Sports campaign tz

Sports campaign tz Sports and Entertainment

Jamaa anajua sana boli....ana utulivu mkubwa sana pale katikati. Kadri anavyokuaa ndio anazidi kuwa mtamu zaidi uwanjani...
24/09/2025

Jamaa anajua sana boli....ana utulivu mkubwa sana pale katikati. Kadri anavyokuaa ndio anazidi kuwa mtamu zaidi uwanjani.

Atasaidia sana kwenye ujenzi wa Azam chini ya Florent Ibenge "Re Profesaire" Mwalimu wa walimu kwenye ukocha.

Anaitwa Yahya Zaid...... Remember the Name. Haimbwi kwa sababu hayuko Kariakoo!!

FT | Azam FC 2 - 0 Mbeya City

RULANI MOKWENA NDIO UFAFANUZI WA UBABE WA MASANDAWANA.⚽ Masandawana, huu ni wakati wa kumeza kiburi na kumrudisha Rulani...
24/09/2025

RULANI MOKWENA NDIO UFAFANUZI WA UBABE WA MASANDAWANA.

⚽ Masandawana, huu ni wakati wa kumeza kiburi na kumrudisha Rulani Mokwena.

Hakuna kocha aliyewahi kuwafanya mashabiki wa Sundowns wapende mpira wa miguu k**a Rulani Mokwena.

Hakuna kocha aliyewahi kuzifanya timu za PSL ziogope Sundowns k**a alivyofanya Rulani Mokwena.

Hakuna kocha atakayewahi kucheza aina ya soka la ubabe k**a lile lililoonekana chini ya Rulani Mokwena.

Tofauti kati ya Sundowns yake na hii ya sasa ni kwamba, kwa sasa yeyote anaweza kuifunga Sundowns.

Sundowns ya Rulani…



Pamoja na ushindi ila bado kuna mistakes nyingi kwa wachezaji. Msako ule wa Yanga hatuuoni kwa sasa. Huenda mbinu zake b...
24/09/2025

Pamoja na ushindi ila bado kuna mistakes nyingi kwa wachezaji. Msako ule wa Yanga hatuuoni kwa sasa. Huenda mbinu zake bado wachezaji hawajazielewa. Tumpe muda ingawa wasiwasiw ni akili.

FT | Yanga 3 - 0 Pamba Jiji

⚽ Lassine Kouma
⚽ Maxi Nzengele
⚽ Mudathir Yahaya

Omeni huyu! Alishindwaje akiwa Simba! Anasema amerudi Raja nyumbani! Kwani Simba alikuwa porini? Eti anautaka ubingwa wa...
24/09/2025

Omeni huyu! Alishindwaje akiwa Simba! Anasema amerudi Raja nyumbani! Kwani Simba alikuwa porini? Eti anautaka ubingwa wa Morocco! Ameshindwaje kuchukua akiwa SIMBA? Wahindi wanasema "Chori Chori" ndio huyu.

FADLU ANAIHUJUMU SIMBA SC! VIONGOZI KUENI MAKINI.Niliwahi kuandika hapa kwamba Kocha Fadlu Davids ana mkakati wa kuihuju...
24/09/2025

FADLU ANAIHUJUMU SIMBA SC! VIONGOZI KUENI MAKINI.

Niliwahi kuandika hapa kwamba Kocha Fadlu Davids ana mkakati wa kuihujumu Simba SC. Inaonekana suala la kuondoka alikuwa nalo muda mrefu ila Mohamed Dewji akamtuliza.

Sasa tatizo lake alianza kufanya mambo yasiyomuhusu kuingilia mambo ya ndani ya Simba. Akaamua kuchagua upande wakati yeye anatakiwa awe hana upande.

Ameeenda Raja Casablanca na ametambulishwa k**a Kocha na wasaidizi wake aliotoka nao Simba SC.

Ameondoka muda ambao wanasimba wanamhitaji. Sio kwamba hawezi kufundisha, anajua sana ila ndio hivyo hujuma.

Sasa ameanza suala la kuanza kurubuni wachezaji wa Simba SC!! Anataka kuwafanya wachezaji washindwe kutulia na kuachana na Simba.

Anachotaka ni nini? Kuihujumu timu! Kuwapa wachezaji hali ya kutaka hela nyingi zaidi. Kwanini asitafute wachezaji wengine.

Anataka kuwa k**a Abdelhack Benchika aliyesema wachezaji wa Simba SC hawafundishiki. Baadae akaanza kuwataka kuwasajili wachezaji wa Simba ambao hawafundishiki.

Akamsajili Abubakar Sarr, Ismael Sawadogo na Sadio Kanoute!!

Hongera sana Kiungo wa boli  . Keep on moving forward!
24/09/2025

Hongera sana Kiungo wa boli . Keep on moving forward!

Ukweli mtupu!! kwanini TRA hawachukui Kodi kwa Wasanii wakati Wana soko kubwa kabisa! Ngoma Moja audio 4 Milioni na Vide...
24/09/2025

Ukweli mtupu!! kwanini TRA hawachukui Kodi kwa Wasanii wakati Wana soko kubwa kabisa! Ngoma Moja audio 4 Milioni na Video Milioni 20?

Hivi ndivyo vilabu vitatu bora vya kijamii nchini Kenya vilivyokusanya mapato katika michezo yao ya ufunguzi wa msimu mp...
24/09/2025

Hivi ndivyo vilabu vitatu bora vya kijamii nchini Kenya vilivyokusanya mapato katika michezo yao ya ufunguzi wa msimu mpya — yakionesha hamasa kubwa ya mashabiki na ushawishi wa timu hizi katika kukuza soka la mitaani!

Bongo vepeee vilabu vyetu mapato yake Mlangoni!! wakenya wanapenda sana boli.

Fadlu Davids na wasaidizi wake ndani ya Raja Casablanca! Huyu ndio kocha chori chori kuliko kocha yoyoye amewahi kuifund...
24/09/2025

Fadlu Davids na wasaidizi wake ndani ya Raja Casablanca! Huyu ndio kocha chori chori kuliko kocha yoyoye amewahi kuifundisha Simba SC.

Kwanini wanaohusika kuwasha taa wasiwepo Kwa mfumo wa shift! Hapa Wizara imebugi step ombeni radhi maana wahusika wanali...
24/09/2025

Kwanini wanaohusika kuwasha taa wasiwepo Kwa mfumo wa shift! Hapa Wizara imebugi step ombeni radhi maana wahusika wanalipwa mishahara na Kodi za Watanzania. Mmefanya uhuni na hampaswi kujitetetea kwa lolote.

Neno moja kwa kikosi ambacho kimekimbiwa na Kocha Fadlu Davids.
23/09/2025

Neno moja kwa kikosi ambacho kimekimbiwa na Kocha Fadlu Davids.

Ahmed Ally amesema kwamba wamekataa rufaa CAF kuhusu kuzuiliwa mashabiki wake kuangalia mechi za marudiano dhidi ya Gabo...
22/09/2025

Ahmed Ally amesema kwamba wamekataa rufaa CAF kuhusu kuzuiliwa mashabiki wake kuangalia mechi za marudiano dhidi ya Gaborone United.

Kifungo hicho kinakuja Kutokana na adhabu ambayo waliipata Simba SC baada ya mashabiki wao kuvunja Sheria mechi ya Shirikisho msimu uliopita.

Je watafanikiwa au hawatafanikiwa ikingatiwa mechi ni Jumapili pale Estadio De Benjamin Mkapa Dar es Salaam.

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports campaign tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports campaign tz:

Share

Category