Jambo FM Tanzania

Jambo FM Tanzania The official page for Jambo FM Radio

Ukurasa rasmi wa Jambo FM Radio


πŸ“» 92.7 Shinyanga
(1)

17/01/2026

Jeshi la Polisi Mkoani Mwanza, linamshikilia Seke Mabirika Sesila, (45) mkazi wa kitongoji cha Tinda,kata ya Mwamabanza, wilaya ya Magu,kwa tuhuma za mauaji ya mke wake aitwaye Rahel Samwel (39) mkulima na mkazi wa kitongoji cha Tinda ,kata ya Mwamabanza, aliyeuawa kwa kushambuliwa kwa ngumi na mateke sehemu mbalimbali za mwili wake.

Akitoa taarifa hiyo K**anda wa Polisi mkoani humo, Wilbroad Mutafungwa amesema tukio hilo lilitokea Januari 15, 2025 baada ya kutokea kwa ugomvi wa kifamilia baina yao.

"Mtuhumiwa alimshambulia mke wake ambaye alikuwa na ujauzito wa miezi miwili kwa mateke na ngumi sehemu mbalimbali za mwili wake ikiwemo tumboni hali iliyosababisha kupoteza nguvu na hatimae kufariki dunia", amesema

✍️ Melkizedeck Anthony.

16/01/2026

Televisheni ya taifa ya Cuba imerusha matangazo ya moja kwa moja Alhamisi asubuhi yakionyesha kurejeshwa kwa mabaki ya miili ya raia 32 wa Cuba, waliopoteza maisha katika mashambulizi ya Marekani nchini Venezuela.

Mashambulizi hayo yalitokea alfajiri ya tarehe 3 Januari, wakati wa operesheni iliyolenga kumk**ata rais wa Venezuela aliyeondolewa madarakani, NicolΓ‘s Maduro.

Miili hiyo iliwasili ikiwa kwenye masanduku madogo, yakiwa yamefunikwa kwa bendera ya taifa la Cuba, ishara ya heshima kwa waliopoteza maisha.

Ikumbukwe kuwa kwa miaka mingi Cuba imekuwa ikituma raia wake wengi kwenda Venezuela, hususan maafisa usalama na majasusi, walimu na madaktari, huku Venezuela ikipeleka mafuta ya petroli nchini Cuba. Hata hivyo, Rais wa Marekani, Donald Trump mara baada ya kumk**ata rais wa Venezuela, Nicolas Maduro amesitisha uingizwaji wa mafuta nchini Cuba kutokea Venezuela.

✍️

16/01/2026

Kaimu Katibu Mkuu wa Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU) Wandiba Kongoro ameeleza namna ambavyo kumeibuka upya wimbi la viongozi wa kisiasa kuwadhalilisha watumishi wa umma hususani katika ziara za ukaguzi wa miradi ya maendeleo zinazoambatana na vyombo vya habari kwa kuwaita wezi au wazembe hadharani.

Kauli hiyo imetolewa Jijini Dodoma mbele ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Ajira na Mahusiano Mhe. Deus Sangu wakati akifungua kikao cha 31 cha baraza kuu la Chama cha Wafanyakazi wa Serikali za Mitaa Tanzania (TALGWU).

✍️ Gideon Gregory.

15/01/2026

Unamuona wapi Sir Nature kwenye uongozi ikiwa angechagua kukomaa na siasa?

Hapa anaeleza alivyokutana na hadi kujiunga na TMK wanaume family.

Tumekuwekea Interview hii kwa urefu kupitia chaneli yetu ya youtube "Jambo FM Radio Tanzania" karibu kutazama.

🎀
πŸŽ₯

15/01/2026

"Msanii unatakiwa uhame usibaki kwenye muziki wa aina moja kwa sababu hata kwaito mimi niliimba moja tu, hakuna kulala" - Juma Nature akitoa mtazamo wake kuhusu muziki wa amapiano unaofanywa na wasanii wa Bongo fleva hivi sasa.

Tumekuwekea Interview hii kwa urefu kupitia chaneli yetu ya youtube "Jambo FM Radio Tanzania" karibu kutazama.

