13/11/2025
Mbunge wa Jimbo la Isimani, William Lukuvi, amesema Waziri Mkuu, Dkt. Mwigulu Lameck Nchemba ni mchumi mbobevu aliyesimamia makusanyo ya kodi na kuisaidia Serikali inayoongozwa na Rais Samia Suluhu Hassan kutekeleza vyema miradi ya maendeleo.
Amesema kwa kazi nzuri iliyofanywa na utawala wa Rais Samia akisaidiwa na Dkt. Nchemba, imewezesha pia wabunge wengi wa CCM kuaminiwa na kurejea tena bungeni.