
11/07/2025
MICHEZO NI AJIRA, HUJENGA AFYA NA HUTANGAZA AMANIβACP AKAMA
Katika uzinduzi wa Kombe la Polisi Jamii lililofanyika katika uwanja wa shule ya msingi Mlowo, Wilaya ya Mbozi, Mkoa wa Songwe, Afisa Mnadhimu wa Polisi Mkoa wa Songwe, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Ak**a Shaaban amesema kuwa michezo ni nyenzo muhimu katika kujenga afya, kutoa ajira kwa vijana, na kutangaza amani katika jamii.
Akizungumza Juli 09, 2025 mbele ya mamia ya wakazi wa Kata ya Mlowo waliokusanyika kushuhudia tukio hilo, ACP Ak**a alisema kuwa "Michezo si burudani pekee bali ni sehemu ya maendeleo ya kijamii na kiuchumi kwani Michezo ni njia ya kuwajenga vijana kimwili na kiakili, lakini pia inatoa ajira kwa maelfu ya watu, kuanzia kwa wachezaji, makocha, waamuzi hadi waandaaji wa matamasha na mashindano"
Aidha, Kamanda Ak**a aliwapongeza wananchi wa Mlowo kwa kuunga mkono juhudi za Jeshi la Polisi kupitia mashindano hayo, akieleza kuwa mashindano ya Polisi Jamii ni sehemu ya mkakati wa kuimarisha uhusiano kati ya polisi na wananchi katika kupunguza uhalifu, vijana kujiepusha na matumizi ya madawa ya kulevya na kutofanya unyanyasaji wa wanawake na watoto ikiwa ni pamoja kupitia michezo, tunawasiliana, tunajifunza kushirikiana na tunajenga amani ya kudumu katika nchi yetu.
Uzinduzi huo uliambatana na mechi ya ufunguzi kati ya timu ya Forest FC na timu ya Changalawe FC ambayo Forest FC iliibuka kidedea kwa ushindi wa goli 01 dhidi ya Changalawe FC na kuchukua ngao ya Polisi Jamii ikiwa ni pamoja na kiasi cha pesa tasilimu kwa kitendo hicho jamii inaendelea kuhamasishwa kushirikiana na Jeshi la Polisi Mkoa wa Songwe ikiwa ni pamoja na kupata elimu juu ya masuala ya ulinzi na usalama katika maeneo yao ili jamii iendelee kuwa salama.
ACP Ak**a, alihitimisha kwa kutoa wito kwa wazazi na walezi kuwahimiza watoto kushiriki katika michezo k**a njia ya kuwajenga kiafya na kuwaepusha na vitendo vya kihalifu, tuwekeze kwenye michezo, tupate afya bora, amani na kukuza uchumi wa taifa letu. Pia aliwataka wananchi kuelekea kipindi cha uchaguzi kuchagua viongozi bora na si bora viongozi ili nchi iendelee kuwa na amani na utulivu.