Swahili Stories

Swahili Stories WHEN ARTISTS GET TO WORK, THEY WILL CHANGE THE WORLD

K**a hujaipata hii kwenye group lako lolote; Jipige kifua mara tatu alafu Sema , nimekosa Mimi nimekosa sana 😂😂😂😂😂 .. We...
02/05/2023

K**a hujaipata hii kwenye group lako lolote; Jipige kifua mara tatu alafu Sema , nimekosa Mimi nimekosa sana 😂😂😂😂😂 ..

We are proud to be part of this love story.
Thank you for choosing to work with us

&Eleno

NA MIMI PIA NI MTOTO WA MUHESHIMIWA MAREHEMUHADITHI YA KUBUNI. : Hii ni hadithi ya kubuni na haina uhusiano wowote na tu...
18/10/2015

NA MIMI PIA NI MTOTO WA MUHESHIMIWA MAREHEMU

HADITHI YA KUBUNI. : Hii ni hadithi ya kubuni na haina uhusiano wowote na tukio lolote linaloendelea. Wito wangu kwa wanasiasa, apandacho mtu ndicho atakachovuna, ukipanda kwa uchawi na dhuluma utavuna LAANA, ila ukipanda kwa HAKI utavuna kwa haki na BARAKA tele. Nawatakia WATANZANIA wenzangu uchaguzi mwema wa haki na amani.
******************************************************************************

Siku kadha zimebaki kabla ya UCHAGUZI mkuu kufanyika na BUNDI wametanda angani wakiimba nyimbo zao za furaha lakini kwa Tafsiri za kibinadamu nyimbo yoyote aimbayo BUNDI ni uchuro na tena BUNDI si ndege wa bahati abaadani, asilani.

Siku hizi habari zinasambaa k**a UKIMWI unavyosambaa kiarahisi kwa kufanya NGONO zembe Na habari za matukio mbali mbali na vifo nazo zina sambaa mpaka zinatisha. Hata sisi WATOTO WA MTAANI tunasikia na kuelewa kila kinacho endelea japo kuwa hakuna mtu anaetuelewa tunavyoendelea na hata mgombea mmoja hajasema chochote juu ya mustakabali wa maisha yetu. Haaaa!!!! mpaka najishangaa mwenyewe WANASIASA watajishuhulishaje na mustakabali wetu WAKATI BAADHI YAO NDIO BABA ZETU na walishatukataa tangu tukiwa TUMBONI?. Jamani eehh! Mimi najitokeza hadharani na kujitambulisha kwenu kuwa NA MIMI PIA NI MTOTO WA MUHESHIMIWA MAREHEMU.

Najua mtashangaa na wengine mtasema NAKUFURU au nilikuwa wapi kipindi chote tangu marehemu akiwa hai. Ni kweli ila pia hamfahamu ni jitihada gani nimefanya kujitambulisha kwake lakini k**a kawaida yao hawezi kukubali asilani kuwa ana mtoto wa nje ya ndoa tena si hilo tu bali mtoto mwenyewe ni CHOKORAA makazi yake ni kwenye mitaro ya maji machafu magomeni.

Nimehudhuria makaburini kwenye mazishi ya marehemu baba yangu mpendwa, nafahamu hakuna hata mmoja anaefahamu au hata kudhania kuwa na mimi ni mmoja kati ya watoto wa marehemu. Machozi na maumivu makali ya moyo nami yamenitanda hasa pale nilipo uona mwili wa marehemu baba ukiingizwa kaburini. Huzuni kubwa zaidi nilipowaona wadogo zangu pamoja na mama mdogo yaani mke wa ndoa wa baba wanavyotambulishwa na kuahidiwa kulindwa na kutunzwa k**a sehemu ya shukrani kwa mchango mkubwa alio utoa marehemu baba kwa TAIFA.

Ndoto yangu ya kuwa siku moja nitamuona baba yangu na kujitambulisha mbele zake ndio imezikwa leo kwa kuwa ni yeye peke yake anae fahamu ukweli juu ya jinsi nilivyopatikana mimi. HAKIKA MWANADAMU NI MAVUMBI NAAM MAVUMBINI TATURUDI. Ukiwa wangu ni mkubwa sana kuliko nnavyoweza kuelezea na hata nikimueleza mtu si rahisi kuniamini. Sina namna ila kwa atakae soma andiko hili anaweza pata japo kwa sehemu ni kwa namna gani kuna waombolezaji wengine tulioko nje tuna maumivu kuliko walioko ndani.

Jamani mimi naitwa SHUKURANI MAKAPUTULA, hili la makaputula sio kuwa ndio la jina la baba yangu la hasha, ni jina nililobatizwa na watoto wenzangu wa mitaani kutokana na nguo zangu nnazovaa.. Amini usiamini ila ukweli wa mungu na mimi ni mtoto wa MAREHEMU muheshimiwa.

Kuna dhana inayosikika chini chini kuwa uchawi unahusika sana katika kushinda nyadhifa mbali mbali za uongozi katika uchaguzi lakini pia uchawi unahusishwa katika vifo hasa kwenye ajali za magari, mauaji ya albino na vifo vya waheshimiwa. Mimi siamini k**a kuna ukweli wowote ila inawezekana ukweli ukawepo. Ila na amini maisha yana sheria zake. Siku zote UKIANZA NA MUNGU BASI UTAMALIZA NA MUNGU ili hali ukitegemea njia zingine basi nako pia kuna mustakabali wake. Najua mtasema nachanganya mada hapa ila nataka niwalete kwenye ukweki wa mambo.