🎀
πŸŽ₯

15/01/2026

Juma Nature anafunguka sababu ya kuvunjika kwa kundi la TMK Wanaume Family na kupelekea kuzaliwa kwa Wanaume Halisi na TMK Wanaume Family.

Tumekuwekea Interview hii kwa urefu kupitia chaneli yetu ya youtube "Jambo FM Radio Tanzania" karibu kutazama.

🎀
πŸŽ₯

15/01/2026

Mkuu wa mkoa wa Simiyu, Anamringi Macha ameshangazwa na mahudhurio ya chini ya wanafunzi wa kidato cha kwanza katika Shule ya sekondari ya wasichana Simiyu iliyopo Kata ya Dutwa wilayani Bariadi mkoani Simiyu Hali ambayo imemlazimu kutoa siku tatu (3) kwa wazazi ambao watoto wao wamechaguliwa kujiunga masomo shuleni hapo kuhakikisha wanawapeleka kabla nafasi zao hawajapewa watoto wengine ambao wanahitaji elimu kutoka shuleni hapo

Macha ameyasema hayo akiwa katika ziara yake ya kikazi na kukagua maendeleo ya Shule hiyo licha ya kuridhishwa na Shule hiyo amewataka wanafunzi ambao wamefika shuleni hapo kujipatia elimu kuhakikisha wanabaki Salama kwa kuzingatia elimu wanayopatiwa na kujiepusha na vishawishi vinavyoweza kukatisha ndoto zao.

✍️ Saada Almasi.

13/01/2026

Msanii wa muziki Hamis Ramadhani H Baba ametangaza rasmi kuwasamehe watu wote aliokuwa akiwadai awali, akisema ameamua kuweka pembeni tofauti na kuanza ukurasa mpya wa maisha yake.

H Baba amesema msamaha huo unatokana na kutambua umuhimu wa amani ya moyo na kuishi bila chuki, akisisitiza kuwa hana tena nia ya kubeba mzigo wa migogoro ya zamani.

Ameeleza kuwa ni kweli kulikuwa na baadhi ya wasanii aliokuwa anawadai kwa sababu mbalimbali, hata hivyo kuanzia sasa amewasamehe wote bila masharti. H Baba amesisitiza kuwa hatasikika tena akiwazungumzia wala kufufua mada hizo, badala yake ataelekeza nguvu zake kwenye kazi zake za muziki na kujenga mahusiano mazuri ndani ya tasnia.

✍️ Melkizedeck Anthony.

12/01/2026

Msanii wa muziki H Baba pamoja na mzazi mwenzake Flora Mvungi wameweka wazi msimamo wao kuhusu suala la kurudiana, wakieleza kuwa kwa sasa kila mmoja anaheshimu maamuzi ya mwenzake bila kulazimishana. Wakizungumza kwa nyakati tofauti, wameeleza kuwa licha ya yaliyopita, wameamua kudumisha heshima na mawasiliano mema kwa ajili ya amani na ustawi wa familia yao.

Wameongeza kuwa wataendelea kuwa wamoja k**a wazazi kwa lengo la kuwalea, kuwalinda na kuwapatia watoto wao malezi bora yenye upendo. Kuhusu uwezekano wa kurudiana, H Baba na Flora wamesema suala hilo ni mipango ya Mungu, na endapo litatokea basi litakuwa kwa wakati wake, huku kwa sasa wakitanguliza wajibu wao wa msingi k**a wazazi na mustakabali wa watoto wao.

✍️ Melkizedeck Anthony.

Mtaa wako noma? K**a unauaminia mtaa wako na unaamini ni noma kuliko wengine basi  hakikisha unaisikiliza Jambo FM Juman...
12/01/2026

Mtaa wako noma? K**a unauaminia mtaa wako na unaamini ni noma kuliko wengine basi hakikisha unaisikiliza Jambo FM Jumanne hii kuanzia saa sita kamili mchana kupitia Ugali Pro Max.

Hosts:

Address

P. O. BOX 71
Shinyanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jambo FM Tanzania posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jambo FM Tanzania:

Share

Category