Sufian Mzimbiri

Sufian Mzimbiri Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Sufian Mzimbiri, Dar es Salaam.
(2)

🔹️Makala za kidini & kijamii
🔸️Visa & historia & hadithi & riwaya
🔹️Simuliz za kufunza & kugusa nyoyo
🔸️Lengo ni kuielimisha jamii nzima.
🔹️Tunasimulia ili ujifunze & uelimike.

Alikaa mtume (s.a.w) ndani ya nyumba yake mara baada ya kufariki  siku ya juma tatu ambayo ndiyo siku aliyokufa.Baasi al...
18/09/2025

Alikaa mtume (s.a.w) ndani ya nyumba yake mara baada ya kufariki siku ya juma tatu ambayo ndiyo siku aliyokufa.

Baasi alikaa siku hiyo ya juma tatu na akakaa usiku wa kuamkia siku ya juma nne na mchana wa siku ya j.tano mpaka walipo komea waislam ktk kumsimamisha Khalifa juu yao waislam.

Kisha akaoshwa na akakafiniwa kwa nguo tatu ambapo hamna ndani yake kanzu wala kilemba.

Kisha akawekwa juu ya kitanda ndani ya nyumba yake, na waislam wakamswalia mtume(s.a.w) swala ya jeneza mtu mmoja mmoja(yaani kila mtu amemswalia mtume swala ya jeneza peke yake bila ya kuwa na imam.

Wakaanza wanaume kisha wakafuatia wanawake kisha watoto.

Kisha mtume(s.a.w) akazikwa ndani ya chumba cha bibi Aisha(r.anha) na likanyanyuliwa kabri lake kutoka usawa wa ardhi kwa kiasi cha shibri moja kisha likanyunyizwa kabri lake kwa maji.

Na kwahakika aliacha mtume(s.a.w) kuwaachia waislam vitu viwili, hakito wadhuru wao waislam kitu chochote muda wa kuwa wao waislam niwenye kudumu kwa kushik**ana kwa vitu hivyo

Navyo vitu hivyo ni:..

1.Kitabu cha Allah(s.wt) ambacho ni (Qur'an) ambacho kamwe hakitoiingilia batwili mbele yake wala nyuma yake, na

2.Sunnah(Hadithi za Mtume s.a.w)ambazo ziko zimeibainisha dini na zikaweka wazi kabsa maksudio ya Qur'an Tukufu

Naamini umesoma mpaka mwisho, baasi angalau mswalie Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasallama ❤️ hakika uki share na wengine pia wakasoma na kunufaika malipo ni juu yako.😍🤲

Follow Sufian Mzimbiri

Allah atudumishe sote ktk ibada ya swala 5
18/09/2025

Allah atudumishe sote ktk ibada ya swala 5

Khidri ni mja miongoni mwa waja wema wa Mwenyezi Mungu. Alitajwa katika Qur’ani katika Surat Al-Kahf (18:60–82). Qur’ani...
18/09/2025

Khidri ni mja miongoni mwa waja wema wa Mwenyezi Mungu. Alitajwa katika Qur’ani katika Surat Al-Kahf (18:60–82). Qur’ani haikutaja jina lake moja kwa moja, bali alitajwa k**a “Mja miongoni mwa waja wetu tuliye mpa rehema kutoka kwetu na tukamfundisha kutoka kwetu elimu (maalum).”

Wanazuoni wengi wa tafsiri wanasema huyo ndiye Al-Khidr (Khidri), na jina lake linahusishwa na “ukijani” (الخضر) kwa sababu kila alipokaa juu ya ardhi kavu, ilijaa kijani cha mimea.

🕳SAFARI YA NABII M***A KUMTAFUTA KHIDRI

Mwenyezi Mungu aliteremsha wahyi kwa Nabii Musa (a.s) kuwa yupo mja maalum ambaye anajua mambo fulani yaliyofichwa. Musa akaazimia kwenda kumtafuta ili ajifunze kutoka kwake.

Nabii M***a (a.s) alisafiri na kijana wake (Yusha’ bin Nun) hadi walipokutana kwenye makutano ya bahari mbili. Alama ya kukutana ilikuwa samaki aliyekufa kuhuika na kupenya baharini.

