17/12/2025
Halmashauri Kuu ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Njombe imetoa pongezi za dhati kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, pamoja na Rais wa Zanzibar, kufuatia ushindi mkubwa na wa kishindo walioupata.
Pongezi hizo zimetolewa kupitia kikao cha kikanuni cha Halmashauri Kuu ya CCM Wilaya ya Njombe kilichofanyika leo Disemba 17, 2025.
Akitoa tamko hilo, Mwenyekiti wa CCM Wilaya ya Njombe, Justine Nusulupila, amesema ushindi huo ni ushahidi wa imani kubwa waliyonayo wananchi kwa uongozi wa Chama Cha Mapinduzi na viongozi wake katika kuwaletea maendeleo.