Sn Tv Online

Sn Tv Online HABARI | MAKALA | MICHEZO | BURUDANI | SIMULIZI. Karibu kwenye ukurasa wetu rasmin. Youtube Link ?

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kik...
18/12/2021

Mwenyekiti wa Chama cha Mapinduzi CCM na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akiongoza Kikao cha Kawaida cha Halmashauri Kuu ya Taifa ya Chama Cha Mapinduzi CCM Kilichokutana leo tarehe 18 Desemba, 2021 katika Ukumbi wa Jakaya Kikwete mkoani Dodoma.

Katika Mwaka Mmoja wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kunamafanikio mbalimbali yaliyopatikana kati...
08/11/2021

Katika Mwaka Mmoja wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kunamafanikio mbalimbali yaliyopatikana katika kila Sekta
Miongozi wa Sekta hizo ni Wizara ya Elimu. https://youtu.be/QSsoBu83fng

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akilihutubia Taifa kwenye kilele cha mbio za Mwenge Ma...
14/10/2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akilihutubia Taifa kwenye kilele cha mbio za Mwenge Maalum wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 zilizofanyika leo Oktoba 14,2021 katika Uwanja wa Magufuli Wilayani Chato Mkoani Geita.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Cheti Kiongozi wa mbio za mwenge Maalum wa...
14/10/2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akimkabidhi Cheti Kiongozi wa mbio za mwenge Maalum wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 Luteni Josephine Paul Mwambashi kwa kutambua mchango wake mkubwa baada ya kuongoza kukimbiza Mwenge huo katika Mikoa yote ya Tanzania Bara na Visiwani, wakati wa  maadhimisho ya kilele cha Mwenge huo yaliyofanyika leo Oktoba 14,2021 katika Uwanja wa Magufuli Wilayani Chato Mkoani Geita.

Kiongozi wa mbio za Mwenge Maalum wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 Luteni Josephine Paul Mwambashi akikabidhi Mwenge Maalum w...
14/10/2021

Kiongozi wa mbio za Mwenge Maalum wa Uhuru Kitaifa mwaka 2021 Luteni Josephine Paul Mwambashi akikabidhi Mwenge Maalum wa Uhuru kwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Amiri Jeshi Mkuu wa Majeshi ya Ulinzi na Usalama Mhe. Samia Suluhu Hassan, baada ya kufikia kilele cha mbio za Mwenge huo Maalum kwa Mwaka 2021 leo Oktoba 14,2021 katika Uwanja wa Magufuli Wilayani Chato Mkoani Geita.

05/10/2021
RAIS DK. MWINYI: SMZ ITAENDELEA KUTHAMINI JITIHADA ZA WALIMU KATIKA KUWANDAA VIJANA WA KULITUMIKIA TAIFARais wa Zanzibar...
05/10/2021

RAIS DK. MWINYI: SMZ ITAENDELEA KUTHAMINI JITIHADA ZA WALIMU KATIKA KUWANDAA VIJANA WA KULITUMIKIA TAIFA

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk Hussein Ali Mwinyi amesema SMZ itaendelea kushirikiana na Chama cha Walimnu Zanzibar katika kutunga sera, sheria na utekelezaji wa mipango na mikakati kwa lengo la kuimarisha sekta ya Elimu Nchini.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla alieleza hayo kupitia hotuba aliyoisoma   kwa niaba ya Rais Dk. Mwinyi katika Maadhimisho ya Siku ya walimu Duniani yaliyofanyika katika viwanja vya kufurahishia watoto Tibirinzi Wilaya ya Chakechake Pemba.

Alisema Chama cha Walimu Zanzibar (ZATU) ni kiungo muhimu kinachofanya kazi ya kutetea maslahi ya walimu pamoja na kuwahimiza kutekeleza vyema majukumu yao kwa jamii na Taifa kwa ujumla.

Makamu wa Pili wa Rais alisema katika kuunga mkono jitihada hizo serikali itaendelea kuthamini jitihada na kazi kubwa inayofanywa na walimu kwa kuendelea kuwaanda vijana kitaaluma kwa kuwapa maarifa na malezi bora licha ya kukabiliwa na changamoto mbali mbali katika utekelezaji wa majukumu yao.

Aidha,Mhe. Hemed aliendelea kutoa wito kwa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar kufanya kazi kwa ukaribu zaidi na chama cha walimu Zanzibar (ZATU) kwa kuwa na vikao vya majadiliano na uhusiano mwema ili kuondokana na malalamiko ya Chama hicho kwa kuzitatua changamoto zinazowakabili.

