Sufian Mzimbiri

Sufian Mzimbiri Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Sufian Mzimbiri, Dar es Salaam.
(3)

🔹️Makala za kidini & kijamii
🔸️Visa & historia & hadithi & riwaya
🔹️Simuliz za kufunza & kugusa nyoyo
🔸️Lengo ni kuielimisha jamii nzima.
🔹️Tunasimulia ili ujifunze & uelimike.

23/07/2025

🌙LEO NI MWEZI 27, MUHARRAM(MFUNGO NNE)-1447H
ALLAH ATUPE KHERI ZITOKANAZO NA SIKU YA LEO 🤲

s.a.w🔥
22/07/2025

s.a.w🔥

22/07/2025

Sema Alhamdulillah, na kumbuka kuwa maisha yako ni bora kuliko ya mamilioni!

Kuagana ni jambo gumu, lakini ni ukweli ambao hauwezi kuepukika. Mauti hayapigi hodi, huja ghafla na huwaacha nyuma mioy...
22/07/2025

Kuagana ni jambo gumu, lakini ni ukweli ambao hauwezi kuepukika. Mauti hayapigi hodi, huja ghafla na huwaacha nyuma mioyo iliyo na maumivu. Basi fanya matendo mema ili sifa yako ibaki njema baada ya kuondoka kwako, wala usiruhusu kifo kikukute huku ukiwa katika hali ya kughafilika.

Wakumbuke wapendwa wako waliotangulia mbele ya haki, kwa kuwa kifo hakichagui kati ya mdogo na mkubwa, wala hakichelewi kinapowadia. Basi jitahidini kwa yale ya baada ya kifo, kwani makaburi hayajazwi kwa kumbukumbu bali kwa matendo mema.

Msimsahau kumswalia Mtume Muhammad (saw)❤️
Allah Atupe Mwisho Mwema, Aamiin

22/07/2025

JE NI SWAHABA NANI AMBAYE MTUME ALIMUAMBIA SWAHABA HUYO KWAMBA ALLAH AMENIAMRISHA NIKUSOMEE QUR'AN?

22/07/2025

Ni Swahaba Nani ambaye Mtume (saw) alimwamuru Swahaba huyo amsomee Mtume(saw) Qur'an?

NABII YA'QUUB KUTAKA KUOAWakati Nabii Ya‘qub alipofikia umri wa kuoa, wazazi wake walimshauri asafiri kwenda ardhi ya Ha...
22/07/2025

NABII YA'QUUB KUTAKA KUOA

Wakati Nabii Ya‘qub alipofikia umri wa kuoa, wazazi wake walimshauri asafiri kwenda ardhi ya Harran iliyoko Iraq, na kumposa mmoja wa mabinti wa mjomba wake Laban. Nabii Yakobo alitii ushauri wa wazazi wake, akaelekea kwa mjomba wake huko Iraq, ambako alimkuta na mabinti wawili:

Lia (aliyekuwa binti mkubwa), na

Raheli (binti mdogo), aliyekuwa mrembo zaidi, msafi, na mwerevu kuliko dada yake.

Yaaqub alimuomba Raheli amuoe kwani alimpenda sana. Lakini baba yake Raheli alimwambia kuwa lazima amfanyie kazi kwa kipindi cha miaka saba k**a mahari ya binti yake. Nabii Yaaquub alikubali, na akafanya kazi kwa bidii kwa miaka saba mfululizo.

Lakini ilipofika siku ya harusi, mjomba wake alimwozesha Yaaqub binti mkubwa (Lia) badala ya Raheli.

Asubuhi ya siku iliyofuata, Yaaqub alikwenda kwa hasira kwa mjomba wake na kumkumbusha kuwa alikuwa amemuomba Raheli, si Lia. Mjomba wake akamweleza kuwa desturi ya nchi hiyo hairuhusu binti mdogo kuolewa kabla ya mkubwa.

Nabii Yaaquub hakuwa na budi ila kukubali pendekezo la kufanya kazi tena kwa miaka saba mingine ili apewe Raheli. Na alikubali.

Kumbuka: Katika wakati huo haikuwa haramu kuoa dada wawili kwa wakati mmoja, k**a ilivyokuja kuwa haramu baada ya kuja kwa Uislamu. Baadhi ya wafasiri wa Qur’an wanasema kwamba huenda Yaaqub alimuoa Raheli baada ya kifo cha Lia.

Katika kipindi hicho cha miaka saba, Lia alimzalia Yaaqub watoto kadhaa, lakini Yaaquub aliendelea kumtamani Raheli aliyekuwa akimpenda kwa dhati, mpaka alipomwoa pia.

Mjomba wake, Laban, aliwapa kila binti wake kijakazi:

Lia alipewa kijakazi aitwaye Zilfa,

Raheli alipewa kijakazi aitwaye Bilha.

