
30/07/2025
Klabu ya Pamba Jiji, ya jijini Mwanza leo tarehe 30 Julai, 2025 kupitia taarifa yao iliyocahpushwa kwenye kurasa zao za mitandao ya kijamii imemtangaza Francis Baraza k**a kocha wake mkuu kwa msimu ujao ikiwa ni siku chache tangu timu hiyo itemane n la aliyekuwa kocha wake msimu wa 2024/2025, Mwalimu Fredy Felix Minziro.
"Pamba imepata bahati ya kuwa na kocha wa mpira wa miguu, zipo timu zinaleta watalii, ligi itakapoanza tutakuja tuulizane kwa nini sisi tulileta kocha wa mpira na wengine wanaleta watalii" - Moses William, Msemaji wa klabu ya Pamba Jiji akizungumza na wanahabari leo.