Scope Media

Scope Media Online Media deals with Sports News 🇹🇿
(2)

03/10/2025

Mzee wa VAR Mchome Mapovu anahoji kwanini Eliud Ambokile wa Mbeya City hajafungiwa alafu Bacca kafungiwa mechi Tano.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media

"Viongozi wote Wameitwa kikao Usiku huu, Tajiri kawa mkali sana huu uzembe wa kuajiri Kocha kutoka nje Halafu hana Vyeti...
03/10/2025

"Viongozi wote Wameitwa kikao Usiku huu, Tajiri kawa mkali sana huu uzembe wa kuajiri Kocha kutoka nje Halafu hana Vyeti. Kawapa Usiku huu wawe wameshapata Ufumbuzi wa hili jambo. Sasa Mpango wa sasa hivi ni kuchezesha k**a kipindi kile Yule CEO aliyetoka Rwanda ionekane jamaa hana vigezo vya kufanya kazi, Wavunje Mkataba chaap."

Jasusi wetu Kasema Leo Tusilale wakuu.. Kunawaka Moto huko".

Ameandika Meneja wa habari na mawasiliano wa Yanga SC Ally Kamwe kupitia ukurasa wake wa Instagram

03/10/2025

Mzee wa VAR Mchome Mapovu anasema kwenye CV 200 ambazo Viongozi wa Simba walisema zimetumwa inakuaje anaajiriwa kocha ambae hana vigezo.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media

Mchezaji wa klabu ya Young Africans, Ibrahim Abdullah amefungiwa michezo mitano (5) kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi ...
03/10/2025

Mchezaji wa klabu ya Young Africans, Ibrahim Abdullah amefungiwa michezo mitano (5) kwa kosa la kumkanyaga kwa makusudi mchezaji wa klabu ya Mbeya City, Ibrahim Ame, rafu ambayo ilionekana kuwa mbaya zaidi na ingeweza kuhatarisha usalama wa mchezaji huyo.

Adhabu ni kwa mujibu wa Kanuni ya 41:21 ya Ligi Kuu kuhusu Udhibiti kwa Wachezaji.

Mwamuzi wa kati wa mchezo tajwa hapo juu, Omary Mdoe kutoka Tanga ameondolewa kwenye orodha ya waamuzi kwa mizunguko mitano (5) kwa kosa la kushindwa kutafsiri vema sheria za mpira wa miguu na kushindwa kuchukua hatua kwa vitendo vya ukiukwaji wa sheria za mpira.

Pamoja na matukio mengine, Omary Mdoe alishindwa kutafsiri sheria katika dakika ya 46 ambapo mchezaji wa Mbeya City, Matheo Anthony alishika mpira ndani ya eneo la penati lakini hakuchukua hatua yoyote. Mwamuzi huyo pia alishindwa kuchukua hatua baada ya mchezaji Ibrahim Abdullah kucheza rafu mbaya katika dakika ya tatu ya mchezo.

03/10/2025

Afisa habari wa TFF ametoa taarifa kuhusu ratiba ya kambi ya Taifa Stars kwaajili ya kujiandaa na mechi mbili, Moja ya kuwania kufuzu Kombe la Dunia dhidi ya Zambia na nyingine mechi ya kirafiki dhidi ya Iran.

Breaking News "kocha wa Gaborone Utd, raia Dimitar Pantev (49) ameaga rasmi ndani yaSimba wamekubali kumpa kila hitaji l...
02/10/2025

Breaking News "kocha wa Gaborone Utd, raia Dimitar Pantev (49) ameaga rasmi ndani ya

Simba wamekubali kumpa kila hitaji lake hivyo muda wowote kuanzia sasa atatua Dar es salaam ili kukamilisha dili lake na Mnyama."

