Scope Media

Scope Media Online Media deals with Sports News ๐Ÿ‡น๐Ÿ‡ฟ
(2)

14/12/2025

Mzee wa VAR anasema amefurahi kuona Shabiki wa Simba SC Aggy Simba kuitwa Polisi Leo kwaajili ya kufanyiwa mahojiano.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media.

Kocha wa zamani wa Yanga SC Nassredine Nabi kupitia ukurasa wake wa insta story ameandika ujumbe wa masikitiko baada ya ...
14/12/2025

Kocha wa zamani wa Yanga SC Nassredine Nabi kupitia ukurasa wake wa insta story ameandika ujumbe wa masikitiko baada ya kupokea taarifa za kifo cha aliewahi kuwa Mchezaji wake kwenye kikosi cha Yanga msimu wa 2021/2022 Chico Ushindi ambae alifariki Dunia December 13,2025

Kwenye andiko hilo Kocha Nabi amemuelezea Chico Ushindi k**a mtu aliekuwa na ukarimu kwa watu wote.

Nabi ameandika ujumbe huo akieleza kuwa

"Dรฉvastรฉ par la triste nouvelle. Un de mes anciens joueurs, mais surtout un homme d'une gentillesse inouรฏe. Repose en paix, Chico. Mes priรจres et pensรฉes vont ร  sa famille.

Kwa lugha ya Kingereza

"Devastated by the sad news. One of my former players, but above all, a man of incredible kindness. Rest in peace, Chico. My prayers and thoughts are with his family."

Kwa tafsiri ya Kiswahili

"Nimehuzunishwa na taarifa za kusikitisha. Mmoja wa wachezaji wangu wa zamani lakini zaidi ya yote ni mtu mwenye ukarimu wa ajabu. Pumzika kwa amani, Chico. Sala na mawazo yangu yako pamoja na familia yake."

14/12/2025

Mzee wa VAR Mchome Mapovu amempongeza Rais wa Yanga Engineer Hersi Said kwa kufundisha kwenye semina ya FIFA huko Doha Qatar.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media.

14/12/2025

Shabiki wa Azam FC amelalamika kitendo cha mchezaji wa Simba Allasane Kante kumpiga buti Feisal Salum na akieleza kuwa kitendo hicho sio cha kiuana Michezo.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media.

13/12/2025

Shabiki wa Azam FC anasema Furaha haiwezi kuisha kirahisi kwa sababu wamepita na Mshangazi wa mtu.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media.

Mshambuliaji wa Pyramids Fiston Mayele ambae amewahi kucheza klabu Moja na Marehemu Chico ushindi wakati wakiwa pamoja k...
13/12/2025

Mshambuliaji wa Pyramids Fiston Mayele ambae amewahi kucheza klabu Moja na Marehemu Chico ushindi wakati wakiwa pamoja kwenye klabu ya Yanga msimu wa 2021-2022 amepokea kwa masikitiko makubwa taarifa za kifo cha mchezaji mwenzake Chico Ushindi kilichotokea Leo December 13,2025

Mayele ameonyesha kusikitishwa a taarifa hizo kwa kupost picha akiwa na Chico Ushindi wakati wakiwa Yanga na kuiwekea ujumbe wa "Pas aujourd'hui frรจre ๐Ÿ’”๐Ÿ˜ญ" kwa kingereza " Not today brother ๐Ÿ˜ญ๐Ÿ’”" akimaanisha insigekuwa Leo kwa nyota huyo kufariki

Chico Ushindi atakumbukwa kwenye mioyo ya Mashabiki wa Yanga ambao aliisaidia Yanga kutwaa Ubingwa wa NBCPL msimu wa 2021/2022.

13/12/2025

Shabiki wa Azam FC anasema shida kubwa ya Simba sio Mangungu wala Matola k**a ambavyo baadhi ya Mashabiki wa Simba wanadai

Mwenezi anadai shida kubwa ya Simba ni Mla pilipili ndio kikwazo unyamani.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media.

Ni huzuni kubwa katika tasnia ya soka barani Afrika baada ya kuthibitishwa kifo cha aliyekuwa mshambuliaji wa klabu za T...
13/12/2025

Ni huzuni kubwa katika tasnia ya soka barani Afrika baada ya kuthibitishwa kifo cha aliyekuwa mshambuliaji wa klabu za TP Mazembe, YANGA na AS Vita Club (VClub), Chico Ushindi, amefariki dunia leo siku ya Jumamosi, December 13.

