Sports campaign tz

Sports campaign tz Sports and Entertainment

STEPHANIE AZIZ KI | BADO ANA KITU AU NDIO VILEEEE!Stephane Aziz Ki amerejea tena kwenye vitabu vya Young Africans SC (Ya...
16/08/2026

STEPHANIE AZIZ KI | BADO ANA KITU AU NDIO VILEEEE!

Stephane Aziz Ki amerejea tena kwenye vitabu vya Young Africans SC (Yanga) k**a X Factor baada ya safari yake ya kuzunguka katika klabu za nje ya Tanzania, ikiwemo Wydad Casablanca ya Morocco na Al-Ittihad Tripoli ya Libya.

Aziz Ki awali aliondoka Yanga na kujiunga na Wydad Casablanca kwa ada ya USD 800,000. Baada ya hapo, Wydad ilimuuza kiungo huyo kwenda Al-Ittihad Tripoli ya Libya kwa USD 500,000.

Sasa Yanga imemrudisha tena Aziz Ki kutoka Al-Ittihad Tripoli kwa USD 300,000.

Kwa hesabu hizo, Yanga ilimuuza mchezaji huyo kwa USD 800,000, lakini sasa imetumia USD 300,000 pekee kumrudisha Jangwani. Tofauti yake ni USD 500,000, kabla hata ya kuangalia thamani na mchango alioutoa katika kipindi chote alichokuwa nje.

Lakini pamoja na hesabu hizo za biashara, swali kubwa lipo kwenye kiwango cha mchezaji.

Aziz Ki anarejea Yanga akiwa na uzoefu wa kucheza nje ya Tanzania, lakini pia anakuja katika mazingira ambayo mashabiki watakuwa na matarajio makubwa kwake. Atahitaji kuonyesha kwamba bado ana uwezo wa kuamua michezo, kufunga mabao na kutengeneza nafasi k**a alivyokuwa akifanya kipindi cha kwanza akiwa Jangwani.

Wachambuzi wa mambo ya Soka wamekuwa na mitazamo tofauti kuhusu faida anazozileta nazo na hasara anazokuja nazo.

Je, safari yake ya Wydad na Al-Ittihad Tripoli imemjenga zaidi k**a mchezaji, au ndio imeashiria kushuka kwa kiwango chake? Jibu halitapatikana kwenye takwimu za uhamisho pekee—litapatikana ndani ya uwanja. Sasa ni zamu ya Aziz Ki kuongea kwa miguu yake.

HONGERA TFF NA TPLB KWA MFUMO WA UNUNUZI WA TIKETI MTANDAONI.Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2026/2027 imeanza rasmi,...
14/08/2026

HONGERA TFF NA TPLB KWA MFUMO WA UNUNUZI WA TIKETI MTANDAONI.

Ligi Kuu ya Tanzania Bara msimu wa 2026/2027 imeanza rasmi, msimu ambao unatarajiwa kuwa na mikiki mikiki mingi kutokana na ratiba yenye ushindani mkubwa, huku timu zikikimbizana na ratiba ya mashindano ya AFCON 2027.

Katika maboresho ya Kanuni za Ligi Kuu msimu huu, TFF imekuja na mfumo mpya wa ununuzi wa tiketi kupitia mtandao. Huu ni mfumo mpya ambao, pamoja na changamoto za awali katika kuuzoea, naamini ni mfumo sahihi unaoweza kusaidia kudhibiti mapato ya viwanja na kuhakikisha fedha zinaenda sehemu husika.

Mfumo huu ulianza kutumika katika mchezo wa Ngao ya Hisani. Kwa baadhi ya mashabiki unaonekana kuwa na ugumu kutokana na kuwa ni jambo jipya, lakini wahusika wanapouelewa vizuri, utakuwa rahisi na wenye manufaa makubwa.

Mfumo huo unaruhusu mtu kununua hadi tiketi nne kwa kutumia namba yake ya simu, huku akiwa anatakiwa kuwa na barua pepe (email).

Akizungumzia mfumo huo baada ya kuanza kutumika, Naibu Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Hamis Mwijuma (MwanaFA), alisema wameona utofauti mkubwa wa mapato katika mchezo wa Ngao ya Hisani uliochezwa Zanzibar. Alieleza kuwa walipata takribani Shilingi milioni mia mbili na kitu, tofauti na Fainali ya Muungano iliyowakutanisha timu zilezile ambapo mapato yalikuwa takribani Shilingi milioni 27 pekee.

Mfumo huu pia unaweza kusaidia kukomesha biashara ya tiketi inayofanywa na baadhi ya maharamia wanaonunua tiketi nyingi kwa bei halali na baadaye kuziuza kwa bei kubwa siku ya mechi. Mfumo huu unatoa nafasi kwa mashabiki kupata tiketi kwa bei halisi na kupunguza mianya ya unyonyaji.

Hata hivyo, tunaomba TFF na TPLB waangalie pia suala la utoaji wa pasi za kuingilia uwanjani. Kuna changamoto inayohusisha baadhi ya watendaji wasio waaminifu kutumia vibaya pasi hizo, hususan pasi za VIP A, VIP B na VIP C.

