Radio Free Africa

Radio Free Africa Ukurasa Rasmi wa Radio Free Africa
Tunasikika Nchi Nzima & Kimataifa. Kazi yake k**a ulivyo wajibu wa vyombo vya Habari, Kuhabarisha, kuelimisha, Kuburudisha.
(444)

Radio yenye Makao Makuu Jijini Mwanza Tanzania na kusikika katika Mikoa Mbalimbali kupitia Masafa ya FM, Masafa ya Kati 1377 ,Mtandao na Kupitia Ving'amuzi/Visimbuzi mbalimbali.

04/08/2026

Rais Samia Suluhu Hassan amesema amani na utulivu ni mtaji mkubwa kuliko fedha katika kufanikisha Dira ya Maendeleo ya Tanzania 2050, akisisitiza kuwa bila mazingira ya amani malengo hayawezi kutekelezwa.

Akizungumza wakati wa hafla ya uzinduzi wa Nyenzo za Utekelezaji wa Dira 2050 iliyofanyika Ikulu jijini Dar es Salaam, Rais Samia amesema hata k**a nchi itakuwa na rasilimali nyingi za kifedha, bila amani na utulivu haitawezekana kufanikisha dira hiyo.

“Unaweza kuwa na trilioni za fedha lakini bila amani na utulivu hii dira haitotekelezeka na hatutaweza kufanya chochote,” amesema Rais Samia.

Amewataka Watanzania wote pamoja na sekta za umma na binafsi kuendelea kuilinda amani ya nchi, akieleza kuwa mazingira tulivu humwezesha mfanyabiashara kufanya kazi bila hofu, jambo linalochochea uwekezaji, biashara na ukuaji wa uchumi.

“Katika safari yetu ya Dira 2050 ni wajibu wetu kulinda amani na utulivu. Tukilinda amani na utulivu tutakuwa tumelinda uwekezaji, ajira, biashara na kasi ya ukuaji wa uchumi,” amesema.

,

04/08/2026

Halmashauri ya wilaya ya makete imeanzisha utaratibu wa kuwafikishia mbolea wakulima hadi maeneo wanayofanya kilimo ili kuwaepusha na adha ya upatikanaji wa mbolea iliyokuwa ikiwachelewesha kuanza kilimo kwa wakati kutokana na kukosa mbolea hasa za kupandia.

Ikiwa ni sehemu ya uwajibikaji katika kuwahudumia wakazi wa wilaya ya makete, Afisa kilimo kwa niaba ya Mkurugenzi wa halmashauri hiyo amesema wameanzisha utaratatibu wa kupeleka mbolea vijijini baada ya kubaini wakulima wengi wanachelewa kuanza kilimo kwa wakati kutokana na kukosa mbolea zinazohitajika hasa wakati wa kupanda.

Jukumu la kufikisha mbolea katika vijiji ambavyo wakulima wanapatikana limekabidhiwa kwa kampuni binafsi ambao wanasema wamejiandaa kikamilifu ili kuhakikisha wakulima wanapata mbolea kwa wakati hata katika kipindi ambacho barabara zinakuwa hazipitiki.

Baadhi ya wakulima wanasema hatua iliyochukuliwa na halmashauri imewapa ahueni kwa kiasi kikubwa tofauti na hali ilivyokuwa awali ambapo walilazimika kutumia gharama kubwa kufuata mbolea, na hata wakati mwingine walichelewa msimu wa kilimo kwa kukosa mbolea.

Ni wakati huu ambao mamlaka ya udhibiti wa mbolea Tanzania (TFRA) kanda ya nyanda za juu kusini wanasema mikoa ya kusini ndio tegemezi katika uzalishaji wa mazao ya chakula hivyo ni vema kutumia kila jitihada kuhakikisha wakulima wanapata mbolea kwa wakati ili waweze kufanya kilimo chenye tija.

Halmashauri zingine zimeaswa kuiga mfano wa halmashauri hizi zilizoanzisha utaratibu wa kufikisha mbolea kwa wakulima ili kupunguza changamoto na kuwapa ahueni wakulima waweze kuzalisha kwa tija.




