24/12/2025
SASA ETI WATU WANABISHANA "JE YESU ALIZALIWA TAREHE 25?"
Na hili ni janga kubwa: na kengeuko la kiroho na kiimani haswa kwa waKristo (maFarisayo na waPinga Kristo hii haiwahusu) ambao kila msimu wa CHRISTMASS, Watu wanakazana kwenye majibizano 'kubishana' kwamba
βYesu hakuzaliwa tarehe 25.β ni sikuu ya Mungu jua (ikiasisiwa na wapagani wa kirumi)
FACT: Iwe kweli au siyo kweli, ni inje ya msimamo wako kiimani 'non of your concerns' ilhali haibadilishi msimamo wako usitake kubadilisha msimamo wa wengine.
Huwezi kusoma juujuu k**a unasoma riwaya, hadithi au tamthilia.... biblia ni fumbo, inayoitaji maarifa ya kiroho kuweza kuisoma na kuielewa ila k**a na wewe usomaji wako ni ule wa kukariri mstari mmoja huwezi kuielewa kamwe hadi umauti wako.
MUHIMU KUHUSU CHRISTMAS NI:
Ukisoma: WAKOLOSAI 2:16
> βBasi mtu asiwahukumu ninyi kwa ajili ya chakula au kinywaji, au kwa habari ya SIKUKUU, au mwandamo wa mwezi, au sabato.β
Hapo Biblia imeweka mstari wazi:
USIHUKUMU MTU KWA SABABU YA SIKUKUU FULANI.
WARUMI 14:5
βMtu mmoja AONA SIKU MOJA KUWA BORA KULIKO NYINGINE, mtu mwingine AONA SIKU ZOTE KUWA SAWA; kila mtu na athibitike sana hakika yake mwenyewe.β NENO (Kila mmoja awe na hakika na yale anayoamini)
Anayetaka kusherekea β ASHEREKEE
Asiyetaka kusherekea β AKAE KWA KUTULIA na sio kupitia unachokiamini wewe sasa ujipe mamlaka ya KUHUKUMU wengine, unajikuta Mungu mtu au!?
Hukumu ni ya Mungu: Mathayo 7:1-5 (hapo mmeitwa wanafiki, acheni unafiki)
Awali 25/12 ilichukuliwa k**a siku ya mungu jua.β ba wapagani wa rumi ya kale. K**a unaamini huyo mungu jua, basi hiyo ni imani yako na upo sahihi pia k**a Biblia ilivyosema hapo (na wala hujakosea umepatia kabisa kwa mujibu wa biblia)
Usiishie hapo endelea na ufafanuzi: Biblia inasema hivi βK**a wewe unaamini kusherekea β SHEREKEA KWA BWANA.
K**a huamini β KAA KIMYA KWA BWANA.β
βYEYE AADHIMISHAYE SIKU, HUIADHIMISHA KWA BWANA; naye alaye, hula kwa Bwana, kwa maana amshukuru Mungu; TENA ASIYEKULA, HALI KWA BWANA, naye pia amshukuru Mungu.β
β Warumi 14:6 (Biblia Takatifu)
Yesu alituhusia:
βMpende jirani yako k**a uipendavyo nafsi yako.βπͺ
Hata vitabu vitakatifu vinatufundisha kuwa umoja ni agizo la Mungu na msingi wa maisha ya kijamii yenye amani. Wafilipi 2:2 β βTimizeni furaha yangu kwa kuwa na nia moja, mkiwa na upendo mmoja" Qurβan 3:103 β βShik**aneni kwa kamba ya Mwenyezi Mungu nyote wala msifarikiane.
MUNGU ATUPE MWISHO MWEMA KATIKA MAPOKEO YETU WANADAMU.....π
from various sources!