Sports campaign tz

Sports campaign tz Sports and Entertainment

BILLO QUEENS WAPEWA SHAVU KUELEKEA MECHI DHIDI YA JKT QUEENS.Mkurugenzi wa White Lake School, Everest Hagila, ambaye pia...
16/11/2025

BILLO QUEENS WAPEWA SHAVU KUELEKEA MECHI DHIDI YA JKT QUEENS.

Mkurugenzi wa White Lake School, Everest Hagila, ambaye pia ni mdau wa soka, amekutana leo na timu ya Billo Queens kwa ajili ya kujadiliana na kuweka mikakati ya pamoja kuelekea mchezo wao muhimu dhidi ya JKT Queens.

Hagila, ambaye pia ni Mwenyekiti wa K**ati ya Mashindano ya timu ya Pamba Jiji inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, amesema wachezaji wa Billo Queens wamempa matumaini makubwa kwa kumhakikishia kuwa watacheza kwa kujituma ili kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri.

“Nimeona morali, nidhamu na kiu ya ushindi miongoni mwa wachezaji. K**a uongozi tupo nyuma yao kwa kila hatua. Tunataka kuona Billo Queens inasimama imara na kupambana hadi dakika ya mwisho ili kupata matokeo chanya,” alisema Hagila.

Kwa upande wa benchi la ufundi, Kocha Mulumba amesema maandalizi yanaendelea vizuri na wachezaji wako tayari kupambana kwenye mchezo huo muhimu.

“Wachezaji wako kwenye hali nzuri na wameonyesha maendeleo mazuri kwenye mazoezi. Tumewaandaa kimkakati na kiakili. Tunajua mchezo dhidi ya JKT Queens si rahisi, lakini tumejipanga kupambana bila kuangalia majina. Lengo letu ni pointi tatu na tutaenda kuzichukua kwa nidhamu na ujasiri,” alisema Mulumba.

Timu ya Billo Queens inaendelea na kambi yake katika Shule ya White Lake jijini Dar es Salaam k**a sehemu ya maandalizi ya michezo ijayo ya Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara.

WAAMUZI NYAMAGANA WAONGEZEWA UELEWA KUPITIA MABORESHO YA SHERIA ZA MPIRA WA MIGUU.Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Nya...
15/11/2025

WAAMUZI NYAMAGANA WAONGEZEWA UELEWA KUPITIA MABORESHO YA SHERIA ZA MPIRA WA MIGUU.

Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Nyamagana (NDFA) mkoani Mwanza kimetoa mafunzo maalum ya kuongeza uelewa kuhusu maboresho ya Sheria za Mpira wa Miguu kwa waamuzi wa madaraja mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha uendeshaji wa mchezo huo katika Wilaya ya Nyamagana.

Mafunzo hayo yalifanyika Ijumaa, Novemba 14, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mkolani – Mwanza, na yaliongozwa na Mkufunzi wa Waamuzi wa Mkoa wa Mwanza, Alfed Lizwa.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Chama cha Soka Nyamagana (NDFA), Said Abdallah “Kizota”, alisema wanafarijika kuona malengo na mikakati waliyoiweka wakati wa kuomba uongozi yakitekelezwa kwa vitendo.

“Tunawashukuru wadau wote wanaotushika mkono katika kutimiza jukumu hili. Sio kazi rahisi, lakini kwa umoja wetu tumefanikiwa kufanya jambo ambalo wengine walishindwa. Tumekuwa wilaya ya kwanza kutoa mafunzo haya kwa waamuzi wetu ili wawe hodari, makini na wafuate sheria ipasavyo uwanjani,” alisema Kizota.

Akifungua rasmi mafunzo hayo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyamagana (DAS), Thomas James Salala, alisema Wilaya imejipanga kuendelea kuuwezesha mchezo wa mpira wa miguu ili mafanikio yaonekane kwa matokeo chanya.

Amewaasa waamuzi kujiendeleza na kufuatilia mabadiliko ya sheria mpya za soka ambazo zimefanyiwa maboresho duniani kote kulingana na mahitaji ya sasa ya mchezo huo.

Kwa upande wake, Mkufunzi Alfed Lizwa alisema amefurahishwa na mwitikio wa waamuzi waliojitokeza na kwamba hatua hiyo itaongeza ubora wa usimamizi wa mechi katika mashindano mbalimbali ya wilaya na mkoa.

