Tumainimedia

Tumainimedia Tumaini Media is Catholic Media Based in Tanzania

Wagonjwa watano wenye mishipa ya damu iliyoziba kwa asilimia zaidi ya 75 wamefanyiwa upasuaji wa kupandikiza mishipa ya ...
18/12/2025

Wagonjwa watano wenye mishipa ya damu iliyoziba kwa asilimia zaidi ya 75 wamefanyiwa upasuaji wa kupandikiza mishipa ya damu ya moyo bila kusimamisha moyo (off – Pump CABG).

Upasuaji huo unafanyika katika kambi maalumu ya siku tano iliyoanza Desemba 16, 2025 na kufanywa na wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) kwa kushirikiana na Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam Mkurugenzi wa Upasuaji wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Dkt. Angela Muhozya amesema kambi hiyo ni maalumu kwa wagonjwa ambao mishipa yao ya moyo imeziba hivyo kusababisha ufanyaji kazi wa mioyo yao kuwa chini ya asilimia 35.

“Wagonjwa tunaowafanyia upasuaji katika kambi hii mara nyingi utuchukua ugumu kidogo kuwafanyia upasuaji kutokana na ufanyaji kazi wa mioyo yao, hivyo ili waweze kuwa na matokeo mazuri mara nyingi wenzetu wanafanya upasuaji huu bila ya kuusimamisha moyo k**a ambavyo tunaenda kufanya katika kambi hii”, alisema Dkt. Angela

Dkt. Angela amesema kupitia kambi hiyo wataalamu wa Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) watajengewa uwezo ambao utasaidia kutoa huduma kwa ufanisi zaidi kwa wagonjwa ambao mioyo yao imechoka kutokana na kuziba kwa mishipa ya damu kwa asilimia zaidi ya 75.

Daktari bingwa wa upasuaji wa moyo na mishipa ya damu kutoka Hospitali ya Jaslok iliyopo Mumbai nchini India, Upendra Bhalerao amesema kuwa ameona aungane na wataalamu wa JKCI kuwasaidia wagonjwa ambao kutokana na matatizo ya mishipa ya damu kuziba kwa asilimia zaidi ya 75 wanashindwa kujishughulisha na wakati mwingine hupoteza maisha.

“Wagonjwa tutakaowafanyia upasuaji kupitia kambi hii wataweza kufanya shughuli ndogondogo ambazo hapo awali walikuwa hawezi kuzifanya”, amesema Dkt. Bhalerao

Dkt. Bhalerao amesema kupitia kambi hiyo wataalamu watatoa huduma sambamba na kupata mafunzo yatakayosaidia kupunguza idadi ya vifo vinavyotokana na matatizo ya mishipa ya damu ya moyo kuziba.



Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro wanafanya uchunguzi kufuatia tukio la waombolezaji wa msiba kuchoma moto magari mawili ...
18/12/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Morogoro wanafanya uchunguzi kufuatia tukio la waombolezaji wa msiba kuchoma moto magari mawili aina ya Mazda CX-5 yenye namba za usajili T 214 EJU na Toyota Noah yenye usajili T 350 DCH yaliyotumika kusafirisha mwili wa marehemu kwa ajili ya shughuli za mazishi toka Jijini Dar es salaam kuja Kijiji cha Lusanga wilayani Mvomero.

Taarifa ya Kamanda wa Polisi Mkoa wa Morogoro SACP Alex Mk**a imeeleza kuwa tukio hilo limetokea Desemba 17, 2025 katika Kitongoji cha Kilingeni kijiji cha Lusanga kata ya Diongoya Tarafa ya Turiani wilaya ya Mvomero mkoani humo.

Aidha, taarifa hiyo imeendelea kufafanua kuwa magari hayo yaliyochomwa moto na kuharibika yalitumika kusafirisha mwili wa Mwanahasan Juma Hamis (18) Mfanyakazi wa Nyumbani aliyefariki kwa maradhi Jijini Dar es salaam alipokuwa akifanya kazi na kusafirishwa nyumbani kwao Lusanga, Tarafa ya Turiani wilayani Mvomero kwa taratibu za mazishi.

Wakati taratibu za mazishi zikiendelea kufanyika, kulizuka sintofahamu baada wanafamilia kutilia shaka juu ya mazingira ya kifo cha msichana huyo, hali iliyopelekea wasindikizaji mwili wa marehemu kufungiwa ndani wakitakiwa kutoa maelezo zaidi kuhusiana na kifo hicho na kuibuka kwa jaziba zilizopelekea kuchomwa moto.