Waliporudi kufuata nyayo, walimkuta Khidri. Musa akamuomba ruhusa ya kumfuata ili apate elimu. Khidri akasema:

“Hakika wewe hutoweza kusubiri pamoja nami… Vipi utasubiri juu ya jambo ambalo huna ujuzi nalo?”
(Qur’an 18:67–68)

Lakini Musa akaahidi kuvumilia.

💫MATUKIO MATATU YA SAFARI

Khidri na Musa walianza safari yao, na matukio matatu makubwa yalitokea:

(a)Jahazi lililochanwa

Walipanda jahazi la maskini waliowabeba bure. Ghafla Khidri akalichana na kuliharibu sehemu yake.
Musa akapinga: “Umelichana ili kuwatumbukiza watu wake baharini? Hakika umekuja na jambo baya.”
Khidri akamkumbusha: “Je, sikukuambia hutoweza kusubiri?”

Sababu ya kuchana: nyuma yao kulikuwa na mfalme dhalimu aliyekuwa akipora jahazi zima lililo zuri, hivyo aliwaharibia kidogo ili waokoke.

(b)Kuuawa kwa kijana

Walikutana na kijana. Khidri akamuua papo hapo. Musa akasema: “Umemuua nafsi isiyo na kosa? Hili ni jambo baya mno.”
Khidri akamwambia tena: “Je, sikukuambia hutoweza kusubiri?”

Sababu ya kuuawa kijana ni: Kijana huyo k**a angeishi, angeliwafanya wazazi wake waumini kuingia katika upotevu na ukafiri. Mwenyezi Mungu akapanga kuwapa mtoto bora zaidi, mchamungu na mwenye rehema.

(c)Ukuta uliosimamishwa

Walifika mji mmoja. Wakaomba chakula, wakaambiwa hapana. Hapo wakakuta ukuta karibu kuanguka. Khidri akauinua akaujenga tena.
Musa akasema: “Lau ungetaka ungalipata ujira juu ya kazi hii.”

Khidri akasema: “Hii ndiyo njia ya kuachana kati yangu na wewe.”

Sababu ya ukuta: Chini yake kulikuwa na hazina ya mayatima wawili. Baba yao alikuwa mwema, na Mwenyezi Mungu alitaka wazikute hazina zao wakiwa watu wazima.

🍁UFAFANUZI WA MATUKIO

Mwisho Khidri akamwambia Musa:

“Sasa nitakutafsiria yale usiyoweza kuyastahimili… Jahazi nililichana kwa sababu ya mfalme dhalimu… Kijana niliua kwa kuwa angewatesa wazazi wake… Ukuta nilisimamisha ili kulinda hazina ya mayatima… Sikutenda haya kwa amri yangu, bali kwa elimu kutoka kwa Mwenyezi Mungu.”
(Qur’an 18:78–82)

MAFUNZO MAKUU
Katika Kisa hiki tunajifunza mambo mengi, miongoni mwayo ni haya yafuatayo.

1.Elimu ya Mwenyezi Mungu ni pana zaidi kuliko akili zetu – Kuna mambo yanayoonekana mabaya kumbe yana hekima kubwa.

2.Subira ni msingi wa kujifunza.
Musa alikosea kwa haraka kuingilia mambo yaliyofanywa mbele yake, lakini mwisho akafahamu hekima yake.

3.Wema wa mzazi huwalinda watoto.
k**a ilivyokuwa kwa baba wa mayatima.

4.Uovu huondolewa kwa hekima – k**a kuharibu jahazi ili kuzuia madhara makubwa zaidi.

5.Kifo cha mtoto kisichotegemewa ni mpango wa Mwenyezi Mungu – kwa hikma ambayo binadamu hawaioni.

HIVYO BAASI
Hivi ndivyo kisa cha Nabii Khidri na Nabii Musa (a.salaam) kwa ukamilifu wake, k**a kilivyopokelewa katika Qur’ani na kufafanuliwa na wanazuoni. Ni kisa cha kutufundisha subira, tawakkul na kuamini hekima ya Mwenyezi Mungu.

Ukimaliza kusoma usiache kumswalia Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasallama.

Allah atupe mahitajio ya nafsi zetu yale yaliyokuwa ya kheri anayo yaridhia na atupe sote kizazi kilichokuwa chema, na k**a yuko mwenye shida ya kupata Ndoa Allah amchagulie na amuelekeze kwa mwenza aliyekuwa mwema na k**a yupo anayehitajia mtoto baasi Allah amzawadie watoto waliokuwa wema, aamiin.🤲🤲🤲❤️

Usiache ku Follow ukurasa wangu ili uweze kujifunza mengi zaidi👍🙏👇
Sufian Mzimbiri

18/09/2025

Manabii ambao waliishi wakiwa Mabachela/ bila kuoa ni Nani na Nani?

