Jua na Junior

  • Home
  • Jua na Junior

Jua na Junior Do you know? Je wajua? Motto: Know what you don't know
Kauli mbiu: Jua usichokijua

Ni ukurasa rasmi wa chombo cha habari cha mtandaoni kiitwacho Junior MedTech Tanzania Limited kwa ajili ya kuwajuza watu mambo ambayo wengi wetu hatufahamu.

Mitandao ya Junior MedTech International imebadili jina na nembo (logo), sasa ni InterMedTech Group na nembo mpya k**a i...
11/07/2025

Mitandao ya Junior MedTech International imebadili jina na nembo (logo), sasa ni InterMedTech Group na nembo mpya k**a inavyoonekana kwenye picha.

Je Wajua?.Mama wa Jack Chan aitwae Lee lee Chan alikuwa mfanyabiashara za madawa ya kulevya na k**ali alipokutana na bab...
11/07/2025

Je Wajua?.

Mama wa Jack Chan aitwae Lee lee Chan alikuwa mfanyabiashara za madawa ya kulevya na k**ali alipokutana na baba yake Jack Chan aitwae Charles Chan ambaye alikuwa mpelelezi wa polisi, mzee Charles aliingia kwenye mapenzi na Lee wakati wa majukumu yake ya kumpeleleza kuhusu biashara haramu alizokuwa akifanya Lee.

Je Wajua?Wanandoa wanatakiwa kuanza na tendo la ndoa kabla ya kuswali ukifika wakati wa swala?.Kwa mujibu wa mafundisho ...
15/05/2025

Je Wajua?
Wanandoa wanatakiwa kuanza na tendo la ndoa kabla ya kuswali ukifika wakati wa swala?.
Kwa mujibu wa mafundisho katika dini ya kiislam, kuna ibada nyingi ambazo wanaadam wanapaswa kuzifanya lakini baadhi ya ibada hizo ni za lazima (faradhi) na nyingine sio lazima kuzifanya, miongoni mwa ibada zote hizo ibada ya swala imepewa kipaumbele zaidi hususani ikapangiwa muda maalum na kila muislam anapaswa kuacha shughuli yoyote anayoifanya aende kuswali ukifika wakati wa swala isipokuwa wanandoa waliopo kwenye tendo la ndoa kwa wakati huo.
Waislam wote waliooa au kuolewa iwapo umefika wakati wa swala za faradhi (lazima) na wakati huo huo wanandoa hao walitaka au walikuwa wakifanya ibada nyingine ya tendo la ndoa dini ya kiislam inasema wanandoa hao wanapaswa kumalizia au kufanya ibada ya tendo kwanza mpaka watakapomaliza kisha waende kuswali.

JE WAJUAJe wajua kuwa wanandoa hawaruhusiwi/ hawalazimishwi kutoleana ushahidi mahak**ani?.Kwa mujibu wa sheria za nchi ...
04/05/2025

JE WAJUA

Je wajua kuwa wanandoa hawaruhusiwi/ hawalazimishwi kutoleana ushahidi mahak**ani?.

Kwa mujibu wa sheria za nchi ya Tanzania kwenye kifungu cha sheria namba 130 mke na mume waliooana kwa ndoa ya aina yoyote kati ya ndoa aina nne zinazotambulika nchini ambazo ni:

1. Ndoa za kidini (Kikristo, Kiislam na Dini nyingine)

2. Ndoa za kimila (Ndoa za kimakabila)

3. Ndoa za kiserikali (Bomani/ kwa mkuu wa wilaya)

4. Kuishi zaidi ya miaka miwili (2) bila ya ndoa

Hawatoruhusiwa  au hawatolazimika kutoleana ushahidi mahak**ani wa kumfunga iwapo mke au mume ameshuhudia mwenzie akifanya kosa aina yoyote isipokuwa makosa ya kimaadili k**a vile Kubaka, Kulawiti, Kunajisi n.k.