Waasindikizaji wa msiba huo waliokolewa na Jeshi la Polisi kwa kushirikiana na uongozi wa Serikali ya Kitongoji na Kijiji, na kwamba kwa sasa uchunguzi wa tukio unaendelea kufanywa na Jeshi la Polisi, na mara baada ya uchunguzi kukalimika, taarifa zaidi zitatolewa, huku ulinzi katika eneo husika ukiendelea kuimarishwa.



18/12/2025

Wafanyabiashara wa dagaa, viazi na vitunguu wa Soko Kuu la Chifu Kingalu manispaa ya Morogoro wamegomea kulipia ushuru wa shilingi 1000 kwa kila gunia linaloshushwa na kuingizwa sokoni hapo kwa madai kuwa utaratibu huo umeanza bila kushirikisha walengwa.

Mwenyekiti wa wafanyabiashara wa dagaa katika soko hilo, Johannes Mkilasi amesema kuwa hatua hiyo ya manispaa kufikia maamuzi ya kutoza ushuru huo haijashirikisha walengwa na kupitishwa kuwa sheria ndogo ya Halmashauri, jambo ambalo limesababisha usumbufu kwa wafanyabiashara licha ya kuwa na vibali na risiti zote zinazoonyesha kulipia ilikotoka mizigo.

Naye, Mwenyekiti wa washushaji dagaa soko Kuu la Kingalu, Ahmed Mustafa ameeleza namna hatua hiyo livyowaathiri katika uendeshaji shughuli zao kibiashara.

Kwa upande wao Julius Stefano ambaye ni mshusha magunia ya dagaa na msafirishaji wa bidhaa hizo kutoka eneo la Kushushia Mizigo hadi soko Kuu la Chifu Kingalu, Isaac Paul wakaeleza namna walivyoathiriwa na zoezi hilo kutokana na kutofanya kazi kwa Siku nzima licha ya kutegemea shughuli hiyo kuwapatia kipato cha kuendesha maisha yao ya kila siku .

Mwenyekiti wa wafanyabiashara soko, Kharid Mkunyegere ameeleza kuwa wamekutana na mchumi wa manispaa ya Morogoro na kukubaliana kusitishwa kwa zoezi hilo hadi watakapota ufumbuzi wa pamoja na kukubaliana kwa pande zote husika.

Zoezi la wafanyabiashara kutakiwa kulipitia ushuru na vibali vyote eneo wanalotoka na kutolipitia ushuru eneo wanalopeleka mzigo lilisitishwa na Rais wa Awamu ya Tano, Dk. John Magufuli (Hayati).



Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Plasduce Mbossa, ameahidi katika mazungum...
17/12/2025

Mwenyekiti mpya wa Bodi ya Wakurugenzi wa Shirika la Umeme Tanzania (TANESCO), Plasduce Mbossa,
ameahidi katika mazungumzo yake kuendelea na jitihada za kuongeza uzalishaji wa umeme ili kuendana na ongezeko la mahitaji ya umeme nchini.

Bw. Mbossa amezungumza hayo jijini Dar es Salaam, katika hafla ya kukabidhiwa ofisi na aliyekuwa Mwenyekiti wa Bodi hiyo, Dkt. Rhimo Nyansaho, ambaye kwa sasa ni Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

Mbossa amebainisha kuwa Dkt. Nyansaho ameiacha TANESCO katika mwelekeo mzuri wa kiutendaji.

Kwa upande mwingine, Dkt. Nyansaho amewashukuru wajumbe wa Bodi, na menejimenti ya TANESCO kwa ushirikiano katika kipindi cha uongozi wake.



Ratiba ya soka leo Jumatano Desemba 17, 2025Spain - Copa del Rey20:00 Leonesa Vs Levante21:00 Albacete Vs Celta Vigo21:0...
17/12/2025

Ratiba ya soka leo Jumatano Desemba 17, 2025

Spain - Copa del Rey
20:00 Leonesa Vs Levante
21:00 Albacete Vs Celta Vigo
21:00 Atletico Baleares Vs Atletico Madrid
21:00 Racing Santander Vs Villarreal
21:00 SD Huesca Vs Osasuna
23:00 CF Talavera de la Reina Vs Real Madrid
23:00 Deportivo Alaves Vs Sevilla

England - EFL Cup
22:30 Manchester City Vs Brentford
23:15 Newcastle United Vs Fulham

(Imeandikwa na )



Askofu wa Jimbo Katoliki la Zomba, nchini Malawi, Mhashamu Alfred Mateyu Chaima, ametoa wito kwa vijana kuhifadhi neema ...
17/12/2025

Askofu wa Jimbo Katoliki la Zomba, nchini Malawi, Mhashamu Alfred Mateyu Chaima, ametoa wito kwa vijana kuhifadhi neema wanayopokea kutoka kwa Mungu, na kukumbatia kikamilifu nafasi yao ya haki ndani ya Kanisa na jamii.

