Kings FM Radio

Kings FM Radio đŸ”»Tunagusa Kila nyanja unayotamani kuisikia👂89.5-Njombe đŸ”»www.kingsfm.co.tz Chaugingi Street:
Njombe, Tanzania. http://tunein.com/radio/Kings-FM-1043-s263641/

Chaguo La Watu: Kings FM Radio Inatangaza Kutoka Njombe Tanzania, Ikiwa Na Lengo La Kuiweka Jamii Katika Level Ya Usawa Katika Burudani, Elimu Na Maadili.

Baadhi ya Vipaumbele vilivyotajwa na Mgombea wa Ubunge Jimbo la Njombe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Deo Mwany...
19/09/2025

Baadhi ya Vipaumbele vilivyotajwa na Mgombea wa Ubunge Jimbo la Njombe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Deo Mwanyika () katika siku tatu za mwanzo za Kampeni za kunadi Sera, Ilani na kuomba kupigiwa kura Oktoba 29, 2025 kupata ridhaa ya kuongoza Wananchi wa jimbo hilo.

KIFANYA JIMBO LA NJOMBE: MHE. DEO MWANYIKA AENDELEA KUNADI ILANI YA CCM 2025/2030 KATIKA KATA YA KIFANYAMgombea Ubunge w...
18/09/2025

KIFANYA JIMBO LA NJOMBE: MHE. DEO MWANYIKA AENDELEA KUNADI ILANI YA CCM 2025/2030 KATIKA KATA YA KIFANYA

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Njombe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Ndugu Deo Mwanyika, ameendelea na mikutano yake ya kampeni kwa kuwaeleza wananchi utekelezaji wa ilani ya uchaguzi na mafanikio yaliyopatikana katika kipindi cha miaka mitano iliyopita. Leo amefanya mikutano katika Kijiji cha Utengule na baadaye Lwangu, ndani ya Kata ya Kifanya.

Akihutubia wananchi wa maeneo hayo, Mwanyika amesema kuwa katika kipindi cha ubunge wake, Kata ya Kifanya imenufaika na fedha nyingi za maendeleo ambazo zimetekeleza miradi ya sekta mbalimbali. Miradi hiyo imejikita kwenye elimu, uboreshaji wa zahanati, miundombinu ya barabara hususan maeneo korofi, pamoja na huduma za umeme vijijini na vitongoji, ambapo zaidi ya shilingi bilioni moja zimewekezwa kwa ajili ya maendeleo ya wananchi.

Aidha, Mwanyika ameahidi kuwa endapo wananchi wa Jimbo la Njombe Mjini watampa ridhaa ya kuendelea kulitumikia taifa kwa muhula wa pili, atahakikisha huduma za kijamii zinaongezwa, kuboreshwa na kuanzishwa miradi mipya ili kuongeza tija kwa wananchi wa Kifanya na maeneo mengine ya jimbo hilo.

“Lengo langu ni kuhakikisha wananchi wa Njombe Mjini wananufaika zaidi na uwepo wa Serikali ya Awamu ya Sita, kupitia miradi ya maendeleo yenye kugusa maisha yao moja kwa moja, hususan katika sekta za elimu, afya, maji na kilimo,” alisema Mwanyika.

Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Mahamoud Hassan Banga amepokea Kompyuta moja (1) aina...
18/09/2025

Kamanda wa Polisi mkoa wa Njombe Kamishna msaidizi wa Polisi (ACP) Mahamoud Hassan Banga amepokea Kompyuta moja (1) aina ya Dell kutoka kwa kampuni Oresco Food Product Co.Ltd kwa ajili ya kutumika katika Ofisi ya dawati Jinsia na Watoto.

Kamanda Banga amemshukuru wakurugenzi wa kampuni kwa kukubali kutoa Kompyuta kwa ajili ya kuliwezesha Jeshi la Polisi kufanya kazi wa weledi na ufanisi.

