Kings FM Radio

Kings FM Radio 🔻Tunagusa Kila nyanja unayotamani kuisikia👂89.5-Njombe 🔻www.kingsfm.co.tz Chaugingi Street:
Njombe, Tanzania. http://tunein.com/radio/Kings-FM-1043-s263641/

Chaguo La Watu: Kings FM Radio Inatangaza Kutoka Njombe Tanzania, Ikiwa Na Lengo La Kuiweka Jamii Katika Level Ya Usawa Katika Burudani, Elimu Na Maadili.

10/05/2026

LIGANGA NA MCHUCHUMA KUONGEZA MEGAWATI 600 ZA UMEME ____

Ni Taarifa ya msemaji mkuu wa serikali Gerson Msigwa akitoa Taarifa ya serikali akiwa mkoani Njombe amezungumzia mchango wa mradi wa Liganga na mchuchuma utakapoanza kitekelezwa ndani ya miezi mitatu ijayo.

Msigwa amesema mradi huo utachangia uzalishaji wa umeme wa megawati 600 kutoka Liganga na mchuchuma.

Timu ya mpira wa miguu ya Manungu FC, iliyopo Njombe Mjini, leo Mei 10, 2026, imetembelea na kufanya matendo ya huruma k...
10/05/2026

Timu ya mpira wa miguu ya Manungu FC, iliyopo Njombe Mjini, leo Mei 10, 2026, imetembelea na kufanya matendo ya huruma kwa watoto wanaolelewa katika kituo cha Compassion Foundation kilichopo mtaa wa Kambarage, Njombe Mjini.

Timu hiyo, iliyokuwa imeambatana na viongozi wake, imetoa msaada wa mahitaji mbalimbali ikiwemo sabuni, unga, sukari, miswaki, mikate pamoja na fedha taslimu.

Baada ya kukabidhi msaada huo, Mwenyekiti wa timu hiyo, Kai Mligo (Mr Kings), amesema kuwa hatua hiyo ni sehemu ya kuendeleza matendo ya huruma, akisisitiza umuhimu wa wachezaji kuwa na maisha yenye maana hata nje ya mpira.

Kwa upande wake, Mkurugenzi wa kituo hicho, Siter Lucy Mlowe, amesema amepata faraja kubwa kuona vijana wamejitokeza kuwajali watoto hao.

Ameongeza kuwa kitendo hicho ni sehemu ya kujenga hazina njema kwa maisha yao ya baadaye.

10/05/2026

UKUBWA WA MIPANGO YAKO UTAAMUA UKUBWA WA MAISHA YAKO YA BAADAYE _______________

Anthony Mtaka
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Amesema hayo leo Mei 10, 2026 wakati akifunga Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini.

10/05/2026

NJOMBE UMEONA BARIDI TU, HAUJAONA FURSA? _______________

Anthony Mtaka
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Amesema hayo leo Mei 10, 2026 wakati akifunga Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini.

10/05/2026

WATU WA NJOMBE NDIO WAHINDI WA KITANZANIA _______________

Anthony Mtaka
Mkuu wa Mkoa wa Njombe Amesema hayo leo Mei 10, 2026 wakati akifunga Kikao Kazi cha 21 cha Maafisa Habari, Mawasiliano, Itifaki na Uhusiano Serikalini.

10/05/2026

TUMEANZA KUPATA MAHUBIRI CHONGANISHI __________

Anthony Mtaka
Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Amesema hayo wakati wa ufunguzi wa Kambi ya Afya ya Bure 2026 inayotolewa na Wataalamu na wajasiriamali Waadventista Wasabato (ATAPE).

📸| Matukio katika Picha Usiku wa GFA Fashion 2026 uliofanyika usiku wa kuamkia leo Mei 09, 2026 Ukumbi RC Igwachanya - N...
09/05/2026

📸| Matukio katika Picha Usiku wa GFA Fashion 2026 uliofanyika usiku wa kuamkia leo Mei 09, 2026 Ukumbi RC Igwachanya - Njombe .

📸| Wahitimu wa Mafunzo ya Ubunifu na Ushonaji wa Nguo kutoka G - Mas Fashion Designers wakionyesha mitindo mbalimbali ya...
09/05/2026

📸| Wahitimu wa Mafunzo ya Ubunifu na Ushonaji wa Nguo kutoka G - Mas Fashion Designers wakionyesha mitindo mbalimbali ya Mavazi kwenye Usiku wa GFA Fashion 2026 usiku wa kuamkia leo Mei 09, 2026 katika Ukumbi wa RC Igwachanya.

📸| Mshindi wa Pili Miss World Tanzania Southern Highlands Zone na Mshiriki wa Miss World Tanzania 2026 Aneth Mwakyusa ()...
09/05/2026

📸| Mshindi wa Pili Miss World Tanzania Southern Highlands Zone na Mshiriki wa Miss World Tanzania 2026 Aneth Mwakyusa () ni miongoni mwa Walioshiriki Usiku wa GFA Fashion 2026 usiku wa kuamkia leo katika Ukumbi wa RC Igwachanya - Njombe.

Shirika la umeme Tanzania  Mkoa wa Njombe limetangaza kusitisha huduma ya umeme kwa muda katika baadhi ya maeneo ya mkoa...
08/05/2026

Shirika la umeme Tanzania Mkoa wa Njombe limetangaza kusitisha huduma ya umeme kwa muda katika baadhi ya maeneo ya mkoa wa Njombe kutokana na kazi za matengenezo kinga na maboresho katika kituo cha kupoza umeme cha Makambako (Substation).

Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na shirika hilo, zoezi hilo litafanyika kesho Mei 09, 2026 kuanzia saa 3:00 asubuhi hadi saa 10:00 jioni.

TANESCO imesema kuwa lengo la matengenezo hayo ni kuboresha hali ya upatikanaji wa umeme pamoja na kuongeza ufanisi wa huduma kwa wateja wake.

Maeneo yatakayokumbwa na ukosefu wa huduma ya umeme ni pamoja na Wilaya ya Njombe, Wilaya ya Makete, Wilaya ya Wanging’ombe pamoja na Wilaya ya Makambako.

Aidha, TANESCO imewaomba wananchi na wateja wake kuwa na uvumilivu katika kipindi chote cha matengenezo huku ikiahidi kuendelea kuboresha huduma hiyo muhimu kwa maendeleo ya wananchi na shughuli za kiuchumi.

08/05/2026

TUICO TUNAMJALI MFANYAKAZI KWA HALI ZOTE _______

Wakili Noel Nchimbi
Mkuu wa Idara ya Sheria - TUICO

Address

Magereza Road, Chaugingi Street
Njombe

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kings FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category