Tumainimedia

Tumainimedia Tumaini Media is Catholic Media Based in Tanzania

09/09/2025
Ratiba ya soka leo Jumanne Agosti 26, 2025African Nations Championship (CHAN)17:30 Madagascar Vs Sudan20:30 Morocco Vs S...
26/08/2025

Ratiba ya soka leo Jumanne Agosti 26, 2025

African Nations Championship (CHAN)
17:30 Madagascar Vs Sudan
20:30 Morocco Vs Senegal

(Imeandikwa na
)



Katika ukumbi wa VETA uliopo katikati ya Manispaa ya Iringa, maafisa na askari wa misitu walikusanyika leo, Agosti 25, 2...
26/08/2025

Katika ukumbi wa VETA uliopo katikati ya Manispaa ya Iringa, maafisa na askari wa misitu walikusanyika leo, Agosti 25, 2025, wakiwa na dhamira moja kuu: kuhakikisha misitu ya Nyanda za Juu Kusini inalindwa kwa kizazi cha sasa na kijacho.

Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) – Kanda ya Nyanda za Juu Kusini umefungua rasmi kikao kazi cha kuhuisha Daftari la Viashiria Hatarishi (Risk Register) kwa mwaka wa fedha 2025/2026. Ni kikao kinachoangalia si tu changamoto zilizopo, bali pia kinatabiri hatari zinazoweza kuathiri malengo ya uhifadhi na kuzitafutia suluhu mapema.

Akizungumza wakati wa kikao hicho, Mhifadhi Mkuu Daraja la Kwanza kutoka TFS Makao Makuu Dodoma, Marium Mrutu, alisema lengo kuu la mchakato huu ni kutambua mapema hatari zinazoweza kuathiri kufikiwa kwa malengo ya taasisi, kuzipima na kuweka mikakati ya kudhibiti au kupunguza madhara yake.

“Tunapopima hatari mapema, tunajipa nafasi ya kuzuia hasara kubwa. Hii ndiyo njia bora ya kulinda rasilimali za taifa na kuhakikisha misitu inawanufaisha Watanzania wote,” alisema.

Mafunzo haya pia yamewezeshwa na PCR Roland Peter Mlingi kutoka TFS Kanda ya Mashariki, ambaye alisisitiza umuhimu wa taasisi za umma kuimarisha Risk Register kila mwaka ili kuongeza uwajibikaji na kuimarisha utawala bora.

Kwa mujibu wa Mrutu, hatua hii ni zaidi ya utaratibu wa kiutawala. Ni dhihirisho la dhamira ya kulinda rasilimali za misitu kwa manufaa ya kijamii, kiuchumi na kimazingira. Hatua hii inalenga kuongeza uimara wa mifumo ya usimamizi wa misitu, kuhakikisha mapato ya serikali hayapotei, na kuendeleza ushirikiano na jamii zinazozunguka hifadhi.

Kikao hiki ni kielelezo cha namna ambavyo taasisi za umma zinavyoweza kujenga misingi ya uthabiti na utawala bora, zikihakikisha rasilimali adimu za taifa hazipotei mikononi mwa kizazi cha sasa, bali zinabaki salama kwa mustakabali wa vizazi vijavyo.



WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Agosti 25, 2025 ni mgeni rasmi katika kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 y...
25/08/2025

WAZIRI MKUU, Kassim Majaliwa leo Agosti 25, 2025 ni mgeni rasmi katika kongamano la kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Taasisi ya Elimu ya Watu Wazima inayofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Julius Nyerere jijini Dar es Salaam.

Lengo kuu la kongamano hilo ni kuhakikisha kuwa elimu ya watu wazima inakuwa chachu ya maendeleo ya kiuchumi, kijamii na kiteknolojia kwa nchini. Pia ni jukwaa la kubadilishana uzoefu, matokeo ya tafiti na mbinu bora zinazoweza kuendeleza ubunifu katika utoaji wa elimu ya watu wazima.

Kongamano hilo linalofanyika kuanzia leo tarehe Agosti 25, 2025 hadi Agosti 27, 2025 lina kaulimbiu isemayo Elimu Bila Ukomo kwa Maendeleo Endelevu."


RAIS MWINYI AKUTANA NA WANAFUNZI WATAKAOITEMBELEA  NASA, MAREKANI NA KUHUDHURIA HACKATHON, OMANRais wa Zanzibar na Mweny...
25/08/2025

RAIS MWINYI AKUTANA NA WANAFUNZI WATAKAOITEMBELEA NASA, MAREKANI NA KUHUDHURIA HACKATHON, OMAN

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi,Mhe. Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amesema kuwa Serikali itaendelea kuunga mkono juhudi za kuwaandaa vijana wengi zaidi wa Zanzibar kuwa wataalamu wa elimu ya anga.

