Radio Free Africa

Radio Free Africa Ukurasa Rasmi wa Radio Free Africa
Tunasikika Nchi Nzima & Kimataifa. Kazi yake k**a ulivyo wajibu wa vyombo vya Habari, Kuhabarisha, kuelimisha, Kuburudisha.
(447)

Radio yenye Makao Makuu Jijini Mwanza Tanzania na kusikika katika Mikoa Mbalimbali kupitia Masafa ya FM, Masafa ya Kati 1377 ,Mtandao na Kupitia Ving'amuzi/Visimbuzi mbalimbali.

13/11/2025

Mbunge wa Jimbo la Isimani, William Lukuvi, amesema Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ni mchumi mbobevu aliyesimamia makusanyo ya kodi na kuisaidia Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kutekeleza vyema miradi ya maendeleo.
Amesema kwa kazi nzuri iliyofanywa na utawala wa Rais Samia akisaidiwa na Dkt. Nchemba, imewezesha pia wabunge wengi wa CCM kuaminiwa na kurejea tena bungeni.

13/11/2025

Waziri Mkuu mteule, Dkt Mwigulu Nchemba amewaahidi Watanzania kuwa kila mwananchi akiwemo wa hali ya nchi atasikilizwa katika ofisi za umma na kwa nidhamu.

Dkt Mwigulu ametoa ahadi hiyo,leo Alhamisi Novemba 13, 2025 bungeni jijini Dodoma, muda mchache baada ya kuthibitishwa na Bunge, akisisitiza kila Mtanzania nchi ni yake.

“Watanzania wote watasikilizwa kwa nidhamu ofisi, watasikilizwa kwa nidhamu katika ofisi za umma, “ amesisitiza Dk Mwigulu huku akipigwa na makofi na wabunge.

13/11/2025

Waziri Mkuu mteule, Dkt Mwigulu Nchemba amesema atahakikisha ndoto ya Rais wa Tanzania, Dkt Samia Suluhu Hassan ya kutengeneza ajira milioni 8 inatimia kwa kuweka utaratibu bora.

Dk Mwigulu ambaye ni Kiongozi na Msimamizi wa shughuli za Serikali bungeni ameeleza hayo leo Novemba 13, 2025 bungeni jijini Dodoma, muda mchache baada ya kuthibitishwa na Bunge, akisema watafanya uratibu na usimamizi ili kutimiza ndoto ya Dk Samia ya vijana kupata ajira.

“Tutaweka utaratibu na mpango mkakati ndani ya Serikali na kushirikisha sekta binafsi ili kuhakikisha dira ya mheshimiwa Rais (Samia) ya kutengeza ajira zisizopungua milioni 8 inakwenda kutumia,”

13/11/2025

Mbunge wa Tunduru Kaskazini na Katibu Mkuu wa ACT Wazalendo Ado Shaibu amesema wabunge walio wachache Bungeni wanamkopesha imani Waziri Mkuu Mwigulu Nchemba kwa matarajio kuwa atajikita katika kusimamia rasilimali za Taifa kwa ajili ya kuwaletea wananchi maendeleo, kuipatia nchi katiba mpya na kushughulikia changamoto za kiuchumi na kijamii za wananchi.

Ado ameyasema hayo alipotakiwa na Spika Hassan Zungu kutoa neno kwenye uteuzi wa Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Tanzania uliofanywa na Rais Samia Suluhu Hassan na kuidhinishwa na Bunge leo tarehe 13 Novemba 2025.

13/11/2025

Waziri Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba amewatumia salamu watumishi wazembe na wavivu katika kazi zao na kusema kuwa wajiandae kufyekwa.

"Kwa watumishi wote wote wazembe, wavivu
Nitakuja na fyekeo na rato. Maono ya Rais lazima yatekelezwe," amesisitiza Dkt Nchemba muda mfupi mara baada ya Bunge kumthitisha kuwa Waziri Mkuu leo Alhamisi Novemba 13, 2025.

