Radio Free Africa

Radio Free Africa Ukurasa Rasmi wa Radio Free Africa
Tunasikika Nchi Nzima & Kimataifa. Kazi yake k**a ulivyo wajibu wa vyombo vya Habari, Kuhabarisha, kuelimisha, Kuburudisha.
(448)

Radio yenye Makao Makuu Jijini Mwanza Tanzania na kusikika katika Mikoa Mbalimbali kupitia Masafa ya FM, Masafa ya Kati 1377 ,Mtandao na Kupitia Ving'amuzi/Visimbuzi mbalimbali.

‎Sudan inakuwa timu ya tatu kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na kati Kisoka (CECAFA) zijanazoshiriki michuano ya Kombe ...
24/12/2025

‎Sudan inakuwa timu ya tatu kutoka ukanda wa Afrika Mashariki na kati Kisoka (CECAFA) zijanazoshiriki michuano ya Kombe la Mataifa Afrika (AFCON) huko Morocco kupoteza mechi za ufunguzi

‎Sudan ambayo iko kundi E imejikuta ikipoteza kwa idadi kubwa ya mabao, huku yenyewe ikokosa hata bao mojala kufutia machozi.

‎Ikumbukwe Tanzania jana ilipoteza kwa mabao 2-1 dhidi Nigeria wakati huo Uganda ikichapika 3-1 kwa Tunisia.

‎Full Time

‎Algeria 3-0Sudan

‎MSIMAMO KUNDI E

‎1.Algeria pointi 3
‎2. Burkina Faso pointi 3
‎3. Equatorial Guinea pointi 0
‎4. Sudan pointi 0

🖋️ Maregesi Nyamaka



‎Wakati ambao Equatorial Guinea kiducu iishangaza Dunia kwa kufunga bao muhimu dakika za mwisho mwisho  ikiwa pungufu uw...
24/12/2025

‎Wakati ambao Equatorial Guinea kiducu iishangaza Dunia kwa kufunga bao muhimu dakika za mwisho mwisho ikiwa pungufu uwajani baada ya mchezaji wao kulimwa kadi nyekundu katikati ya mchezo, lakini Burkina Faso kwenye dakika za nyongeza wanasawazisha na kuweka chuma ya pili na ya ushindi. What A Mission.

‎Ni Kupitia mchezo wa kwanza wa kundi E muendelezo wa michuano ya Kombe la Mataifa Africa (Afcon), Morocco

‎Ni Burkina Faso ambayo muda mwingiwa mchezo kila dalili ya kushinda mchezo ilikuwa upande wao, lakinikikwazo kikubwa ikajikuta inakumbuna na wakati mgumu sana kuwafungua wapinzani kwenye 18.

‎Dakika za majeruhi zikawa na faida mno baada ya kuongeza kasi ya mashambulizi, attack more, unlock ikakubali.

‎Full Time

‎Equatorial Guinea 1-2 Burkina Faso

🖋️

Katika maisha ya mahusiano, wanaume wengi huingia kwenye maumivu ya hiari kwa kupenda wasipopendwa. Mwanaume anaweza kum...
24/12/2025

Katika maisha ya mahusiano, wanaume wengi huingia kwenye maumivu ya hiari kwa kupenda wasipopendwa.

Mwanaume anaweza kumpenda msichana kwa dhati, akaamua kumtafuta kila siku, kumjali, kumthamini — lakini majibu anayopata ni dharau, ukatili wa maneno, au kupuuzwa.

Cha kushangaza, licha ya ishara zote hizo, bado jamaa anaendelea kuvumilia, akiamini kwamba siku moja huyo dada atamwona na kumpa nafasi.

Huu ni mtego wa kihisia unaowaumiza wengi kimya kimya. Na kifupi ni Ujinga.

Wanasaikolojia wanasema:
"Mapenzi ni ya pande mbili. Mtu anayekupenda hawezi kukudharaulisha. Ukiona hulipwi heshima, acha moyo upumzike. Mpende anayekupenda, na usitese nafsi yako kwa matumaini yasiyo na uhalisia."

Utafiti wa shirika la Mayo Clinic (2023) umebaini kuwa wanaume wanaoishi kwenye mahusiano yenye msongo wa kihisia au mapenzi ya upande mmoja huwa na hatari kubwa zaidi ya kupata msongo wa mawazo, shinikizo la damu, na hata vifo vya mapema.

Hii ni kwa sababu mwili hujenga mfadhaiko wa ndani usioonekana, unaoathiri afya ya moyo na akili.

