15/06/2026
Kwa nini Morocco ilikaa nje ya Umoja wa Afrika kwa miaka 33?
Mwaka 1984, Morocco ilijiondoa katika Umoja wa Nchi Huru za Afrika (OAU) baada ya umoja huo kuikubali Sahrawi Arab Democratic Republic (SADR) kuwa mwanachama. SADR inadai uhuru wa eneo la Western Sahara, wakati Morocco inaliona eneo hilo kuwa sehemu ya himaya yake.
Morocco iliona hatua hiyo k**a kutambua upande unaopinga mamlaka yake katika Western Sahara, hivyo ikaamua kujiondoa. Kwa miaka 33 iliyofuata, iliendelea kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kisiasa na mataifa mbalimbali, hasa ya Ulaya, bila kuacha kuwa sehemu ya bara la Afrika.
Wengi walidhani Morocco iliikataa Afrika, lakini sababu kuu ya kujiondoa ilikuwa msimamo wake kuhusu mgogoro wa Western Sahara. Hatimaye, mwaka 2017, Morocco ilirejea rasmi katika Umoja wa Afrika (AU) baada ya kuwa nje ya umoja huo kwa zaidi ya miongo mitatu.