Ufunuo TV

Ufunuo TV TV maalumu kwa Neno la Mungu kwa Watu wote Ulimwenguni

07/07/2024

Bwana Yesu apewe Sifa.

Karibuni Wana wa Ufalme.

Send a message to learn more

Bwana Yesu asifiwe Wapendwa. Kwasasa mutapata mafundisho Kila siku ya neno la MUNGU, kutoka kwa Mwalimu wa Neno la MUNGU...
07/07/2024

Bwana Yesu asifiwe Wapendwa.

Kwasasa mutapata mafundisho Kila siku ya neno la MUNGU, kutoka kwa Mwalimu wa Neno la MUNGU Mwl. "FIDELIS TEGEMEO JOHN"

Swali la Leo linajibiwa hivi, si kweli kwamba Wana wa Esrael hawakuwaoa Waafrica.

1. Yusufu mwana wa yakobo alioa mmisiri akiwa kwa farao.

2. Ibrahimu babu wa Imani alizaa na Hajri mjakazi wa sara. Hajri alikuwa anatoka misiri.

3. Suremani alizaa na malikia wa sheba. Leo hii sheba ni nchi ya Ethiopia.

4. Musa. Mke wa pili wa Musa alikuwa Mwafrica kutoka Kushi. Kushi Leo hii ni nchi ya Sudani. Tena baada ya kumuoa mtu mweusi kutoka Kushi, Miliamu akaanza kueneza uongo Musa amepotoka kuoa mtu mweusi, lakini maneno hayo MUNGU alikasirika na kumpiga ukoma Miliamu.

HESABU 12:1-15.

1 Kisha Miriamu na Haruni wakamnenea Musa kwa sababu ya mwanamke Mkushi aliyekuwa amemwoa; maana, alikuwa amemwoa mwanamke Mkushi.

2 Wakasema, Je! Ni kweli Bwana amenena na Musa tu? Hakunena na sisi pia? Bwana akasikia maneno yao.

3 Basi huyo mtu, huyo Musa, alikuwa mpole sana zaidi ya wanadamu wote waliokuwa juu ya uso wa nchi.

4 Bwana akanena ghafula na Musa, na Haruni na Miriamu, na kuwaambia, Tokeni nje ninyi watatu, mwende hemani mwa kukutania. Basi hao watatu wakatoka nje.

5 Bwana akashuka katika nguzo ya wingu akasimama pale mlangoni pa Hema, akawaita Haruni na Miriamu, nao wakatoka nje wote wawili.

6 Kisha akawaambia,Sikizeni basi maneno yangu;Akiwapo nabii kati yenu,Mimi,Bwana,nitajifunua kwake katika maono,Nitasema naye katika ndoto.

7 Sivyo ilivyo kwa mtumishi wangu, Musa; Yeye ni mwaminifu katika nyumba yangu yote;

8 Kwake nitanena mdomo kwa mdomo, Maana, waziwazi wala si kwa mafumbo; Na umbo la Bwana yeye ataliona. Mbona basi ninyi hamkuogopa Kumnenea mtumishi wangu, huyo Musa?

9 Hasira za Bwana zikawaka juu yao; naye akaenda zake.

10 Kisha hilo wingu likaondoka kutoka pale juu ya hema; na tazama, Miriamu akawa mwenye ukoma, mweupe k**a theluji; Haruni akamwangalia Miriamu, na tazama, yu mwenye ukoma.

11 Kisha Haruni akamwambia Musa, Ee bwana wangu nakusihi sana usituwekee dhambi juu yetu, kwa kuwa tumefanya ya upumbavu, na kufanya dhambi.

12 Nakusihi, asiwe k**a mmoja aliyekufa, ambaye nyama ya mwili wake nusu imelika hapo atokapo tumbo la mama yake.

13 Musa akamlilia Bwana, akasema, Mpoze, Ee Mungu, nakusihi sana.

14 Bwana akamwambia Musa, Je! K**a baba yake angalimtemea mate usoni tu, hangaliona aibu muda wa siku saba? Na afungwe nje ya kambi muda wa siku saba, kisha baada ya hayo ataletwa ndani tena.

15 Basi Miriamu alifungwa nje ya kambi muda wa siku saba; wala watu hawakusafiri hata Miriamu alipoletwa ndani tena.

MUHIMU: Hao ni baadhi tu wapo wengi sana, lakini wayahudi walizaa na waafrica na tena uzao huo ulitoa manabii wakubwa ambao walikuwa chotara waafrica na uyahudi.

Kwa Maswali wasiliana nami.

Simu & Whatsapp: 0785043326.

