Jembefmtz

Jembefmtz Jembe FM was created with one goal in mind: to bring the world’s most popular music and creative

Kocha timu ya  Issa Shabani akizungumza baada ya kupata sare na timu ya  kwenye mchezo wa ligi kuu ya wanawake Tanzania ...
14/05/2026

Kocha timu ya Issa Shabani akizungumza baada ya kupata sare na timu ya kwenye mchezo wa ligi kuu ya wanawake Tanzania bara ulimalizika kwa sare ya kufungana bao moja kwa moja.

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Kocha wa timu ya  Martinez akizungumzia mchezo wao na timu ya   mchezo uliotamatika kwa sare ya kufungana bao moja kwa m...
14/05/2026

Kocha wa timu ya Martinez akizungumzia mchezo wao na timu ya mchezo uliotamatika kwa sare ya kufungana bao moja kwa moja

Mchezo huo umepigwa kwenye uwanja wa Nyamagana jijini Mwanza .

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Klabu ya Pamba Jiji FC ya Mwanza imejikuta pambaya baada ya kupokea kichapo cha mabao mawili kwa bila kutoka kwa Azam FC...
14/05/2026

Klabu ya Pamba Jiji FC ya Mwanza imejikuta pambaya baada ya kupokea kichapo cha mabao mawili kwa bila kutoka kwa Azam FC kupitia mabao ya dakika za nyongeza ya 91 na 94 ya kifungwa mchezaji Feisal Salum

Kupitia mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Azam Complex Chamazi Pamba jiji inasalia na alama zake 30 katika nafasi ya nane huku timu ya Azam FC inafikisha alama 46 kwenye nafasi ya tatu ya ligi kuu baada ya kucheza michezo 23 kwa kila timu

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Michuano ya Fahari Super Cup msimu wa tano imeendelea kulindima kwenye uwanja wa Ngomeni Kisesa wilaya ya Magu mkoani Mw...
14/05/2026

Michuano ya Fahari Super Cup msimu wa tano imeendelea kulindima kwenye uwanja wa Ngomeni Kisesa wilaya ya Magu mkoani Mwanza katika hatua ya 32 bora kupigwa

Timu ya First Green FC ya Buswelu Ilemela imetupwa nje ya michuano hiyo na timu ya Watubaki FC ya Kanyama baada ya kuibuka na ushindi wa mabao matano kwa bila

Baada ya mchezo huo kupigwa Watubaki FC inakuwa timu ya sita kutinga kwenye hatua ya 16 bora ikiungana na timu za Talent boys,Zabona ,Cho cha Mipango,Mkemia na Chamalawana(Sabasaba).

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Klabu ya Simba imefufua upya matumaini ya kutwaa ubingwa wa michuano ya ligi kuu ya NBC Tanzania bara kufuatia ushindi w...
14/05/2026

Klabu ya Simba imefufua upya matumaini ya kutwaa ubingwa wa michuano ya ligi kuu ya NBC Tanzania bara kufuatia ushindi wa mabao mawili kwa bila dhidi ya Mashujaa FC

Baada ya ushindi wa leo klabu ya Simba inazidiwa alama mbili sasa na kinara wa ligi kuu ya NBC Tanzania bara klabu ya Yanga ikiwa na alama 54 huku Simba ikiwa na alama 52 kwwnye nafasi ya pili huku kila timu ikicheza michezo 23 na michezo saba ikisalia kwa kila timu.

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia na linaendelea kumhoji mchungaji wa Kanisa la Habari Njema, Kasese Gervas Bi...
14/05/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Geita linamshikilia na linaendelea kumhoji mchungaji wa Kanisa la Habari Njema, Kasese Gervas Bilalo (47), kwa tuhuma za kumuua mke wake, Martha Faustine (45).

Tukio hilo limebainika Mei 12, 2026 majira ya saa 6:00 mchana katika Kijiji cha Nyarututu, Kata ya Bwanga, Wilaya ya Chato, mkoani Geita, ambapo marehemu alikutwa amefariki ndani ya nyumba yao katika mazingira ambayo Jeshi la Polisi limebaini kuwa ni ya kutengenezwa. Uchunguzi wa awali umeonesha kuwa mtuhumiwa alimvizia mkewe akiwa amelala, kisha akamkaba shingoni kwa kutumia kamba ya katani kabla ya kumning’iniza juu ya kenchi ili tukio hilo lionekane k**a kujinyonga.

Chanzo cha tukio hilo kinadaiwa kuwa marehemu alikuwa akimtuhumu mumewe kuwa na mahusiano ya nje ya ndoa yao, hali iliyosababisha migogoro ya mara kwa mara katika familia hiyo.

Mwili wa marehemu umehifadhiwa katika Hospitali ya Wilaya ya Chato kwa ajili ya uchunguzi, huku taratibu nyingine za kisheria zikiendelea kukamilishwa ili mtuhumiwa afikishwe katika mamlaka husika za kisheria.

Jeshi la Polisi linatoa wito kwa wananchi kutumia njia za amani na za kisheria katika kutatua migogoro badala ya kujichukulia sheria mkononi, jambo linaloweza kusababisha madhara makubwa au kupoteza maisha.

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limewafikisha Mahak**ani mlinzi (baunsa) pamoja na mfanyakazi wa usafi waliokuwa wakifany...
14/05/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza limewafikisha Mahak**ani mlinzi (baunsa) pamoja na mfanyakazi wa usafi waliokuwa wakifanya kazi katika baa ya Las Vegas, wakituhumiwa kwa mauaji ya Mkazi wa Mwanza, Mzafuru Faisal Yunusu.

