Btv online

Btv online HARD NEWS || SOFT NEWS || GOSPEL NEWS
"ON TIME EVERY TIME". we reach wherever you're

 :Lionel Messi ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Argentina  baada ya miaka 20 ya kuitumikia nchi yake.Messi...
31/08/2026

:Lionel Messi ametangaza kustaafu kuichezea timu ya taifa ya Argentina baada ya miaka 20 ya kuitumikia nchi yake.

Messi amecheza jumla ya michezo 207, akifunga mabao 125 na kutoa asisti 68 akiwa na Argentina

Katika kipindi chake na timu hiyo, Messi ameshinda Kombe la Dunia 2022, pamoja na Copa América mara mbili. Pia amefika fainali ya Kombe la Dunia 2026.

Ni mwisho wa safari ya kipekee kwa Messi akiwa mmoja wa wachezaji walioacha historia kubwa katika timu ya taifa ya Argentina.

| Follow us

 :Mwanamke mwenye umri wa miaka 19 raia wa Brazil amejifungua mapacha (watoto wawili) wenye baba tofauti wa kibiolojia k...
31/08/2026

:Mwanamke mwenye umri wa miaka 19 raia wa Brazil amejifungua mapacha (watoto wawili) wenye baba tofauti wa kibiolojia kwa mujibu wa vipimo vya DNA ambapo hali hiyo hutokea baada ya kufanya tendo la ndoa na wanaume wawili katika siku moja.

Vipimo vya DNA vilithibitisha kuwa kila pacha alitungishwa mimba na mwanaume tofauti... hali adimu sana inayojulikana k**a *heteropaternal superfecundation*.

Hali hii hutokea pale ambapo mayai mawili yaliyoachiliwa katika mzunguko mmoja wa hedhi yanapohutubishwa na mbegu za kiume kutoka kwa wanaume wawili tofauti..✍️

| Follow us .

 :Chelsea imetangaza rasmi kumsajili kipa wa kimataifa wa Argentina, Emiliano Martínez, kutoka Aston Villa.Kipa huyo mwe...
30/08/2026

:Chelsea imetangaza rasmi kumsajili kipa wa kimataifa wa Argentina, Emiliano Martínez, kutoka Aston Villa.

Kipa huyo mwenye umri wa miaka 33 amekamilisha uhamisho wake kwenda Stamford Bridge baada ya Chelsea na Aston Villa kufikia makubaliano ya uhamisho wenye thamani ya £7.5 milioni.

Martínez amesaini mkataba wa miaka miwili, huku Chelsea ikiwa na uwezekano wa kuongeza mkataba huo kwa mwaka mmoja zaidi.

“Ni ndoto kuwa hapa! Natamani sana kupata mafanikio hapa. Mimi ni mtu ambaye nataka kushinda kila kitu ninachokifanya, na ninataka kuleta roho hiyo kwenye klabu hii ya soka.” Amesema Martinez baada ya kusaini kandarasi

| Follow us

29/08/2026

makamu wa rais Deogratias Ndejembi aapishwa kuwa makamu wa rais wa 13 Tanzania...✍️

28/08/2026

PENATI AU SIO PENATI🤌

Kutokana na matukio mawili yaliyotokea kati ya Simba SC na Coastal Union ambayo yalihusisha mikwaju ya penati kwa wewe unavyoona ilikuwa penati au vp..??

| Follow us.

27/08/2026

KUGOMBANA KIVYAMA NI UJINGA BY DKT NCHIMBI..✍️

 : Waziri wa Nishati ambaye ni Mbunge wa Chamwino Deogratius Ndejembi, ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanz...
26/08/2026

: Waziri wa Nishati ambaye ni Mbunge wa Chamwino Deogratius Ndejembi, ameteuliwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, kuwa Makamu wa Rais.

Uteuzi huo umetangazwa leo na Katibu Mkuu wa CCM Dkt. Asha Rose Migiro wakati akitangaza maazimio ya Kikao Maalum cha Halmashauri Kuu ya CCM kilichofanyika jijini Dar es Salaam, mapema leo Jumatano tarehe 26 Agosti 2026 na kuongozwa na Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi (CCM) Dkt. Samia Suluhu Hassan.

| Follow us..

Address

Mwanza

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Btv online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share