Famara Media

Famara Media Famara Media - Inform, Entertain and Educate.

SIMBA: MWAMBIE KOCHA WENU AACHE KUPENDELEA, VIPAJI VISIPOTEZWE!Mwambieni Kocha wenu kwamba aliikuta Simba, na siku moja ...
09/09/2026

SIMBA: MWAMBIE KOCHA WENU AACHE KUPENDELEA, VIPAJI VISIPOTEZWE!

Mwambieni Kocha wenu kwamba aliikuta Simba, na siku moja ataondoka na kuiacha Simba. Hivyo basi, asiingie kwenye historia ya klabu kwa kuharibu vipaji vya watoto wa watu kwa maamuzi ambayo hayaeleweki!

Inawezekanaje mchezaji asajiliwe ndani ya timu halafu kocha asihusishwe au asipitishe usajili huo? K**a kweli mfumo huo upo, basi kuna maswali mengi yanahitaji majibu. Becker asiwaone watu wajinga!

Na swali kubwa zaidi ni hili: Kwa nini Kelvin Nashon, ambaye ni mchezaji wa nafasi ya 6, akae pembeni wakati Gift Maema anaonekana kupewa nafasi hiyo? Hii ni aina ya maamuzi ambayo yanawafanya mashabiki kujiuliza k**a kweli vipaji vinatumika kwa haki.

Hata Inno Loemba naye amekuwa akipata nafasi chache. K**a wachezaji wenye uwezo hawapati nafasi ya kuonyesha walichonacho, basi tutaanza kujiuliza: tatizo ni wachezaji au ni namna wanavyotumiwa?

Kwa upande wetu sisi Wana Mwanza, Kelvin Nashon si mchezaji wa kawaida tu. Ni moja ya brand za soka la Mwanza, kijana ambaye tunamtazamia kuonyesha dira na kuiwakilisha Mwanza kwenye ramani kubwa ya soka.

Tunataka kuona vipaji vinapewa nafasi, vinajengwa na kutumika kwa usahihi—si kukaa benchi bila maelezo yanayoeleweka.

Kocha, Simba ni kubwa kuliko mtu mmoja.
Aliyekuja leo ataondoka kesho, lakini historia ya maamuzi yake itabaki.

Kwa hiyo, mwambieni Becker aache utoto. Aache kufanya maamuzi yanayoweza kuua morali na kupoteza vipaji.

Kelvin Nashon anastahili nafasi ya kuonyesha uwezo wake. Mwanza tunamtazama. Simba tunaitazama. Soka la Tanzania linamtazama.

VIPAJI VISIZUIWE. VIPAJI VITUMIKE! 🔥⚽

Magazeti Septemba 9, 2026.
09/09/2026

Magazeti Septemba 9, 2026.

Magazeti Septemba 7, 2026.
07/09/2026

Magazeti Septemba 7, 2026.

05/09/2026

POLISI MWANZA WAZINDUA KAMPENI YA USALIMISHAJI SILAHA

JESHI la Polisi Mkoa wa Mwanza limeanza kampeni ya kuhamasisha wananchi kusalimisha silaha zinazomilikiwa kinyume cha sheria, kufuatia uzinduzi wa kampeni hiyo kitaifa uliofanywa na Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, Patrobas Katambi, Agosti 31, 2026.

Kampeni hiyo imeanza Septemba 1 na inatarajiwa kuhitimishwa Oktoba 31, 2026, ikiwa na lengo la kuwapa wananchi wanaomiliki silaha bila usajili au vibali halali fursa ya kuzisalimisha kwa hiari.

Polisi imesema silaha zinazolengwa ni pamoja na zisizo na usajili au vibali, silaha za watu waliofariki ambazo hazijawasilishwa serikalini, pamoja na zile zinazomilikiwa na watu waliopoteza sifa za kuzimiliki.

Zoezi hilo litafanyika kupitia vituo vya Polisi, Ofisi za Wakuu wa Wilaya, viongozi wa Serikali za Mitaa na Vijiji pamoja na viongozi wengine wa maeneo husika.

Jeshi la Polisi limewataka wananchi kutumia kipindi hicho cha msamaha kusalimisha silaha hizo kwa hiari, likisisitiza kuwa baada ya muda huo kumalizika, hatua za kisheria zitachukuliwa dhidi ya watakaobainika kumiliki silaha kinyume cha sheria.

Kampeni hiyo inalenga kuimarisha amani, utulivu na usalama kwa kushirikisha wananchi katika kudhibiti uzagaaji wa silaha zinazomilikiwa kinyume cha sheria.

05/09/2026

MATEMBEZI YA HISANI YA MTOTO NI MALEZI YAFANYIKA MWANZA.

MWANZA: MatembezI ya hisani ya “Mtoto ni Malezi Fun Run” yamefanyika leo, Septemba 5, 2026, katika Uwanja wa CCM Kirumba jijini Mwanza, yakilenga kuhamasisha jamii kuhusu umuhimu wa malezi chanya na ulinzi wa watoto katika familia na jamii.

Matembezi hayo yaliandaliwa na Shirika la Compassion International Tanzania kwa kushirikiana na SOS Children’s Villages pamoja na ICD, yakihusisha wadau mbalimbali wa masuala ya watoto, wazazi na wananchi waliojitokeza kuunga mkono kampeni hiyo.

