07/11/2025
(AFRIKA YETU)
Haki + Maadili + Sheria (Justice, Ethics & Laws): ni mambo makuu matatu yeye kulibeba taifa na ikikosekana kimoja wapo hapo lazima kutakuwepo na kundi fulani litakalo-neemeka na lipo kundi lingine litakalo-umizwa, na jingine litakua halielewi wapi lishikilie au liachilie.
ipo hivi: imebeba 'usawa na ukweli' ikisimamiwa na maadili ya nyanja zote pamoja na sheria. Maadili na sheria inazalisha tamaa, chuki, visasi, ufisadi na vifo, ambapo vyote hivi kwa pamoja ni k**a mimba iliyokomaa na kuzalisha kiumbe kiitwacho (Ukosefu wa amani)..
UKOSEFU WA AMANI: hauna CHAMA, hauna DINI, hauna UMRI au RIKA, hauna KABILA, hauna JINSIA' wote wanakuwa wahanga na waathiriwa wa amani hiyo iliyopotezwa.
โ.Meena
๐น๐ฟ๐น๐ฟ
Inawezekana sasahivi kuna mioyo ya watu waliobeba chuki, visasi, hasira na maumivu, wapo wengine mioyo yao imebeba furaha, amani na usalama wa kipato kwa familia zao kulingana na wakati uliopo.
Swali la kujiuliza hapa ni: unazotoa zitajenga au kubomoa!?
Ukweli: Siku zote lawama (kulaumiana) hakutatui tatizo, ipokuwa Huwa zinaongeza tatizo.
Kilichotokea Tanzania' kisichukuliwe kwa lawama za kuelekeza upande fulani kuwa wao ndio wakulaumiwa zaidi kwenye hilo lililotokea isipokuwa kutafutwe kujua chanzo cha hayo ni nini au kipi!?. Kisha kutafutwe dawa au tiba ya kutibu tatizo husika.
"Wanasiasa, Wanausalama, Wananchi, Diaspora, Viongozi wa dini, Media, Wasanii nk." Wote tunawajibika kwa hilo lililotokea.
Huwezi kutibu ikiwa hujui chanzo' kwani ni sawa na kwenda hospitali daktari anakuuliza unaumwa nini? Unajibu sijui nachoumwa docta!๐งญ hapo daktari hawezi kukupa tu dawa, bali itabidi afanye vipimo vyote kung'amua ugonjwa ndio autibu.
Haya maswala kisiasa, utasema ni mbinu na mipango ya wapinzani kutuchafua!๐คทโโ๏ธ ukiyachukulia kiimani, kikabila au kiuraia utasema upande wa pili pia..
Genocide ya Rwanda !?
Vurugu za zanzibar (ccm na cuf) wakati ule baada ya uchaguzi ilikuwaje? (Mataifa mengine ya Afrika, Libya, Nigeria, Congo DRC - imekuwaje!?)
ni tunu ambayo inatakiwa kulindwa kwa gharama zozote, ukiipoteza kuirudisha ni kazi kwelikweli na wakati mwingine ni ndoto kurejea.
Ni wakati ufaao sasa wa pande zote haswa kwa viongozi waliopo madarakani, wanasheria na vyama husika vya siasa Tanzania. Kurudi tena hawa wananchi ambao ndio wamewapa dhamana ya kuwaongoza kwani wanahoja ambazo kimsingi au kwa makusudi hamtaki kuwasikiliza kwa nguvu ya mamlaka mlizonazo.
Swali ni!: wakasemee wapi ikiwa nchi yao wenyewe kupitia taasisi zake (pillars of state) hazitaki kuwasikiliza.?
Kazi ya bunge ni ipi!? Mahak**a ni ipi!? Serekali kazi yake ni ipi!?๐คทโโ๏ธ
Majibu ya hilo swali" unagundua mzizi wake upo kwenye KATIBA' swali je' katiba inajitosheleza kwa wakati tuliopo bila kulenga maslahi ya upande mmoja!? Au inahitaji 'amendment'
Je! Katiba inaelezea mipaka ya kila kimojawapo!? Katiba hiyo je! Kila mhimili unaifuata inavyotakikana!? ๐ด
Chanzo cha tatizo kipo hapaa: mfano. sheria, anavutia upande wake (ili sheria hiyo isimbane inapotokea amevuka mipaka yake ya kiuongozi au mamalaka)
sheria anaongoza kuvunja hizo sheria!
Sasa unategemea vipi kwa huyu mliyemtungia sheria kutaka azifuate ilhali nyie dola wenyewe hamzifuati!?
Itaendelea..........