CG FM Radio

CG FM Radio ๐Ÿ“ŒCG FM RADIO
๐Ÿ“Œ88. 5 MHz
๐Ÿ“ŒTabora - Tanzania
๐Ÿ“Œ+255769354641
๐Ÿ“ŒCG Online Tv Owned by C.G. Throughout its existence it has never been involved in any legal wrangle.

Traders, the C.G fm Radio Station started broadcasting services in Tabora municipality in 2004 after being registered by the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) on September 1, 2004. The Radio Station has built a good working relations at high level of integrity with many residents of Tabora region and other audiences in the neighbouring regions of Singida, Shinyanga and Kigoma reg

ions. On top of that it has good working relations with government leaders, policy makers, religious leaders, Civic Organisations, Community Based Organisations (CBOs), Faith Based Organisations (FBOs), Small and Medium Enterprises (SMEs) and other actors in the media arena

The Radio Station has ample potentials for growth and expansion of services in the forthcoming years, because is well prepared in terms of coping with the the latest transmission technology in Tanzania.

02/09/2026

Timu ya soka la Mbeya Kwanza imeendelea na maandalizi ya kuelekea mashindano ya Championship yatakayoanza kutimua vumbi Septemba 11 mwaka huu
Uongozi wa timu hiyo umesema una imani kuwa msimu huu utakuwa bora sana huku wakiweka wazi mpango kazi wa kubadili jina la timu na kuwa Tabora United.

02/09/2026

Wanamichezo kutoka shule ya sekondari ya Unyanyembe ya Tabora mjini wanatarajia kuondoka jumamosi ya wiki hii kuelekea jijini Dar es salaam kushiriki mashindano ya Shule zinazomilikiwa na Jeshi la Ulinzi la Wananchi wa Tanzania-JWTZ huku wanamichezo hao wakiahidi kushika nafasi ya kwanza.

Akizungumza na wanamichezo hao,Mkuu wa Shule ya Sekondari Unyanyembe,Luteni Kanali Albinus Komba amewataka wachezaji hao kudumisha nidhamu,kujituma na kuhakikisha wanarudi na ushindi.

02/09/2026

Usikose Kuungana Nasi Katika Taarifa Yetu ya Habari Ifikapo Saa 10:00 Jioni leo, September 02, 2026.

1. Wanaume mkoani Tabora wameshauriwa kukutana mara kwa mara ili badili itikadi na mitazamo inayoweza kubadili itikadi na mitazamo inayoweza kuzalisha migogoro katika familia

2. Na katika hari za Kimataifa Wanaharaka wa haki za kibinadamu na siasa wameandamana jijini Nairobi nchini Kenya kushinikizwa kuachiwa kwa wafungwa wa kisiasa kwenye nchini Tanzania na Uganda.

Sikiliza Kupitia: 88.5 MHz | Sauti ya Mamlaka,๐Ÿ’ป YouTube: .
Usipitwe na Taarifa ya Ifikapo saa Kumi Jioni

Endelea Kutufuatilia kwenye Mitandao yetu ya Kijamii Instagram,Facebook,Tiktok na Youtube na Sikiliza CG Fm 88.5Mhz.

02/09/2026
02/09/2026

Maswali Polisi Kujinyonga Mahabusu | Moring Power | September 02.

YAS ZANZIBAR INTERNATIONAL MARATHON 2026: JEZI RASMI ZAZINDULIWAMaandalizi ya Yas Zanzibar International Marathon 2026 y...
02/09/2026

YAS ZANZIBAR INTERNATIONAL MARATHON 2026: JEZI RASMI ZAZINDULIWA

Maandalizi ya Yas Zanzibar International Marathon 2026 yameingia hatua nyingine baada ya kutambulishwa rasmi kwa jezi za mashindano hayo yanayotarajiwa kufanyika Zanzibar Septemba 20, 2026.

Mashindano hayo yanafanyika chini ya kauli mbiu โ€œKasi Swadakta kwa Viwango,โ€ ikiwa ni sehemu ya kuhamasisha ushiriki wa Watanzania katika michezo na kukuza viwango vya ubora.

Waandaaji wamewahimiza washiriki kujisajili mapema na kuwa sehemu ya mbio hizo.

Usajili unapatikana kupitia 15001 #.


