Jembefmtz

Jembefmtz Jembe FM was created with one goal in mind: to bring the world’s most popular music and creative

Jembe FM imepata nafasi ya kuzungumza na mwanamke Jembe SUKI'S CRAFTS mwanamke mlemavu shupavu anayejishughulisha na  sa...
04/09/2026

Jembe FM imepata nafasi ya kuzungumza na mwanamke Jembe SUKI'S CRAFTS mwanamke mlemavu shupavu anayejishughulisha na sanaa ya utengenezaji wa vitu mbalimbali vya asili anayepatikana Mwanza.

Akizungumza na Jembe FM baada ya kumtembelea kwenye banda lake katika viwanja vya Furahisha, SUKI'S CRAFTS amezungumzia juu ya watu kuacha utegemezi kwa familia na ndugu bali kufanya kazi kwa bidii bila kujali hali waliyonayo hasa ulemavu kwa watu wote hasa walemavu.

Jembe FM imepata nafasi ya kuzungumza na mwanamke Jembe SUKI'S CRAFTS mwanamke mlemavu shupavu anayejishughulisha na  sa...
04/09/2026

Jembe FM imepata nafasi ya kuzungumza na mwanamke Jembe SUKI'S CRAFTS mwanamke mlemavu shupavu anayejishughulisha na sanaa ya utengenezaji wa vitu mbalimbali vya asili anayepatikana Mwanza.

SUKI'S CRAFTS ametoa ushauri kwa watu wote hasa walemavu kujituma na kujishughulisha alipozungumza na Jembe FM kwenye banda lake katika uwanja wa Furahisha kwenye maonyesho ya 21 ya kibiashara ya Afrika Mashariki.

Follow Us On Social Media
‎Instagram - Jembe Fm
‎Facebook - Jembe Fm
‎X(Twitter) - Jembe Fm
‎TikTok - Jembe Fm
‎Thread - Jembe Fm




Wazazi na walezi wametakiwa kupunguza ubize wa shughuli zao na kutenga muda wa kukaa karibu na watoto wao.Wito huo umeto...
04/09/2026

Wazazi na walezi wametakiwa kupunguza ubize wa shughuli zao na kutenga muda wa kukaa karibu na watoto wao.

Wito huo umetolewa na Katibu wa Seneti ya vyuo na vyuo vikuu Mwanza, Maua Sabasaba Sarungi, akizungumza na waandishi wa habari Mwanza ameeleza kuwa ukaribu huo ni nguzo muhimu katika kubaini changamoto za watoto na kuwapatia msaada unaofaa kwa wakati.

Kiongozi huyo amebainisha kuwa watoto wengi kwa sasa wanakabiliwa na msongo mkubwa wa mawazo na changamoto za kisaikolojia kwa kukosa msaada na ukaribu kutokana na migogoro ya ndoa pamoja na ukosefu wa ushirikiano wa karibu kutoka kwa wazazi.

Athari za matatizo haya zimekuwa zikishusha maendeleo ya kitaaluma na hata kupelekea baadhi ya wanafunzi kuacha shule kabisa.
Ni wajibu wa kifamilia kuhakikisha watoto wanakingwa dhidi ya madhara haya ili kulinda ustawi na afya zao za akili.

Kutokana na hali hiyo, Sarungi ameishauri Serikali kuongeza juhudi za kuajiri wataalamu wa saikolojia katika taasisi za elimu ambapo wataalamu hao watasaidia kutoa unasihi kwa wanafunzi kuanzia ngazi ya shule za msingi hadi vyuo vikuu nchini kote juu ya uhalisia wa maisha na mabadiliko ya ulimwengu unavyokwenda.

Follow Us On Social Media
‎Instagram - Jembe Fm
‎Facebook - Jembe Fm
‎X(Twitter) - Jembe Fm
‎TikTok - Jembe Fm
‎Thread - Jembe Fm




04/09/2026
Watu wawili wameokolewa wakiwa hai nchini Nepal baada ya kukaa chini ya kifusi kwa muda wa siku tisa kufuatia tetemeko k...
04/09/2026

Watu wawili wameokolewa wakiwa hai nchini Nepal baada ya kukaa chini ya kifusi kwa muda wa siku tisa kufuatia tetemeko kubwa la ardhi lililotokea hivi karibuni.

