Sports campaign tz

Sports campaign tz Sports and Entertainment

Tanzania imefungwa 1 - 0 na Morocco katika mechi ya raundi ya 16 na kuondolewa kwenye mashindano ya Afcon 2025 pale Moro...
04/01/2026

Tanzania imefungwa 1 - 0 na Morocco katika mechi ya raundi ya 16 na kuondolewa kwenye mashindano ya Afcon 2025 pale Morocco.

Gumzo kubwa ni maamuzi ya refarii uwanjani yameancha maswali mengi yasiokuwa majibu..Wengi wanasema amewaumiza Tanzania huko akiipendelea Morocco.

Wewe umeonaje mechi na maamuzi ya refarii huyu raia wa Mali?

MAKILAGI SPORTS WEAR YATOA SHUKRANI KWA WATEJA WAKE.Duka la vifaa vya michezo la Makilagi Sports Wear, lililopo katika o...
02/01/2026

MAKILAGI SPORTS WEAR YATOA SHUKRANI KWA WATEJA WAKE.

Duka la vifaa vya michezo la Makilagi Sports Wear, lililopo katika ofisi za Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, limetoa shukrani za dhati kwa wateja wake wote waliounga mkono huduma na bidhaa zake kwa kipindi cha mwaka 2025.

Akizungumza mwanzoni mwa mwaka mpya 2026, Mkurugenzi wa Makilagi Sports Wear, Bi. Sophia Makilagi, amesema mafanikio yaliyopatikana yametokana na imani na ushirikiano mkubwa kutoka kwa wateja wao wa ndani ya Mkoa wa Mwanza na nje ya mkoa.

Bi. Makilagi amesema katika mwaka 2025, duka hilo lilifanikiwa kuuza bidhaa mbalimbali za michezo zikiwemo jezi, mipira pamoja na vifaa vya mazoezi kwa wadau wengi wa michezo, hali iliyochangia ukuaji na uimara wa biashara hiyo.

“Tunamshukuru Mungu kwa kutuvusha salama mwaka 2025 na kutuwezesha kuanza mwaka mpya 2026 kwa mafanikio. Tunatoa shukrani za dhati kwa wateja wetu wote waliotufikia dukani pamoja na wale waliokuwa mbali waliotuamini kwa kuagiza bidhaa zetu. Tunaomba ushirikiano huu uendelee na uwe mkubwa zaidi katika mwaka huu wa 2026,” amesema Bi. Makilagi.

Katika wateja waliotoa mchango mkubwa kwa kununua mizigo kwa wingi mwaka 2025, Bi. Makilagi amewataja Mwenyekiti wa Copco FC, Simon Romli, Nyaitato Stephano, Augustino Yassaya Mbogo pamoja na Wilbert Mweta, akisema walionesha mfano mzuri wa kuunga mkono biashara za ndani.

Aidha, Makilagi Sports Wear imeeleza mpango wake wa kuwaandalia Vyeti vya Shukrani wadau hao k**a sehemu ya kutambua mchango wao katika kusaidia kukuza duka hilo na maendeleo ya vifaa vya michezo Mkoa wa Mwanza.

Cc

30/12/2025

Uganda na Kenya ni bure kabisa.... endeleeni kulinda Ziwa Victoria. Sisi Tanzania bado ngoma mbichi, Morocco wajipange maana tutawanyoa bila wembe.

unaijua maana ni one kondingiliiii.....Ambia kwamba Taifa Stars tutachukua Afcon 2027.

Credit:

29/12/2025
Morocco wa moto sana! Wapeni Kombe lao mapema maana sio kwa mpira huu.
29/12/2025

Morocco wa moto sana! Wapeni Kombe lao mapema maana sio kwa mpira huu.

DANNY NAMASO NI NANI?“Jude Bellingham wa Cameroon” 🇨🇲Daniel Edimesumbe Namaso, maarufu k**a Danny Namaso, ni mchezaji wa...
29/12/2025

DANNY NAMASO NI NANI?

“Jude Bellingham wa Cameroon” 🇨🇲

Daniel Edimesumbe Namaso, maarufu k**a Danny Namaso, ni mchezaji wa mpira wa miguu anayechezea klabu ya FC Porto (kwa sasa akiwa kwa mkopo katika klabu ya Auxerre, Ufaransa). Alifanya debuti yake katika Timu ya Taifa ya Cameroon (Indomitable Lions) mwezi Machi, 2025.