HARUFU NZURI YA MTUME (S.A.W)❤️Harufu ya Mtume Muhammad (s.a.w) ilikuwa nzuri sana na bora zaidi kuliko harufu ya misk n...
18/09/2025

HARUFU NZURI YA MTUME (S.A.W)❤️

Harufu ya Mtume Muhammad (s.a.w) ilikuwa nzuri sana na bora zaidi kuliko harufu ya misk na bora zaidi kuliko harufu ya udi (amber).

Imepokewa kutoka kwa Anas (R.A) kwamba alisema:

“Mtume wa Mwenyezi Mungu (rehema na amani zimshukie) alikuwa na rangi ya mwili ang’avu, na jasho lake lilikuwa k**a lulu. Alipokuwa akitembea, alitembea kwa utulivu wenye haiba. Sijawahi kugusa hariri wala kitambaa laini zaidi ya kiganja cha Mtume wa Mwenyezi Mungu (saw), na sijawahi kunusa misk wala udi ulio na harufu nzuri zaidi kuliko harufu ya Mtume.”

Nini tunajifunza kutoka katika hadith ya Anas? Tunajifunza kwamba...

1.Utukufu na ubora wa Mtume(s.a.w)
Mwenyezi Mungu alimpa sifa za kipekee, hata mwili wake na harufu yake zikawa bora kuliko chochote, jambo linaloonyesha heshima na daraja lake tukufu.

2.Upendo wa Maswahaba kwa Mtume(saw)
Maswahaba walimpenda Mtume kwa moyo wote, wakamtolea nafsi zao, na walitamani kila kitu chao kiwe fidia kwake. Hii ni alama ya imani ya kweli.

3.Kumfuata Mtume (s.a.w) ni njia ya kheri Kwa kuwa Mtume ndiye mfano bora, kila sifa yake ni kioo cha kheri. Kutafuta kufanana naye kwa maadili, ibada na mwenendo ni njia ya ukaribu na Allah.

Mswalieni Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasallama ❤️

Swahaba Abdulrahman bin Auf (R.A) alikuwa miongoni mwa maswahaba matajiri, na urithi wake ulifikia sawa na takribani dol...
18/09/2025

Swahaba Abdulrahman bin Auf (R.A) alikuwa miongoni mwa maswahaba matajiri, na urithi wake ulifikia sawa na takribani dola milioni 850 za Kimarekani kwa thamani ya sasa. Yeye pia ni mmoja kati ya wale maswahaba kumi waliobashiriwa Pepo.

Siku moja aliwahi kuuza shamba kwa dinari elfu arobaini, kisha pesa hiyo akaigawa kwa jamaa zake wa Bani Zuhra, na kwa wake wa Mtume (Mama wa Waumini), na kwa masikini wa Waislamu.

Siku nyingine aliwapa majeshi ya Kiislamu farasi mia tano, na siku nyingine akatoa ngamia elfu moja na mia tano.

Aidha, alifanya ukombozi wa jumla ya watu elfu thelathini (30,000) kutoka kwenye utumwa.

Alipofariki, aliacha wosia wa dinari elfu hamsini zitolewe katika njia ya Mwenyezi Mungu, na akawaachia kila aliyebakia miongoni mwa waliokuwa kwenye vita vya Badr dinari mia nne kila mmoja.

Ilisemekana kuhusu yeye:

“Watu wote wa Madina walikuwa ni washirika wa mali ya Ibn Auf.”

Tatu ya mali yake alikuwa anawakopesha.

Tatu nyingine alikuwa analipa madeni yao.

Na tatu iliyobaki alikuwa anawasaidia na kuwapa.

Tunajifunza kwamba.

1.Kutoa mali kwa ajili ya Uislamu ni njia ya kupata radhi za Allah – Alitumia utajiri wake kuunga mkono Uislamu, kuwasaidia masikini na kuisaidia jamii kwa ukarimu mkubwa.

2.Utajiri wa kweli ni baraka unapoutumia vizuri – Ingawa alikuwa tajiri sana, hakufanya mali iwe kikwazo cha ibada, bali aliitumia kuondoa mateso ya wengine na kueneza kheri.