Baada ya Raheli kuona kuwa dada yake Lia alikuwa ameshamzalia Yaaquub watoto wanne naye hakuwa na mtoto, alimpa Yaaqub kijakazi wake Bilha, ambaye alimzalia watoto.

Lia naye, kwa kuona hilo, alifanya k**a Raheli, akampa Yaaqub kijakazi wake Zilfa, naye akazaa.

Raheli, licha ya kuwa mpendwa zaidi kwa Nabii Ya‘qub, alihisi huzuni kwa kukosa mtoto kwa muda mrefu. Akaamua kujielekeza kwa mwenyezi Mungu kwa unyenyekevu, maombi na machozi, akimwomba amruzuku mtoto mwema.

Allah, Mwingi wa Rehema, akamjibu dua yake. Baada ya muda, Raheli akapata ujauzito, na akamzaa mtoto wa kiume aliyeitwa:

Yusuf (a.s) mtoto mcha Mungu, mrembo kwa sura na tabia, na baadaye akawa miongoni mwa Manabii wakubwa wa Bani Israil.

Huu ulikuwa ni ujira mkubwa kwa subira na maombi ya Raheli.

Baada ya Yusuf:

Baadaye Raheli alipata mtoto mwingine aitwaye Binyamin Lakini wakati wa kujifungua kwake Bin'yamin Raheli alipata matatizo na akafariki dunia.

Hili lilimvunja moyo sana Nabii Ya‘qub, kwani alimpenda sana Raheli kuliko wake wengine.

Mtoto wa Upendo:
Yusuf na Bin'yamiin walikua wakiwa ni watoto waliopendwa sana na baba yao Yaaqub, hasa Yusuf kutokana na tabia yake njema, heshima, na maono aliyopewa na Allah tangu akiwa mdogo.

Lakini upendo huu ulisababisha wivu mkubwa kwa kaka zake Yusuf waliotokana na wake wengine, hasa kutoka kwa watoto wa Lia na watoto wa mjakazi wake.

Wivu huo ndio ulipelekea kisa mashuhuri cha Yusuf kutupwa kisimani, ambacho kimeelezewa kwa kina katika Surat Yusuf (Surah ya 12) ya Qur’an Tukufu.

Hitimisho: Hekima kubwa katika hadithi hii ni kwamba:

Subira na dua huzaa matunda.

Upendo wa kweli hujaribiwa na wakati.

Na kwamba mipango ya Mwenyezi Mungu daima ni bora hata k**a mwanzo wake unaonekana kuwa mgumu

Sufian Mzimbiri .

KWANINI INAKUWA HIVI?Mume akiwa mkorofi, mkali na mwenye tabia mbaya: mke huambiwa avumilie (asubiri) na hukumbushwa kuh...
22/07/2025

KWANINI INAKUWA HIVI?

Mume akiwa mkorofi, mkali na mwenye tabia mbaya: mke huambiwa avumilie (asubiri) na hukumbushwa kuhusu wajibu wa mke mwema katika Uislamu.

Lakini mke akiwa mkorofi na mwenye hasira: mume huambiwa atafute mke mwenye dini zaidi, na mke huyo huambiwa kuwa wanawake hawafai kuwa na tabia hizo, na huanza kusemwa vibaya kuhusu tabia yake.

Imepokewa kuwa mwanamume mmoja alikuja kwa Sayyidina Umar ibn Al-Khattab (Radhiya Allahu ‘Anhu) ili amlalamikie Umar kuhusu mke wake kwa kuwa na hasira na kumlalamikia sana. Na mume huyo alipokuwa akisubiri nje ya nyumba ya ‘Umar, alisikia mke wa ‘Umar akimkaripia Sayyidna Umar kwa sauti, na ‘Umar alikuwa akimsikiliza kimya kimya bila kumjibu.

Yule mwanaume akageuka na kuanza kuondoka kurudi alikotoka huku akijinong’oneza: “K**a hali iko hivi kwa ‘Umar, kiongozi wa Waumini, anayejulikana kwa uadilifu na ukak**avu wake, basi mimi masikini nifanyeje?”

Wakati huo ‘Umar akatoka nje ya nyumba yake na kumwona mwanaume huyo akiondoka. Akamwita na kusema:
“Ewe mtu, ulikuwa unahitaji nini kutoka kwangu?”

Yule mwanaume akajibu:
“Ewe Kiongozi wa Waumini, nilikuja kukulalamikia kuhusu mke wangu mwenye hasira na anayenilalamikia kila mara. Lakini niliposikia mke wako akikufanyia hivyo hivyo, nikageuka na kuondoka nikinong’ona, ‘K**a hali ya Kiongozi wa Waumini iko hivi, basi mimi hali yangu si ya kushangaza.’”

