09/12/2022
Tume ya Ushindani Tanzania (FCC) imewataka wazalishaji kuhakikisha bidhaa wanazozalisha ndani zinakidhi viwango lakini pia zinavutia wanunuzi hali itakayopelekea kuokoa matumizi ya fedha za kigeni, kuvutia wawekezaji nchini, kuongeza ajira kwa watanzania na kumlinda mlaji.
Hayo ameyasema Mkurugenzi Mkuu wa Tume ya Ushindani Tanzania, William Erio wakati wa maonesho ya saba ya bidhaa za viwanda vya Tanzania yaliyoenda sambamba na kauli mbiu inayosema 'Nunua bidhaa za Tanzania, Jenga Tanzania', katika uwanja wa maonesho wa Mwl. J. K. Nyerere jijini Dar es salaam
"Kwa kufanya hivyo watafanya bidhaa za Tanzania kuwa nyingi na hata fedha za kigeni ambazo serikali inatumia katika kuagiza bidhaa kutoka nje ya nchi zikatumika kwa matumizi mengine ambayo hayapatikani hapa nchini k**a teknolojia yake ni kubwa bado haijafika na hivyo kuokoa matumizi ya fedha za kigeni na kuongeza ajira kwa watanzania kwasababu viwanda hivi lazima viajiri watu watakaofanya kazi"
Erio amesema Katika shughuli ya uzalishaji, kuna njia ya kupata mtaji kwa urahisi na teknolojia mpya inayoambatana na mtaji huo ambapo unaweza kupata kwa kuungana na kampuni nyingine na kuongeza uzalishaji ulionao lakini pia kuwashirikisha FCC ili mawazo hayo yaweze kupitishwa na kupelekea kufikia lengo la kutanua soko.
"Katika kufanya biashara unaweza ukahitaji nyongeza ya mtaji, au aina mpya ya teknolojia ambayo itakuwezesha biashara yako iwe nzuri zaidi ni lazima wakakope benki, unaweza ukapata mtaji mpya na teknolojia mpya kwa kuungana na kampuni nyingine ambapo hiyo ni kazi yetu FCC kuhakikisha kwamba katika mazingira k**a hayo mtu akipata muwekezaji anataka kupanua biashara yake au kuleta teknolojia anaweza akaja FCC tukamuwezesha kwa kupitisha mawazo yake na kumuwezesha kufikia hatua hiyo"
Pia Erio amesema wamekuwa wakitoa elimu husika kwa kuwafikia wazalishaji wakiwemo watu wenye ulemavu kwa kufanya ziara mbalimbali, kuwapa semina na kuwahamasisha kushiriki katika maonesho mbalimbali nchini.