Mwendokasi Media

  • Home
  • Mwendokasi Media

Mwendokasi Media Kupitia picha tunaileta dunia kiganjani mwako,

Permanently closed.

Kwahuduma za matangazo, kupitia ukurasa wetu wa Facebook, Twitter, Instagram pamoja na YouTube, Tafadhali wasiliana nasi kwa nambari +255759269138 Karibu sana.

Tanzania imechomoza kuwa nchi ya nne barani Afrika kwa uzalishaji wa dhahabu, nyuma ya mataifa yenye historia ndefu ya m...
11/07/2025

Tanzania imechomoza kuwa nchi ya nne barani Afrika kwa uzalishaji wa dhahabu, nyuma ya mataifa yenye historia ndefu ya madini ikiwemo Afrika Kusini, Ghana na Mali, ikichangia asilimia 1.3 ya dhahabu yote duniani.

Takwimu zinaonesha kuwa tangu Rais Samia Suluhu Hassan aingie madarakani mwaka 2021, uzalishaji wa dhahabu umepaa kutoka tani 55.6 mwaka 2020/21 hadi kufikia wastani wa tani 60,000 mwaka wa fedha 2024/25, hatua inayoashiria mafanikio makubwa katika sekta ya madini.

Mauzo ya dhahabu pia yamevuka matarajio, yakifikia TZS trilioni 7.27 kwa mwaka 2023 kutokana na uuzaji wa tani 55. Hali hii imechochewa na kuimarika kwa bei ya dhahabu duniani, ambayo kwa mwaka 2024 ilifikia wastani wa dola 2,386 kwa ounce, huku robo ya mwisho ya mwaka ikirekodi hadi dola 2,663 kwa ounce.

Mnamo Januari 2025, sekta ya madini nchini iling’ara kwa kufanikisha biashara ya madini ya jumla ya dola bilioni 4.1, ambapo dola bilioni 3.4 zilihusiana moja kwa moja na dhahabu pekee. Hili linawakilisha zaidi ya asilimia 50 ya mauzo yote ya nje ya bidhaa zisizo za kawaida (non-traditional exports).

Mafanikio haya yametokana na sera thabiti za serikali ya awamu ya sita, ikiwemo ile ya kuwataka wachimbaji wakubwa kutenga asilimia 20 ya uzalishaji kwa ajili ya usindikaji na biashara ndani ya nchi, hatua iliyosaidia kuongeza mapato ya ndani na kukuza uchumi.

Kwa ujumla, mchango wa sekta ya madini kwenye Pato la Taifa (GDP) umekua hadi kufikia asilimia 10.1 mwaka 2025, lengo lililowekwa mapema na serikali likitimia ndani ya muda mfupi.


Katika mjadala uliopeperushwa Jana kupitia kipindi cha Jana na Leo cha Wasafi FM, hoja ya maridhiano kati ya vyama vikuu...
10/07/2025

Katika mjadala uliopeperushwa Jana kupitia kipindi cha Jana na Leo cha Wasafi FM, hoja ya maridhiano kati ya vyama vikuu vya siasa nchini – CHADEMA na CCM – imeibuliwa kwa msisitizo mkubwa, ambapo imeelezwa kuwa ni busara kwa pande hizo mbili kurudi kukaa mezani kwa maslahi ya taifa.

Kupitia kipande cha video kilichowekwa kwenye ukurasa wa Instagram wa Wasafi FM, mmoja wa wachangiaji amesema wazi kuwa:

“Ni busara kwa CHADEMA na CCM kurudi kukaa mezani tena.”

Kauli hiyo imeibua mjadala mpana mitandaoni huku wengi wakitafsiri kuwa ni wito wa amani na mshik**ano wa kitaifa, hasa katika kipindi ambacho Watanzania wanaendelea kudai haki, uwajibikaji na mageuzi ya kisiasa yenye tija.

Wachambuzi wa masuala ya siasa wanasema mazungumzo ya kisiasa kati ya vyama vikuu hayaepukiki iwapo taifa linataka kuimarisha misingi ya demokrasia, uchaguzi huru na utawala wa sheria.

Wameeleza kuwa ni muhimu kwa viongozi wa pande zote kuweka pembeni tofauti zao na kuzungumza kwa ajili ya mustakabali wa taifa.