Naye Makamu Mwenyekiti wa NDFA na Mratibu wa Warsha hiyo, Oscar Kapinga, alisema chama kitaendelea kuratibu mafunzo k**a hayo si kwa waamuzi pekee, bali pia kwa makundi mengine yanayohusika na usimamizi wa mchezo wa mpira wa miguu katika Wilaya ya Nyamagana, ili kuongeza ufanisi na kuleta maendeleo.

Kuna mambo yanashangaa yakitamkwa na mtu anayeshimika. Tena mtu halisia kwenye nafasi nyeti ambayo ameaminiwa nayo.Sitak...
12/11/2025

Kuna mambo yanashangaa yakitamkwa na mtu anayeshimika. Tena mtu halisia kwenye nafasi nyeti ambayo ameaminiwa nayo.

Sitaki kuwakurudisha nyuma kwa kile kinachoendelea baina ya Wasimamizi wa Idara ya Habari Yanga na Mwanahabari Nguli Nassib Mkomwa Mr Ripota.

Mr Ripota ametoa taarifa kwa Umma kuhusu Mchezaji Aziz Andambwile kuidai Yanga wanaomwona adui wakati kawasanua.

Msimamizi wa Mchezaji huyo amezungumza kupitia Media mojawapo leo nae inaonekana ni Winga k**a vile walivyomuita Jasmine Razak.

Kwani kudaiwa ni DHAMBI? Mbona watu wengi wanadaiwa! Taasisi nyingi zinadaiwa na hakuna tatizo? Au Kuna Nini mnaficha?

Idara ya Habari imeanza kupambana kusawazisha ili ionekane hakuna tatizo kumbe tatizo ni kubwa tu.

Mbona sasa hivi Yanga kuanzia kwa wanene hadi kwa mashabiki ni wakali sana. Mkiambiwa timu yenu imechoka, Mnakuja juu k**a pilipili.

Mkiambiwa Kocha wenu bado sana, mnaona kuna tatizo kwamba watu wanaisak**a timu yao! Kwani mkikaa kimia Kuna ubaya gani?

Kuna wakati inafirikisha sana kwamba kwanini mnajihami? Mnaficha Nini au mnataka Jamii ielewe kwamba nyinyi ni watu wa aina gani?

09/11/2025

Dakika 90 za henyahenya baina ya Yanga SC vs KMC pale KMC Complex Mwenge Dar es Salaam.

Good Start ya teka Andy Boyeli, amefunga Magoli 2z Pacome 1 na Maxi Nzengele 1.

KMC Ina Ina timu ila Ina wachezaji wenye ubora wachache. Kocha Maximo naona k**a vile jahazi linaenda mrama.

Huenda kuanzia leo mkasikia jambo linaitwa taarifa kwa umma maana sio kwa mwenendo huo wa tia maji tia maji.

Saliboko, M***a na Chambo wana kitu. Kuna yule Kiungo Nindi Jr naye ana mambo mambo miguuni kwake.

Yanga amepata ushindi ila Soka la leo ni Soka fakamia fakamia. Mipango mipango haijaonekana.

Tumpe Muda Kocha Pedro na wasaidizi wake huenda wakikutana na JS Kabylie ya kina Babacar Sarr watatupa mechi ya maana.

FT | Yanga SC 4 - 1 KMC

09/11/2025

✅ 1. Isaya 43:2

“Upitapo katika maji mengi nitakuwa pamoja nawe; na katika mito haitakugharikisha; uendapo katika moto hutateketea, wala mwali wa moto hautakuunguza.”

✅ 2. Zaburi 34:19

“Mateso ya mwenye haki ni mengi; lakini Bwana humponyoka katika hayo yote.”

✅ 3. Zaburi 23:4

“Naam ijapokuwa nitapita kati ya bonde la uvuli wa mauti, sitaogopa mabaya; kwa maana wewe upo pamoja nami; gongo lako na fimbo yako vyanifariji.”

✅ 4. Isaya 41:10

“Usiogope kwa maana mimi ni pamoja nawe; usifadhaike kwa maana mimi ni Mungu wako; nitakutia nguvu, naam, nitakusaidia; nitakushika kwa mkono wa kuume wa haki yangu.”

✅ 5. Zaburi 46:1

“Mungu ni kimbilio letu na nguvu yetu, msaada wa haraka sana wakati wa mateso.”

✅ 6. Matayo 28:20

“…naye tazama, mimi nipo pamoja nanyi siku zote, hata ukamilifu wa dahari.”

✅ 7. 2 Wakorintho 4:8-9

“Tunaonewa pande zote, lakini hatukati tamaa; tunafadhaika, lakini hatukati tamaa; tunateswa, lakini hatuachi; tunangushwa, lakini hatuangamizwi.”