01/09/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mwanza linafanya uchunguzi kufuatia kifo cha mwanafunzi wa kidato cha tatu katika Shule ya Sekondari ya Wasichana Loreto, Stellah Wangaluke Shilingi (15), aliyefariki dunia baada ya kujirusha kutoka ghorofa ya kwanza ya shule hiyo iliyopo Kata ya Nyakato, Wilaya ya Ilemela.

Tukio hilo lilitokea Agosti 31, 2026 asubuhi wakati akielekea kufanya usafi na wenzake, ambapo alikimbizwa Hospitali ya Rufaa ya Kanda Bugando kwa matibabu lakini ilibainika kuwa tayari alikuwa amefariki dunia.

Uchunguzi wa awali wa polisi umebaini kuwa chanzo cha tukio hilo ni msongo wa mawazo wa muda mrefu uliotokana na migogoro ya kifamilia kati yake na mama yake mzazi, huku marehemu akiacha ujumbe wa maandishi unaoeleza dhamira yake kabla ya kujirusha.

Imebainika pia kuwa mwanafunzi huyo aliwahi kujaribu kukatisha uhai wake kwa kumeza vidonge wakati wa likizo ya Juni 2026 lakini aliokolewa, sambamba na kuonyesha tabia ya kujitenga akiwa shuleni.

Kufuatia msiba huo, Jeshi la Polisi limetoa pole kwa familia na uongozi wa shule huku likitoa wito kwa wazazi, walezi, na walimu kuimarisha mifumo ya ushauri nasaha na kuwa karibu na vijana ili kubaini mapema changamoto za kisaikolojia.

Polisi wamesisitiza umuhimu wa jamii kusikiliza na kutatua kero za watoto kwa wakati kabla hawajachukua maamuzi magumu ya kukatisha maisha yao.

Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora limemsaidia mwanafunzi Simoni Masanja, aliyekwama kuendelea na masomo ya Kidato cha Tano ...
01/09/2026

Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora limemsaidia mwanafunzi Simoni Masanja, aliyekwama kuendelea na masomo ya Kidato cha Tano kutokana na kukosa mahitaji muhimu ya shule, kwa kumkabidhi vifaa mbalimbali vitakavyomwezesha kuanza masomo katika Shule ya Sekondari Lugugu, Mkoani Kigoma.

Msaada huo umekabidhiwa Septemba 1, 2026 katika Ofisi ya Polisi Mkoa wa Tabora na Mkuu wa Kitengo cha Polisi Wasaidizi kutoka Makao Makuu ya Polisi Dodoma, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi (SACP) Dkt. Debora Magiligimba, kwa kushirikiana na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Tabora, Kamishna Msaidizi wa Polisi (ACP) Twaha Lulengelule.

Msaada huo umetolewa baada ya kubainika kuwa wazazi wa mwanafunzi huyo, wanaoishi Kata ya Kalunde, Manispaa ya Tabora, hawakuwa na uwezo wa kugharamia mahitaji muhimu ya shule tangu alipochaguliwa kuendelea na masomo ya Kidato cha Tano.

Akizungumza wakati wa kukabidhi msaada huo, SACP Dkt. Debora Magiligimba amesema hatua hiyo ni sehemu ya mwendelezo wa Jeshi la Polisi katika kushirikiana na jamii, hususan kuwasaidia watoto na wanafunzi wenye uhitaji ili waweze kutimiza ndoto zao za kielimu.

Kwa upande wake, mwanafunzi Simoni Masanja amelishukuru Jeshi la Polisi kwa msaada huo, akisema ndoto yake ya kuendelea na masomo ilikuwa mbioni kutoweka kutokana na ukosefu wa mahitaji muhimu ya shule. Ameahidi kutumia fursa hiyo kwa kusoma kwa bidii na kufanya vizuri katika masomo yake.

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Camillus Wambura amesema Serikali imetoa fursa kwa Wananchi wenye silaha haramu kuz...
31/08/2026

Mkuu wa Jeshi la Polisi nchini (IGP) Camillus Wambura amesema Serikali imetoa fursa kwa Wananchi wenye silaha haramu kuzisalimisha kwa hiari bila kuchukuliwa hatua za kisheria, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa sheria ya udhibiti wa silaha na risasi ya mwaka 2023.