Vikosi vya uokoaji vilifanikiwa kuwatoa watu hao jana jioni huku umati mkubwa wa wananchi ukishuhudia tukio hilo la miujiza. Manusura hao walikuwa wamekwama kwenye mabaki ya jengo la ghorofa lililoanguka vibaya mjini Kathmandu.

Madaktari waliowapokea wameeleza kuwa manusura hao wana hali nzuri kiafya licha ya kukabiliwa na upungufu mkubwa wa maji na msh*tuko wa kisaikolojia. Walilazimika kunywa maji yaliyokuwa yakichuruzika kutoka kwenye mabomba yaliyopasuka ili kuweza kuishi kwa siku zote hizo tisa.

Ndugu na jamaa zao wamefurahi kupita kiasi baada ya kupoteza matumaini ya kuwapata wakiwa hai.Zoezi la utafutaji linaendelea nchini humo huku mamlaka zikisema bado kuna matumaini madogo ya kupata manusura wengine maeneo ya vijijini.

Changamoto kubwa inayokabili waokoaji kwa sasa ni hali mbaya ya hewa na barabara zilizofungwa na maporomoko ya ardhi.

Jamii ya kimataifa inaendelea kutuma misaada ya kibinadamu na vifaa vya kisasa ili kurahisisha kazi hiyo.

Follow Us On Social Media
‎Instagram - Jembe Fm
‎Facebook - Jembe Fm
‎X(Twitter) - Jembe Fm
‎TikTok - Jembe Fm
‎Thread - Jembe Fm




Mkuu wa idara ya habari na Mawasiliano wa klabu ya Singida Black Stars Hussein Massanza amepigwa faini ya milioni  10 za...
04/09/2026

Mkuu wa idara ya habari na Mawasiliano wa klabu ya Singida Black Stars Hussein Massanza amepigwa faini ya milioni 10 za kitanzania kwa kosa la chapisha taarifa ya kumshutumu na kutoa lugha ya matusi kwa mwamuzi wa mchezo wa ligi kuu kati ya Singida BS dhidi ya Simba SC

Mchezo uliotamatika kwa klabu ya Simba kuibuka na ushindi wa mabao mawili kwa moja kwenye uwanja wa Airtel mkoani Singida.

Follow Us On Social Media
‎Instagram - Jembe Fm
‎Facebook - Jembe Fm
‎X(Twitter) - Jembe Fm
‎TikTok - Jembe Fm
‎Thread - Jembe Fm




Kampuni ya Ndege ya Air Tanzania (ATCL) imetangaza kusitisha kwa muda safari zake za ndege kwenda nchini Urusi uamuzi hu...
03/09/2026

Kampuni ya Ndege ya Air Tanzania (ATCL) imetangaza kusitisha kwa muda safari zake za ndege kwenda nchini Urusi uamuzi huo umeanza kutekelezwa rasmi kuanzia tarehe 04 Septemba mpaka taarifa ya kurejesha huduma itakaporejeshwa.

Safari hizo zilizosimamishwa ni zile zilizokuwa zikihusisha namba za ndege za TC422 na TC423.Hatua hii inahusu usafiri uliokuwa ukifanyika kati ya Dar es Salaam na Moscow.Sababu kuu ya kusitishwa kwa safari hizi ni kufanyika kwa tathmini ya kiusalama.

Tathmini hiyo inalenga kuangalia kwa karibu mazingira halisi ya uendeshaji wa ndege hizo,iongozi wa shirika wamesema usalama wa abiria na wafanyakazi unapewa kipaumbele cha juu.Hivyo, uamuzi huu ulichukuliwa ili kuepusha hatari zozote zinazoweza kujitokeza angani.

