Famara Media

Famara Media Famara Media - Inform, Entertain and Educate.

05/06/2026

HII NDIO ESTADIO BANORTE (zamani Estadio Azteca) – Mexico.

Estadio Banorte ni moja ya viwanja maarufu zaidi duniani na iko katika Jiji la Mexico (Mexico City). Uwanja huu unafanyiwa maboresho makubwa kuelekea Kombe la Dunia la FIFA 2026.
Taarifa Muhimu za Uwanja.

✓Jina la sasa: Estadio Banorte
✓Jina la awali: Estadio Azteca
✓Mahali: Coyoacán, Mexico City, Mexico
Mwaka uliojengwa: 1966
✓Uwezo wa mashabiki: Takribani watu 83,000–87,000 (kutegemea mpangilio wa viti baada ya maboresho)
✓Aina ya uwanja: Uwanja wa mpira wa miguu wenye nyasi za asili
✓Wamiliki: Grupo Ollamani

Vilabu vinavyoutumia: ✓Club América na Cruz Azul (kwa baadhi ya mechi).

Estadio Banorte ni moja ya viwanja vya kihistoria zaidi katika soka duniani. Ni uwanja pekee ambao umewahi kuandaa fainali mbili za Kombe la Dunia la FIFA:
FIFA World Cup 1970
FIFA World Cup 1986

Katika uwanja huu:
Pelé alitwaa Kombe la Dunia mwaka 1970 akiwa na Brazil.
Diego Maradona aliiongoza Argentina kutwaa ubingwa mwaka 1986 na kufunga mabao maarufu ya "Hand of God" na "Goal of the Century".

Estadio Banorte itakuwa moja ya viwanja vya mashindano nchini Mexico.

Inatarajiwa kuwa uwanja wa kwanza duniani kuandaa mechi za Kombe la Dunia katika matoleo matatu tofauti (1970, 1986 na 2026).

Umefanyiwa maboresho ya miundombinu, maeneo ya wageni wa VIP, vyumba vya waandishi wa habari, sehemu za mashabiki na teknolojia za kisasa za usalama.

Vipimo vya uwanja: mita 105 × 68 (viwango vya FIFA)
Aina ya nyasi: Nyasi za asili zilizoboreshwa kwa viwango vya FIFA
Vyumba vya kubadilishia nguo: Vya kisasa kwa timu na waamuzi
Mifumo ya taa: Taa za kisasa za LED zinazokidhi viwango vya matangazo ya kimataifa
Kamera za kisasa, njia za dharura na udhibiti wa umati.

Estadio Banorte ni moja ya alama kuu za Kombe la Dunia 2026 kwa sababu ya historia yake kubwa, uwezo wake wa kubeba mashabiki wengi, na nafasi yake katika maendeleo ya soka la kimataifa.

Uwanja huu unatarajiwa kuwa miongoni mwa viwanja vitakavyovutia mashabiki wengi zaidi.

03/06/2026

Tumjibu huyu wanayanga?

02/06/2026

📢 tunaungana na Watanzania wote kuisapoti katika mchezo wa Fainali dhidi ya Senegal leo.

Tukiwa pamoja na Mkuu wa Mkoa wa Mwanza , tumeungana katika kuwapa hamasa na nguvu vijana wetu wanaoiwakilisha Tanzania katika hatua hii muhimu.

Tunawatakia kila la heri Serengeti Boys. Pambaneni kwa moyo, nidhamu na uzalendo. Tanzania ipo nyuma yenu na inaamini katika uwezo wenu.

🇹🇿⚽ Mshik**ano wetu ni nguvu yao, ushindi wetu ni fahari ya Taifa.

MASHABIKI WENYE WIVU WOTE, TIMU ZENU ZINA WACHEZAJI WANGAPI KATIKA KIKOSI BORA CHA UEFA?Ukweli hauwezi kufichwa. Wakati ...
01/06/2026

MASHABIKI WENYE WIVU WOTE, TIMU ZENU ZINA WACHEZAJI WANGAPI KATIKA KIKOSI BORA CHA UEFA?

Ukweli hauwezi kufichwa. Wakati wengine wakitafuta sababu za kubeza mafanikio ya wenzao, takwimu na utendaji wa wachezaji uwanjani ndivyo vinavyozungumza. Kuwa na wachezaji wengi katika kikosi bora cha UEFA ni ishara ya ubora, juhudi na kiwango cha juu cha ushindani.

Wivu hauongezi mafanikio wala haupunguzi mafanikio ya wengine. Badala ya kutafuta kasoro kwenye mafanikio ya wapinzani, ni vyema kuthamini ubora na kujifunza kutoka kwa waliopiga hatua. Soka ni mchezo wa ushindani, lakini pia ni mchezo wa kuheshimu mafanikio yanayopatikana kwa jasho na uwezo. ⚽🔥🏆

- Mdau DM

01/06/2026

Mwanza kutazama Fainali ya Serengeti Boys vs Senegal U17 pale Sato Sagara Rock City Mall. RC wa Mwanza Said Mtanda athibithisha.

01/06/2026

Ujenzi wa Uwanja wa Kisasa wa Arusha unaoendelea chini ya Serikali ya Tanzania umefikia hatua za kuridhisha, jambo linaloonyesha dhamira ya nchi kujiandaa kwa mafanikio kuelekea mashindano ya Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027.

