Sports campaign tz

  • Home
  • Sports campaign tz

Sports campaign tz Sports and Entertainment

HAPA SIMBA SC MMEBUGI SANA | BAADAYE MSIANZE KULAUMUKupitia ukurasa rasmi wa Instagram wa Singida Black Stars, taarifa i...
27/07/2025

HAPA SIMBA SC MMEBUGI SANA | BAADAYE MSIANZE KULAUMU

Kupitia ukurasa rasmi wa Instagram wa Singida Black Stars, taarifa imetolewa kuwa Jonathan Sowah amesajiliwa rasmi na Simba SC. Mwanzoni, hizi zilionekana k**a tetesi zisizo na mashiko — lakini sasa ni rasmi. Hili, kwangu binafsi, si jambo la kushangaza.

Soka ni k**a siasa. Hakuna adui wa kudumu, wala rafiki wa kudumu. Lakini kuna baadhi ya matukio yanayozua maswali ya msingi.

Kabla ya kujiunga na Singida Black Stars, Sowah alipokuwa Medeama, alionekana wazi kuwa na mapenzi na heshima kubwa kwa Yanga SC. Aliposajiliwa na Singida, bado alikuwa na uhusiano wa karibu na miamba hao wa Jangwani. Hakuficha mapenzi yake kwa Yanga — hata Rais wa Yanga, Injinia Hersi Said, alionekana kumwelewa na kumkubali.

Lakini leo, Sowah kasaini Simba SC. Swali ni, nini kilitokea kati ya Sowah na Hersi? Walikoseana wapi? Ni mazungumzo gani yalivunjika? Mambo haya hayapo wazi, lakini tunajua moja — mpango wa kumsajili Sowah Yanga umezimika, na Simba wamechukua nafasi hiyo.

Kumbuka: Huyu ni mchezaji ambaye alijiunga na Singida dirisha dogo la usajili, akasaidia timu hiyo kufuzu hadi Nusu Fainali ya CRDB Federation Cup, na pia akaipeleka Simba nje ya mashindano hayo! Leo hii huyo huyo amejiunga na Simba. Ajabu, siyo?

Inasemekana usajili huu umefanywa kwa ushawishi wa Mlezi wa Singida Black Stars, Mwigulu Nchemba, na Rais wa Simba, Mohamed Dewji. Je, hili ni tukio la mpango maalum au dili lililotengenezwa chini ya meza?

Wapo wanaosema kuwa Sowah ni chaguo la Kocha Fadlu Davids. K**a ni kweli, basi Fadlu anaamini anaweza kumrekebisha kiutendaji na kimaadili. Lakini je, Sowah ataweza kuendana na utamaduni wa soka la Kibongo? Ataweza kuhimili presha ya mashabiki, vyombo vya habari, na mahasimu wa jadi?

Tusisahau, kuna madai ya muda mrefu kwamba baadhi ya wachezaji hujihusisha na michezo ya kupanga matokeo — kuuza mechi! Siwezi kusema hili linamhusu Sowah, lakini kila tetesi ina chanzo chake. Wasiwasi ni kinga.

Kocha Sead Ramovic anamtaka Pacome Zouzoua na Clement Mzize kwa madolali ya kutosha kujenga uwanja wa Yanga pale Jangwan...
26/07/2025

Kocha Sead Ramovic anamtaka Pacome Zouzoua na Clement Mzize kwa madolali ya kutosha kujenga uwanja wa Yanga pale Jangwani.

Halafu Injinia anasema eti bado wanamahitaji na wachezaji hao. Eti wanataka kuchukua ubingwa wa Afrika.

Anawanyima wachezaji kupata hela, Pacome Mshahara Milion 98 | Mzize milioni 101 kila mwezi. Hamwoni Shemeji anakula 119 Kila mwezi.

Yanga hawawezi kuwalipa hao wachezaji hizo pesa kwa Kila mwezi. Nasikia Pacome anakula Milioni 30 na Mzize 25.

Viongozi wengine bana wanawakosesha maisha wachezaji wakati mpira ni suala la muda tu na sio Kila siku. Pia ikumbukwe Kuna majeraha!! God forbid.

.

 nawaomba msilete timu yenu uwanjani maana mtakula 7. Na hapo kwenye line up hayupo Duke Abuya na Maxi Nzengeli.Mtapigwa...
26/07/2025

nawaomba msilete timu yenu uwanjani maana mtakula 7. Na hapo kwenye line up hayupo Duke Abuya na Maxi Nzengeli.

Mtapigwaaaa kipigo cha mwitu!! Yanga naona wamejipanga kuchukua Kombe la CAFCL msimu huu.

