Marhaba online

Marhaba online Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Marhaba online, TV Network, kiembesamaki, Unguja.

19/04/2025

Athari za mabadiliko ya tabia ya nchi

MAMLAKA YA UDHIBITI WA HUDUMA ZA MAJI NA NISHATI ZANZIBAR ZURA  IMETANGAZA BEI MPYA YA UMEME KWA WATEJA WA HUDUMA HIYO I...
19/01/2025

MAMLAKA YA UDHIBITI WA HUDUMA ZA MAJI NA NISHATI ZANZIBAR ZURA IMETANGAZA BEI MPYA YA UMEME KWA WATEJA WA HUDUMA HIYO INAYOTARAJIWA KUTUMIKA RASMI JANUARY 20 MWAKA HUU.

AKITOA TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI MENEJA UHUSIANO MAMLAKA YA UDHIBITI WA HUDUMA ZA MAJI NA NISHATI ZANZIBAR ZURA MBARAKA HASSAN HUKO KATIKA OFISI ZA MAMKALA HIYI MAISARA AMESEMA ZURA IMEPOKEA MAOMBI YA KUBADILISHA BEI YA UMEME KULIKOTOKANA NA MAHITAJI YA MABIRESHO YA LAZIMA YA MIUNDOMBINU YA UMEME ILI KUKIDHI MAHITAJI YA MABORESHO HAYO

AKITAJA MABADILIKO HAYO MBARAKA AMEFAHAMISHA KUWA TOZO NA KUTOA HUDUMA ( SAVES CHAGE) KWA MWEZI NI SHILINGI 2.100 K**A ILIVYOKUWA HAPO AWALI

AIDHA AMEFAHAMISHA KUWA BEI HIZO ZIMETOA PUNGUZO LA TZS SHILINGI 190 KWA WATUMIAJI WADOGO WADOGO AMBAO WALIKUWA WAKILIPA TZS 480 KWA UNIT KILA WANAPOVUKA MATUMIZI YA UNITI 50 KWA MWEZI AMBAPO KWA SASA WATALIPA TZS 290 KWA UNIT

HATA HIVYO MBARAKA AMEBAINISHA KUWA MABADILIKO HAYO HAYATAHUSISHA TOZO ZA KUTOA HUDUMA ( SERVES CHARGE) NA BEI YA MAHITAJI YA JUU ( DEMAND CHARGE) ZITABAKI K**A ZILIVYO.

MKUU WA MKOA WA KUSINI UNGUJA MH AYOUB MOHAMMED MAHAMOUD ANEWATAKA WANANCHI WA U*I N'GAMBWA NA WALIOFIKIWA NA MRADI WA Z...
13/12/2024

MKUU WA MKOA WA KUSINI UNGUJA MH AYOUB MOHAMMED MAHAMOUD ANEWATAKA WANANCHI WA U*I N'GAMBWA NA WALIOFIKIWA NA MRADI WA ZAN UDAPTY KUVIFANYIA KAZI VIFAA WALIVYOPATIWA ILI KUFIKIA LENGO LA MRADI HUO LA KUWAINUA WANAWAKE KIUCHUMI KUPITIA KILIMO MSETO KILIMO BIASHARA

MH AYOUB AMETOA WITO HUO WAKATI AKIZUNGUMZA NA WANANCHI KATIKA ZOEZI LA UGAWAJI WA VIFAA VYA MIUNDOMBINU YA MAJI KWA WANANCHI WALIOFIKIWA NA MRADI HUO WA ZAN UDAPTY UNAOTEKELEZWA NA TASISI YA COMMUNITY FOREST PEMBA KWA KUSHIRIKIANA NA TASISI YA COMMUITIY FOREST INTANETINAL, ULIOHUSISHA SHEHIYA NNE ZA WILAYA YA KATI MKOA WA KUSINI UNGUJA HAFLA ILIYOFANYIKA HUKO KATIKA KISIWA CHA U*I N'GAMBWA MKOA WA KUSINI UNGUJA

