Ombiney Digital

Ombiney Digital Ombiney media

05/02/2026

Chama Cha Mapinduzi (CCM) Kata ya Kisima washerehekea miaka 49 ya chama kwa vitendo vya kijamii. Kwa kutembelea Hospitali ya mji wa Same na kufanya shughuli za usafi wa mazingira,
CCM inaonyesha kujitolea kwao na dhamira ya kuboresha mazingira ya afya kwa jamii.

Mwenyekiti wa CCM kata ya Kisima , Ndugu Athumani Mbwambo, amesisitiza umuhimu wa viongozi wa kata na wananchi kuwa na jukumu la kusaidia hospitali hiyo, ikizingatiwa kwamba ipo ndani ya eneo la kata yao. Hii ni hatua nzuri inayowatia moyo wananchi kuungana katika juhudi za kuboresha huduma za afya.

Vilevile, Mganga Mkuu wa Wilaya (DMO) amewashukuru wana CCM na Umoja wa Wanawake wa CCM wilaya ya same (UWT) kwa kujitoa kwao katika shughuli hizi. Pia, aliwataka wananchi kuendelea kutoa taarifa kuhusu changamoto zinazokabili hospitali, ambayo ni muhimu kwa kuhakikisha huduma bora za afya zinapatikana.

Hatua hii ya CCM Kata ya Kisima ni mfano mzuri wa uongozi na ushirikiano katika kuboresha afya za wananchi na mazingira ya kuishi.

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Same limepitisha mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/2027 wenye juml...
05/02/2026

Baraza la Madiwani wa Halmashauri ya Wilaya ya Same limepitisha mpango wa bajeti kwa mwaka wa fedha 2026/2027 wenye jumla ya zaidi ya shilingi bilioni 60.3, hatua inayolenga kuimarisha maendeleo ya kiuchumi na kijamii pamoja na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi wa wilaya hiyo.

Bajeti hiyo imepitishwa katika kikao cha Baraza la Madiwani kilichofanyika Februari 04, 2026, katika ukumbi wa mikutano wa Halmashauri ya Wilaya ya Same.

Akizungumza katika kikao hicho, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Same, Bw. Yusto Mapande, alisema kuwa bajeti hiyo imelenga ustawi wa wananchi wa Same kwa kuzingatia mahitaji yao ya msingi na vipaumbele vya maendeleo.

Alieleza kuwa bajeti hiyo imejikita katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya kimaendeleo ikiwemo sekta za afya na elimu, ujenzi wa jengo la utawala la Halmashauri ya Wilaya ya Same, uendeshaji wa halmashauri, ujenzi wa uwanja wa michezo pamoja na kuboresha miundombinu mingine ya kimaendeleo ili kukuza uchumi wa wilaya hiyo.

Kwa upande wake, Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, alitumia fursa hiyo kutoa elimu kwa madiwani kuhusu umuhimu wa wananchi kujiunga na bima ya afya kwa wote, Aliwataka madiwani kuhakikisha wanawaelimisha wananchi kuhusu faida za bima ya afya kwa wote ili kuwawezesha kupata huduma bora na za uhakika za matibabu.

Aidha, alipongeza kupitishwa kwa bajeti hiyo na kusisitiza umuhimu wa usimamizi mzuri wa fedha za umma ili zitumike kwa malengo yaliyokusudiwa.

Katika hatua nyingine, Mhe. Kasilda aliwasisitiza madiwani na watumishi wote wa umma kuhakikisha wanawaelimisha wananchi na kuhamasisha utunzaji wa mazingira pamoja na upandaji wa miti, hususan miti ya matunda, ili kukabiliana na athari za mabadiliko ya tabianchi.

Naye Mwenyekiti wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Same, Bw. Abdallah Mnyambo, aliwasisitiza watumishi wa umma pamoja na viongozi wa serikali kusimamia ipasavyo miradi na miundombinu yote ya kimaendeleo ili idumu kwa muda mrefu na kuepusha uharibifu wa rasilimali za umma.

**MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA CCM – KATA YA KISIMA**Katika kuadhimisha miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanachama w...
04/02/2026

**MAADHIMISHO YA MIAKA 49 YA CCM – KATA YA KISIMA**

Katika kuadhimisha miaka 49 ya Chama Cha Mapinduzi (CCM), wanachama wa CCM wa Kata ya Kisima walifanya zoezi la usafi wa mazingira katika Hospitali ya Mji. Hili lilikuwa ni sehemu ya kuonesha mshik**ano, uzalendo, na uwajibikaji kwa jamii.