Mstari upi umekugusa zaidi hapo?

Jumapili njema kwako popote ulipo!! Ubarikiwe.

Mechi nzuri sana yenye hadhi ya Ligi Kuu. JKT Tanzania wameipa Simba SC mechi halisia. Wamecheza vizuri ingawa Simba wam...
08/11/2025

Mechi nzuri sana yenye hadhi ya Ligi Kuu. JKT Tanzania wameipa Simba SC mechi halisia. Wamecheza vizuri ingawa Simba wamebadilika kipindi cha pili na kupata ushindi.

Goli la Wilson Nangu na Jonathan Sowah limewapa Lunyasi alama 3 na goli 2 huku wajenga nchi wa JKT Tanzania wakipata goli Moja kwenye akaunti yao.

Naby Camara ni nyota kweli kweli! Kipindi cha kwanza amecheza beki, kipindi cha pili anacheza Kiungo namba Sita. Yale mapande ni balaaa.

Morice Abraham, Allasane Kante na Mpanzu Kibasawala ni namba hatari sana kwenye kutengenezea Mashambulizi.

Meneja Pandev ameanza kupata kikosi cha kwanza. Mpaka sasa eneo la Kiungo wale watatu wanaanza hawa.

Naby Camara
Allasane Kante
Morice Abraham

Nje wanasuburi
Yusuph Kagoma
Neo Maema
Jean Ahoua
Hussein Semfuko

FT | JKT Tanzania 1 - 2 Simba SC.

07/11/2025

Muziki ni asili na tulizo la Roho na Nafasi!! Sikiliza mambo haya!! Unajua Ala hiyo ya muziki ni ya wimbo gani?

07/11/2025

Kutoa maoni kwa shabiki au mwanachama wa timu yoyote ni jambo la msingi kwa sababu linawasaidia viongozi kujitathmini upya—katika mazuri waliyoyafanya na katika changamoto zilizoibuliwa.
Serikali yetu ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania imetoa uhuru kwa kila mtu kutoa mawazo yake.

Hata hivyo, pamoja na uhuru huo, kuna namna sahihi ya kuwasilisha maoni.
Kuna namna ambayo ukitoa mawazo yako yataheshimiwa, yatasikilizwa, na yatapewa uzito stahiki.

Swali linabaki:

Unatoa maoni yako kwa malengo gani?

Unataka kupata nini au kufanikisha nini kupitia hoja zako?

Je, uliwafuata viongozi kwa njia rasmi wakakataa kukusikiliza, ndiyo maana ukaamua kutumia mitandao?

Linapofika suala la kutoa maoni kwenye mitandao kwa lugha ya kuharibu chapa (brand) ya taasisi, uniacha maswali mengi kwa watu wanaofuatilia mambo kwa kina. Unakuwa hujengi, unavunja—na athari zake ni pana kuliko maneno ya mtandaoni.

Kumekuwa na malalamiko mengi yanayomhusu Said Mchome, ambaye inaelezwa ni mwanasimba. Hata hivyo, namna anavyoandika mara kwa mara inaonekana k**a ana mradi wa kuiharibu timu yake mwenyewe.

Hakuna siku anaandika kuhusu mambo mazuri yaliyowahi kufanywa na Simba.
Kila mara ni kuponda, kubeza, na kuonyesha kuwa timu ina udhaifu zaidi kuliko mafanikio.

Hata k**a kweli kuna changamoto—kwa nini kuwasilisha kwa namna ya kuichafua timu hadharani?

Mfano: Kauli k**a “Simba imemkopa Meneja Pandev kutoka Gaborone United na suala lipo FIFA” inaweza kuwa na ukweli au isiwe na ukweli. Lakini kwa shabiki, inamsaidiaje?

Kauli kwamba wachezaji wote wamekopwa, hakuna aliyenunuliwa—mashabiki wanapata nini kwa taarifa k**a hizi?

Halafu anadai Moo amemwondoa Try Again, ambaye ndiye aliyekuwa chachu ya mafanikio, na kwamba ndiyo chanzo cha Simba kufilisika.
Siwezi kukubali wala kukataa—lakini k**a ana hoja, kuna njia ya kuwasilisha bila kuharibu heshima ya klabu.

Taarifa nyeti, za tetesi, au zisizothibitishwa zikiwekwa mitandaoni zinaumiza chapa ya Simba SC.

Hemed Morocco kimemlamba!!
04/11/2025

Hemed Morocco kimemlamba!!

04/11/2025
04/11/2025

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports campaign tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports campaign tz:

Share

Category