Jembefmtz

Jembefmtz Jembe FM was created with one goal in mind: to bring the world’s most popular music and creative

Heri ya Miaka 61 ya Muungano 🤝
26/04/2025

Heri ya Miaka 61 ya Muungano 🤝

  “Niseme kuwa, hakuna aliye juu ya sheria, na wote tunatakiwa kuendesha shughuli zetu za kisiasa tukizingatia kuwa aman...
25/04/2025

“Niseme kuwa, hakuna aliye juu ya sheria, na wote tunatakiwa kuendesha shughuli zetu za kisiasa tukizingatia kuwa amani na usalama wa nchi ndio kipaumbele cha kwanza.”
- Rais Dkt. Samia Suluhu akihutubia Taifa kuelekea Miaka 61 ya Muungano”-Dkt.Samia Suluhu Hassan - Rais wa Tanzania

“Dola ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasimamiwa na mihimili mitatu ambayo ni Serikali, Bunge na Mahak**a, k**a nchi...
25/04/2025

“Dola ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inasimamiwa na mihimili mitatu ambayo ni Serikali, Bunge na Mahak**a, k**a nchi tumeamua pia uendeshaji wa shughuli za nchi yetu ushirikishe taasisi nyingine za ndani na nje ya nchi,
taasisi za serikali na zisizo za serikali, taasisi za kidini na kiraia, shughuli zote zinazofanywa na taasisi hizi zinaongozwa kwa
mujibu wa katiba, sheria na kanuni zinazotungwa na miongozo na makubaliano mbalimbali ya kitaifa na kimataifa,” - Rais

Aidha ameongeza “Nyenzo hizi nilizozitaja zimeeleza masharti na mipaka ya kazi kwa taasisi mbalimbali zinazofanya shughuli zake hapa nchini,
ili kuiwezesha serikali kuendelea kulinda haki za kiraia ikiwemo
haki ya kujieleza na kutoa maoni ni vyema sote tusivuke nje ya
mipaka yetu, tusisahau kwamba mfumo ya dola yetu ni kuongozana, kusimamiana na kuwajibishana,” - Rais Samia

Mamelodi Sundowns wanatinga FAINALI Ya Ligi Ya Mabingwa Afrika baada ya kumtoa Al Ahly kwa faida ya goli la ugenini.
25/04/2025

Mamelodi Sundowns wanatinga FAINALI Ya Ligi Ya Mabingwa Afrika baada ya kumtoa Al Ahly kwa faida ya goli la ugenini.

  Tupe comments yako hapo chini😁
25/04/2025

Tupe comments yako hapo chini😁

Tanzania, mpo tayari? Bahati Nasibu ya Taifa inakuja hivi karibuni na zawadi kubwa za pesa taslimu, michezo ya kusisimua...
25/04/2025

Tanzania, mpo tayari? Bahati Nasibu ya Taifa inakuja hivi karibuni na zawadi kubwa za pesa taslimu, michezo ya kusisimua na burudani isiyoisha. Jiandae, nafasi yako ya kushinda ipo karibu sana!



FRIDAY Y ON HITZONE Join Team Hitzone via  Leo tunapiga STORY na mkali   Mwanza   kuhusu muziki kwa ujumla stay tuned in...
25/04/2025

FRIDAY Y ON HITZONE
Join Team Hitzone via Leo tunapiga STORY na mkali Mwanza kuhusu muziki kwa ujumla stay tuned in.
______________________________
Host :
📻 93.7

CPA Renata Casmir Ndege ameteuliwa kuwa Kiamu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchiniTANESCO, Kabla ya Uteuzi huu...
25/04/2025

CPA Renata Casmir Ndege ameteuliwa kuwa Kiamu Mkurugenzi Mtendaji wa Shirika la Umeme nchini
TANESCO, Kabla ya Uteuzi huu CPA. Renata alikuwa Naibu
Mkurugenzi Mtendaji Mipango, Tafiti na Uwekezaji.

“Mwenyekiti wetu [Tundu Lissu] yuko imara na ndio maana amesema yeye hana haraka, kuliko kesi iendeshwe uchochoroni, yuk...
24/04/2025

“Mwenyekiti wetu [Tundu Lissu] yuko imara na ndio maana amesema yeye hana haraka, kuliko kesi iendeshwe uchochoroni, yuko tayari asije mahak**ani hata miaka 20 mpaka pale watakapoamua kesi yake isikilizwe kwa uwazi na watu wote waruhusiwe kuisikiliza.” - Boniface Jacob, Mwenyekiti CHADEMA Kanda ya Pwani

WEDNESDAY ON HITZONE Join Team Hitzone via  Leo tunapiga story na Hiphop artist kutoka nchini Mwanza    kuhusu muziki kw...
23/04/2025

WEDNESDAY ON HITZONE
Join Team Hitzone via Leo tunapiga story na Hiphop artist kutoka nchini Mwanza kuhusu muziki kwa ujumla stay tuned in.
______________________________
Host :
📻 93.7

Anaandika  Kwa niaba ya Klabu ya Simba Sports Club, napenda kutoa shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Mu...
23/04/2025

Anaandika Kwa niaba ya Klabu ya Simba Sports Club, napenda kutoa shukrani za dhati kwa Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kwa kuiwezesha klabu yetu kushiriki mashindano ya kimataifa.

