Radio Free Africa

Radio Free Africa Ukurasa Rasmi wa Radio Free Africa
Tunasikika Nchi Nzima & Kimataifa. Kazi yake k**a ulivyo wajibu wa vyombo vya Habari, Kuhabarisha, kuelimisha, Kuburudisha.
(447)

Radio yenye Makao Makuu Jijini Mwanza Tanzania na kusikika katika Mikoa Mbalimbali kupitia Masafa ya FM, Masafa ya Kati 1377 ,Mtandao na Kupitia Ving'amuzi/Visimbuzi mbalimbali.

Mgombea wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo Fatma Fereji ameanza ...
18/08/2025

Mgombea wa Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa tiketi ya Chama cha ACT Wazalendo Fatma Fereji ameanza zoezi kutafuta wadhamini wa Mgombea wa Urais wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama hicho Luhaga Mpina katika Mkoa wa Kusini Unguja leo tarehe 18 Agosti 2025.

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa amri ya kusitishwa matangazo ya moja kwa moja (live streaming) ya mwenendo wa sha...
18/08/2025

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu imetoa amri ya kusitishwa matangazo ya moja kwa moja (live streaming) ya mwenendo wa shauri la uhaini linalomkabili Mwenyekiti wa CHADEMA, Tundu Lissu, wakati wote wa "committal proceedings".

Hakimu Mkazi Mkuu, Franco Kiswaga amebainisha juu ya amri hiyo ambapo amesema lengo ni kuwalinda mashahidi wa kiraia ambao watatoa ushahidi wao.

Akitoa amri kuhusu kesi dhidi ya Tundu Lissu kurushwa moja kwa moja ( ), Agosti 18, 2025 Hakimu Mkazi Mfawidhi,

Kiswaga amesema Mahak**a imesitisha matangazo ya moja kwa moja (LIVE), utangazaji, usambazaji wa moja kwa moja au aina nyingine ya uenezaji wa moja kwa moja kwa umma ikijumuisha mitandao ya kijamii hadi pale itakapotolewa amri nyingineyo.

Mahak**a pia imezuia taarifa yoyote itakayopelekea mashahidi hao au familia zao kutambulika na pia mtu yeyote atakayetoa taarifa ya kuwafanya mashahidi hao au familia zao kutambulika, au kugundua sauti zao au makazi yao atakuwa ametenda kosa la jinai na atashtakiwa.

Waziri wa habari sanaa na michezo Prof. Palamagamba  Kabudi amesema wizara imeingia makubaliano na chuo kikuu huria cha ...
18/08/2025

Waziri wa habari sanaa na michezo Prof. Palamagamba Kabudi amesema wizara imeingia makubaliano na chuo kikuu huria cha Tanzania (OUT) ili kuruhusu waandishi wa habari waliokosa sifa za kuwa na Angalau Stashahada ya taaluma ya habari, wakasome katika chuo hicho ili kukidhi sifa na masharti yanayotakiwa kwa Mujibu wa sheria.

Ametoa kauli hiyo wakati akihitimisha mazungumzo yake na wanahabari wa kanda ya Nyanda za juu kusini, katika mafunzo maalumu yanayolenga kuwajengea uwezo kuelekea Uchaguzi mkuu wa mwaka 2025.

 Leo live ndani ya   HOSTED BY  Music :dj_bonny255Gfx by   💪🏿🔥🔥18.08.2025 Monday2025unakuhusu2pm_4pm
18/08/2025

Leo live ndani ya HOSTED BY
Music :dj_bonny255
Gfx by
💪🏿🔥🔥
18.08.2025 Monday

2025unakuhusu
2pm_4pm

Baadhi ya abiria waliokuwa wakisafiri kwa basi la Mbeya City Express lenye namba za usajili T 667 EMK, linalofanya safar...
17/08/2025

Baadhi ya abiria waliokuwa wakisafiri kwa basi la Mbeya City Express lenye namba za usajili T 667 EMK, linalofanya safari kati ya Mbeya na Tanga, wanahofiwa kupoteza maisha baada ya basi hilo kupata ajali katika eneo la Mengele–Chimala, Wilaya ya Mbarali mkoani Mbeya, majira ya saa 11 jioni, tarehe 17 Agosti 2025.

