Radio Nuur Tanga

Radio Nuur Tanga 📻 94.5MHz TANGA

Kituo cha Hikma !!!

20/08/2025
𝗨𝗝𝗨𝗠𝗕𝗘 𝗪𝗔 𝗟𝗘𝗢 !!! ✍
20/08/2025

𝗨𝗝𝗨𝗠𝗕𝗘 𝗪𝗔 𝗟𝗘𝗢 !!! ✍

19/08/2025

Tutengeneze mazingira ya kuwalea Watoto wetu kujiheshimu...

Sheikh Mohammed Al-Busaidy Istiqaama Tanga Tz

Katika harakati za kusaidia kaya duni Afisa ustawi wa jamii jijini Tanga Godfrey Akuno  amewata wananchi wenye mahitaji ...
19/08/2025

Katika harakati za kusaidia kaya duni Afisa ustawi wa jamii jijini Tanga Godfrey Akuno amewata wananchi wenye mahitaji maalumu kujitokeza kwa wingi kuchukua mikopo ya asilimia kumi (10%) inayotolewa na Halmashauri yao ili kuhakikisha familia hizo zinapata fedha hizo zitakazowasaidia kufungua biashara na kuwawezesha kuondokana na hali ya utegemezi.

‎Akuno ameyasema hayo alipokuwa akizungumza na Radio Nuur fm na kueleza kuwa kaya maskini zijitahidi kujitokeza kwa wingi ili waweze kuwezeshwa kiuchumi na kuwa wajasirimali imara kwa kupata mikopo hiyo ambayo haina riba.

‎"Kaya masikini zinawezeshwa kiuchumi na serikali imeleta mikopo hiyo ili kuwawezesha wahusika kupata mitaji na kujikwamua kiuchumi kwani ni mikopo ambayo haina riba hivyo jamii ijitokeze kwa wingi",Amesema Akuno.

‎Aidha, amewaomba wananchi hao kuachana na dhana potofu au kuona aibu kujitokeza katika kupata misaada ili kukidhi mahitaji hayo na kuepukana na hali ngumu ya kimaisha.

‎Vilevile amewataka wananchi kuonesha usihrikiano na wafanyakazi mbalimbali ili kupata msaada unapohitajika.

‎"Watu wenye mahitaji maalumu wasikae kimya kwa kuona haya kwani mikopo hii ipo kwa ajili ya kukwamua hali za wananchi kiuchumi na kuimarisha maendeleo kwa ujumla,pia watoe ushirikiano kwa viongozi waliopo karibu kwa msaada zaidi",Akuno ameongezea .

‎Nae Mwenyekiti wa Mtaa wa Kwanjeka A kata ya Mnyanjani Hussein Ramadhan Mndogi mesema yupo tayari kuwasaidia kuwasaidia wale wote wanaoishi kwenye familia duni ndani ya mtaa wake lengo ni kuwawezesha kupata kupata mahitaji yao na kukabiliana na hali ngumu ya Maisha kupitia mikopo hiyo.

‎Pia, amewaomba wakazi wa mtaa huo kuwa na umoja katika kuwasaidia na kuwakwamua kiuchumi familia zenye mahitaji maalumu ii kuimarisha maendeleo ya jamii na taifa kwa ujumla.

‎"Nitahakikisha kwa upande wangu k**a Mwenyekiti wa mtaa huu kwa kusaidia kaya masikini zinapata elimu na msaada kwa kushirikiana na wadau mbalimbali", amesema Mndogi.

‎Mwandishi | Nastaini Hamisi
‎Mhariri | Khatib Omari

18/08/2025
18/08/2025

Huyu ndiye Maskini...

Sheikh Salim Al-Abry Istiqaama Tanga Tz

Katika kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika October 29 mwaka huu, Waandishi wa habari nchini wametakiwa  kufany...
18/08/2025

Katika kuelekea uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika October 29 mwaka huu, Waandishi wa habari nchini wametakiwa kufanya shughuli zao kwa kuzingatia maadili ya taaluma hiyo.

‎Aidha wametakiwa kutoa elimu kwa wananchi ili waweze kupata taarifa sahihi na kwa wakati sisizokuwa na upendeleo wowote, zisizokweza utu wa mtu ili kufanya uchaguzi huo kuwa wa haki usalama na amani kwa maslahi ya Taifa.