Mwaka 2000 mama yangu mpenzi alikuwa akiendesha maisha yake KATI KATI YA UWANJA WA MAKABURI YA KIZOTA. Kwa wenyeji wa eneo hilo najua mtakua mna mkumbuka mwanamke mmoja aliekuwa na KICHAA anae imba usiku makaburini. Huyo mimi ndio mama yangu alienizaa. Nafahamu mnakumbuka mwaka huo huo ulikuwa mwaka wa uchaguzi k**a sasa na kwa taarifa nilizopewa muheshimiwa nae alikuwa mgombea kipindi hicho.Sijui ilikuaje au alipewa ushauri huo na MGANGA kutoka wapi ila alikwenda KUMUINGILIA MAMA YANGU(KICHAA) KIMWILI USIKU NA KUSHIRIKI NAE TENDO LA NDOA LILIPOLEKEA MIMI KUPATIKANA..

Siku zote za maisha yangu nimekuwa nikiwaza kitendo hicho na kujiuliza maswali mengi sana. Ivi ni kweli muheshimiwa na sifa alizo nazo zote alidiriki kufanya kitu kigumu namna hiyo? Cha kujiuliza zaidi alienda kulala na kichaa akiwa amelewa au ana akili timamu? BAHATI NZURI zaidi alienda na dereva wa gari lake ambaye mpaka leo moyo una msuta na kumuuma na ni yeye ndio alinisimulia habari hii. Kweli WASWAHILI WALISEMA “ukitaka cha mvunguni sharti uiname”. Na nafahamu mpaka kipindi hiki kuna watu wametumwa na WAGANGA kufanya mambo ya ajabu zaidi ya HAYO na wameyashayatekeleza ili tu kupata madaraka.

Masikini mama yangu japo kuwa alikuwa ana kichaa lakini alinizaa, alinilea na kunitunza mpaka mauti ilipomchukua na kunikabidhi rasmi kwa ULIMWENGU ambao umekua ndio mama na baba yangu mpaka sasa. Kwa muda mrefu nilitafuta kuonana na baba yangu ili tu nimueleze kuwa mimi ni matunda ya alicho kifanya kwa yule mwanamke kichaa lakini BAHATI haikua yangu. K**a huko kuzimu aliko ana nafasi ya kusoma andiko hili na asome ili afahamu kuwa NA MIMI PIA NI MTOTO WA MUHESHIMIWA MAREHEMU. .

MTUNZI: AMON TAMILWAI

HADITHI: ETI WEWE NDIYE ULIYE MUUA BABA YANGU?MTUNZI. AMON TAMILWAI 071200781Pilika pilika za uchaguzi mkuu zimeanza na ...
20/05/2015

HADITHI: ETI WEWE NDIYE ULIYE MUUA BABA YANGU?

MTUNZI. AMON TAMILWAI 071200781

Pilika pilika za uchaguzi mkuu zimeanza na kila mwenye nia ya kuwania nafasi yoyote katika uchaguzi mkuu ujao amesha anza kuonyesha cheche zake. Ni ukweli usiopingika kuwa mara nyingi Demokrasia ina tamkwa kwenye majukwaa ya kisiasa lakini kwa uhalisia kuna pilika pilika nyingi sana ambazo haziangalii hilo. Nafahamu watu wengi wana mshawasha sana na uchaguzi huu ujao kutokana na sababu mbali mbali.

Na mimi mwaka huu nimeamua kujitosa kwenye kinyang’anyiro hicho. Nikiwa na sababu kuu tano zinazonipelekea kusonga mbele. Kwanza ni nia yangu ya ndani na ndoto zangu za kuwa kiongozi. Pili ni nia thabiti ya kuwa mtatuzi wa kero sugu za wananchi wa jimboni kwangu. Tatu ni kurudisha tumaini kwa wananchi wajimbo langu ambao kwa kipindi cha miaka 50 sasa tangu uhuru wamekua wakidanganywa na wanasiasa na kutumiwa k**a ngazi. Nne nia yangu ya dhati kabisa ya kutatua mgogoro mkubwa unaowatafuna wananchi wa jimbo langu na unaosababisha vifo vya mamia ya wananchi wasio na hatia kisa tu serikali haija toa ufumbuzi wa dhati juu ya migogoro ya wafugaji na wakulima. Tano na mwisho nimeamua kuingia kwenye kinyang’anyiro hiki ili tu kuwahakikishia watu wa jimbo langu la KIBADA JUU kuwa TUNAWEZA KUFANYA SIASA BILA kusababisha maafa na upotevu wowote wa mali na amani.
********************************************************************************************
Ni kweli kuwa nchi yetu ina amani na ni tamaa yangu kuona kuwa amani inadumu kwa vizazi na vizazi. Ila ni ukweli usiopingika kuwa katika nchi hii kuna watu wanatembea wakiwa na visasi na risasi miyoni mwao juu ya yale ambayo wametendewa wao wenyewe, wazazi wao au ndugu zao wa karibu. UTAMU WA NGOMA MUULIZE MCHEZAJI,na hata maumivu muulize anaye ugua. Sitaki kuwakumbusha visa na mikasa iliyowapata watu hasa kwa kipindi k**a hichi cha uchaguzi ila nataka kuwaambia ukweli kuwa, wale waliofiwa na wazazi wao kwa sababu za kisiasa, wale walioshuhudia wapendwa wao waki kata roho hospitalini kisa hakuna dawa au kwa kuwa madakrari wamegoma kamwe hawaja sahau. Unadhani wale waliopoteza viongo vyao kisa mabomu yaliyolipuka bila utaratibu watakuwa wamesahau? Au wale waliopoteza maisha kisa jeshi la polisi limetumia nguvu kuwa sambaratisha watu wasio hatia, unadhani wamesahau? Haki ya MUNGU vile hawaja sahau na sio kwamba hawaumii mpaka sasa.

Wakati naendelea na harakati zangu hizi za kuhakkiisha kipyenga kitakapo pulizwa na mimi niwemo uwanjani niliamua kurudi jimboni kwangu moja kwa moja ili nishirikiane vyema na wananchi wenzangu. Na nimekua maarufu sana na mpaka watoto wadogo wana niita mbunge. Jambo hilo linanipa faraja sana na kunifanya nisichoke.
Lakini kila mara ninapotoka nyumbani kwangu kuna mtoto mmoja mwenye umri takribani miaka saba au nane hivi huwa ana niangalia na wakati watoto wenzie wana nisemesha yeye hukaa kimya na hugeuza uso k**a ana aibu fulani hivi. Mara ya kwanza nilidhani ni utoto tu ila jambo hilo amelirudia zaidi ya mara kumi tulizokutana. Nilitamani kujua kwa nini anafanya vile lakini sikuweza na ktokana na ratiba zangu na kwa mda mrefu nili lipuuzia jambo hilo.

