13/05/2026
SIMBA NA YANGA KWANINI HAZICHEZI MCHANA KWENYE JUA KALI?
Kocha Mkuu wa Namungo FC, Juma Ramadhani Mgunda amesema timu yake imelazimika kucheza katika mazingira magumu kutokana na jua kali wakati wa mchezo uliochezwa majira ya saa nane mchana.Mgunda amewataka wenye mamlaka ya soka kufanya maamuzi ya kuahirisha michezo pale ambapo hali ya hewa ni ya joto kali, sawa na ambavyo mechi huahirishwa kunapokuwa na mvua kubwa.
Kocha huyo pia ameibua mjadala kwa kuhoji kwanini baadhi ya vilabu vikubwa k**a Simba SC na Young Africans SC mara nyingi havipewi ratiba ya kucheza saa nane mchana kwenye jua kali k**a ilivyo kwa baadhi ya timu nyingine za ligi.Kauli hiyo imezua mjadala mkubwa miongoni mwa mashabiki na wadau wa soka kuhusu usawa wa ratiba pamoja na afya za wachezaji ndani ya NBC Premier League.