‎Kauli hiyo imetolewa leo Agost 16, 2025 na mkuu wa wilaya ya Longido Salum Kali kwa niaba ya mkuu wa mkoa wa Arusha Kenan Kihongosi alipokua akifungua mkutano wa wadau wa sekta ya habari na utangazaji kuelekea uchaguzi mkuu uliofanyika katika ukumbi wa kimataifa wa AICC jijini Arusha.

‎Awali Kaimu Mkurugenzi wa idara ya Habari maelezo Rodney Mbuya amesema kutokana na sekta ya habari kubeba dhamana kubwa ya kiusalama nchini ndio maana idara ya habari maelezo imeandaa mkutano huo kwa lengo la kubadilisha mawazo ili wananchi waweze kupata taarifa za msingi, sahihi na kwa wakati na zisizo na upendeleo.

‎Akitoa mada kuhusu mwongozo wa waandishi wa habari katika uandishi wa habari za uchaguzi Mhadhiri kutoka chuo kikuu cha Dar es salaam (UDSM) Dkt. Egbert Mkoko amesema mwandishi wa habari anayepaswa kuripoti habari za uchaguzi ni yule aliyethibitishwa na bodi ya ithibati (JAB)

‎Akiwasilisha mada kuhusu kanuni za utangazaji wa uchaguzi kwa vyama vya siasa za mwaka 2020 Meneja wa Huduma za Utangazaji wa TCRA, Mhandisi Andrew Kisaka, amesema vyombo vya habari vinapaswa kuweka mizania kwa vyama vya siasa ili kuepuka kuegemea upande wowote.

‎Akiwasilisha mada kuhusu wajibu wa waandishi wa habari na Jeshi la Polisi katika kulinda usalama kuelekea uchaguzi mkuu Msemaji wa Jeshi la Polisi nchini DCP David Misime amesema waandishi wa habari na Jeshi la Polisi wana wajibu wa kulinda amani kabla wakati na baada ya uchaguzi.

‎"Waandi wa habari na Keshi la Polisi tuna jukumu kubwa la kulinda usalama wa nchi, Jeshi la Polisi likishirikiana vyema na waandishi wa habari nchi itabaki salama hivyo mtumie kalamu zenu vizuri wakati wa kuripoti habari za uchaguzi" Amesema Misime.

‎Na Salimu Omari Ally

Waislamu wamehimizwa kujiandaa kwa kuweka akiba ya fedha ili iwe rahisi kuiendea ibada tukufu ya hijja ambayo ni miongon...
18/08/2025

Waislamu wamehimizwa kujiandaa kwa kuweka akiba ya fedha ili iwe rahisi kuiendea ibada tukufu ya hijja ambayo ni miongoni mwa nguzo za uislamu.

‎Nasaha hizo zimetolewa leo na Sheikh Salim Awadh Bafadhwil alipokuwa akizungumza na waumini dini ya Kiislamu waliohudhuria semina na mafundisho ya ibada ya Hijjah yaliyoandaliwa na Taasisi ya AL HUSNA HAJJ TRUST yaliyofanyika katika ukumbi wa Tanga International jijini Tanga.

‎“Ibada ya Hijja inataka subra katika kumtwii Mola na kujiepusha na maneno machafu yatakayosababisha kumuudhi Allah katika ibada hiyo”,amesema Sheikh Bafadhil.

‎Naye Sheikh Ally Zuber amewataka waislamu kuikusudia ibada ya Hijja ili kuitikia wito wa Mola, kwani mtu anapokwenda Hijja au Umrah anajisafisha na maovu mbalimbali aliyotenda, na atarejea akiwa msafi k**a siku aliyozaliwa na mama yake.

‎“Muislamu ukiwa na uwezo lazima ukusudie kuitikia Ibada ya Mola wako ili udumu kuzitafuta radhi za Mola wako ”amesema Sheikh Zuber.

‎Kwa upande wake Katibu wa AL HUSNA HAJJ TRUST, Ahmad Kizigo amesema wameweka utaratibu wa malipo utakaompa wepesi muislamu anayetaraji kuhiji na kuongeza kuwa zipo njia nyepesi ambazo wameziweka ikiwa ni pamoja na kuwekeza pesa kidogo kidogo kwa kila siku iwe shilingi alfu tano au kumi.

‎Musa Said, Afisa masoko kutoka Benki ya Amana amesema wameweka akaunti maalumu ya kumuwekea muumini pesa yake ili aweze kutekeleza ibada hiyo kwa wepesi.


‎Mwandishi | Abdallah Ngereza
‎Mhariri | Khatib Omari

Address

Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Nuur Tanga posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category