Chakushangaza wiki iliyopita nilikutana nae njiani akiwa peke yake, hapo ndipo nilistushwa na kinachomsumbua mtoto huyu masikini. Nilimfuata karibu na alijaribu kukimbia lakini nilimk**ata kirafiki na kumbeba kisha nika muangalia na kumuuliza jina lake, anakoishi anasoma wapi na maswali madogo madogo k**a hayo. Kwa kweli alinijibu lakini alikua anogopa sana na anatetemeka. Nilimbembeleza na nilienda nae dukani nikamnunulia soda na biskuti kisha nikamuacha aondoke. Kwenye akili yangu nilijua kuwa nimesha jenga urafiki nae na nilitegemea tuki kutana tena tutasalimiana vizuri. Nilipokutana nae tena aliningalia k**a mwanzo na hakuonesha mabadiliko yoyote, nilidharau ila mara akatoa sauti akaniita, “mbunge, mbungee”…. Niligeuka nyuma nakumsogelea, nikamuambia, “ehe niambie rafiki yangu”.. huku sauti yake ikiwa na hofu hofu ali inua kinywa chake na kusema, “ ETI WEWE NDIYE ULIYE MUUA BABA YANGU?”
**********************************************************************************************
Moyo wangu uliwaka moto wa ghafla “waaaahh” Kisha midomo ikapigwa breki na kubaki k**a bubu huku ikitetemeka na mtoto alikua ananiangalia huku macho yake yakitoka machozi ya uchungu. Nili mkumbatia kwa nguvu na mimi machozi yalinza kunitoka. Nilimungalia huku wote machozi yakitutoka na baada ya mda k**a dakika kumi nilimfuta machozi na kisha nikamuambia, “HAPANA MIMI SIJAMUUA BABA YAKO” .Kisha nika muuliza, “Kwani nani amekuambia kuwa baba yako ameuliwa? alijing’ata nga’ata kisha akasema, “Bibi aliniambia kuwa baba na mama waliuliwa na mbunge.” Hapo ndipo nlipopata picha kuwa alaaah!, kumbe amedhani ni mimi kwa kuwa wenzie wana niita MBUNGE…

Siasa imejeruhi na kuumiza watu wengi sana, majeraha ambayo kila iitwapo leo yanazidi kuongezeka. Kila ifikapo kipindi cha uchaguzi au kwa wengine kila wawaonapo viongozi wao wanakumbuka uovu na unyama waliofanyiwa au waliofanyiwa watu wao wa karibu. Nawasihi watia nia na wagombea wenzangu tufanye siasa zilizo safi na kuacha kutumia njia ambazo zitaumiaza wananchi wenzetu na vizazi vyao. Tusije kuulizwa siku moja kuwa, “ETI WEWE NDIYE ULIYE MUUA BABA YANGU?”

HADITHI: WALIMUUA BABA YANGU NA MAMA YANGU LAKINI BADO NITAWACHAGUA.(THEY KILLED MY PA, THEY KILLED MY MA, BUT I WILL VO...
08/04/2015

HADITHI: WALIMUUA BABA YANGU NA MAMA YANGU LAKINI BADO NITAWACHAGUA.

(THEY KILLED MY PA, THEY KILLED MY MA, BUT I WILL VOTE FOR THEM)

MTUNZI: AMON TAMILWAI

Wakati joto na mihemko ya kisiasa ikizidi kupamba moto, huku kila mtu akijaribu kutangaza nia na k**a si nia basi kutangaza wapi ataegemea mara tu kipyenga kitakapo lia mimi na wadanganyika wengine tumebaki kimya tukiangalia jinsi mtanange unavyo endelea. Wenye nguvu wanazidi kuonesha nguvu zao na wanyonge bila aibu nao wanaonyesha unyonge wao hadharani.

Ni jambo la ajabu sana katika Dunia ya leo kwa wanyonge badala ya kupigania maisha yao wamebaki kuwa washabiki tena wasio na faida na hata k**a ni faida basi ni mkate wa siku moja tu ambao hautulizi hata njaa. Wanyonge wamezidi kutumika k**a ngazi ya kuwapeleka mabwanyenye kwenye nchi ya ahadi ilihali wao wakibakia k**a bendera au vibao vya matangazo. Poleni sana wadanganyika na sikuwahi kujua tabu yenu mpaka nami nilipo poromoroshwa chini na kuwa sawa nanyi.

Sikuwahi kuota hata siku moja kuwa na mimi naweza kuwa kwenye kundi la washangilia badala ya kuwa mshangiliwa. Tangu kuzaliwa kwangu nimeishi kwenye maisha ya kula,kunywa, kuvaa na kulala mahala pazuri pasipo na bughudha wala mawaa. Na sikua naona kadhia yoyote , hata watu wakilalamika maisha magumu ,haki ya MUNGU vile mimi sikuwa najua ladha yake. Maisha magumu kwangu ni kukosa gari jipya, au simu mpya. Huu ugumu wa kukosa chakula, matibabu bora, elimu nzuri, maji safi na kadhalika kwangu ilikua ni ndoto kubwa na kamwe sikua najua k**a kuna mambo k**a haya hapa duniani.

Hivi mna kumbuka April 8, 2000? Ilikua miezi kadhaa tu kuelekea uchaguzi mkuu na joto na mihemko ilikua k**a hii ya wakati huu. Ni kweli hamkumbuki? Hamkumbuki tukio lililo pamba vyombo vya habari kipindi kile?