MUBARIKIWE SANA WANA WA UFALME:

21/12/2021

HAPO MWANZO NDOA YA WAKE WENGI HAIKUWA DHAMBI:

Mwanzo 30:1-13
[1]Naye Raheli alipoona ya kuwa hamzalii Yakobo mwana, Raheli alimwonea ndugu yake wivu. Akamwambia Yakobo, Nipe wana; k**a sivyo, nitakufa mimi.
And when Rachel saw that she bare Jacob no children, Rachel envied her sister; and said unto Jacob, Give me children, or else I die.
[2]Yakobo akamghadhibikia Raheli, akasema, Je! Mimi ni badala ya Mungu, aliyekuzuilia uzao wa mimba?
And Jacob's anger was kindled against Rachel: and he said, Am I in God's stead, who hath withheld from thee the fruit of the womb?
[3]Akasema, Yuko mjakazi wangu, Bilha, uingie kwake ili kwamba azae juu ya magoti yangu, nami nipate uzao kwa yeye.
And she said, Behold my maid Bilhah, go in unto her; and she shall bear upon my knees, that I may also have children by her.
[4]Basi akampa Bilha mjakazi wake kuwa mkewe. Yakobo akaingia kwake.
And she gave him Bilhah her handmaid to wife: and Jacob went in unto her.
[5]Naye Bilha akapata mimba, akamzalia Yakobo mwana.
And Bilhah conceived, and bare Jacob a son.
[6]Raheli akasema, Mungu amenipa haki yangu, naye amesikia sauti yangu, akanipa mwana. Kwa hiyo akamwita jina lake Dani.
And Rachel said, God hath judged me, and hath also heard my voice, and hath given me a son: therefore called she his name Dan.
[7]Bilha, mjakazi wa Raheli, akapata mimba tena, akamzalia Yakobo mwana wa pili.
And Bilhah Rachel's maid conceived again, and bare Jacob a second son.
[8]Raheli akasema, Kwa mashindano makuu nimeshindana na ndugu yangu, nikashinda. Akamwita jina lake Naftali.
And Rachel said, With great wrestlings have I wrestled with my sister, and I have prevailed: and she called his name Naphtali.
[9]Lea alipoona ya kuwa ameacha kuzaa, alimtwaa Zilpa, mjakazi wake, akampa Yakobo kuwa mkewe.
When Leah saw that she had left bearing, she took Zilpah her maid, and gave her Jacob to wife.
[10]Zilpa, mjakazi wa Lea, akamzalia Yakobo mwana.
And Zilpah Leah's maid bare Jacob a son.
[11]Lea akasema, Bahati njema! Akamwita jina lake Gadi.
And Leah

20/12/2021

Yohana 1:34-42
[34]Wanafunzi wa kwanza wa Yesu
[35]Tena siku ya pili yake Yohana alikuwa amesimama pamoja na wawili katika wanafunzi wake.
Again the next day after John stood, and two of his disciples;
[36]Akamtazama Yesu akitembea, akasema, Tazama, Mwana-kondoo wa Mungu!
And looking upon Jesus as he walked, he saith, Behold the Lamb of God!
[37]Wale wanafunzi wawili wakamsikia akinena, wakamfuata Yesu.
And the two disciples heard him speak, and they followed Jesus.
[38]Yesu aligeuka, akawaona wakimfuata, akawaambia, Mnatafuta nini? Wakamwambia, Rabi, (maana yake, Mwalimu), unakaa wapi?
Then Jesus turned, and saw them following, and saith unto them, What seek ye? They said unto him, Rabbi, (which is to say, being interpreted, Master,) where dwellest thou?
[39]Akawaambia, Njoni, nanyi mtaona. Wakaenda, wakaona akaapo, wakakaa kwake siku ile. Nayo ilikuwa yapata saa kumi.
He saith unto them, Come and see. They came and saw where he dwelt, and abode with him that day: for it was about the tenth hour.
[40]Andrea, nduguye Simoni Petro, alikuwa mmoja wa wale wawili waliomsikia Yohana na kumfuata Yesu.
One of the two which heard John speak, and followed him, was Andrew, Simon Peter's brother.
[41]Huyo akamwona kwanza Simoni, ndugu yake mwenyewe, akamwambia, Tumemwona Masihi (maana yake, Kristo).
He first findeth his own brother Simon, and saith unto him, We have found the Messias, which is, being interpreted, the Christ.
[42]Akampeleka kwa Yesu. Naye Yesu akamtazama, akasema, Wewe u Simoni, mwana wa Yohana; nawe utaitwa Kefa (tafsiri yake Petro, au Jiwe).
And he brought him to Jesus. And when Jesus beheld him, he said, Thou art Simon the son of Jona: thou shalt be called Cephas, which is by interpretation, A stone.