TFF na TPLB tunaomba suala hili liangaliwe kwa umakini na kuwekwa mfumo madhubuti wa udhibiti ili kila pasi inayotolewa iwe na ufuatiliaji.

ARTETA: TUNATAKA KUJENGA HIMAYA YA ARSENALKocha wa Arsenal, Mikel Arteta, amesema dhamira yake ni kuifanya klabu hiyo ku...
10/08/2026

ARTETA: TUNATAKA KUJENGA HIMAYA YA ARSENAL

Kocha wa Arsenal, Mikel Arteta, amesema dhamira yake ni kuifanya klabu hiyo kushinda tena na kujenga “himaya” ya soka yenye mafanikio kwa muda mrefu.

Arteta amesema maandalizi yote aliyoyafanya wakati wa mapumziko ya msimu yalilenga kutambua mambo ambayo Arsenal inapaswa kuyafanya ili kurejea kwenye mafanikio na kuendelea kushinda mataji.

“Tunaenda kupigania kila kombe. Kazi yote niliyoifanya wakati wa mapumziko ya msimu ilikuwa ni kuelewa tunachohitaji kufanya ili kushinda tena na kujenga himaya katika klabu hii. Hilo ndilo lengo, na hilo ndilo dhamira ya klabu yetu,” amesema Arteta.

Kauli hiyo inaonyesha wazi kuwa Arsenal inalenga sio tu kushinda mataji msimu ujao, bali pia kujenga timu yenye uwezo wa kutawala soka kwa miaka ijayo.

  | 2026 - 2027.Leo Jumatatu Agosti 10, 2026   tumeamua kuzimulika jeza timu mbalimbali ambazo zinashiriki  Nchini Tanza...
10/08/2026

| 2026 - 2027.

Leo Jumatatu Agosti 10, 2026 tumeamua kuzimulika jeza timu mbalimbali ambazo zinashiriki Nchini Tanzania.

Jezi za zinatengenezwa na , kampuni ya Mtanzania mzalendo .

wanashirikiana na kuzalisha Jezi hizo za kiwango cha Kimataifa.

Nanukuu maneno ya Mkurugenzi wa

"Jezi za Simba ambazo zimetoka msimu huu zina ubora wa Jezi za Manchester united, Arsenal, Barcelona na timu zingine za Ulaya"

Kwa maneno haya, Bosi Joe anawahakikishia Wanasimba kwamba wanunue jezi original ambazo zinatoka

Pia CPA Joe amesema ni vizuri Wanasimba wasinunue Jezi ambazo sio original maana ni kuhujumu Uchumi wa timu hiyo.

Mmoja wa Wana lialia Mchekeshaji nguli Tanzania amesema Jezi hii Ina ubora na utamu wa aina yake.

Naomba kufahamu maoni kutoka kwa wanasimba_

1. Ubora wa Jezi unaridhisha?
2. Je bei ya Jezi inalingana na ubora wake?
3. Mchanganyo wa rangi na designing ya jezi ya home, away na third kit zinavutia machoni?

Mwisho: Ukweli amependeza na jezi yake ingawa uzuri wake unachangia.

KUMBUKUMBU YA SAFARI YA HABARI: FABIAN FANEUL & MAGANGA JAMES GWENSAGA 🔥🎙️Mwanzilishi wa  na , Mr. Fabian Fanuel ( ), ak...
10/08/2026

KUMBUKUMBU YA SAFARI YA HABARI: FABIAN FANEUL & MAGANGA JAMES GWENSAGA 🔥🎙️

Mwanzilishi wa na , Mr. Fabian Fanuel ( ), akiwa katika picha na ndugu na rafiki yake wa karibu, Maganga James Gwensaga, wakati wakitekeleza majukumu yao katika tasnia ya Habari na Mawasiliano.

Fabian Fanuel na Maganga James Gwensaga walifahamiana mwaka 2007, wakati wakifanya kazi pamoja katika Living Water FM 103.3 MHz, iliyokuwa Mwaloni, Mwanza.

Wakati huo, hii ilikuwa combo iliyokuwa ikiwasha moto wa redio! 🔥📻

Maganga James Gwensaga alikuwa akiendesha kipindi cha Morning Glory, kilichokuwa kikianza saa 12:00 alfajiri hadi 3:00 asubuhi, huku Fabian Fanuel akiwa mtangazaji wa kipindi cha Promotion Time, kilichokuwa kikianza saa 3:00 hadi 5:00 asubuhi.

Baada ya miaka mingi ya safari katika tasnia ya habari, Maganga James Gwensaga kwa sasa yupo tena Living Water FM, baada ya kumaliza mkataba wake na Divine FM ya Kahama.

Kwa upande wake, Fabian Fanuel anaendelea na majukumu yake katika Inland Radio na Inland TV, akiendelea kulisukuma gurudumu la Habari na Mawasiliano.

Kumbukumbu zinarejea pia timu ya Living Water FM ya kipindi hicho, akiwemo Esther Tindos Kusekwa, Marehemu Janeth Mwenda, Ayub Daudi, Leah Mnyambwa, Gertruda Shimba, Caroline Mwaipungu na Pastor Maronge.