Ngoja niwakumbushe; Rubaa za kitaifa na ki mataifa zilipambwa na picha ya ajali mbaya iliyotokea eneo la MKANYAMALI njia kuu kuelekea Dar es salaam. Ajali hiyo ili ipata familia ya aliyekuwa waziri wa Fedha na Rasimali wa wakati ule Mheshimiwa Robert William Nyamakamba ambaye ndie alikua baba yangu mpenzi.
Sitamani kuanza kusimulia hadithi ya ajali iliyochukua maisha ya marehemu baba, mama na wadogo zangu wa wawili na kuniacha mimi k**a mkiwa nisiye na ndugu wala rafiki ; ila nataka kusimulia maisha baada ya ajali.

Ni kweli Macho yangu yalishuhudia,moyo wangu ulihisi na kila kiungo cha mwili wangu kili onja uchungu usioweza tamkika mara baada ya kugundua kua ni mimi peke yangu niliyetoka hai kwenye ajali ile na takribani watu saba wote walipoteza maisha pale pale. Sijui kwa nini MUNGU aliamua kuniacha mimi kua hai na kuwachukua ndugu zangu wote, lakini pia sijui kwa nini mara baada ya mazishi ya gharama na ufahari ya ndugu zangu watu wote walinigeuzia visogo na kunisahau kabisa.

Nilihojiwa na vyombo vingi vya habari na wengi walitamani kujua chanzo cha ajali. Lakini mimi mwenyewe sikujua chanzo nini zaidi ya kuliona gari moja jeusi lisilo na namba kuja kutugonga na kutoweka. Taarifa za madaktari zilionesha kuwa marehemu baba hakufa tu kwa ajali bali pia alipigwa risasi kichwani na wengine walipuliziwa sumu ambayo haikutambulika mpaka leo.Ukiniuliza kwa nini mimi nimeachwa hai hata sijui sababu.
Maisha yamebadilika ghafla na kwa kipindi cha miaka kumi nimeporomoka kutoka kwenye ufalme mpaka kwenye ulofa usio na kiasi. Hakuna rafiki wala mshabiki wa marehemu baba aliyejitokeza kujua hali yangu na kunisaidia mpaka leo. Maisha yamenifundisha kua mali na vyeo ni k**a maua. Huwa mazuri sana pindi yachanuapo lakini husikitisha wakati wa kunyauka.

Huwezi amini lakini kwa kweli nimeonja ladha ya maisha ya wananchi wa kawaida, na nimejifunza kua walio na mamlaka hawajua kinacho wakuta wanyonge. Watawala wana sikia tu hali halisi ya watu wao ila hawajui uhalisia. Hawajuai ladha ya kulala chini hospitalini, hawajui dhiki ya kutafuta maji, hawajui uchungu wa kuzunguka juani k**a machinga, hawajui kadhia ya kuishi bila senti mfukoni. Watawala hawajui shida ya kukatikiwa umeme wakati wa oparesheni kitandani, hawajui adha ya mafuriko wala kuezuliwa kwa mapaa ya nyumba kwa upepo.

Nimekua mtoto wa mtawala na nimeishi maisha ya utawala, nafahamu ladha ya kuwa mtoto wa mkubwa na sasa nafahamu ladha ya kuwa KAPUKU. Baba yangu angebaki hai nisingejua uuchungu wa maisha na kamwe nisinge andika waraka huu. Sina namna ya kujitoa tena huku mavumbini zaidi ya kuwashangilia na kuwapigia chepuo wakubwa wana weza waka niona na kumkumbuka marehemu baba yangu. Ngoja uchaguzi ufike mimi nitakua mstari wa mbele kuimba nyimbo za sifa na mapambio. Kupiga vigelegele na kusambaza sifa zao njema. Roho wa utu aweza warudia na kunikumbuka kua na mimi nilikua mtoto wa mwenzi wao. WALIMUUA BABA YANGU NA MAMA YANGU LAKINI BADO NITAWACHAGUA.

N.B HADITHI YA KUBUNI KABISA.

HADITHI:  SISI NI WATOTO WA EVA YULE HOUSE GIRL WA ZAMANI (SEHEMU YA PILI)MTUNZI: AMON TAMILWAI.Habari ya historia ya ma...
16/12/2014

HADITHI: SISI NI WATOTO WA EVA YULE HOUSE GIRL WA ZAMANI (SEHEMU YA PILI)
MTUNZI: AMON TAMILWAI.

Habari ya historia ya maisha yetu imeanza kusambaa kila kona na watu wamejaribu kuhusisha yale aliyoyafanya VICKY k**a ni malipizi kwa familia ya FRANK. Mimi bado sija amini hilo, namfahamu vizuri VICKY ni kweli ana hasira na uchungu mkubwa hasa akikumbuka kuwa sisi tulikataliwa tangu siku mimba yetu inatungwa na kunyanyasika tangu kuzaliwa kwetu mpaka leo hii. Hatumfahamu baba yetu halisi na mama yetu mpaka ana aga Dunia ametuachia kitendawili ambacho ni kigumu kukitegeu. Kwa wasio na habari; Mimi naitwa VICTA pacha wake na VICKY yule dada wa kazi alie waudhi na kuwaumiza watu wengi kwa vitendo vya kinyama alivyo vifanya kwa mtoto mdogo alieachiwa kumlea.

Leo nime amini kweli VICKY amewaudhi na kuwamiza watu wengi, mahak**a imefurika watu kuliko kawaida, wengine wakiwa wameshikilia mabango yenye jumbe mbalimbali kushinikiza adhabu kali kwa VICKY, Watu wamepandisha hasira na wanataka adhabu atakayopewa vicky iwe kali kupitukia ili iwe fundisho kwa wasichana wengine wa kazi walioko majumbani. FRANK, familia yake na Marafiki zake wamevalia fulana zenye ujumbe mkali unaoitaka mahak**a kutokufanya ajizi na suala hilo. Sio mtaalamu wa sheria na sifahamu k**a sheria inaruhusu yote haya kutendeka ila pia sina uwezo wala mtu wa kunisaidia kuniambia kuwa ni haki au si haki.

