Famara Media

Famara Media Famara Media - Inform, Entertain and Educate.

17/11/2025

Mousa Balla Conte ni floop - Wilson Oruma.

“Usichukue muda mwingi kulinda cheo, chukua muda mwingi kutoa matokeo kwenye kazi yako maana cheo hakilindwi k**a ambavy...
17/11/2025

“Usichukue muda mwingi kulinda cheo, chukua muda mwingi kutoa matokeo kwenye kazi yako maana cheo hakilindwi k**a ambavyo kilikuja kwako bila kukipambania kitaondoka siku moja na utake usitake atakuja Mtu mwingine kwasababu wewe ulikuta Mtu mwingine, sasa kitakachobaki ni kazi ulizofanya wakati upo kwenye dawati”

- Mheshimiwa Doto Mashaka Biteko aliyekuwa Naibu Waziri Mkuu na Waziri Nishati

GSM wana mambo mazuri sana. Hili pigo la dela lilienda wapi? Mbona zuri sana kwa wadada..? Injinia mwambie Ghalib mzigo ...
17/11/2025

GSM wana mambo mazuri sana. Hili pigo la dela lilienda wapi? Mbona zuri sana kwa wadada..? Injinia mwambie Ghalib mzigo uongezeke mtaani.

Huki Sangabuye hazipo!! Ongezaaaaaaaaaaaaa!!!

BILLO QUEENS WAPEWA SHAVU KUELEKEA MECHI DHIDI YA JKT QUEENS.Mkurugenzi wa White Lake School, Everest Hagila, ambaye pia...
16/11/2025

BILLO QUEENS WAPEWA SHAVU KUELEKEA MECHI DHIDI YA JKT QUEENS.

Mkurugenzi wa White Lake School, Everest Hagila, ambaye pia ni mdau wa soka, amekutana leo na timu ya Billo Queens kwa ajili ya kujadiliana na kuweka mikakati ya pamoja kuelekea mchezo wao muhimu dhidi ya JKT Queens.

Hagila, ambaye pia ni Mwenyekiti wa K**ati ya Mashindano ya timu ya Pamba Jiji inayoshiriki Ligi Kuu Tanzania Bara, amesema wachezaji wa Billo Queens wamempa matumaini makubwa kwa kumhakikishia kuwa watacheza kwa kujituma ili kuhakikisha timu inapata matokeo mazuri.

“Nimeona morali, nidhamu na kiu ya ushindi miongoni mwa wachezaji. K**a uongozi tupo nyuma yao kwa kila hatua. Tunataka kuona Billo Queens inasimama imara na kupambana hadi dakika ya mwisho ili kupata matokeo chanya,” alisema Hagila.

Kwa upande wa benchi la ufundi, Kocha Mulumba amesema maandalizi yanaendelea vizuri na wachezaji wako tayari kupambana kwenye mchezo huo muhimu.

“Wachezaji wako kwenye hali nzuri na wameonyesha maendeleo mazuri kwenye mazoezi. Tumewaandaa kimkakati na kiakili. Tunajua mchezo dhidi ya JKT Queens si rahisi, lakini tumejipanga kupambana bila kuangalia majina. Lengo letu ni pointi tatu na tutaenda kuzichukua kwa nidhamu na ujasiri,” alisema Mulumba.

Timu ya Billo Queens inaendelea na kambi yake katika Shule ya White Lake jijini Dar es Salaam k**a sehemu ya maandalizi ya michezo ijayo ya Ligi Kuu ya Wanawake Tanzania Bara.

WAAMUZI NYAMAGANA WAONGEZEWA UELEWA KUPITIA MABORESHO YA SHERIA ZA MPIRA WA MIGUU.Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Nya...
15/11/2025

WAAMUZI NYAMAGANA WAONGEZEWA UELEWA KUPITIA MABORESHO YA SHERIA ZA MPIRA WA MIGUU.

Chama cha Mpira wa Miguu Wilaya ya Nyamagana (NDFA) mkoani Mwanza kimetoa mafunzo maalum ya kuongeza uelewa kuhusu maboresho ya Sheria za Mpira wa Miguu kwa waamuzi wa madaraja mbalimbali, ikiwa ni sehemu ya mkakati wa kuboresha uendeshaji wa mchezo huo katika Wilaya ya Nyamagana.

Mafunzo hayo yalifanyika Ijumaa, Novemba 14, 2025 katika Ukumbi wa Mikutano wa Ofisi ya Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Mkolani – Mwanza, na yaliongozwa na Mkufunzi wa Waamuzi wa Mkoa wa Mwanza, Alfed Lizwa.

Akizungumza wakati wa kumkaribisha mgeni rasmi, Mwenyekiti wa Chama cha Soka Nyamagana (NDFA), Said Abdallah “Kizota”, alisema wanafarijika kuona malengo na mikakati waliyoiweka wakati wa kuomba uongozi yakitekelezwa kwa vitendo.

“Tunawashukuru wadau wote wanaotushika mkono katika kutimiza jukumu hili. Sio kazi rahisi, lakini kwa umoja wetu tumefanikiwa kufanya jambo ambalo wengine walishindwa. Tumekuwa wilaya ya kwanza kutoa mafunzo haya kwa waamuzi wetu ili wawe hodari, makini na wafuate sheria ipasavyo uwanjani,” alisema Kizota.