Kupitia mtambo mkubwa    Leo Exclusive interview kuanzia Saa 2pm -4pmHosted by    Music by Artwork  04.8.2026 📻
04/08/2026

Kupitia mtambo mkubwa

Leo

Exclusive interview kuanzia Saa 2pm -4pm

Hosted by

Music by

Artwork
04.8.2026 📻

04/08/2026


04/08/2026

Rais wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameitaka sekta binafsi kuongeza uwekezaji katika uzalishaji na uchakataji wa bidhaa za ndani, ikiwemo mchele, ili kukidhi mahitaji yanayoongezeka katika soko la Afrika.

Amesema Serikali inaendelea kuboresha mazingira ya biashara kwa kuimarisha miundombinu na kuunganisha Tanzania na mataifa jirani, hatua itakayorahisisha usafirishaji wa bidhaa na kupanua masoko ya wazalishaji wa ndani.

Dkt. Samia ameyasema hayo leo, Agosti 3, 2026, Ikulu jijini Dar es Salaam, wakati wa uzinduzi wa nyenzo za utekelezaji wa Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mkuu huyo wa nchi, ametoa mfano wa fursa zilizopo, amesema katika ziara zake nchini Ghana na Angola alibaini kuwa mchele wa Mbeya unafahamika na kuthaminiwa kutokana na ubora wake.

“Nilikwenda Ghana na Angola ndani ya Afrika. Nilishangazwa zaidi na Ghana walipokuwa wanazungumzia mchele wa Mbeya. Nikawauliza kwa nini mchele wa Mbeya, wakaniambia ukiupika nyumba nzima unanukia,” amesema.

Ameongeza kuwa viongozi na wafanyabiashara wa Ghana walieleza kuwa wanahitaji mchele huo kutoka Tanzania, lakini changamoto kubwa ni namna ya kuufikisha kwenye masoko hayo.
“Wakaniambia wanahitaji mchele wa Mbeya kutoka Tanzania. Tatizo letu ni connectivity ya kufikisha huko. Hiyo ndiyo kazi yenu sekta binafsi, mkae, mchemshe kichwa, tuone tunapelekaje bidhaa kwenye nchi jirani,” amesema.

Rais Samia amesema Serikali inaendelea kuwekeza katika uboreshaji wa miundombinu ya usafiri, ikiwemo Reli ya Kati na Reli ya TAZARA, ambayo itasaidia kuunganisha Tanzania na Angola kupitia Kapiri Mposhi hadi Bandari ya Lobito.

Amesisitiza kuwa ushirikiano kati ya Serikali na sekta binafsi ni muhimu katika kuondoa vikwazo vya usafirishaji wa bidhaa, huku akitoa wito wa kuongeza uzalishaji na uwekezaji katika viwanda vya kuongeza thamani ya mazao ili Tanzania inufaike zaidi na fursa za soko la Afrika.

“Tunajitahidi kufanya connection, lakini sekta binafsi mkiweka misuli tutakwenda haraka zaidi. Tatizo ni connectivity, lakini bidhaa za kuuza tunazo. Tujitahidi kuzalisha kwa wingi na kujenga viwanda vitakavyoongeza thamani ya bidhaa,” amesema.

Kupitia mtambo mkubwa    Leo Exclusive interview kuanzia Saa 2pm -4pmHosted by    Music by Artwork  03.8.2026 📻
03/08/2026

Kupitia mtambo mkubwa

Leo

Exclusive interview kuanzia Saa 2pm -4pm

Hosted by

Music by

Artwork
03.8.2026 📻

Asante Kwa kushiriki mjadala wa Je unasemaje Usiku huu ulioangazia Namna Bora ya kuhamia Kwenye Nishati safi ya kupikia ...
02/08/2026

Asante Kwa kushiriki mjadala wa Je unasemaje Usiku huu ulioangazia Namna Bora ya kuhamia Kwenye Nishati safi ya kupikia na Nafasi ya Gas ya Kwenye mitungi LPG

Maoni Zaidi 👇

Viongozi wa siasa na serikali  mkoa wa Njombe wamesema wanaendelea kuwekeza muda mwingi katika kuhubiri na kuelimisha wa...
02/08/2026

Viongozi wa siasa na serikali mkoa wa Njombe wamesema wanaendelea kuwekeza muda mwingi katika kuhubiri na kuelimisha watu kuhusu Uchumi na siasa za kistaarabu zinatakazi saidia kuleta maendeleo ya mkoa wa watu wake.