Dkt. Mwinyi ameyasema hayo alipokutana na wanafunzi watano waliochaguliwa kutembelea makao makuu ya NASA yaliyopo Washington D.C., Marekani, pamoja na kushiriki katika mashindano ya NASA International Space Apps Challenge 2025 yatakayofanyika jijini Ibra, Oman. Mkutano huo umefanyika Ikulu Zanzibar leo tarehe 25 Agosti 2025.

Fursa hiyo imetokana na uwezo mkubwa waliouonesha waliposhiriki katika programu ya Kimataifa ya IASC (International Astronomical Search Collaboration) inayohusu uvumbuzi wa asteroids kwa kushirikiana na NASA (National Aeronautics and Space Administration) ya Marekani. Jumla ya wanafunzi 22 kutoka Taasisi ya Sayansi na Teknolojia Karume, Chuo Kikuu cha Taifa cha Zanzibar na Chuo Kikuu cha Abdulrahman Al-Sumait ambao walishiriki kwa utambulisho wa Zanzibar Space Team na kufanikiwa kugundua asteroids mpya kupitia picha za anga zinazotumwa na NASA kwa programu ya Astrometrica.

Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu na Mafunzo ya Amali, Khamis Abdulla Said, amewataja Majid Khalfan Omar, Nadhifa Mashaka na Is-haka Harith Salim kuwa watatembelea makao makuu ya NASA nchini Marekani, huku Mulhat Abdallah na Feisal Issa Minchoum wanatarajiwa kuhudhuria Hackathon nchini Oman.

Aidha kwa upande wake, Mkurugenzi wa Taasisi ya Royal Astronomy and Space Society, Bi. Amina Ahmad, amesema wanakusudia kuanzisha utalii wa anga Zanzibar pamoja na kuzindua programu maalum za mafunzo kwa wanafunzi kutoka skuli mbalimbali ili kujifunza taaluma hiyo.
Katika ziara hiyo inayotarajiwa kuanza Oktoba 2025, wanafunzi watapewa mafunzo kuhusu sayansi ya anga, uvumbuzi na teknolojia mbalimbali zitakazowawezesha kuimarika kitaalamu na kitaaluma.


ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU ZA KILA SIKU ASUBUHI.WEEK HII NI KUTOKA VIJIBWENI MISA ITAKUA LIVE INSTAGRAM:Tumaini_mediPIA ...
25/08/2025

ADHIMISHO LA MISA TAKATIFU ZA KILA SIKU ASUBUHI.
WEEK HII NI KUTOKA VIJIBWENI
MISA ITAKUA LIVE
INSTAGRAM:Tumaini_medi
PIA
YOUTUBE: Tumainitv
KARIBU TUSALI PAMOJA.

Tanzania imeanza ujenzi wa maabara kubwa na ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini ambayo itakuwa ni kubwa kuliko z...
25/08/2025

Tanzania imeanza ujenzi wa maabara kubwa na ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini ambayo itakuwa ni kubwa kuliko zote kwa nchi za Afrika Mashariki na Kati na ambayo itatoa huduma ya kimaabara kwa ubora na kwa uharaka kwa wadau wa sekta ya madini nchini.

Hayo yamesemwa leo na Waziri wa Madini Mh. Anthony Mavunde wakati wa kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa maabara ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini katika eneo la Kizota,Jijini Dodoma.

“Tunamshukuru Mh. Rais Dkt. Samia S. Hassan kwa kuwa kinara wa mageuzi makubwa ya sekta ya madini na kwa kuandika historia ya ujenzi wa maabara hii ya kisasa miaka 100 baadaye tangu kuanzishwa kwa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa madini(GST) mwaka 1925.

Leo tunaandika historia kuanza kwa ujenzi wa maabara kubwa ambayo itafungwa mitambo na vifaa vya kisasa katika kutoa huduma za kimaabara ndani na nje ya nchi.

Huu ni ukombozi mkubwa kwa wadau wa sekta ya madini katika kupata taarifa sahihi za kimaabara kwa wakati na zenye ubora wa hali ya juu.

Ni imani yangu maabara hii itachochea ukuaji na maendeleo ya sekta ya madini”Alisema Mavunde

Naye Kaimu Mtendaji Mkuu wa Taasisi ya Jiolojia na Utafiti wa Madini(*GST*) Dkt. Notka Huruma Batenze amesema Maabara hiyo ya kisasa ya uchunguzi wa sampuli za madini utaleta tija kwa wadau wa sekta ya madini na kurahisisha upatikanaji wa huduma hii muhimu kwa maendeleo ya sekta ya madini.

Gharama za ujenzi wa maabara hii unatarajiwa kuwa Tsh Bilioni 14.3 na muda wa ujenzi wa kukamilika maabara ni siku 690.



Address

Kristo Mfalme Tabata
Tabata
9916

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 14:30
Sunday 08:00 - 14:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tumainimedia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tumainimedia:

Share

Category