Jambo FM Tanzania

Jambo FM Tanzania The official page for Jambo FM Radio

Ukurasa rasmi wa Jambo FM Radio


📻 92.7 Shinyanga
(1)

14/11/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ameungana na wabunge wa Bunge la 13 kuwakumbuka watanzania waliopoteza maisha yao kwenye vurugu zilizojitokeza siku ya Oktoba 29.

Hayo yamejili leo Novemba 14,2025 Bungeni Jijini Dodoma wakati akilihutubia Bunge hilo la 13.

14/11/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan alivyowasili katika viwanja vya Bunge Jijini Dodoma kuhutubia na kufungua Bunge la 13 leo Novemba 14,2025

13/11/2025

Baada ya kupitishwa na wabunge wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania leo Novemba 13,2025 Waziri Mkuu Mteule Dkt. Nchemba amewaonya watumishi wa umma wazembe, wavivu na wala rushwa kujiandaa kukumbana na hatua kali mara baada ya kuanza rasmi majukumu yake.

Dkt Mwigulu Lameck Nchemba, mzaliwa wa Iramba, Singida , Tanzania  aliyeidhinishwa na bunge kwa kura 369 kati ya 371 zil...
13/11/2025

Dkt Mwigulu Lameck Nchemba, mzaliwa wa Iramba, Singida , Tanzania aliyeidhinishwa na bunge kwa kura 369 kati ya 371 zilizopigwa na Wabunge baada ya kuteuliwa na Rais Dkt Samia Suluhu Hassan kuwa Waziri Mkuu wa 12 wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania anajulikana k**a mchumi kitaaluma, mwenye uzoefu katika masuala ya fedha, uchumi wa maendeleo, na sera za umma, aliyewahi kuhudumu Benki Kuu ya Tanzania (BoT) na amekuwa miongoni mwa wanasiasa vijana waliopanda vyeo haraka kutokana na uwezo wa kitaaluma na utendaji wake serikalini.

Vilevile amehudumu kwenye Nafasi ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) k**a Mjumbe wa Halmashauri Kuu ya Taifa (NEC) – CCM, Mjumbe wa Kamati Kuu (CCM) – nafasi ya juu katika chama inayohusisha maamuzi ya kitaifa na kuhusika katika k**ati za sera na uchumi ndani ya chama kutokana na taaluma yake ya uchumi.

13/11/2025

Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemteua Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Jina la Mbunge huyo wa Iramba Magharibi limewasilishwa Bungeni na Mpambe wa Rais (ADC) Brigedia Jenerali Nyamburi Mashauri kwa ajili ya Bunge kumthibitisha kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muuungano wa Tanzania leo Novemba 13, 2025.

11/11/2025

Mbunge wa Kigoma Mjini Clayton Revocatus (Baba Levo) ajichanganya wakati akila kiapo Bungeni leo Novemba 11,2025 Jijini Dodoma.

11/11/2025

Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, M***a Azzan Zungu ameapa rasmi leo Novemba 11,2025 kuliongoza Bunge hilo la 13 baada kupata ushindi wa kura 378.

Ushindi huo umetangazwa na Katibu wa Bunge Baraka Leonard ambapo amesema matokeo hayo yamethibitishwa kwa kusaini kwa baadhi ya wagombea na wasimamizi wao, ikumbukwe kuwa Mhe. Zungu anakuwa Spika wa Tisa kuliongoza Bunge hilo.

11/11/2025

Wabunge wateule wakiwasili Bungeni kushiriki Bunge la 13 la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambapo leo Novemba 11,2025 linaanza rasmi vikao vyake kwa kufanyika kwa kikao cha kwanza cha mkutano wa kwanza wa Bunge hilo.

Kazi kubwa inayotarajiwa kufanyika leo ni uchaguzi wa Spika na Naibu Spika wa Bunge.