Liwalo na liwe, mikono yangu imekua minyonge, mwili wangu umedhoofu na moyo wangu umefunikwa na giza nene lisilo na mfano, sijui la kufanya, natamani kumsaidia dada yangu mpenzi lakini sina jinsi, najua hali aliyo nayo anatamani angepata hata wa kumwambia pole na kumpa neno moja la matumaini lakini hayupo. Dunia nzima imemgeuzia kisogo na kumuona k**a mnyama asiye na thamani, muuaji asiye na huruma,firauni,jambazi na mdhambi kuliko wadhabi wote.

Ahhhhhh!!! Nyamazaa…. Muuaji… jambaziii….Muongoooo, muongoo…. Afungweee….kelele za ghafla na zenye kila aina ya chuki zilisikika mara pale tu VICKY alipojitetea kuwa alifanya unyama ule kwa kua mke wa FRANK alikua akimtesa sana. Hakimu aliamuru watu wakae kimya na aliomba ushauri kidogo kwa wazee wa baraza kisha akasema, “VICKY una lolote la kujitetea zaidi?”...vicky huku mwili na moyo wake ukiwa umedhoofu na kukosa tumaini, alijikaza na kuinua kichwa chake kuuangalia uma wa watu uliokuwa kinyume naye, kisha akasema, “ MUHESHIMIWA HAKIMU SIJUI K**A INARUHUSIWA, ILA NAOMBA JAMBO MOJA MNISAIDIE , MIMI NINA MDOGO WANGU ANAITWA VICTA NA NDIO MTU WA PEKEE NINAE MTEGEMEA NA ANAYENITEGEMEA PIA, NAOMBA AJE HAPA NIMUELEZE MAMBO MACHACHE TU AMBAYO NIMEKUTANA NAYO NIKIWA NYUMBANI KWA FRANK ILI HATA K**A MNANIHUKUMU KIFO AJUE NI KWA NINI MIMI DADA YAKE NIMEFANYA JAMBO HILI.”Watu wote waliofika pale mahak**ani walikaa kimya, na hata sijui maneno yale ya VICKY yalikua na nguvu kiasi gani, lakini bila kupinga hakimu aliruhusu kwa dakika tano VICKY aweze kuniambia anachotaka kuniambia.

Dakika tano, dakika tano nilizo ziona chungu kuliko shubiri, dakika tano zilizo ongeza kidonda kikubwa maishani mwangu, dakika tano zilizonipa roho ya kikatili na hasira ya kufanya kila liwezekanalo ili KUUFUNDISHA ULIMWENGU KUA MALIPO NI HAPA HAPA DUNIANI. Sitasahau maneno ya dada yangu pale kizimbani, alinikumbatia kwa uchungu kisha akaniambia, “VICTA, ni kweli nimekosea, nisamehe mdogo wangu. Maisha yamezidi kuwa magumu kwetu, nimeshindwa kuvumilia. Unakumbuka nilikwenda kufanya kazi kwa FRANK ili tu niweze kumuambia ukweli kuwa sisi ni Damu yao. Mmoja Kati ya yeye au BABA yake mzazi ndio atakuwa BABA YETU kwa kuwa wote wawili walitembea na marehemu mama yetu kipindi anafanya kazi za ndani nyumbani kwao na kumtelekeza baada ya kubeba ujauzito wetu. Jambo hilo halikufanikiwa mdogo wangu, FRANK na mke wake waliendeleza unyama wao kwangu, FRANK alinilazimisha kulala nae mara kadhaa na alikua akiniingilia kinyume cha maumbile. Mkewe alipohisi hayo alichukua kisu na kukipasha moto kisha kunichoma nacho sehemu za siri bila huruma. Jambo hilo limeniumiza sana mdogo wangu, hapa nilipo sina hamu ya kuishi. Bora nife nimfuate mama yetu huko aliko. Nisamehe mdogo wangu, sijui nikwambieje ila mpaka sasa nina ujauzito wa yule hayawani pale FRANK na analifahamu hilo, amenipiga kwa mawili ,la kwanza ni kwa sababu ya kumuumiza mtoto wake na la pili amenipiga ili hii mimba itoke. Sijui ntapewa adhabu gani, lakini nakukabizi KIHANJIFU hichi kilicholowa damu yangu ili iwe ukumbusho na alama kwako, Kikutie nguvu, kikufariji,kikuliwaze na kukusaidia katika kila ufanyalo. Zaidi nakuomba fanya kila njia mdogo wangu uwa fahamishe watu KUWA SISI NI WATOTO WA EVA YULE HOUSE GIRL WAZAMANI.

N.B hii ni hadithi ya kubuni tu na majina yalyotumika hayana uhusiano wala ukweli wowote juu ya tukio lolote lililotekea. (I WISH YOU MERRY CHRIST MASS AND HAPPY NEW YEAR).