Waziri Mkuu Nchemba amesema yale yote yaliyoahidiwa na Rais, Makamu wa Rais na wabunge yatatimia tu k**a Taifa litakuwa na amani.

"Bila amani yote hayawezi kufikiwa. Tumtangulize Mungu hata kwa yale tunayoona ni magumu kwa sababu kwake yote ni mepesi."

Katika hatua nyingine Waziri Mkuu, Dkt Nchemba ameahidi katika uongozi wake kuwasikiliza watu wa makundi yote bila ubaguzi.

Dkt Nchemba amesema anatambua umaskini mkubwa walionao Watanzania hivyo atahakikisha kila Mtanzania anasikilizwa kero yake.

"Maisha yangu yamezungukwa na watu wenye mahitaji, nina bweni la wanafunzi zaidi ya 100 wenye mahitaji ninajua ninapozungumzia umaskini."

"Lazima tuende kwa gia ya kupita katika barabara yenye milima, kupitia katika bahari yenye mawingu na anga lenye mawingu,amesisitiza Waziri Mkuu Nchemba.

Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kesho Ijumaa, Novemba...
13/11/2025

Rais Samia Suluhu Hassan anatarajiwa kuzindua rasmi Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kesho Ijumaa, Novemba 14,2025.

Aidha, katika uzinduzi huo Rais Samia atalihutubia Bunge Kwa mara ya kwanza tangu kuanza kwake.

Alitangaza shughuli hiyo, Spika M***a Azzan maarufu 'Zungu' amesema Bunge litaanza rasmi saa 9: 00 na kila mmoja awe tayariI kwa ugeni huo

Awali akiitengua Kanuni za Bunge ili kuruhusu wagenj ambao si wabunge kuingia ndani ya Bunge wakati wa shughuli hiyo, Mwanasheria Mkuu wa Serikali, Hamza Johari alitoa hoja kwa wabunge ili waridhie wageni mbalimbali waruhusiwe kuingia ndani ya ukumbi huo.

Johari aliwataja wageni hao kuwa ni pamoja Makamu wa Rais, Dkt Emmanuel Nchimbi na Rais wa Zanzibar na Mwenyeki wa Baraza la Wawakilishi, Dkt Hussein Ali Mwinyi.

Wengine ni Jaji Mkuu, Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar na Spika wa Bunge la Afika Mashariki.

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limemthibitisha kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Lameck Nchemba kuwa...
13/11/2025

Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, limemthibitisha kada wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu.

Nchemba amethibitishwa Kwa kura 369 za ndiyo kati ya 371 zilizopigwa ambako kura mbili zimeharibika.

Awali Rais Samia Suluhu Hassan alimteua Mwigulu Lameck Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Jina la Nchemba limetangazwa bungeni leo asubuhi Alhamisi Novemba 13,2025 na Spika wa Bunge, M***a Azzan Zungu baada ya kupokea ujumbe maalumu kutoka kwa mpambe wa kijeshi wa Rais Samia.

Kabla ya uteuzi huo, Nchema alikuwa Waziri wa Fedha Pia ameshawahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara.

Nchemba anapokea kijiti kutoka kwa Majaliwa Kassim Majaliwa aliyehudumu nafasi hiyo kwa miaka 10 Mfululizo.

13/11/2025

Kesi ya wizi wa mtoto inayowakabili wash*takiwa watatu imeahirishwa katika Mahak**a ya Wilaya ya Ubungo, Dar es Salaam, baada ya msh*takiwa wa tatu kushindwa kufika mahak**ani bila taarifa yoyote. Kutokana na hali hiyo, Mahak**a imetoa hati ya kumk**ata msh*takiwa huyo.

