CG FM Radio

CG FM Radio This is CG Fm Radio's official page,unakaribishwa kuweza kuchangia mada na kupata habari mb Owned by C.G.

Traders, the C.G fm Radio Station started broadcasting services in Tabora municipality in 2004 after being registered by the Tanzania Communications Regulatory Authority (TCRA) on September 1, 2004. Throughout its existence it has never been involved in any legal wrangle. The Radio Station has built a good working relations at high level of integrity with many residents of Tabora region and other

audiences in the neighbouring regions of Singida, Shinyanga and Kigoma regions. On top of that it has good working relations with government leaders, policy makers, religious leaders, Civic Organisations, Community Based Organisations (CBOs), Faith Based Organisations (FBOs), Small and Medium Enterprises (SMEs) and other actors in the media arena

The Radio Station has ample potentials for growth and expansion of services in the forthcoming years, because is well prepared in terms of coping with the the latest transmission technology in Tanzania.

WIZARA YA FEDHA YAITA WADAU KUTOA MAONI YA KUBORESHA MWONGOZO WA USIMAMIZI WA MALI ZA SERIKALIWizara ya Fedha imetoa rai...
17/12/2025

WIZARA YA FEDHA YAITA WADAU KUTOA MAONI YA KUBORESHA MWONGOZO WA USIMAMIZI WA MALI ZA SERIKALI

Wizara ya Fedha imetoa rai kwa wadau kutoa maoni yatakayowezesha kuboresha Rasimu ya Mwongozo wa Usimamizi wa Mali za Umma wa mwaka 2025 utakaosaidia kusimamia mali zilizo kwenye Taasisi za Umma  kwa tija na ufanisi zaidi ili kuimarisha na kuboresha huduma zinazotolewa na Serikali kupitia mali hizo.

Rai hiyo ilitolewa na Mkurugenzi wa Idara ya Usimamizi wa Mali za Serikali, Wizara ya Fedha, Chotto Sendo, wakati akifungua kikao kazi cha kukusanya maoni ya wadau kutoka taasisi 25 za Umma zinazowakilisha Mkoa wa Dodoma, Wasimamizi wa Mali wa Mikoa kutoka mikoa saba (7), Wasimamizi wa Mali za Serikali kutoka Ofisi ya Makao Makuu na Mkoa wa Dodoma, kuhusu Rasimu ya Mwongozo wa Usimamizi wa Mali za Umma wa mwaka 2025, kilichofanyika katika ukumbi wa Kilimanjaro, Treasury Square, Jijini Dodoma.

Sendo alisema, Rasimu ya Mwongozo wa Usimamizi wa Mali za Umma wa mwaka 2025, ambao wadau wanatarajiwa kutoa maoni ya kuuboresha inatokana na fursa mbalimbali  zilizojitokeza katika usimamizi wa mali za umma katika kipindi cha utekelezaji wa Mwongozo wa Usimamizi wa Mali za Umma wa mwaka 2019.

Aliongeza kuwa rasimu hiyo pia imejumuisha usimamizi wa mali chini ya ushirikiano wa umma na binafsi (PPP-Projects), Upatikanaji wa mali, matumizi ya mali, usimamizi wa mali za miradi, kushughulikia ajali na potevu za mali za Umma, Ufutaji na uondoshaji wa mali chakavu pamoja usajili wa vyombo vya moto.

Alisema kuwa mwongozo huo utakapokamilika na kusainiwa na Mlipaji Mkuu wa Serikali (PMG) utaanza kutumika pamoja na Kanuni za Usimamizi wa Mali za Umma za mwaka 2024 hivyo kuwataka kujadili kwa uwazi ili kujenga uelewa wa pamoja katika suala la usimamizi wa mali za umma na kuhakikisha utendaji bora ,uwajibikaji wa kifedha na utoaji wa huduma bora.

Magic TipNi kwa nini Marafiki wanakuwa wazito kuwaungisha Biashara  Marafiki zao???
17/12/2025

Magic Tip

Ni kwa nini Marafiki wanakuwa wazito kuwaungisha Biashara Marafiki zao???

TUZO YA JAFO YALENGA KUINUA VIWANGO VYA UTENDAJI KWA WENYEVITI WA VIJIJI KISARAWENa.Mwandishi Wetu-KisaraweMBUNGE wa Jim...
17/12/2025

TUZO YA JAFO YALENGA KUINUA VIWANGO VYA UTENDAJI KWA WENYEVITI WA VIJIJI KISARAWE

Na.Mwandishi Wetu-Kisarawe

MBUNGE wa Jimbo la Kisarawe, Dkt. Selemani Jafo, ametangaza kuanza kutolewa kwa Tuzo ya Jafo ya Ufanisi wa Juu kwa Mradi wa Maendeleo, ikiwa ni mpango wa kutambua na kuhamasisha utendaji bora, ubunifu na uwajibikaji miongoni mwa Wenyeviti wa Vijiji katika Halmashauri ya Wilaya ya Kisarawe.