Psychology Today pia imeripoti kuwa wanaume huwa na uwezekano mdogo wa kuzungumza au kutafuta msaada, hivyo huzidi kuumia kimya kimya huku wakiteseka kwa sababu ya kutokupendwa.

Usiumie kwa hiari. Mapenzi sio mateso. Si kwa ubaya chagua kamseleleko maisha ya Mahusiano sio magumu ukikutana na dada ambaye anakujali



RFAONLINE
🖋️

Waziri Mkuu,  Dkt Mwigulu Nchemba ameagiza kufutwa kazi na kufikishwa katika vyombo vya sheria kwa aliyekuwa Mtendaji Mk...
24/12/2025

Waziri Mkuu, Dkt Mwigulu Nchemba ameagiza kufutwa kazi na kufikishwa katika vyombo vya sheria kwa aliyekuwa Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Ufundi na Umeme Tanzania (TEMESA) pamoja na menejimenti yake yote kutokana na ubadhirifu wa zaidi ya TSH 2.5 bilioni.

Amemuagiza Waziri wa Ujenzi, Abdallah Ulega kufanya uchunguzi wa vivuko vyote ili kubaini vyanzo vya uharibifu kwa sababu kuna taarifa kwamba vinaharibiwa kwa makusudi ili wahusika wajipatie fedha kupitia matengenezo.

Amesema uamuzi huo unatokana na matokeo ya Tume maalumu iliyoundwa kuchunguza tuhuma za matumizi mabaya ya fedha za umma katika wakala huo
“Vyombo husika vichukue hatua kwa wahusika, haya mambo ya kutoheshimu fedha za umma, kutokuwa na huruma na Watanzania lazima yafike mwisho.”

Ametoa agizo hilo leo Jumatano, Desemba 24, 2025 akizungumza na viongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam na wakazi wa Kigamboni akiwa katika ziara ya kukagua hali ya utoaji wa huduma katika Kivuko cha Magogoni, Kigamboni, jijini Dar es Salaam.

Amesema ubadhirifu uliofanyika ni sawa na watendaji hao kugawana vivuko pamoja na kuiba nauli zinazotolewa na wananchi mambo ambayo yanamkera Rais Samia Suluhu Hassan na amewaagiza wayakomeshe ili wananchi waendelee kupata huduma bora na za uhakika.

Kwa upande wake, Kaimu Mtendaji Mkuu wa TEMESA, Moses Mabamba amesema Serikali inamiliki vivuko vitatu kwa ajili ya Kivukoni na Kigamboni ambapo kwa sasa kinachotoa huduma ni kimoja tu cha MV. Kazi huku kivuko cha MV. Magogoni kipo kwenye matengenezo Mombasa tangu mwaka 2023 kwa at gharama ya Sh75 bilioni.

Amesema kabla ya kuharibika kwa vivuko hivyo walikuwa wanakusanya Sh20 milioni kwa siku na sasa zinakusanywa Sh3.61 milioni pekee.

Serikali imezitaka jamii  zenye changamoto ya usimamizi wa mirathi kutoa taarifa kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udham...
24/12/2025

Serikali imezitaka jamii zenye changamoto ya usimamizi wa mirathi kutoa taarifa kwa Wakala wa Usajili, Ufilisi na Udhamini (RITA) ili kupata mwongozo wa kisheria.

Naibu Waziri wa Katiba na Sheria, Zainabu Katimba amesema hayo katika hafla ya kumpongeza Anna Zambi, aliyepatiwa msaada wa kisheria na RITA kupitia huduma ya udhamini wa umma.

Waziri Katimba amesema bado kuna wananchi wengi wenye uhitaji wa huduma za msaada wa kisheria kuhusu mirathi, lakini wanashindwa kufikiwa au hawajui mahali sahihi hivyo kupoteza haki zao.

Amesema changamoto hizo husababishwa na watu wenye tamaa ndani ya familia wanaotumia nguvu kupora mali za warithi na kitoa mfano wa tukio la Anna aliyepewa msaada wa kusimamiwa mirathi yake kupitia amri ya mahak**a.

“Msaada wa kisheria alioupata Anna ni ushahidi wa dhamira ya Serikali katika kuhakikisha wanufaika wa huduma ya udhamini wa umma wanalindwa na kupata haki zao stahiki kupitia RITA."