Aliyasema hayo hivi karibuni wakati wa Adhimisho la Misa Takatifu ya Vijana ya mwaka wa Jubilee, iliyofanyika katika Parokia ya Mtakatifu Theresa, huko Liwonde nchini humo.

“Kila kijana ameombwa kuhifadhi neema anazopokea kutoka kwa Bwana na kucheza nafasi yao ya haki ndani ya Kanisa na jamii Kijana wa Kikristo anapaswa kuongoza kwa mfano na kuzaa matunda chanya katika jamii,” alisema.

Aidha Askofu huyo aliwahimiza vijana kuepuka tabia zinazoathiri ustawi wao na ukuaji wao wa kiroho, akirejelea ukatili shuleni, matumizi ya dawa za kulevya, uhusiano usio na afya, kubeti na k**ari, na matukio ya kujiua k**a mwelekeo unaotia wasiwasi.

Pia, aliwasihi vijana kukumbatia mazungumzo na utatuzi wa migogoro kwa amani, akionyesha wasiwasi kuhusu maandamano ya hivi karibuni ya wanafunzi yaliyosababisha uharibifu wa mali za shule.

Mbali na hayo, alisema kuwa Misa ya Jubilee iliwaleta pamoja wawakilishi wa vijana kutoka makanisa 20 katika Jimbo Katoliki la Zomba, ikionyesha wakati muhimu wa tafakari, upya na ahadi ya pamoja ya kuishi kwa misingi ya Kikristo.



Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Leo XIV amemteuwa Mheshimiwa sana Padri Vicent Ouma Odundo, kuto...
16/12/2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Leo XIV amemteuwa Mheshimiwa sana Padri Vicent Ouma Odundo, kutoka Jimbo Kuu Katoliki la Kisumu nchini Kenya, kuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo hilo.

Hadi kuteuliwa kwake, Askofu Msaidizi Mteule huyo, alikuwa ni Makmu wa Askofu wa Jimbo Kuu hilo.

Itakumbukwa kwamba, Askofu Msaidizi Mteule, Vicent Ouma Odundo alizaliwa Juni Mosi, 1978 mjini Kisumu, ambapo baada ya malezi na majiundo yake ya Kipadre, Februari 20, 2008 akapewa Daraja Takatifu ya Upadri.

Tangu wakati huo k**a Padre, ametumikia k**a Paroko na Msimamizi wa Parokia ya Mtakatifu Augustino - Nyamonye kati ya mwaka 2009 hadi mwaka 2012; Paroko wa Holy Cross Siaya kati ya Mwaka 2012 hadi Mwaka 2013.

Baadaye, alitumwa na Jimbo Kuu Katoliki la Kisumu kuendelea na masomo ya juu kwenye Chuo Kikuu cha Kipapa cha Urbaniana na kujipatia Shahada ya Uzamili na Shahada ya Uzamivu katika Sheria za Kanisa kutoka Chuo Kikuu cha Kipapa cha Laterano.

Baada ya masomo yake, alirejea nchini Kenya na kupangiwa kuwa Msimamizi wa Parokia ya St. Andrew, huko Bondo kati ya Mwaka 2018 hadi mwaka 2019. Akateuliwa kuwa Hakimu wa Mahak**a ya Jimbo Kuu Katoliki la Kisumu kati ya Mwaka 2018 hadi mwaka 2020.

Pia, amekuwa Chansela wa Jimbo Kuu Katoliki la Kisumu kati ya Mwaka 2019 hadi 2023. Na hatimaye tangu Mwaka 2019 hadi kuteuliwa kwake kuwa Askofu Msaidizi wa Jimbo Kuu Katoliki la Kisumu, alikuwa ni Makamu wa Askofu.

