Radio Nuur Tanga

Radio Nuur Tanga πŸ“» 94.5MHz TANGA

Kituo cha Hikma !!!

01/12/2025
π—¨π—π—¨π— π—•π—˜ π—ͺ𝗔 π—Ÿπ—˜π—’ !!! ✍
01/12/2025

π—¨π—π—¨π— π—•π—˜ π—ͺ𝗔 π—Ÿπ—˜π—’ !!! ✍

30/11/2025

Naibu Waziri, Ofisi ya Waziri Mkuu (Sera, Bunge, Uratibu na wenye Ulemavu) Mhe. Ummy Hamisi Nderiananga amepongeza Mwenyekiti wa Taasisi ya Riziki Lulida foundation Mh.Bi Riziki Lulida kwa kujitolea kwake kupigania na kutetea haki za watu wenye ulemavu nchini bila kuchoka.

Akizungumza katika hafla ya uzinduzi wa Mshindano ya Kusoma Qur’an tukufu kwa watu wenye ulemavu msimu wa pili iliyofanyika kwenye ukumbi wa NSSF Jijini Dodoma,Mh.Naibu Waziri Ndaraingana amesema Bi Lulida amekuwa mfano bora kwa kujitoa kwake katika maendeleo ya sera na mikakati ya ustawi wa watu wenye ulemavu.

Mhe. Nderiananga amesema hatoi sifa hizo kwa sababu amenzisha mashindano ya Qur’an kwa watu wenye ulemavu bali ni muda mrefu amekuwa akishuhudia harakati zake katika kutetea kundi hilo muhimu katika jamii.

Ameisifu Taasisi ya Riziki Lulida foundation kwa kuanzisha mashindano ya kuhifadhi Qur’an kwa watu wenye ulemavu maana hiyo yote inatoa taswira ya kuwa ni moja wapo ya kuwathamini na kuwajali watu wenye ulemavu.

Ameongeza kuwa serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania chini ya DKT Samia Suluhu Hassan itaendelea kutengeneza na kusimamia mikakati ya kuwasaidia watu wenye ulemavu ili haki zao zisiminywe katika nyanja zote.

Nae Mwenyekiti wa Taasisi ya Riziki Lulida foundation Hajjat Riziki Lulida amemshukuru Rais wa awamu ya sita wa Jamhuri ya muungano wa Tanzania kwa jitihada zake za kuboresha maisha ya watu wenye ulemavu nchini.

Kuzinduliwa kwa mashindano hayo yanatoa fursa kwa washiriki watakaopita kwenye mchujo ngazi ya mkoa kwenda kwenye fainali zitakazofanyika jijini Dodoma mwishoni mwa mwezi wa desemba mwaka huu ambapo licha ya washiriki kutoka ndani ya nchi lakini pia mwaka huu kutakuwa na washiriki kutoka nje ya nchi.

Khatib Omari

"Msikate tamaa na Rehma za Mwenyezi Mungu." - [Surah Az-Zumar, Ayah 53]
30/11/2025

"Msikate tamaa na Rehma za Mwenyezi Mungu." - [Surah Az-Zumar, Ayah 53]

"Ajabu kila mmoja anajaribu kumtafuta mtu aliye sawa, lakini hakuna anayejaribu yeye mwenyewe kujiweka sawa." ~ Shk. Has...
30/11/2025

"Ajabu kila mmoja anajaribu kumtafuta mtu aliye sawa, lakini hakuna anayejaribu yeye mwenyewe kujiweka sawa." ~ Shk. Hassan Ahmed πŸ‡°πŸ‡ͺ

"Anayeomba au kuuliza usimkaripie." - [Surah Adh-Dhuha, Ayah 10]
30/11/2025

"Anayeomba au kuuliza usimkaripie." - [Surah Adh-Dhuha, Ayah 10]

29/11/2025

Miongoni mwa Watu wenye akili...

Kufunguka kwa fursa za kiuchumi mkoani Tanga kumepelekea Shirika la nyumba la Taifa (NHC) mkoani Tanga kujenga jengo la ...
29/11/2025

Kufunguka kwa fursa za kiuchumi mkoani Tanga kumepelekea Shirika la nyumba la Taifa (NHC) mkoani Tanga kujenga jengo la kisasa litakalokuwa na ghorofa 7 katika maeneo ya Mkwakwani jijini Tanga ambapo ujenzi wake utagharimu shilingi bilioni 8.4.

Furza hizo za kiuchumi ni pamoja na Bomba la mafuta, maboresho ya Bandari ya Tanga, kufunguliwa kwa viwanda pamoja na zao la Mkonge zimepelekea mkoa wa Tanga kumiminika wageni kutoka ndani na nje ya nchi ambao wanauhitaji wa makazi na ofisi.

