366 Entertainment MEDIA

366 Entertainment MEDIA Burudani basically we write different type of story, script,books, for the company and anyone who wants it.

and also making filims,music and start some tv and radio shows are our strategies especially reality shows and other entertainment which involve the youth.

Baada ya watu wengi kuonesha shauku ya kujua sasa hivi wapo wapi, Kayumba  kwa sasa yupo Uturuki akiendelea kufanya kazi...
05/08/2023

Baada ya watu wengi kuonesha shauku ya kujua sasa hivi wapo wapi, Kayumba kwa sasa yupo Uturuki akiendelea kufanya kazi za sanaa, na Emmy yupo Sweden.

Je ulitegemea wangekuwa wapi?

⚠️"Nilikuwa naumwa sana, nililazwa Muhimbili kwa muda wa wiki mbili na nusu, Sikukuu ya Pasaka ilinikuta Muhimbili, Siku...
21/06/2023

⚠️"Nilikuwa naumwa sana, nililazwa Muhimbili kwa muda wa wiki mbili na nusu, Sikukuu ya Pasaka ilinikuta Muhimbili, Sikukuu ya Eid ilinikuta Muhimbili, Meimosi ilinikuta pale nikiwa nimelazwa na hata Birthday yangu ya mwaka huu ilinikuta kitandani, kwahiyo mwaka huu kwangu umekuja na mazonge k**a mwaka jana alipoondoka binti yangu 'Maunda Zoro'" - amesema Zahir Zoro msanii mkongwe wa muziki nchini na kuongeza

"Nilianza kuumwa ile siku aliyofariki Maunda, tarehe 13 April ndiyo nilianza kujisikia naumwa hadi baadae ambapo ilikuwa too much, nilikuwa natapika sana nyongo na uchafu mwingine, namshukuru Mungu, namshukuru Banana Zorro na Mwana FA ambao walipambana kwa kusimamia vipimo na gharama, wamenipigania sana kwasababu wakati nimelazwa Muhimbili nilikuwa siwezi kula nilikuwa naweza kula tu matunda k**a tikitimaji na juice kwa muda wa wiki mbili"

"Namkumbuka mwanangu kwa kila kitu, naweza nikawa naangalia movie kwenye simu au kwenye TV, nikiona mtu anambembeleza mtoto analia namkumbuka mwanangu Maunda Zorro kwasababu watoto wangu nimewalea mwenyewe tangu wakiwa wadogo sana, nimewalea mimi mwenyewe kwa mikono yangu na nilikuwa natoka jeshini nikiondoka nilikuwa nawafungia ndani kwenye chumba changu"

"Niliporudi kutoka hospitali nilikuta watoto wangu wametoa makochi yote sebreni, wamesafisha nyumba, naona walijua k**a nitakufa sitarudi, nilishtuka sana, sijui walifikiria nini ila nawashukuru kwa yote, tangu Maunda afariki nimesitisha kufanya kazi za muziki, nimejikita kwenye kumuombea dua, namuombea dua kila siku"- Zahir Zorro, baba mzazi wa wasanii Banana Zoro na Maunda Zoro

"Mume Wangu Alinificha Ana Watoto 5, Alikuwa Anaogopa Kuniambia K**a Alikuwa na Mtoto Nje ya Ndoa" - Diva
18/02/2023

"Mume Wangu Alinificha Ana Watoto 5, Alikuwa Anaogopa Kuniambia K**a Alikuwa na Mtoto Nje ya Ndoa" - Diva

ESMA " NIMEOKOKA "Esma Platnumz; ni dada’ke msanii nguli nchini Tanzania, Diamond Platnumz ambaye ameonesha furaha yake ...
09/12/2022

ESMA " NIMEOKOKA "

Esma Platnumz; ni dada’ke msanii nguli nchini Tanzania, Diamond Platnumz ambaye ameonesha furaha yake baada ya kuchukua vipimo vya janga la Ukimwi (HIV) na majibu kutoka kuwa yu mzima.

Esma ameposti majibu hayo na kwa furaha akasujudu na kutoa shukrani kwa Mungu huku akiahidi kuwa sasa anaokoka kabisa na hataingia katika mahusiano ambayo yatahatarisha hali yake ya afya.
“Ahsante Mungu, sasa ndugu zangu nimeokoka rasmi,” Esma amesema.

Esma ni mmoja kati ya wanamama wa kisasa wenye tija na ufanisi mkubwa maishani, lakini nyota ya ndoa imemkataa kabisa au tuseme imekawia kumuangazia.

Kumbukumbu zinaonesha kwamba Esma ambaye ni muuza vitambaa, madera na mitandio ya wanawake bado yuko singo zaidi ya miaka miwili tangu alipoachana na mfanyabiashara Msizwa.

Msizwa alimuoa Esma k**a mke wake wa tatu katika sherehe ya harusi iliyotangazwa sana mwezi Julai 2020 katikati ya janga la Korona, lakini waliachana miezi mitatu baada ya harusi yao.

