Tumainimedia

Tumainimedia Tumaini Media is Catholic Media Based in Tanzania

MICHEZO NI AJIRA, HUJENGA AFYA NA HUTANGAZA AMANI–ACP AKAMAKatika uzinduzi wa Kombe la Polisi Jamii lililofanyika katika...
11/07/2025

MICHEZO NI AJIRA, HUJENGA AFYA NA HUTANGAZA AMANI–ACP AKAMA

Katika uzinduzi wa Kombe la Polisi Jamii lililofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mlowo, Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe, Afisa Mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Songwe, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ak**a Shaaban amesema kuwa michezo ni nyenzo muhimu katika kujenga afya, kutoa ajira kwa vijana, na kutangaza amani katika jamii.

Akizungumza Juli 09, 2025 mbele ya mamia ya wakazi wa Kata ya Mlowo waliokusanyika kushuhudia tukio hilo, ACP Ak**a alisema kuwa "Michezo si burudani pekee bali ni sehemu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwani Michezo ni njia ya kuwajenga vijana kimwili na kiakili, lakini pia inatoa ajira kwa maelfu ya watu, kuanzia kwa wachezaji, makocha, waamuzi hadi waandaaji wa matamasha na mashindano"

Aidha, Kamanda Ak**a aliwapongeza wananchi wa Mlowo kwa kuunga mkono juhudi za Jeshi la Polisi kupitia mashindano hayo, akieleza kuwa mashindano ya Polisi Jamii ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uhusiano kati ya polisi na wananchi katika kupunguza uhalifu, vijana kujiepusha na matumizi ya madawa ya kulevya na kutofanya unyanyasaji wa wanawake na watoto ikiwa ni pamoja kupitia michezo, tunawasiliana, tunajifunza kushirikiana na tunajenga amani ya kudumu katika nchi yetu.

Uzinduzi huo uliambatana na mechi ya ufunguzi kati ya timu ya Forest FC na timu ya Changalawe FC ambayo Forest FC iliibuka kidedea kwa ushindi wa goli 01 dhidi ya Changalawe FC na kuchukua ngao ya Polisi Jamii ikiwa ni pamoja na kiasi cha pesa tasilimu kwa kitendo hicho jamii inaendelea kuhamasishwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe ikiwa ni pamoja na kupata elimu juu ya masuala ya ulinzi na usalama katika maeneo yao ili jamii iendelee kuwa salama.

ACP Ak**a, alihitimisha kwa kutoa wito kwa wazazi na walezi kuwahimiza watoto kushiriki katika michezo k**a njia ya kuwajenga kiafya na kuwaepusha na vitendo vya kihalifu, tuwekeze kwenye michezo, tupate afya bora, amani na kukuza uchumi wa taifa letu. Pia aliwataka wananchi kuelekea kipindi cha uchaguzi kuchagua viongozi bora na si bora viongozi ili nchi iendelee kuwa na amani na utulivu.



Muelimishaji Mkuu wa Elimu kwa Umma Mkoa wa TAKUKURU Ilala, jijini Dar es Salaam, Bi. Nerry Mwakyusa ametoa wito kwa wan...
11/07/2025

Muelimishaji Mkuu wa Elimu kwa Umma Mkoa wa TAKUKURU Ilala, jijini Dar es Salaam, Bi. Nerry Mwakyusa ametoa wito kwa wananchi kuelekea katika Uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika Oktoba mwaka huu, waepuke kuwachagua wagombea wanaotumia hongo (rushwa), kwani kiongozi sahihi si mwenye fedha, bali ni yule mwenye nia ya dhati ya kuwaongoza wananchi, ambaye katika kuomba kura, hatumii hongo.

Nerry ameyasema hayo leo Julai 11, wakati akizungumza katika kipindi cha KAHAWA AU CHAI kinachorushwa na Tumaini Televishen kila siku za Jumatatu hadi Ijumaa kwanzia saa 12:30 alfajiri hadi saa 3:00 asubuhi.

Slide kusikia wito wa Bi. Nerry.



Ratiba ya soka leo Ijumaa Julai 11, 2025Women’s Euro 2025Group B22:00 Italy Women Vs Spain Women22:00 Portugal Women Vs ...
11/07/2025

Ratiba ya soka leo Ijumaa Julai 11, 2025

Women’s Euro 2025
Group B
22:00 Italy Women Vs Spain Women
22:00 Portugal Women Vs Belgium Women

(Imeandikwa na )



π“π”πŒπ€πˆππˆ 𝐋𝐄𝐓𝐔 wiki hii.Pata nakala yako kwa Tsh. 1,000/= tu
11/07/2025

π“π”πŒπ€πˆππˆ 𝐋𝐄𝐓𝐔 wiki hii.
Pata nakala yako kwa Tsh. 1,000/= tu



Ufaransa kupitia mtandao wa kijamii wa timu yake ya Taifa, umewapongeza wachezaji wake waliofanikiwa kutinga katika hatu...
10/07/2025

Ufaransa kupitia mtandao wa kijamii wa timu yake ya Taifa, umewapongeza wachezaji wake waliofanikiwa kutinga katika hatua ya fainali ya Kombe la Dunia la Klabu linalochezwa nchini Marekani.

