Sport STAR TV

  • Home
  • Sport STAR TV
28/07/2025

“Kwanza tukimuuza Fei kwenda Simba tunapaswa kuilipa Yanga bilioni 1, maana yake ni kwamba tunatakiwa tupate pesa nyingi zaidi ya kubaki nayo. Haiwezekani tumuuze mchezaji kwa bei ambayo bilioni ikienda Yanga sisi tubakiwe na milioni 200 au tubaki na kiasi sawa na Yanga, haiwezekani”.

“Mchezaji akisema amechoka kucheza Azam football club na anataka kuondoka hakuna mtu atakayemuuliza swali lolote, ataambiwa tu soma vipengele vya mkataba, tekeleza nenda huko unakotaka kwenda”. Zaka Zakazi

TISA WAAGWA MBEYA CITY Uongozi wa klabu ya Mbeya City Fc  umetangaza kuachana na wachezaji wake tisa baada ya kumalizika...
28/07/2025

TISA WAAGWA MBEYA CITY

Uongozi wa klabu ya Mbeya City Fc umetangaza kuachana na wachezaji wake tisa baada ya kumalizika kwa mikataba yao ya kuitumikia klabu hiyo ambayo imepanda daraja.

Kupitia taarifa yake klabu hiyo imewatakia kila la kheri wachezaji hao katika maisha mengine nje ya Mbeya City Fc ambao ni Kilaza Mazoea, Pius Joseph, Jeremiah Thomas, Fred Mlelwa, Mudathir Abdalah, Andrew Kihumbi, Feisal Mganga, Medson Mwakatundu na Chesco Mwasimba

Sport STAR TV

SIMBA YAPEWA BURE JONATHAN SOWAH "Hapo awali nilisema hakuna timu Tanzania ya kumnunua Jonathan Sowah lakini baada ya ta...
27/07/2025

SIMBA YAPEWA BURE JONATHAN SOWAH

"Hapo awali nilisema hakuna timu Tanzania ya kumnunua Jonathan Sowah lakini baada ya taarifa ile nimeona watu wananishambulia. Niweke wazi hakuna pesa ambayo Simba sports club wametoa bali ni mahusiano mazuri na Rais wetu na Simba akawapa mchezaji huyo k**a mchango wake tu sio kwamba Simba wamemnunua.

Mimi ndio msemaji wa taasisi nikisema kitu nakua na uhakika na kitu ambacho nakisema , kitu pekee ambacho sisi tuliwambia Simba wakakubaliane tu na mchezaji ". Hussein Massanza afisa habari wa Singida Black Stars

Sport STAR TV

"Leo nataka niwambie ukweli sasa achana na haya yote yaliyokua yanaendelea na sisi tunacheka. Pacome ZOUZOUA alisaini mk...
25/07/2025

"Leo nataka niwambie ukweli sasa achana na haya yote yaliyokua yanaendelea na sisi tunacheka. Pacome ZOUZOUA alisaini mkataba mpya siku ya ndoa ya Aziz Ki". Ally Kamwe afisa habari wa Young Africans Sports club.

Sport STAR TV

Kocha wa Magolikipa Majdi Mnasria raia wa Tunisia 🇹🇳 amejiunga na Young Africans 🇹🇿Mnasria amewahi kupita  Sportives de ...
25/07/2025

Kocha wa Magolikipa Majdi Mnasria raia wa Tunisia 🇹🇳 amejiunga na Young Africans 🇹🇿

Mnasria amewahi kupita Sportives de Gafsa, Stade Gabsien Sports, Averine Sportif de Casserine, ES Metlaoui, Golden Arrows na Olympique Akbou.

“Huwa najutia kumpoteza Gerrard (Pique)…! Dunia itaniona kituko ila ndio ukweli unaonitesa muda mwingi…! Sikuwa mwanamke...
25/07/2025

“Huwa najutia kumpoteza Gerrard (Pique)…! Dunia itaniona kituko ila ndio ukweli unaonitesa muda mwingi…! Sikuwa mwanamke mzuri kwenye siku za karibuni…! Sikusimama kwenye nafasi ya mwanamke…! Sikuwa Mke mzuri kwa mume wangu…!”

