Famara Media

Famara Media Famara Media - Inform, Entertain and Educate.

22/08/2025
21/08/2025

Kiungo mshambuliaji aliyesajiliwa na wekundu wa msimbazi Simba Sports Club Neo Maema maarufu k**a Neymar huyu hapa.

Kuna kazi pale mbele dhidi ya timu pinzani. Inahitaji akili kubwa sana kumkaba na kuzuia asisambaze pasi za Upendo.

Johnathan Sowah! Seleman Mwalimu! Steven Mukwala watafunga sana.

Ni k**a vile Rally Bwalya, k**a vile Bukayo Saka na k**a vile Lionel Messi.

Ukisema ni mchezaji wa kawaida au hana maajabu, wewe ni BANDOKI!!!

Mpe maksi zakooo bila kupendelea na kuangalia upande A u B.

JEAN CHARLES AHOUA | SPINNING DOCTOR.✓Msimu wa kwanza amehusika na jumla ya Magoli 25. Magoli 16 | Assist 9.✓Ndiye mfung...
21/08/2025

JEAN CHARLES AHOUA | SPINNING DOCTOR.

✓Msimu wa kwanza amehusika na jumla ya Magoli 25.
Magoli 16 | Assist 9.

✓Ndiye mfungaji bora wa msimu uliyopita NBC Premier League

✓Anapewa nafasi ya kuwa MVP wa msimu uliopita kutokana na mchango na namba zake.

✓Bado mdogo anakua na huenda msimu huu akafanya vizuri zaidi k**a atapewa namba mara kwa mara.

✓Kwenye nafasi yake wapo wachezaji waliosajili na waliokuwepo msimu uliopita.

✓Swali la kujiuliza, uhakika wa yeye kucheza utakuwepo! Je atapata namba mara kwa mara?

✓Namba anayocheza 10 wapo wachezaji wengi.

1. Awesu Awesu - aliyekuwepo toka msimu uliopita
2. Neymar Maema - bado hajatangazwa
3. Elie Mpanzu - anaweza kucheza namba hiyo ingawa anaweza pia kutokea pembeni
4. Mohamed Bajaber - anamudi hiyo namba pamoja kwamba anaweza kuwa anatoka pembeni.

Mimi bado naona JEAN CHARLES AHOUA ana nafasi ya kucheza kwa sababu ya ubora wake.

Upigaji penalti
Upigaji set peace

Wewe unaonaje?

USAJILI WA SELEMAN MWALIMU "GOMEZ" AMEFAULU AU AMEFELI?Seleman Mwalimu maarufu k**a Gomez amejiunga Simba SC akitokea Wy...
18/08/2025

USAJILI WA SELEMAN MWALIMU "GOMEZ" AMEFAULU AU AMEFELI?

Seleman Mwalimu maarufu k**a Gomez amejiunga Simba SC akitokea Wydad Casablanca ya Morocco.

Maneno yamekuwa mengi sana. Watu wanajiuliza amefaulu au amefeli katika usajili huu?

1. Mtazamo wa namba za CAF Club Ranking

Wydad Casablanca ipo nafasi ya chini (namba 8 Afrika).

Simba SC ipo nafasi ya juu (namba 5).
Kihesabu, mtu akihama kutoka timu ya chini kwenda ya juu, watu wanaweza kusema “amepungua thamani”. Lakini mpira sio tu namba, kuna mambo ya ndani zaidi.

2. Sababu zinazothibitisha kuwa Mwalimu “amefaulu” kujiunga Simba SC

Simba ni Klabu Kubwa Afrika Mashariki: Ina mashabiki wengi sana, nguvu ya kibiashara, na heshima kwenye mashindano ya CAF. Hivyo, hadhi ya kimataifa inabaki kubwa.

Nafasi ya Kujitambulisha: Wydad imejaa majina makubwa, mara nyingi makocha na wachezaji wanamezwa.

Simba inampa Gomez jukwaa la kuonekana k**a staa namba moja na kuendesha kikosi.

Fursa ya Kibiashara na Kifedha: Simba inalipa vizuri, na mara nyingi hulipa sawasawa au zaidi kwa baadhi ya makocha/wachezaji kulingana na kiwango chao.

Ubora wa Mashindano: Simba inashiriki Ligi ya Mabingwa CAF mara kwa mara. Hivyo hakuondoka kwenye mashindano makubwa.

Mikakati ya Maendeleo: Simba inajenga brand yake kushindana na Wydad, Al Ahly, na Mamelodi. Kujiunga nayo ni kuwa sehemu ya “mradi wa ukuaji”.

3. Sababu zinazoweza kuleta tafsiri ya “amepungua”

Kwa mtu anayetazama namba tu, kutoka namba 8 kwenda namba 5 kwamba ni kushuka. Sio kweli kweli 5 ni kubwa kuliko 8.

Ligi ya Morocco inatajwa kuwa ngumu zaidi kimashindano ukilinganisha na Tanzania. Kwa hiyo kuna anaweza kusema amepunguza changamoto za ushindani.

4. Hitimisho
Kujiunga Simba SC si kushuka bali ni hatua ya kimkakati.

Gomez amehama kutoka klabu yenye jina kubwa kwenda nyingine yenye mradi mkubwa unaokua haraka.

Hapa anapata nafasi ya kujulikana zaidi, kuwa kiongozi uwanjani, na kuendeleza jina lake kwenye ramani ya CAF.

Kwa hiyo tafsiri sahihi ni kwamba amefaulu

Jonathan Sowah ni mshambuliaji mpya wa timu ya Simba SC. Amesajiliwa kutoka Singida Black Stars.Singida Black Stars wali...
12/08/2025

Jonathan Sowah ni mshambuliaji mpya wa timu ya Simba SC. Amesajiliwa kutoka Singida Black Stars.

Singida Black Stars walimchukua kutoka FC Madeama dirisha dogo na alisaidia Singida kupata ushindi katika mchezo mbalimbali.

Alifanikiwa kufunga goli 13 pamoja na kuingia kwenye dirisha dogo.

Sowah sasa anaenda kuanza kampeni ya kuitafutia Simba SC ushindi kwa kufunga Magoli?

Kwa jicho lako unavyomwona na ulivyomwona kipindi akiwa Singida Black Stars, anaweza kuisaidia Simba?

Umahiri wake anaweza kufunga goli ngapi kwa zile pasi za Ahoua na Mpanzu?

Powered by

Sielewi viongozi wa Yanga Wana tatizo gani? Kwanini mnamwambia Clement Mzize aachane na Msimamizi wake? Kwanini mnapenda...
10/08/2025

Sielewi viongozi wa Yanga Wana tatizo gani? Kwanini mnamwambia Clement Mzize aachane na Msimamizi wake? Kwanini mnapenda sana kuwapangia wachezaji nani awasimamie? Mlianza kwa Farid M***a Malik, Metacha Mnata. Kwanini hampendi msimamizi wa mchezaji kutoa mawazo ya mchezaji maana yeye k**a player hawezi kuzungumza na nyinyi? Hii Inaitwa ROHO MBAYA.

"Achana na Jasmine k**a unataka ufanikiwe" Kataaeni ofa na sio kumshinikiza mchezaji. K**a mtapata Nini au mnataka nyinyi ndio muwe Mabosi wake na wasimamizi wake? Sijui tutawaambia muwe professional mara ngapi?

Acheni uzamani na muwe focus kiweledi.

Ni AIBU.

KOSA LA JASMINE RAZAK NI LIPI?Jasmine Razak ni mwanasheria na wakili wa michezo ambaye amejiwekea heshima kubwa kwa kute...
10/08/2025

KOSA LA JASMINE RAZAK NI LIPI?

Jasmine Razak ni mwanasheria na wakili wa michezo ambaye amejiwekea heshima kubwa kwa kutetea maslahi ya wachezaji anaowasimamia kwa weledi wa hali ya juu katika nyanja za sheria na ushauri wa kitaaluma.

Umaarufu wake ulianza kung’aa wakati alipomsimamia Simon Msuva kwenye mzozo na klabu ya Wydad Casablanca, Morocco. Kupitia juhudi na ujuzi wake, Msuva alishinda kesi hiyo na kulipwa haki zake zote.

Safari ya mafanikio ya Jasmine haikuishia hapo. Alisimamia kwa ustadi uhamisho wa Feisal Salum "Feitoto" kutoka Yanga SC kwenda Azam FC. K**a ilivyokuwa kwa Msuva, Feitoto alihama kwa dau kubwa na kuanza kulipwa mshahara wa heshima. Taarifa za ndani zinaeleza kuwa Yanga alikuwa analipwa milioni 2 tu kwa mwezi, lakini Azam anapata takribani milioni 24 – ongezeko la mara kumi! Hakika, signing fee, mshahara na marupurupu yake vilipanda maradufu chini ya usimamizi wa Jasmine.

Umahiri wake uliendelea kung’aa aliposimamia dili kubwa la Fiston Mayele kutoka Yanga SC kwenda Pyramids FC ya Misri. Licha ya Yanga kumhitaji, Waarabu walikuja na dau nono na kumchukua. Kwa sasa Mayele analipwa mara saba zaidi ya alivyokuwa Yanga, na motisha hiyo imemsaidia kung’ara hadi kufanikisha ubingwa wa CAF Champions League.

Kwa rekodi hii safi ya mafanikio – kutoka kwa Msuva, Feisal, hadi Mayele – ni swali linalozuka: kwa nini kwa Clement Mzize mambo yamekwama?

Mzize ni mchezaji anayehitajika na vilabu vikubwa kutoka Uarabuni na Ulaya. Thamani yake imepanda sana ukilinganisha na mwaka jana. Hata hivyo, Yanga SC wanagoma kumuuza licha ya ofa zenye uwezo wa kulipa dau wanalodai.

Ikiwa Yanga wanamwitaji, basi wanapaswa kumpa mshahara unaoendana na thamani yake. Mshahara wa milioni 15 kwa mwezi si kiwango cha staa wa hadhi ya Mzize. Kwa kipimo cha soko, analingana kulipwa angalau dola 30,000 (takribani milioni 78) kwa mwezi. Ni jambo la kushangaza kuona Prince Dube akimzidi mshahara ilhali mchango na work rate ya Mzize uwanjani ni mkubwa zaidi.

UWANJA WA KASARANI KUWEKWA JUU KABLA YA MECHI YA KENYA NA MOROCCOImethibitishwa kuwa kesho, uwanja wa Moi International ...
08/08/2025

UWANJA WA KASARANI KUWEKWA JUU KABLA YA MECHI YA KENYA NA MOROCCO

Imethibitishwa kuwa kesho, uwanja wa Moi International Sports Centre, Kasarani utafunikwa juu wakati Kenya itakaposhuka dimbani kuumana na Morocco.

Uwanja wa Kasarani ulijengwa wakati wa utawala wa aliyekuwa Rais wa Kenya, hayati Daniel Toroitich Arap Moi, kwa usaidizi wa wahandisi kutoka China. Hata hivyo, baada ya miaka ya matumizi, hali ya uwanja huo ilidorora na kuwa mbaya.

Kupitia maandalizi ya michuano ya CHAN 2024, ambapo Kenya ni mwenyeji kwa kushirikiana na Tanzania na Uganda, serikali ya Kenya imefanya maboresho makubwa katika miundombinu ya uwanja huo.

Maboresho hayo yamefanywa chini ya uongozi wa Rais wa sasa, Dkt. William Samoei Arap Ruto, k**a sehemu ya maandalizi ya fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika (AFCON) 2027, ambazo Kenya pia itakuwa mwenyeji kwa kushirikiana na mataifa jirani.

YANGA INAENDESWA KIHUNI.“Kuna wakati huu uongozi wa Yanga SC unaonekana kuendeshwa kiholela kabisa. Vuta picha hii – Max...
08/08/2025

YANGA INAENDESWA KIHUNI.

“Kuna wakati huu uongozi wa Yanga SC unaonekana kuendeshwa kiholela kabisa. Vuta picha hii – Maxi Kahamba amegoma kuongeza mkataba hadi pale ambapo Nkane naye atakuwa ameongezewa mkataba. Hapo ndipo na yeye yuko tayari kusaini.

Nasikia hata Clatous Chama kabla ya kusaini mkataba mpya, alitaka kupata uhakika kwamba Mkude naye ataongezewa mkataba k**a masharti yanayofanana na yake.

Hawa Yanga wanacheza na klabu kubwa kana kwamba ni kikundi cha utani. Kwa mwenendo huu, sioni kabisa Yanga ikivuka hatua ya makundi kwenye mashindano ya kimataifa msimu huu.”

Jemedari Said - Mchambuzi wa Soka Tanzania.