Kabidhi Wasii Mkuu na Afisa Mtendaji Mkuu wa RITA, Frank Kanyusi amesema taasisi hiyo inatekeleza jukumu la udhamini wa umma kwa mujibu wa Sheria ya Mdhamini wa Umma (Mamlaka na Majukumu) Sura ya 31.

Ujenzi wa Bwawa kubwa la kilimo cha umwagiliaji la Mkomazi lililopo kijiji cha Manga Mtindiro, Wilaya ya Korogwe, Tanga ...
24/12/2025

Ujenzi wa Bwawa kubwa la kilimo cha umwagiliaji la Mkomazi lililopo kijiji cha Manga Mtindiro, Wilaya ya Korogwe, Tanga umefikia asilimia 85.

Kukamilika kwa Bwawa hilo linalojengwa na Tume ya Taifa ya Umwagiliaji (NIRC), kutasaidia kuongeza uzalishaji wa mazao mwaka mzima kwa wakulima wa wilaya hiyo badala ya kusubiri mvua ambazo kwa muda mrefu zmeshindwa kuleta tija.

Akizungumza katika ziara ya kukagua maendeleo ya miradi huo, Mkurugenzi Mkuu wa NIRC, Raymond Mndolwa amesisitiza umuhimu wa kuhakikisha mradi huo unakamilika kwa wakati na kwa viwango vinavyotakiwa ili kuwanufaisha wakulima wa eneo hilo.

"Nimefika nijionee mwenyewe maendeleo ya mradi, kusikiliza changamoto zinazojitokeza pamoja na kuhakikisha kuwa mradi unatekelezwa kwa mujibu wa mpango kazi na fedha zilizotengwa."

Amesema Tume inaendelea kutekeleza miradi mingine ya umwagiliaji katika maeneo mbalimbali nchini ikiwa ni sehemu ya mkakati wa Serikali wa kuboresha sekta ya kilimo na kuondokana na kilimo kinachotegemea mvua.

Meneja wa Tume ya Taifa ya Umwagiliaji Mkoa wa Tanga, Mhandisi Leonard Someke, amesema bwawa hilo linatarajiwa kukamilika Februari, 2026 na kuwa na uwezo wa kuhifadhi maji ya kutosha kwa ajili ya kilimo cha umwagiliaji katika msimu wote wa mwaka, jambo litakalosaidia kuongeza uzalishaji wa mazao kwa wakulima wa eneo hilo.

Tafiti nyingi zimethibitisha kuwa *mabadiliko ya tabia nchi* ni tishio kubwa kwa kilimo—hasa barani Afrika na Tanzania. ...
24/12/2025

Tafiti nyingi zimethibitisha kuwa *mabadiliko ya tabia nchi* ni tishio kubwa kwa kilimo—hasa barani Afrika na Tanzania. Mabadiliko haya huleta athari k**a vile:

- Kupungua kwa mvua au kutokea kwa mvua zisizotabirika
- Kuongezeka kwa joto na ukame
- Maambukizi ya magonjwa mapya ya mimea
- Kupungua kwa rutuba ya udongo
- Kuongezeka kwa majanga k**a mafuriko na upepo mkali

Athari hizi husababisha kupungua kwa mavuno, kupanda kwa bei ya chakula, na kuongezeka kwa umasikini hasa vijijini.

Kwa mujibu wa taasisi k**a FAO, World Bank na Taasisi ya Utafiti wa Kilimo Tanzania (TARI), njia bora za kukabiliana na hali hiyo ni:

1. Kilimo hifadhi (Conservation Agriculture) kutumia mbinu zisizoharibu udongo k**a kulima kwa vishina, kupanda kwa mistari, na kutumia mabaki ya mazao kufunika udongo.

2. Mbegu zinazovumilia ukame na joto
kuwekeza katika mbegu za kisasa zinazoweza kustahimili hali ngumu ya tabia nchi.

3. Kilimo mseto (agroforestry)
kupanda miti kwenye mashamba ili kulinda mazingira na kuhifadhi unyevunyevu wa udongo.

4. Ukusanyaji na uhifadhi wa maji ya mvua – kutumia matenki, mabwawa au mifereji kuhifadhi maji kwa matumizi ya baadaye.

5. Ushirikiano wa wakulima na taasisi za hali ya hewa
kupata taarifa za utabiri wa hali ya hewa kwa wakati ili kupanga kilimo kulingana na mabadiliko ya mvua.

6. Elimu kwa wakulima
kuwapa maarifa ya kisasa kupitia mafunzo ya mara kwa mara kuhusu kilimo kinachokabiliana na tabia nchi.