Kauli hii inakuja wakati ambapo mijadala kuhusu hali ya kisiasa na uchaguzi wa mwaka 2025 inazidi kupamba moto, huku wananchi wakionesha kiu ya kuwa na Tanzania yenye maelewano, umoja na mwelekeo mmoja wa maendeleo.


Tanzania inaendelea kushuhudia mapinduzi makubwa katika sekta ya ujenzi chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, ha...
10/07/2025

Tanzania inaendelea kushuhudia mapinduzi makubwa katika sekta ya ujenzi chini ya uongozi wa Rais Samia Suluhu Hassan, hali inayopelekea nyumba na miundombinu mipya kuota kila kona k**a uyoga.

Takwimu zinaonesha kuwa kabla ya Rais Samia kuingia madarakani, vifaa vya ujenzi vilivyoagizwa kutoka nje ya nchi (k**a mabati, saruji, mabomba na vifaa vingine) vilikuwa na thamani ya Dola za Marekani milioni 925.5 (sawa na takribani TZS bilioni 64).

Lakini kufikia mwaka 2024, thamani hiyo imepaa na kufikia Dola za Marekani bilioni 1.67 (sawa na TZS trilioni 4.4) – ongezeko la asilimia 12.4.

Hili ni ishara ya kuimarika kwa mazingira ya uwekezaji, kuongezeka kwa ujenzi wa nyumba za kisasa, na uhitaji mkubwa wa makazi bora kwa Watanzania. Serikali ya Awamu ya Sita inaendelea kuweka msukumo katika maendeleo ya miundombinu, jambo linalochochea ukuaji wa uchumi na kuboresha maisha ya wananchi.


Katibu Mkuu wa UVCCM, Ndg. Jokate Urban Mwegelo (MNEC) amesema Vijana wa Afrika wasichukuliwe k**a watazamaji wa histori...
09/07/2025

Katibu Mkuu wa UVCCM, Ndg. Jokate Urban Mwegelo (MNEC) amesema Vijana wa Afrika wasichukuliwe k**a watazamaji wa historia bali wawe watekelezaji wakuu wa dira mpya ya ukombozi wa Afrika wa kiuchumi, kidijitali na kisiasa.

Ndg. Jokate amesema hayo jana Julai 08 2025 alipowasilisha mada kwenye mkutano uliofanyika kwa njia ya mtandao ambapo Makatibu Wakuu wa Jumuiya za Vijana kutoka nchi za ukombozi ZANU-PF, SWAPO, FRELIMO, MPLA, ANC walishiriki na kiliendeshwa na Katibu Mkuu wa Jumuiya ya vijana wa ANC, Cde. Mntuwoxolo Ngudle.

Mkutano huo wa jana ni sehemu ya maandalizi ya mkutano mkubwa utakaofanyika nchini Afrika Kusini mwisho wa mwezi huu.

Ndg. Jokate katika hotuba yake alieleza kuwa miradi mikubwa ya kimkakati k**a Reli ya Kisasa ya SGR inayounganisha Tanzania, Burundi na DRC ni zaidi ya miundombinu, ni alama ya mshik**ano wa Afrika na chombo cha ukombozi wa kiuchumi. UVCCM kwa ushirikiano na Serikali ya Rais Dkt. Samia imehakikisha kuwa vijana wanashiriki moja kwa moja katika ujenzi wa miradi hiyo wakijifunza kujiajiri.

Ndg. Jokate pia aligusia suala la usimamizi wa rasilimali za Afrika kwa kusema; *”Africa’s mineral wealth must serve African people first”* ambapo aliwataka vijana kutobaki nyuma katika sekta ya madini, bali wawe sehemu ya mabadiliko ya kisera, kimuundo na kimaadili katika uchimbaji na usimamizi wa rasilimali.


Utafiti mpya wa Afrobarometer wa mwaka 2024 umeonesha kuwa asilimia 66 ya Watanzania wanaamini kuwa demokrasia na uhuru ...
09/07/2025

Utafiti mpya wa Afrobarometer wa mwaka 2024 umeonesha kuwa asilimia 66 ya Watanzania wanaamini kuwa demokrasia na uhuru wa kujieleza umeimarika nchini, ukilinganishwa na asilimia 46 tu ya mwaka 2017.

Matokeo haya yanadhihirisha mafanikio ya wazi katika jitihada za kukuza mazingira ya kisiasa huru na jumuishi, hususan kupitia juhudi za Rais Samia Suluhu Hassan. Tangu aingie madarakani, Rais Samia amechukua hatua madhubuti kuhakikisha wigo wa demokrasia unaongezeka na haki za kiraia zinalindwa.