Ameandika Mchambuzi Hans Rafael kupitia ukurasa wake wa Instagram

"Siwezi kusema Mpanzu ni mchezani bora kwenye kikosi cha Simba, ila alikuwa mchezaji wa pili au wa tatu kwenye klabu ya ...
02/10/2025

"Siwezi kusema Mpanzu ni mchezani bora kwenye kikosi cha Simba, ila alikuwa mchezaji wa pili au wa tatu kwenye klabu ya Simba SC.

Tangu amejiunga na SIMBA msimu uliopita amehusika kwenye mabao tisa, akifunga manne akiassist mara tano, na ni mtu aliyeingia dirisha dogo maana yake amecheza zaidi y amechi kumi, wakati ambao Ahoua amefunga zaidi ya magoli kumi tokea january kuelekea mwisho wa msimu. Hiki anachokifanya msimu huu Mpanzo ndio uhalisia wa uwezo wake sasa"

Mchambuzi wa soka Alex Ngereza

Bernardo Lopes, mchezaji chipukizi wa soka kutoka Rio De Janeiro Brazil, ambaye anacheza kwenye akademi ya BotafogoHali ...
02/10/2025

Bernardo Lopes, mchezaji chipukizi wa soka kutoka Rio De Janeiro Brazil, ambaye anacheza kwenye akademi ya Botafogo

Hali aliyonayoo usoni Bernardo imevuta hisia za watu wengi na kufanya picha zake siku za hivi karibuni kusambaa sana kwenye mitandao ya kijamii

Sasa swali ni je hali yake ya makovu aliyonayo usoni imesababishwa na nini?

Ukweli ni kwamba wakati Bernardo akiwa na umri wa mwaka mmoja tu alipata ajali mbaya ya kumwagikiwa na Maji ya moto akiwa nyumbani kwao.

Mama yake alikuwa akichemsha Maji ya kuoga kwenye birika, lakini alitoka kidogo kwenda nje na Bernardo akaingia jikoni na kwa bahati mbaya akavuta birika lenye maji yanayochemka ambayo yalimmwagikia usoni na mwilini mwake.

Madaktari wengi walidhani angekufa kutokana na kuungua vibaya sana, lakini baada ya miezi 7 ya upasuaji, kupandikizwa ngozi na muda wa kulazwa hospitalini aliweza kuendelea vizuri

Tangu wakati huo, alipenda kucheza mpira wa miguu. Alianza kucheza soka la mtaani na wajomba zake.Kisha alijiunga na akademi ya mtaani, na hivi majuzi alicheza katika mashindano mbele ya maskauti na baada ya kuvutiwa nae alichukuliwa na Botafogo. Baada ya kufanya majaribio yenye mafanikio, sasa ni sehemu ya wachezaji chipukizi wanaocheza kwenye akademi ya Botafogo na tayari amecheza mchezo wake wa kwanza akiwa kwenye akademi ya Botafogo

Bernardo ni mfano wa Hadithi ya kutokukata tamaa, ujasiri na kujiamini, kwani haogopi wala haoni haya juu ya makovu yake badala yake anaonyesha kipaji chake.

Image: Rising Ballers

02/10/2025

Jamaa anauliza au Yanga ndio timu ya Taifa yenyewe nini maana timu zinazoifunga Yanga lazima ziuzwe.

Osbon Musa

02/10/2025

Meneja wa habari na mawasiliano wa Yanga Ally Kamwe amethibitisha kuwa alama mbili ambazo Yanga wamezipoteza Jijini Mbeya wanajua pakuzipata na hata alie nazo anajijua.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media

02/10/2025

Meneja wa habari na mawasiliano wa Yanga Ally Kamwe anawauliza Wachambuzi Kocha Ibenge nae hafai maana amepata sare dhidi ya JKT Tanzania.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media

02/10/2025

Meneja wa habari na mawasiliano wa Yanga SC Ally Kamwe ametoa majibu kuhusu taarifa zinazosambaa mitandaoni kuwa Viongozi wa Yanga walikaa vikao vya kujadili kuhusu kumfukuza kocha Roman Folz baada ya kupata Sara dhidi ya Mbeya City

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media

Address

Tandika

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Scope Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share