Mapema mwezi wa Novemba 2020, Esma ambaye ni mama wa watoto wawili aliozaa na wanaume tofauti alisema kwamba, aliachana na ndoa hiyo kwa sababu mwanaume wake alikuwa na jicho la nje.

Hadi muungano wake na Msizwa, Esma alikuwa bado katika uhusiano usio na mwelekeo thabiti na baba wa mtoto wake, Petit Man Wakuache ambaye hivi karibuni ameoa.

INASRMEKANA KAJALA NA HARMONIZEKwa mujibu wa mtangazaji wa wasafi Diva, harmonize na kajala na kuandika visa mbalimbali ...
09/12/2022

INASRMEKANA KAJALA NA HARMONIZE

Kwa mujibu wa mtangazaji wa wasafi Diva, harmonize na kajala na kuandika visa mbalimbali vilivyo pelekea kuachana kwa wawili hao


Hii Ni soft news inawajia live toka kwa Diva kwanza ni Muhtasari wake.
ameachwa , ame blockiwa kila Mahali ..
Mapenzi haya kweli hayana Mwalimu . love hurts ...
link in my bio nimeelezea Jinsi Ya Kutibu kuvunjika kwa moyo ...

ila ukiskiza Mkasa Mzima ... sehemu kuu 2.
alipofumwaaaa anaongea na simu akaulizwa unaongea na nani akalowa ghafla , sehemu Ya Pili alipobambwa ananyata kwa dada , Sehemu Kubwa kuliko ni alipoanza vunja Pafyum za watu ati hasiraaaaa kumbe wee wee language ...

Haya Mambo bwana ... Sijaelewa Kwann bro kavunja sana Pafyum za watu alipofukuzwa ... kaulizwa unavunja umenunua wewe akamind ... Maana unaambiwa Pafyum ziko very expensive kaenda vunja kwa hasira aaaah no sio hasira .. ni wee wee languageeee 😔
Sema Maskini Ka angel kamechomolewa ki 🤰cha Miez 5 ... sema safari hii dogo alikuwa anahudumiaaaaaaaaaaaaaaa

MAYELE AZAMA KWENYE PENZI ZITO NA UWOYA.Habari za uhakika ni kuwa mshambuliaji wa Kimataifa raia wa Congo anayekipiga ka...
09/12/2022

MAYELE AZAMA KWENYE PENZI ZITO NA UWOYA.

Habari za uhakika ni kuwa mshambuliaji wa Kimataifa raia wa Congo anayekipiga katika klabu yenye maskani yake mitaa ya Twiga na Jangwani ( Yanga), ameshindwa kujizuia na kufikia hatua za mwisho kumuoa Uwoya k**a mke wa pili.
Awali ilidaiwa Uwoya anatembea na boss GSM lakini ukweli umebainika Mayele na Uwoya wameanza kudate mda kidogo.

Kwa sasa inasemekana Mke wa Mayele hana Furaha kabisa na mda wowote ndoa yao inaweza kuvunjika kwani hayuko tayari kuletewa mke mweza.

Video zinasambaa zikukuonesha Mayele akiwa kwenye Mahaba mazito na inasemekana ndiyo chanzo cha kutocheza mechi iliyopita kwani alikuwa Fiesta akiwa na Uwoya.

Toa maoni yako

Zaiylissa afiwa na mtoto, amfungukia kwa uchungu baba mtoto wake kwa manyanyaso yaliyokithiri. Zaiylissa au Naira wa Jua...
22/08/2022

Zaiylissa afiwa na mtoto, amfungukia kwa uchungu baba mtoto wake kwa manyanyaso yaliyokithiri. Zaiylissa au Naira wa Juakali amepost picha zinazoonesha kujeruhiwa na kushonwa na kuondoka

"Athumani Ahsanteeee🙌💔
Nilivumilia vingiiiiiiii wallahy…Guys sorry kwa hizi picha🙏
I can’t hide anymore…Na nafanya hivi labda ntakuwa na amani ya moyo wangu🙏
Coz k**a kulia nimelia vya kutoshaaaaaaa,
Ochu sina maana kwamba ww ni m,baya kupitiliza! Lahasha kuna mema pia umenitendea k**a binaadam,Lakini ubaya wako ni mkubwa sana kwangu na umefunika mema yako yote!💔🙌
Kinachoniuma zaidi ni mapito ulonipitisha wakati wa ujauzito!
Umenitesa bila kujali ata nna kiumbe chako tumboni!

Ochu umenipiga kipigo cha mbwaa mwizi nikiwa na tumbo langu la miezi8! Na hukujali na mimi nilinyanyua miguu yangu siku ya tatu tu kuja kwenu kukuomba msamaha kwa kuhofia kuwa single mama tena😥Nilijishusha aijalishi umenikosea au nimekukosea!