Wanandoa wanaruhusiwa au wanalazimishwa kuteteana mahak**ani hata k**a ameshuhudia mwenzie akifanya kosa hilo

Je wajua?.Alan Walker sio mwanamuziki na sio mwanamke k**a wanavyofahamu watu wengi?.Kijana wa kiume aitwaye Alan Olav W...
24/08/2024

Je wajua?.
Alan Walker sio mwanamuziki na sio mwanamke k**a wanavyofahamu watu wengi?.
Kijana wa kiume aitwaye Alan Olav Walker maarufu k**a Alan Walker au pia anafahamika k**a DJ Walkzz aliyezaliwa tarehe 24 Agosti 1997 Northampton, England, ambaye anamiliki vibao kadhaa vya muziki k**a vile Alone part 1, 2 na 3, Sing me to sleep, Faded n.k sio msanii wa muziki k**a watu wengi wanavyojua bali Alan ni mtayarishaji wa muziki (Producer) na Disc Jookey (DJ) wa muziki kutokea nchini Norway.
Alan huwa anaandaa beat za muziki kisha huwashirikisha wasanii mbalimbali maarufu wengi wao ni wa k**e na ndio maana watu wengi hujua kuwa Alan ni mwanamke k**a wanavyosikia nyimbo zikiimbwa na watu wengi wanajua kuwa Alan ni mwanamke na ndiye anaeimba, Alan pia huwa amejiweka kuwa na alama ya kuziba uso kwa barakoa na kubakiza usawa wa macho jambo ambalo limewafanya watu wengi kushindwa kumjua.

Je wajua?.Ukiandika namba 241543903 google kisha ukatafuta (uki-search google) yatakuja matokeo ya picha nyingi za watu ...
14/08/2024

Je wajua?.
Ukiandika namba 241543903 google kisha ukatafuta (uki-search google) yatakuja matokeo ya picha nyingi za watu wameweka vichwa kwenye friji?.
Ukiingia google kisha ukatafuta (sachi) namba 241543903 matokeo yatakayokuja ni picha nyingi sana za watu wakiwa wameweka vichwa kwenye friji.
Mnamo tarehe 6 aprili 2009 mjini New York nchini Marekani msanii mmoja aitwae David Horvitz alipost mtandaoni picha akiwa ameweka kichwa ndani ya friji na namba 241543903 ilikuwa ni jina (kichwa) cha ile picha, baada ya hapo dakika chache mbele mtu mwingine alipost picha akiwa ameweka kicwa ndani ya friji lilelile aliloweka Horvitz, baada ya miezi kadhaa picha za watu nyingi zilisambaa mitandaoni zikionesha watu tofauti tofauti wakiwa wameweka vichwa kwenye friji k**a alivyofanya Horvitz na namba 241543903 pia.
Akihojiwa bwana Horvitz alisema yeye alipata wazo hilo baada ya kuambiwa na rafiki yake kuwa anaumwa kichwa na yeye akamshauri rafiki yake huyo aweke kichwa ndani ya friji ili apunguze maumivu ya kichwa.

Je Wajua?Viumbe hatari zaidi wenye kuua watu kwa haraka zaidi kwa mwaka?Duniani kuna viumbe mbalimbali wenye uwezo wa ku...
14/06/2024