3.Kuwasaidia watu ni urithi bora – Ibn Auf (R.A) alijulikana kwa kulipa madeni ya watu, kuwakopesha na kuwasaidia, akawa tegemeo la jamii nzima ya Madina.

Hata Matajiri wa Kiislamu wa zama hizi wanapaswa kuiga maswahaba ni namna gani walitumia Mali zao walizoneemeshwa ktk kuhakikisha wanaupeleka mbele Uislamu.

Allah atutunuku Mali na Atupe nguvu ya pesa ili tuweze kuupeleka Mbele Uislamu, Uislamu unahitaji Uchumi ulio imara ili uweze kusonga Mbele.💸💸💸

Ukimaliza kusoma Mswalie Mtume Muhammad (s.a.w)❤️✅️🔥💫

Sufian Mzimbiri 👉 Mzimbiri TV

Kioo cha jamii, Naomba mni remove kwenye hiyo jamii inayotizama kioo hiki kujifunza😄
18/09/2025

Kioo cha jamii, Naomba mni remove kwenye hiyo jamii inayotizama kioo hiki kujifunza😄

18/09/2025

🌙Leo ni mwezi 25, Rabiiul Awwal (mfunguo sita)-1447H
Allah atumiminie kheri zote zitokanazo na siku ya leo, aamiin🤲

SIMBA WA JANGWANI OMAR MUKHTARJe, unajua kwamba Shekh Omar Al-Mukhtar aliongoza jihad dhidi ya ukoloni wa Kiitaliano kwa...
17/09/2025

SIMBA WA JANGWANI OMAR MUKHTAR

Je, unajua kwamba Shekh Omar Al-Mukhtar aliongoza jihad dhidi ya ukoloni wa Kiitaliano kwa zaidi ya miaka 20 akiwa na umri wa zaidi ya miaka 60?!
Alikuwa amehifadhi Qur’an nzima kichwani na alikuwa akiwafundisha wanafunzi wake katika madrasa.

Na licha ya kwamba majeshi ya Italia yalituma zaidi ya askari 100,000 kupambana naye, hawakuweza kumshinda isipokuwa baada ya kumteka.

🔹Hata katika wakati wa kunyongwa kwake mnamo mwaka 1931, alisema maneno yake yatakayo ishi milele:

Alisema.
‘Sisi hatujisalimishi… tunashinda au tunakufa.’

Allah Amraham Shujaa huyu Mkubwa Na Amuingize ktk pepo yake aamiin yaa Rabb 🤲

YESU KUZUNGUMZA AKIWA KICHANGANabii Issa (Yesu) alayhi salaam ni miongoni mwa watoto wachanga ambao waliweza kuzungumza ...
17/09/2025

YESU KUZUNGUMZA AKIWA KICHANGA
Nabii Issa (Yesu) alayhi salaam ni miongoni mwa watoto wachanga ambao waliweza kuzungumza maneno fasaha kwa uwezo wa Allah (s.wt) wakiwa wangali bado vitoto vichanga kabsa.

Kisa cha Nabii Issa (A.S) Kuzungumza Utotoni

Bibi Mariam bint Imraan baada ya kumzaa Nabii Issa kwa muujiza bila ya baba, alirudi kwa kaumu yake akiwa amembeba mtoto mchanga. Watu waliposhamiri kumshutumu kwa kusema:

“Ewe Mariam! Hakika umefanya jambo la ajabu. Ewe dada wa Harun! Baba yako hakuwa mtu mbaya, wala mama yako hakuwa kahaba.”
(Surat Maryam 19:27–28)

Mariam hakujibizana nao, bali akawaonyesha (akawaashiria) kwa mtoto mchanga kwa ishara (kwamba wanaweza wakamuuliza yeye). Watu wakashangaa wakasema:

“Vipi tutazungumza na mtoto mchanga aliye bado yungali kwenye utoto(kitoto kichanga ambacho kimepakatwa na mama yake kisichoweza kufanya chochote)?”