Wakiwa katika hafla ya Utoaji wa tuzo maalumu za kutambua jitihada na upambanaji wa vijana kichumi katika kada mbambali wamesema kipaumbele cha mkoa kwa sasa ni uchumi wa watu, sambamba na siasa za kistaarabu zitakazo saidia kuwajenga watu na kuinua uchumi wao.

Anthony Mtaka mkuu wa mkoa wa njombe amesema atashirikiana na viongozi wote bila kujali itikadi zao, katika kujenga uchumi wa mkoa wa njombe na watu wake.

Kwa upande wake Salum Mwalimu aliyewahi kuwa mgombea wa Urais wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania mwaka 2025, amewataka vijana kujikita katika kufanya kazi na kuendeleza vipaji vyao ili waweze kutengeneza Maisha kwaajili ya familia.

Sigrada mligo Mbunge viti maalumu ambae ndie mdhamini mkuu wa tuzo za Njombe Smart Talents amesema atahakikisha anadhirikiana na serikali katika kuishauri, ili kutatua changamoto zinazowakabili wakazi wa njombe hususani vijana.

Tuzo zilizotolewa zililenga kutambua uwajibikaji wa vijana katika kujitafutia maisha katika kada mbalimbali ikiwemo, madereva, mama ntilie, wanahabari, madalali, wapiga picha na wakulima.

Baadhi ya waliofanikiwa kutwaa tuzo hizo wakiwemo wanahabari (Elizabeth Kilindi) wamesema tuzo hizo zinawaongezea morali wa kufanya kazi kwa bidii katika kuwasaidia wananchi.

Na,Dickson Kanyika

02/08/2026

Wakati Tanzania ikiadhimisha maonesho ya Nane nane kitaifa jijijini Dodoma, mamalka ya udhibiti mbolea kanda ya nyanda za juu kusini, imeonesha kwa vitendo jinsi matumizi sahihi ya mbolea yalivyoleta tija kwenye mazao.

Afisa mdhibiti ubora wa mbolea kanda ya mbeya Mshoborozi Kristian ameonesha kwa vitendo jinsi ambavyo wamezingatia matumizi sahibi ya mbolea yaliyoenda sambamba na upimaji wa udongo.



01/08/2026

Vijana 60 waliohitimu katika Chuo cha Ufundi Stadi Veta wilayani Songea, Ruvuma wametakiwa kutobweteka na badala yake kuendelea kuboresha ujuzi ili kuendana na kasi ya mabadiliko ya teknolojia duniani.

Mafunzo hayo ya wiki mbiili yametolewa chini ya mradi wa Dumisha Amani kwa ufadhili wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa (UNDP).

Mkurugenzi wa Veta Kanda ya Nyanda za Juu Kusini, Suzan Magan amelishukutu UNDP kufadhili mradi huo na kuonyesha namna taasisi za maendeleo zinavyoweza kushirikiana na Serikali kuwawezesha vijana kupata stadi za kazi na kujenga misingi ya amani na mashik**ano wa Kitaifa.

Kwa upande wake Mkuu wa Chuo cha Veta Songea, Rahabu Mwakatundu amesema
lengo la mradi huo ni kuwapatia vijana ujuzi wa kiufundi pamoja na kuwajengea uwezo katika maadili, uzalendo, utamaduni, amani, mshik**amo wa kitaifa na stadi za maisha.

Naye Afisa miradi wa Shirika la Mpango wa Maendeleo la Umoja wa Mataifa, Josephine Sepeku amewataka wahitimu kuhakikisha wanakwenda kutumia ujuzi waliopa kujiajiri ili waweze kujikwamua kimaisha.

Akisoma risala ya wahitimu hao, Godlove Komba wameshukuru washirika hao wa maendeleo kufadhili mradi huo kwa kuwa umewajengea uwezo, kupata elimu ya amani, stadi za maisha,ujuzi wa ufundi na ujasiriamali utakaowawezesha kujitegemea na kuchangia maendeleo ya jamii yetu na Taifa.

Address

7-C, Ilemela Industrial Area, Airport Road
Mwanza
POBOX1732

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Free Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Free Africa:

Shortcuts

Share