Jumatatu, tarehe 18 Agosti 2025 kesi mbili zitaendelea; Mosi, Kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Taifa  kat...
17/08/2025

Jumatatu, tarehe 18 Agosti 2025 kesi mbili zitaendelea; Mosi, Kesi ya Uhaini inayomkabili Mwenyekiti wa Chama Taifa katika Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu kuanzia saa tatu asubuhi.

Pili, Kesi ya madai iliyofunguliwa Mahak**a Kuu Kanda ya Dar es salaam na Said Issa Mohamed dhidi ya Bodi ya Wadhamini ya Chama, ambapo Jaji anakusudiwa kutoa uamuzi mdogo juu ya Chama kuendelea na shughuli zake au la!

17/08/2025

Wananchi wa mataifa ya Tanzania na Burundi watapata ahueni ya usafiri baada ya nchi hizo kuanza ujenzi wa Reli ya Kisasa...
17/08/2025

Wananchi wa mataifa ya Tanzania na Burundi watapata ahueni ya usafiri baada ya nchi hizo kuanza ujenzi wa Reli ya Kisasa ya SGR.

Tayari mataifa hayo yameweka rasmi jiwe la msingi la ujenzi wa eli hiyo ya ksasa kwa kipande cha kutoka Uvinza mkoani Kigoma hadi Msongati nchini Burundi.

Halfa hiyo ya Uwekaji wa jiwe la Msingi umefanyika katika eneo la Msongati Mkoa wa Burungu nchini Burundi ambapo uwekaji huo wa jiwe la Msingi uliongozwa na Rais wa Burundi, Evariste Ndayishimiye na Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa akmwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan.

Akizungumza katika hafka hiyo, Waziri Mkuu wa Tanzania, Kassim Majaliwa amesema utekelezaji wa mradi huo ni hatua kubwa kwa nchi hizo katika kuimarisha uchumi wa nchi hizo lakini pia mahusiano ya kindugu yaliyopo baina ya nchi hizo mbili.

Naye Rais wa Burundi, amesema utekelezaji wa mradi huo ni jambo kubwa kiuchumi kwa nchi hiyo katika kusafirisha mizigo hasa madini ya Nikel ambayo yanapatikana kwa wingi katika eneo hilo la Msongati mkoa Burungu nchini Burundi lakini hayakuwa yakichangia sana uchumi wa nchi hiyo kwa kukosa miundo mbinu ya kuyasafirishia.

Mkurugenzi Mkuu wa Shirika la reli nchini (TRC), Machibya Masanja alisema kuwa uwekaji wa jiwe hilo la msingi unahusisha utekelezaji wa mradi wa reli ya kisasa yenye urefu wa kilometa 190 kutoka Uvinza mkoani Kigoma nchini Tanzania hadi Msongati mkoa wa Burungu nchini Burundi wenye thamani ya Dola Zaidi ya Milioni mbili za Marekani ukiwa mradi wa miaka sita.

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameshiriki uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kisasa ya kutoka Uvinza hadi Muso...
17/08/2025

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa ameshiriki uwekaji wa jiwe la msingi la ujenzi wa reli ya kisasa ya kutoka Uvinza hadi Musongati na kuwahahikishia Watanzania na Burundi.

Akimwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan, Majaliwa amesema reli hiyo itakayokuwa na urefu wa km.240 pindi ikikamilika, itakuwa ndiyo reli ya kwanza inayounganisha nchi na nchi katika ukanda wa Afrika Mashariki.

Katika hafla hiyo iliyofanyika eneo la Musongati, Burundi, Waziri Mkuu amesema kukamilika kwa ujenzi wa reli hiyo kutasaidia kuunganisha masoko na kuendeleza biashara baina ya Tanzania na Burundi.

Kwa upande wake, Rais wa Burundi, Meja Jenerali Evarist Ndayishimiye alisema kuanza kwa ujenzi wa reli hiyo kutatibu shauku ya muda mrefu ya nchi hiyo kuwa na usafiri wa reli.

"Leo ni siku ya furaha sana kwetu. Tumepata jawabu la tangu enzi na enzi. Mwaka 1921, mradi huu ulianzishwa na Wabelgiji kisha wakaja Wajerumani lakini wakashindwa. Leo hii Tanzania na Burundi tumeweza," amesisitiza

Rais Ndayishimiye amempongeza Rais Samia kwa kufikia hatua kubwa za maendeleo. "Ukirudi nyumbani mwambie Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan kwamba tunampongeza sana kwa kuleta maendeleo ya haraka nchini Tanzania."

