02/01/2026
MAKILAGI SPORTS WEAR YATOA SHUKRANI KWA WATEJA WAKE.
Duka la vifaa vya michezo la Makilagi Sports Wear, lililopo katika ofisi za Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, limetoa shukrani za dhati kwa wateja wake wote waliounga mkono huduma na bidhaa zake kwa kipindi cha mwaka 2025.
Akizungumza mwanzoni mwa mwaka mpya 2026, Mkurugenzi wa Makilagi Sports Wear, Bi. Sophia Makilagi, amesema mafanikio yaliyopatikana yametokana na imani na ushirikiano mkubwa kutoka kwa wateja wao wa ndani ya Mkoa wa Mwanza na nje ya mkoa.
Bi. Makilagi amesema katika mwaka 2025, duka hilo lilifanikiwa kuuza bidhaa mbalimbali za michezo zikiwemo jezi, mipira pamoja na vifaa vya mazoezi kwa wadau wengi wa michezo, hali iliyochangia ukuaji na uimara wa biashara hiyo.
“Tunamshukuru Mungu kwa kutuvusha salama mwaka 2025 na kutuwezesha kuanza mwaka mpya 2026 kwa mafanikio. Tunatoa shukrani za dhati kwa wateja wetu wote waliotufikia dukani pamoja na wale waliokuwa mbali waliotuamini kwa kuagiza bidhaa zetu. Tunaomba ushirikiano huu uendelee na uwe mkubwa zaidi katika mwaka huu wa 2026,” amesema Bi. Makilagi.
Katika wateja waliotoa mchango mkubwa kwa kununua mizigo kwa wingi mwaka 2025, Bi. Makilagi amewataja Mwenyekiti wa Copco FC, Simon Romli, Nyaitato Stephano Mwenyekiti wa Alliance Sports Academy Augustino Yassaya Mbogo ambaye ni Katibu wa CCM Wilaya ya Ngorongoro, pamoja na Wilbert Mweta Mkurugenzi wa Mweta Sports Centre, akisema walionesha mfano mzuri wa kuunga mkono biashara za ndani.
Aidha, Makilagi Sports Wear imeeleza mpango wake wa kuwaandalia Vyeti vya Shukrani wadau hao k**a sehemu ya kutambua mchango wao katika kusaidia kukuza duka hilo na maendeleo ya vifaa vya michezo Mkoa wa Mwanza.
Cc