Radio Free Africa

Radio Free Africa Ukurasa Rasmi wa Radio Free Africa
Tunasikika Nchi Nzima & Kimataifa. Kazi yake k**a ulivyo wajibu wa vyombo vya Habari, Kuhabarisha, kuelimisha, Kuburudisha.
(446)

Radio yenye Makao Makuu Jijini Mwanza Tanzania na kusikika katika Mikoa Mbalimbali kupitia Masafa ya FM, Masafa ya Kati 1377 ,Mtandao na Kupitia Ving'amuzi/Visimbuzi mbalimbali.

03/06/2026

Imekuwa k**a mtoko wa sikukuu kwa familia mbalimbali jijini Dar es Salaam, baada ya Serikali kuandaa maeneo maalumu kwa wananchi kuangalia mechi ya fainali ya mataifa bingwa Afrika kwa vijana wenye umri wa chini ya miaka 17.

Katika maeneo mbalimbali ya Jiji hilo, Televisheni kubwa zimefungwa mitaani kutoa nafasi kwa wananchi kuangalia mechi hiyo ya fainali inayoihusisha timu ya Taifa ya vijana chini ya miaka 17 ya Tanzania 'Serengeti Boys' dhidi ya Senegal.

Mbali na wananchi katika maeneo hayo, viongozi mbalimbali wa Serikali ngazi za Mikoa na Wilaya, wameshuhudiwa wakikusanyika sambamba na wananchi kufuatilia mechi hiyo, inayoiweka Tanzania katika ramani ya soka duniani.

Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, alitoa ndege maalumu kuwabeba wachezaji na mashabiki kwa ajili ya kwenda kuishabikia timu hiyo ya vijana.

Hata hivyo, Dkt Samia pia alitoa Sh500 milioni k**a motisha kwa vijana hao, baada ya kufanikiwa kuingia hatua ya fainali ya michuano hiyo

Amani na utulivu umetawaka katika maeneo hayo, wananchi wakifuatilia mechi hiyo.

02/06/2026

Mbunge kupitia Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Simai Mohamed Said, amekemea vitendo vya usaliti vinavyofanywa na baadhi ya viongozi ndani ya Serikali, akisema vinakwenda kinyume na dhamira na juhudi za Rais Dkt Samia Suluhu Hassan.

Simai, ameijenga hoja yake hiyo akiwafananisha viongozi wasaliti na Yuda, huku akiwasihi waache kutumia majina ya viongozi wastaafu na kufanya siasa za 2030 mapema, jambo alilosema linalochonganisha na kuharibu utulivu.

Mbunge huyo, ameeleza hayo bungeni jijini Dodoma leo, Jumanne Juni 2, 2026 alipochangia hoja katika mjadala wa Bajeti ya Wizara ya Fedha kwa mwaka wa fedha 2026/27.

Amesema Rais Dkt Samia Suluhu Hassan, anaongoza Serikali yake na Watanzania kwa upendo na mshik**ano, lakini kufanikiwa kwa Taifa wakati mwingine kuna watu wanaotembea kinyume.

“Leo nambatiza mmoja aliyekuwepo ndani ya Serikali, ni Yuda. Nasema hivyo kwanini, sisi tunataka maendeleo ya nchi yetu, kosa la mama (Dkt Samia) ni wapi? Kwa sababu ya kumuamini mtu kumbe ni Yuda,” amehoji.

Amesisitiza kiongozi huyo msaliti ameibuka hadi katika nyumba za ibada akitafuta huruma za watu na kutumia majina ya viongozi wastaafu ilimradi aonyeshe anapendwa.

02/06/2026

Maadhimisho ya Wiki ya Maziwa nchini yamefikia kilele chake Juni 1, ambayo pia ni Siku ya Maziwa Duniani, huku wadau wa sekta hiyo wakijivunia mafanikio yaliyopatikana na kuweka mikakati ya kufikia lengo la kuzalisha lita bilioni 13 za maziwa kwa mwaka ifikapo mwaka 2030.