Kupitia falsafa yake ya R4 inayolenga kuunganisha makundi mbalimbali ya kijamii, Rais Samia ameongoza mageuzi ya sheria kadhaa kati ya mwaka 2022 hadi 2025. Miongoni mwa hatua muhimu ni pamoja na kufuta zuio la mikutano ya hadhara kwa vyama vya siasa, hatua iliyotafsiriwa k**a ishara ya heshima kwa misingi ya kidemokrasia na utawala wa sheria.

Aidha, hatua hizi zimewapa wananchi nafasi ya kujieleza kwa uhuru zaidi, kushiriki katika mchakato wa kisiasa, na kuongeza imani kwa taasisi za kidemokrasia nchini. Utafiti huu unaweka Tanzania kwenye ramani ya nchi zinazopiga hatua kubwa katika kukuza demokrasia barani Afrika.


Rais wa Kenya William Ruto ameweka wazi kuwa hataruhusu yeyote kujaribu kuipindua serikali kwa njia zisizofuata katibaRa...
09/07/2025

Rais wa Kenya William Ruto ameweka wazi kuwa hataruhusu yeyote kujaribu kuipindua serikali kwa njia zisizofuata katiba

Rais Ruto ameeleza kuwa kuwa nchi haitakubali kusambaratishwa na watu wachache wasiopenda utaratibu wa kidemokrasia, na kuongeza kuwa serikali yake itasimamia sheria kwa uthabiti.

Ruto pia amewataka viongozi wa upinzani waache siasa za vurugu na badala yake wajipange kwa uchaguzi mkuu wa mwaka 2027 kwa kuwasilisha sera na mipango yao kwa wananchi kwa njia ya amani na demokrasia.


Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania(TEC), Padri Dkt. Charles Kitima, amesema tukio la yeye kushambuliwa ...
09/07/2025

Katibu Mkuu wa Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania
(TEC), Padri Dkt. Charles Kitima, amesema tukio la yeye kushambuliwa na watu wasiojulikana linafahamika vizuri na vyombo vya dola, na kwamba hatua zaidi kuhusu uchunguzi na haki zipo katika vyombo hivyo vya usalama.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na Jambo TV, Padri Kitima amesema kuwa tayari amehojiwa na maofisa wa usalama ambao walipata maelezo yake, na sasa anasubiri hatua zao.

“Vyombo vya dola vimekuja kunihoji, nimewaeleza niliyodhani kwa wakati ule waliyahitaji. Wenyewe wanajua, wanalijua hili tukio vizuri... mbele ya Mungu wanalijua vizuri,” amesema Padri Kitima.

Ameeleza kuwa haitakuwa vyema kwa vyombo vya dola kufanya kwa Watanzania wengine kile alichokumbana nacho yeye, na ameonesha masikitiko yake kuhusu ukimya wa kisheria licha ya tukio hilo kujulikana vyema kwa mamlaka husika.

“Nisingependa Mtanzania yeyote vyombo vinavyolifanya kazi suala langu wanavyonifanyia mimi wawafanyie wengine hivyo, nisingependa wafanye hivyo kwasababu k**a watu wanalijua tukio, na huoni kinachoendelea, nisingependa wengine wakosewe kiasi hicho”, ameeleza.

Kwa mujibu wa taarifa ya Jeshi la Polisi, Padri Kitima alishambuliwa na watu wawili wasiojulikana usiku wa Aprili 30, 2025, akiwa njiani kuelekea maliwatoni katika makazi yake yaliyopo Kurasini, Dar es Salaam. Alijeruhiwa na kulazwa katika Hospitali ya Aga Khan, ambako alitibiwa na kuruhusiwa baadaye.

Mei 25, 2025 Jeshi la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam kupitia taarifa iliyotolewa na Kamanda wa Polisi Kanda maalum ya Dar es Salaam Jumanne Muliro, lilieleza kumshikilia Rauli Mahabi/ Haraja, mkazi wa Kurasini, kwa tuhuma za kuhusika katika shambulio dhidi ya Kitima na kwamba lililenga kumfanyia mahojiano.