Abiria wote walioathiriwa na mabadiliko haya watapewa huduma stahiki bila usumbufu mkubwa,Watakaopenda wanaweza kupata marejesho kamili ya fedha zao za tiketi walizolipa.Pia, wateja wanaruhusiwa kubadilisha tarehe za safari zao kwa kadri watakavyohitaji.

Shirika litaendelea kutoa taarifa rasmi pindi safari hizo zitakapopangiwa kuanza tena.

Follow Us On Social Media
‎Instagram - Jembe Fm
‎Facebook - Jembe Fm
‎X(Twitter) - Jembe Fm
‎TikTok - Jembe Fm
‎Thread - Jembe Fm




Mwanaume mmoja jijini San Francisco nchini Marekani amesalimika kifo baada ya kukwama ndani ya gari la kubeba taka siku ...
03/09/2026

Mwanaume mmoja jijini San Francisco nchini Marekani amesalimika kifo baada ya kukwama ndani ya gari la kubeba taka siku ya Jumatano.

Dereva wa gari hilo la kampuni ya Recology alishtuliwa na sauti za mayowe ya mtu aliyekuwa akililia msaada kutoka ndani ya sehemu ya nyuma ya gari hilo la taka.

Inasemekana kuwa kabla ya tukio hilo, mwanaume huyo alikuwa akitafuta vitu au chakula kwenye p**a kubwa la taka kabla ya p**a hilo kuinuliwa na kumiminiwa ndani ya gari.

Kikosi cha wazima moto zaidi ya 20 cha San Francisco kilifika eneo la tukio mapema saa kumi alfajiri ili kuanza operesheni ya uokoaji.

Waokoaji hao walilazimika kuondoa rundo kubwa la takataka kwa mikono yao ili kufikia eneo ambalo mhanga huyo alikuwa amefukiwa.

Wakati zoezi hilo gumu likiendelea, wahudumu wa afya walifanikiwa kupenyeza na kumwekea mwanaume huyo mpira wa drip (IV) ili kuokoa maisha yake.

Follow Us On Social Media
‎Instagram - Jembe Fm
‎Facebook - Jembe Fm
‎X(Twitter) - Jembe Fm
‎TikTok - Jembe Fm
‎Thread - Jembe Fm




Upekee wa usindikaji na uandaaji wa asali Mariam Mbusa (Marinyazi honey) mkazi wa Igoma umemtambulisha k**a mwandaaji bo...
03/09/2026

Upekee wa usindikaji na uandaaji wa asali Mariam Mbusa (Marinyazi honey) mkazi wa Igoma umemtambulisha k**a mwandaaji bora na mashindi wa tuzo kwenye maonesho ya Afrika Mashariki ya 21 yanayoendelea kwenye viwanja vya Furahisha jijini Mwanza

Kufuatia utengenezaji wa asali ya kipekee amesema kuwa umekuwa ukichagizwa na kuwa na muda mrefu kwenye uandaaji na uuzaji wa bidhaa hiyo kwenye mkoa na jiji la Mwanza kwa zaidi ya miaka 10.

Follow Us On Social Media
‎Instagram - Jembe Fm
‎Facebook - Jembe Fm
‎X(Twitter) - Jembe Fm
‎TikTok - Jembe Fm
‎Thread - Jembe Fm




03/09/2026

Walimbwende kutoka kata 19 za Ilemela jijini Mwanza wanatarajiwa kuitikisa Ilemela ambapo mshindi wa kwanza akitarajiwa kutwaa milioni moja ,mshindi wa pili laki tano na Laki mbili na nusu kwa mshindi wa tatu Septemba 19,2026 The Breeze Complex - Mwanza.

Follow Us On Social Media
‎Instagram - Jembe Fm
‎Facebook - Jembe Fm
‎X(Twitter) - Jembe Fm
‎TikTok - Jembe Fm
‎Thread - Jembe Fm




Address

Jembe FM/Makongoro Road/Makongoro Street
Mwanza
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jembefmtz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jembefmtz:

Share

Category