Tumepokea kwa moyo wa shukrani mchango wa malazi na usafiri kuelekea mchezo wetu wa marudiano wa nusu fainali ya Kombe la Shirikisho Afrika dhidi ya Stellenbosch utakaofanyika nchini Afrika Kusini.

Klabu ya Simba inatambua na kuthamini kwa dhati juhudi za Mheshimiwa Rais katika kuimarisha sekta ya michezo hapa nchini, hususan mpira wa miguu.

Tumetiwa moyo pia na motisha ya Goli la Mama, ambayo imekuwa chanzo cha hamasa na ari kwa wachezaji na mashabiki wetu.

Tunapenda pia kutoa shukrani kwa Wizara ya Fedha pamoja na Wizara ya Habari, Sanaa, Utamaduni na Michezo kwa uratibu wa karibu wa safari hii.

Aidha, tunazishukuru taasisi zilizoonyesha ushirikiano mkubwa katika mchakato huu: Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA), Shirika la Ndege la Tanzania (ATCL), Mamlaka ya Bandari Tanzania (TPA), na Shirika la Reli Tanzania (TRL).

Asanteni kwa kutuamini, kutuunga mkono, na kushiriki nasi katika safari hii ya kuinua soka la Tanzania.

22/04/2025


Malkia    📸
22/04/2025

Malkia

📸

Anaandika  Ninawashukuru Watanzania wote, kwa mshikamono wenu wa kupiga vita udikteta katika Nchi yetu.Polisi waliotuk**...
22/04/2025

Anaandika Ninawashukuru Watanzania wote, kwa mshikamono wenu wa kupiga vita udikteta katika Nchi yetu.
Polisi waliotuk**ata wamezunguka na sisi kwenye magari yao kisha kututelekeza barabarani.

Kesho saa saba mchana baada ya kikao cha viongozi wakuu wa chama tutazungumza na vyombo
vya habari.

Msiogope hata kidogo, tutashinda vita hii.

Matokeo ya droo ya LOTTO na LOTTO PLUS 1 iliyofanyika tarehe 22/04/2025.LOTTO: 02,17, 31, 36, 38, 39Mpira wa Bonasi: 09L...
22/04/2025

Matokeo ya droo ya LOTTO na LOTTO PLUS 1 iliyofanyika tarehe 22/04/2025.

LOTTO: 02,17, 31, 36, 38, 39
Mpira wa Bonasi: 09
LOTTO PLUS 1: 09, 11, 26, 30, 34, 48
Mpira wa Bonasi: 08

HONGERA kwa Washindi wote.
Angalia tiketi yako sasa.

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Muliro Jumanne Muliro amesema jeshi hilo halijamk**ata mtu, ila li...
22/04/2025

Kamanda wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, SACP Muliro Jumanne Muliro amesema jeshi hilo halijamk**ata mtu, ila limezuia fujo eneo la biashara Kariakoo kwa sababu hakuna uwanja wa mikutano wa hadhara.

Kamanda Mliro amesema kwamba watu wote walioondolewa eneo la Kariakoo wako huru na kusisitiza kwamba hawajashikiliwa.

Muda mfupi uliopita Chama cha Demokrasia na Maendeleo
(CHADEMA) kimesema baada ya Heche kuk**atwa, alipelekwa Kituo cha Polisi Msimbazi, lakini baadaye aliondolewa na polisi na viongozi walipoenda kuuliza walijibiwa kuwa hakufikishwa kituoni hapo.

Matokeo ya droo ya LOTTO na LOTTO PLUS 1 tarehe 21/04/2025.LOTTO: 04, 18, 34, 37, 40, 48Mpira wa Bonasi: 16LOTTO PLUS 1:...
22/04/2025

Matokeo ya droo ya LOTTO na LOTTO PLUS 1 tarehe 21/04/2025.

LOTTO: 04, 18, 34, 37, 40, 48
Mpira wa Bonasi: 16
LOTTO PLUS 1: 02, 03, 06, 36, 38, 49
Mpira wa Bonasi: 30

HONGERA kwa Washindi wote!
Angalia tiketi yako sasa!

Habari kutoka vaticannews: Papa Francis amefariki dunia Jumatatu ya Pasaka, Aprili 21, 2025, akiwa na umri wa miaka 88 k...
21/04/2025

Habari kutoka vaticannews: Papa Francis amefariki dunia Jumatatu ya Pasaka, Aprili 21, 2025, akiwa na umri wa miaka 88 katika makazi yake ya Casa mjini Vatican

Address

Jembe FM/Makongoro Road/Makongoro Street
Mwanza
255

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jembefmtz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jembefmtz:

Share

Category