Zoezi hilo lilifanyika kwa mafanikio makubwa na lilihusisha usafishaji wa maeneo mbalimbali ya hospitali, kuondoa taka, na kufyeka majani. Mwenyekiti wa CCM Kata, Cde. Athumani Wiliam, alizungumza baada ya zoezi hilo na kusisitiza kuwa chama kitaendelea kushiriki katika shughuli za kijamii zinazolenga kuboresha maisha ya wananchi. Aidha, alieleza umuhimu wa kuunga mkono juhudi za Serikali katika sekta ya afya na usafi wa mazingira.

Mganga Mkuu wa Wilaya, Dr. Alex Alexander, pamoja na uongozi wa Hospitali ya Mji, waliwapongeza wana-CCM kwa moyo wao wa kujitolea. Walihimiza wadau wengine kuiga mfano huo kwa kushiriki kikamilifu katika kutunza mazingira.

Maadhimisho ya miaka 49 ya CCM yanaendelea kuwa chachu ya mshik**ano, amani, na maendeleo kwa Taifa letu, huku wakitilia mkazo umuhimu wa kazi za kijamii na uhifadhi wa mazingira.

Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, ametoa wito kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kutafsiri sh...
03/02/2026

Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, ametoa wito kwa Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kutafsiri sheria mbalimbali kwa lugha adhimu ya Kiswahili ili ziweze kuwafikia wananchi wengi zaidi na kuongeza uelewa wa masuala ya kisheria hasa kwa wananchi wasio na uelewa wa kutosha wa lugha ya kingereza.

Mhe. Kasilda ametoa rai hiyo Februari 2, 2026 wakati akizungumza katika maadhimisho ya Siku ya Sheria Nchini, ambapo kwa wilaya ya Same maadhimisho hayo yamefanyika katika viwanja vya Mahak**a ya Wilaya ya Same.

Amesema kuwa utoaji wa maamuzi ya kimahak**a kwa lugha ya Kiingereza umekuwa changamoto kwa baadhi ya wananchi kutokana na kushindwa kuelewa lugha hiyo, hali inayoweza kuathiri uelewa wao kuhusu haki zao na maamuzi yanayotolewa na Mahak**a.

“Niombe Ofisi ya Mwanasheria Mkuu wa Serikali kuendelea kuzitafsiri sheria kwa lugha yetu adhimu ya Kiswahili ili ziweze kuwafikia wananchi wengi na kuongeza uelewa kwa wananchi tunaowahudumia,” amesema Mhe. Kasilda.

Aidha, amewasisitiza mahakimu, wanasheria pamoja na vyombo vyote vya utoaji haki wilayani humo kuzingatia weledi, maadili na uwajibikaji katika utekelezaji wa majukumu yao ili kujenga imani ya wananchi katika mfumo wa utoaji haki.

Kwa upande wake, Hakimu Mkazi Mfawidhi wa Mahak**a ya Wilaya ya Same amesema kuwa mikakati iliyotekelezwa na Mahak**a kwa mwaka 2025 imeongeza ufanisi katika usikilizaji wa mashauri, kupunguza muda wa mashauri kusikilizwa na kuamuliwa, kupungua kwa mlundikano wa mashauri katika ngazi mbalimbali za mahak**a, pamoja na kuongezeka kwa imani ya wananchi kwa Mahak**a na mfumo wa utoaji haki kwa ujumla.

Kwa mujibu wa Ibara ya 107A ya Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ya mwaka 1977, k**a ilivyorekebishwa mwaka 2023, Mahak**a ni chombo cha mwisho katika utoaji haki. Miongoni mwa majukumu yake ni kusikiliza na kuamua mashauri, kutatua migogoro kwa njia ya usuluhishi kwa mujibu wa sheria, kutafsiri sheria pamoja na kutoa elimu kwa umma kuhusu masuala mbalimbali ya kisheria.

Maadhimisho yasherehe za Ccm kutimiza miaka 49ya tangu kuzaliwa kwake Jumuiya ya wazazi (W) Sameimeadhimisha kwa kutembe...
02/02/2026

Maadhimisho yasherehe za Ccm kutimiza miaka 49
ya tangu kuzaliwa kwake Jumuiya ya wazazi (W) Same
imeadhimisha kwa kutembelea watoto yatima
ccM 49
katika kituo cha Rafiki Children Center
Kilichopo kata ya Kisima.