Watu 11 wameuwawa katika maandamano ya kuipinga serikali yaliyofanyika Kenya 07.07.2025. Jeshi la polisi la nchi hiyo li...
08/07/2025

Watu 11 wameuwawa katika maandamano ya kuipinga serikali yaliyofanyika Kenya 07.07.2025. Jeshi la polisi la nchi hiyo limetoa takwimu hizo na kuongeza pia kuwa makumi ya maafisa wa polisi wamejeruhiwa.

Wakati wa maandamano hayo ya Saba Saba, polisi walilazimika kutumia maji ya kuwasha kuwatawanya waandamanaji katika eneo la Kangemeni jijini Nairobi.

Mamlaka zililazimika kufunga barabara kubwa zinazoingia katika mji mkuu na shughuli nyingi za biashara zilifungwa k**a njia ya kudhibiti machafuko.

Julai 7 yalipofanyika maandamano hayo ni siku ya kihistoria nchini Kenya inayojulikana k**a ‘Saba-Saba’ inayoadhimisha sasa miaka 35 ya kuwakumbuka watu waliopigania demokrasia na mfumo wa vyama vingi mwaka 1990.


Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo amebainisha kuwa Serikali ya awamu ya sita na Ch...
08/07/2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Mipango na Uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo amebainisha kuwa Serikali ya awamu ya sita na Chama Cha Mapinduzi Kinathamini uwepo wa Vyombo vya habari imara, katika kukuza uwajibikaji na kuimarisha utawala bora nchini.

Akizungumza na wahariri wa Vyombo vya Habari na wanahabari leo Julai 08, 2025 Mjini Dar Es Salaam kuelezea kuhusu kutamatika kwa mchakato wa uandaaji wa Dira 2050, Prof. Kitila amebainisha kwamba tayari Serikali pia imeanza mchakato wa kuona namna ya kufadhili ruzuku kwa Vyombo vya habari nchini kwa kutumia Kodi za wananchi k**a sehemu ya kuviimarisha katika utendajikazi wake.

“Mtu ambaye anadharau Vyombo vya habari ni mtu mpumbavu sana. Vyombo vya habari ni sehemu ya jambo muhimu kwenye jamii yoyote iliyoelimika kwahiyo tuzungumze kuziimarisha k**a zipo dhaifu lakini huwezi kudharau media.”Amesema Prof. Kitila.

Akisisitiza umuhimu wa Vyombo vya habari kuwa wakweli na kutosita kufanya kazi yake kwa kuzingatia misingi ya taaluma yao bila upendeleo, Kitila amebainisha kuwa Vyombo vya habari kupata ruzuku hiyo haitakuwa sehemu ya kutengeneza upendeleo, akitaka Vyombo vya habari kuwa wakweli bila kuchagua upande ili kuisaidia serikali katika kukuza uwajibikaji na utawala bora serikalini.


Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, alhamisi ya Julai 17, 2025 Kwenye Ukumbi wa Mikutano w...
08/07/2025

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. Samia Suluhu Hassan, alhamisi ya Julai 17, 2025 Kwenye Ukumbi wa Mikutano wa Jakaya Kikwete Mjini Dodoma, atazindua rasmi Dira ya maendeleo ya Taifa ya mwaka 2050, akiweka rekodi ya kuwa Rais wa Pili wa Tanzania kusimamia na kuratibu uandikaji wa Dira hiyo ya miaka 25 ijayo.

Akizungumza na wahariri wa Vyombo vya habari leo Jumanne Julai 08, 2025 Jijini Dar Es Salaam, Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais mipango na uwekezaji Prof. Kitila Mkumbo, ameeleza kuwa uzinduzi wa Dira 2050 unafuatia hatua muhimu ya Baraza la Mawaziri kuidhinisha dira hiyo pamoja na kuridhiwa kwa Dira 2050 na Bunge la Tanzania.

"Kwa mara ya pili nchi yetu inaandaa Dira ya maendeleo ambayo haina mwelekeo wa kiitikadi ya Chama cha siasa na Rais Samia Suluhu Hassan anakuwa Rais wa Pili kuandika Dira, Rais wa kwanza alikuwa Hayati Benjamini Mkapa." Amesema Prof. Kitila.

Aidha Waziri Kitila amebainisha kuwa wakati wa uzinduzi wa Dira 2050, Watanzania ndipo watakapopata fursa pia ya kufahamu yaliyomo ndani ya Dira hiyo, akiwashukuru wadau mbalimbali kwa ushiriki wao kikamilifu katika hatua zote 12 za Mchakato wa uandaaji wa Dira hiyo ya Maendeleo ya Taifa.