Akizungumza na Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji wilayani humo, ikiwa ni sehemu ya ziara yake ya kuwashukuru kwa kuchaguliwa tena kuwa Mbunge wa jimbo hilo, Dkt. Jafo amesema tuzo hiyo (JAFO’s High Perfomance Development Project Award), inalenga kukuza ufanisi wa juu katika usimamizi wa miradi ya maendeleo, kuongeza uwajibikaji na kuibua ushindani chanya miongoni mwa wenyeviti hao.

Amesema tuzo hiyo itatolewa kila mwaka ili kumtambua na kumzawadia Mwenyekiti au Mwakilishi wa Kijiji aliyeonesha utendaji wa hali ya juu, ubunifu na matokeo yanayopimika katika kusimamia mradi ndani ya Halmashauri hiyo

“Tuzo hii ni kwa Mwenyekiti wa Kijiji au mwakilishi wa kijiji atakayeng’ara kwa mafanikio ya kipekee katika kuibua, kutekeleza miradi ya maendeleo kwa kasi, hususan ile yenye athari chanya katika sekta za afya, elimu, kilimo, biashara, michezo na miundombinu, ninalenga kuhamasisha viongozi wetu wa vijiji kufanya kazi kwa bidii, ubunifu na uwazi zaidi. Tunataka kuona matokeo halisi yanayogusa maisha ya wananchi,” amesema Dkt. Jafo.

Mbunge huyo ameongeza kuwa tathmini ya mshindi wa tuzo hiyo itazingatia vigezo mbalimbali, ikiwemo utekelezaji wa miradi yenye athari kubwa ndani ya muda uliopangwa, maboresho yanayopimika katika utoaji wa huduma, usimamizi bora wa rasilimali, ushiriki wa wananchi na wadau pamoja na uendelevu wa miradi iliyotekelezwa.

Amesema pia tuzo hiyo itahusishwa moja kwa moja na mradi au mpango mahsusi wa maendeleo, ambapo ushahidi wa matokeo k**a ongezeko la ufanisi, ubora wa huduma na kuridhika kwa wananchi utatumika k**a msingi wa tathmini.

Awali, Dkt. Jafo amepongeza mchango mkubwa wa Wenyeviti wa Vijiji na Vitongoji, akisema wao ni kiungo muhimu katika utekelezaji wa mipango ya maendeleo ya serikali ngazi ya msingi.

15/12/2025

JESHI LA POLISI MKOA WA TABORA LAWATAKA VIJANA KUENDELEA KULINDA AMANI.

Jeshi la Polisi likishirikiana na Serikali katika Wilaya ya Kaliua Mkoani Tabora limeendesha Mashindano ya Mpira wa Miguu baina ya timu ya Polisi Wilayani humo na Maafisa usafirishaji Maarufu k**a boda boda lengo ikiwa ni kuendelea kukomaza Mahusiano ya Jeshi la Polisi na Wananchi.

Katika Mashindano hayo ambayo yamefanyika Disemba 13,2025 katika Uwanja wa Kolimba wilayani Kaliua awali akizungumza Kamanda wa Jeshi la Polisi Mkoa wa Tabora Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Jeshi la Polisi (Sacp) Richard Abwao amewataka Wananchi hasa vijana kuwa mabalozi wa kulinda amani na sio kutumika katika vitendo vinavyochochea uvunjifu wa Amani.

Mkuu wa Wilaya ya Urambo Dkt Khamis Mkanachi akimwakilisha Mkuu wa Mkoa wa Tabora Bwana Paul Chacha katika Mashindano hayo mbali na kutoka pongezi kwa Jeshi la Polisi kwa hatua ya kuendelea kujenga Mahusiano imara na Wananchi amesema kuwepo kwa utulivu ni sababu tosha ya kuwafanya kujiimarisha kiuchumi kupitia shughuli zao za kila siku.

Kwa upande wao baadhi ya Wananchi wakiwemo Maafisa usafirishaji (Bodaboda) John Venas na Mihayo Peter wameishukuru Serikali ya Wilaya hiyo kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi katika kuandaa Mashindano hayo huku wakieleza kuendelea kutoka ushirikiano wa dhati kwa Jeshi la Polisi katika kukabiliana na vitendo vya uhalifu na uvunjifu wa amani.