"Nimekaa Tanzania kwa muda mrefu lakini kwa sasa nikija naweza kupotea. Magomeni napajua, Tabata na Vingunguti napajua, Mwenge napajua, na Kinondoni nilishakaa; lakini kwa sababu ya maendeleo yaliyopatikana, naweza kupotea. Tunamshukuru kwa uongozi wake imara,"

Mapema, Waziri wa Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa ameisema utekelezaji wa mradi huo unaenda sambamba na Ajenda 63 ya Umoja wa Afrika ambayo inataka bara la Afrika liunganishwe kwa mtandao wa reli ya kisasa.

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Iva...
16/08/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dk Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Ivato – Antananarivo nchini Madagascar.

Dk Mpango amewasili Ijumaa Agosti 15,2025 ambako anamwakilisha Rais Samia Suluhu Hassan katika Mkutano wa 45 wa Wakuu wa Nchi na Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo Kusini mwa Afrika (SADC) unaofanyika Antananarivo Madagascar kuanzia leo mpaka Agosti 17, 2025.

Wizara ya Afya imesema taarifa zinazozagaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa idadi ya vipimo vya Virusi vya Ukimwi...
16/08/2025

Wizara ya Afya imesema taarifa zinazozagaa kwenye mitandao ya kijamii zikidai kuwa idadi ya vipimo vya Virusi vya Ukimwi (VVU) kwa wajawazito na wanaonyonyesha imepunguzwa kutoka vitano hadi viwili si sahihi na kwamba wanapaswa kupimwa mara tatu.

Kupitia taarifa yake Mganga Mkuu wa Serikali, Dk Grace Magembe, jijini Dodoma leo Ijumaaa Agosti 15, 2025 amesema madai hayo hayana ukweli wowote na ni upotoshaji unaoweza kuleta taharuki kwa jamii

“Kwa mujibu wa mwongozo wa Taifa unaozingatia mapendekezo ya Shirika la Afya Duniani (WHO), tafiti za kisayansi na mikakati ya kitaifa, wajawazito na wanaonyonyesha wanapaswa kupima VVU angalau mara tatu tangu kutungwa kwa mimba hadi kipindi cha kunyonyesha."

Ameongeza kuwa, upimaji wa kwanza wa VVU, Kaswende na Homa ya Ini hufanywa katika hudhurio la kwanza la kliniki. Upimaji wa pili hufanyika kati ya wiki ya 32 na 36 za ujauzito na wa tatu ndani ya miezi mitatu baada ya kujifungua wakati katika makundi hatarishi.

Amesema kuwa vipimo hivyo hufanyika kila baada ya miezi mitatu sambamba na utoaji wa dawa kinga.

Dk Grace amesena huduma hizo zinatolewa bure kote nchini na hata katika kipindi ambacho ufadhili wa wahisani umepungua, Serikali imeendelea kutoa huduma hizo kutokana na uwekezaji mkubwa kutoka vyanzo vya ndani. Katika mwaka wa fedha 2024/25.

"Serikali imetoa Sh141.98 bilioni na mwaka 2025/26 imelenga kutumia Sh 158 bilioni mwaka 2025 wa ajili ya huduma za UkimwiI, malaria na Kifua Kikuu, zikiwamo huduma za upimaji wa VVU kwa wajawazito ili kulinda afya ya mama na mtoto.

Wizara ya Afya imeonya kuwa hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya yeyote atakayetoa taarifa za afya zisizo sahihi bila kuwa na taaluma wala mamlaka ya kutoa taarifa za afya

Jumamosi Agosti 16, 2025 kwenye kipindi cha Ukimwi na Jamii tutakuwa na Mkuu wa Kitengo cha Usalama wa Chakula, Maji na ...
15/08/2025

Jumamosi Agosti 16, 2025 kwenye kipindi cha Ukimwi na Jamii tutakuwa na Mkuu wa Kitengo cha Usalama wa Chakula, Maji na Usafi wa Mazingira kutoka Wizara ya Afya, Anyitike Mwakitalima.

Atakueleza msikilizaji mambo mengi yanayohusu afya ikiwemo Usafi wa Mazingira unavyosaidia kudhibiti magonjwa ya kuambukiza pia jinsi usalama wa chakula na maji unavyosaidia kuboresha afya ya mtu anayeishi na Virusi vya Ukimwi.

Mtu ni Afya, " fanya kweli Usibali Nyuma"

Address

Mwanza

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Free Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Free Africa:

Share