AMESEMA NI JUKUMU LA WANANCHI WA KISIWA HICHO NA MAENEO MENGINE KUHAKIKISHA WANATUNZA ARDHI NA MAZINGIRA YAO YALIYOWAZUNGUKA ILI KUKABILIANA NA ATHARI ZITOKANAZO NA MABADILIKO YA TABIA YA NCHI YANAYOENDELEA KUATHIRI MATAIFA MENGI ULIMWENGUNI KWA LENGO LA KUENDELEZA MAENDELEO ENDELEVU

AIDHA MH AYOUB AMEFAHAMISHA KUWA KAZI YA UHIFADHI WA MISITU NI KAZI KUBWA INAYOHITAJI UTAYARI WA KIPEKEE KWANI WATU WA MAENEO MENGI YA HIFADHI HAWANA KIPATO CHOCHOTE WANACHOKIPATA ,HIVYO AMETUMIA FURSA HIYO KUWAPONGEZA WANANCHI WA MKOA WA KUSINI UNGUJA KWA JITIHADA KUBWA WANAYOIFANYA KATIKA KUTUNZA MAZINGIRA YAO.

AKIWA KATIKA MAKABIDHIANO HAYO KATIBU MKUU WIZARA YA KILIMO MALI ASILI UMWAGILIAJI NA MIFUGO ND.ALI KHAMIS JUMA AMEELEZA KUWA SERIKALI KWA KUSHIRIKIANA NA TASISI ZA CFP KUTAFUTA MASOKO YA MAZAO ZITAZOZALISHWA NA WANANCHI ILI KWENDA SAMBAMBA NA SERA YA SERIKALI YA MAPINDU*I YA ZANZIABAR YA KILIMO BIASHARA

AWALI MKURIGENZI MUENDESHAJI WA TASISI YA COMMUNITY FOREST PEMBA ND.MBAROUK M***A OMAR AMEMUELEZA MH AYOUB KWAMBA MRADI HUO WENYE THAMINI YA SHILINGI ZA KITANZANIA BILIONI 9.9 KATIKA UTEKELEZAJI WAKE UMEJIKITA KATIKA MAENEO MAKUU MATATU IKIWEMO USAWA WA KIJINSIA AMBAO UNA LENGO LA KUONGEZA USHAWISHI NA NGUVU ZA UONGOZI KWA WANAWAKE KATIKA BIASHARA NA KUKABILIANA NA MABADILIKO YA HALI YA HEWA KATIKA JAMII ZA PWANI ZA ZANZIBAR NA TANZANIA.

VIFAA VYA UKARABATI WA MIUNDOMBINU YA MAJI VILIVYOKABIDHIWA NI PAMOJA NA MASHINE YA KUSUKUMIA MAJI, MIPIRA, VIUNGUO, TANKI PAMOJA NA SOLA AMBAPO MRADI HUO UMEWAFIKIA WANANCHI WA SHEHIA NNE ZA WILAYA YA KATI NAZO NI SHEHIA YA BUNGI, U.UKUU, U*I NA U*I NGAMBWA .
Taarifa na Leila Khamis

RAIS MWINYI: WEKENI VIWANGO VIDOGO VYA MALIPO KWA WAFANYABIASHARA WA MASOKO MAPYA.Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Bara...
27/10/2024

RAIS MWINYI: WEKENI VIWANGO VIDOGO VYA MALIPO KWA WAFANYABIASHARA WA MASOKO MAPYA.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi ameaziagiza taasisi zinazosimamia masoko mapya kuweka Viwango vidogo vya malipo kwa Wafanyabiashara na Wajasiriamali ili wamudu kulipa na kuendelea na biashara katika mazingira mazuri.

Rais Dk,Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 27 Oktoba 2024 alipofungua soko jipya la kisasa la Jumbi, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Aidha Rais Dk, Mwinyi amewahakikishia Wafanyabiashara kuwa Serikali itaendelea kuwaandalia mazingira Bora zaidi sokoni hapo yatakayoendana na soko hilo.

Rais Dk, Mwinyi amesisitiza kuwa Serikali imetenga kiasi cha shillingi Bilioni Mia moja kwa ajili ya kuwapatia mitaji Wajasiriamali na Wafanyabiashara kuimarisha Biashara zao .