Akizungumzia maslahi ya walimu Mhe. Hemed alisema kuwa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar imejipanga katika kuwapataia stahiki zao walimu pamoja na walimu wakuu na kuwataka kuendelea kuwa wavumilivu wakati Serikali ikilishughulikia suala hilo.

Katika maadhimisho hayo Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar alitumia fursa hiyo kuwaasa wazazi na walezi kuenelea kutoa mashirikiano katika suala la malezi ili kupunguza matendo ya udhalilishaji na unyanyasaji wa watoto ili kurudisha heshima na malezi bora kwa wanafunzi.

05/10/2021

Miongoni mwa Wananchi wa Shehia ya Kianga wakitoa maoni Yao kuhusu kuondoa janga la uzalilishaji

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea Mkuki na Ngao kutoka kwa Chifu Fundi Kira Mak...
08/09/2021

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan, akipokea Mkuki na Ngao kutoka kwa Chifu Fundi Kira Makamu Mwenyekiti wa Umoja wa Machifu Tanzania mara baada ya kusimikwa kuwa Mkuu wa Machifu wote Tanzania na kuitwa jina la Hangaya yani Nyota inayong`aa, katika Tamasha la Utamaduni (Mila na Desturi zetu) lililofanyika leo Sept,08,2021 katika Viwanja vya Redcross Kisesa Magu, Mkoani Mwanza

*Wanawake ni Waalimu wa jamii – Mama Zuhra* Mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mama Zuhra Kassim Ali, amesema j...
05/09/2021

*Wanawake ni Waalimu wa jamii – Mama Zuhra*
 

Mke wa Makamu wa Kwanza wa Rais wa Zanzibar Mama Zuhra Kassim Ali, amesema jitihada zinazooneshwa na wanawake wa kislamu hapa Zanzibar ni ishara kuwa jamii ya Wazanzibar wanaunga mkono jitihada za Serikali za kuleta maendeleo na ustawi wa jamii nchini na zitasaidia kuijenga jamii iliyo bora.
 
Mama Zuhra, ameyasema hayo leo huko Jumbi wilaya ya Magharibi ‘B’ Unguja, alipotoa salamu kwa wanawake wa kiislamu wa Madrasa ya Almujitahidina  iliyopo Jumbi  Uwandani, katika sherehe maalum zilizoandaliwa na madrasa hiyo za kuukaribisha mwaka mpya wa kiisalam wa 1443 Hijiria.
 
Amesema juhudi hizo za wanawake katika masuala mbali mbali ni muhimu sana katika kuchangia na kukuza jitihada za kuendeleza uislamu Zanzibar.
 
Aidha Mama Zuhra amesema kwamba amevutiwa sana na jitihada za wanawake wa madrasa hiyo za kujikwamua na utegemezi kwa kufanya shughuli mbali mbali za uzalishaji mali na maendeleo yao kwa lengo la kuondokana na umasikini.
 
Sambamba na kuunga mkono jitihada hizo, ameeleza kwamba ni muhimu kuendelezwa kwa juhudi kubwa, kwani zitasaidia kuwanyanyua kiuchumi wanawake na kuondokana na changamoto mbali mbali zinazowakabili katika kuendeleza maisha yao. 
 
“Wanawake wa madrasa hii  mumedhihirisha kwamba wanawake wa Zanzibar wanauwezo mkubwa wa kuisaidia jamii kuondokana na matatizo mbali mbali yakiwemo ya kifamilia,kiuchumi na kuijenga jamii iliyo bora".
 
Amesema pia madrsa hiyo tayari imeonesha kupata mafanikio ya kuibua vipaji mbali mbali k**a vile usomaji wa Quraan na hukumu zake, uoshaji maiti na mambo mengine mema, jambo ambalo ni muhimu katika harakati za kuendeleza mbele dini ya  kiislamu hapa Zanzibar.
 
Aidha Mama Zuhra ameridhia ombi la ulezi wa madrasa hio na kuwataka watambue kwamba Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, inathamini sana michango yao katika kuijenga jamii yenye amani na utulivu.
 
Pamoja na hayo Mama Zuhra ameahidi kushirikiana na wadau mbali mbali ikiwemo Serikali katika kutatua changamoto zinazoikabili madrasa hio ikiwemo ukarabati wa mabanda ya kusomea, umeme na kuongezewa mtaji wa fedha kwaajili ya kuendeleza shughuli za uzalishaji mali kwalengo la kujikimu.
 
Mapema kiongozi wa Madrasa h

Address

Mpendae Unguja Zanzibar
Stone Town

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sn Tv Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category