Kings FM Radio

Kings FM Radio 🔻Tunagusa Kila nyanja unayotamani kuisikia👂89.5-Njombe 🔻www.kingsfm.co.tz Chaugingi Street:
Njombe, Tanzania. http://tunein.com/radio/Kings-FM-1043-s263641/
(1)

Chaguo La Watu: Kings FM Radio Inatangaza Kutoka Njombe Tanzania, Ikiwa Na Lengo La Kuiweka Jamii Katika Level Ya Usawa Katika Burudani, Elimu Na Maadili.

📸| Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi Deo Mwanyika (MB) alipotembelea Ma...
09/08/2026

📸| Mwenyekiti wa Kamati ya Kudumu ya Bunge Viwanda, Biashara, Kilimo, Mifugo na Uvuvi Deo Mwanyika (MB) alipotembelea Mabanda mbalimbali katika Maonesho ya Wakulima Nanenane viwanja vya Dkt. John Malechela Nzuguni Dodoma .

Sherehe za Kilele cha Maadhimisho ya Siku ya Wakulima Nanenane zimefanyika Agosti 08, 2026 katika viwanja hivyo ambapo Mgeni Rasmi alikuwa ni Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan.

Wataalamu mtuambie hii alamainaamana gani?
09/08/2026

Wataalamu mtuambie hii alama
inaamana gani?

Msimu Mpya wa Mashindano ya Deo Mwanyika Cup unafunguliwa rasmi leo hii kwa mechi ya ufunguzi kupigwa katika Tarafa ya I...
09/08/2026

Msimu Mpya wa Mashindano ya Deo Mwanyika Cup unafunguliwa rasmi leo hii kwa mechi ya ufunguzi kupigwa katika Tarafa ya Igominyi ambapo Kifanya wataivaa Uwemba katika Uwanja wa Yakobi Majira ya saa 10:00 Jioni.

Mashindano haya yaliyofanyiwa maboresho makubwa ikiwepo ongezeko la zawadi kwa mabingwa, yanatarajia kufikia tamati Disemba 24 ambapo itapigwa fainali ya Kumpata Bingwa wa Jimbo kati ya Tarafa ya Igominyi na Tarafa ya Njombe Mjini.

Kwa msimu huu wadau mbalimbali wamejitokeza kuunga mkono mashindano ambao ni .tanzania


08/08/2026

Mwenyekiti wa Halmashauri ya Mji Njombe, Erasto Mpete amesema Parachichi ni zao lenye tija ambapo Mkulima anaweza kupata zaidi ya TSH. Milioni 5 akiwa na Miti 10.

Mpete amesema hayo alipotembelea
Mabanda ya Halmashauri ya Mji Njombe
kwenye Maonesho ya Wakulima Nanenane Kanda ya Nyanda za Juu Kusini - Mbeya
akiongoza na Madiwani na kuongeza kuwa kwa sasa Mtu wa Njombe kuwa Maskini ni
kujitakia mwenyewe.

Ameongeza kuwa ni muhimu Madiwani na
Wataalamu kuendelea kuhamasisha Wakulima kufanya kilimo cha kisasa ili kuongeza ubora
wa Parachichi na tija.

06/08/2026

Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika amesema mgao wa Maji katika Mji wa Njombe umaanza kupungua baada ya miradi miwili ya maji kukamilika ambayo ni Mradi wa Lugenge na Mradi wa Ijunilo.

Ameongeza kuwa matarajio ni kumaliza changamoto ya Maji katika Mji huo baada ya Mradi wa Miji 28 unaojengwa katika Mto wa Hagafilo eneo la Lunyanywi wenye thamani ya TSH. Bilioni 41.

Mwanyika amesema hayo wakati akizungumza na Wakazi wa Mtaa wa SIDO kata ya Njombe Mjini kwenye Mkutano ulioambatana na zoezi la kukabidhi Madawati 40 kwenye Shule ya Msingi Mabatini yaliyopatikana kupitia michango ya Wadau wa Chama cha Mapinduzi (CCM) kata ya Njombe Mjini.

06/08/2026

Wanachama wa Kikundi cha Juakali kinacho jihusisha na kuponda Mawe kuwa Kokoto wamemuomba Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika kuwajengea Banda lenye ubora litakalo wasaidia kipindi cha Mvua wakidai banda lililopo sasa halina Ubora.

Wametoa Ombi hilo wakati wa Hafla ya Kukabidhi Madawati 40 yaliyotengenezwa kwa fedha za Wadau wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) katika Shule ya Msingi Mabatini iliyopo Mtaa wa SIDO.

Kwa upande wa Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika amesema aliposikia kuna Mbunge mwingine amejenga Banda alijua changamoto hiyo imeshatatuliwa, kwa kuwa bado halikidhi mahitaji ya Wananchi ameahidi kujenga Banda lingine lenye Ubora katika eneo hilo.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kipimo kikuu cha viongozi Afrika si idadi ya ma...
05/08/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan amesema kipimo kikuu cha viongozi Afrika si idadi ya matamko yanayotolewa, bali ni uwezo wa kuleta matokeo yanayoboresha maisha ya wananchi kupitia utekelezaji wa miradi ya maendeleo na uwekezaji wenye tija.