Akifungua rasmi mafunzo hayo, Katibu Tawala wa Wilaya ya Nyamagana (DAS), Thomas James Salala, alisema Wilaya imejipanga kuendelea kuuwezesha mchezo wa mpira wa miguu ili mafanikio yaonekane kwa matokeo chanya.

Amewaasa waamuzi kujiendeleza na kufuatilia mabadiliko ya sheria mpya za soka ambazo zimefanyiwa maboresho duniani kote kulingana na mahitaji ya sasa ya mchezo huo.

Kwa upande wake, Mkufunzi Alfed Lizwa alisema amefurahishwa na mwitikio wa waamuzi waliojitokeza na kwamba hatua hiyo itaongeza ubora wa usimamizi wa mechi katika mashindano mbalimbali ya wilaya na mkoa.

Naye Makamu Mwenyekiti wa NDFA na Mratibu wa Warsha hiyo, Oscar Kapinga, alisema chama kitaendelea kuratibu mafunzo k**a hayo si kwa waamuzi pekee, bali pia kwa makundi mengine yanayohusika na usimamizi wa mchezo wa mpira wa miguu katika Wilaya ya Nyamagana, ili kuongeza ufanisi na kuleta maendeleo.

13/11/2025

Ukambani mnasemaje? Anaitwa William Samoei Arap RUTO

12/11/2025

Rafiki wa kweli yupoo!! Mtegemee yeye.

12/11/2025

Makamu Mwenyekiti wa Chama Cha Demokrasia na Maendeleo Chadema John Heche ameiomba Mahak**a iharakishe usikilizwaji wa Kesi ya Uhaini inayomhusu Mwenyekiti wa Chama hicho Tundu Lissu.

Kuna mambo yanashangaa yakitamkwa na mtu anayeshimika. Tena mtu halisia kwenye nafasi nyeti ambayo ameaminiwa nayo.Sitak...
12/11/2025

Kuna mambo yanashangaa yakitamkwa na mtu anayeshimika. Tena mtu halisia kwenye nafasi nyeti ambayo ameaminiwa nayo.

Sitaki kuwakurudisha nyuma kwa kile kinachoendelea baina ya Wasimamizi wa Idara ya Habari Yanga na Mwanahabari Nguli Nassib Mkomwa Mr Ripota.

Mr Ripota ametoa taarifa kwa Umma kuhusu Mchezaji Aziz Andambwile kuidai Yanga wanaomwona adui wakati kawasanua.

Msimamizi wa Mchezaji huyo amezungumza kupitia Media mojawapo leo nae inaonekana ni Winga k**a vile walivyomuita Jasmine Razak.

Kwani kudaiwa ni DHAMBI? Mbona watu wengi wanadaiwa! Taasisi nyingi zinadaiwa na hakuna tatizo? Au Kuna Nini mnaficha?

Idara ya Habari imeanza kupambana kusawazisha ili ionekane hakuna tatizo kumbe tatizo ni kubwa tu.

Mbona sasa hivi Yanga kuanzia kwa wanene hadi kwa mashabiki ni wakali sana. Mkiambiwa timu yenu imechoka, Mnakuja juu k**a pilipili.

Mkiambiwa Kocha wenu bado sana, mnaona kuna tatizo kwamba watu wanaisak**a timu yao! Kwani mkikaa kimia Kuna ubaya gani?

Kuna wakati inafirikisha sana kwamba kwanini mnajihami? Mnaficha Nini au mnataka Jamii ielewe kwamba nyinyi ni watu wa aina gani?

11/11/2025

“Mkuu wa Mkoa wa Mwanza, Mheshimiwa Said Mohamed Mtanda, ametangaza rasmi kuondolewa kwa zuio la kufunga maeneo ya uuzaji wa vinywaji baridi na moto saa 4 usiku. Kuanzia sasa, maeneo hayo yanaruhusiwa kuendelea na shughuli zao bila kikwazo—ni mseleleko tu.”

09/11/2025

Dakika 90 za henyahenya baina ya Yanga SC vs KMC pale KMC Complex Mwenge Dar es Salaam.

Good Start ya teka Andy Boyeli, amefunga Magoli 2z Pacome 1 na Maxi Nzengele 1.

KMC Ina Ina timu ila Ina wachezaji wenye ubora wachache. Kocha Maximo naona k**a vile jahazi linaenda mrama.

Huenda kuanzia leo mkasikia jambo linaitwa taarifa kwa umma maana sio kwa mwenendo huo wa tia maji tia maji.

Saliboko, M***a na Chambo wana kitu. Kuna yule Kiungo Nindi Jr naye ana mambo mambo miguuni kwake.

Yanga amepata ushindi ila Soka la leo ni Soka fakamia fakamia. Mipango mipango haijaonekana.

Tumpe Muda Kocha Pedro na wasaidizi wake huenda wakikutana na JS Kabylie ya kina Babacar Sarr watatupa mechi ya maana.

FT | Yanga SC 4 - 1 KMC

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Famara Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Famara Media:

Share