Danny Namaso alizaliwa nchini Uingereza, akiwa na baba raia wa Uingereza aitwaye E. Loader, na mama raia wa Cameroon aitwaye Ma Muke Celine Edimesumbe, mzaliwa wa Kijiji cha Muebah, ukoo wa Nninong, katika Tarafa ya Bangem.

Babu yake Danny Namaso ni marehemu Nhon Edimesumbe Masango, ambaye alifunga ndoa na marehemu N. Namaso Mbile, mwenye asili ya Oroko, kutoka Kijiji cha Bima.

Jina “Namaso” linatokana na mjomba wa bibi yake, marehemu Mheshimiwa N. N. Mbile, mzaliwa wa Divisheni ya Ndian.

Danny Namaso ana mdogo wake anayeitwa Danny NAD, ambaye ni mchezaji wa Rugby nchini Afrika Kusini.

Wangapi walimwona jana Namaso alizima mbele ya Frank Kassie, Ibrahim Sangare na Seko Fofana? Dogo anajua sana boli.

SIMBA SC NI K**A MANCHESTER UNITED TU.Iwapo SIMBA SC wataamua kuingia sokoni kutafuta kipa mwingine, basi watakuwa wanam...
28/12/2025

SIMBA SC NI K**A MANCHESTER UNITED TU.

Iwapo SIMBA SC wataamua kuingia sokoni kutafuta kipa mwingine, basi watakuwa wanamkosea kwa kiwango kikubwa Hussein Abel. Ukweli ni kwamba, Abel ni mmoja wa walinda mlango bora kabisa na mwenye uwezo mkubwa wa kulinda lango kwa muda mrefu.

Swali la msingi la kujiuliza ni hili: k**a SIMBA wataingia sokoni kusaka kipa mwingine, je, aliyependekeza na kumsajili Hussein Abel aliwadanganya uongozi? Au tatizo si wachezaji, bali ni maamuzi ya kiufundi yanayokosa mwelekeo?

Ukweli mchungu ni kwamba, SIMBA SC wamekuwa na mtindo wa kufanya maamuzi magumu lakini yasiyo na uthabiti, ambayo hatimaye yanawaponza. Mfano hai ni kuwaacha wachezaji muhimu k**a Inonga, Che Malone na Aishi Manula—maamuzi yaliyowaacha mashabiki wengi wakiwa na maswali kuliko majibu.

Kwa klabu kubwa k**a SIMBA, uthabiti katika maamuzi na imani kwa rasilimali walizonazo ni jambo la msingi. Bila hilo, hata usajili bora hauwezi kuleta matokeo yaliyokusudiwa.

Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Zambia, Chipolopolo, Moses Sichone amesema kuwa mtizamo chanya utakuwa jambo la msingi wa...
28/12/2025

Kocha Mkuu wa timu ya taifa ya Zambia, Chipolopolo, Moses Sichone amesema kuwa mtizamo chanya utakuwa jambo la msingi wakati timu hiyo ikijiandaa kuivaa Morocco, wenyeji wa mchezo wa mwisho wa Kundi A, kesho jioni.

Akizungumza na vyombo vya habari katika mkutano wa kabla ya mechi uliofanyika Rabat, Sichone alionyesha imani kubwa kwa kikosi chake, akisisitiza kuwa Morocco inaweza kushindwa iwapo Zambia itaingia uwanjani ikiwa na nia sahihi.

“Tunahitaji kuwa na mtizamo chanya. Morocco inaweza kushindwa,” alisema Sichone.

Sichone alipuuza umuhimu wa rekodi za nyuma za mikutano kati ya timu hizo mbili, akibainisha kuwa kinachopaswa kuangaliwa ni kiwango cha sasa cha timu hizo katika mashindano haya.

“Kinachojali si mara ngapi tumekutana na Morocco, bali ni namna walivyocheza katika mashindano haya,” aliongeza.

Kufuatia sare ya bao 1-1 kati ya Morocco na Mali, Sichone alisisitiza kuwa hakuna timu itakayoweza kutegemea matokeo ya wengine.

