Tumainimedia

Tumainimedia Tumaini Media is Catholic Media Based in Tanzania

10/05/2026

Ikiwa leo ni sikukuu ya akina Mama duniani Paroko Msaidizi wa Parokia ya Bikira Maria wafatima Msimbazi,Mario Dias OFMCap ameizindua na kuibariki Rozari kubwa lenye urefu wa mita 34 ikiwa ni sehemu ya kumkumbuka Mama bikira Maria ili watu watambue nguvu ya rozari katika kuleta amani na umoja.

10/05/2026

ASKOFU MKUU WA JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM, MHASHAMU SANA JUDE THADDAEUS RUWA’ICHI OFMCap, AKIWAPATIA VYETI VIJANA BAADA YA KUWAIMARISHA KWA SAKRAMENTI TAKATIFU YA KIPAIMARA WAKATI WA ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU KATIKA PAROKIA YA MTAKATIFU STEPHANO SHAHIDI - KISARAWE, JIMBONI HUMO, LEO MEI 10, 2026.

MISA HII TAKATIFU ILIKUWA ‘LIVE’ KUPITIA YOUTUBE YA TUMAINI TV KWA KUANDIKA TUMAINI_TV.



10/05/2026

ASKOFU MKUU WA JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM, MHASHAMU SANA JUDE THADDAEUS RUWA’ICHI OFMCap, AKITOA SAKRAMENTI TAKATIFU YA KIPAIMARA KWA VIJANA WA PAROKIA YA MTAKATIFU STEPHANO SHAHIDI - KISARAWE, JIMBONI HUMO, WAKATI WA ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU DOMINIKA YA LEO MEI 10, 2026.

MISA HII TAKATIFU IPO ‘LIVE’ MUDA HUU KUPITIA YOUTUBE YA TUMAINI TV KWA KUANDIKA TUMAINI_TV.



10/05/2026

ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU YA SAKRAMENTI YA KIPAIMARA, PAROKIA YA MTAKATIFU STEPHANO SHAHIDI - KISARAWE, JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM, KATIKA DOMINIKA YA LEO MEI 10, 2026.

MISA HII TAKATIFU IPO ‘LIVE’ MUDA HUU KUPITIA YOUTUBE YA TUMAINI TV KWA KUANDIKA TUMAINI_TV.



10/05/2026

KWAYA YA UKWAKATA YA PAROKIA YA MTAKATIFU STEPHANO SHAHIDI - KISARAWE, JIMBO KUU LA DAR ES SALAAM, IKIIMBA WAKATI WA ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU YA SAKRAMENTI YA KIPAIMARA PAROKIANI HAPO, KATIKA DOMINIKA YA LEO MEI 10, 2026.

MISA HII TAKATIFU IPO ‘LIVE’ MUDA HUU KUPITIA YOUTUBE YA TUMAINI TV KWA KUANDIKA TUMAINI_TV.



Ratiba ya soka leo Jumapili Mei 10, 2026Tanzania 🇹🇿 (NBC Premier League)14:00 KMC Vs Fountain Gate FC16:00 Pamba SC Vs D...
10/05/2026

Ratiba ya soka leo Jumapili Mei 10, 2026

Tanzania 🇹🇿 (NBC Premier League)
14:00 KMC Vs Fountain Gate FC
16:00 Pamba SC Vs Dodoma Jiji FC
19:00 Simba SC Vs Tanzania Prisons

England 🏴󠁧󠁢󠁥󠁮󠁧󠁿 Premier League
16:00 Burnley Vs Aston Villa
16:00 Crystal Palace Vs Everton
16:00 Nottingham Forest Vs Newcastle United
18:30 West Ham United Vs Arsenal

Spain 🇪🇸 LaLiga
15:00 Mallorca Vs Villarreal
17:15 Athletic Club Vs Valencia
19:30 Real Oviedo Vs Getafe
22:00 Barcelona Vs Real Madrid

Germany 🇩🇪 Bundesliga
16:30 Hamburger SV Vs Freiburg
18:30 FC Cologne Vs FC Heidenheim
20:30 Mainz 05 Vs Union Berlin

Italy 🇮🇹 Serie A
13:30 Hellas Verona Vs Como 1907
16:00 Cremonese Vs Pisa
16:00 Fiorentina Vs Genoa
19:00 Parma Vs AS Roma
21:45 AC Milan Vs Atalanta

