigingi vya hema yako.
3 Kwa maana utaenea upande wa kuume na upande wa kushoto; na wazao wako watawamiliki mataifa; wataifanya miji iliyokuwa ukiwa kukaliwa na watu.
4 Usiogope; maana hutatahayarika; wala usifadhaike; maana hutaaibishwa; kwa kuwa utaisahau aibu ya ujana wako, pia mashutumu ya ujane wako hutayakumbuka tena."

Unapoambiwa imba maana yake ufurahi na utanue mapana yako ili upate kile unachostahili.
Ni lazima kwanza ujue kizuizi chako ni kipi na ndipo uimbe na wakati huo ukiwa unajua ni nani aliye mtetezi wako.

Wimbo wa furaha hauwezi kuimba mpaka ujue ni kipi kinachokusumbua, ni kipi kizuizi chako cha kuikamilisha furaha yako.
Mfano:- Binti au mama aliyeolewa halafu hana mtoto ni lazima ajue ni kwanini yeye ni tasa ili aweze kuondoa kizuizi hicho na ndipo aweze kuimba.
Ni lazima ujue kizuizi ni nini na umjue yule anayeweza kukiondoa kizuizi hicho na inawezekana unamjua lakini humuamini k**a yeye anaweza kuondoa hicho kizuizi, Hakuna kitakachofanyika. Amua kumuamini ili kizuizi kiondoke kwako.

Usiangalie vizuizi na mazingira, yani ukishajua kizuizi chako ni nini wewe kiache na usonge mbele. Maana ukishakijua kizuizi inakuja hofu lakini ukishamjua aliyekuwa anakutishia wewe songa mbele ukifurahi maana Mungu atafanya.
PRISCA .A. KILYA

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 10 JANUARY 2021, KANISA LA EFATHA KILOMBEROMCHUNGAJI PRISCA .A. KILYAKuwepo hemani mwa Bwana ni...
10/01/2021

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 10 JANUARY 2021, KANISA LA EFATHA KILOMBERO
MCHUNGAJI PRISCA .A. KILYA

Kuwepo hemani mwa Bwana ni neema , hivyo unapokuwepo, mshukuru Bwana maana amekuandalia jambo jema.

Mungu wetu anahitaji kutufanikisha pale alipotukusudia na ndio maana tumeambiwa ni mwaka wa kusonga mbele maana ameshatutambulisha mwaka 2020. Hivyo mwaka huu ni mwaka wa kuanza safari, wana wa Israel walipoanza safari alikuwa na lengo la kutupeleka kaanani, kanani yako iko mbele yako hivyo anza safari kuelekea kaanani yako.

Ili kuifikia Kaanani kuna bahari, lakini hiyo isikurudishe nyuma bali songa mbele.
Wana wa Israel walipoanza safari ilibidi wawe watii, waaminifu na wawe tayari kujitoa kwa kile wanachoelekezwa. Lakini kabla hawajaanza safari, walitambulishwa katika nchi ya Misri kwa kuambiwa waweke alama katika miimo ya milango yao. Na ndipo sasa baada ya kutambulika walipata kuanza safari yao ya kuelekea Kaanani.

Kwako wewe muimo umeshapita na umeingia kwenye kuanza safari maana Mungu wa Efatha anataka akutufikishe pale alipotukusudia.
MIMI NIMEKUSUDIWA KUSONGA MBELE, HIVYO NAHITAJI KUWA MTII, MUAMINIFU NA MTU WA KUJITOA KWA AJILI YA KUANZA SAFARI YA KWENDA KAANANI.

Wimbo huu wa pastor philipo, sasa upo youtube, boomplay n.k, so gusa link hapa chini kusikiliza mwanzo mwishooo.Ukiutaka...
10/01/2021

Wimbo huu wa pastor philipo, sasa upo youtube, boomplay n.k, so gusa link hapa chini kusikiliza mwanzo mwishooo.

Ukiutaka nicheki kwa 0788644312 nikutumie
By:JOHANES SAMWEL NYAHORI
JOHANESmedia
johanessamwelnyahori



Philipo Mollel

Karibu kutazama yana mwisho Lyrics.Macho Yangu Yaone Ukuu Wa Mungu Nione Kubarikiwa Juu Yangu Niuone Uwepo Wake Mbele YanguNipokee Uponyeji Wake Ndani Yangu...

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA - KANISA LA EFATHA MWENGE.Ni rahisi kujua mambo ya Mungu k**a utaruhusu kuzingati...
10/01/2021

MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA - KANISA LA EFATHA MWENGE.

Ni rahisi kujua mambo ya Mungu k**a utaruhusu kuzingatia katika kumpendeza YEYE. Kamwe hautaangamia kwa maradhi, magonjwa, moto wala ajali au kwa niaba ya mwingine bali utatimiliza siku zako.

Jifunze namna ya kupanda mambo katika roho kwa sababu utakapopanda katika roho utakuwa na furaha ndani yako wakati wote.

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 10/1/2021 KANISA LA EFATHA MWENGEMTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA 1Wakoritho 2:12 “ Lakin...
10/01/2021

IBADA YA JUMAPILI TAREHE 10/1/2021 KANISA LA EFATHA MWENGE
MTUME NA NABII JOSEPHAT ELIAS MWINGIRA

1Wakoritho 2:12 “ Lakini sisi hatukuipokea roho ya dunia, bali Roho atokaye kwa Mungu, makusudi tupate kuyajua tuliyokirimiwa na Mungu.” Tunapaswa kujua yale ambayo Mungu ametukirimia, karama uliyopewa inatoka kwa Mungu, ili kujua nini umekirimiwa kwanza kabisa ijue Roho ya Mungu na utendaji wake wa kazi, katika kujua unatakiwa uijue Biblia, hakikisha unaisoma Biblia vizuri.

Kuna vitu ambavyo Mungu ameviandaa kwa ajili yetu viko mahali fulani, usiishi k**a watu wa dunia bali unapaswa uishi sawa sawa na Roho wa Mungu ili akuwezeshe kuyajua hayo.

1Wakorintho 2:13-14 “Nayo twayanena, si kwa maneno yanayofundishwa kwa hekima ya kibinadamu, bali yanayofundishwa na Roho, tukiyafasiri mambo ya rohoni kwa maneno ya rohoni. Basi mwanadamu wa tabia ya asili hayapokei mambo ya Roho wa Mungu; maana kwake huyo ni upuzi, wala hawezi kuyafahamu, kwa kuwa yatambulikana kwa jinsi ya rohoni.” unapo soma Biblia k**a kuna mstari au neno usilolielewa roho atakufafanushia.

Wale wanaoishi katika tabia za asili kamwe hawatapokea mambo ya roho, hii inamaana kuwa k**a utaendelea kutunza mambo yaliyopita kamwe hautaweza kupokea mambo mengine. Jambo la muhimu hapa siyo watu wanasema nini au nani kafanya nini, soma Biblia na uelewe kile Mungu amekusudia kwako ndivyo utaweza kupokea mambo ya rohoni lakini ukiyaangalia yaliyopita kamwe hautaweza kwenda mbele.

Hivyo hakikisha unaondoa uchungu ndani yako maana k**a hutauondoa utakupelekea kupata magonjwa.

Address

Mwanza
P.O.BOX103

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when JOHANESmedia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share