25/11/2014

HADITHI: SISI NI WATOTO WA EVA YULE HOUSE GIRL WA ZAMANI
MTUNZI: AMON TAMILWAI.
Vyombo vya habari, mitandao ya kijamii na stori za vijiweni na mitaani zote zimepambwa na kisa hiki cha dada wa kazi (house girl) aliemsulubisha mtoto mdogo asie na hatia ambaye aliachiwa kumlea. Wazazi, walezi na wananchi wa Afrika mashariki kwa ujumla wameonyesha hisia zao kwa namna mbalimbali na wengi wakilaani ukafiri huu alioufanya dada huyo aliejulikana kwa jina moja tu la VICKY. Watu wengi wamelaani kitendo hicho na kila mtu ametoa maono yake kwamba k**a ingemtokea yeye angemfanya nini VICKY.. Wengi wameguswa na tukio hili na wengi wamemhukumu dada huyu kwa hukumu kuu wengine wakisema anyongwe, afungwe maisha, apigwe mawe mpaka kifo na kadhalika. Adhabu zote zimekuja kutokana na unyama alioufanya kwa mtoto mdogo asiye na hatia. Hakuna hata mmoja kati ya niliowasikia alietamani kumpa dada huyu nafasi ya pili ya kujitetea au kueleza kwa nini ametekeleza unyama huu kwa malaika yule mtoto.
Wakati yote hayo yakiendelea majumbani hali imebadilika, wazazi wameanza kuwa waangalifu na watoto wao ,kila wanapowaacha,wengine wameamua kuwa wanawahi kurudi toka mishughulikoni na wengine wametoa maonyo mbalimbali kwa wadada wa kazi huku wakiwaonyesha mfano wa alichofanya na alichofanyiwa mwenzi wao. Kila dada wa kazi kwa sasa anajitahidi kutimiza wajibu wake na kuonyesha upendo kwa watoto anao walea ili tu kupinga kile alichokifanya mwenzi wao na pia kujijengea kuaminika kwa tajiri wake.
Masikini dada VICKY njia aliyoitumia kufikisha ujumbe kwa DUNIA haikuwa sahihi; hata mimi mdogo wake sijaiunga mkono, sikutegemea k**a angefanya kwa ukatili kiasi kile. Hata k**a alikua na uchungu na hasira zipitazo hasira za mtoa roho, hakutakiwa kufanya unyama ule kwa mtoto. Hakuna mtu atakae muelewa hata akifumbua kinywa chake kueleza kwa nini amefanya vile. Nafahamu hakuna atakae ona uzito wa sababu yake kwa kua amefanya unyama ule kwa mtoto asie na hatia. Na naamini ni mimi tu ndio naweza kuuambia ulimwengu kwa nini Vicky amefanya vile alivyofanya. Labda ulimwengu unaweza kufungua masikio na kusikia hata kwa sehemu sababu iliyompelekea Vicky kufanya vile.
Mimi naitwa VICTA pacha wake na VICKY yule dada wa kazi alie ICU (chumba cha wagonjwa mahututi). Desember mwaka huu mimi na pacha wangu tunatimiza miaka kumi na mi tatu ya umri, lakini maisha yametufundisha kuishi k**a watu wenye umri wa miaka arobaini. Dunia imefumba macho juu yetu tangu siku ya kwanza ya mimba yetu kutungwa. Sitashangaa kumuona dada yangu VICKY akifungwa maisha au akiuwawa kwa sababu tulishakufa siku nyingi ilihali tu hai. Na amini imebaki siku tu mizoga yetu kuliwa na mbwa na hayawani wa Dunia. Sio kuwa tumekata tamaa ya maisha la hasha ila tangu siku ya kuzaliwa kwetu mawingu meusi yalishatanda juu ya anga k**a ishara ya anga na ardhi kutukataa. Jua lilifunguliwa mpaka mwisho na kuelekezwa vichwani mwetu tangu siku ile mbegu za uzazi wetu zilipotungwa, anga halikutamani tupate kimvuli hata siku moja ya uhai. Jasho na fukuto vimetufuata , vilio huzuni, bahati mbaya, uchungu na kila aina ya dhiki hilo ndio limekuwa fungu la maisha yetu kwa miaka yote kumi na mitatu.Ngoja niache nahau na mashairi nianze kuwaeleza kwa ufupi historia yetu.
******************************************************************************
Sisi ni watoto wa pekee wa dada mmoja aliejulikana kwa jina la EVA, najua wengi mme msahau kwa kuwa ni miaka mingi imepita tangu jina lake lifutike katika DUNIA. Usiulize baba yetu ni nani kwa kuwa jibu ndio nitakupatia.
Tulipotimiza umri wa miaka takribani mitatu au minne tangu kuzaliwa mama yetu alituchukua huku akiwa kwenye hali mbaya sana kia afya na kutupeleka kwenye nyumba moja ya kifahari kidogo. Tulipofika getini mlinzi alituzuia lakini mama alimsihi sana amuite mama mwenye nyumba. Yule mlinzi aliita kwa woga kidogo, “mama, mama kuna wageni wako”. Sauti ya mama asiye wa makamo sana ilisikika ikimuamuru mlinzi aturuhusu kuingia. Mama yetu mpenzi alitususuma lakini tulipoingiza nyuso zetu tu getini, yule mama alimaka kwa sauti, “haaaaaa!!!! Haaaaaa!!!haaaaa!!! Eva? Umerudi tena? umefuata nini hapa?”. Sote tulistushwa na sauti ile kali na tulimshika mama yetu aliekuwa anakohoa ili aweze kujieleza. Sitasahau siku ile maishani mwangu, mama yule alikuja na kutusukuma huku akisema, “unataka nini? Umekuja kunichafulia familia yangu tena eeee??” mama kwa kujikongoja alianza kuongea na maneno yake nayakumbuka mpaka leo. “Mama mimi sijakuja kwa shari, naomba unisikilize kidogo tu kisha nitaondoka,|” yule mama akiwa anajifunga kibwebwe chake vizuri alitema mate kwa dharau kisha akasema eehhh ongea…. Mama aliendelea, “Dada mimi nitakufa siku si nyingi, nimejitahidi sana kuwalea hawa watoto tangu siku ya kwanza ya ujauzito mpaka leo, nimefanya kila niwezalo kunusuru uhai wao, lakini mpaka sasa hali yangu si njema tena. naumia sana kwamba nitawaacha hawa watoto wakiwa hawana msaada wowote; dada naongea maneno haya kutoka moyoni mwangu na wewe ni binadamu tena mwanamke mwenzangu. Naomba unielewe, haki ya mungu dada na apa mbele yako, hawa watoto ni damu yenu. Katika maisha yangu yote ya kukaa hapa kwako k**a house girl sikuwahi kutembea na mwanaume yeyote narudia tena yeyote nje ya wanaume walio humu ndani ya nyumba yako. Najua ukweli unauma ila bora niseme ili kunusuru maisha ya malaika hawa wasio na hatia. Dada, hawa watoto baba yao k**a sio mumeo basi ni watoto wa mwanao mkubwa frank kwa kuwa wote nilitembea nao kwa nyakati tofauti.”
******************************************************************************
Paaaaaaaaahhhh!!!! Sauti kubwa ya kishindo cha kofi kikifuatiwa na yowe kubwa kutoka kwa mama vilitustua na mimi na VICKY tulikimbia moja kwa moja na kumkumbatia mama alierushwa takribani hatua tatu kwa uzito wa kofi lile alilopigwa na yule mama. Tulikuwa wadogo sana lakini uchungu alioupata mama ulitufikia mpaka ndani kabisa na kupasua maini. Mama alizimia pale chini akituacha sisi tukimkumbatia bila msaada wowote. Yule mlinzi alikuja na kumwagia maji na alipo zinduka ali amriwa atuondoe haraka. Alitubeba mzega mzega mpaka nje kisha akafunga geti kwa nguvu pwaaaaaah.
Hapo ndipo nilipojua kuwa sisi tumekataliwa na hatuna namna tena ya kuhesabu kuwa tuna baba. Kwanza hajulikani ni nani kati ya mtoto au baba wa ile nyumba, pili haitatokea yeyote kati yao kuja kutufuata kwa kuwa sisi ni aibu na chanzo cha vurugu katika ile familia. Masikini mama yetu mpenzi, hakuwa na nguvu tena na kutokana na magonjwa yaliyokuwa yakimuandama aliaga dunia na kuacha ulimwengu utulee. Mimi ndio nilikuwa baba wa vicky na vicky alikua mama yangu. Jua, mvua, mitaro, magunia, vyakula vya majalalani na kulala mitaroni ndio yalikua malezi yetu kwa miaka na miaka. K**a binadamu wengine wenye hisia nasi tulihisi uchungu wa Dunia huku tukijua fika tumezaliwa kwa bahati mbaya na ni haramu k**a kilivyo kitimoto kwa muislamu. Hakuna mtu alikuja kutuambia chochote cha kutupa tumaini la maisha zaidi ya kunyanyasika kusiko na mwisho. Wakati watoto wengine wanalelewa kwa upendo na furaha, sisi dunia ilitulea kwa kisirani na chuki, wengine wakiambiwa kuna MUNGU sisi tulijua kuwa MUNGU amefumba macho na masikio tena yuko bize hatuoni. Wakati nyie mnawalisha watoto maneno ya upendo na matumaini sisi Dunia imetulisha chuki, visasi, ugomvi, maonevu na ukatili. Vicky alibakwa akiwa na miaka saba, alianza kufanya kazi za ndani akiwa na miaka tisa ama kumi hivi na kila siku aliniambia kuwa lazima unyama aliofanyiwa mama yetu pamoja na sisi lazima alipe kisasi. Yuko radhi kufa lakini lazima awafundishe walimwengu kuwa binadamu wote ni sawa na tofauti yetu ni mazingira tu.
Sikutegemea k**a atalipiza kisasi kwa mtoto wa Frank ambae anaweza kuwa ndio baba yetu k**a mama alivyosema, lakini pia sidhani k**a frank anamfahamu vicky kuwa ni mmoja wa watoto wa yule house girl aliemuingilia kipindi kile anakaa pale kwao. Ulimwengu haufahamu sababu ya vicky kufanya unyama alioufanya .Vicky atafikishwa mahakani na kush*takiwa na hata hukumu kali itamuangukia. Sina jinsi ya kumsaidia dada yangu mpenzi, moyo wangu umetandwa na huzuni kubwa isiyo mfano. Mikono yangu haina nguvu ya kutengua hukumu yoyote anayopewa wala ile atakayopewa Vicky. Ila asomaye na afahamu liwalo na liwe waambieni wajue SISI NI WATOTO WA EVA YULE HOUSE GIRL WA ZAMANI.
N.B hii ni hadithi ya kubuni tu na majina yalyotumika hayana uhusiano wala ukweli wowote juu ya tukio lolote lililotekea. (KILA JAMBO LITOKEALO CHINI YA JUA LINA CHANZO, SABABU NA MWISHO).