France 🇫🇷 Ligue 1
22:00 AS Monaco Vs Lille
22:00 Angers Vs Strasbourg
22:00 Auxerre Vs Nice
22:00 Le Havre Vs Marseille
22:00 Metz Vs Lorient
22:00 PSG Vs Brest
22:00 Rennes Vs Paris FC
22:00 Toulouse Vs Lyon

✍️



Katika hali isiyokuwa ya kawaida, ni kuona wachezaji hasa wanaocheza timu moja kugombana kwa kupigana.Hivi karibuni Klab...
09/05/2026

Katika hali isiyokuwa ya kawaida, ni kuona wachezaji hasa wanaocheza timu moja kugombana kwa kupigana.

Hivi karibuni Klabu ya Real Madrid imewatoza faini ya jumla ya Euro milioni 1, wachezaji wake Federico Valverde na Aurélien Tchouaméni, sawa na takriban Shilingi bilioni 1.53 za Kitanzania kwa kila mmoja, kufuatia tukio la kupigana wakiwa kambini, jambo lililosababisha kufunguliwa kwa shauri la kinidhamu ndani ya klabu hiyo.

Katika taarifa yake, Real Madrid imeeleza kuwa wachezaji hao walionyesha majuto makubwa kwa tukio hilo, wakaombana msamaha, na pia kuomba radhi kwa klabu, wachezaji wenzao, benchi la ufundi na mashabiki, huku wakiahidi kushirikiana kikamilifu na klabu na kukubali adhabu yoyote itakayotolewa.

Kwa kufuata msimamo huo, uongozi umeamua kutoza faini hiyo na kufunga shauri hilo la ndani.

Katika historia ya Real Madrid tangu kuanzishwa kwake Machi 6, 1902, hii ndiyo adhabu kubwa zaidi iliyowahi kutolewa kwa wachezaji wake.

Mbali na adhabu hiyo ya kupigwa faini kwa kila mmoja, awali zilitoka tetesi kwamba huenda wachezaji hao wawili wakakosa mchezo mkubwa wa ‘derby’ ya Hispania kati ya FC Barcelona dhidi ya Real Madrid (maarufu El Clasico), unaotarajiwa kupigwa kesho Mei 10, 2026 kwanzia saa 4:00 usiku, licha ya kwamba klabu yenyewe bado haijathibitisha chochote kuhusu hilo hadi sasa.



09/05/2026

Mkuu wa Wilaya ya Ilala, Edward Mpogolo, amewataka wazazi na walezi kushiriki kikamilifu katika malezi na maendeleo ya elimu ya watoto wao kwa kuhudhuria vikao vya shule na kushirikiana na walimu kufuatilia maendeleo ya watoto hao.

Akizungumza katika Shule ya Zawadi iliyopo Tabata, jijini Dar es Salaam, Mpogolo amesema mafanikio ya mtoto yanategemea ushirikiano wa pande tatu ambazo ni Serikali, wazazi pamoja na jamii, na wanafunzi wenyewe.

Amesema Serikali ina jukumu la kuboresha miundombinu na kuhakikisha mazingira bora ya kufundishia na kujifunzia kupitia walimu, huku wazazi na jamii wakipaswa kusimamia malezi na kufuatilia mwenendo wa watoto wao. Aidha, wanafunzi wanapaswa kuwa na nidhamu, kuzingatia maadili mema na kuongeza bidii katika masomo yao.

“Tunapozungumzia mafanikio ya mtoto lazima tuzungumzie maeneo matatu makubwa. Serikali ina wajibu wake kupitia walimu, wazazi wana wajibu wao, na wanafunzi nao wanapaswa kuwa na nidhamu na bidii,” amesema Mpogolo.

Aidha, amesema changamoto kubwa inayojitokeza katika shule nyingi za serikali ni mwitikio mdogo wa wazazi wanapoitwa kuhudhuria vikao vya shule, tofauti na ilivyo katika shule binafsi ambapo wazazi wengi hujitokeza kwa wingi kufuatilia maendeleo ya watoto wao.

Mpogolo amesema baadhi ya wazazi huwatuma ndugu, wafanyakazi wa nyumbani au hata madereva wa bodaboda kuhudhuria vikao hivyo kwa niaba yao, jambo ambalo linaathiri mafanikio ya kitaaluma ya mwanafunzi kwa kuwa ushirikiano muhimu kati ya mzazi, mwalimu na mwanafunzi haukamiliki.

