Tumainimedia

Tumainimedia Tumaini Media is Catholic Media Based in Tanzania

Askofu wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Southern Highlands- MBEYA, Jacob Kahemele, amewataka waumini na jamii kwa ujumla ...
07/06/2026

Askofu wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Southern Highlands- MBEYA, Jacob Kahemele, amewataka waumini na jamii kwa ujumla kutafuta na kuishi katika upendo wa Mungu badala ya kujikita katika migogoro na hila za shetani zinazolenga kuvuruga amani na umoja miongoni mwa watu.

Akihubiri katika Ibada Takatifu iliyofanyika Kanisa la Mtakatifu Agnes Yombo Vituka jijini Dar es Salaam leo, Askofu Kahemele amesema waumini wanapaswa kutenga muda wa kutafakari upendo wa Mungu na kuuenzi katika maisha yao ya kila siku ili kudumisha amani, utulivu na mazingira yanayowezesha kumtumikia Mungu na kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

Amesema shetani hutumia mambo madogo yanayotokea katika familia, jumuiya na jamii kuharibu mahusiano ya watu na kuvunja amani iliyopo, hivyo ni muhimu kwa Wakristo kutambua njama hizo na kuzikabili kwa kuishi katika upendo wa kweli.
Askofu Kahemele amesisitiza kuwa upendo wa Mungu si nadharia wala maneno matupu, bali ni jambo linalopaswa kuonekana kwa vitendo.



Viongozi Wastaafu wa Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (VIWAWA), Taifa walioongoza tangu 2023, wakiwa katika picha ya pamoja...
07/06/2026

Viongozi Wastaafu wa Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (VIWAWA), Taifa walioongoza tangu 2023, wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Mkutano wa Makabidhiano, uliofanyika Juni 6, 2026 Makao Makuu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Kurasini, Jumbo Kuu la Dar es Salaam.

Viongozi hao Wastaafu ni;
1.Leonard Mapolu-M/Kiti
2.Anna Kiyanga-M/M/Kiti
3.Benedicto Kiwia - Katibu
4.Veronica Paul-K/Msaidizi
5.Richard Kisusi-Mhazini
6.Ferdinand Sh*tobero-Mjumbe
7.Modesta Lyimo-Mjumbe

Wa pili kutoka kulia, Veronica Paul kutoka Jimbo Katoliki la Kigoma, ambaye alikuwa Katibu Msaidizi, amerejea tena kwenye uongozi mpya wa VIWAWA Taifa, akiwa k**a Makamu Mwenyekiti.



Taasisi ya Al -Hikma leo Jun 7,2026 imewafungisha ndoa za pamoja za  Vijana 130 wa Kiislamu Hafla hiyo imefanyika katika...
07/06/2026

Taasisi ya Al -Hikma leo Jun 7,2026 imewafungisha ndoa za pamoja za Vijana 130 wa Kiislamu
Hafla hiyo imefanyika katika Ukumbi wa Dycc Temeke Jijini Dar es Saalam ambapo vijana hao wamehudhuria kutoka maeneo mbalimbali ikiwa ni sehemu ya juhudi za taasisi hiyo kuwasaidia kutimiza ibada ya ndoa kwa mujibu wa mafundisho ya dini ya Kiislamu.



 Matukio katika picha ni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara katika Parokia ya Mtak...
07/06/2026



Matukio katika picha ni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti Takatifu ya Kipaimara katika Parokia ya Mtakatifu Nicholaus wa Tolentino - Msingwa, Jimbo Kuu la Dar es Salaam, jana Juni 6, 2026.

Misa hiyo Takatifu iliadhimishwa na Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa`ichi OFMCap, Askofu Mkuu wa Jimbo hilo.



 Askofu wa Jimbo Katoliki la Bagamoyo, Mhashamu Stephano Musomba OSA, akiongoza Ibada ya kubariki na kuzindua Tawi jipya...
07/06/2026



Askofu wa Jimbo Katoliki la Bagamoyo, Mhashamu Stephano Musomba OSA, akiongoza Ibada ya kubariki na kuzindua Tawi jipya la Benki ya Mkombozi iliyopo maeneo ya Marian - jimboni humo.

Uzinduzi huo wa Tawi jipya la Benki ya Mkombozi Bagamoyo, umehudhuriwa na Viongozi mbalimbali wa Mkombozi Benki, Mapadre, Watawa, Waamini walei pamoja na wageni waalikwa.



07/06/2026

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam, Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa'ichi amewata Waimarishwa kutoona aibu kusema kwamba wanamuungama Kristo katika maisha yao.

Askofu huyo ameyasema hayo Juni 6, 2026 wakati wa homilia yake katika Adhimisho la Misa Takatifu ya Sakramenti ya Kipaimara katika Parokia ya Mtakatifu Nicholaus wa Tolentino - Msingwa, jimboni humo.

Sambamba na hayo, Askofu Mkuu Ruwa'ichi ametoa wito kwa wazazi kushirikiana na watoto wao katika kuuendeleza utume huo unaowapasa.

