27/07/2025
Mabadiliko ya kasi ya teknolojia yameleta mageuzi makubwa katika mfumo wa malezi ya watoto hapa nchini, hasa kutokana na muingiliano wa tamaduni kupitia vifaa vya kidijitali k**a simu janja. Wazazi na walezi wamesema hali hiyo inaleta athari mseto kwa vijana, ikiwemo kupotea kwa maadili ya kitanzania.
Wakizungumza na , baadhi yao wamehimiza jamii kuchukua hatua madhubuti kwa kuweka mipaka ya matumizi ya teknolojia kwa watoto, sambamba na kuwalea katika misingi bora ya maadili ili teknolojia iwe msaada na si tishio kwa maendeleo ya watoto.
✍Joyce Mwakalinga
Mhariri|