“Hivyo ushirikiano wa karibu kati ya wazazi, walimu na wanafunzi ni muhimu sana katika kuhakikisha mtoto anafanya vizuri kitaaluma na kimaadili,” ameongeza.

Amesema Halmashauri ya Jiji la Dar es Salaam imedhamiria kuimarisha ushiriki wa viongozi katika vikao vya wazazi ili kuongeza hamasa ya kufuatilia maendeleo ya wanafunzi.

“Mimi mwenyewe nitafika katika shule zitakazokuwa na vikao vya wazazi ili tuzungumzie maendeleo ya watoto wetu na namna ya kuboresha ufaulu wao,” amesema Mpogolo.

Wadau michezo na wanamichezo nchini wamehimizwa kutumia huduma za Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kwa ku...
09/05/2026

Wadau michezo na wanamichezo nchini wamehimizwa kutumia huduma za Wakala wa Usajili wa Biashara na Leseni (BRELA) kwa kusajili kazi zao za ubunifu na kujifunza kuhusu haki zao ili kuleta tija na ufanisi wa wanamichezo kwa kuwakomboa kiuchumi.

Wito huo umetolewa tarehe 08 Mei, 2026 na Waziri wa Viwanda na Biashara Mhe. Judith Salvio Kapinga wakati wa hotuba yake ya ufunguzi wa sherehe za maadhimisho ya siku ya Miliki Ubunifu Duniani iliyofanyika hoteli ya Hyatt Jijini Dar es Salaam.

Aidha, Mhe. Judith Kapinga alisema kuwa bado kuna kazi kubwa ya kufanya ili kuhahikisha wanamichezo na wadau wa sekta hiyo wanatumia Miliki Ubunifu kukuza tasnia ya michezo hapa nchini.

“Niwasihi viongozi wa vilabu vya michezo, mashirikisho na wadau wote wa michezo kuwasaidia wanamichezo katika vilabu na mashirikisho yenu kuhakikisha wanalinda haki zao ikiwemo matumizi ya picha au taswira zao katika bidhaa au biashara za watu wengine,’’ alisema Bi. Judith Kapinga.

Naye Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya Wizara kwa BRELA Prof. Neema Mori alisema ni muhimu wadau wa michezo wakajiepusha kabisa kutumia Miliki Ubunifu k**a vile Alama za biashara (logo) zisizo zao pasipo idhini ya wamiliki halisi ili kuepuka kuingia katika matatizo ya kisheria kwa kutumia Alama zilizosajiliwa na watu wengine.

Kwa upande wake Afisa Mtendaji Mkuu wa BRELA Bw. Godfrey Nyaisa aliwakumbusha wadau na wanamichezo kutumia majina yao vizuri ‘Brand Names’ kujiandaa na maisha mengine baada ya kustaafu michezo.

“Naomba nitoe mifano michache kwa wachezaji wa kimatiafa wanaoendelea kunufaika kwa kutumia Alama za Biashara ingawa wengine wameshajiuzulu michezo, Alama ya biashara (logo) ya CR7 inayomilikiwa na mchezaji wa mpira wa miguu Christiano Ronaldo ni Dola za Kimarekani Milioni 900,” alisema Bw. Nyaisa.

Kwa upande mwingine Mwenyeki wa Baraza la Michezo Tanzania (BMT) Mhandisi Leodigar Tenga alisema wakati taifa likiwa kwenye maandalizi ya AFCON 2027 ni vyema wafanyabiashara na wadau wote wa michezo wakahakikisha wamelinda bunifu zao ili kuepuka wizi na uharamia kwenye bidhaa na huduma kwa upande wa matumizi ya Alama (brands)

09/05/2026

Shuhudia Askofu Mkuu wa Jimbo kuu la Dar es Saalam Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa'ichi OFMCap alivyozindua ujenzi wa Kanisa Kuu Mbadala la Bikira Maria Mama wa Mungu (Theotokos), pamoja na kubariki eneo la ujenzi huo,



09/05/2026

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu la Dar es Salaam Mhashamu Sana Jude Thaddaeus Ruwa'ichi OFMCap lamezindua kitambu cha historia ya Kanisa kuu la Mtakatifu Josefu lililopo Posta

Address

Kristo Mfalme Tabata
Tabata
9916

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 14:30
Sunday 08:00 - 14:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tumainimedia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tumainimedia:

Share

Category