“Sare ya Morocco dhidi ya Mali inaonyesha wazi kuwa kila timu inalazimika kushinda kwa jitihada zake mwenyewe,” alisema.

Kocha huyo pia alisifu miundombinu ya michezo ya Morocco, akiielezea kuwa ni ya kiwango cha kimataifa na mfano bora kwa bara la Afrika.

“Tumevutiwa na miundombinu iliyopo hapa, na tunatumaini nchi nyingine za Afrika zitaiga kile ambacho Wamorocco wamekifanya,” alisema.

Kwa upande wake, nahodha wa Chipolopolo, Fashion Sakala, amesema mechi hiyo itakuwa ya ushindani mkubwa, akieleza kuwa timu zote zina historia kubwa barani Afrika.

“Ni mechi ya asilimia 50 kwa 50. Zambia na Morocco zote zimewahi kutwaa ubingwa wa AFCON,” alisema Sakala.

Zambia bado haijapoteza mchezo wowote katika kundi hilo na itahitaji matokeo mazuri dhidi ya wenyeji ili kujihakikishia kufuzu hatua ya mtoano.

Mchezo huo utapigwa saa 3:00 usiku kwa saa za Afrika ya Kati (21:00 CAT) katika Uwanja wa Prince Moulay Abdellah, jijini Rabat.

BEKI KISIKI WA PAMBA JIJI ATIMKIA SINGIDA BLACK STARS.Beki kisiki wa Pamba Jiji FC ya Mwanza, Abadalla Kheri maarufu k**...
28/12/2025

BEKI KISIKI WA PAMBA JIJI ATIMKIA SINGIDA BLACK STARS.

Beki kisiki wa Pamba Jiji FC ya Mwanza, Abadalla Kheri maarufu k**a Sebo ametimkia klabu ya Singida Black Stars ya Singida.

Ikumbukwe kuwa Sebo alisajiliwa na Pamba Jiji FC akitokea Azam FC kwa mkopo wa mwaka mmoja kwa msimu wa 2025/2026, na aliitumikia timu hiyo katika baadhi ya mechi za mwanzo wa msimu.

Hata hivyo, baada ya michezo kadhaa kupita, ukimya wa Sebo ndani ya kikosi cha Pamba Jiji FC ulianza kuonekana, huku asionekane tena kwenye mazoezi wala kwenye mechi za Ligi Kuu, hali iliyoibua maswali miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka.

Kuelekea mechi ya Pamba Jiji FC dhidi ya Fountain Gate FC iliyochezwa kwenye Uwanja wa CCM Kirumba, Kocha Mkuu wa Pamba Jiji FC, Francis Baraza, alithibitisha kuwa miongoni mwa wachezaji waliokosekana katika mchezo huo ni beki Abadalla Kheri Sebo.

Akijibu swali la mmoja wa waandishi wa habari, Kocha Baraza alisema kuwa Sebo alikuwa ameomba ruhusa kwenda kwao kumuguza mama yake aliyekuwa akiugua.

Hata hivyo, jambo la kushangaza ni kwamba leo hii beki huyo ameonekana akiwa amevaa jezi ya Singida Black Stars, akiitumikia timu hiyo katika mchezo wa Kombe la Mapinduzi unaochezwa visiwani Zanzibar.

Hali hiyo imezua maswali mazito miongoni mwa wadau wa soka: Je, Abadalla Kheri Sebo ni mchezaji halali wa Pamba Jiji FC au tayari ni mali ya Singida Black Stars? Je, Azam FC walimtoa kwa mkopo kwenda Pamba Jiji FC au Singida Black Stars, ilhali dirisha la usajili bado halijafunguliwa?

Hata hivyo, ikumbukwe kuwa Kombe la Mapinduzi lina utaratibu unaoruhusu timu kutumia wachezaji wa majaribio au wachezaji ambao bado hawajasajiliwa rasmi, jambo linaloweza kueleza uwepo wa SEBO ndani ya Singida Black Stars.

Meneja wa Pamba Jiji FC Ezekiel Ntabikeha ameiambia Famara Media kwamba wameachana na Sebo na sasa yuko huru kwenda timu yoyote. Ingawa habari za ndani zinasema Sebo hakuwa anaelewana na baadhi ya Viongozi kwenye benchi la ufundi la Pamba Jiji FC.