09/12/2017

KRISTO NI BWANA NA MWOKOZI WETU:

Kwa maana jinsi hii Mungu aliupenda ulimwengu, hata akamtoa Mwanawe pekee, ili kila mtu amwaminiye asipotee, bali awe na uzima wa milele. Baada ya anguko la mwanadamu katika bustani ya Edeni na adhabu kutolewa na MUNGU mwenyewe kwa Adamu kwa Hawa na kwa Nyoka lakini MUNGU aliendelea kumtafuta mwanadamu ili aendelee kuwa na mahusiano naye, aliwainua, Mitume, Manabii na Wafalme ili kuendelea kurejesha Uhusiano huo na hata kuleta Sheria (Amri) kwa Mkono wa MUSA ili mwanadamu aweze kuwa na Mahusiano mazuri na MUNGU.Ndipo MUNGU BABA alipoamua kumtuma mwana wake wa Pelee Yesu Kristo ili kuleta upatanisho kati ya MUNGU na Mwanadamu kwa njia ya kifo pale msalabani.

Neno la Mungu linasema “kwa sababu wote wamefanya dhambi, na kupungukiwa na utukufu wa Mungu; Warumi 3:23”
Na pia tunatambua kwamba dhambi haijawahi kumuacha MTU salama kwani Maandiko yanasema “Kwa maana mshahara wa dhambi ni mauti; bali karama ya Mungu ni uzima wa milele katika Kristo Yesu Bwana wetu. Warumi 6:23”
MTU anaweza kuona ya kuwa dhambi na nzuri na pengine hata kuifurahia lakini tambua ya kwamba furaha ya dhambi no ya kitambo kidogo tu na mshahara wake ni mauti; Neno la MUNGU linasema kuwa tamaa ikichukua mimba huzaa dhambi na dhambi ikiisha kukomaa huzaa mauti.

Yesu Kristo anakualika kwa kusema “Mimi ndimi njia, na kweli, na uzima; mtu haji kwa Baba, ila kwa njia ya mimi. Yohana 14:6 tambua ya kuwa hatuna namna yoyote ya kupatanishwa na MUNGU ila kwa njia ya Yesu Kristo ni kwa kutubu dhambi zako na kuziacha na kuliamini Jina la Yesu Kristo na ndipo tunapokuwa wana wa MUNGU k**a maandiko yasemavyo “Bali wote waliompokea aliwapa uwezo wa kufanyika watoto wa Mungu, ndio wale waliaminio jina lake; Yohana 1:12

Unachotakiwa ni wewe kutubu na kuacha dhambi kwani ni Yesu tu ndiyo anayesamehe dhambi na ijapokuwa dhambi zako ni nyingi mno nanpengine ni nyekundu k**a damu au k**a bendera Yesu anakusamehe na kukusafisha na zitakuwa nyeupe k**a theruji au k**a sufu. NENO la MUNGU linatuambia kuwa
“ Tukiziungama dhambi zetu, Yeye ni mwaminifu na wa haki hata atuondolee dhambi zetu, na kutusafisha na udhalimu wote.
1 Yohana 1:9”
Yesu Kristo ametuahidi kwamba tunapofungua mioyo yetu na kumpokea yeye kuwa no Bwana na Mwokozi wa maisha yako atakaa kwako.” Tazama, nasimama mlangoni, nabisha; mtu akiisikia sauti yangu, na kuufungua mlango, nitaingia kwake, nami nitakula pamoja naye, na yeye pamoja nami. Ufunuo wa Yohana 3:20”
Neno lake pia lakuhakikishia kuwa ni muhimu ukamkiri Yesu kwa kinywa chako na kumwamini moyoni mwako ya Kuwa Mungu alimfufua kutoka katika wafu ndipo utakpokuwa umeokoka haya tunayasoma katika kitabu cha warumi “ Kwa sababu, ukimkiri Yesu kwa kinywa chako ya kuwa ni Bwana, na kuamini moyoni mwako ya kuwa Mungu alimfufua katika wafu, utaokoka. Kwa maana kwa moyo mtu huamini hata kupata haki, na kwa kinywa hukiri hata kupata wokovu. kwa kuwa, Kila atakayeliitia Jina la Bwana ataokoka. Warumi 10:9, 10, 13”
Pia unapookoka unakuwa ni kiumbe kipya na kwamba yakale yote yanakwisha, dhambi zako zote zinakwisha na unaanza maisha mapya ya ushindi ndani ya YESU KRISTO “Hata imekuwa, mtu akiwa ndani ya Kristo amekuwa kiumbe kipya; ya kale yamepita tazama! Yamekuwa mapya. 2 Wakorintho 5:17”

Kwa maana mmeokolewa kwa neema, kwa njia ya imani; ambayo hiyo haikutokana na nafsi zenu, ni kipawa cha Mungu; wala si kwa matendo, mtu awaye yote asije akajisifu. Waefeso 2:8, 9

WAKATI NDIYO HUU USINGOJE KESHO, MWAMINI YESU SASA, MKIRI YEYE NA UOKOKE

TAFADHALI MSHIRIKISHE NA MWENZAKO

MUNGU AKUBARIKI

Address

Nyegezi

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ufunuo TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share