‘Umar akamjibu:
“Ewe ndugu yangu, ninamvumilia kwa sababu ya haki alizonazo juu yangu. Yeye hunipikia chakula, hunichomelea mkate, hunioshea nguo, humnyonyesha mwanangu... na yote haya si wajibu wake. Tena ni faraja kwa moyo wangu na hunilinda na mambo haramu. Hivyo basi, namvumilia.”

Yule mwanaume akasema:
“Hali yangu ni k**a yako, ewe Kiongozi wa Waumini.”
‘Umar akamwambia:
“Basi ewe ndugu yangu, mvumilie. Hakika maisha haya ni mafupi.”
(Rejea: Adh-Dhahabi, Al-Kabâ'ir uk. 194)

Kwa nini hakuna mtu anayetoa jibu k**a hili leo?

Mpende mke wako, Mvumilie mke wako, mheshimu mke wako, kila mmoja anamapungufu yake hakuna aliye kamilika hata wewe mwanaume huyo mke wako anakuvumilia kwa mengi ni vile hakuambii

Allah atupe awape uvumilivu wanandoa wote, aamiin

Sufian Mzimbiri

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara linamshikilia Jumanne Kibagi, mkazi wa kijiji cha Nyarufu wilayani Bunda, kwa tuhuma za kum...
22/07/2025

Jeshi la Polisi Mkoa wa Mara linamshikilia Jumanne Kibagi, mkazi wa kijiji cha Nyarufu wilayani Bunda, kwa tuhuma za kumuua mama mkwe wake na kumjeruhi mke wake kwa kutumia panga.

Tukio hilo limetokea Julai 19, 2025 katika kijiji cha Chumwi kilichopo wilayani Musoma, ambapo chanzo kimetajwa kuwa ni mgogoro wa kifamilia kati ya mtuhumiwa na mke wake.

Mke wa mtuhumiwa, Nyangeta, akizungumza akiwa katika Hospitali ya Kumbukumbu ya Mwalimu Nyerere alikolazwa kwa ajili ya kupatiwa matibabu ameeleza kuwa mtuhumiwa alifika nyumbani kwao usiku na kutekeleza tukio hilo.

Amesema Jumanne alikuwa mume wake ambaye waliishi pamoja kwa muda wa mwaka mmoja, na waliachana baada ya kugundua mwanaume huyo anajihusisha na matukio ya kihalifu.

Nyangeta amesema kabla ya tukio hilo, Jumanne alimpigia simu mama yake akimjulisha nia ya kwenda kumchukua mke wake (Nyangeta), ambapo mama yake alikataa, na ndipo siku ya tukio alipovamia na kuwakata panga yeye na mama yake.

K**anda wa Polisi wa Mkoa wa Mara, Pius Lutumo amethibitisha kutokea kwa tukio hilo na kusema kuwa Jeshi la Polisi linamshikilia mtuhumiwa huyo kwa uchunguzi zaidi.

C&P

22/07/2025

TUMEFUNGA ZOEZI LA MCHANGO WETU
TUMEKUSANYA 259,875
TUMEFIKIA MALENGO NA KUYAVUKA, ALLAH AWAZIDISHIE WOTE WALIOTOA

Wale mabibi na mabwana mnaonifuata inbox mkihitaji niwaunganishe na wanaotafuta wachumba naweza nikawasaidiaLakini msaad...
22/07/2025

Wale mabibi na mabwana mnaonifuata inbox mkihitaji niwaunganishe na wanaotafuta wachumba naweza nikawasaidia

Lakini msaada wangu ni mama ifuatavyo
Wewe utaandaa Tangazo lako ukiwa umeandika humo ukijielezea wewe uko wapi, ukoje, umri wako, nk na unahitaji mtu wa aina gani, wa wapi na aweje nk

Ukiwa umeambatanisha namba yako ya simu ili anayekidhi vigezo vyako akutafute mhusika moja kwa moja badala ya kunitafuta mimi

Kwahiyo K**a Mtu yuko tayari ataandaa Tangazo lake mimi nitamsaidia kupost humu.

Tunataka watu waoane wapate stara

Matangazo nitatuma mawili ndani ya Wiki moja

Karibuni inbox kwangu K**a mmeelewa,
Hakikisha unakuja WhatsApp na sio Messenger

Wapo wale vijana anaoa mwanamke ambaye umri wake ni mkubwa kuliko Umri wa Mama yake. Baasi vijana k**a hao huwa wanawaud...
22/07/2025

Wapo wale vijana anaoa mwanamke ambaye umri wake ni mkubwa kuliko Umri wa Mama yake. Baasi vijana k**a hao huwa wanawaudhi sana mama zao ni viletu mama zao hawawaambii na wengine huwaambia kabsa umekosa mabint wa rika lako mpaka ukaoe mwanamke mzima?

Je wewe unaweza kuoa mwanamke ambaye amemzidi mama yako Umri?

Address

Dar Es Salaam

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Sufian Mzimbiri posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Sufian Mzimbiri:

Share