Hapo ndipo muujiza mkubwa ukatokea. Nabii Issa (A.S), akiwa mtoto mchanga bado kwenye mikono ya mama yake, akazungumza kwa ufasaha akasema:

“Mimi ni mja wa Mwenyezi Mungu. Amenipa Kitabu na amenifanya Nabii. Na amenibariki popote pale nitakapokuwa, na ameniusia kuswali na kutoa zaka maadamu nipo hai. Na (ameniusia) niwe ni mwenye kumtendea wema mama yangu, wala hakunifanya jeuri mwenye taabu. Na amani iko juu yangu siku niliyozaliwa, na siku nitakapokufa, na siku nitakapofufuliwa kuwa hai.”
(Surat Maryam 19:30–33)

Mafunzo Kutokana na Kisa Hiki

1.Muujiza wa Mwenyezi Mungu:
Nabii Issa (A.S) alizaliwa kwa muujiza bila baba, na akazungumza utotoni ili kuthibitisha usafi wa mama yake Mariam (A.S)na kulinda heshima yake.

2.Utume wa Nabii Issa (A.S)
Maneno yake ya mwanzo yalithibitisha kuwa yeye ni mtumwa wa Allah na Nabii, sio mwana wa Mungu.

3.Heshima ya mama
Aliweka wazi wajibu wake wa kumtendea wema mama yake.

4.Ibada na Zaka
Alifundisha umuhimu wa kuswali na kutoa zaka tangu mwanzo wa maisha yake.

5.Uhai, kifo na kufufuliwa.
Aliashiria safari ya mwanadamu: kuzaliwa, kufa, na kufufuliwa Siku ya Mwisho.

Hadithi yake imetajwa wazi ndani ya Surat Maryam:

Maryam alipojifungua, akaambiwa na Mwenyezi Mungu ale na anywe, lakini asiongee na watu.

👉Maneno yake yalibainisha utume wake na ukamilifu wa mama yake, akimtetea kutokana na tuhuma nzito.

Ukimaliza kusoma usiache kumswalia Mtume Muhammad swallallahu alayhi wasallama.❤️❤️❤️

Amani pia ishuke juu ya Nabii Issa (a.s) siku aliyozaliwa na siku atakayokufa na siku atakayofufuliwa kuwa hai.

Endelea kufuatilia Ukurasa wangu kwa ku
👉 Sufian Mzimbiri 👍

KISA CHA NABII M***A (A.S) NA KHIDR Kisa chetu cha leo kutoka katika Qur’ani ni hadithi ya mwanafunzi maarufu wa elimu a...
17/09/2025

KISA CHA NABII M***A (A.S) NA KHIDR

Kisa chetu cha leo kutoka katika Qur’ani ni hadithi ya mwanafunzi maarufu wa elimu ambaye alianza safari ya kutafuta elimu baada ya kuwa nabii. Ni hadithi ya Nabii Musa na Khidr, na hadithi hii imetajwa katika Qur’ani Tukufu na pia katika Hadith za Mtume Muhammad (s.a.w).

Sababu ya kushuka kwa hadithi hii katika Qur’ani kwa Mtume Muhammad (s.a.w):

K**a ilivyopokelewa katika hadithi ya Mtume (s.a.w) kutoka kwa Ibn Abbas, siku moja Nabii Musa alisimama akihutubia watu wake. Baada ya kumaliza hotuba yake, mmoja wa watu wa Bani Israil akamuuliza: "Ewe Musa, je, kuna mtu yeyote duniani aliye na elimu kuliko wewe?" Musa akajibu: "Hapana. Mimi ndiye mwenye elimu zaidi duniani."

Hapo Allah akamlaumu Nabii Musa(a.s) kwa kutorudisha Nabii M***a elimu kwa Allah (yaani hakusema 'Allah ndiye ajuaye zaidi'). Kisha Allah akamwambia Musa: "Ewe Musa, kuna mtu mmoja mahali panapoitwa 'Makutano wa Bahari Mbili' (Majma’ul-Bahrayn), ana elimu zaidi kuliko wewe. Nenda kwake ukajifunze."

Hapo Musa akamuamuru mtumishi wake Yusha’ bin Nun ajiandae kwa safari ya kumtafuta mtu huyo. Allah alimpa Musa alama ya kumwelekeza mahali mtu huyo alipo: Atakapopoteza samaki waliowekwa kwenye chombo chake, baasi hapo ndipo atakapomkuta.mtu huyo.

