Sing'ongo Tz

Sing'ongo Tz Film Director

📸📸📸  ...   #0652296300
16/06/2025

📸📸📸 ...

#0652296300

  """    #0652296300
24/05/2025



"
"
"

#0652296300

24/05/2025

18/05/2025



Hii ni picha iliyobeba maana kubwa kwenye jinsia zetu na matatizo mengi yaliyokosa maelewano..Mwanaume hajui kuwa chini ...
19/11/2024

Hii ni picha iliyobeba maana kubwa kwenye jinsia zetu na matatizo mengi yaliyokosa maelewano..

Mwanaume hajui kuwa chini kuna nyoka. Na mwanamke haelewi kuwa juu kuna jiwe kubwa limemkandamiza Mwanaume wake..

Mwanamke anafikiri, naenda kuanguka na siwezi kupanda, kwasababu nyoka atanin'gata..

Lakini kwanini jamaa hanivuti kwa nguvu?

Mwanaume anafikiri, nipo kwenye maumivu makali, bado namvuta kwa kadri ya uwezo wangu,

Kwanini hajitahidi kujivuta juu na yeye?

Mwanamke anahisi mwanamme wake anatoa msaada k**a hataki vile/ amelazimishwa.

Mwanaume anadhani, mwanamke wake anadeka, anajiendekeza na hataki kusaidiwa.

Somo tunalojifunza hapa, huwezi kuona presha anayopitia mwenzio, na yeye hawezi kuona maumivu yako..

Mwanamke anamlaumu mwanaume yupo bize hampi muda, kumbe anabanwa na kazi zake..

Mwanaume anamlaumu mwanamke amepoteza upendo kumbe ana madeni ya vikoba vyake..

Mwanamke asipopata kwa wakati alichokiomba anajihisi amenyimwa ama hajaliwi tena.

Unapoambiwa moyo wamtu kicha unapaswa kuelewa k**a mtu alie komaa akili.

Kwenye maisha tunayoishi kila mmoja anajaribu kuficha siri yamachungu yanayomuumiza moyo na akili yake ,k**a watu wangefunguliwa mioyo yao ata wale waliokwisha tengana Wangeoneana huruma maana kipo kitu ambacho hakikuwekwa wazi.

Jifunze kuwa nauvumilivu pasipo kua na lawama .

Kila mmoja wetu anajambo linalomuumiza , haswaa kwamaisha yasasa tunayoishi.

Chakushangaza tubebakia kulaumiana na kila mmoja humuona mwenzake nimkosefu kila siku, hakuna anaweza kujiuliza kwanini makosa yapo?.

Kwakweli inauzunisha sana na k**a kipo kitu umejifunza , basi jifunze kuishi maisha yasio na lawama kwa wengine.

Shere ujumbe huu kuwasaidia wanaoitaji.

Pia usiache kufollow page hii uzidi kujifunza kitu katika maisha yakila siku.

Mimi na mke wangu hatukua na maelewano usiku wa jana, na hata asubuhi ya leo kabla ya kuondoka kwenda kazini, Kila mmoja...
13/11/2024

Mimi na mke wangu hatukua na maelewano usiku wa jana, na hata asubuhi ya leo kabla ya kuondoka kwenda kazini, Kila mmoja bado alikua kamkasirikia mwenzie.

Mimi na yeye wote tunafanya kazi mjini, na ni kawaida yetu kila siku kutoka pamoja kwenda kazini, tumekua ni watu wa kutaniana wakati wa kujiandaa na tunapotoka ndani anaechelewa kutoka ndo hua anatakiwa kufunga mlango, kuna wakati hua namfichia mafuta yake ya kupaka ili tu achelewe kumaliza kujiandaa na afunge mlango, utani na kuchezeana hapa na pale mda huo hua ni jadi yetu.

ila leo mambo yalikua tofauti kidogo kutokana na kutokua na maelewano.

Leo baada ya kujiandaa nilitoka nje tofauti na ilivyozoeleka na yeye akanifata nyuma, akafunga mlango tukaanza kutembea kwenda stand kupanda gari, kawaida yetu hua tunakaa seat ya pamoja ila leo kila mtu alikaa seat yake, ye alikaa mbele mie nikawa nyuma.