Kufuatia hali hiyo Shirika la nyumba la Taifa (NHC) mkoani Tanga likaanza rasmi ujenzi wa mradi huo na linatarajia kujenga na miradi mengine mikubwa ili kukidhi matakwa ya ongezeko la wateja wanaohitaji nyumba za kuishi pamoja na ofisi.

Akizungumza na Radio nuur fm ofisini kwake leo Novemba 28,2025 Meneja wa Shirika la nyumba la Taifa (NHC) mkoa wa Tanga Mhandisi M***a Patrick Kamendu amesema jengo hilo lipo maeneo ya Mkwakwani na ndio maana likapewa jina la Mkwakwani Plaza.

"Jengo hili litakuwa na ghorofa saba, sakafu ya chini na sakafu ya pili itakuwa ni kwa ajili ya shughuli za biashara, sakafu ya tatu mpaka sakafu ya saba itakuwa ni nyumba za makazi, kutakuwa na nyumba mbili zenye vyumba viwili na nyumba mbili zenye vyumba vitatu kwa kila sakafu" Amesema Mhandisi M***a

Mhandisi M***a amewaasa wananchi kujitokeza kununua nyumba na kupangisha kwani wakati jengo linaendelea kujengwa tayari kuna watanzania wamejitokeza kununua na kupangisha katika jengo hilo.

Kwa upande wake Msimamizi msaidizi wa ujenzi huo Mhandisi John Joseph Mchechu amesema mradi huo upo katika asilimia 16 ambao utekelezaji wake ulianza mwezi June mwaka 2025 na unatarajia kukamilika mwezi June mwaka 2027.

"Nawaasa wananchi wauone mradi huu kuwa ni wao ni mradi ambao upo kwa ajili yao, kuna vyumba vya maduka, kuna nyumba za kuishi na pia kuna ofisi" Amesema Mhandisi John

Na Salimu Omari Ally

Uwekezaji wa shilingi bilioni 429.1 uliofanywa na Serikali ya Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassani katika Bandari ya Tanga um...
29/11/2025

Uwekezaji wa shilingi bilioni 429.1 uliofanywa na Serikali ya Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassani katika Bandari ya Tanga umeendelea kuleta matunda katika Bandari hiyo.

Matunda hayo ni kutokana na mfululizo wa Meli zinazotia nanga Bandarini hapo ambapo wiki mbili zilizopita Bandari ya Tanga ilipokea Meli yenye tani elfu 33 na leo imepokea Meli ya PARNIA yenye kontena 463 kutoka nchini Iran.

Meli hiyo yenye tani 13 imetia nanga katika Bandari ya Tanga ambapo kati ya kontena hizo 463, kontena 261 ni za mizigo ya ndani ya nchi na kontena 182 ni za mizigo ya Afika Mashariki na SADIC.

Akizungumza na waandishi wa habari leo Novemba 28,2025 baada ya Meli hiyo kuanza kupakuwa mizigo Bandarini hapo mkuu wa mkoa wa Tanga Balozi Dkt. Batilda Burian amesema lango la Afrika Mashariki na SADIC ni kupitia Bandari ya Tanga na Bandari ya Dar es salaam.

"Na ndio maana tunasema hakuna mtaji mkubwa hakuna tunu kubwa k**a tunu ya amani na utulivu katika nchi, sisi utulivu huu sio kwa manufaa ya Tanzania lakini ni kwa manufaa hata ya majirani zetu"

"Leo kukiwa na vurugu ina maana wenzetu tunawakwamisha na sisi wenyewe tunajikwamisha" Amesema Dkt. Batilda

Kwa upande wake kaimu Meneja wa Bandari ya Tanga Peter Milanzi amemshukuru Mhe. Raisi Dkt. Samia Suluhu Hassani kwa kufanya uwekezaji huo ambao unasaidia Meli kubwa kuhudumiwa gatini tofauti na zamani Meli hizo zilikuwa zikihudumiwa kwenye kina cha maji yapata kilometa 2 kutoka Bandarini.

Akizungumza kwa niaba ya wafanyabiashara wa Tanga Mwenyekiti wa Soko la Tangamano Elisi Mohammed amesema wafanyabiashara wanafurahishwa kuona Tanga inafunguka kiuchumi huku akihamasisha wafanyabiashara wenzake kutumia fursa ya uwepo wa Bandari hiyo kusafirisha na kupokea mizigo.

Na Salimu Omari

"Usihuzunike mazuri yako yasipotambulika ardhini, tambua una Mola anakubarikia mbinguni." ~ Shk. Hassan Ahmed πŸ‡°πŸ‡ͺ
29/11/2025

"Usihuzunike mazuri yako yasipotambulika ardhini, tambua una Mola anakubarikia mbinguni." ~ Shk. Hassan Ahmed πŸ‡°πŸ‡ͺ

Address

Tanga

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Radio Nuur Tanga posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category