​Washtakiwa hao ni Yohana Paul Peter (22), ambaye ni mlinzi wa eneo lilipotokea tukio hilo na Hamis Juma M***a (27), mfanyakazi wa usafi.

Wawili hao wamepandishwa kizimbani leo Alhamisi Mei 14, 2026, katika Mahak**a ya Wilaya ya Ilemela na kusomewa shtaka la mauaji.

​Akisoma shauri hilo la jinai namba 10492 la mwaka 2026 mbele ya Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahak**a ya Wilaya ya Ilemela, Mhe. Christian Mwalimu, Wakili wa Serikali Clara Muhando, akisaidiana na Evance Kaiza, aliieleza mahak**a kuwa washtakiwa walitenda kosa hilo mnamo tarehe 05.02.2026 katika baa ya Las Vegas iliyopo eneo la Kona ya Bwiru, mtaa wa Nyamanoro, wilaya ya Ilemela.

​Washtakiwa wote wawili, wakiwa katika baa hiyo ya Las Vegas, wanadaiwa kumshambulia na kumuua Mzafuru Faisal Yunusu kinyume na kifungu cha 196 na 197 cha Sheria ya Kanuni ya Adhabu, Sura ya 16 k**a ilivyofanyiwa marejeo mwaka 2023.

​Hata hivyo, watuhumiwa hao hawakutakiwa kujibu chochote kwa kuwa mahak**a hiyo haina mamlaka ya kisheria ya kusikiliza mashauri ya mauaji.

​"Mahak**a haina mamlaka ya kusikiliza shauri hili, kwa hiyo hamtatakiwa kujibu chochote juu ya tuhuma zenu. Vilevile, kesi inayowakabili haina dhamana, hivyo mtaendelea kuwa mahabusu hadi pale upelelezi utakapokamilika," alisema Hakimu Mwalimu.

​Kesi hiyo imeahirishwa hadi Mei 28, 2026, na washtakiwa wamerejeshwa rumande.

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba leo bungeni wakati akijibu swali ya mbunge wa viti maalum...
14/05/2026

Hayo yamesemwa na Waziri Mkuu wa Tanzania Dkt. Mwigulu Nchemba leo bungeni wakati akijibu swali ya mbunge wa viti maalumu vijana latifa Juakali.

Waziri Mkuu amezitaka taasisi za elimu ya juu nchini kutumia utaratibu wa zamani wa kuwaruhusu wanafunzi waliokosa ada kwa changamoto mbalimbali kufanya mitihani na kulipa ada baadae muda wa kufuata vyeti vyao.

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Klabu ya Simba leo inatarajiwa kupa karata yake ya 23 kucheza na timu ya Mashujaa FC mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania ...
14/05/2026

Klabu ya Simba leo inatarajiwa kupa karata yake ya 23 kucheza na timu ya Mashujaa FC mchezo wa ligi kuu ya NBC Tanzania bara

Mchezo huo unatarajiwa kupigwa kwenye uwanja wa Lake Tanganyika mkoani Kigoma majira ya saa kumi na robo jioni

Simba inakwenda kucheza na Mashujaa FC ikiwa na alama 49 kwenye nafasi ya pili baada kucheza michezo 22 sawa na Mashujaa FC ikiwa na alama 26 kwenye nafasi ya tisa

K**a Simba SC itafanikiwa kupata ushindi wa alama tatu dhidi ya Mashujaa itapunguza utofauti wa alama tano hadi mbili dhidi ya vinara wa ligi hiyo klabu ya Yanga yenye alama 54 baada ya kupoteza mchezo wa jana dhidi ya Dodoma Jiji FC

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Kauli hiyo imetolewa na Simon Mwamasala  mwanafunzi wa chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino cha Tanzania kampasi ya Mwanza...
13/05/2026

Kauli hiyo imetolewa na Simon Mwamasala mwanafunzi wa chuo kikuu cha Mtakatifu Augustino cha Tanzania kampasi ya Mwanza (SAUT) wakati wa kongamano la wanafunzi wa vyuo vikuu Mwanza (CHASO) liliofanyika leo Mei 13,2026 Nyakahoja jijini Mwanza

Kwa taarifa zaidi tembelea channel yetu ya YouTube

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Klabu ya Yanga  hatimaye imepoteza kwenye michuano ya ligi kuu ya NBC Tanzania bara baada ya kupokea kichapo cha mabao m...
13/05/2026

Klabu ya Yanga hatimaye imepoteza kwenye michuano ya ligi kuu ya NBC Tanzania bara baada ya kupokea kichapo cha mabao matatu kwa mawili dhidi ya Dodoma Jiji FC mchezo uliopigwa kwenye uwanja wa Airtel mkoani Singida

Katika mchezo huo mabao ya Yanga yamefungwa na Allan Okello huku kwa upande wa Dodoma jiji FC yamefungwa na Waziri Junior ,Mwanakibuta na bao la kujifunga la Bakari Mwamnyeto

Baada ya mchezo wa leo Yanga inaendelea kusalia kileleni na alama zake 54 huku Dodoma jiji FC ikifikisha alama 32 kwenye nafasi ya saba.

Follow Us On Social Media
‎Instagram -
‎Facebook -
‎X(Twitter) -
‎TikTok -
‎Thread -




Address

Jembe FM/Makongoro Road/Makongoro Street
Mwanza
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jembefmtz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jembefmtz:

Share

Category