Wash*takiwa ni Brighton Augustine, mfanyabiashara wa madini kutoka Mwanza, Alfa Kivuyo, dereva wa pikipiki mkazi wa Arusha, na Moses Fusi kutoka Dar es Salaam. Wanatuhumiwa kumteka mtoto wa miaka mitatu aliyechukuliwa akiwa nje ya nyumba yao akisubiri gari la shule, mnamo Agosti 26, 2025.

Mtoto huyo baadaye alipatikana maeneo ya Mbwewe, Bagamoyo akiwa amefunikwa kwenye mfuko wa sandarusi juu ya pikipiki.

Kesi hiyo imeahirishwa hadi Novemba 26, 2025 huku msh*takiwa wa kwanza akiomba muda wa wiki mbili kwa ajili ya matibabu baada ya kudai kushambuliwa na wananchi wenye hasira siku ya tukio.

**aUbungo

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Mwigulu Lameck Mchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.Jina la Nch...
13/11/2025

Rais Samia Suluhu Hassan amemteua Mwigulu Lameck Mchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Jina la Nchemba limetangazwa bungeni leo Alhamisi Novemba 13,2025 na Spika wa Bunge, M***a Azzan Zungu baada ya kupokea ujumbe maalumu kutoka kwa mpambe wa kijeshi wa Rais Samia.

Kabla ya uteuzi huo, Nchema alikuwa Waziri wa Fedha
Pia ameshawahi kuwa Naibu Katibu Mkuu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Bara.

Nchemba anapokea kijiti kutoka kwa Majaliwa Kassim Majaliwa aliyehudumu nafasi hiyo kwa miaka 10 Mfululizo.

Harakati ni jitihada za pamoja au za mtu binafsi za kupigania mabadiliko fulani ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, au kiutam...
13/11/2025

Harakati ni jitihada za pamoja au za mtu binafsi za kupigania mabadiliko fulani ya kijamii, kisiasa, kiuchumi, au kiutamaduni. Huwa na malengo maalum — k**a vile haki za binadamu, mazingira, elimu bora, au usawa.

Mwana harakati ni mtu anayeshiriki kikamilifu katika harakati hizo — kwa kupaza sauti, kushiriki mijadala, maandamano, kampeni au kutoa elimu ili kusukuma mbele ajenda fulani ya mabadiliko au uboreshaji katika jamii.

Unadhani kwanini UANAHARAKATI siku za Hivi karibuni umeonekana kitu kibaya? Mathalani mtu anaambiwa Acha UANAHARAKATI?!

13/11/2025

Makamu Mwenyekiti wa Chama cha Demokrasia (CHADEMA) ametoa pongezi za chama hicho kwa Umoja wa Mataifa (UN) iliyoielekeza serikali ya Tanzania kufanya uchunguzi wa wazi juu ya matukio ya mauaji ya watu yaliyotokea siku ya uchaguzi Mkuu uliofanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Amesema CHADEMA inasisitiza uchunguzi ufanywe na Mashirika ya kimataifa ili kutenda haki kwa pande zote zinazohusika na kwamba chama hicho pamoja na mambo mengine kinaitaka serikali kuwaachilia huru watuhumiwa wote wa uhaini wanaoshikiliwa na jeshi la polisi tangu Oktoba 29 katika mikoa mbalimbali nchini..

Kutoka Geita hadi Rock City – SportPesa imeendelea kuwasha moto wa soka mitaani!  Vijana wamechuana vikali, wakionesha v...
12/11/2025

Kutoka Geita hadi Rock City – SportPesa imeendelea kuwasha moto wa soka mitaani!
Vijana wamechuana vikali, wakionesha vipaji na ushindani wa hali ya juu kwenye safari ya "Pasi kwa Pasi hadi Ubingwa"

Kwa kila pasi na kila goli, ndoto zao zinazidi kushika kasi.

SportPesa si tu mdhamini, ni daraja la matumaini kwa wanasoka chipukizi!






Address

7-C, Ilemela Industrial Area, Airport Road
Mwanza
POBOX1732

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Free Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Free Africa:

Share