KUMBUKUMBU:

Chico Ushindi anakumbukwa k**a mmoja wa washambuliaji mahiri waliowahi kuichezea klabu hizo kubwa za Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo, pamoja na Young Africans ya Tanzania akitoa mchango mkubwa katika mafanikio yao kwenye mashindano ya ndani na ya kimataifa.

Kifo chake kimeacha pengo kubwa kwa familia yake, marafiki, pamoja na jamii nzima ya michezo, hususan mashabiki wa TP Mazembe na AS Vita Club.

Familia ya michezo na wadau mbalimbali wameendelea kutoa salamu za rambirambi, wakimtaja marehemu k**a mchezaji aliyekuwa na nidhamu, kipaji na mchango mkubwa katika maendeleo ya soka la Afrika.

13/12/2025

Shabiki wa Azam FC Mwenezi wa Azam FC anasema kuwa Mashabiki wa Simba wametafuta njia mpya ya kutaka kunywa supu tu hakuna cha Albadir.

Tazama mahojiano haya kwa urefu zaidi kwenye YouTube channel ya Scope Media.

Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani [FIFA], Limemchagua Rais wa Klabu ya yangasc na Mwenyekiti wa Umoja wa vilabu Afrik...
13/12/2025

Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani [FIFA], Limemchagua Rais wa Klabu ya yangasc na Mwenyekiti wa Umoja wa vilabu Afrika [ACA], Eng. Hersi Said kuwa miongoni mwa Wataalam watakaofundisha kwenye Kongamano kubwa la Mpira litakalofanyika Doha, Qatar, siku ya kesho, Desemba 14,2025.

Eng. Hersi, amepangiwa na FIFA kufundisha kwenye mada ya KEY ELEMENTS FOR CLUB SUCCESSFUL TRANFORMATION [MFUMO WA MABADILIKO YA KLABU].

Miongoni mwa Wataalam wengine wa mpira Duniani watakaozungumza kwenye Kongamano hili ni Kocha wa zamani wa Arsenal, Arsene Wenger, Roberto Di Mateo, Dennis Wise, Alexander Pato, Eric Abidal na wengine kibao

Eng Hersi Said ndiye mtaalamu pekee wa Mpira kutoka Afrika aliyepata nafasi ya kufundisha Kwenye Kongamano hilo.

Meneja wa habari na mawasiliano wa Yanga SC Ally Kamwe kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika โœ๐Ÿฟ ""Dogo kwema? Jama...
11/12/2025

Meneja wa habari na mawasiliano wa Yanga SC Ally Kamwe kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika โœ๐Ÿฟ

""Dogo kwema? Jamaa jana wamepiga biti picha za kikao zisipande ili kuua soo, Lakini moja katika maamuzi waliyokubaliana ni Kumfukuza kazi yule kocha msaidizi. Wanasema kwenye hili janga lazima watafute mbuzi wa kumtoa kafara ili wao wawe salama kwa mashabiki, hivyo wamemla kichwa. Taarifa yake itatoka muda sio mrefu. Kumejadiliwa mengi sana jana na nitakupa habari zote, tatizo lako umekuwa mzito siku hizi kutoa hizi habari kwa haraka, shida nini?"

JASUSI KACHUKIA NINAVYOCHELEWESHA HABARI๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚๐Ÿ˜‚".

Meneja wa habari na mawasiliano wa Simba SC Ahmed Ally kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika โœ๐Ÿฟ "Nimefikiria jambo...
11/12/2025

Meneja wa habari na mawasiliano wa Simba SC Ahmed Ally kupitia ukurasa wake wa Instagram ameandika โœ๐Ÿฟ

"Nimefikiria jambo la kuwaziba midomo hawa mashabiki Nyuma mwiko, nimefikiria mambo mawili tuandae pambano la masumbwi tuwatandike au tuandae mechi ya boli tuwapelekee moto"

Baada ya Ahmed Ally kuandika ujumbe huo Meneja wa habari na mawasiliano wa Yanga SC Ally Kamwe amekoment kwenye post hiyo kwa kuandika

"HUJACHOKA KUGAWA UTAMU TU?๐Ÿ˜„"

Unadhani nini kiandaliwe ili kupunguza Maneno ๐Ÿ˜„..?

Address

Tandika

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Scope Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share