Je Wajua?
Viumbe hatari zaidi wenye kuua watu kwa haraka zaidi kwa mwaka?
Duniani kuna viumbe mbalimbali wenye uwezo wa kuua mtu, kati ya hao wapo viumbe hatari zaidi ya wote wenye uwezo wa kuua watu kwa haraka zaidi.
Wafuatao ni viumbe 10 hatari zaidi wenye uwezo wa kuua watu wengi kwa mwaka.
1. MBU (Mosquito)
Mbu ndiye kiumbe anayeongoza kwa kuua watu wengi kwa mwaka na ana uwezo wa kuua watu wapatao laki saba na elfu ishirini na tano (725,000).
2. BINADAMU (Human)
Binadamu nachukua nafasi ya pili duniani kwa kuweza kufanya mauaji ya watu wengi zaidi kwa mwaka na ana uwezo wa kuua watu wapatao laki nne (400,000) kwa mwaka.
3. NYOKA (Snake)
Nyoka huchukua nafasi ya tatu na anao uwezo wa kuua watu wapatao laki moja na elfu thelathini na nane (138,000) kwa mwaka.
4. MBWA (Dog)
Mbwa huchukua nafasi ya nne na ana uwezo wa kuua watu wapatao elfu hamsini na tisa (59,000) kwa mwaka.
5. KUNGUNI (Reduviidae)
Si kunguni wote wanaua ila kuna aina maalum ya kunguni waitwao REDUVIIDAE ndio wenye kuua na huchukua nafasi ya tano na ana uwezo wa kuua watu wapatao elfu kumi kwa mwaka (10,000).
6. NG'E (Scorpion)
Nafasi ya sita inachukuliwa na ng'e ambae ana uwezo wa kuua watu wapatao elfu tatu na mia tatu kwa mwaka (3,300).
7. MAMBA (Crocodile)
Nafasi ya saba inachukuliwa na Mamba ambae ana uwezo wa kuua watu wapatao elfu moja kwa mwaka (1,000).
8. TEMBO (Elephant)
Nafasi ya nane inachukuliwa na tembo ambae ana uwezo wa kuua watu wapatao mia sita kwa mwaka (600)
9. KIBOKO (Hippopotamus)
Kiboko anashika nafasi ya tisa na ana uwezo wa kuua watu wapatao mia tano (500) kwa mwaka.
10. SIMBA (Lion)
Simba anachukua nafasi ya kumi ambapo ana uwezo wa kuua watu wapatao mia mbili (200) kwa mwaka.
Ahsanteni.

Je wajua?Kukopa mikopo kwenye apps hufikia kwenye matusi na kuhack simu?.Muendelezo.....10. Inawezekana ukalipa deni mar...
20/05/2024

Je wajua?
Kukopa mikopo kwenye apps hufikia kwenye matusi na kuhack simu?.
Muendelezo.....
10. Inawezekana ukalipa deni mara 2.
Kwa uthibitisho tulionao tumegundua unaweza ukalipa deni moja mara mbili yaani mfano unadaiwa 50,000 ukajikuta unalipa 100,000, tuliwasikia wakisema iwapo utalipia kwa njia nyingine tofauti na waliyosema wakati wamekupigia, kwa mfano ukipigiwa simu kisha ukaambiwa tunakutumia link uingize namba ya siri ili ulipe ukakataa kwa sababu hauwaamini bali utaenda kulipa kwenye app uliyokopa huenda watakwambia kwamba usiende kulipa kwenye app kwasababu mtandao unasumbua na watakwambia ukilipa kwenye app basi utalipa mara 2.
11. Kufungiwa kukopa kwenye taasisi nyingine za mikopo.
Iwapo utashindwa kulipa mkopo kwenye app au taasisi ya mikopo taarifa zako zitatumwa kwenye mtandao wa alama za mkopaji ambapo itamuwezesha mkopeshaji mwingne kufahamu taarifa zako za mikopo iliyopita k**a ulilipa vizuri au haukulipa vizuri ama haukulipa kabisa, hivyo huenda ukakosa mkopo kwenye taasisi nyingine kwasababu ya apps hizo.
Kwa atakayetaka uthibitisho wa hivyo vilivyoandikwa anaweza kiwasiliana nasi.
Kwa ushauri wetu ili kukwepana na hayo yote ni vyema ukaacha kabisa tabia ya kuchukua mikopo kwenye apps hizo.
Ahsanteni.

Je wajua?Kukopa mikopo kwenye apps hufikia kwenye matusi na kuhack simu?Muendelezo....5. Kuingiliwa katika simu yako ( k...
20/05/2024