“G ni mpole lakini alichoshwa na tabia zangu…! Tulikuwa k**a wanaume wawili…! Niliamini naweza kufanya kila kitu mwenyewe na yeye akalea tu watoto kutoka mbali…! Sio kweli…! Kuna furaha naikosa. Hakuna siku mwanaume atakuwa sawa na mimi mwanamke…!”

“Ninajikuta k**a nawaumiza watoto kwa muda fulani…! Katika hasira kubwa ya Pique nilichangia pakubwa…! Kuzingatia kazi pekee bila kumzingatia Baba wa watoto wangu, kurudi nimechoka na kujiona ninaweza kufanya majukumu mengine sikumpa utulivu G na haikuwa ngumu kwake kuniacha dunia inioneshe umuhimu wake…! Ni maumivu”

Shakira, Msanii na mtumbuizaji raia wa Colombia kuhusu maisha baada ya kuachana na Gerrard Pique

Nyota ya Afrika.TAYE TAIWO,KISIKI,KIBOKO YA MAWINGA.Na    Honorius Mpangala Ukitazama 'lineup' ya Super eagles timu ya t...
25/07/2025

Nyota ya Afrika.

TAYE TAIWO,KISIKI,KIBOKO YA MAWINGA.

Na
Honorius Mpangala

Ukitazama 'lineup' ya Super eagles timu ya taifa ya Nigeria au kikosi cha Olympiaue de Marseille lazima uwaze. Si unajua vikosi vikiwa katika mstari wa kutaka kuingia uwanjani watu hupenda kutazamana k**a nani kaanza kwa timu pinzani. K**a ni winga utaanza kunyanyua shingo yako ili upate kuona alikosimama huyu jamaa. Nywele zake timu timu ,zisizo onyesha dalili ya kukutana na chanuo kwa muda mrefu sana. Zimevurugika mithiri ya nywele za mgonjwa wa akili.

Sura ngumu yenye alama ndogo ndogo ya mipasuko ya mejeraha ya chini ya macho na juu ya macho. Unaweza kuwaza kuwa jamaa alikuwa na kazi ya kubiringisha magogo ya kupasua mbao huko mapori ya misitu ya Goboni au misitu ya pori la Akiba la Moyowosi Kakonko huko Kigoma,au Sao Hill huko Mafinga.

Rangi yake nyeusi yenye kutambulisha uafrika wake asili. Mtu fulani mwenye kimo cha wastani akiwa na urefu Wa sentimeta 183 ni k**a futi 6 hivi. Mjuvi Wa kazi ,mwili uliojengeka kwa misuli iliyojipanga vyema kila sehemu ya mwili wake.

Ni Taye Ismaila Taiwo mchezaji Wa soka. Raia Wa Nigeria aliyezaliwa April 16,1985 jijini Lagos.

Alianza safari ya soka katika klabu ya Gabros nchini Nigeria mwaka 2003 baadae akatua Lobi stars ya hapohapo Nigeria mwaka 2004. Baada ya kufanya vizuri katika timu ya vijana akaonwa na Marseille ya Ufaransa na mwaka 2005 wakamsajili.

Katika klabu ya Marseille ndipo dunia ilimtambua fullback huyu Wa kushoto.Akiwa na uwezo mkubwa Wa kupiga mipira ya faulo kwa kuachia makombora makali. Ni k**a alikuwa anaiga mambo Mengi ya Roberto Carlos.

Wajihi wake Wa kikuda asiyecheka uwanjani,kwake ilikuwa kazi kazi hadi dakika ya tisini.

Alitua klabu ya Ac Milan 2011 baada ya kuitumikia Marseille kwa muda mrefu. Alipelekwa kwa mkopo katika klabu ya QPR ya uingereza na Dynamo kiev ya Ukraine.

Ac Milan ilimwachia mwaka 2013 alipojiunga na miamba ya Uturuki ya Bursaspor. Alidumu hapo hadi 2015.Alijunga na Klabu ya HJK Helsinki pale nchini Finland na kudumu kwa mwaka mmoja hadi 2016.

Atua Lausanne mwaka 2017 na baadae kubadili upepo mwaka huo huo. Akajiunga na klabu ya AFC Eskilstuna.

