Sports Halisi

Sports Halisi We provides a wide range of Sports News , in Kiswahili and English, and highlights sports events, Sports Match...

MATANGAZO YA MUBASHARA YAGEUKA KUWA MOJA TUKIO LA KUCHEKESHA KATIKA UPDATE ZA KOMBE LA DUNIA.Mwandishi mmoja wa habari k...
12/06/2026

MATANGAZO YA MUBASHARA YAGEUKA KUWA MOJA TUKIO LA KUCHEKESHA KATIKA UPDATE ZA KOMBE LA DUNIA.

Mwandishi mmoja wa habari kutoka Korea Kusini πŸ‡°πŸ‡· alikuwa mubashara kwenye televisheni ya MBC, akiwa makini kabisa na majukumu yake... lakini ghafla shabiki mmoja wa Mexico alitokea pembeni yake na kubadilisha kila kitu.

Shabiki huyo alimshika mkono kwa furaha kubwa, huku mwandishi akionekana kutokuwa na raha lakini akijitahidi kubaki kawaida mbele ya kamera.

Akiwa anaendelea na matangazo hayo ya Mubashara huku akionekana kwamba angeweza kumaliza matangazo yake bila tatizo licha ya uwepo wa shabiki huyo pembeni yake.

Ghafla yule shabiki alimgeukia na kumbusu shavuni akiwa bado anaendelea na matangazo hayo ya mubashara hewani!πŸ‘€

Ndiyo... ni wazi kabisa kwamba hakutarajia jambo hilo kutokea hivyo ilimbidi atabasamu..

Timu ya taifa ya DR Congo yawasili Marekani, tayari kwa Kombe la Dunia πŸ‡¨πŸ‡©βš½Baada ya kukamilisha karantini ya siku kadhaa,...
12/06/2026

Timu ya taifa ya DR Congo yawasili Marekani, tayari kwa Kombe la Dunia πŸ‡¨πŸ‡©βš½

Baada ya kukamilisha karantini ya siku kadhaa, timu ya taifa ya DR Congo imewasili rasmi Marekani. Maandalizi yao yalikuwa na changamoto kutokana na hofu ya ugonjwa wa Ebola, jambo lilililazimisha kambi yao ya maandalizi kuhamia Ubelgiji, huku baadhi ya mechi za kirafiki zikichezwa Hispania.

Sasa, wakiwa tayari na moyo wa kushirikisha Afrika kwenye michuano ya dunia, mashabiki wanatarajia kuona juhudi zao uwanjani. 🌍πŸ’ͺ

🚨 Ronwen Williams Aeleza Masikitiko Yake Kuhusu Msaada wa WaafrikaKipa wa Afrika Kusini, Ronwen Williams, amesema alihuz...
12/06/2026

🚨 Ronwen Williams Aeleza Masikitiko Yake Kuhusu Msaada wa Waafrika

Kipa wa Afrika Kusini, Ronwen Williams, amesema alihuzunishwa na kuona baadhi ya mashabiki kutoka mataifa mbalimbali ya Afrika wakiiunga mkono Mexico badala ya kuisapoti Afrika Kusini.
Williams alisema alitarajia kuona mshik**ano mkubwa kutoka kwa bara la Afrika katika mashindano hayo, lakini hali ilikuwa tofauti na matarajio yake.

πŸ—£οΈ "Nilidhani Waafrika wengi wangekuwa upande wetu, lakini niliona wengi wakishangilia Mexico. Hilo liliniumiza kwa kiasi fulani,Kushindwa kwetu leo hakukutokana tu na kutotoa kiwango chetu bora. Ninaamini pia ukosefu wa sapoti kutoka kwa Waafrika wenzetu ulichangia kwa kiasi fulani. Afrika ni bara ambalo nimekuwa nikilifahamu kwa kusimama pamoja na timu zake wakati wa Kombe la Dunia au mashindano ya kimataifa, lakini safari hii ilionekana tofauti.
Badala ya umoja, ilionekana kana kwamba kushindwa kwetu kulileta furaha kwa wengine, hata ndani ya Afrika yenyewe. Hilo lilitukatisha tamaa, kwa sababu tulitarajia bara letu lingeungana nasi na kutuunga mkono katika nyakati k**a hizi." πŸ‡ΏπŸ‡¦πŸ’”πŸŒ Alisema

Hata hivyo, kwenye mchezo wa jana ilionekana mashabiki wengi kutoka Afrika walikuwa wamevaa jezi za Mexico, jambo lililoibua mjadala mkubwa mitandaoni kuhusu mshik**ano wa Waafrika kwenye mashindano makubwa ya kimataifa.

Je, unaona Waafrika wanapaswa kuunga mkono timu za Afrika bila kujali ni nchi gani, au kila mmoja ana uhuru wa kuisapoti timu anayoipenda? πŸ‘‡πŸΎπŸ€”

Kwa sasa tunaanza kuhisi maumivu kwa ndugu zetu wa Afrika Kusini πŸ‡ΏπŸ‡¦.Wachezaji wawili wa Afrika Kusini wamepewa kadi nyek...
11/06/2026

Kwa sasa tunaanza kuhisi maumivu kwa ndugu zetu wa Afrika Kusini πŸ‡ΏπŸ‡¦.
Wachezaji wawili wa Afrika Kusini wamepewa kadi nyekundu.
Themba Zwane na Sithole πŸŸ₯πŸŸ₯

Wanapoteza kwa Magoli 2-0

Tangu mwaka 2006, hakuna timu ya mpira wa miguu iliyowahi kupata kadi nyekundu mbili katika mchezo wake wa ufunguzi wa Kombe la Dunia.
Ndugu zetu wa Afrika Kusini, mnaona sasa? Huenda huu ni wakati wa kutafakari na kuungana zaidi.