Ochu sitasahau siku nilioumwa nakupigia simu zangu hupokei, Mama angu anakupigia hupokei! Unatumiwa sms naumwa tunaomba utupatie card ya clinic coz ipo kwako unajibu umesafiri ilihali upo kwenu! Haikutosha nimetoka hospital usiku ule nikajikaza kuja kwenu tenaaaaa niongee na ww ukagoma kunifungulia mlango🙌Nimekaa nje na tumbo langu usiku manyunyu ya mvua yananipigia kuanzia saa6 mpaka saa8 usiku ndo unatoka AHSANTE BABA UMEWEZA🙏🙌

Yote tisaaa kumi hakuna siku nlokuhitaji k**a jana!!!!
Umekuja hospital saa3 usiku, Saa5 nimezidiwa chupu chupu nipate sijui ni kifafa au degedege sielewi yaraby na lakini ukapata nguvu ya kuondoka na kuniacha kwenye ile haliiiii🙌

Kuondoka sawa ochuuu ulishindwa ata kunipigia au kumpigia ata nlokuwa nae kumuuliza naendeleaje!
Nimejifungua mtoto amefariki saa10 Alfajir nakupigia simu toka saa10 mpaka 3 Asubuh nimepiga si chini ya mara10! Tuseme ulilala?????????
Ulivoamka hukukuta missed call zangu?????

Ata kushtuka?????????💔
Una roho ya namna gani????????
Niambie k**a kuna mahali niliwahi kukukosea ata unilipe yote hayo!

Mtoto Amefariki ndo unajali kuhusu mimi! Faraja yako mimi ya nn sasa?! Nimetosheka….
AHSANTE!
NA NIMESHAKUSAMEHE FIL DUNIA WAL AKHERA!
NIMETOA NYONGO YOTE…
NIACHE NIOMBOLEZE MWENYEWE!🙏"

Mimi Mars amesema yeye yupo singo hajawahi kuwa katika mahusiano na Marioo k**a watu wanavyodhani, amesisitiza kuwa hata...
04/06/2022

Mimi Mars amesema yeye yupo singo hajawahi kuwa katika mahusiano na Marioo k**a watu wanavyodhani, amesisitiza kuwa hata alipokuwa karibu na Young Lunya ilivumishwa kuwa ni wapenzi lakini hakukuwa na ukweli

Kipindi cha nyuma mrembo huyo aliwahi kukaririwa akisema kwamba hana matarajio yoyote ya kuwa na mwanaume wa Kibongo akidai kuwa wengi huwa hawaheshimu wanawake katika mahusiano

Flaviana Matata awataka watu wengine maarufu Tanzania wajifunze hiki kwa Diamond PlatnumzMwanamitindo huyo wa kimataifa ...
04/06/2022

Flaviana Matata awataka watu wengine maarufu Tanzania wajifunze hiki kwa Diamond Platnumz

Mwanamitindo huyo wa kimataifa amesema Diamond hataki mchezo linapokuja suala la kazi na amejiwekea thamani katika hilo. Anamaanisha kuwa Mond huwa hajitokezi ovyo ovyo katika matukio au shughuli za watu zenye mlengo wa kibiashara bila kumlipa kwanza na hilo ni lazima kwa watu ambao hana ukaribu nao wowote wa kikazi au kirafiki.

Amewataka mastaa wengine waupe thamani umaarufu wao na kazi zao badala ya kujichukulia poa na kuishia kuchukuliwa poa na wengine hata katika kazi

Mastaa wengi wa Ulaya, Marekani na Asia huingiza pesa nzuri kufanya appearances katika matukio mbalimbali hata k**a ni kwa dakika kadhaa wanalipwa pesa nzuri huku nyuma yao wakiwa na wasaidizi wenye weledi wa kazi

Ingawa Flaviana kamtolea mfano Diamond, lakini hata yeye Flaviana Matata kuna kitu mastaa wa Bongo wanatakiwa kumuiga

Flaviana ambaye aliwahi kuingia final top 6 ya Miss Universe nchini Mexico mwaka 2007, katika pages zake za mitandao ya kijamii kwa miaka mingi huwa anafuta logo yoyote ya bidhaa aliyoshikilia au kupigwa picha nayo ndio apost ikiwa hana makubaliano yoyote ya kikazi na kampuni husika kuepeuka kuwatangazia watu biashara zao bure kupitia umaarufu na jina lake. Hii hufanyika hata katika vipindi vingi vya TVs nje huwa wanaweka kivuli katika bidhaa hata mtu akifungua friji ikiwa hawana makubaliano ya kazi na wenye bidhaa husika kuepuka kuwapa promo bure

Ila mastaa wengi Bongo hawajichukulii serious, wanaona ufahari kununua kitu cha brand flani na kuringishia mitandaoni na kuwatag kabisa kampuni husika bila makubaliano yoyote ya biashara au mastaa Bongo wanakusanywa pamoja k**a kundi la wanafunzi kisha wanagaiwa pesa kiduchu wapost bidhaa flani huku wajanja wakila pesa nzuri kupitia majina yao matokeo yake hata endorsements kubwa kubwa ambazo wengezipata wanaishia kuzikosa

Ni mastaa wachache sana wenye maono Bongo

04/06/2022
Muonekano mpya wa harmonize
29/05/2022

Muonekano mpya wa harmonize

Address

Mwanza

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when 366 Entertainment MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to 366 Entertainment MEDIA:

Share