Sports Halisi

Sports Halisi We provides a wide range of Sports News , in Kiswahili and English, and highlights sports events, Sports Match...

SIMBA NA YANGA KWANINI HAZICHEZI MCHANA KWENYE JUA KALI?Kocha Mkuu wa Namungo FC, Juma Ramadhani Mgunda amesema timu yak...
13/05/2026

SIMBA NA YANGA KWANINI HAZICHEZI MCHANA KWENYE JUA KALI?

Kocha Mkuu wa Namungo FC, Juma Ramadhani Mgunda amesema timu yake imelazimika kucheza katika mazingira magumu kutokana na jua kali wakati wa mchezo uliochezwa majira ya saa nane mchana.Mgunda amewataka wenye mamlaka ya soka kufanya maamuzi ya kuahirisha michezo pale ambapo hali ya hewa ni ya joto kali, sawa na ambavyo mechi huahirishwa kunapokuwa na mvua kubwa.

Kocha huyo pia ameibua mjadala kwa kuhoji kwanini baadhi ya vilabu vikubwa k**a Simba SC na Young Africans SC mara nyingi havipewi ratiba ya kucheza saa nane mchana kwenye jua kali k**a ilivyo kwa baadhi ya timu nyingine za ligi.Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka kuhusu usawa wa ratiba pamoja na afya za wachezaji ndani ya NBC Premier League.

YANGA SC YAFUNGIWA NA FIFA⚠️FIFA Yafungia Vilabu 7 vya Tanzania Kufanya Usajili wa Wachezaji 🔒Shirikisho la Mpira wa Mig...
12/05/2026

YANGA SC YAFUNGIWA NA FIFA

⚠️FIFA Yafungia Vilabu 7 vya Tanzania Kufanya Usajili wa Wachezaji 🔒

Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) limeweka vikwazo vya usajili (Registration Bans) kwa vilabu saba vya Tanzania kutokana na ukiukwaji wa kanuni za usajili na mikataba. Hatua hii inazuia vilabu hivi kushiriki kwenye soko la usajili wa ndani na kimataifa hadi vitakapokamilisha masharti yaliyowekwa, yanayohusiana zaidi na malipo ya madeni kwa wachezaji au makocha wa zamani.

🔹 Vilabu Vilivyokumbwa na Adhabu na Muda Wake:
1️⃣ Young Africans (Yanga SC)
Kizuizi kimeanza: Mei 7, 2026
Muda: Hadi kukamilisha taratibu zote za adhabu

2️⃣ Dodoma Jiji FC
Kizuizi kimeanza: Aprili 29, 2026
Muda: Vipindi vitatu vya usajili

3️⃣ Pamba Jiji FC
Kizuizi kimeanza: Mei 7, 2026
Muda: Vipindi vitatu vya usajili

4️⃣ Kengold SC
Kizuizi kimeanza: Oktoba 1, 2025
Muda: Vipindi vitatu vya usajili

5️⃣ Fountain Gate FC
Kizuizi cha kwanza: Januari 1, 2026 (Vipindi 2)
Kizuizi cha pili: Aprili 22, 2026 (hadi kukamilisha taratibu zote za adhabu)

6️⃣ TRA United
Vikwazo: Mei 4, 2026 na Mei 7, 2026
Muda: Vipindi vitatu vya usajili

7️⃣ BigMan Football
Kizuizi kimeanza: Mach 17, 2026
Muda: Vipindi vitatu vya usajili

Mashabiki wa Yanga vipi mtachanha Tena kulipa Deni 😂✍️

YANGA BADO UTOTO NI MWINGI SANA"Siwezi kuchanga Utoto wanatufanyia wanafanya makosa makusudi ili tulipe sisi faini, Yang...
12/05/2026

YANGA BADO UTOTO NI MWINGI SANA

"Siwezi kuchanga Utoto wanatufanyia wanafanya makosa makusudi ili tulipe sisi faini, Yanga ni Timu yangu pendwa walikuwa wanafahanu wanachokifanya na madhara yake ni haya wao ndio walipe faini kwa mwana yanga yeyote anayejua sheria na anajua mpira hawezi kutoa pesa yake kwenye Makosa ya kitoto k**a.yale

Bodi ya Ligi kwenye adhabu wamejitahidi lakini bado nawalaumu Adhabu waliyoitoa haifanani na kosa tulilofanya ilitakiwa tutozwe faini Shilingi Milioni 30, Mashabiki wafungiwe kuingia uwanjani na tukatwe Alama 3 Kwa maana kwamba tumekiuka Sheria za Mpira! tumeenda kubadilishia nguo kwenye nyumba Nje kabisa ya uwanja,

kule tulipoenda (Jumba la Maajabu) huwezi kujua tulitumia madawa au kuchoma sindano ili kupata Nguvu ilitakiwa tuonywe Kwa Kukatwa alama 3 ili isije kujirudi" Shabiki wa Yanga akihojiwa kupitia 69link

12/05/2026

YANGA BADO UTOTO NI MWINGI SANA
Anasema Shabiki wa timu hiyo

Eti Hii huwa inasaidia nini? Huyo ni Mchezaji wa timu ya Gormahia queens 👑.
12/05/2026

Eti Hii huwa inasaidia nini?
Huyo ni Mchezaji wa timu ya Gormahia queens 👑.