Lengo kuu la matembezi hayo lilikuwa kuongeza uelewa kwa wazazi na walezi kuhusu umuhimu wa kutoa malezi yenye upendo, usalama, mawasiliano mazuri na muda wa kutosha kwa watoto, hasa katika kipindi ambacho familia zinakabiliwa na changamoto mbalimbali za kijamii na mabadiliko ya teknolojia.

Akizungumza wakati wa tukio hilo, Mkuu wa Wilaya ya Nyamagana, Amina Makilagi, aliyemwakilisha Waziri wa Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Dkt. Dorothy Gwajima, amesema malezi ya watoto ni jukumu la msingi linalohitaji ushirikiano wa wazazi, walezi, jamii na wadau mbalimbali.

Amesema wazazi wanapaswa kutenga muda wa kutosha kwa ajili ya watoto wao, kwa kuwa uwepo wa mzazi katika maisha ya mtoto ni muhimu katika kujenga msingi mzuri wa ukuaji, maadili, kujiamini na maendeleo ya mtoto.

«“Malezi ni jambo muhimu sana. Wazazi tunapaswa kutenga muda wa kutosha kwa watoto wetu, kuwasikiliza, kuwafundisha na kuwapa mazingira salama ya kukua. Tukifanya hivyo, tunajenga kizazi bora kwa ajili ya taifa letu,” amesema Makilagi.»

Aidha, ametoa wito kwa jamii kuendelea kushirikiana katika kuhakikisha watoto wanalelewa katika mazingira salama na yenye upendo, huku akisisitiza umuhimu wa kuwakinga dhidi ya ukatili, unyanyasaji na vitendo vinavyoweza kuhatarisha ustawi wao.

Kwa upande wao, waandaaji wa kampeni hiyo wameeleza kuwa “Mtoto ni Malezi Fun Run” si tukio la michezo pekee, bali ni sehemu ya juhudi za kuifikia jamii.

Magazeti Septemba 5, 2026.
05/09/2026

Magazeti Septemba 5, 2026.

04/09/2026

Watafiti kutoka taasisi mbalimbali nchini wametakiwa kufanya tafiti zitakazosaidia kubaini namna bora ya kulea watoto katika dunia ya sasa, inayokabiliwa na mabadiliko makubwa ya teknolojia, uchumi na jamii.

Wito huo umetolewa leo, Septemba 4, 2026, jijini Mwanza na Kaimu Katibu Tawala wa Mkoa wa Mwanza, Dk. Silas Wambura, aliyemwakilisha Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wanawake na Makundi Maalum, Eliakim Maswi, wakati akifungua mdahalo kuhusu kuimarisha afua za malezi nchini.

Dk. Wambura amesema mabadiliko ya teknolojia, ikiwemo matumizi ya akili bandia (AI) na mitandao ya kijamii, yameleta mazingira mapya ambayo yanahitaji utafiti wa kina ili jamii iweze kupata mbinu sahihi za malezi ya watoto.

Kwa upande wake, Ofisa Tarafa wa Ilemela, James Chuwa, aliyemwakilisha Mkuu wa Wilaya ya Ilemela, Amir Mkalipa, amesema malezi si jukumu la Serikali pekee, bali yanahitaji ushirikiano wa wazazi, Serikali, asasi za kiraia, taasisi za dini na wadau wengine.

Amesema Serikali haiwezi kufika kila mahali bila ushirikiano wa jamii na wadau wanaoshiriki katika kuhakikisha watoto wanalelewa katika mazingira salama na yenye kuwawezesha kukua vizuri.

Akizungumzia changamoto hizo, Askofu Mkuu wa AICT, M***a Magwesela, amesema mwingiliano wa tamaduni, matumizi ya teknolojia, akili bandia na mitandao ya kijamii umeongeza changamoto katika malezi, hivyo wazazi wanapaswa kupata uelewa mpya unaoendana na dunia ya sasa.

Naye Mkurugenzi wa Compassion International Tanzania, Mary Lema, amesema shirika hilo lina vituo 600 vya malezi vinavyosimamiwa na makanisa katika wilaya 91 nchini, akisisitiza kuwa ushirikiano wa wadau ni muhimu katika kuimarisha malezi ya watoto.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Miradi wa SOS Children’s Villages Tanzania, John Fulli, amesema malezi bora ni msingi wa ulinzi na ustawi wa mtoto, hivyo yanapaswa kuangalia kwa pamoja ustawi wa familia, ulinzi, lishe bora na usalama wa mtoto.

Nini kinaendelea kwa wachezaji hawa! Hawana kiwango au hati za uraia hazijakamilika?
04/09/2026

Nini kinaendelea kwa wachezaji hawa! Hawana kiwango au hati za uraia hazijakamilika?

"Uhuru Kenyatta alimdanganya Shemeji yangu Raila Odinga kwa atalipia agents huko Mlima Kenya.  K**a tulikuwa na Kila kit...
04/09/2026

"Uhuru Kenyatta alimdanganya Shemeji yangu Raila Odinga kwa atalipia agents huko Mlima Kenya. K**a tulikuwa na Kila kitu, Serikali, majeshi na nguvu ya pesa ila William Ruto akatushinda? Nani anaweza kumshinda Ruto? Huyu Sifuna hana kura Western zaidi ya kutaka kugawa kura ila tutashida"

Francis Atwoli - Katibu Mkuu COTU

Magazeti Septemba 4, 2026.
04/09/2026

Magazeti Septemba 4, 2026.

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Famara Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Famara Media:

Shortcuts

Share