Kings FM Radio

Kings FM Radio 🔻Tunagusa Kila nyanja unayotamani kuisikia👂89.5-Njombe 🔻www.kingsfm.co.tz Chaugingi Street:
Njombe, Tanzania. http://tunein.com/radio/Kings-FM-1043-s263641/

Chaguo La Watu: Kings FM Radio Inatangaza Kutoka Njombe Tanzania, Ikiwa Na Lengo La Kuiweka Jamii Katika Level Ya Usawa Katika Burudani, Elimu Na Maadili.

17/12/2025

Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Njombe imetoa pongezi za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Rais wa Zanzibar, kufuatia ushindi mkubwa na wa kishindo walioupata.

Pongezi hizo zimetolewa kupitia kikao cha kikanuni cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Njombe kilichofanyika leo Disemba 17, 2025.

Akitoa tamko hilo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Njombe, Justine Nusulupila, amesema ushindi huo ni ushahidi wa imani kubwa waliyonayo wananchi kwa uongozi wa Chama Cha Mapinduzi na viongozi wake katika kuwaletea maendeleo.

17/12/2025

Zaidi ya vijana 160 wanaojishughulisha na kilimo katika Wilaya ya Makete Mkoani Njombe wamepewa mbolea bure na serikali Wilayani humo ili kuwapunguzia mzigo katika msimu huu wa kilimo.

Anilea Sanga na Yusuph Tweve ni miongoni mwa vijana wilayani humo waliofanikia kukabidhiwa mbole ambao wanasema walifikisha ombi la kusaidiwa mbolea kwa Mkuu wa wilaya hiyo Kissa Kasongwa kutokana na changamoto ya upatikanaji kwenye maeneo yao ya kilimo.

Akizungumza baada ya kukabidhi Mbolea DC Kissa amesema alipokutana na baadhi ya vijana walitoa ombi hilo ambapo kwa kushirikiana na baadhi ya wadau wa kilimo wakiwemo wafanyabiashara wa pembejeo,TFC pamoja na TFRA wameweza kuanza na vijana 160 kati ya walengwa zaidi ya 1500 ambapo Mbolea mifuko 290 yenye thamani ya zaidi ya Milioni ishirini na moja ikitolewa kwa vijana hao.

"Vijana waliniambia tunahitaji kusukumwa kidogo lakini tunachokosa ni mbolea kwa hiyo ninaamini shughuli ya leo inaenda kuacha tabasamu kwa vijana, na ambao kweli watachukua mbolea hii na kwenda kupeleka kwenye kilimo tunaamini mwakani tutakuwa tunaongea mengine"amesema DC Kissa.

16/12/2025

Mbunge wa Jimbo la Njombe Mjini, Deo Mwanyika, kupitia mwakilishi wake Emanuel Kayombo amekabidhi mipira miwili ya miguu kwa Mwenyekiti wa Yard ya Maroli iliyopo Mtaa wa Sido, mjini Njombe.

Makabidhiano hayo yamefanyika ikiwa ni utekelezaji wa ahadi ya Mbunge Mwanyika aliyotoa wakati wa kipindi cha kampeni, ambapo lengo ni kuhamasisha michezo, kuimarisha afya na kuendeleza mshik**ano miongoni mwa vijana pamoja na wadau wa sekta ya usafirishaji katika eneo hilo.

Akizungumza baada ya kupokea mipira hiyo, Mwenyekiti wa Yard ya Maroli, Peregrine Emanuel, ameishukuru Ofisi ya Mbunge kwa kutimiza ahadi yake na kuonyesha kujali michezo k**a sehemu muhimu ya ustawi wa jamii.

Kwa upande wake, dereva Exavery Mwabena amesema anamshukuru Mbunge Mwanyika kwa kutimiza ahadi hiyo, akieleza kuwa michezo ya mpira wa miguu itasaidia kuboresha afya za madereva. Amesema mara nyingi baada ya safari ndefu mwili hususan mgongo huuma, lakini kushiriki michezo husaidia kuuweka mwili katika hali nzuri na kusaidia kuepuka magonjwa.

16/12/2025

Naibu Waziri wa Maji Mhandisi Kundo Mathew ameagiza mkandarasi anayejenga mradi wa maji wa miji 28 mkoani Njombe kuhakikisha mpaka ifikapo Mei 2026 mradi huo uwe umekamilika ili wananchi wa mkoa huo waweze kupata maji ya uhakika.

Kundo ametoa agizo hilo leo December 15 kwa kampuni ya L&T inayotekeleza mradi huo baada ya kukagua maendeleo ya ujenzi ambapo amesema mradi huo ulipaswa kukamilika October 10,2025 lakini mkandarasi aliongezewa muda kutokana na sababu mbalimbali na hivyo hakuna sababu nyingine ya kuchelewesha mradi.

"Tumewapa maelekezo mpaka ifikapo tarehe moja mwezi wa tano 2026 mradi uwe umekamilika na uanze kutoa maji na wananchi waweze kufurahia huduma ya maji safi na salama" amesema Mhandisi Kundo Mathew

Amesema mradi wa miji 28 Njombe unaotekelezwa kwenye maeneo matatu ya Makambako,Njombe Mjini na Wanging'ombe wenye thamani ya zaidi ya Bilioni 125 utakuwa mkombozi wa huduma za maji kwenye ukanda wa Njombe.

Vibe la Wafalme katika kufungua rasmi msimu wa Mazaga ya Kifalme 2025.
15/12/2025

Vibe la Wafalme katika kufungua rasmi msimu wa Mazaga ya Kifalme 2025.

15/12/2025

VITU VILIVYOMO KWENYE KAPU LA MAZAGA YA KIFALME ______________

🎤 | |

15/12/2025

Mbunge wa viti Maalum Mkoa wa Njombe (CHAUMMA) Sigrada Mligo amewatahadharisha watendaji hususani watu wa mapato na kuwataka kutenda haki huku akidai kuwa watu wanaolipa faini zisizo halali hulipa wakiwa na vinyongo jambo ambalo linaweza kuwaletea shida watendaji.

Sigrada ameeleza hayo jana Desember 12 wakati akizungumza mambo mbalimbali juu ya maendeleo ya mkoa wa Njombe katika kikao kazi cha mkuu wa mkoa wa Njombe Anthony Mtaka pamoja na madiwani,CMT na viongozi wote wa taasisi na sekta binafsi za mkoa huo.

"Niliwahi kuwa mfanyabiashara wa mbao na mkaa,faini zilizopo barabarani zinatia hasira,kuna muda mfanyabiashara anaweza akatoa faini ukahisi umemuweza kesho na kesho kutwa unapata matatizo ya kifamilia kumbe Mfanyabiashara alitoa kwa hasira faini halafu mbele alikuwa anawaza hivi yule mganga alikufa yule,tutende haki ushirikina upo"amesema Sigrada

Aidha amesema halmashauri zinapaswa kutunga sheria rafiki ikiwemo kulipa faini ndogo zinazolipika ili wanaok**atwa na makosa kuzilipa haraka na halmashauri kujipatia fedha kuliko faini kubwa zisizo lipika na kupelekea wasimamizi wa mapato kupokea rushwa.

15/12/2025


akapita na Challenge kwa staff na swali likiwa Jimbo la Njombe Mjini linaundwa na Tarafa ngapi, Kata ngapi, Vijiji vingapi, Vitongoji vingapi na Mitaa mingapi.

Cc | | | |
|

Tuambie pia hapo chini kwenye comment.

15/12/2025

Tucheke kidogo kwanza 😂😂😂

15/12/2025
15/12/2025

MAZAGA YA KIFALME YAMEZINDULIWA RASMI HAPA UFALMENI _______________

🎤 | |

Address

Magereza Road, Chaugingi Street
Njombe

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Kings FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Kings FM Radio:

Share

Category