Allah anasema katika Qur’ani:

“Na Musa akamwambia kijana wake: ‘Sitakoma mpaka nifike mahali zinapokutana bahari mbili, au nitembee muda mrefu.’ Walipofika mahali pa kukutana bahari mbili, walimsahau samaki wao, naye alichukua njia yake baharini kwa njia ya ajabu. Walipokwisha pita, Musa akamwambia kijana wake: ‘Lete chakula chetu; kwa yakini tumepata taabu sana katika safari yetu hii .’” (Surat Al-Kahf 18:60–62)

Baada ya kuanza safari, Musa na mtumishi wake walitembea hadi wakafika kwenye jabali na wakakaa kupumzika. Wakiwa wamelala, samaki akaruka kutoka kwenye chombo na kuingia baharini kwa namna ya ajabu – maji yalikuwa yakipasuliwa naye samaki, kisha yanagandia nyuma yake.

Walipoamka, waliendelea na safari. Baada ya siku moja na nusu, Musa akamwambia kijana wake: "Tule chakula chetu." Hapo mtumishi akakumbuka tukio la samaki na akamwambia Musa:

“Je, unakumbuka tulipoketi kwenye lile jabali? Nilimsahau yule samaki. Na aliyenisahaulisha ni Shetani, nisimsimulia. Naye alichukua njia yake baharini kwa ajabu.” (18:63)

Musa akasema: "Hicho ndicho tulichokuwa tukikitafuta!" Basi walirudi kwa kufuata alama zao hadi wakamkuta mja miongoni mwa waja wa Allah ambaye Allah alimpa rehema kutoka kwake na alimfundisha elimu kutoka kwake.

Kitu cha muhimu hapa ni hiki: Ingawa Musa ni Nabii, Allah alimwamuru atafute elimu kwa mtu ambaye daraja lake ni la chini kuliko yeye, yaani Khidr. Hii inatufundisha umuhimu wa kutafuta elimu.

Mtume Muhammad (s.a.w) alikuwa kila mara akihimiza umma wake kutafuta elimu. Alisema:

"Fikisheni kutoka kwangu hata aya moja."

Na alisema kuhusu fadhila za elimu:
“Yeyote anayelingania kwenye uongofu atapata thawabu sawa na yule anayefuata hadi Siku ya Kiyama.”

Pia Mtume alisema:
"Pindi akifa mwanadamu , Amali zake zote hukatika isipokuwa mambo matatu: Sadaka yenye kuendelea, au elimu yenye kupatikanwa manufaa au mtoto mwema mwenye kumuombea Dua Mzazi wake"

Na alisema tena:
"Mwenye kupita njia hali ya kuwa anataka ktk njia hiyo ilmu, Allah humrahisishia njia ya kwenda Peponi. Hakika Allah, malaika Wake, viumbe wa mbinguni na ardhini – hadi mchwa kwenye shimo lake, na hata samaki majini – humuombea rehema yule anayefundisha watu mema."

Wanazuoni na watu wema walipojua maneno haya ya Mtume (s.a.w), walijitolea maisha yao yote kwa ajili ya elimu. Safari ya kumjua Allah inahitaji elimu ya nguvu, juhudi za kiutendaji, bidii kubwa, na umakini.

Nabii Daud alisema:
"Elimu moyoni ni k**a taa ndani ya nyumba."

Na Luqman al-Hakim alimwambia mwanawe:
"Ewe mwanangu, kaa na wanazuoni na waandame kwa magoti yako, kwani Allah huhuisha mioyo kwa nuru ya hekima na elimu k**a anavyohuisha ardhi kwa mvua kutoka mbinguni."

Hivyo, somo na faida kutoka katika hadithi ya Musa na Khidr ni kwamba hata mtu mwenye daraja ya juu k**a Musa, alisafiri mamia ya kilomita kutafuta elimu kwa mtu wa daraja la chini kuliko yeye.

Sufyan ath-Thawri alisema:
"Mtu hawezi kuwa na heshima ya kweli mpaka ajifunze kutoka kwa walio juu yake, walio chini yake, na walio sawa naye."

Ushauri wangu kwenu ni: tutafuteni elimu!

Allah awalipe kheri. Na avijaze vizazi vyenu ilmu yenye manufaa duniani na akhera, aamiin🤲

K**a umemaliza kusoma, mswalie Mtume Muhammad (s.a.w)❤️❤️❤️

Like, Share and
Sufian Mzimbiri & Mzimbiri TV

MAMA WA NABII ISMAIL (A.SALAAM)Kisa Cha Mama yake Nabii Ismail ambaye ni Haajar(a.s) na ni moja ya hadithi zenye kugusa ...
17/09/2025

MAMA WA NABII ISMAIL (A.SALAAM)
Kisa Cha Mama yake Nabii Ismail ambaye ni Haajar(a.s) na ni moja ya hadithi zenye kugusa sana katika historia ya Uislamu.