Pia, amewasihimi Mapadri, Makatekista pamoja na Viongozi wa K**ati Tendaji, kuhakikisha wanashik**ana na kusindikizana hao katika safari ya kuujenga Ufalme wa Mungu.



Askofu Osório Citora wa Jimbo Katoliki la Quelimane, Msumbiji, amefariki dunia leo Juni 6, 2026 ndani ya makazi ya Maask...
06/06/2026

Askofu Osório Citora wa Jimbo Katoliki la Quelimane, Msumbiji, amefariki dunia leo Juni 6, 2026 ndani ya makazi ya Maaskofu, katika kile ambacho mamlaka zinakichukulia k**a kitendo kinachoshukiwa cha mauaji ya kikatili.

Kwa mujibu wa Aid to the Church in Need, Mmisionari huyo wa Consolata mwenye umri wa miaka 54 alipatikana katika korido ya makazi hayo akiwa na jeraha la risasi kifuani karibu na moyo.

Mazingira yaliyozunguka kifo chake bado hayajafahamika, na utambulisho wa mshambuliaji bado haujajulikana.

Askofu Mkuu Inácio Saure wa Nampula, ambaye pia ni Rais wa Baraza la Maaskofu nchini Msumbiji, alithibitisha kwamba Askofu huyo alipatikana amekufa, na katika hali za ajabu ambazo bado hazijafafanuliwa, akisisitiza kutokuwa na uhakika kuhusu kesi hiyo.

Katika hatua hiyo, wachunguzi wametoa maelezo machache, na nia ya shambulio hilo haijabainika.

Urais wa Msumbiji ulitoa taarifa inayoelezea “huzuni kubwa na mfadhaiko” kutokana na mauaji hayo.

Rais Daniel Chapo alielezea kifo cha Askofu Osório k**a “hasara isiyoweza kurekebishwa” kwa taifa na jamii ya Wakatoliki, akisisitiza kujitolea kwake kwa maisha yote kwa unyenyekevu, huduma ya kichungaji, na kukuza amani na maridhiano.

Mauaji hayo yanakuja wakati wa ukosefu wa utulivu unaoendelea katika sehemu za Msumbiji, hasa katika mkoa wa Kaskazini wa Cabo Delgado, ambapo vikundi vyenye silaha vimefanya mashambulizi ya mara kwa mara dhidi ya raia na miundombinu ya kidini.

Matukio ya hivi karibuni yamejumuisha uharibifu wa makanisa, majengo ya misheni, na shule, na kuzisumbua zaidi jamii ambazo tayari ziko katika mazingira magumu.

Msumbiji inabaki kuwa kitovu cha wasiwasi wa kibinadamu wa kimataifa wa Kikatoliki, huku mashirika k**a vile Aid to the Church in Need yakiunga mkono juhudi za kichungaji na ujenzi wa kijamii.

Msiba huo unaongeza changamoto zinazokabili Kanisa nchini humo ambalo linaendelea kufanya kazi, huku kukiwa na ukosefu wa usalama na vurugu za hapa na pale katika maeneo kadhaa.



06/06/2026

Je K**a kijana mkatoliki unafahamu viongozi wako wapya wa Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (VIWAWA), Taifa basi k**a huwafahamu wajue hapa kwa majina na sura zao.
Elia Patrick Mshana - Mwenyekiti
Veronica Paul - Makamu M/Kiti
Benedicto Chacha - Katibu
Patricia David - Katibu Msaidizi
Revocatus Miranzi - Mhazini
Sabina Ntandu - Mjumbe
Frank Yohana Buganda - Mjumbe
Alpha Joseph - Mjumbe.


Viongozi wapya wa Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (VIWAWA), Taifa wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Mkutano wa Makabi...
06/06/2026

Viongozi wapya wa Vijana Wakatoliki Wafanyakazi (VIWAWA), Taifa wakiwa katika picha ya pamoja baada ya Mkutano wa Makabidhiano, uliofanyika leo Juni 6, 2026 Makao Makuu ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania (TEC), Kurasini, Jumbo Kuu la Dar es Salaam.

Ikumbukwe kuwa hivi karibuni VIWAWA Taifa walifanya Uchanguzi Mkuu, na hivyo kuwapata Viongozi watakaoongoza Utume huo wa vijana hadi 2029.

Viongozi hao wapya ni;
1.Elia Patrick Mshana - Mwenyekiti
2.Veronica Paul - Makamu M/Kiti
3.Benedicto Chacha - Katibu
4.Patricia David - Katibu Msaidizi
5.Revocatus Miranzi - Mhazini
6.Sabina Ntandu - Mjumbe
7.Frank Yohana Buganda - Mjumbe
8.Alpha Joseph - Mjumbe



06/06/2026

Je unakumbuka nini ukisikiliza wimbo huu



Address

Kristo Mfalme Tabata
Tabata
9916

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 14:30
Sunday 08:00 - 14:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tumainimedia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tumainimedia:

Share

Category