Je wajua?
Kukopa mikopo kwenye apps hufikia kwenye matusi na kuhack simu?
Muendelezo....
5. Kuingiliwa katika simu yako ( kuhack).
Utakapoanza kuzozana nao ndani ya siku ya 6 na ya 7 na ukasema huna pesa wataanza kukuingilia kwenye mfumo wako wa mawasiliano (simu yako) na kuiba taarifa zako za ujumbe (meseji) na majina na namba za simu zilizopo kwenye simu yako, kitu ambacho ni kosa kisheria kuhack mawasiliano ya mtu.
6. Vitisho.
Utaanza kutishiwa kwa kupigiwa simu au kwa meseji kwamba wataingilia simu yako na kuchukua namba za watu wako kisha kuwatumia meseji, kuwapigia na kuwaweka kwenye group la WhatsApp ili wawataarifu wakusaidie kulipa na pia watakwambia kwamba watatuma matusi kwa ndugu zako na watakuita wewe ni tapeli na watakukomesha.
7. Kuvujisha taarifa zako.
Usalama wa taarifa zako pia ni mdogo huenda wakachukua taarifa zako na kupeana na wakopeshaji wengine ili wakuharibie au kutoa tahadhari kwa wenzao na pia watatoa taarifa zako kwa ndugu na marafiki zako wa kwenye simu yako, kitu ambacho pia ni kosa kisheria kuvujisha taarifa za mtu
8. Njia ya malipo isiyo salama.
Tumegundua pia njia yao ya kulipa mkopo huo sio salama hususani kwa wakati huu ambapo wasomi wa IT wapo wengi mtaani wakifanya utapeli, ikifika siku ya 6 watakupigia watu usiowafahamu na watakutumia link ambayo itakuwa imeshaandikwa kiasi cha kulipa na jina la app uliyokopa na watakwambia uweke namba ya siri tu ili ulipe kitu ambacho kwa sasa sio salama kwani anaweza mtu yoyote anayeweza akakutumia link na akataka ulipe kwa njia hiyo au unaweza ukalipishwa pesa kiwango cha juu zaidi ya ulichokopa kwasababu haujaamua wewe kiasi unakuta umeshaamliwa.
9. Matusi.
Pia tumegundua pia katika kudai kwa watumishi wao watatumia lugha chafu na matusi mbalimbali kukulazimisha ulipe hata k**a muda wa malipo haujaisha au hata k**a hauna cha kulipa lakini watakutukana iwapo ukiwa hujalipa k**a wanavyotaka wao.
10. Inawezekana ukalipa deni mara 2.
Itaendelea

Je wajua?.Madhara ya kukopa mikopo kwenye mitandao ya mikopo mtandaoni (Loan Apps) hufikikia kwenye matusi na kuhack?Kwa...
20/05/2024

Je wajua?.
Madhara ya kukopa mikopo kwenye mitandao ya mikopo mtandaoni (Loan Apps) hufikikia kwenye matusi na kuhack?
Kwa sasa kuna Application mbalimbali zimekuwa zikitangazwa kwenye mitandao na sehemu mbalimbali zinazojihusisha na utoaji mikopo online ndani ya muda mchache kwa vigezo vya kuwa na namba ya nida, kitambulisho cha kura au cha taifa na namba ya simu ya mkopaji na za wadhamini, lakini hakuna sehemu tunaposikia au kutajwa usalama wa apps hizo ukizitumia au madhara yake wala hatuoni vibali walivyopewa kuendesha biashara hiyo na wala hatuoni sheria zinazokatazwa kufanywa au kukatazwa kwa makampuni au apps hizo.
Kwa utafiti mfupi uliofanywa na JUNIOR MEDTECH INTERNATIONAL tumegundua baadhi ya madhara ya kutumia baadhi ya apps hizo, hivyo tunawashauri watu kutotumia apps hizo kwa sababu hazijulikani zipi apps salama na zipi si salama.
Yafuatayo ni baadhi ya madhara tuliyogundua kutoka kwenye baadhi ya apps;
1. Unatamanishwa kwa viwango vikubwa vya mkopo.
Ukitazama matangazo mbalimbali utagundua kuwa wanatangaza unaweza kukopa pesa nyingi mfano 100,000 hivi lakini ukiingia kukopa utakopeshwa kiwango kidogo sana.
2. Unakopeshwa kiwango kidogo tofauti na ulivyoomba.
Pamoja na kukopeshwa pesa ndogo ila utakapoomba mkopo utaambiwa unakopa kiasi kikubwa mfano 50,000 lakini ukishakubaliwa kukopeshwa utapokea 30,000 tu na sio ile uliyoomba na utaona upungufu wa 20,000 na hujui inaenda wapi.
3. Utalipa pesa nyingi zaidi ya uliyokopa.
Ukiachana na mkopo ulioomba ni 50,000 na ukapewa 30,000 bado utaongezewa riba na itaambiwa unalipa 70,000 utakuta umeongezewa 20,000 tena riba ukijumlisha na ile 20,000 usiyopewa utakuta unakopa 30,000 unaongeza na 40,000 jumla 70,000 ndo ulipe.
4. Utadaiwa kabla ya muda kuisha.
Wakati unakopa utaambiwa ulipe ndani ya labda wiki hivi yaani siku 7 lakini watakuacha siku 5 tu ikifika siku ya 6 utaanza kupigiwa ili ulipe na watakulazimisha ulipe hata k**a hauna kabla ya siku ya 7.
5. Kuingiliwa katika simu yako ( kuhack).
Itaendelea.