Kwa upande Wake Meneja Rasilimali watu Devota Msigwa amesema Kompyuta hiyo ni sehemu ya kurejesha katika jamii kile kilichopatikana kutokana na ushirikiano nzuri kati ya Jeshi la Polisi na kampuni hiyo.

✍| Mkoa wa Njombe Wafanya Tathmini ya Utekelezaji wa PJT–MMMAMLeo, Septemba 17, 2025, mkoa wa Njombe umefanya kikao cha...
17/09/2025

✍| Mkoa wa Njombe Wafanya Tathmini ya Utekelezaji wa PJT–MMMAM

Leo, Septemba 17, 2025, mkoa wa Njombe umefanya kikao cha tathmini ya utekelezaji wa Programu Jumuishi ya Taifa ya Malezi, Makuzi na Maendeleo ya Awali ya Mtoto (PJT–MMMAM), ambayo inatekelezwa katika mikoa mbalimbali nchini, ikiwemo Njombe.

Programu hii inalenga kuhakikisha watoto wanapata malezi bora, lishe ya kutosha, na nafasi ya kustawi kwa njia endelevu.

Kikao hicho kimeongozwa na Mkuu wa Wilaya ya Njombe, Mhe. Juma Sweda, kwa niaba ya Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Mhe. Antony Mtaka, na kilihusisha wadau mbalimbali wakiwemo mashirika binafsi, viongozi wa kidini, vyombo vya ulinzi, maafisa lishe, na wataalamu wa afya na ustawi wa jamii.

Lengo kuu la vikao hivi ni kujenga ushirikiano wa pamoja kati ya sekta mbalimbali, wadau, na taasisi, ili kushughulikia changamoto zinazokabili watoto chini ya miaka 8 kwa njia endelevu na yenye matokeo chanya.

Mambo yaliyoangaziwa katika kikao hiki ni pamoja na:
Kupima mafanikio yaliyofikiwa katika malezi, makuzi, na maendeleo ya awali ya mtoto.

·Kutambua changamoto zilizopo na kuandaa mikakati ya pamoja ili kuboresha utekelezaji.

· Kuimarisha mshikamano kati ya Serikali, jamii, na wadau wengine ili kuongeza kasi ya utekelezaji.

Mkuu wa Wilaya, Mhe. Juma Sweda, ameagiza halmashauri zote kutenga bajeti kwa ajili ya utekelezaji wa afua mbalimbali kwenye maeneo yao, ikiwa ni pamoja na suala la lishe, pamoja na mikakati madhubuti ya kulea watoto kwa ustawi wao.

Shirika la Uwodo, linalotekeleza mradi wa “Mtoto Kwanza” katika Mkoa wa Njombe, kupitia kwa mkurugenzi wake Hamisi Kasapa limehimiza wazazi kutenga muda wa kuzungumza na watoto wao pindi wanapokuwa nyumbani, ili kujua maendeleo yao katika afya, lishe, elimu, na malezi jumuishi.

Afisa Ustawi wa Jamii wa Mkoa wa Njombe, Bi. Subilaga Mwaigisya, pia amesisitiza umuhimu wa vituo vya kulelea watoto kutengeneza mazingira rafiki kwa ajili ya watoto kucheza na kujifunza, ili kusaidia ukuaji wa ubongo wa mtoto na kuendeleza uwezo wao wa kijifunza.

17/09/2025

TUCHAGUENI TUTAENDELEA KUBORESHA MIUNDOMBINU YA ELIMU NA AFYA___________

Deo Mwanyika, Mgombea Ubunge wa Jimbo la Njombe Mjini kupitia CCM akinadi sera kwa Wananchi wa kijiji cha Utalingolo na Mfereke.

17/09/2025

Ikiwa ni siku moja imepita Tangu Mchezo wa Derby ya Kariakoo upigwe na Kushuhudia Yanga wakipata ushindi wa bao 1-0, mashabiki mbalimbali wa Yanga Njombe mjini wameonekana kufurahishwa na Wao kuendelea kupata ushindi katika michezo 6 mfululizo.

