06/01/2026
MCHANGO MKUBWA KWA JAMII YA LUDEWA WHATSAPP GROUP WABADILISHA MAISHA GEREZA LA IBIHI NA SHULE YA MAHITAJI MAALUM MUNDINDI, ZAIDI YA MILIONI 3.2 ZACHANGIWA
Kundi la WhatsApp la โWilaya ya Ludewaโ limetumia jumla ya Shilingi Milioni 3.28 kufanikisha sadaka yake ya mwaka 2025, ambapo limekabidhi mabuti ya mvua 160 yenye thamani ya Shilingi Milioni 1.6 kwa wafungwa wa Gereza la Ibihi pamoja na mashine ya kufulia na kukausha nguo yenye thamani ya Shilingi Milioni 1.78 kwa Shule ya Watoto Wenye Ulemavu Mundindi.
Makabidhiano hayo yalifanyika tarehe 5 Januari 2026 kupitia msafara wa wanakikundi, ambapo msaada wa mabuti ya mvua ulikabidhiwa na kupokelewa na Mkuu wa Gereza la Wilaya ya Ludewa la Ibihi kwa niaba ya uongozi na wafungwa, huku uongozi wa Shule ya Mundindi ukipokea mashine hiyo kwa shukrani kubwa.
Kiongozi wa msafara huo, Bw. Vasco Mgimba, alisema kundi hilo limekuwa na utamaduni wa kutoa sadaka kila mwisho wa mwaka, huku michango ikitolewa na wadau mbalimbali kutoka ndani na nje ya Wilaya ya Ludewa. Alitoa wito kwa wadau wengine na makundi ya kijamii kuiga mfano huo kwa kutoa msaada kwa wahitaji mbalimbali ili kuendelea kuleta faraja na kuunga mkono maendeleo ya jamii.
Kwa mwaka 2025, wanakikundi waliamua kugusa makundi mawili muhimu katika jamii โ wafungwa na watoto wenye ulemavu โ wakitambua changamoto wanazokutana nazo na umuhimu wa kuwasaidia. Uwakilishi wa kundi ulihusisha wanachama mbalimbali akiwemo Bi. Christer Nyenza pamoja na wajumbe wengine wakiwemo Ally Ponda Shaula, Damian Kunambi na Wise Mgina.
Uongozi wa Gereza la Ibihi pamoja na ule wa Shule ya Watoto Wenye Ulemavu Mundindi waliwashukuru kwa msaada huo, wakisema utaongeza ufanisi katika mazingira ya huduma na maisha ya walengwa.
Aidha, wanakikundi hao walimshukuru kwa dhati Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Wilaya ya Ludewa, Ndugu Sunday Deogratias, kwa ushirikiano wake mkubwa na mchango wake chanya katika kundi hilo, hatua ambayo imekuwa kichocheo cha umoja, mshik**ano na utekelezaji wa shughuli za kijamii zenye manufaa kwa wananchi.
Hatua hii imeendelea kuthibitisha Kundi la WhatsApp la Wilaya ya Ludewa k**a jukwaa linalochochea mshik**ano, huruma na uwajibikaji wa kijamii zaidi