YOA MEDIA

YOA MEDIA Habari na matukio mkoani Singida

Na:  Yosia Emannuel HAMISI MOHAMED Maarufu kwa jina la Kimondo, ni mlewavu wa Miguu aliyekulia kwenye familia  ya wakuli...
11/03/2025

Na: Yosia Emannuel
HAMISI MOHAMED Maarufu kwa jina la Kimondo, ni mlewavu wa Miguu aliyekulia kwenye familia ya wakulima na wafugaji, Katika Tarafa ya Ndago wilayani Iramba mkoani Singida.

Ngano za Wasemi husema kuwa "Mungu akikupa ukilema anakupa na mwendo", Licha ya Ulemavu alionao Mr. Kimondo, Mungu amemjaalia kipawa cha ubunifu wa zana mbalimbali za Chuma kupitia Uhunzi, ambao unamsaidia kuingiza kipato cha kila siku, na kuendesha familia yake ya watoto nane.

Ulemavu wa miguu Umekuwa ni Changamoto Iliyompa fursa na Upekee katika Bunifu zake, ukilinganisha na wabunifu wengine, kwani anaeleza kuwa changamoto ya Ulemavu alionao ulimpa Fursa ya kubuni na kuunda Ndege inayotumia Upepo.

"Nilikuwa nasimamia mifugo mbugani, eneo ambalo lilikuwa na matope sana, Ilinipa tabu kutembea kwenye matope, hivyo ilinifanya nibuni NDEGE Inayotumia upepo AIRPLANE ✈️ ilí niwe naruka matope na kutua kwenye nchi kavu kwa uharaka bila kuhangaika sana" Ameeleza Mr. Kimondo”

Mbunifu huyu hakuishia hapo, bali katika makala hii anaieleza kwamba, amewahi pia kubuni baiskeli za walemavu, na kuwasaidia walemavu wengi wilayani Iramba, Na sasa Amebuni zaidi ya pikipiki tatu za miguu mitatu zinazo wasaidia watu wenye ulemavu.

Changamoto kubwa anayopitia katika shughuli zake ni kukosa mtaji wa kutosha kwaajili ya kununulia vifaa chuma pamoja na mtambo wa kufua vyuma kwaajili ya ubunifu,

Mbunifu huyu Anatueleza kuwa amekata tamaa kufuatilia mikopo ya Asilimia 10, inayotolewa na halmashauri kwaajili ya walemavu, kwasababu ya mizunguko mingi na Masharti magumu ya mikopo.

Mr. Kimondo (jina lake Maarufu) Bado anaamini kwamba anabunifu nyingi anazoweza kuzifanya na kuwasaidia wengi zaidi. anawaomba watanzania na Serikali kumshika mkono, ili aweze kupata mtaji wa kununua zana chuma, ambazo zitamsaidia kubuni zana mbalimbali, za kilimo pamoja na Usafiri kwa walemavu.

UNAWEZA KUWASILIANA NAYE MOJA KWA MOJA AU KUMCHANGIA CHOCHOTE KUPITIA NAMBA YA SIMU YA VODACOM 0749277227, Namba ya Usajili wa Line M-PESA ni MAGRETH MKUMBO.

Na: Yosia Emannuel HAMISI MOHAMED Maarufu kwa jina la Kimondo, ni mlewavu wa Miguu aliyekulia kwenye familia ya wakulima na wafugaji, Katika Tarafa ya Ndag...

11/02/2025

Minister of Natural Resources and Tourism in Tanzania Dr. Pindi Chana (Mb) has officially opened the Italian Designers Week Exhibition which shows the photos...

❤️
05/02/2025

❤️

07/11/2024

CEO Yoa Medía

07/11/2024
03/11/2024
TAASISI ZA USAMBAZAJI WA PEMBEJEO ZAPEWA SIKU 15 KUHAKIKISHA WAKULIMA WOTE WANAPATA PEMBEJEONa Yosia Emmanuel Mkuu wa wi...
01/11/2024

TAASISI ZA USAMBAZAJI WA PEMBEJEO ZAPEWA SIKU 15 KUHAKIKISHA WAKULIMA WOTE WANAPATA PEMBEJEO

Na Yosia Emmanuel

Mkuu wa wilaya ya Iramba Mh. Suleiman Yusufu mwenda, amezigiza taasisi zinazohusika na udhibiti na usambazaji wa mbolea pamoja mbegu, kuhakikisha pembejeo zinawafikia wakulima kwa wakati

Agizo hilo amelitoa katika kongamano la ufunguzi wa msimu wa kilimo linaloendelea Wilayani Iramba Mkoani Singida, ambapo ametoa siku 15 za usambazaji wa pembejeo hizo.
"Mpaka sasa pembejeo bado hazijawafikia wakulima, mimi pamoja na wakulima wangu nataka kabla ya tarehe 15, pembejeo ziwe zimewafikia wakulima" DC MWENDA

Godson Basinda ni mkaguzi wa mbegu kutoka taasisi ya kudhibiti ubora wa mbegu TOSCI amesema kuwa wamepokea agizo na tayari zoezi la usambazaji wa mbegu Unaendelea.
"Tumepokea agizo la mh. Dc, na tayari mpaka sasa zoezi la usambazaji wa mbegu linaendelea"

Naye mtaalamu kutoka taasisi ya usambazaji wa mbolea amewataka wananchi wa mkoa wa Singida kujitokeza kwa wingi katika zoezi la kujiandikisha ili kupata mbolea za ruzuku.

Kwa upande wao wananchi wa mkoa wa Singida wamepongeza juhudi za serikali kwa kuwaletea ruzuku ya mbegu pamoja na mbolea.

Katika mwaka wa kilimo 2024/2025,Wilaya ya Iramba inatarajia kuzalisha tani za chakula laki tatu na elf kumi na nane 318000/=.

Malengo ya uzinduzi wa kilimo ni kuelimisha wananchi na kuwapa mbinu bora za uzalishaji wa mazao ya chakula na mazao ya Biashara. Kaulimbiu ya Kongamano hilo ni UTALII NA UWEKEZAJI KATIKA KILIMO, UFUGAJI NA UVUVI SINGIDA INAWEZEKANA, SHIRIKI UCHAGUZI WA SERIKALI ZA MITAA KWA MAENDELEO YA KILIMO UFUGAJI NA UVUVI.
Wasafi TV

TAASISI ZA USAMBAZAJI WA PEMBEJEO ZAPEWA SIKU 15 KUHAKIKISHA WAKULIMA WOTE WANAPATA PEMBEJEOnNa Yosia Emmanuel Mkuu wa wilaya ya Iramba Mh. Suleiman Yusufu m...

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Elia Kingu, Amis Nkenge
27/06/2024

Shout out to my newest followers! Excited to have you onboard! Elia Kingu, Amis Nkenge

23/05/2024

Hii ni taarifa ya kustajabisha kidogo baada ya kupoteza Kwa Bwana Yohana Jonh Kingu takribani siku 15 sasa hajulikani alipo ambaye pia ni Katibu wa Chama ch...

22/05/2024

Mamia ya wachimbaji Mgodi wa Misigir Singida wajitokeza kumuaga kijana mwenzao M***a Orgeness (30) aliye fariki Kwa Ajali wakati anaingia shimoni May 20, 202...

Address

Misigiri, Iramba
Singida
43303

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when YOA MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share