16/11/2025
BILLO QUEENS WAPEWA SHAVU KUELEKEA MECHI DHIDI YA JKT QUEENS.
Mkurugenzi wa White Lake School, Everest Hagila, ambaye pia ni mdau wa soka, amekutana leo na timu ya Billo Queens kwa ajili ya kujadiliana na kuweka mikakati ya pamoja kuelekea mchezo wao muhimu dhidi ya JKT Queens.
Hagila, ambaye pia ni Mwenyekiti wa K**ati ya Mashindano ya timu ya Pamba Jiji inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, amesema wachezaji wa Billo Queens wamempa matumaini makubwa kwa kumhakikishia kuwa watacheza kwa kujituma ili kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri.
“Nimeona morali, nidhamu na kiu ya ushindi miongoni mwa wachezaji. K**a uongozi tupo nyuma yao kwa kila hatua. Tunataka kuona Billo Queens inasimama imara na kupambana hadi dakika ya mwisho ili kupata matokeo chanya,” alisema Hagila.
Kwa upande wa benchi la ufundi, Kocha Mulumba amesema maandalizi yanaendelea vizuri na wachezaji wako tayari kupambana kwenye mchezo huo muhimu.
“Wachezaji wako kwenye hali nzuri na wameonyesha maendeleo mazuri kwenye mazoezi. Tumewaandaa kimkakati na kiakili. Tunajua mchezo dhidi ya JKT Queens si rahisi, lakini tumejipanga kupambana bila kuangalia majina. Lengo letu ni pointi tatu na tutaenda kuzichukua kwa nidhamu na ujasiri,” alisema Mulumba.
Timu ya Billo Queens inaendelea na kambi yake katika Shule ya White Lake jijini Dar es Salaam k**a sehemu ya maandalizi ya michezo ijayo ya Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara.