24/12/2025
Katika maisha ya mahusiano, wanaume wengi huingia kwenye maumivu ya hiari kwa kupenda wasipopendwa.
Mwanaume anaweza kumpenda msichana kwa dhati, akaamua kumtafuta kila siku, kumjali, kumthamini — lakini majibu anayopata ni dharau, ukatili wa maneno, au kupuuzwa.
Cha kushangaza, licha ya ishara zote hizo, bado jamaa anaendelea kuvumilia, akiamini kwamba siku moja huyo dada atamwona na kumpa nafasi.
Huu ni mtego wa kihisia unaowaumiza wengi kimya kimya. Na kifupi ni Ujinga.
Wanasaikolojia wanasema:
"Mapenzi ni ya pande mbili. Mtu anayekupenda hawezi kukudharaulisha. Ukiona hulipwi heshima, acha moyo upumzike. Mpende anayekupenda, na usitese nafsi yako kwa matumaini yasiyo na uhalisia."
Utafiti wa shirika la Mayo Clinic (2023) umebaini kuwa wanaume wanaoishi kwenye mahusiano yenye msongo wa kihisia au mapenzi ya upande mmoja huwa na hatari kubwa zaidi ya kupata msongo wa mawazo, shinikizo la damu, na hata vifo vya mapema.
Hii ni kwa sababu mwili hujenga mfadhaiko wa ndani usioonekana, unaoathiri afya ya moyo na akili.
Psychology Today pia imeripoti kuwa wanaume huwa na uwezekano mdogo wa kuzungumza au kutafuta msaada, hivyo huzidi kuumia kimya kimya huku wakiteseka kwa sababu ya kutokupendwa.
Usiumie kwa hiari. Mapenzi sio mateso. Si kwa ubaya chagua kamseleleko maisha ya Mahusiano sio magumu ukikutana na dada ambaye anakujali
RFAONLINE
🖋️