Akizungumza katika uzinduzi wa Kampeni ya msamaha wa usalimishaji wa Silaha haramu kwa hiari uliofanyika katika viwanja vya Nyerere Square jijini Dodoma, IGP Wambura amesema zoezi hilo litaanza Septemba mosi hadi Oktoba 31, 2026, huku akiwataka wananchi kutumia fursa hiyo kabla silaha hizo hazijatumika katika matukio ya uhalifu.

Amesema katika kipindi cha miaka mitatu na nusu kuanzia mwaka 2023, Jeshi la Polisi limekamata silaha 990 kupitia operesheni mbalimbali za kupambana na uhalifu, ambapo asilimia 75 ni magobore, huku nyingine zikiwa silaha zilizokuwa zikimilikiwa kihalali na wamiliki ambao wamefariki na kubaki mikononi mwa ndugu na warithi.

IGP Wambura amesisitiza kuwa kampeni hiyo haiwezi kufanikiwa bila ushirikiano wa Viongozi wa Serikali, Dini, Kimila, Vyombo vya habari na Wananchi, akiwataka wenye taarifa kuhusu uwepo wa silaha haramu kutoa taarifa kwa Jeshi la Polisi ili kuzuia madhara yanayoweza kujitokeza katika jamii.

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua mkoani Tabora limewaonya watumishi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya ...
31/08/2026

Baraza la Madiwani la Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua mkoani Tabora limewaonya watumishi wa Mamlaka ya Vitambulisho vya Taifa (NIDA) wilayani humo dhidi ya kutumia lugha zisizo na staha wanapowahudumia wananchi wanaokwenda kufuatilia vitambulisho vya Taifa.

Akizungumza katika kikao cha Baraza la Madiwani, Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Kaliua, Anastazia Bebete, amesema baadhi ya wananchi wamekuwa wakilalamikia namna wanavyopokelewa na kuhudumiwa katika ofisi za NIDA, hali ambayo amesema inaweza kudhoofisha zoezi la usajili na ugawaji wa vitambulisho vya Taifa.

Amesema badala ya watumishi kutumia lugha zisizo na staha, wanapaswa kuwaelimisha wananchi na kutatua changamoto zao kwa kuzingatia misingi ya utoaji wa huduma bora.

Kwa upande wake, Katibu wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) Wilaya ya Kaliua, Eliud Shemauya, amesema changamoto nyingine inayowakabili wananchi ni kutozwa fedha wanapokwenda kubadilisha taarifa zao, licha ya zoezi hilo kuwa linapaswa kutolewa bila malipo, jambo ambalo amesema limekuwa likileta sintofahamu.

Wakichangia hoja hiyo, baadhi ya madiwani akiwemo Abdallah Hamisi wa Kata ya Kazaroh, Selina Manamba wa Kata ya Kamsekwa na Sadick Kallah wa Kata ya Ugunga, wameomba zoezi la usajili na utoaji wa vitambulisho liendelee kuwafikia wananchi katika maeneo yao ili kupunguza gharama za kusafiri umbali mrefu kufuata huduma hiyo katika makao makuu ya wilaya.

Awali, akisoma taarifa ya utekelezaji wa zoezi la usajili na utoaji wa vitambulisho vya Taifa kwa kipindi cha robo ya nne ya mwaka wa fedha 2025/2026, Afisa kutoka NIDA Wilaya ya Kaliua, Khamisi Serenge, amesema mamlaka hiyo imefanikiwa kusajili wananchi 7,872, kati ya lengo la wananchi 7,839, baada ya kuwafuata wananchi katika kata za Ichemba, Igwisi, Kanoge, Mwongozo, Nhwande na Silambo.

Hata hivyo, amesema zoezi la ugawaji wa vitambulisho bado linakabiliwa na changamoto, ambapo kati ya vitambulisho 6,779 vilivyopelekwa katika kata hizo ili wananchi wavichukue, ni vitambulisho 1,204 pekee vilivyochukuliwa na wahusika.

Aidha, Serenge amesema ucheleweshwaji wa upatikanaji wa rasilimali fedha umekuwa ukisababisha kuchelewa kwa utekelezaji wa zoezi la usajili kwa kuwafuata wananchi.

Address

PO Box 2207 TABORA
Tabora

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when CG FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to CG FM Radio:

Shortcuts

Share