Ametoa rai kwa Wajasiriamali ambao bado hawajapata mitaji kujipanga vema katika Vikundi ili Serikali iwapatie mitaji hiyo.

Halikadhalika Rais Dk, Mwinyi ameruhusu wafanyabishara kufanya shughuli zao muda wote na kuagiza soko kuwa wazi Usiku na mchana.

Vilevile Rais Dk,Mwinyi amewaahidi wananchi kuwa ataendelea kujipambanua kwa Vitendo kutimiza ahadi alizoziahidi wakati wa Kampeni mwaka 2020.

26/10/2024
13/08/2024

Watch, follow, and discover more trending content.

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, a...
13/08/2024

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar, Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewahakikishia wananchi kuwa Serikali inaendelea na ujenzi wa barabara mijini na vijijini, na imepanga hivi karibuni kujenga barabara ya kisasa kuanzia Tunguu hadi Makunduchi yenye urefu wa kilomita 43.

Amesema barabara hiyo itakuwa na njia nne, taa, njia za wapita kwa miguu, mitaro ya maji, pamoja na bustani.

Dk. Mwinyi ameyasema hayo leo, tarehe 13 Agosti 2024, ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kuzungumza na Wajumbe wa Kamati za Siasa za Halmashauri Kuu ya CCM za Tawi, Wadi, Jimbo, Wilaya, na Mkoa wa Magharibi kichama katika Ukumbi wa Mikutano, Viwanja vya Maonesho Nyamanzi, Dimani.

Aidha, Dk. Mwinyi amesema kuwa uwepo wa vyama vingi ni kukuza demokrasia na siyo kuleta chuki na ubaguzi nchini, na amewataka wanasiasa kuhubiri amani na kunadi sera za maendeleo kwa wananchi.

Vilevile, Dk. Mwinyi amewahimiza wanachama wa CCM kujiandikisha katika Daftari la Kudumu la Wapiga Kura ili kuwa na sifa ya kushiriki Uchaguzi Mkuu mwakani na kukihakikishia Chama Cha Mapinduzi ushindi wa kishindo.

Kwa upande mwingine, Dk. Mwinyi amewasisitiza viongozi wa CCM ngazi zote kunadi mafanikio ya Ilani ya Utekelezaji ya CCM 2020-2025 katika sekta mbalimbali zilizotekelezwa na Serikali kwa asilimia mia moja.

*CCM ITAENDELEA KUHUBIRI AMANI, UMOJA  NA MSHIK**ANO-RAIS MWINYI*Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi...
12/08/2024

*CCM ITAENDELEA KUHUBIRI AMANI, UMOJA NA MSHIK**ANO-RAIS MWINYI*

Makamu Mwenyekiti wa CCM Zanzibar Dk.Hussein Ali Mwinyi amesema Chama cha Mapinduzi kitaendelea na msingi yake ya kudumu ya kujenga Amani, Umoja na Mshikamano na kuwahimiza wana CCM kuwa wastahamili wakati huu kuelekea Uchaguzi Ujao.

Dk.Mwinyi ameyasema hayo leo tarehe 12 Agosti 2024 ikiwa ni mwendelezo wa ziara yake ya kuzungumza na Wajumbe wa Kamati za Siasa za Wadi, Tawi, Jimbo, Wilaya na Mkoa za Mkoa wa Kusini kichama katika ukumbi wa Dkt.Ali Mohamed Shein, Tunguu.

Aidha Dk.Mwinyi amewanasihi Viongozi wa Vyama vya Siasa kuacha kuhubiri Siasa za chuki na badala yake kuhubiri Amani kwa dhamira ya kuimarisha Amani ya nchi.

Halikadhalika Dk.Mwinyi amesema Chama cha Mapinduzi kimefanikiwa kwa asilimia mia moja katika utekelezaji wa Ilani na kuwahimiza wananchi kuunga mkono hatua hiyo.