🚨BREAKING: Omar Artan ameteuliwa kuchezesha fainali ya UEFA Super Cup baada ya kukosa nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia...
11/06/2026

🚨BREAKING: Omar Artan ameteuliwa kuchezesha fainali ya UEFA Super Cup baada ya kukosa nafasi ya kushiriki Kombe la Dunia! πŸ€©πŸ‡ΈπŸ‡΄

Safari ya Artan imechukua mwelekeo usiotarajiwa siku chache tu Baada ya kunyimwa ruhusa ya kuingia nchini Marekani kwa ajili ya Kombe la Dunia, wengi walidhani hiyo ingekuwa pigo kubwa kwake. Hata hivyo, sasa amepewa jukumu la kuchezesha mechi ya UEFA Super Cup mwezi Agosti.

Mashabiki wa Somalia wamempokea k**a shujaa, na sasa atapata fursa kubwa ya kuonyesha uwezo wake kwenye jukwaa la kimataifa katika pambano kati ya Paris Saint-Germain na Aston Villa kuwania taji hilo.πŸ†

Funzo la Maadili: Marekani wana shida zao Binafsi

Umemtambua nani.✍️
11/06/2026

Umemtambua nani.✍️

Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo anashiriki kombe la dunia kwa Mara ya mwisho huku akiweka historia ya kushiriki makala ...
11/06/2026

Nyota wa Ureno Cristiano Ronaldo anashiriki kombe la dunia kwa Mara ya mwisho huku akiweka historia ya kushiriki makala 6 ya dimba la kombe la dunia rekodi ambayo anashikilia na Lionel Messi
Je Portugal πŸ‡΅πŸ‡Ή ataweza shinda taji hili mwaka huu

Mchambuzi nguli wa Michezo  Edo Kumwembe amehoji kwanini baadhi ya Watanzania wanashangilia baada ya Hassan Mwakinyo kup...
11/06/2026

Mchambuzi nguli wa Michezo Edo Kumwembe amehoji kwanini baadhi ya Watanzania wanashangilia baada ya Hassan Mwakinyo kupoteza pambano lake dhidi ya Michael Soro wa Ivory Coast.

"Hiki kitu kimeniuma, lakini sina cha kufanya. Watanzania wengi wanashangilia mjomba wangu, Hassan Mwakinyo Jr, kupoteza pambano lake. Nimemuita mjomba kwa sababu mama yangu anatokea Tanga."

"Tatizo ni mjomba Hassan au Watanzania? Tufungue mjadala. Ingekuwa ni pambano la ndani, isingekuwa shida. Lakini sisi na yule jamaa Soro, ilipaswa kuwa ni pambano la SISI dhidi ya YEYE."

"Hili limekuwa tofauti. Imekuwa k**a vile SISI na Soro dhidi ya Mjomba Hassan. Labda kuna mahali Anko amekosea wakati akijenga maisha yake katika mchezo huu."

"Vyovyote ilivyo, yeye ndiye bondia bora zaidi Tanzania kwa sasa. Hata hivyo, kuwa na mahusiano mazuri na jamii yako ni jambo muhimu katika maisha ya kila siku."

"Nani anamchukia Mbwana Samatta kiasi cha kufurahia akikosa goli? Sidhani. All the best, Anko Hassan. We will rise again..." - Ameandika Edo Kumwembe.

Chonde Chonde Watanzania Tusimkatishe tamaa Mwakinyo kisa amepoteza Pambano lake katika Ubondia kuna mawili kushinda na ...
11/06/2026

Chonde Chonde Watanzania Tusimkatishe tamaa Mwakinyo kisa amepoteza Pambano lake katika Ubondia kuna mawili kushinda na kushindwa, leo kashindwa basi kesho itakuwa siku yake, isiwe sababu ya kumsimanga please πŸ™πŸ‘

SIMBA NA YANGA KWANINI HAZICHEZI MCHANA KWENYE JUA KALI?Kocha Mkuu wa Namungo FC, Juma Ramadhani Mgunda amesema timu yak...
13/05/2026

SIMBA NA YANGA KWANINI HAZICHEZI MCHANA KWENYE JUA KALI?

Kocha Mkuu wa Namungo FC, Juma Ramadhani Mgunda amesema timu yake imelazimika kucheza katika mazingira magumu kutokana na jua kali wakati wa mchezo uliochezwa majira ya saa nane mchana.Mgunda amewataka wenye mamlaka ya soka kufanya maamuzi ya kuahirisha michezo pale ambapo hali ya hewa ni ya joto kali, sawa na ambavyo mechi huahirishwa kunapokuwa na mvua kubwa.

Kocha huyo pia ameibua mjadala kwa kuhoji kwanini baadhi ya vilabu vikubwa k**a Simba SC na Young Africans SC mara nyingi havipewi ratiba ya kucheza saa nane mchana kwenye jua kali k**a ilivyo kwa baadhi ya timu nyingine za ligi.Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka kuhusu usawa wa ratiba pamoja na afya za wachezaji ndani ya NBC Premier League.

Address

Mbezi
Temeke

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sports Halisi posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sports Halisi:

Share