Pembeni ya mke wangu alikua amekaa Askari mmoja..

Asikari yule akamwangalia mke wangu Niliona jinsi alivyoangalia nywele na uso wake kwa kupendeza sana. Kisha akamwambia amependeza. Mke wangu alitabasamu na kumwambia asante.

Alimuuliza mke wangu anaenda wapi akamwambia anaenda job

Wakati wote huu, nilikuwa nimeiketi nyuma na kusikiliza mazungumzo yao.

"Naitwa Hemed" Mimi ni askari k**a unavyoniona kwenye sare zangu, nimetoka depo mwezi uliopita na sasa naelekea kwenye kituo changu cha kazi nilichopangiwa, Mke wangu alitikisa kichwa.

Kondakta alipoomba nauli kwa mke wangu, afande alijitolea kulipa, akatoa noti ya 2000 alafu akasema wawili inamaana yeye pamoja na mke wangu.

Mke wangu akamshukuru na akatabasamu

Basi afande akaendelea

"Mie nitashuka hapo mbele kituo kinachofata, hivyo naomba ukipata nafasi unawezapita hapo unisalimie nitakuepo katika kituo kidogo cha police hicho hapo mbele, lakini pia naomba nipate namba yako kwa mawasiliano zaidi”

Mie kwakua nilikua nyuma ya mke wangu niliyasikia maongezi yao yote, baada ya kusikia mke wangu kuombwa namba na afande Sikupoteza muda wowote tena. Nilimpiga mke wangu mabega yake mara moja.

Kageuka

Kisha nikamwambia

"I hope ulikumbuka kuweka kijiko ndani ya lunch box ya Gift? Unajua huwa unasahau.”

Mke wangu alichanganyikiwa Pengine alikuwa anajiuliza Gift ni nani, na kwanini nimeamua kuzungumza naye. Kabla hajaniuliza maswali yoyote zaidi niliongeza.

"Jaribu kumchukua kutoka shuleni mapema leo. Mie Nitachelewa kurudi nyumbani. Pia itapendeza leo upike chapati na nyama rost kwa ajili ya chakula cha usuku "

Mke wangu alizidi kuchanganyikiwa

Kisha akamtazama askari na kunirudishia macho yake. Alielewa kile nilikuwa najaribu kufanya.

"Sawa honey" Alitabasamu.

Askari aligeuka na kunitazama kisha akanisalimia sana Kisha akamuuliza mke wangu.

"Huyu ni mume wako?"

Mke wangu alitabasamu. Askari kaniangalia tena na tena

Kisha akatazama kwa mara ya mwisho na akatabasamu kwangu.

Mie Sikutabasamu hata kidogo

Tulipofika kwenye kituo tunachoshukia ili tupate kupanda basi lingine nilishuka kutoka kwenye basi na kumvuta mke wangu kwa nguvu.

Mke wangu alishindwa kujizuia kuacha kucheka. Tukiwa tunatembea huku nimemshika mkono nikamsikia akiuliza.

"Honey Gift ni nani? "

"Gift ni binti yetu wa baadae. Nilimjibu huku nimemkazia macho"

Mke wangu akacheka sana.

Tulipanda basi lingine na safari hii sikutaka tena kukaa mbali na mke wangu, na konda alipoomba nauli nilitoa chapu na kusema “wawili” tulitazamana na mke wangu tukajikuta tunacheka wote kwa pamoja, na jioni ilipofika tulilejea nyumbani na nambo yalikua bam bam na ugomvi wetu ukawa umeishia hapo.

NB: Unapompa mpenzi wako umbali, kiroho na kimwili, unampa shetani akae kwenye nafasi hiyo.

Anachukua nafasi yako bila ruhusa yako na anajijengea makao kwako.
Usiruhusu shetani awe na nafasi nyumbani kwako. funga njia zote za shetani kuweza kupitia.

Fanya uwepo wako ujulikane

Mungu aibariki ndoa yako na mahusiano yako Sing'ongo Tz

13/11/2024
   📸📸📸Mua: Shot by
19/10/2024

📸📸📸
Mua:
Shot by

Address


Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sing'ongo Tz posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sing'ongo Tz:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share