Mdau DM: “Milioni 10 Bora Zingetumika kwa Watoto Yatima!”Mfanyabiashara na mwanachama wa Club ya YANGA SC, Jennifer Jovi...
11/05/2026

Mdau DM: “Milioni 10 Bora Zingetumika kwa Watoto Yatima!”

Mfanyabiashara na mwanachama wa Club ya YANGA SC, Jennifer Jovin, maarufu k**a NIFFER, ameichangia Shilingi Milioni 1 kwa ajili ya kulipa faini ya Shilingi Milioni 30 iliyotolewa na Bodi ya Ligi, kutokana na kosa la kutotumia vyumba rasmi vya kubadilishia nguo siku ya Kariakoo Derby dhidi ya Mej Isamuyo.

Hata hivyo, baadhi ya wadau wamesema kwamba bora hiyo milioni moja Niffer angeitumia kuwasaidia watoto yatima, kuwa pesa hizo zingekuwa na manufaa makubwa zaidi kwa jamii.

Je, unakubaliana na maoni ya mdau huyu?

Chama wa Simba SC ni tofauti kabisa na chama aliyecheza Young Africans Sports Club shida nini ?
11/05/2026

Chama wa Simba SC ni tofauti kabisa na chama aliyecheza Young Africans Sports Club shida nini ?

TFF INGEKUJA NA RUNGU ZITO KUKATA ALAMA TATU HESHIMA INGEKUWEPOAmeandika Mudumoh ✍️Baada ya Yanga kukutana na Rungu zito...
11/05/2026

TFF INGEKUJA NA RUNGU ZITO KUKATA ALAMA TATU HESHIMA INGEKUWEPO

Ameandika Mudumoh ✍️

Baada ya Yanga kukutana na Rungu zito kutokana matukio ya Kwenye Derby dhidi ya Simba SC

1️⃣ Kutozwa Milioni 30 kushindwa kuingia vyumba Rasmi vya kubadilishia nguo💸
2️⃣ Meneja wao kufungiwa mechi 3 ⚠️
3️⃣ Shabiki wao kufungiwa miezi 12 kuingia uwanjani 🚫

Kumejitokeza Kampeni kwenye Magroup ya Mashabiki wa Yanga SC kuanza kuchangisha Hela hiyo ili kulipa Deni... Jamani hii si k**a Dharau kwa Mamlaka za soka inawezekanaje TFF inaipa Adhabu klabu halafu Kampeni inaanzishwa Mitandaoni Kwaajili ya Kuchangisha kulipa deni Tena na Mashabiki!.

Ndio maana Makosa yanafanywa Wazi Wazi Kwa sababu wanajua hata wakitozwa Milioni 100 Mashabiki watachanga

Ombi TFF Ingekuja na Kanuni Kukata Point Tatu ili iwe fundisho
Kwa wengine Hii ingefanya mashabiki wajue kuwa kuna adhabu thabiti, na timu kujifunza kutorudia Makosa ya kipuuz k**a hayo.

10/05/2026

Mchome Hajaafiki Simba SC Kupewa Tuzo ya klabu Bora

10/05/2026

Kwahiyo Tujiandae kumuona Clatous Chama kwenye Timu ya Taifa ya Tanzania 'Taifastars' si atakuwa ameshakana Uraia wa Zambia au inakuwaje?🤔

CHAMA KUPEWA URAIA WA TANZANIA Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema serikali imeanza kuon...
10/05/2026

CHAMA KUPEWA URAIA WA TANZANIA

Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Paul Makonda amesema serikali imeanza kuona taratibu za kumpatia uraia kiungo mshambuliaji wa Simba SC, Clatous Chama baada ya kuonyesha kiwango kikubwa katika soka la Tanzania.

Akizungumza katika usiku wa Tuzo za BMT 2025, Makonda alisema kiwango alichoonyesha Chama, ikiwemo bao lake la hivi karibuni, kimeongeza hoja ya kumtaka achezee Taifa Stars.

“Kwa lile goli la juzi, wizara imeanza mchakato wa kuona taratibu za kumpatia uraia Chama ili kuongeza uwezo wa timu yetu ya taifa,” alisema Makonda.

Alisema Chama ameonyesha uwezo mkubwa wa kubadilika kulingana na mahitaji ya timu na kufanikiwa kucheza kwa ushindani katika vilabu vikubwa vya Tanzania.

Una Maoni Gani 🤔

Address

Mbezi
Temeke

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports Halisi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports Halisi:

Share