SABRI KONDO AJIUNGA NA BK HACKEN YA USWIDI KWA BILIONI 6.Mchezaji chipukizi wa Kitanzania, Sabri Kondo, amejiunga rasmi ...
08/08/2025

SABRI KONDO AJIUNGA NA BK HACKEN YA USWIDI KWA BILIONI 6.

Mchezaji chipukizi wa Kitanzania, Sabri Kondo, amejiunga rasmi na klabu ya BK Häcken ya Ligi Kuu nchini Uswidi (Allsvenskan) kwa mkataba wa muda mrefu. Usajili huu ni hatua kubwa kwa kijana huyo ambaye ameonyesha kiwango bora akiwa na timu za vijana na pia katika mashindano ya kimataifa.

Sabri Kondo, ambaye ni mshambuliaji mwenye kasi, mbunifu na uwezo mkubwa wa kumalizia, amekuwa gumzo kwenye soka la vijana nchini Tanzania kutokana na kipaji chake na maono ya kiuchezaji. BK Häcken wamevutiwa na uwezo wake wa kipekee na wameamua kumpa nafasi ya kuendelea kukuza kipaji chake Ulaya.

Klabu hiyo imetangaza usajili huo kupitia kurasa zao rasmi za mitandao ya kijamii, wakimkaribisha Sabri k**a sehemu ya mpango wao wa kuendeleza vipaji vijana kutoka Afrika.

Sabri amesema:
"Nashukuru Mungu kwa hatua hii muhimu. Ni ndoto yangu kucheza Ulaya na sasa imekuwa kweli. Nitajituma kwa bidii kuonyesha uwezo wangu na kupeperusha bendera ya Tanzania."

Usajili wa Sabri Kondo unaongeza idadi ya Watanzania wanaocheza soka la kulipwa barani Ulaya, jambo linaloashiria maendeleo ya vipaji na nafasi kwa vijana kutoka Tanzania kwenye ramani ya dunia. Kabla ya kwenda Sweden alikuwa mchezaji wa Singida Black Stars.

MAKOMBE HAYA... NDUGU ZETU WANA SIMBA MNAONAE TU KWENYE PICHA! 🏆📸Miaka minne si mchezo!Mtoto aliyezaliwa kipindi hicho, ...
06/08/2025

MAKOMBE HAYA... NDUGU ZETU WANA SIMBA MNAONAE TU KWENYE PICHA! 🏆📸

Miaka minne si mchezo!

Mtoto aliyezaliwa kipindi hicho, kwa sasa anaongea kwa ufasaha. Wengine tayari wako Pre-unit (vidudu), na wengine wanawatambua vizuri baba na mama zao.

Hali hii inaonesha ni muda mrefu sana tangu Wana Simba walipoonja ladha ya kombe kuu. Lakini, mvumilivu hula mbivu — labda usajili wa Fadlu msimu huu ukawaletea faraja.

Kwa upande wa Yanga SC, ushindi wa makombe back to back kwa miaka minne si lelemama. Baadhi ya wachezaji huenda wamechoka. Ili kuendelea kuwa na ubabe, itawahitaji nguvu mpya kabisa.

Lakini kwa mtazamo wangu — msimu huu utakuwa mgumu zaidi kwa Yanga kuliko kwa Simba. Kumbuka: Yanga hawana washirika tena msimu huu!

Hata hivyo, wanayo silaha kubwa — Tajiri wao GSM ambaye hafichi pochi! Anatoa pesa bila kusita.

Ndugu zetu Wana Simba, endeleeni kujifua na kusugua goti mimbarini... 😅
Lakini Yanga nanyi msijiamini sana — wekaeni ulinzi makombe yenu, msije mkayaona yakiibwa kimyakimya!

Ukurasa wa  umeripoti kwamba Spika wa zamani wa Bunge la Tanzania Job Ndugai amefariki Dunia.Amefariki leo tarehe 6 Agos...
06/08/2025

Ukurasa wa umeripoti kwamba Spika wa zamani wa Bunge la Tanzania Job Ndugai amefariki Dunia.

Amefariki leo tarehe 6 Agosti 2025 akiwa anapatiwa matibabu baada ya kuuga ghafla.

Cc Poster - Millard Ayo

Address

Nyamagana
Mwanza
994

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Famara Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Famara Media:

Share