CC. Vatican News



Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Leo XIV amelaani shambulio la kutisha lililotokea hivi karibuni ...
16/12/2025

Kiongozi wa Kanisa Katoliki Ulimwenguni, Baba Mtakatifu Leo XIV amelaani shambulio la kutisha lililotokea hivi karibuni huko Sydney nchini Australia, ambalo lilisababisha vifo vya wanajumuiya wa Kiyahudi waliokusanyika kwa ajili ya sherehe ya Hanukkah kwenye Ufukwe wa Bondi.

Papa alisikitishwa na tukio hilo, akilielezea k**a kitendo cha vurugu kisicho na maana, alipozungumza wakati wa Mkutano na Wafadhili wa tukio la kupamba mti na Pango la kuzaliwa kwa Yesu katika Uwanja wa Mtakatifu Petro, mjini Vatican, huku akitoa wito wa kukomesha aina zote za vurugu dhidi ya Wayahudi.

Kwa njia hiyo, Papa alituma telegramu yake kutoa rambirambi iliyosainiwa na Katibu wa Mkuu wa Vatican, Mwadhama Pietro Kardinali Parolin, kwa Askofu Mkuu Anthony Fisher wa Jimbo Kuu Katoliki la Sydney, nchini Australia, ambapo alionesha huzuni yake kubwa kuhusu mauaji hayo yaliyotokea wakati wa likizo ya Kiyahudi ya Sikukuu ya Hanukkah.

Shambulio hilo lilifanywa na washambuliaji wawili, baba na mtoto wake, ambapo mmoja wao alisimamishwa kishujaa na raia mmoja, mmiliki wa duka la matunda katika kitongoji cha Sutherland, ambaye alimpokonya silaha mtu huyo kwa mikono mitupu.

Mmoja wa wahalifu, baadaye aliuawa na polisi ambao walifika haraka ufukweni, huku watu 15 wakiwa wameuawa hadi sasa, na takriban watu 30 wakijeruhiwa.

Kwa wale walioguswa na kitendo hiki kisicho na maana cha vurugu, Papa Leo anaelezea ukaribu wake wa kiroho kwao, ambapo kwa matumaini mapya, aliomba kwamba wale wanaojaribiwa na vurugu wageuke na kutafuta njia ya amani na mshik**ano.

Katika telegram hiyo, Papa aliwahakikishia maombi yake kwa ajili ya uponyaji wa wale ambao bado wanaendelea kupona, na kwa ajili ya faraja ya wale wanaoomboleza kufiwa na mpendwa wao.

Kwa upande wake, Askofu Mkuu Fisher, baada ya tukio la kupigwa risasi waathrika, alitoa taarifa, huku akishutumu shambulio hilo k**a kutojali maisha ya binadamu kwa ukali na bila huruma, ambapo aliita kitendo hicho k**a chuki ya baadhi ya watu kwa Wayahudi wote, uovu usioelezeka ambao lazima ukataliwe na kila Mwaaustralia.



Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe.Angela Kairuki amesema mageuzi ya kidijiti yanalenga kujenga serikali...
16/12/2025

Waziri wa Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Mhe.Angela Kairuki amesema mageuzi ya kidijiti yanalenga kujenga serikali ya kisasa.

Angela alisema hayo Dodoma katika hafla ya kutoa vifaa vya Tehama kwa taasisi zinazotoa haki.

Alisema lengo la mageuzi ya kidijiti ni kujenga serikali yenye uwezo wa kufanya kazi kwa ufanisi katika mazingira, inayotumia teknolojia k**a chombo cha kuharakisha maendeleo ya kijamii na kiuchumi.



Kocha mkuu wa Timu ya Tanzania amezungumzia namna ambavyo wachezaji wake wamejiandaa vyema kuelekea mashindano ya  .Amey...
15/12/2025

Kocha mkuu wa Timu ya Tanzania amezungumzia namna ambavyo wachezaji wake wamejiandaa vyema kuelekea mashindano ya .

Ameyazungumza hayo siku ya leo Desemba 15 baada ya mazoezi akisisitiza mashabiki wategemee kuona mpira wa kiwango cha juu.



Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila ameitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DA...
14/12/2025

Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Albert Chalamila ameitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Dar es Salaam (DAWASA) kuweka mikakati madhubuti na kutafuta suluhisho la kudumu dhidi ya changamoto ya upungufu wa maji katika Mto Ruvu hususani katika kipindi kirefu cha ukosefu wa mvua.