Akizungumza leo Agosti 5, 2026 katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50 na Jukwaa la Miundombinu kwa Afrika uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam, Samia amesema Afrika sasa inapaswa kuelekeza nguvu katika utekelezaji wa maono yake ya maendeleo ili wananchi waone mabadiliko halisi.

Amesema Afrika haijawahi kukosa maono ya maendeleo, akitaja mipango mbalimbali ikiwemo Ajenda 2063 ya Umoja wa Afrika, Eneo Huru la Biashara Afrika (AfCFTA) pamoja na mipango ya maendeleo ya kitaifa ambayo imeweka malengo makubwa ya kuleta mabadiliko ya kijamii na kiuchumi.

“Hakuna ubishi kwamba wananchi wetu wanapima maendeleo si kwa matamko tunayoyatoa, bali kwa matokeo yanayoonekana k**a vile barabara, nishati ya uhakika, bandari zenye ufanisi, reli, muunganiko wa kidijitali na miundombinu inayotengeneza ajira, kuvutia uwekezaji na kuboresha maisha,” amesema.

Akizungumzia Tanzania kuwa mwenyeji wa mkutano huo, amesema ni kutokana na kuongezeka kwa imani katika mageuzi yake ya kiuchumi, uwezo wa uwekezaji na nafasi yake ya kimkakati k**a lango linalounganisha masoko ya Afrika.

“Mkutano huu unaimarisha imani kwamba mustakabali wa Afrika utaongozwa na uongozi wa Waafrika, mitaji ya Afrika na ushirikiano wa Afrika,” amesema mkuu huyo wa nchi.

05/08/2026

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, amewaalika wageni kutoka mataifa mbalimbali kutembelea Tanzania ili kujionea utajiri wa vivutio vya utalii, urithi wa utamaduni pamoja na fursa mbalimbali za uwekezaji zilizopo nchini.

Akizungumza leo Agosti 5, 2026 katika ufunguzi wa Mkutano Mkuu wa Wanahisa wa Africa50 na Jukwaa la Miundombinu kwa Afrika uliofanyika katika Ukumbi wa Kimataifa wa Mikutano wa Julius Nyerere (JNICC), jijini Dar es Salaam, Samia amesema Tanzania ina nafasi kubwa katika sekta ya utalii na uwekezaji kutokana na rasilimali zake za asili, mazingira rafiki ya biashara na utamaduni wake wa kipekee.

“Ninawaalika mje muione Tanzania. Mjionee ukarimu wa watu wetu, utajiri wa utamaduni wetu na uzuri wa nchi yetu. Kuanzia tambarare za Serengeti, Mlima Kilimanjaro hadi visiwa vya kuvutia vya Zanzibar, Tanzania inatoa uzoefu wa kipekee wa utalii na fursa nyingi za uwekezaji,” amesema Rais Dkt. Samia.

Amesema Serikali itaendelea kuboresha mazingira ya biashara na uwekezaji kwa kuweka mikakati itakayowezesha kuvutia wawekezaji zaidi, kukuza uchumi na kuimarisha nafasi ya Tanzania k**a eneo lenye fursa mbalimbali za maendeleo.

Pia Rais Dkt. Samia amesisitiza kuwa Tanzania ipo tayari kushirikiana na wawekezaji na wadau wa kimataifa kutumia fursa zilizopo katika sekta mbalimbali kwa ajili ya kukuza uchumi na kuleta manufaa kwa wananchi.

05/08/2026

Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika leo Agosti 04, 2026 ametembelea na kupokea taarifa ya Utekelezaji wa Mradi wa Ujenzi wa Daraja na Barabara kiwango cha Lami Kibena-NBC.

Mradi huo wenye thamani ya TSH. Bilioni 6.6 unatajwa kuwa sehemu ya uboreshaji wa taswira ya Mji wa Njombe kwenye miundombinu ya barabara.

05/08/2026

Mkazi mmoja wa Mtaa wa Mgodechi aliyejitambulisha kwa jina la Bakari Kilamlya amependekeza serikali kuweka mpango wa Matibabu bure ili kupunguza gharama kwa Wananchi wanapofika bospitali kutibiwa.

Kilamlya amesema hayo wakati Mkutano wa Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika na kuongeza kuwa badala ya serikali kuweka elimu bure iweke matibabu bure.

Akitoa ufafanuzi Mwakilishi wa Mganga Mfawidhi wa Hospitali ya Rufaa mkoa wa Njombe Dkt. Rasuli Chihako amesema bei za matibabu zinatofautiana kutokana na Hospitali, ambapo Zahanati, Kituo cha Afya na Hospitali za Rufaa haziwezi kufanana.

Kwa upande wa Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini Deo Mwanyika amesema katika kupunguza gharama ya Matibabu serikali tayari imeanzisha mpango wa Bima kwa Afya kwa wote.

Address

Magereza Road, Chaugingi Street
Njombe

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kings FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Shortcuts

Share

Category