Dreams Tz

Dreams Tz Telling untold stories, opinions, innovation, news and trending topics, seven days a week.
(2)

06/08/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Grace Darabe, Cyprix Smoker

30/07/2025

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Ally Ommy, Saiduna Gama, Ibrahim Keira

Lassine Kouma 8⃣ ➑️ πŸ”°
25/07/2025

Lassine Kouma 8⃣ ➑️ πŸ”°

SIMBA YAMNASA RUSHINE DE REUCK KUTOKA MAMELODI SUNDOWNSDar es Salaam, Tanzania – Julai 21, 2025β€” Klabu ya Simba SC imefa...
25/07/2025

SIMBA YAMNASA RUSHINE DE REUCK KUTOKA MAMELODI SUNDOWNS

Dar es Salaam, Tanzania – Julai 21, 2025β€” Klabu ya Simba SC imefanikiwa kumsajili beki wa kati wa Afrika Kusini, Rushine De Reuck, kutoka Mamelodi Sundowns kwa mkataba wa mwaka mmoja, ukiambatana na kipengele cha kuongeza mwaka mwingine kulingana na makubaliano ya pande zote.

Kwa mujibu wa tovuti ya Transfermarkt, thamani ya mchezaji huyo mwenye umri wa miaka 29 inakadiriwa kufikia Pauni 650,000 (sawa na zaidi ya Shilingi Bilioni 1.67 za Kitanzania).

Rushine De Reuck ameweka historia akiwa na Mamelodi Sundowns kwa kutwaa mataji 8
, ambapo 5 kati ya hayo ni ya Ligi Kuu ya Afrika Kusini (PSL), jambo linalomfanya kuwa miongoni mwa wachezaji wenye uzoefu mkubwa wa mafanikio.

Usajili wake unaleta matumaini makubwa kwa mashabiki wa Simba SC ambao wanatarajia kuona uimara zaidi katika safu ya ulinzi kuelekea msimu ujao wa Ligi Kuu Tanzania Bara na mashindano ya kimataifa.

Dreams Tz – Habari za Uhakika za Michezo, Siasa, Burudani na Jamii

ELIE MPANZU AGOMA KUREJEA SIMBA SC, ADAI MALIPO YA UHAMISHO NA AHADI YA GARIDar es Salaam, Tanzania Julai 24, 2025 Winga...
25/07/2025

ELIE MPANZU AGOMA KUREJEA SIMBA SC, ADAI MALIPO YA UHAMISHO NA AHADI YA GARI

Dar es Salaam, Tanzania Julai 24, 2025 Winga wa klabu ya Simba SC, Elie Mpanzu, ameripotiwa kugoma kurejea kambini kwa ajili ya maandalizi ya msimu mpya wa Ligi Kuu Tanzania Bara, akidai kutotimizwa kwa masharti kadhaa ya mkataba wake.

Kwa mujibu wa vyanzo vya karibu na mchezaji huyo, Mpanzu amesitisha kurejea klabuni hadi klabu hiyo itakapolipa kiasi cha dola 70,000 za Kimarekani (sawa na zaidi ya shilingi milioni 181 za Kitanzania) kinachodaiwa kuwa ni sehemu ya ada ya uhamisho kwenda klabu yake ya zamani, Aj Vancuer.

Mbali na hilo, nyota huyo pia anadai kuwa aliahidiwa gari la kifahari wakati akisajiliwa na Simba SC, ahadi ambayo hadi sasa haijatimizwa.

Sakata hili limezua hofu kwa mashabiki wa klabu hiyo, huku baadhi wakitoa wito kwa uongozi wa Simba SC kulimaliza suala hilo haraka ili kuepusha usumbufu kabla ya msimu kuanza rasmi. Mpanzu, ambaye alijiunga na Wekundu wa Msimbazi msimu uliopita, alionyesha kiwango kizuri kilichowavutia mashabiki wengi wa timu hiyo.

Uongozi wa Simba SC bado haujatoa tamko rasmi kuhusu madai hayo.

Dreams Tz – Kilele cha Habari za Michezo, Siasa na Jamii

Kiungo mahiri kutoka Guinea, Moussa Balla Conte, leo ametambulishwa rasmi kuwa mchezaji mpya wa Klabu ya Yanga SC akitok...
18/07/2025

Kiungo mahiri kutoka Guinea, Moussa Balla Conte, leo ametambulishwa rasmi kuwa mchezaji mpya wa Klabu ya Yanga SC akitokea CS Sfaxien ya Tunisia. Kupitia kurasa zake rasmi za mitandao ya kijamii, Yanga SC imethibitisha kuipata saini ya kiungo huyo ambaye anasifika kwa uwezo mkubwa wa kukaba, kupiga pasi za mwisho, pamoja na kusaidia safu ya ulinzi na ushambuliaji.

Usajili wa Conte ni habari njema kwa mashabiki wa Yanga, kwani unaongeza nguvu mpya katika kikosi kuelekea msimu mpya wa mashindano ya ndani na ya kimataifa, hasa katika harakati za kutetea mataji ya ligi na kufanya vizuri kwenye michuano ya CAF.

Hata hivyo, usajili wake uliwahi kuibua sintofahamu kubwa, huku ripoti zikidai kuwa alikuwa mbioni kujiunga na mahasimu wao wa jadi, Simba SC. Taarifa hizo zilieleza kuwa Conte alikuwa karibu kutua Msimbazi, jambo lililozua mijadala mikubwa mitandaoni. Hata hivyo, Yanga SC imeweka mambo hadharani kwa kumtambulisha rasmi kiungo huyo, na hivyo kuweka mwisho wa tetesi zote.

Conte sasa ni mali ya Wananchi, na mashabiki wa Yanga wana kila sababu ya kuwa na matumaini makubwa kwa msimu ujao kutokana na saini hii ya kimkakati.




Klabu ya Yanga imekamilisha usajili wa kiungo πŒπŽπ”π’π’π€ 𝐁𝐀𝐋𝐋𝐀 π‚πŽππ“π„ kutoka klabu ya CS Sfaxien ya nchini Tunisia. Umeuonaje...
18/07/2025

Klabu ya Yanga imekamilisha usajili wa kiungo πŒπŽπ”π’π’π€ 𝐁𝐀𝐋𝐋𝐀 π‚πŽππ“π„ kutoka klabu ya CS Sfaxien ya nchini Tunisia.

Umeuonaje Usajili Huu? Njoo Tuzungumze

https://youtu.be/zzOtJzwB6L8?si=I22xkwbHgfJ4lDw3Takwa letu la kwanza na la pili linahusu ukiukwaji wa kanuni uliofanyika...
09/06/2025

https://youtu.be/zzOtJzwB6L8?si=I22xkwbHgfJ4lDw3

Takwa letu la kwanza na la pili linahusu ukiukwaji wa kanuni uliofanyika Machi 8. Tunataka K**ati ya Uendeshaji na Usimamizi wa Ligi pamoja na CEO wa Bodi ya Ligi Almasi Kasongo wawajibike kwa kujiuzulu kwa kushindwa kusimamia kanuni na kuutia doa mpira wetu. Ligi yetu ni kubwa sana Afrika na inataka watu makini wenye weledi kuiongoza” Ally Kamwe - Meneja Habari na Mawasiliano Yanga SC.

Ally Kamwe πŸ—£._K**a Hatutalipwa Pesa yetu ya Komba la FA Msimu Uliopita Fainali saana Barua kwa Bodi Lakini Naona Tunapotezewa ...

Address

Singida

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dreams Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Dreams Tz:

Share