11/11/2025

Mbunge mteule wa jimbo la Meatu kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Salum Khamis Salum akiwasili Bungeni Jijini Dodoma kuhudhuria Bunge la 13, Mkutano wa kwanza kikao cha 1 akiwa ameambatana na Mbunge wa Shinyanga Mjini Patrobas Katambi.

10/11/2025

Jumla ya watuhumiwa 114 waliok**atwa wilayani Ilemela mkoani Mwanza kati ya Oktoba 28 na 29, 2025 wamefikishwa katika Mahak**a ya Wilaya ya Ilemela wakikabiliwa na mash*taka mbalimbali ikiwemo kula njama na uhaini.
 
Washtakiwa hao wamesomewa hati za mashtaka yao leo Jumatatu Novemba 10, 2025 kuanzia saa 7 mchana hadi saa 10 jioni katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Buswelu, mbele ya Mahakimu Wakazi Wakuu Christian Mwalimu na Stella Kiama.
 
Watuhumiwa hao wameshtakiwa katika kesi tatu tofauti — kesi ya kwanza ikiwa na watuhumiwa 22, kesi ya pili 64, na kesi ya tatu 28 — ambapo upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Mawakili wa Serikali Mwandamizi Mwanahawa Changale na Safi Amani wakisaidiwa na Adam Murusuli. Upande wa utetezi uliwakilishwa na mawakili tisa kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) wakiongozwa na Erick M***a.
 
Mahak**a ilielezwa kuwa washtakiwa wote hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na mahak**a hiyo kukosa mamlaka ya kusikiliza mashauri ya aina hiyo, huku makosa yote yakiwa hayana dhamana hivyo washtakiwa wote wataendelea kuwa rumande wakati upelelezi ukiendelea.
 
Katika kesi hizo, upande wa utetezi uliibua hoja tano ukitaka Mahak**a iielekeze Jamhuri kuzifanyia kazi haraka kabla ya tarehe nyingine ya kutajwa kwa mashauri hayo, ikiwemo ombi la kuwapatia matibabu watuhumiwa wenye maradhi na kuwapatia nguo na viatu wale wasiokuwa navyo.
 
Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Mkazi Mkuu Christian Mwalimu aliagiza Mkuu wa Gereza la Butimba kuwapeleka hospitalini watuhumiwa tisa na kuwasilisha ripoti za kitabibu mahak**ani siku ya kutajwa kwa kesi, pamoja na kuhakikisha washtakiwa wote wanapatiwa mavazi na viatu.
 
Naye Hakimu Mkazi Mkuu Stella Kiama aliagiza jeshi la Magereza kuhakikisha watuhumiwa wanapata haki zao wakiwa chini ya ulinzi, wakiwemo kuonana na ndugu zao kwa kufuata utaratibu uliowekwa na vyombo vya usalama.

Hata hivyo Washtakiwa wote wamerudishwa rumande hadi Novemba 24, 2025 kesi hizo zitakapotajwa tena.

✍️ Melkizedeck Anthony.

08/11/2025

MAN OF THE MATCH ⚽️

Baada ya mechi kati ya Pamba Jiji FC dhidi ya Singida Black Stars kumalizika hapa 106.9 Mwanza kwa matokeo ya bao 1 - 1, huyu hapa nyota wa mchezo kiungo kutokea Pamba Jiji FC, kelvin Nashon.



28/10/2025

Mgombea urais wa Tanzania kwa tiketi ya CCM, Dkt. Samia Suluhu Hassan amewaomba wananchi wote wajitokeze kwa wingi kwenda kupiga kura kesho Oktoba 29.

Pia amesema Serikali imetangaza rasmi siku hiyo itakuwa ni siku ya mapumziko kitaifa kwa lengo la kupisha upigaji wa kura.

Ameyasema hayo kwenye uhitimishaji wa kampeni za CCM jijini Mwanza.

Address

P. O. BOX 71
Shinyanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jambo FM Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jambo FM Tanzania:

Share

Category