
07/10/2025
Kampuni ya mawasiliano ya kwa kushirikiana na huduma za kifedha za kidijitali Mixx, imeungana na wadau mbalimbali wa michezo katika kuunga mkono mbio za Lake Victoria Half Marathon zilizofanyika jijini Mwanza, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuchangia maendeleo ya jamii na kuendeleza michezo nchini.
Akizungumza wakati wa hafla hiyo, Kaimu Mkurugenzi wa Yas kanda ya ziwa, Ndg. Robert Sanyagi, alisema mbio hizo hazikulenga tu ushindani wa riadha, bali zilikuwa na dhamira pana zaidi ya kusaidia watoto njiti katika hospitali za rufaa za sekou toure na bugando, ambao huhitaji uangalizi maalum ili waweze kukua na kufanikisha ndoto zao.
kwa upande wake, mratibu wa mbio za lake victoria half marathon, bi. hilda vigo, aliishukuru yas na mixx kwa mchango wao mkubwa katika kufanikisha mbio hizo, akisema ushirikiano wa sekta binafsi ni nguzo muhimu katika kukuza michezo nchini.