Wakati huohuo kwa upande wa mashabiki wa Simba baadhi yao wameonekana kutoridhishwa na maamuzi ya Bao hilo huku baadhi yao wakikubali ubora walionao Yanga.

17/09/2025

Mgombea Ubunge Jimbo la Njombe kupitia Chama cha Mapinduzi (CCM) Deo Mwanyika ameomba Wananchi wa kijiji cha Mfereke kumpigia kura Oktoba 29, 2025 ili akaendelee pale alipoishia katika kuhakikisha Wananchi wanapata nishati ya Umeme hasa katika vijiji.

Mwanyika amesema katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2025/30 kipaumbele ni kupeleka umeme katika Vitongoji na baada ya kuchaguliwa atafanya kazi hiyo kuhakikisha mpaka 2030 vitongoji vya kata 10 za Njombe vinapata Umeme.

Ikumbukwe katika Ilani ya 2020/25 Vijiji 21 ambavyo havikuwa na Umeme vilifikishiwa Umeme na sasa ombi la Wananchi ni Umeme katika Vitongoji.

17/09/2025

đŸ“č| Mgombea Ubunge wa Jimbo la Njombe Mjini kupitia CCM Deo Mwanyika () leo Septemba 17, 2025 ameendelea kunadi sera na vipaumbele katika Ilani ya Uchaguzi ya CCM Jimbo la Njombe Mjini katika kijiji cha Utalingolo na Mfereke.

Asante Utalingolo, naamini mtanipigia kura Oktoba 29, 2025________Deo Mwanyika (), Mgombea Ubuge Jimbo la Njombe Mjini. ...
17/09/2025

Asante Utalingolo, naamini mtanipigia kura Oktoba 29, 2025________

Deo Mwanyika (), Mgombea Ubuge Jimbo la Njombe Mjini.

Mgombea Ubunge Jimbo la Njombe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Deo Mwanyika () leo Septemba 17,2025 atanadi Sera...
17/09/2025

Mgombea Ubunge Jimbo la Njombe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Deo Mwanyika () leo Septemba 17,2025 atanadi Sera, Ilani ya Uchaguzi ya CCM 2025/30 na kuomba kura kwa Wananchi wa kijiji cha Utalingolo na Mfereke.

16/09/2025

Mgombea Ubunge wa Jimbo la Njombe Mjini kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM) Deo Mwanyika amewaomba Wananchi wa kijiji cha Madobole na Luponde kumchagua tena ili amalizie kazi alizozianza katika kipindi kilichopita.

Mwanyika amesema hayo wakati wa Mkutano wa Kampeni katika vijiji hivyo leo Septemba 16, 2025 na kuongeza kuwa siku hiyo Wananchi wajitokeze kwa wingi kuwapigia kura Wagombea wa CCM ambao ni Mgombea Urais Dkt. Samia Suluhu Hassan, Mgombea Ubunge (Deo Mwanyika) na Madiwani wa kata 13 za Jimbo hilo.

Pia ametaja baadhi ya kazi na vipaumbele pindi atakapochaguliwa na Wananchi ambavyo ni

1. Kuhakikisha ujenzi wa barabara ya Itoni-Lusitu KM. 56 unakamilika.

2. ⁠Kuhakikisha Umeme unafika ngazi ya Vitongoji baada ya kufika Vijiji vyote vya Jimbo hilo.

3. ⁠Kukamilisha mradi wa Maji Igongwi.

4. ⁠Kuwasemea Wakulima ikiwemo la Chai na Soko la Uhakika.

5. ⁠Kumalizia na kuanzisha miradi mipya ya Afya na Elimu.

6. ⁠Ujenzi wa Barabara katika maeneo ya uzalishaji wa mazao mbalimbali katika jimbo hilo.

FT : Yanga SC 1 Vs 0 Simba SC
16/09/2025

FT : Yanga SC 1 Vs 0 Simba SC

Address

Magereza Road, Chaugingi Street
Njombe

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kings FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kings FM Radio:

Share

Category