Pia ameeleza kuwa Serikali bado ina mpango wa kujenga barabara ya kisasa kuanzia Tunguu hadi Makunduchi yenye urefu wa takriban kilomita 43. Barabara hiyo itakuwa ya njia nne na yote itafungwa taa.

Kwa upande mwingine Dk.Mwinyi amewasisitiza wana CCM kujiandikisha katika Daftari la kudumu la Wapiga kura ili kuwa na sifa ya kushiriki Uchaguzi mkuu mwakani na kukihakikishia Chama cha Mapinduzi Ushindi.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema tayari Serikali imeshatenga ki...
12/08/2024

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mhe. Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema tayari Serikali imeshatenga kiasi cha shilingi bilioni 31.8 kupitia Wakala wa Uwezeshaji wa Wananchi Kiuchumi, ikiwemo kuwawezesha vijana. Tayari shilingi milioni 338.6 zimetolewa kwa makundi mbalimbali.

Dk. Mwinyi ameyasema hayo katika maadhimisho ya kilele cha Siku ya Vijana Kimataifa 2024, yaliyofanyika Golden Tulip Hotel, Airport, Mkoa wa Mjini Magharibi, Unguja.

Aidha, Dk. Mwinyi ameeleza kuwa tayari vijana 500,000 wanaendelea kupata mafunzo ya stadi za maisha, mafunzo ya matumizi ya TEHAMA, na ujasiriamali.

Rais Mwinyi ameridhia maombi yaliyotolewa na vijana katika maadhimisho hayo, ikiwa ni pamoja na kuzingatia suala la maendeleo ya vijana katika mipango yao na kuongezwa kwa bajeti ya wizara katika masuala yanayohusu vijana na taasisi za mikopo ili kuwawezesha vijana kupata mikopo kwa wepesi na kwa urahisi.

Aidha, Dk. Mwinyi amewataka vijana kushiriki kwa wingi na kugombea katika uchaguzi mkuu ujao na kuahidi kuongeza idadi ya vijana katika uteuzi wa nyadhifa mbalimbali Serikalini.

Naye, Waziri wa Habari, Vijana, Utamaduni, na Michezo Mhe. Tabia Maulid Mwita amesema juhudi zinaendelea za kuimarisha vituo vya stadi za maisha na tayari Serikali imetenga shilingi bilioni 4.5 kwa ajili ya ujenzi wa kituo kikubwa cha kuwawezesha vijana.

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imejipanga kuhakikisha vij...
12/08/2024

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Ali Mwinyi amesema Serikali imejipanga kuhakikisha vijana wanapata elimu bora inayohitajika katika soko la ajira.

Amewahakikishia vijana kuwa Serikali itaendelea kuwekeza katika miundombinu ya elimu ya ufundi, ujuzi, na maarifa kwa ajili ya kuwajengea vijana uwezo.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo tarehe: 10 Agosti 2024, wakati alipofungua Kongamano la Vijana la Kitaifa lililobeba kauli mbiu inayosoma “Kuwa Kijana wa Tofauti” katika Hoteli ya Zanzibar Beach Resort, Mbweni, Mkoa wa Mjini Magharibi Unguja.

Aidha, amewataka vijana kuzichangamkia fursa zilizopo zinazoandaliwa na Serikali kwa lengo la kuzifikia ndoto zao.
Kuhusu suala la uongozi, ametoa wito kwa vijana kushiriki kikamilifu na kujitokeza kwa wingi kugombea nafasi za uongozi katika Uchaguzi Mkuu ujao wa mwaka 2025.


Wakati huo huo, katika hafla hiyo, Rais Dk. Mwinyi aliwatunuku vijana mbalimbali Tuzo za Umahiri kwa kufanya vizuri katika fani tofauti ambazo zimechangia kuwajengea uwezo vijana nchini.

Naye, mwanzilishi wa Taasisi ya Global Youth Empowerment, Ndg. Amina Sanga, alimtunuku Rais Dk. Mwinyi Tuzo Maalum ya Uongozi uliotukuka katika jukwaa hilo.

Address

Kiembesamaki
Unguja
255

Telephone

+255 773 010 006

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Marhaba online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Marhaba online:

Share

Category