Katika maonesho hayo yaliyofanyika mkoani Iringa, wadau kutoka sekta za uzalishaji, usindikaji, biashara na maendeleo walijadili namna ya kuongeza tija ya uzalishaji wa maziwa, kuboresha masoko na kuimarisha ubora wa bidhaa za maziwa ili kukidhi mahitaji ya ndani na nje ya nchi.

Takwimu zinaonesha kuwa uzalishaji wa maziwa nchini umeendelea kuongezeka kutoka takribani lita bilioni 3.4 mwaka 2022/23 hadi zaidi ya lita bilioni 4 katika miaka ya hivi karibuni, hatua inayotoa matumaini ya kufikia malengo makubwa ya sekta hiyo. Serikali na wadau pia wanaendelea kuhamasisha matumizi ya maziwa kutokana na mchango wake katika lishe bora, hasa kwa watoto, vijana na wanawake.

Akizungumza wakati wa kufunga maadhimisho hayo, Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Hery James, aliwapongeza wadau wa tasnia ya maziwa kwa kuchagua Iringa kuwa mwenyeji wa maonesho hayo na kuwakaribisha kuendelea kuitumia mkoa huo kwa shughuli za maendeleo ya sekta ya mifugo na maziwa.

alisema Iringa ina mazingira mazuri kwa ufugaji wa kisasa na uzalishaji wa maziwa, huku akisisitiza umuhimu wa kuendelea kuhakikisha ubora wa maziwa yanayozalishwa na kusindikwa ili kulinda afya za walaji na kuongeza ushindani wa bidhaa za Tanzania katika masoko mbalimbali.

Aidha, wadau wameahidi kuendelea kuwekeza katika kuboresha mifugo ya maziwa, uzalishaji wa malisho bora, huduma za ugani, teknolojia za usindikaji pamoja na kukabiliana na changamoto za mabadiliko ya tabianchi ili kuongeza uzalishaji na kipato cha wafugaji nchini. Kupitia juhudi hizo, sekta ya maziwa inatarajiwa kuwa moja ya nguzo muhimu za kukuza uchumi na kuimarisha usalama wa chakula na lishe nchini.

02/06/2026
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofauti ya Picha alipoondoka Katika Uwan...
02/06/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan katika Matukio tofauti ya Picha alipoondoka Katika Uwanja wa Ndege wa Julius Nyerere Dar es salaam kuelekea Nchini Urusi kwenye Ziara ya Kitaifa ikiwa ni Mwaliko wa Rais wa Shirikisho la Urusi Mhe. Vladimir Putin Leo Juni 02, 2026.

Watu wana Siri sana
02/06/2026

Watu wana Siri sana



Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania, Profesa George Msalya, akitoa ufafanuzi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Heri James,...
01/06/2026

Msajili wa Bodi ya Maziwa Tanzania, Profesa George Msalya, akitoa ufafanuzi mbele ya Mkuu wa Mkoa wa Iringa, Heri James, akiwa ameambatana na viongozi mbalimbali wa Mkoa, akiwepo DC wa Mufindi DKT. Linda Selekwa, kulia kwa RC

Profesa Msalya amesema Wiki ya Maziwa iliyofanyika mkoani Iringa imefanikiwa kuwakutanisha wadau wa tasnia ya maziwa kutoka maeneo mbalimbali nchini kwa lengo la kujadili fursa, changamoto na mikakati ya kuimarisha sekta hiyo.

Wadau hao kupitia wiki hii kuelezea dhamira ya kuongeza uzalishaji wa maziwa nchini hadi kufikia lita bilioni 13 katika miaka michache ijayo, hatua itakayochangia kuimarisha usalama wa chakula, lishe na ukuaji wa uchumi.

🖊️ 📸

Address

7-C, Ilemela Industrial Area, Airport Road
Mwanza
POBOX1732

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Free Africa posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Free Africa:

Share