07/06/2026
Askofu wa Kanisa Anglikana Dayosisi ya Southern Highlands- MBEYA, Jacob Kahemele, amewataka waumini na jamii kwa ujumla kutafuta na kuishi katika upendo wa Mungu badala ya kujikita katika migogoro na hila za shetani zinazolenga kuvuruga amani na umoja miongoni mwa watu.
Akihubiri katika Ibada Takatifu iliyofanyika Kanisa la Mtakatifu Agnes Yombo Vituka jijini Dar es Salaam leo, Askofu Kahemele amesema waumini wanapaswa kutenga muda wa kutafakari upendo wa Mungu na kuuenzi katika maisha yao ya kila siku ili kudumisha amani, utulivu na mazingira yanayowezesha kumtumikia Mungu na kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.
Amesema shetani hutumia mambo madogo yanayotokea katika familia, jumuiya na jamii kuharibu mahusiano ya watu na kuvunja amani iliyopo, hivyo ni muhimu kwa Wakristo kutambua njama hizo na kuzikabili kwa kuishi katika upendo wa kweli.
Askofu Kahemele amesisitiza kuwa upendo wa Mungu si nadharia wala maneno matupu, bali ni jambo linalopaswa kuonekana kwa vitendo.