Andaeni timu mapema msije kula 7-0 na muanze kusema mara oooh mara eeeeh! Mpira ni uwekezaji (Fedha) sio maneno.

ELIZABETH KULOLA – NYOTA INAYOCHIPUKIA KATIKA MUZIKI WA INJILI.Elizabeth Kulola ni mwimbaji chipukizi wa muziki wa Injil...
26/07/2025

ELIZABETH KULOLA – NYOTA INAYOCHIPUKIA KATIKA MUZIKI WA INJILI.

Elizabeth Kulola ni mwimbaji chipukizi wa muziki wa Injili kutoka jijini Mwanza, ambaye sasa anazidi kung’aa na kuonesha dira ya mafanikio katika huduma ya uimbaji. Ingawa alianza kuimba tangu akiwa mdogo kwenye kwaya za Sunday School, Elizabeth alianza rasmi kufanya muziki kwa mtazamo wa kitaalamu kuanzia mwezi Juni 2025.

Anasali katika Kanisa la Jesus Restoration Centre (JRC) lililopo Kirumba Polisi, barabara ya kuelekea Ibanda, chini ya uongozi wa watumishi wa Mungu Pasta George na Janeth Mukabwa. Ni mwimbaji mwenye kipaji halisi cha uimbaji wa moja kwa moja (live performance), akiwa na sauti yenye mvuto na uwezo wa kipekee wa kumiliki jukwaa pamoja na kipaza sauti (microphone).

Elizabeth amekuwa na shauku na maono ya kumtumikia Mungu kupitia muziki wa Injili, na sasa amejitosa rasmi akiwa na malengo ya kufikia viwango vya juu ndani na nje ya Tanzania. Lengo lake kuu ni kumtukuza Mungu, kumhubiri Kristo kupitia nyimbo, na kuwafikia watu kwa ujumbe wa matumaini na wokovu.

Tayari amerekodi nyimbo kadhaa kwenye studio, huku wimbo wake wa kwanza uliotambulika kwa jina la "Amenitosheleza" ukiwa umeshaanza kupigwa katika redio mbalimbali, na kupokelewa kwa moyo wa shukrani na mashabiki wa muziki wa Injili.

Akizungumza katika kipindi cha Ukombozi Jumamosi kilichorushwa na redio Ukombozi FM 104.1 MHz tarehe 26 Julai 2025, Elizabeth alieleza dhamira yake ya kujitolea kwa dhati katika kazi ya Mungu. Alisema yuko tayari kusimama kwa nguvu zote kulitangaza jina la Yesu kupitia muziki.

Mwimbaji huyu anawaomba mashabiki wa muziki wa Injili kumpokea kwa upendo na kumpa ushirikiano ili aweze kutimiza wito na maono yake. Vilevile, anatoa wito kwa watumishi wa Mungu waendelee kumuombea ili aweze kusimama imara katika huduma hii.

"Lengo langu si umaarufu bali ni kumtumikia Mungu kwa moyo wangu wote na kufikia roho nyingi kupitia muziki," alisema Elizabeth kwa unyenyekevu.

Hatimaye wameona wamalize mchezo maana mchelea mwana kulia utalia wewe. Amekubali kamba miaka miwili...Haya ndio mambo s...
24/07/2025

Hatimaye wameona wamalize mchezo maana mchelea mwana kulia utalia wewe.

Amekubali kamba miaka miwili...

Haya ndio mambo so kuanzia kubagain k**a zimekuwa nyanya.

Timu kubwa kwa Mchezajii mkubwa hakuna stori ni kumwaga hela tu. Maneno yanakuwa machache vitendo vingi.

Majirani wameachwa njia panda bila kujua watafanyaje. Ingawa walikuwa wanamtamani sana.

Ngoja tuone ugomvi baina ya Kulwa na Doto nani atashinda. Nasikia Nyuma mwiko wanamtaka Eliiiiieee Kibisawala.

Wa matopeni walikuwa wanamtaka Mzee wa Bleach ila ndio baaaaaaaaaasi!! Imekwishaaaaaa.

Ngoja tuone nani atakuwa bingwa katika mpambano huu.

Mchezajii wa Singida Black Stars mghana Jonathan Sowah anahusishwa kuhitajika ndani ya Simba SC.Johnathan Sowah ni mchez...
24/07/2025

Mchezajii wa Singida Black Stars mghana Jonathan Sowah anahusishwa kuhitajika ndani ya Simba SC.

Johnathan Sowah ni mchezaji mwandamizi wa idara ya ushambuliaji ndani ya Singida Black Stars.

Toka afike kutoka Madeama ya Ghana amekuwa akitupia ingawa alikuwa dirisha dogo.

