09/09/2026
SIMBA: MWAMBIE KOCHA WENU AACHE KUPENDELEA, VIPAJI VISIPOTEZWE!
Mwambieni Kocha wenu kwamba aliikuta Simba, na siku moja ataondoka na kuiacha Simba. Hivyo basi, asiingie kwenye historia ya klabu kwa kuharibu vipaji vya watoto wa watu kwa maamuzi ambayo hayaeleweki!
Inawezekanaje mchezaji asajiliwe ndani ya timu halafu kocha asihusishwe au asipitishe usajili huo? K**a kweli mfumo huo upo, basi kuna maswali mengi yanahitaji majibu. Becker asiwaone watu wajinga!
Na swali kubwa zaidi ni hili: Kwa nini Kelvin Nashon, ambaye ni mchezaji wa nafasi ya 6, akae pembeni wakati Gift Maema anaonekana kupewa nafasi hiyo? Hii ni aina ya maamuzi ambayo yanawafanya mashabiki kujiuliza k**a kweli vipaji vinatumika kwa haki.
Hata Inno Loemba naye amekuwa akipata nafasi chache. K**a wachezaji wenye uwezo hawapati nafasi ya kuonyesha walichonacho, basi tutaanza kujiuliza: tatizo ni wachezaji au ni namna wanavyotumiwa?
Kwa upande wetu sisi Wana Mwanza, Kelvin Nashon si mchezaji wa kawaida tu. Ni moja ya brand za soka la Mwanza, kijana ambaye tunamtazamia kuonyesha dira na kuiwakilisha Mwanza kwenye ramani kubwa ya soka.
Tunataka kuona vipaji vinapewa nafasi, vinajengwa na kutumika kwa usahihi—si kukaa benchi bila maelezo yanayoeleweka.
Kocha, Simba ni kubwa kuliko mtu mmoja.
Aliyekuja leo ataondoka kesho, lakini historia ya maamuzi yake itabaki.
Kwa hiyo, mwambieni Becker aache utoto. Aache kufanya maamuzi yanayoweza kuua morali na kupoteza vipaji.
Kelvin Nashon anastahili nafasi ya kuonyesha uwezo wake. Mwanza tunamtazama. Simba tunaitazama. Soka la Tanzania linamtazama.
VIPAJI VISIZUIWE. VIPAJI VITUMIKE! 🔥⚽