Wachezaji hao ni wale wanaozichezea klabu za Chelsea ya Uingereza, na PSG ya Ufaransa, ambazo zimetinga fainali, na zitashuka dimbani kumalizia mechi yao ya fainali siku ya Jumapili Julai 13, 2025 katika dimba la MetLife nchini Marekani.



Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo Julai 10, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurug...
10/07/2025

Waziri wa Maliasili na Utalii, Mhe. Balozi Dkt. Pindi Chana leo Julai 10, 2025 amekutana na kufanya mazungumzo na Mkurugenzi Msaidizi wa UNESCO anayeshugulikia masuala ya Utamaduni, Bw. Ernesto Ottone, pembezoni mwa Mkutano wa 47 wa Kamati ya Urithi wa Dunia unaoendelea mjini Paris, Ufaransa.

Kupitia kikao hicho, viongozi hao wameazimia kukuza ushirikiano kati ya UNESCO na Tanzania katika uhifadhi wa Maeneo ya Urithi wa Dunia yaliyopo nchini Tanzania.

Kadhalika, Mkurugenzi huyo ameahidi kuimarisha ushirikiano katika uendelezaji wa shughuli za kiutamaduni nchini Tanzania na kukuza uhifadhi wa vivutio vyake vya kipekee.

Kikao hicho kimehudhuriwa pia na Balozi wa Tanzania nchini Ufaransa Mhe. Ali J. Mwadini, pamoja na wataalam wengine kutoka Tanzania.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema pamoja na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii B...
10/07/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango amesema pamoja na Mifuko ya Hifadhi ya Jamii Barani Afrika kutumika kuwekeza katika kuendeleza miundombinu ni vema kuhakikisha michango ya wanachama ambayo imetengwa k**a kinga dhidi ya misukosuko ya kiuchumi na kijamii pamoja na kukabiliana na umaskini inabaki kuwa ya kutosha kukidhi malengo ya msingi ya uanzishwaji wake.

Makamu wa Rais ametoa wito huo wakati akifungua Mkutano wa 14 wa Kimataifa wa Watunga Sera wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Barani Afrika unaofanyika katika Kituo cha Mikutano cha Kimataifa cha Arusha (AICC). Amesisitiza kuwepo umakini kwenye uwekezaji wa miradi ya miundombinu kwani miradi ambayo haiwezi kutekelezeka inaweza kudhoofisha uwezo wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii kutimiza wajibu wake.

Aidha Makamu wa Rais amesema ni muhimu tahadhari ichukuliwe ili kuepusha miradi iliyobuniwa vibaya, yenye gharama kubwa kupita kiasi au miradi migumu kupita kiasi ambayo ni ngumu kuisimamia na ile isiyokidhi mahitaji ya walengwa wa mifuko ya hifadhi ya jamii. Ameongeza kwamba iwapo upembuzi yakinifu na thabiti wa miradi ya miundombinu hautafanywa mapema inaweza kusababisha kuchelewa kwa malipo ya walengwa au hata kushindwa kabisa kuirejesha.

Makamu wa Rais amesema ufadhili wa miundombinu Barani Afrika unakadiriwa kuwa na upungufu kati ya dola bilioni 68 -108 kila mwaka hali inayopelekea wachambuzi wengi wa maendeleo kukubaliana kwamba Mifuko ya Hifadhi ya Jamii ipo katika nafasi nzuri ya kufanya kazi zaidi k**a chachu ya kuharakisha maendeleo ya miundombinu barani Afrika kwa kuondoa upungufu huo wa ufadhili.

Mkutano huo umehudhuriwa na Viongozi mbalimbali kutoka Mataifa ya Afrika ikiwemo Mawaziri na Wataalamu wa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii.

Imetolewa na
Ofisi ya Makamu wa Rais
10 Julai 2025
Arusha.



Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Doto Biteko akibonyesha kitufe kuzindua rasmi Mfumo wa Usajili wa Waandishi wa Habari unaoju...
10/07/2025

Naibu Waziri Mkuu Mhe. Dkt. Doto Biteko akibonyesha kitufe kuzindua rasmi Mfumo wa Usajili wa Waandishi wa Habari unaojulikana kwa jina la TAI-Habari leo tarehe 09 Julai, 2025 wakati wa Mkutano wa Wadau kujadili Mchango wa Sekta ya Habari katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2025 uliofanyika Ukumbi wa Mlimani City.

Kulia ni Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Prof. Palamagamba Kabudi, (kushoto) Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo na Msemaji Mkuu wa Serikali Bw. Gerson Msigwa. Wa kwanza kulia ni Kaimu Mkurugenzi Idara ya Habari Maelezo Rodne Mbuya.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa ...
10/07/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jana Julai 9, 2025 wakati akielekea Mkoani Arusha kwaajili ya kufungua Kongamano la Kimataifa la Watunga Sera wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Bara la Afrika litakalofanyika tarehe 10 Julai 2025.



Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa ...
10/07/2025

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango akiwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) jana Julai 9, 2025 wakati akielekea Mkoani Arusha kwaajili ya kufungua Kongamano la Kimataifa la Watunga Sera wa Sekta ya Hifadhi ya Jamii Bara la Afrika litakalofanyika leo Julai 10, 2025.



Evetha Mboya  , Afisa Utumishi Mwandamizi na Mtaalamu wa Masuala ya Huduma kwa Mteja, akitoa elimu kuhusu namna ya kuwaf...
10/07/2025

Evetha Mboya , Afisa Utumishi Mwandamizi na Mtaalamu wa Masuala ya Huduma kwa Mteja, akitoa elimu kuhusu namna ya kuwafahamu wateja na jinsi ya kuwahudumia.

Ametoa elimu hiyo katika kipindi cha DIRA YA MTEJA, kilichoruka jana Julai 9, 2025 ambacho kinarushwa na Radio Tumaini kila Jumatano kwanzia saa 1:00 usiku hadi saa 2:00 usiku, na marudio ni kila Jumapili saa 12:30 jioni hadi saa 1:30 usiku.

Slide πŸ‘‰ kuona elimu iliyotolewa na Mtaalam huyo…

Mtangazaji:



Akifungua Mkutano wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya Habari katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2025, jijini Dar es Sala...
09/07/2025

Akifungua Mkutano wa Wadau Kujadili Mchango wa Sekta ya Habari katika kufanikisha Uchaguzi Mkuu 2025, jijini Dar es Salaam, Naibu Waziri Mkuu na Waziri wa Nishati, Mhe. Dkt. Doto Biteko amewaasa waandishi wa habari nchini kuwa walinzi wa ukweli, wajenzi wa amani na wachochezi wa uwajibikaji wa kisiasa.

Amevitaka vyombo vya habari kuwa kioo cha jamii na kujiepusha na uzushi, chuki au upendeleo na badala yake kuhimiza maelewano, uvumilivu wa kisiasa, na utamaduni wa kuheshimu tofauti za maoni.

β€œNi wajibu wa Serikali kuhakikisha waandishi wa habari katika kipindi chote cha mchakato wa uchaguzi wanabaki salama pamoja na vitendea kazi vyao. Aidha, Serikali, tutaendelea kulisimamia hili kwa nguvu zetu zote. Tutahakikisha kuwa, mnakuwa na mazingira salama, huru na rafiki wakati wote wa majukumu yenu, amesema Dkt. Biteko.

Ameendelea kusema katika kuelekea Uchaguzi Mkuu 20205 katika jamii kutakuwa na watu wenye mitazamo todauti kulingana na vipaumbele vyao hata hivyo vyombo vya habari vina fursa ya kutoa uelekeo kwa taifa.

β€œUchaguzi ni kipindi cha muda mfupi, tumuombe Mungu hata baada ya Uchaguzi tubaki kuwa Taifa moja lenye ustahimilivu na kila mmoja akitoka kwake aende kutafuta mkate arudi nyumbani kwa familia yake kukiwa na amani, sisi kupitia mkutano huu tuungane kuhakikisha Taifa letu linabaki salama. Sekta ya habari ni nyenzo muhimu katika kulinda na kudumisha amani katika kipindi chote cha uchaguzi,” amesisitiza Dkt. Biteko.



Address

Tabata

Opening Hours

Monday 08:00 - 17:00
Tuesday 08:00 - 17:00
Wednesday 08:00 - 17:00
Thursday 08:00 - 17:00
Friday 08:00 - 17:00
Saturday 08:00 - 14:30
Sunday 08:00 - 14:30

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Tumainimedia posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Tumainimedia:

Share

Category