Haajar alikuwa mke wa Nabii Ibrahim ‘alayhis-salaam, na mama wa Nabii Ismail ‘alayhis-salaam.

Haajar alitoka Misri, na awali alikuwa mjakazi wa Sarah, mke wa Nabii Ibrahim.

Baada ya Sarah kushindwa kupata mtoto kwa miaka mingi ya ndoa, alijitolea kwa mumewe Ibrahim akamuomba amuoe Haajar ili apate mtoto.

Nabii Ibrahim akakubali na akamuoa Haajar, naye akamzalia mtoto Ismail.

Haajar alikuwa mwanamke mwenye moyo mzuri, na mama mwenye subira. Aliamini ujumbe wa mumewe Ibrahim, na alimsaidia katika hali mbalimbali.

Muda ulipokwenda, Allah alimwamuru Ibrahim amuache Haajar pamoja na mtoto wake Ismail katika bonde la Maka — sehemu isiyo na watu, maji wala mimea, na yenye joto kali.

Ibrahim akawachukua Haajar na mtoto wake, na akamwambia awe na subira na amtegemee Allah.

Baada ya kuwaacha hapo, Haajar akagundua kuwa huu ni mtihani kutoka kwa Allah.

Ibrahim ‘alayhis-salaam alikuwa analia alipokuwa akiwaacha katika jangwa hilo.

Haajar akamuuliza:
“Ewe Nabii wa Allah, unatuacha hapa bila maji wala chakula?”
Akasema: “Ndiyo, Allah ndiye aliyeniamuru.”

Haajar akajibu kwa imani kubwa:
“Basi Allah hatatuangamiza.”

Baada ya Ibrahim kuondoka, akiba ya maji ilipoisha, Haajar hakuwa na la kufanya. Akawa anakimbia baina ya milima miwili — Safa na Marwa — mara saba, akitafuta maji kwa ajili ya mtoto wake aliyekuwa na kiu kali.

Katika moja ya mbio hizo, Haajar alipokuwa karibu kurudi kwa mtoto wake, akashuhudia jambo la ajabu — maji yakaanza kutoka chini ya mguu wa Ismail. Hayo ndiyo maji ya Zamzam, na yakawa chanzo cha uhai mahali pale.

Maji ya Zamzam yalikuwa ni muujiza kutoka kwa Allah, na ndiyo yaliyomuwezesha Haajar na mtoto wake kuishi hapo.

Baada ya muda, watu wa kabila la Quraish na makabila mengine ya Kiarabu wakaanza kuhamia Maka, wakivutiwa na uwepo wa maji, na eneo hilo likaanza kustawi na kuwa kituo cha biashara.

Haajar na mtoto wake wakaishi Maka. Ibrahim alikuwa anawatembelea mara kwa mara.

Ismail alipokuwa kijana, Allah alimpa Ibrahim amri ya kumchinja mwanawe, k**a jaribio la utiifu.

Ismail alipomweleza mama yake amri hiyo ya Allah, Haajar alikubali kwa subira na kusalim amri kwa Mwenyezi Mungu.

Ismail Akamwambia baba yake: “Fanya k**a ulivyoamrishwa, utanikuta – InshaAllah – miongoni mwa wanaosubiri.”

Baada ya kufaulu mtihani huo, Allah akamkomboa Ismail kwa kondoo mkubwa.

Baada ya hayo, Allah akamuamuru Ibrahim ajenge Al-Kaaba huko Maka kwa msaada wa mwanawe Ismail.✅️📚

Haajar alikuwa sehemu ya tukio hili tukufu, na akawa na nafasi kubwa katika historia ya Uislamu k**a mama shujaa mwenye subira.

Allah awajaalie wanawake wote Subra k**a walivyokuwa na subra wanawake watukufu wa mitume amani ishuke juu yao🤲🤲🤲

♥️Ukiishamaliza kusoma, mswalie Mtume Muhammad (Swalla Allahu ‘alayhi wasallam)
KISHA SHARE NA

Follow Mzimbiri TV na Sufian Mzimbiri

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sufian Mzimbiri posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sufian Mzimbiri:

Share