Katika hatua nyingine, Prof. Kitila ameeleza kuwa Rais Samia alielekeza dira hiyo kupitishwa Bungeni, ikiwa ni mara ya kwanza kufanya hivyo ili kuweka kinga ya kisheria kwa Dira 2050 katika kudhibiti Serikali zijazo kukiuka ama kuachana na yaliyomo katika Dira hiyo kwa miaka 25 Ijayo.

Katika kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Taifa la Comoro, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt...
07/07/2025

Katika kilele cha maadhimisho ya miaka 50 ya Uhuru wa Taifa la Comoro, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, ameonesha kwa mara nyingine nafasi ya Tanzania katika jukwaa la kimataifa kwa kushiriki moja kwa moja katika tukio hilo la kihistoria.

Rais Samia aliwasili nchini Comoro akipokelewa kwa heshima kubwa na mwenyeji wake, Rais Azali Assoumani, pamoja na viongozi waandamizi wa taifa hilo. Katika hotuba yake, Rais Samia alisisitiza mshik**ano wa kidugu kati ya mataifa hayo mawili na kuhimiza mshik**ano wa Afrika k**a nyenzo ya maendeleo ya kweli.

“Maadhimisho haya si ya Comoro peke yake, bali ni ya Afrika yote. Uhuru wa taifa moja ni ushindi wa bara lote,” alisisitiza Rais Samia huku akishangiliwa na umati mkubwa uliohudhuria uwanjani.

Mbali na kushiriki katika gwaride na shughuli mbalimbali za kitaifa, Rais Samia alitumia ziara hiyo kuimarisha uhusiano wa kiuchumi na kijamii kati ya Tanzania na Comoro. Ujumbe wake ulijumuisha mawaziri na wakuu wa taasisi mbalimbali za serikali waliowasiliana na wenzao kwa ajili ya mikataba ya ushirikiano.

Ziara hii inaonesha kwa dhahiri kwamba Tanzania chini ya uongozi wa Rais Samia inazidi kushika nafasi muhimu katika siasa za kanda na bara zima la Afrika, kwa kutumia diplomasia ya maelewano, mshik**ano na maendeleo ya pamoja.


Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva ameendelea na ziara ya kikazi ya kata kwa kata katika kuwafikia wananchi wa w...
07/07/2025

Mkuu wa Wilaya ya Lindi, Victoria Mwanziva ameendelea na ziara ya kikazi ya kata kwa kata katika kuwafikia wananchi wa wilaya hiyo kwa ukaribu na kutimiza adhma mbalimbali kwa mujibu wa ratiba yake ikiwa ni pamoja na Kuwa na mkakati maalum wa kusikiliza na kutatua changamoto mbalimbali za wananchi pamoja na Muendelezo wa ukaguzi wa utendaji wa watendaji wa serikali na kukagua, kuweka mawe ya msingi, kutembelea na kuzindua miradi mbalimbali iliotekelezwa chini yake Serikali ya awamu ya sita.

Aidha, Mhe Victoria ameendelea na ukaguzi wa miradi ya maendeleo ambapo amepata nafasi ya kufanya ukaguzi wa umaliziaji wa Ujenzi wa mabweni mawili katika shule ya Sekondari Nangaru- yenye thamani ya 103,727,096 na kuweka jiwe la msingi katika mradi huo sambamba na kuzungumza na watumishi, wanafunzi na wananchi waishio eneo jirani.

Akiendelea na ziara yake, Sambamba na hapo DC Mwanziva amekagua Ujenzi wa madarasa 3 na matundu 6 ya vyoo shule ya Msingi Makumba ambapo pia ameweka jiwe la msingi katika mradi huu wenye gharama ya 83,200,000 na kupokelewa kwa kishinda na wanachi wenye hamasa kubwa baada ya kupokea mradi huo.

Katika hatua nyingine, Akizungumza na wananchi waliojitokeza katika maeneo ya Mradi DC Mwanziva amemshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Dkt Samia Suluhu Hassan kwa maendeleo makubwa ambayo wana-Lindi wanaendelea kupata na kunufaika katika nyanja na Sekta mbalimbali zikiwemo Elimu, Afya, Miundombinu na Kilimo.


Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Mwendokasi Media posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Mwendokasi Media:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share