Je wajua?PG, SPG, R na X ni alama zinazoonyeshwa kwenye filamu na tamthiliya katika runinga (TV) humaanisha usimamizi kw...
29/04/2024

Je wajua?
PG, SPG, R na X ni alama zinazoonyeshwa kwenye filamu na tamthiliya katika runinga (TV) humaanisha usimamizi kwa watoto na watu wazima pia?
Kwa kawaida filamu na tamthiliya huwa na maudhui na muonekano tofauti tofauti, ukiachana na maonyesho ya kawaida yanayofaa kutazamwa na mtu yeyote ila wakati mwingne kuna maonyesho huchagua umri na jamii kutokana na maudhui yaliyopo, kwa mfano maonyesho mengine huwa na maudhui ya ngono, maudhui ya kimapenzi, maudhui ya watoto tu, maudhui ya wakubwa tu, maudhui ya matusi, matumizi ya madawa ya kulevya na ulevi, au maudhui ya dharau, jeuri au madhui yasiyo na heshima au maudhui ya kutisha ambayo kuna baadhi ya jamii ya watu yanaweza kuwaathiri hivyo hawafai kuitazama.
Baadhi ya alama hizo ni k**a zifuatazo na maana zake;
G. Humaanisha GENERAL GUIDANCE maonyesho haya yanaruhusiwa kutazamwa na watu wote.
PG. Humaanisha PARENTAL GUIDANCE hii humaanisha onyesho hilo linahitaji watoto wasiangalie bila ya uongozi wa wazazi, alama hii huonekana ikiwa na namba k**a vile PG-13 humaanisha watoto wenye umri chini ya miaka 13 wasitazame bila ya uongozi wa wazazi, nyingne ni PG-16 humaanisha watoto wenye umri chini ya miaka 16 wasitazame bila ya uongozi wa wazazi, nyingne PG-18 humaanisha watoto wenye umri chini ya miaka 18 wasitazame bila ya uongozi wa wazazi n.k.
SPG. humaanisha STRONG PARENTAL GUIDANCE hii pia humaanisha onyesho hilo linahitaji uangalizi mkubwa sana kutoka kwa wazazi hivyo wazazi wahakikishe wanakuwa makini sana na watoto wao kwenye onyesho hilo.
R. Humaanisha RESTRICTED humaanisha onyesho hilo lisitazamwe kabisa kwa watu maalum, na hii pia huwa inaonekana ikiwa na namba k**a vile R-13 humaanisha watoto wenye umri chini ya miaka 13 wasitazame kabisa, nyingne R-16 humaanisha watoto wenye umri chini ya miaka 16 wasitazame kabisa, nyingne R-18 humaanisha watoto wenye umri chini ya miaka 18 wasitazame kabisa n.k.
X. Humaanisha NOT FOR PUBLIC EXHIBITION humaanisha onyesho hilo lisitazamwe mbele ya jamii ya watu wengi badala yake litazamwe na watu wachache au mmoja na wawe faragha, hii mara nyingi hutumika kwenye maonyesho ya ngono n.k.
Ahsanteni

Je wajua?MUHAMMED IQBAL DAR ndiye aliyebuni jina la nchi ya TANZANIA?Muhammed Iqbal Dar ni mtanzania mwenye asili ya Ind...
28/04/2024

