15/10/2025
BURUDANI: Mwanamziki maarufu wa R&B, D' Angelo, ambaye jina lake halisi ni (Michael Eugene Archer) amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 51 baada ya kupambana kwa mda mrefu na Saratani ya kongosho.
D'Angelo anayefahamika kwa vibao k**a "Brown Sugar" na Untitled (How Does It Feel) alikuwa miongoni mwa waanzilishi wa muziki wa Neo-soul, akichanganya mitindo ya Gospel, funk na R&B kwa umahiri mkubwa uliomtofautisha na wasanii wengine.
Kupitia album zake maarufu k**a Brown sugar (1995), Voodoo (2000)- iliyompa tuzo ya Grammy na Black Messiah (2014) D'Angelo alibadilisha kabisa sura ya muziki wa kisasa na urithi mkubwa katika tasnia ya muziki duniani.
Katika safari yake ya muziki, alishirikiana na wasanii wenye majina makubwa k**a Jay Z, Erykah Badu, Q-Tip na wasanii wengine akiacha alama isiyofutika katika ulimwengu wa muziki wa R$B.