Mradi huo mkubwa wa kimkakati unalenga kuimarisha miundombinu ya michezo nchini na kuiwezesha Tanzania kuwa mwenyeji wa mashindano ya kimataifa kwa viwango vinavyokubalika na Shirikisho la Soka Afrika (CAF). Uwanja huo unatarajiwa kuwa miongoni mwa viwanja vitakavyotumika wakati wa AFCON 2027, ambayo Tanzania itashirikiana kuandaa pamoja na Kenya na Uganda.

Picha za maendeleo ya ujenzi zinaonyesha kazi mbalimbali zikiendelea kwa kasi, ikiwemo uwekaji wa miundombinu ya msingi, maeneo ya watazamaji na huduma nyingine muhimu zinazohitajika katika uwanja wa kisasa.

Kukamilika kwa mradi huo kutaleta manufaa makubwa kwa sekta ya michezo, utalii na uchumi wa Mkoa wa Arusha, huku ukifungua fursa zaidi za ajira na biashara kwa wananchi wa eneo hilo.

Maendeleo hayo yanaendelea kuwapa matumaini Watanzania wengi wanaosubiri kuona nchi yao ikiandika historia kwa kuwa sehemu ya waandaaji wa AFCON 2027, mashindano makubwa zaidi ya soka barani Afrika.

KWANINI ARSENAL INACHUKIWA?Mashabiki wa Arsenal wameendelea kuhoji sababu za kuonekana kwa upinzani mkubwa kutoka kwa ma...
31/05/2026

KWANINI ARSENAL INACHUKIWA?

Mashabiki wa Arsenal wameendelea kuhoji sababu za kuonekana kwa upinzani mkubwa kutoka kwa mashabiki wa timu nyingine baada ya mafanikio ya klabu hiyo.

Baadhi yao wanaamini kuwa ushindani huo umeongezeka kutokana na Arsenal kurejea katika kiwango cha juu na kusherehekea mafanikio yake kwa nguvu.

Wanasema hawana tatizo na timu nyingine, bali wanaona ni kawaida kushangilia mafanikio makubwa k**a ubingwa wa EPL.

Huku wakitazama mbele, mashabiki wa Gunners wana matumaini kuwa usajili mpya, maandalizi bora na mbinu sahihi zitaiwezesha timu yao kufanya vizuri zaidi na kuwania taji la UEFA msimu ujao.

"Mafanikio si bahati, ni matokeo ya mipango na mikakati sahihi.

🔴⚪️🏆

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: Klabu ya Slavia Prague ya Czech Republic,imetuma ofa ya €190,000 (tsh 580,944,000) ili kuipata huduma ya kinda...
30/05/2026

𝐁𝐑𝐄𝐀𝐊𝐈𝐍𝐆: Klabu ya Slavia Prague ya Czech Republic,imetuma ofa ya €190,000 (tsh 580,944,000) ili kuipata huduma ya kinda wa Serengeti Boys na klabu ya Fountain Gate,Issah Chole (16).

Ofa hiyo bado inachakatwa kwani pia vilabu vya Como ya Italia na Malmo FF ya Sweeden🇸🇪 vinamtaka kiungo huyo wa chini.

Chole anaweza kucheza k**a kiungo namba 6 na 8 pia Simba na Yanga wameilizia upatikanaji wake.

Chanzo:

28/05/2026

🇲🇦 Morocco yaaga AFCON U-17 nyumbani baada ya kutolewa na Senegal kwa mikwaju 7-6 ya penalti katika mchezo wa nusu fainali uliochezwa usiku wa leo.

Timu hizo zilimaliza dakika 90 kwa sare ya 1-1 kabla ya Senegal kuibuka na ushindi kwenye changamoto ya mikwaju ya penalti na kufuzu fainali.

Kwa ushindi huo, Senegal sasa itakutana na Serengeti Boys 🇹🇿 kwenye mchezo wa fainali utakaopigwa Jumapili, Mei 31, 2026.

Wakati huohuo, Morocco itachuana na Misri kuwania nafasi ya tatu ya mashindano hayo.

28/05/2026

Timu ya Taifa ya Vijana wenye Umri wa chini ya Miaka 17, Serengeti Boys 🇹🇿 imeandika historia nyingine baada ya kufanikiwa kutinga fainali kwa kishindo, kufuatia ushindi wa mikwaju ya penalti 4-2 dhidi ya Misri katika mchezo wa nusu fainali uliokuwa na ushindani mkubwa na wenye presha ya hali ya juu.

Mchezo huo ulionesha nidhamu, moyo wa kupambana na umoja wa hali ya juu kutoka kwa vijana wetu, ambao hawakukata tamaa hadi dakika ya mwisho, hali iliyowawezesha kuibuka na ushindi muhimu na wa kihistoria.

Baada ya mafanikio hayo, Serengeti Boys sasa wanasubiri mshindi wa nusu fainali ya pili kati ya Morocco dhidi ya Senegal, mchezo unaotarajiwa kuchezwa leo saa 4:00 usiku.

Hongereni sana Serengeti Boys 🇹🇿 kwa kutuletea furaha, kujituma na kulitangaza vyema taifa letu kimataifa. Mmeifanya Tanzania ijivunie leo—endelea kuandika historia mpya ya soka la vijana Afrika! 👏⚽🇹🇿

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Famara Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Famara Media:

Share