01/02/2026
TANGAZO MUHIMU SAME UTALII FESTIVAL (SUF) – SEASON 3, 2026:Kamati ya Same Utalii Festival (SUF) chini ya uongozi waMweny...
28/01/2026

TANGAZO MUHIMU
SAME UTALII FESTIVAL (SUF) – SEASON 3, 2026:

Kamati ya Same Utalii Festival (SUF) chini ya uongozi wa
Mwenyekiti – Mhe. Kasilda Jeremiah Mgeni,
Mkuu wa Wilaya ya Same,
inawatangazia Wananchi wa Same, Watanzania na Wadau wa Utalii ndani na nje ya nchi kuwa:

Baada ya kupokea maoni ya WanaSame, na kwa kuzingatia na kuheshimu Mfungo wa Ramadhani na Mfungo wa Pasaka (Kwaresma), Kamati imeona itumie busara na KUSOGEZA MBELE Tamasha.

TAREHE MPYA ZA TAMASHA:
05 | 06 | 07 APRILI, 2026

Aidha Kamati inawatakia Waislamu na Wakristo wote maandalizi mema ya ibada na kuomba radhi kwa mabadiliko haya.

Wadau wote wanaendelea kuhimizwa kushiriki maandalizi yanayoendelea.

Imetolewa: 26/01/2026
Kamati ya Same Utalii Festival (SUF)

Katika juhudi za Serikali kuhakikisha inawakwamua wananchi kiuchumi kwa kuwawezesha ujuzi, mikopo pamoja na vifaa kwa ku...
26/01/2026

Katika juhudi za Serikali kuhakikisha inawakwamua wananchi kiuchumi kwa kuwawezesha ujuzi, mikopo pamoja na vifaa kwa kushirikiana na wadau mbalimbali, Mkuu wa Wilaya ya Same, Mhe. Kasilda Mgeni, amekabidhi mtambo wa kisasa kwa ajili ya kuchimba madini (excavator) uliogharimu zaidi ya shilingi milioni 333, kupitia mkopo wa Benki ya NMB, kwa mmoja wa wachimbaji wa madini ya jasi katika Kata ya Makanya.

Akizungumza katika hafla hiyo, Mhe. Kasilda Mgeni aliwasisitiza wananchi na wachimbaji wa madini kutumia vyema fursa mbalimbali za mikopo na uwezeshaji zinazotolewa na Serikali pamoja na taasisi za fedha ili waweze kunufaika kwa kujikwamua kiuchumi.

“Fursa za mikopo zipo, ni wajibu wa wananchi kuwa na shughuli rasmi na halali, kufanya kazi kwa umoja au kupitia vikundi, ili Serikali na wadau wa maendeleo ikiwemo Benki ya NMB waweze kuwawezesha na kuwainua kiuchumi, pia epukeni mikopo umiza hiyo itawarudisha nyuma kimaendeleo,” alisema Mhe. Kasilda.

Aidha, aliwakumbusha wachimbaji wa madini kufuata sheria na taratibu za uchimbaji, ikiwemo kulinda mazingira kwa kufukia mashimo baada ya kumaliza shughuli za uchimbaji, hatua inayolenga kuhakikisha uchimbaji unaendeshwa kwa usalama na kwa manufaa ya wote.

Kwa upande wake, Meneja wa Benki ya NMB Kanda ya Kaskazini,Ndg. Baraka Ladislaus alisema benki hiyo imedhamiria kufanya mapinduzi katika sekta ya madini kwa kuwainua wachimbaji wadogo wadogo.

Alibainisha kuwa NMB imetenga fedha kwa ajili ya kuwawezesha wachimbaji kwa kutoa mitaji na vifaa, lengo likiwa ni kuhakikisha sekta hiyo inakua zaidi na inachangia maendeleo ya kiuchumi kwa wananchi.

Naye mnufaika wa mkopo huo, Bw. Juma Moses, aliishukuru Benki ya NMB kwa kushirikiana na Serikali ya Wilaya ya Same kwa kumuwezesha kupata mtambo huo na kueleza kuwa mtambo unaenda kubadilisha uchumi na kuongeza tija katika sekta ya madini kwa wachimbaji wadogowadogo katika eneo la Makanya.

I Inakuja hivi karibuniii
07/01/2026

I Inakuja hivi karibuniii

09/12/2025
Hongera sana mwenyekiti wa awali na mtarajiwa
01/12/2025

Hongera sana mwenyekiti wa awali na mtarajiwa

Address

Ngusero/manzese
Same

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Ombiney Digital posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Ombiney Digital:

Share

Category