Radio Kwizera

Radio Kwizera The Official page of Radio Kwizera
97.7 Kagera, Geita and Mwanza | 93.7 Kigoma | 89.5 Shinyanga.
(205)

Community Radio, seeks to restore hope, peace and development in the North-West Tanzania.

Timu ya nje ya Dimba iko hewani kukupa updates za kimichezo zinazoendelea kutokea ndani ya ardhi ya tanzania na nje ya m...
06/08/2026

Timu ya nje ya Dimba iko hewani kukupa updates za kimichezo zinazoendelea kutokea ndani ya ardhi ya tanzania na nje ya mipaka ya Tanzania.

Ungana na na 7

Unaweza kusikiliza kupitia App ya Radio kwizera Fm ambayo inapatikana playstore na App store

06/08/2026

NJE YA DIMBA: Story za kimichezo kupitia kuanzia ndani ya nchi hadi kimataifa.

06/08/2026

ASUBUHI NJEMA ya Radio Kwizera
• Taarifa kupitia Yaliyojiri
• Tutasoma SMS ya Kero yako kupitia 0710 977 977 na kujadili mambo muhimu kupitia
• Hoja ya Asubuhi

05/08/2026

SPORTS CORNER: Habari za kimichezo kupitia Kona ya Kwanza na ya Pili yaani kuanzia ndani ya nchi hadi kimataifa.

05/08/2026

MSETO LEO: Ujumbe huu ukufikie wewe mhusika katika jambo hili muhimu.

05/08/2026

DURU ZETU ALASIRI: Habari kuu jioni ya leo kitaifa, kimataifa, Ujumbe pitia Waza Wazua, Uchumi na biashara pamoja na na Dondoo za Michezo bila kusahau maoni yako kupitia 0710 977 977

05/08/2026

CONNECTOR: Tunapiga na story vijana, wadau wa muziki pamoja na wakali kwenye tasnia ya burudani.

‎KAGERA: ‎Wakazi wa Kata ya Kibirizi, Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, wameiomba Serikali kujenga kituo ch...
05/08/2026

‎KAGERA: ‎Wakazi wa Kata ya Kibirizi, Halmashauri ya Wilaya ya Bukoba mkoani Kagera, wameiomba Serikali kujenga kituo cha Askari Wanyamapori ili kukabiliana na tatizo la tembo wanaovamia makazi na mashamba yao, hali inayosababisha uharibifu wa mazao na kuhatarisha usalama wa wananchi.

‎Ombi hilo limetolewa katika mkutano wa hadhara uliohudhuriwa na Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji, ambae kiserikali ni mlezi wa mkoa wa Kagera ambapo wananchi wamesema uvamizi wa tembo umedumu kwa muda mrefu na umeendelea kuathiri maisha yao pamoja na shughuli za uzalishaji.

‎Baadhi ya wananchi, akiwemo Anesius Aloyce na Scolastika Deogratias, wameiomba Serikali kuharakisha utekelezaji wa hatua za kudhibiti tembo hao ili kulinda maisha ya wananchi, mazao na mali zao dhidi ya uvamizi unaojitokeza mara kwa mara.

‎Akijibu hoja hizo, Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji, amesema Serikali imepanga kujenga kituo cha askari wanyamapori katika eneo hilo ili kuimarisha ulinzi na kuongeza kasi ya kukabiliana na changamoto ya tembo wanaovamia makazi ya wananchi.

‎Ameongeza kuwa Serikali itaendelea na utaratibu wa kuwaswaga tembo kurejea katika maeneo yao ya hifadhi, huku ikisisitiza ushirikiano kati ya wananchi na mamlaka husika ili kupunguza migongano kati ya binadamu na wanyamapori.

‎✍🏿 Enock Yoronimo- Bukoba, Kagera

Mhariri:



05/08/2026

MCHAKATO: Changamsha ubongo ndani ya Kabrasha, yaani swali juu swali mpaka tupate majibu.

KAGERA: ‎Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji, amewataka viongozi wa Serikali Mkoani Kagera kusimamia wakandaras...
05/08/2026

KAGERA: ‎Waziri wa Maliasili na Utalii, Ashatu Kijaji, amewataka viongozi wa Serikali Mkoani Kagera kusimamia wakandarasi wanaotekeleza ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Kyakailabwa na Soko Kuu la Bukoba ili miradi hiyo ikamilike kwa wakati, kulingana na masharti ya mkataba yanayotaka ikamilike ifikapo Januari 2027.

‎Waziri Kijaji ametoa maagizo hayo wakati wa ziara yake ya siku nne mkoani Kagera, ambapo alikagua maendeleo ya miradi hiyo inayotekelezwa katika Manispaa ya Bukoba kwa gharama ya shilingi bilioni 18.

‎Akizungumza baada ya ukaguzi, Kijaji amesema ufuatiliaji na usimamizi madhubuti wa miradi ya maendeleo ni muhimu ili kuhakikisha wananchi wanapata huduma zilizokusudiwa kwa wakati.

‎Kwa mujibu wa taarifa ya utekelezaji wa miradi hiyo, ujenzi wa Soko Kuu la Bukoba umefikia asilimia 50, huku ujenzi wa Stendi ya Mabasi ya Kyakailabwa ukifikia asilimia 10.

‎Mkandarasi wa miradi hiyo, Mhandisi Mnyala Mwambungu, amesema kampuni yake imejipanga kuhakikisha miradi yote inakamilika kwa wakati k**a ilivyoainishwa kwenye mkataba.

‎Nao baadhi ya wananchi wa Bukoba, akiwemo Alhaj Murshid Byabato na Silivia Amandius, wameiomba Serikali kuendelea kusimamia kwa karibu miradi yote ya maendeleo ili ikamilike kwa wakati na kuwanufaisha wananchi k**a ilivyokusudiwa.

‎✍🏿 Enock Yoronimo- Bukoba, Kagera

Mhariri:

Address

P. O. Box 154
Ngara

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Kwizera posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Kwizera:

Shortcuts

Share