Amesema kwa kuwa changamoto hiyo ya upungufu wa maji katika vyanzo vya maji hususani Mto Ruvu huwa inatokea mara kwa mara, ni vyema Watendaji na Wataalamu kukaa na kuweka mikakati ya kudumu ya namna ya kutatua changamoto hiyo.

“Kutokana na hali hii, DAWASA mnakabiliwa na jukumu la kubuni miradi ya maji ambayo itawezesha kupatikana kwa huduma ya maji kwa kipindi chote cha upungufu wa majisafi, na ili kuweza kukidhi mahitaji ya maji kwa wananchi wa DaresSalaam,” amesema Mkuu wa Mkoa, Chalamila.

Mbali na hapo, ameitaka DAWASA kuwekeza nguvu katika kufufua visima vilivyopo vya maji ili viweze kutoa huduma na kupunguza malalamiko ya wananchi kuhusu upungufu wa huduma.

Kwa upande wake Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi DAWASA, Mhandisi Romanus Mwangingo amesema kuwa Mamlaka imepokea maelekezo yote, na kazi inaendelea ya kuhakikisha wananchi wanapata huduma ikiwemo kutoa maji kwa mgao sawia katika maeneo yote ya Jiji.

Ameongeza kuwa jitihada mbalimbali zinaendelea kutekelezwa, ikiwemo kufufua visima vilivyopo vya maji kwa lengo la kuongeza upatikanaji wa maji na kupunguza makali ya uhaba wa huduma kwa wananchi.

Naye Mkurugenzi wa Bonde la Wami Ruvu, Mhandisi Elibariki Mmasi amesema kuwa changamoto hiyo iliyotokea ni kutokana na athari za mabadiliko ya tabianchi yanayoathiri maeneo mengi ya kihuduma na kusababisha vyanzo vya maji kupungua.



13/12/2025

VYUO VIKUU VIWE NA MIONGOZO YA MATUMIZI YA AKILI UNDE - KARDINALI RUGAMBWA

Askofu Mkuu wa Jimbo Kuu Katoliki la Tabora Mwadhama Protace Kardinali Rugambwa ameitahadharisha jamii kuhusu matumizi ya akili unde, akisema ni lazima kuwe na namna bora ya kuitumia.

Mwadhama Kardinali Rugambwa ameyasema hayo leo Jumamosi Disemba 13, 2025 katika mahafali ya 28 ya Chuo KIkuu cha Mtakatifu Augustino cha Tanzania ( SAUT ) Jijini Mwanza ambapo amesema teknolojia pamoja na mazuri yake imekuja na changamoto nyingi, zikiwemo za kimaadili na kiusalama.

" Kupitia maendeleo haya ya Sayansi na Teknolojia tumegundua hicho ambacho kinaitwa Artificial Intelligence - AI, wengine wanakiita Akili - Unde, wengine wanakiita Akili Mnemba, leo hatujui lipi la kweli na lipi la uongo, je wasomi mnaisaidiaje jamii yenu ili suala la AI liweze kutumika kwa usahihi ni swali tunajiuliza ?" amehoji Askofu Mkuu Rugambwa.

Ameongeza: " Tupo katika mnyukano wa taarifa kwa kutumia akili unde, ni bahati mbaya matumizi haya ya akili unde na ambayo sasa yamevuma mpaka kwenye kuta za vyuo vikuu, tusipokuwa makini, tunaiona hatari ya wasomi wetu wa sasa ya kuikabidhi akili unde kila kitu na wao kwenda likizo, tusipokuwa makini hiyo AI na Akili Unde itakwenda kuchukua nafasi ya kufikiri badala ya sisi kufikiri, sisemi kwamba maendeleo hayo ni mabaya ila ni vizuri tukawa na mwongozo wa namna bora ya kutumia hii sayansi ya akili unde kwenye taaluma.

Jumla ya wahitimu 2,976 wametunukiwa Astashahada, Stashahada, Shahada ya Kwanza, Stashahada ya Uzamili, Shahada ya Uzamili huku wahitimu wawili Pius Lufutu na Mtaib Othman muongoni mwa hao wakitunukiwa Shahada ya Uzamivu PhD na Mkuu wa Chuo Kikuu cha Mtakatifu Augustino Cha Tanzania Askofu Wolfgang Pisa ambaye aliwakilishwa na Askofu wa Jimbo Katoliki.la Bunda Mhashamu Simon Chibuga Masondole

Address

Kristo Mfalme Tabata
Tabata
9916

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 14:30
Sunday 08:00 - 14:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tumainimedia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tumainimedia:

Share

Category