Je wajua?
MUHAMMED IQBAL DAR ndiye aliyebuni jina la nchi ya TANZANIA?
Muhammed Iqbal Dar ni mtanzania mwenye asili ya India mzaliwa wa mkoani Tanga mwaka 1944, dini yake ni Muislamu dhehebu la Ahmadiya, baba yake aitwaye Dokta Tufail Ahmad Dar alikuwa ni daktari wa binadamu aliyehamia Tanzania kutoka India mwaka 1930 na walikuwa wakiishi mkoani Morogoro.
Mwandishi wa kituo cha Redio Safari ya mkoani Mtwara aitwae Alphonce Tonny Kapelah aliwahi kumhoji Muhammed ana kwa ana na ndipo Muhammed alianza kuhadithia jinsi alivyoweza kubuni jina TANZANIA k**a ifuatavyo;
Mnamo mwaka 1964 Tanganyika na Zanzibar zilipoungana serikali waliita muungano huo jina la "Republic of Tanganyika & Zanzibar" jina ambalo lilikuwa refu sana hivyo serikali ikatoa tangazo kwa raia kutoa mapendekezo ya majina ili kupata jina moja zuri litakalobeba maana ya Tanganyika na Zanzibar kwa pamoja na atakaeshinda atapewa zawadi ya Tsh 200, Mohammed anasema siku moja alikuwa maktaba akisoma gazeti la Tanganyika Standard ambalo kwa sasa linaitwa Daily News akaona tangazo hilo ndipo akaamua ashiriki shindano hilo, akachukua karatasi kisha akaandika maneno BISMILLAH RAHMAN RAHIM kisha akaandika TANGANYIKA kisha akaandika ZANZIBAR alafu akaandika jina lake IQBAL kisha akaandika dhehebu la dini yake AHMADIYA kisha akaomba Mungu amjaalie apate jina zuri litakalofaa, baada ya hapo akaandika herufi tatu za mwanzo kwenye neno TANGANYIKA akaunganisha na herufi tatu nyingine za mwanzo kutoka kwenye neno ZANZIBAR (TAN+ZAN) akapata neno TANZAN lakini akaona hili neno bado halijakamilika kuitwa muungano huo, akaweka herufi moja ya mwanzo kutoka kwenye jina lake IQBAL (TAN+ZAN+I) kisha akaongeza na herufi moja ya mwanzo ya neno AHMADIYA (TAN+ZAN+I+A) akapata neno TANZANIA kisha akahisi huenda hili likawa jina sahihi akaamua kufanya utafiti akagundua nchi nyingi za Afrika majina yake yanaishia na herufi IA nchi k**a ETHIOPIA, ZAMBIA, NIGERIA, TUNISIA, SOMALIA, GAMBIA, NAMIBIA, LIBERIA, MAURITANIA ndipo akaona hili ndio jina sahihi.
Baada ya hapo akatuma jina hilo kwa k**ati ya kuratibu shindano hilo kisha alikaa miezi kadhaa baadae akapokea barua iliyoeleza kuwa ameshinda shindano hilo na aende ili apewe zawadi yake kisha akapewa pongezi, Muhammed alienda lakini kuna mtu mwingne aitwae Yusufal Pir Mohammed na yeye pia alienda akidai yeye ndie aliyeshinda lakini alipoambiwa aonyeshe barua ya uthibitisho na pongezi k**a ya Muhammed hakuwa nayo hivyo Muhammed alipewa cheki yake ya Tsh 200 na zawadi ya ngao, Muhammed pia alisema kwamba washiriki walioshiriki shindano hilo walikuwa 16 lakini alishinda yeye.
Kwa wakati huo ambao Muhammed alikuwa anahojiwa na Alphonce Muhammed alikuwa anaishi nchini Uingereza mjini Birmingham.
Ahsante

Address


Telephone

+255768612251

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Jua na Junior posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Jua na Junior:

Shortcuts

  • Address
  • Telephone
  • Alerts
  • Contact The Business
  • Claim ownership or report listing
  • Want your business to be the top-listed Media Company?

Share