Radio Kwizera

Radio Kwizera The Official page of Radio Kwizera
97.7 Kagera, Geita and Mwanza | 93.7 Kigoma | 89.5 Shinyanga.
(205)

Community Radio, seeks to restore hope, peace and development in the North-West Tanzania.

Baada ya janga kutokea, sekunde za mwanzo huokoa maisha 😇Je, unajua unaweza kuwa shujaa hata kabla ya Jeshi la Zimamoto ...
15/10/2025

Baada ya janga kutokea, sekunde za mwanzo huokoa maisha 😇
Je, unajua unaweza kuwa shujaa hata kabla ya Jeshi la Zimamoto kufika? 🚒

Ungana na Asubuhi Njema Alhamisi hii kufahamu mengi zaidi ❤️‍

DODOMA: Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma, imetupilia mbali Shauri la Kikatiba Namba 24027 la mwaka 2025 lili...
15/10/2025

DODOMA: Mahak**a Kuu ya Tanzania, Masjala Kuu Dodoma, imetupilia mbali Shauri la Kikatiba Namba 24027 la mwaka 2025 lililofunguliwa na mwanachama wa Chama cha ACT Wazalendo, Luhaga Mpina, pamoja na chama hicho, wakipinga kuondolewa kwenye orodha ya wagombea wa urais.

Hukumu hiyo imetolewa leo, baada ya Mahak**a kusikiliza hoja za pande zote mbili.

Katika maamuzi yake, Mahak**a imeeleza kuwa haina mamlaka ya kuhoji au kuchunguza jambo lolote linalotekelezwa na Tume Huru ya Uchaguzi (INEC) katika utaratibu wake wa kikatiba na kisheria, bila kuingiliwa na chombo chochote.

Soma zaidi kupitia www.radiokwizera.co.tz

15/10/2025

Habari za kimichezo kupitia Kona ya Kwanza na ya Pili yaani kuanzia ndani ya nchi hadi kimataifa.

MICHEZO: Kiungo wa Barcelona Frenkie De Jong ameongeza mkataba wake na klabu hiyo hadi mwaka 2029.Mholanzi huyo amesaini...
15/10/2025

MICHEZO: Kiungo wa Barcelona Frenkie De Jong ameongeza mkataba wake na klabu hiyo hadi mwaka 2029.

Mholanzi huyo amesaini mkataba huo katika ofisi za klabu akiwa pamoja na Rais Joan Laporta, mkurugenzi wa michezo Decco na na maofisa wengine wa klabu.

Baada ya kusaini mkataba mpya De Jong alisema kuwa amekuwa na furaha kurndelea kubaki Barcelona.

Pia De Jong amempongeza kocha Hans Flick kwa kumwamini na kumtia motisha kuendelea kuboresha kiwango chake.

15/10/2025

Habari kuu usiku wa leo, kitaifa na kimataifa pamoja na Ujumbe kupitia Waza Wazua.

15/10/2025

MSETO LEO: Habari kwa kina jioni ya leo kupitia Mseto Leo katika Furushi.



15/10/2025

Wakenya watamkumbuka Odinga kwa lipi?- Dakika 1 ya Habari | Oct 15, 2025

MULEBA: ‎Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan ameen...
15/10/2025

MULEBA: ‎Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan ameendelea na kampeni leo akiwa Mkoani Kagera huku akihaidi kujenga mradi wa maji kutoka ziwa Victoria wenye thamani ya zaidi ya shilingi bilioni
‎39 ili uwanufaishe wakazi wa Wilaya ya Muleba.

‎Mgombea Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia chama cha Mapinduzi CCM Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema hayo leo hii akiwa katika Uwanja wa Zimbihile Wilayani Muleba.

‎Awali Mgombea Ubunge Jimbo la Muleba Kusini Dkt. Oscar Kikoyo ameomba kutatuliwa kwa changamoto ya umeme kwenye visiwa ambavyo vipo ziwa Victoria kwani wanatumia umeme ambao hauna uhakika.

✍🏾 Shafiru Yusuph- Muleba, Kagera

15/10/2025

MSETO LEO: Ujumbe huu ukufikie wewe mhusika katika jambo hili muhimu.

MICHEZO: Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania TFF imesitisha kwa kufungia Uwanja wa CCM LITI uliopo mkoani Singi...
15/10/2025

MICHEZO: Shirikisho la mpira wa miguu nchini Tanzania TFF imesitisha kwa kufungia Uwanja wa CCM LITI uliopo mkoani Singida na SOKOINE uliopo mkoani Mbeya kwa kushidwa kukidhi vigezo vya shirikisho hilo la soka.

15/10/2025

DURU ZETU ALASIRI: Habari kuu jioni ya leo kitaifa, kimataifa, Ujumbe pitia Waza Wazua, Uchumi na biashara pamoja na na Dondoo za Michezo bila kusahau maoni yako kupitia 0692 573 615.

BURUDANI: Mwanamziki maarufu wa R&B, D' Angelo, ambaye jina lake halisi ni (Michael Eugene Archer) amefariki dunia akiwa...
15/10/2025

BURUDANI: Mwanamziki maarufu wa R&B, D' Angelo, ambaye jina lake halisi ni (Michael Eugene Archer) amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 51 baada ya kupambana kwa mda mrefu na Saratani ya kongosho.

D'Angelo anayefahamika kwa vibao k**a "Brown Sugar" na Untitled (How Does It Feel) alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa muziki wa Neo-soul, akichanganya mitindo ya Gospel, funk na R&B kwa umahiri mkubwa uliomtofautisha na wasanii wengine.

Kupitia album zake maarufu k**a Brown sugar (1995), Voodoo (2000)- iliyompa tuzo ya Grammy na Black Messiah (2014) D'Angelo alibadilisha kabisa sura ya muziki wa kisasa na urithi mkubwa katika tasnia ya muziki duniani.

Katika safari yake ya muziki, alishirikiana na wasanii wenye majina makubwa k**a Jay Z, Erykah Badu, Q-Tip na wasanii wengine akiacha alama isiyofutika katika ulimwengu wa muziki wa R$B.

Address

P. O. Box 154
Ngara

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Kwizera posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Radio Kwizera:

Share