10/11/2025
Jumla ya watuhumiwa 114 waliok**atwa wilayani Ilemela mkoani Mwanza kati ya Oktoba 28 na 29, 2025 wamefikishwa katika Mahak**a ya Wilaya ya Ilemela wakikabiliwa na mash*taka mbalimbali ikiwemo kula njama na uhaini.
Washtakiwa hao wamesomewa hati za mashtaka yao leo Jumatatu Novemba 10, 2025 kuanzia saa 7 mchana hadi saa 10 jioni katika Kituo Jumuishi cha Utoaji Haki Buswelu, mbele ya Mahakimu Wakazi Wakuu Christian Mwalimu na Stella Kiama.
Watuhumiwa hao wameshtakiwa katika kesi tatu tofauti — kesi ya kwanza ikiwa na watuhumiwa 22, kesi ya pili 64, na kesi ya tatu 28 — ambapo upande wa Jamhuri uliwakilishwa na Mawakili wa Serikali Mwandamizi Mwanahawa Changale na Safi Amani wakisaidiwa na Adam Murusuli. Upande wa utetezi uliwakilishwa na mawakili tisa kutoka Chama cha Wanasheria Tanganyika (TLS) wakiongozwa na Erick M***a.
Mahak**a ilielezwa kuwa washtakiwa wote hawakutakiwa kujibu chochote kutokana na mahak**a hiyo kukosa mamlaka ya kusikiliza mashauri ya aina hiyo, huku makosa yote yakiwa hayana dhamana hivyo washtakiwa wote wataendelea kuwa rumande wakati upelelezi ukiendelea.
Katika kesi hizo, upande wa utetezi uliibua hoja tano ukitaka Mahak**a iielekeze Jamhuri kuzifanyia kazi haraka kabla ya tarehe nyingine ya kutajwa kwa mashauri hayo, ikiwemo ombi la kuwapatia matibabu watuhumiwa wenye maradhi na kuwapatia nguo na viatu wale wasiokuwa navyo.
Baada ya kusikiliza hoja hizo, Hakimu Mkazi Mkuu Christian Mwalimu aliagiza Mkuu wa Gereza la Butimba kuwapeleka hospitalini watuhumiwa tisa na kuwasilisha ripoti za kitabibu mahak**ani siku ya kutajwa kwa kesi, pamoja na kuhakikisha washtakiwa wote wanapatiwa mavazi na viatu.
Naye Hakimu Mkazi Mkuu Stella Kiama aliagiza jeshi la Magereza kuhakikisha watuhumiwa wanapata haki zao wakiwa chini ya ulinzi, wakiwemo kuonana na ndugu zao kwa kufuata utaratibu uliowekwa na vyombo vya usalama.
Hata hivyo Washtakiwa wote wamerudishwa rumande hadi Novemba 24, 2025 kesi hizo zitakapotajwa tena.
✍️ Melkizedeck Anthony.