Mataifa k**a Ethiopia, Burkina Faso na Kenya yameanza kufanikisha baadhi ya mbinu hizi, kwa kushirikiana na sekta binafsi, serikali na mashirika ya maendeleo.

Chanzo: FAO, World Bank, TARI, CGIAR, UNEP

Je, unafikiri ni hatua gani Tanzania inaweza kuanza nayo haraka zaidi kusaidia wakulima wetu? Tuambie kwenye comments. 👇



"Spirit ya upambanaji na nidhamu iliyooneshwa na Taifa Stars hapo jana jana dhidi ya Nigeria inapaswa kuwa endelevu husu...
24/12/2025

"Spirit ya upambanaji na nidhamu iliyooneshwa na Taifa Stars hapo jana jana dhidi ya Nigeria inapaswa kuwa endelevu hususani mechi mbili zijazo dhidi ya Uganda na Tunisia."

Muda wa Michezo na Burudani na   na  Maoni Yako tuachie Hapa  👇
24/12/2025

Muda wa Michezo na Burudani na na

Maoni Yako tuachie Hapa 👇

Utafiti wa kisayansi unabainisha kuwa ubongo wa binadamu una tabia ya kudumu na kukumbatia zaidi kumbukumbu za maumivu a...
24/12/2025

Utafiti wa kisayansi unabainisha kuwa ubongo wa binadamu una tabia ya kudumu na kukumbatia zaidi kumbukumbu za maumivu au matukio yenye hisia kali kuliko mafanikio au sifa nzuri.

Kwa mujibu wa jarida la Frontiers in Psychology (2022), binadamu anaweza kukumbuka tukio la maumivu kwa zaidi ya miaka 20, lakini asahau sifa nzuri alizopewa ndani ya siku 30.

Hii ni kwa sababu maumivu huambatana na msisimko mkubwa wa kihisia na kuchochea homoni za msongo, ambazo huimarisha kumbukumbu kwenye ubongo.

Watafiti wanaeleza kuwa hii ni sehemu ya "negativity bias" ya ubongo – tabia ya kiasili ya kupendelea kukumbuka mabaya ili kumlinda mtu dhidi ya hatari katika siku zijazo.

📌 Kwa kifupi:
- Ubongo hutunza zaidi kumbukumbu zenye msisimko mkubwa, hasa hasi.
- Sifa na mafanikio huweza kusahaulika haraka ikiwa hayakuhusisha hisia kubwa.
- Kutambua tabia hii kunaweza kusaidia watu kujifunza kuachilia maumivu ya zamani na kujenga mtazamo chanya wa maisha.

💭 Je, umewahi kusahau sifa nzuri lakini ukakumbuka tukio la huzuni kwa miaka mingi? Tueleze kwenye comments.

🖋️



Cheza IZEE LOTTO kwa JERO tu!Chagua NAMBA 9 kati ya 1-40 na unaweza kushinda hadi TZS Milioni 20 PAPO HAPOCHEZA kwa kute...
24/12/2025

Cheza IZEE LOTTO kwa JERO tu!
Chagua NAMBA 9 kati ya 1-40 na unaweza kushinda hadi TZS Milioni 20 PAPO HAPO
CHEZA kwa kutembelea https://bit.ly/nationallotterytz SASA.

18+. Cheza Kistaarabu. ITHUBA ni mwendeshaji rasmi wa Bahati Nasibu ya Taifa.

"Overall technically kuna improvement kiasi chake imeonekana kwa Taifa Stars namna ya kuzicheza mechi kubwa. Fomu nzuri,...
23/12/2025

"Overall technically kuna improvement kiasi chake imeonekana kwa Taifa Stars namna ya kuzicheza mechi kubwa.

Fomu nzuri, tactical discipline, budluck matokeo yamekataa.

‎Nimependa reaction tukipoteza umiliki wa mpira, kustiki kwenye mpangi kazi more defend, kaba njia k**a mtu eneo nyeti, lakini pia uharaka wa kujenga shambulizi, bahati mbaya finishing imetuhukumu.

‎Super iko Eagles wamecheza kikubwa experience matter kwenye mashindano makubwa, quality wachezaji wakubwa imeendelea kuwanyanyasa Tanzania."

‎Full Time

‎Nigeria 2-1 Tanzania

🖋️

Je,.k**a umetazama mchezo unaonaje? Maoni yako hapo chini 👇‎

Address

7-C, Ilemela Industrial Area, Airport Road
Mwanza
POBOX1732

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Free Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Free Africa:

Share