29/07/2014

EE... MWENYEZI MUNGU NIOMBEE MSAMAHA KWA MAREHEMU MKE WANGU.

“Mimi AMON TANGIRAI nakubali kukuchukua wewe CHOSENFLORAH BARUTI kuwa mke wangu wa ndoa na nahidi kukupenda, kukuheshimu, kukutunza na kukulinda siku zote za maisha yetu. Nitakuwa mume mwaminifu kwako na kamwe sitasaliti ahadi hii, nita ambatana nawe kuanzia leo hii mpaka pale kifo kitakapo tutenganisha amen…”

Hii ndio ahadi niliyoitoa kwa mke wangu miaka nane iliyopita katika madhabahu mbele ya MUNGU, Mchungaji na Washarika wa Kanisa la Kiinjili la Kilutheri la Tanzania (KKKT) usharika wa majumba mabovu mkoani TANGA. Kwa ahadi hii nilipata kibali cha kuambata nae na kuishi nae k**a mke na mume. Maisha yalikua mazuri ya Furaha na amani. Mke wangu alikua ni mwalimu kwa taaluma na mimi ni Muandishi wa habari. Tulipendana kwa kweli na kila alie tuoana alitutamani na kutufurahia. Hata baada ya miaka mitatu ya ndoa yetu tulishajaliwa kupata mtoto, kujenga nyumba yetu nzuri pamoja na kumiliki vitega uchumi mbalibali. Kwa kifupi maisha yalikua mazuri ila kulianza kutokea kasoro ndogo ndogo na kutoelewana hapa na pale. Nilijitahidi kwa kutumia hekima kusuluhisha migogoro yote kati yetu bila kushirikisha watu, na kwa kuwa mke wangu alikua mpole sana, mara zote hujishusha na kuomba msamaha jambo ambalo kwangu nililitumia k**a silaha ya kumkandamizia.