AKIPIGA NA ULIMWENGU,AMKARIBISHA NDEMLA.

Akiwa katika klabu ya AFC Eskilstuna nchini Sweden hapo alikipiga na Ulimwengu aliyekuwa katika klabu hiyo. Saidi Ndemla aliwahi pata kwenda kufanya majaribio katika klabu hiyo ikiwa imeshuka daraja toka ligi kuu.Iliposhuka ndipo Taye alipoondoka na kwenda kujiunga na klabu ya Rovaniemen Palloseura mwaka 2018 inayo julikana k**a RoPs anakocheza hadi sasa.

AITUMIKIA SUPER EAGLES MIAKA NANE.

Tangu mwaka 2004 akiwa Olympique Marseille aliitumikia timu ya taifa ya Nigeria hadi 2012.

Moha vivutio vikubwa toka kwa Taye ni namna alivyokuwa na uwiano mzuri Wa kushambulia na kukaba. Mawinga aliwakomesha kwa tackling murua na ustadi mkubwa Wa kukab kwa akili. Hakika hakuna aliyetaka kukutana na Taye.

BINGWA WA LUPINYO/CHIKWINDA

Wachezaji wengi wana uvaaji Fulani Wa jezi ambao unajenga au kuota mizizi kwao. Kwa hapa Tanzania miaka ya nyuma kidogo Kiungo Wa Simba Hussein Marsha alifahamika kwa namna alivyopenda kuchomekea safi jezi na kuwa msafi nyakati zote.

Sasa Taye alipenda kuchomekea lakini 'bukta' yake aliviringisha kwa kuipindua kiuno chake. Akichomekea halafu anapiga mtindo huo mbao hata Frank Lampard aliuhusudu sana Wa kukunja seheme ya kiunoni 'bukta' yake. Mtindo ule ukiwa Nyasa tunaita Chikwinda au ukiwa Mbeya wanaita Lupinyo.

'Bukta' ikipigwa chikwinda au Lupinyo na winga au Fullback ujue kazi ni pevu. Hata k**a ni kiungo atafanya hivyo ujue kazi ni kubwa katika huo mchezo. Au mwingine huwa ndiyo kawaida yake lazima apige lupinyo au chikwinda ndipo soka lichezwe.

Walati wengi wakidhani Taye kastaafu lakini kumbe sivyo. Jamaa bado yuko uwanjani akicheza soka. Alistaafu kuchezea timu ya taifa akiwa kacheza mechi 54 pekee huku akifunga magoli 8.

Huyu ndiye Taye Taiwo fullback ya kazi kutoka Nigeria.

Sport STAR TV

Zanzibar ni njema atakae na aje, k**a huji kutembea maeneo tofauti ya Zanzibar basi njoo uchukue Viungo bora na mabeki b...
23/07/2025

Zanzibar ni njema atakae na aje, k**a huji kutembea maeneo tofauti ya Zanzibar basi njoo uchukue Viungo bora na mabeki bora, Zanzibar imebarikiwa katika hilo.

Abdulnassir Mohamed tayari ni mwananchi ,atavaa jezi ya Young Africans Sports Club msimu wa 2025-2026


TETESI:- Marcio Maximo kocha wa zamani wa Taifa Stars na Young Africans sports club inaelezwa atarudi tena Tanzania awam...
22/07/2025

TETESI:-

Marcio Maximo kocha wa zamani wa Taifa Stars na Young Africans sports club inaelezwa atarudi tena Tanzania awamu hii ikiwa ni zamu ya kuionoa timu ya Kmc football club ya Kinondoni.

Vipi ataiweza ..?

Sport STAR TV

22/07/2025

Taarifa ya asubuhi hii ni kwamba mpiga siku wa Young Africans Sports club, Mudathir Yahya kaongezewa mkataba wa miaka miwili. Hivyo yupo sana Jangwani hadi 2027.

Vipi wananchi mmependa au mlitaka aondoke tu..?

Sport STAR TV

USIMWAMINI MCHEZAJI UKADHANI SHABIKI WA TIMU YENU.Na    Cosmasy William Choga Maisha yamebadilika sana. Yale ambayo tuli...
20/07/2025

USIMWAMINI MCHEZAJI UKADHANI SHABIKI WA TIMU YENU.