USAJILI WA YANGA MSIMU HUU: NANI WA KULAUMIWA? INJINIA HERSI ATUPE MAJIBU.Msimu wa mashindano unaoendelea, klabu ya Youn...
24/12/2025

USAJILI WA YANGA MSIMU HUU: NANI WA KULAUMIWA? INJINIA HERSI ATUPE MAJIBU.

Msimu wa mashindano unaoendelea, klabu ya Young Africans SC ilifanya usajili mkubwa wa wachezaji wapya kwa lengo la kuimarisha maeneo mbalimbali ya kikosi ikiwemo kiungo, ulinzi na safu ya ushambuliaji.

Usajili huo uliibua matumaini makubwa miongoni mwa mashabiki, wengi wakiamini Yanga ingeruka kiushindani ndani na nje ya nchi.

Hata hivyo, baada ya michezo kadhaa kupita, tathmini ya uwanjani inaonyesha kuwa kwa zaidi ya asilimia 80, usajili huo haujaleta matokeo yaliyotarajiwa.

Wachezaji wengi wapya wamekuwa na mchango mdogo ndani ya kikosi, hali iliyolazimisha benchi la ufundi kuendelea kuwategemea wachezaji wa zamani kuibeba timu katika nyakati ngumu.

Mpaka sasa, Mohammed Hussein ndiye mchezaji pekee kati ya waliosajiliwa aliyefanikiwa kujihakikishia namba ya kudumu katika kikosi cha kwanza na kuonyesha kiwango kinachokubalika uwanjani.

Kwa upande mwingine, wachezaji k**a Frank Assinki, Lassine Kouma, Musa Konte, Mohammed Doumbia, Andy Boyeli na Celestine Ecua bado hawajaonyesha mchango wa kuridhisha unaolingana na matarajio ya usajili wao.

Licha ya hali hiyo, sauti za ukosoaji zimekuwa chache, jambo linalozua maswali mazito: Je, tatizo ni wachezaji wenyewe, benchi la ufundi, au uongozi uliofanya maamuzi ya usajili? Kiongozi tunayemuita bora, je kweli ameleta kilicho bora kwa maslahi ya klabu?

Kwa kuondoa Tshabalala, ambaye naye ameonyesha dalili za ubora, bado hakuna mchezaji mpya anayetoa kitu cha ziada kinachoweza kuibadilisha timu pale mambo yanapokwenda kombo. Swali linalobaki ni moja—je, mashabiki hawaoni hali hii au tayari wameridhika?

Haya ni maswali yanayohitaji majibu ya wazi, kwa sababu Yanga kubwa haiwezi kujengwa kwa jina la usajili pekee, bali kwa mchango halisi unaoonekana uwanjani.

23/12/2025

Mazoezi ya hivi ni kitu kizuri sana. Tufanye mazoezi.

Elizabeth Michael “Lulu” ni mwigizaji maarufu wa filamu za Tanzania (Bongo Movie), aliyezaliwa 16 Aprili 1995 jijini Dar...
23/12/2025

Elizabeth Michael “Lulu” ni mwigizaji maarufu wa filamu za Tanzania (Bongo Movie), aliyezaliwa 16 Aprili 1995 jijini Dar es Salaam. Alianza uigizaji akiwa na umri mdogo wa takribani miaka 5, akijenga umaarufu mapema kupitia filamu k**a Foolish Age.

Katika safari yake, Lulu amejipambanua kwa uigizaji wenye hisia na ukomavu, akishiriki filamu nyingi zilizompa heshima kitaifa na kimataifa. Mwaka 2013, alitajwa na Forbes Africa kuwa miongoni mwa vijana 30 wenye ushawishi barani Afrika chini ya umri wa miaka 30.

Pamoja na changamoto za maisha na masuala ya kisheria yaliyomweka pembeni kwa muda, Lulu alirejea katika sanaa akiwa na mtazamo mpya. Leo anatambulika k**a nembo ya kizazi cha Bongo Movie, pia akiwa mjasiriamali na mshiriki wa miradi ya kijamii, hasa kwa wanawake na watoto.

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports campaign tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports campaign tz:

Share

Category