Aliweza kumweka benchi Elvis Rupia kutoka Kenya kwenye nafasi ya ufungaji wa Magoli ndani ya timu hiyo.

Inasemekana huduma yake inatakiwa na Simba sc yenye manguli k**a Dese Mukwala na Lionel Ateba.

Itabidi mmoja wao akimpishe Sowah Ili aingie Simba SC.

Kati ya Mukwala na Ateba nani aondoke Ili Sowah ainge!

Je anaweza kutibu tatizo sugu la ufungaji ndani ya wekundu wa Msimbazi?

Karibu Yanga.
23/07/2025

Karibu Yanga.

YANGA MALIZENI MCHEZO MAPEMA!!! SHAURI YENU.Taarifa za chini sana zilizotufikia ni kwamba  mchezaji wa Yanga msimu ujao ...
23/07/2025

YANGA MALIZENI MCHEZO MAPEMA!!! SHAURI YENU.

Taarifa za chini sana zilizotufikia ni kwamba mchezaji wa Yanga msimu ujao anaweza kucheza kwa mahasimu wao Yanga Simba SC.

Mpaka sasa Mkataba wa Pacome ndani ya Yanga umeisha ingawa mazungumzo yako mezani yakiendelea.

Inasemekana eti jamaa anataka pesa za USAJILI k**a aliyopewa Shemeji 1.3 na Mshahara k**a wa Shemeji.

Sababu inasemekana kwamba yeye ndio anaibeba timu hiyo kwa sasa.

Na ukweli usemwe jamaa ni mashine kwelikweli! Anajua sana. NI HALALI KUPEWA MTONYO MKUBWA.

NB. Mkifanya mchezo anaenda Simba na msije mkasema hatujasema.

🔥 BREAKING! Simba SC yamkamilisha usajili wa kiungo fundi Allasane Kanté kutoka CA Bizertin 🇹🇳 – moja ya klabu kongwe kw...
22/07/2025

🔥 BREAKING! Simba SC yamkamilisha usajili wa kiungo fundi Allasane Kanté kutoka CA Bizertin 🇹🇳 – moja ya klabu kongwe kwenye Ligi Kuu Tunisia!

🖊️ Mkataba wake wa mwaka mmoja uliokuwa umebaki umenunuliwa kwa USD 258,000 (≈ Tsh Milioni 672)! 💰

🛬 Kanté anawasili Bongo wikiendi hii kwa ajili ya kutambulishwa rasmi mbele ya mashabiki wa Wekundu wa Msimbazi! 🔴⚪

Simba hawachezi, wanajipanga vilivyo kwa msimu mpya! 🦁🔥

______________

🔥 BREAKING! Simba SC have officially completed the signing of midfield maestro Allasane Kanté from CA Bizertin 🇹🇳, one of the top-flight clubs in Tunisia!

🖊️ The Tanzanian giants paid USD 258,000 (approx. TSh 672 million) to buy out the final year of his contract.

🛬 Kanté is expected to land in Dar es Salaam this weekend for official unveiling before the passionate Simba fans! 🔴⚪

The Lions mean business this season! 🦁💥

USAJILI WA SIMBA SC | UNA MASWALI MENGI KULIKO MAJIBU.Kipindi Simba SC anataka kucheza na RS Berkane, Wachambuzi wa Soka...
22/07/2025

USAJILI WA SIMBA SC | UNA MASWALI MENGI KULIKO MAJIBU.

Kipindi Simba SC anataka kucheza na RS Berkane, Wachambuzi wa Soka Tanzania walisema kwamba SIMBA SC hana Quality Player wa kushindana na Berkane.

Tena walipofungwa 2-0 kule Morocco ndio stori zikawa hizo hizo kwamba Simba Ina wachezaji wa kawaida sana. Na ndio sababu imefungwa Fainali na kukosa Kombe la Shirikisho barani Afrika CAFCC.

Kipindi hiki cha usajili Simba wameamua kuachana na wachezaji ambao wachambuzi walisema hawana ubora na uwezo wa kuisaidia Simba, tena imekuwa nong'wa!!

Kila siku stori ni Simba imebomeka, Simba inaacha wachezaji wazuri, Viongozi Simba wanataka kuanza upya! Stori zimekuwa hizo hizo!!

Najiuliza Viongozi wa Simba wako sahihi au wachambuzi ndio wako sahihi? Au ndio maisha bila unafiki hayaendi.

Watu wanataka wachezaji wapya ila hawataki wachezaji wa zamani kuondoka...Lugha gongana.
20/07/2025

Watu wanataka wachezaji wapya ila hawataki wachezaji wa zamani kuondoka...Lugha gongana.

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports campaign tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports campaign tz:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share