Na
Cosmasy William Choga

Maisha yamebadilika sana. Yale ambayo tuliyaona yanafanyika Ulaya Kwa Sasa yanafanyika Tanzania. Kwa bahati mbaya sisi mashabiki wa soka la kitanzani hatuko tayari hatuna utayari huo ambayo wenzetu wamefikia hatua wameshakomaa nao. Lakini taratibu dawa inatuingia.

Nani alikuwa Feitoto angeondoka vile Yanga. Hakuna shabiki aliamini Fei anaondoka Yanga.

Nani anaamini k**a Zimbwe kaaga Simba . Wako wanaodhani Akaunti yake ime tapeliwa na wahuni na wanaiendesha. Hawaamini watu.

Kuto kuamini Kwa mchezaji kipenzi kuondoka katika klabu yetu ni sababu tunawapa ushabiki Hawa wachezaji katika timu zetu tukasahau k**a wao wanafanya maisha kupitia soka.

Wachezaji wa Sasa hawataki kuja kuishi k**a ilivyo kuwa Kwa wale wakongwe wetu kina Mzee Jella Mtagwa na wengine.

Kila kheri Mtumishi mwadilifu wa klabu ya Simba. Licha ya kuwa shabiki wa Yanga tangu utotoni k**a ilivyokuwa Kwa Jonas lakini Utumishi wako ndani ya Simba ulikuwa mkubwa mno. K**a ambavyo Simon msiba alivyokuwa mtumishi mwadilifu Yanga lakini ni mpenzi wa Simba tangu utotoni.

Kwa hili la Fei na la Zimbwe naona Sasa tutaanza kuishi kihalisia Kwa kutambua wachezaji sio mashabiki.

"Mchezaji mwenye malengo hawezi kuingia kwenye mtego wa ushabiki katika timu. Kitu pekee Cha kuzingatia ni umeajiriwa Ili ufanye kazi" Kelvin Yondani 'Cottom juice Mweni, Injinia, Vidic".

Sport STAR TV

"Prisons niliwapa ripoti ya kuboresha timu kuelekea msimu ujao lakini hakuna mazungumzo yeyote kuhusu mkataba mpya ambac...
18/07/2025

"Prisons niliwapa ripoti ya kuboresha timu kuelekea msimu ujao lakini hakuna mazungumzo yeyote kuhusu mkataba mpya ambacho nimeweza kufanya ni kufanikisha malengo ya timu ,Mimi k**a kiongozi wa Benchi la Ufundi nasema kuwa tumefanikiwa Kwa pamoja lakini kwenye ripoti nimeeleza mahitaji ya kikosi kuelekea msimu ujao ambavyo kinapaswa kuwa

Nafasi ambayo nilipewa Tanzania Prisons ilikuwa nzuri sababu ilinitambulisha Kwa mashabiki wa Soka Tanzania kutoka kufundisha ligi ya Wilaya ,Mkoa ,Mabingwa wa mikoa ,ligi ya Daraja la Kwanza na hata ligi kuu kupitia Tanzania Prisons ilikuwa Jambo zuri kutokana na watu ambao wamenipa nafasi ya kufanya Kazi hasa kwenye Daraja la juu la Tanzania

Malengo ya klabu ndio huamua Hatma ya mwalimu wanayemtaka ,Malengo yalikuwa ni kubakiza timu ligi kuu kwenye hilo nilifanikiwa lakini malengo ya klabu na project Yao imebadilika wanaona ni Bora kuwa na Mwalimu ambaye anaweza kuwafikisha kwenye malengo husika,Malengo ndio huamua Aina ya mwalimu ambaye anahitajika na klabu

Nimepokea ofa kadhaa kutoka vilabu vya ligi kuu na vile vya championship,Nasubiri Tu commitment kuona mambo yatakuendaje ,Lakini Kwa sasa sina makubaliano yeyote ya kuwa na Tanzania Prisons Kwa msimu ujao miezi 6 yangu imeisha"

Amani Josiah aliyekuwa kocha wa Tanzania Prisons

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sport STAR TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sport STAR TV:

Shortcuts

  • Address
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share