15/12/2025

Mratibu wa BEVAC ngazi ya taifa, Flora Nandi, amesema utekelezaji wa Sera ya Taifa ya Ufugaji Nyuki umeleta tija kubwa katika kuimarisha na kuendeleza shughuli za ufugaji nyuki mkoani Tabora, hatua inayochochea ukuaji wa sekta hiyo na kuinua kipato cha wafugaji.

Akizungumza na CG FM Nandi amesema sera hiyo imeweka misingi imara ya maendeleo kwa kuboresha mazingira ya ufugaji, kuimarisha uzalishaji na kuongeza ushindani wa bidhaa za nyuki katika masoko ya ndani na nje ya nchi.

Ameeleza pia mikakati ya kuanzisha hifadhi na kanda za nyuki, akibainisha kuwa hadi sasa hifadhi saba zimekamilisha michakato ya uanzishwaji, jambo linalolenga kulinda mazingira ya nyuki, kuongeza uzalishaji endelevu na kudhibiti uharibifu wa misitu.

“Uanzishwaji wa hifadhi na kanda za nyuki ni hatua muhimu katika kuhakikisha rasilimali hii inalindwa na kunufaisha kizazi cha sasa na kijacho,” alisema Nandi.

Vilevile, amepongeza mradi wa BEVAC kwa mchango wake mkubwa katika kuongeza thamani ya zao la nyuki, hususan kupitia uboreshaji wa ubora wa asali na bidhaa zake, uendelezaji wa masoko, pamoja na kuwajengea uwezo wafugaji na wadau wa sekta hiyo.

15/12/2025

Ligi daraja la tatu ngazi ya mkoa w Tabora imeendelea kutimu vumbi katika viwanja mbalimbali mkoani hapa ambapo katika uwanja wa Kumbukumbu ya Vita mjini Tabora leo zimechezwa mechi mbili.

Moja ya michezo hiyo ni ule uliozikutanisha Majimaji FC dhidi ya Mwenge FC ambapo mchezo huo umemalizika kwa timu hizo kugawana alama moja.

Magic TipKitu gani Kilisababisha Ukajulikana sana  kwenye Shule uliyosoma??
15/12/2025

Magic Tip

Kitu gani Kilisababisha Ukajulikana sana kwenye Shule uliyosoma??

15/12/2025

WANAWAKE MANISPAA YA TABORA WASHAURIWA KUWAUNGA MKONO WAUME ZAO JUU YA MATUMIZI YA KONDOM.
Usikose kusikiliza Taarifa yetu ya Habari Saa 10:00 Jioni
Leo Desemba 15,2025

MWAMBE AACHIWA KWA DHAMANA, MAHAKAMA YAONDOA MAOMBI DHIDI YAKEAliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji)...
15/12/2025

MWAMBE AACHIWA KWA DHAMANA, MAHAKAMA YAONDOA MAOMBI DHIDI YAKE

Aliyekuwa Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu (Uwekezaji), Geofrey Mwambe, ameachiwa kwa masharti ya dhamana katika Kituo cha Polisi cha Kati (Central Police), hatua iliyobadili mwelekeo wa shauri lake lililokuwa likisubiriwa..

Kutokana na kuachiwa kwake, Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kisutu imeyaondoa rasmi maombi Na. 289778/2025 ambayo Mwambe alikuwa ameyafungua kupitia wakili wake, Hekima Mwasipu.

Akizungumza nje ya mahak**a, Wakili Mwasipu alisema kuwa waliwasilisha ombi la kuondoa maombi hayo baada ya mteja wao kupatiwa dhamana tangu Alhamisi, Desemba 14, 2025.

Alibainisha kuwa hoja hiyo haikupingwa na upande wa Jamhuri, hivyo mahak**a ikaidhinisha kuondolewa kwa maombi hayo bila pingamizi.

15/12/2025

Karibu kwenye Gumzo la Mseto leo! Leo tunawasha mjadala mzito unaotikisa vikundi vingi vya kuweka na kukopa.
🔥 Mvutano upo kwenye suala la Uvunjaji wa Vikoba! Swali letu la leo: Je, ni sahihi mwanaume kuongoza na mwenza wake au mke wake katika uvunjaji wa Vikoba?
Tuambie maoni yako hapo chini 👇 Unadhani inapaswa kuwa vipi na kwa nini.
Endelea kusikiliza CGFM… Wiki yetu imeanza rasmi na mada moto kuhusu Vikoba!

Address

PO Box 2207 TABORA
Tabora

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when CG FM Radio posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to CG FM Radio:

Share