Sifahamu nini kilinitokea ila kwa kweli nilianza kumchukia mke wangu kwa chuki isiyoelezeka, nilijitahidi kwa nguvu zangu kutaka kurudisha ule upendo wetu wa kwanza lakini haikuwezekana. Mara zote nilikuwa nikimuona k**a kuna kitu kinatembea kwenye damu yangu na kupandisha chuki ya hali ya juu. Kila alicho kifanya au kukisema kwangu kilikuwa nikosa, na kwa kuwa anaomba msamaha mara kwa mara neno NISAMEHE kwangu LILIKOSA MASHIKO.

Nakumbuka siku moja nilirudi nyumbani toka kazini na nilimkuta akiwa anajitengeneza nywele, siku hiyo nilirudi mara moja tu kuchukua dokumenti fulani ili nikafanye mahojiano KWENYE TELEVISHENI. Nilipokuwa naondoka aliniita na kunirekebisha shati langu lililokuwa JEUPE maalumu kwa siku hiyo, lakini alisahau kuwa mikono yake ilikuwa michafu hivyo alinichafua. DAH! Kwa kweli aliniudhi,nilimuangalia kwa jicho la hasira, hakuwa na lakufanya zaidi ya kutetemeka na kuniomba msamaha, upendo wake uligeuka kuwa kwazo kwangu. Nilifikiria mengi, “ sijui nimpige, nimfokee au nimsamehe” mawazo mengi yalipita kichwani na yeye kwa upendo aliingia ndani haraka na kunibadilishia shati., “ Unadhani ndio umefumbua tatizo?” nilimuuliza kwa hasira kisha nikalitupa lile shati na kuondoka zangu nikiwa nimevaa shati lenye doa. NILIJUA FIKA NITAFUNIKA LILE DOA KWA KOTI, ila kitendo hicho najishangaa mpaka leo kiliniumiza sana na kunifanya nikalale nyumba ya wageni (GUEST HOUSE) mara baada ya kumaliza kipindi.

Kesho yake niliporudi aliniuliza nili lala wapi ila sikumjibu, alijitahidi kunibembeleza lakini ROHO YA KIBURI ILINIJAA, chuki na kila aina ya dharau, nilimsukuma pembeni k**a takataka na kuendelea kuafanya mambo yangu k**a hakuna lililotokea. Huo ndio ulikua mwanzo wa tabia zangu mbaya, NILIENDELEA KULALA NJE YA NYUMBANI KWANGU NA KUISALITI NDOA YANGU BILA WOGA, HOFU YA MUNGU ILINITOKA NA ROHO WA IBILISI ALINITAWALA. Kwa kuwa ni mtangazaji maarufu na nina pesa ilikuwa rahisi kwangu kubadilisha wanawake k**a nguo, SITA SAHAU NILIWAHI KULALA NA WANAFUNZI WA NNE WA CHUO KIKUU KWA MPIGO NDANI YA CHUMBA CHA HOSTEL.Ukiniuliza kwa nini nafanya ufuska na ushetani wa namna hiyo hata sielewi nikujibu nini. Lakini ukweli ni kwamba mke wangu alikua amenichujuka, nikimuona ni k**a nimeona gari la takataka za sokoni, nyumba yangu niliiona k**a jalala na sikuwa na hamu ya kurudi nyumbani hata kidogo. Maskini mtoto wangu alitamani kucheza na mimi lakini sikua na muda, mke wangu alijitahidi kuwaita washauri, wazazi na wachungaji lakini sikuwasikia. “Nilitamka hadharani mkitaka nirudi nyumbani kwangu labda huyu mwanamke afe”.
Najua nimemuumiza sana mke wangu, aliamua kuishi k**a mjane wakati mumewe bado ni hai, alijitahidi kunibembeleza kwa kila njia sikuweza kumuelewa, mwili wake ulisinyaa kwa mawazo na maumivu makali ya nafsi kuona mumewe anacheza na visichana vidogo vya mtaani na vyuoni, hakuchoka kuomba akiamini kuwa ipo siku nitarejea ila ndoto yake haikuweza kutimia.Kuna kipindi nilijirudi na kujifanya nimetubu kumbe hakujua ulikua ni mtego wa mauti kwake, Mimi nilishaathirikia na UKIMWI na nikamuambikiza yeye.

HAKUWA NA HATIA , LILE NILILOLITAKA LEO LIMETIMIA, NI KWELI AMESHA FARIKI, AMENIACHIA NYUMBA NA NIMERUDI NYUMBANI. NIKO PEKE YANGU, UPWEKE NA MAJUTO NILIYO NAYO SIWEZI KUYAELEZA. NATAMANI HATA ANGERUDI KWA DAKIKA MOJA NIMKUMBATIE NA KUMUOMBA MSAMAHA. NATAMANI NINGEPATA NAFASI YA KUFUTA MAKOSA YANGU NA KUMUONESHA UPENDO K**A VILE ALIVYOKUWA ANA NIPENDA YEYE, NATAMANI AFUNGUE JICHO NIMWAMBIE TENA AHADI MPYA YA MAISHA MAPYA. HAIWEZEKANI.

Ivi kweli kuna mtu anampiga mke wake au mume wake? kweli kuna watu tunasaliti ndoa zetu na kutelekeza familia? Umefika mahali humuoni tena wa thamani na uzuri wake umepepea k**a upepo? Hebu njoo kwangu nikusimulie maumivu yake. Natamani hili nipitialo mimi lisikukute, Njoo nikuonjeshe kidogo maumivu ya moyo niliyo nayo. HAKIKA HUTARUDIA TENA UKIFANYACHO.EE MWENYEZI MUNGU NIOMBEE MSAMAHA KWA MAREHEMU MKE WANGU.

N.B... HII NI HADITHI YA KUTUNGA by Mc Amon 0712000781.

TUOMBEANE NA TUSHAURIANE NAANDIKA KITABU KIITWACHO MACHOZI YA MBWA MWITU "TEARS OF THE WILD DOG" KITAKACHOKUA MOVIE PIA.

Address

Pangani

Telephone

0712000781

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Swahili Stories posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category