Akikumbuka safari hiyo, Fabian Fanuel amesema:

“Leo nimekumbuka mbali sana na ndugu yangu Maganga James! Mungu ni mwema. Bado tunaendelea na majukumu yetu katika kazi hizi za Habari na Mawasiliano.”

Miaka inapita, vitu vinabadilika, lakini urafiki, kumbukumbu na mapenzi ya kazi vinaendelea kubaki.🎥

Mchambuzi wa video wa Kenya Police Bullets FC, Samuel Thuku, ameondoka rasmi katika klabu hiyo na kujiunga na Pamba Jiji...
09/08/2026

Mchambuzi wa video wa Kenya Police Bullets FC, Samuel Thuku, ameondoka rasmi katika klabu hiyo na kujiunga na Pamba Jiji FC ya Tanzania.

Thuku ni mchambuzi mwenye uzoefu mkubwa katika soka, ambapo pia ni sehemu ya benchi la ufundi la timu ya Taifa ya Kenya U17.

Kabla ya kujiunga na Pamba Jiji FC, Thuku amewahi kufanya kazi k**a mchambuzi wa video katika klabu mbalimbali nchini Kenya, zikiwemo Kenya Police FC, Sofapaka FC na Kariobangi Sharks FC.

Kuwasili kwake Pamba Jiji FC kunatarajiwa kuongeza nguvu katika eneo la uchambuzi wa kiufundi na maandalizi ya timu kuelekea msimu mpya.

Yanga amesajili wachezaji wengi ila huyu Peter Shalulile  ni mchezaji hatari sana.K**a atakuwa kwenye fomu yake mama ali...
09/08/2026

Yanga amesajili wachezaji wengi ila huyu Peter Shalulile ni mchezaji hatari sana.

K**a atakuwa kwenye fomu yake mama alivyo, magoli wengi ligi kuu watapata shida maana anajua kufunga.

Kila laheri kwako

Neno moja kwao

SIMBA YA STEVE BECKER 2026/27: MTEGO AU TIMU BADO INAJENGWA?Jana mashabiki wa Simba waliona Simba mpya ya Kocha Steve Be...
09/08/2026

SIMBA YA STEVE BECKER 2026/27: MTEGO AU TIMU BADO INAJENGWA?

Jana mashabiki wa Simba waliona Simba mpya ya Kocha Steve Becker kwenye Simba Day Uwanja wa Uhuru, Dar es Salaam.

Simba ilicheza kirafiki dhidi ya Kenya Police FC na kupoteza 1-0.

Mchezo huo ulionyesha kikosi kipya cha 2026/27, wachezaji wengi wapya wakionekana.

Baada ya dakika 90, mjadala ukaibuka: Je, Simba hii imekamilika au bado inajengwa?

KIPINDI CHA KWANZA: SIMBA ILIKUWAJE?

Simba ilijaribu kutawala mpira na kujenga mashambulizi kutoka nyuma, lakini ilikosa ubunifu na nafasi za hatari.

Hii ilizua maswali kuhusu usajili mpya, ingawa wengine wanaamini timu mpya haiwezi kuhukumiwa mapema.

KIPINDI CHA PILI: BECKER ALIONYESHA NINI?

Kulikuwa na mabadiliko madogo, lakini Simba bado ilikosa umaliziaji.

Swali likabaki: Je, timu inaonyesha dalili za ushindani wa msimu ujao?

Maoni yamegawanyika—wengine wanaona Becker anaficha uwezo, wengine wanaona timu bado dhaifu.

SIMBA BADO INAHITAJI MUDA?

Ni mapema kuihukumu Simba kwa mechi moja. Mfumo mpya na wachezaji wapya bado wanahitaji muda.

Hii ni kipimo cha mwanzo tu, si hitimisho.

NGAO YA JAMII — 12 AGOSTI 2026

Simba itakutana na Yanga SC Zanzibar kwenye Ngao ya Jamii.

Hapo ndipo mtihani mkubwa utaanza dhidi ya mpinzani wa kweli.

Kwa sasa, Simba bado inajengwa.

Swali ni: Je, Becker anaficha uwezo au hii ndiyo Simba halisi?

Tarehe 12 Agosti Zanzibar itatoa majibu.

Namba wa Yanga atakayetangazwa leo yuko hapo pichani. Anaitwa Alphonce Mabula. Leo ni Kilele cha Siku ya Mwananchi. Happ...
09/08/2026

Namba wa Yanga atakayetangazwa leo yuko hapo pichani. Anaitwa Alphonce Mabula.

Leo ni Kilele cha Siku ya Mwananchi. Happy Wannachi Day.

Huu moto Arteta anaotengeneza mnauona? pale katikati yupo Declaine Rice, Bruno Grumaeles na Martin Odergard.....Shauri y...
08/08/2026

Huu moto Arteta anaotengeneza mnauona? pale katikati yupo Declaine Rice, Bruno Grumaeles na Martin Odergard.....Shauri yenu.

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports campaign tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports campaign tz:

Shortcuts

Share

Category