20/09/2025
*Mudir wa Taasisi ya Ansaar Muslim Youth Centre Sheikh Salim Barahiyan ameupongeza Uongozi wa tawi la Kigombe kwa juhudi za kukuza ufaulu wa wanafunzi wa shule ya Tawheed kukua kwa kasi na kuifanya shule hiyo kuwa bora.*
Akizungumza katika mahafali ya 17 ya shule ya Tawheed iliyopo kata ya Kigombe wilaya Muheza mkoa wa Tanga, ameupongeza uongozi na kuwataka kujipanga kwa ajili ya mfumo mpya wa elimu ambao unatarajiwa kuanza huku akisisitiza kuboresha mawasiliano kati yao na makao makuu ya taasisi ili kuweza kuleta maboresho ya pamoja.
Naye Afisa Elimu Kata Kigombe Seif Ally Mahiku amewataka wakazi wa Kigombe haswa wazazi wa wanafunzi kujitahidi kulipa michango kwa wakati ikiwemo ada za shule ili kutowapa wakati mgumu waendeshaji wa shule ya Tawheed sanjari na kufika shuleni ili kuweza kujadili maendeleo ya wanafunzi, kuboresha maadili na kutatua changamoto kwa pamoja.
Kwa upande wake Kiongozi wa tawi la Kigombe Sheikh, Yusuph Muhammad amewahimiza waumini kujitolea katika mambo ya kheri ili kujitengezea amali njema mbele ya mola wao, ikiwemo kuchangia ujenzi wa madarasa ya Tawheed ambayo yatatumika kujifunza dini.
.1