Taarifa ZOTE

Taarifa ZOTE Hapa utapata habari za kila saa.Ila huruhusiwi kutupatia habari za Matusi.

Pia unaruhusiwa kutangaza biashara yako.Anayekiuka masharti ataondolewa kwenye kundi Karibuni sana ila vigezo na Masharti kuzingatiwa.

01/08/2025

Chama Cha Mapinduzi(CCM) kimemteua Mtoto wa Rais wa awamu ya tano Hayati John Pombe Magufuli Magufuli, Jessica Magufuli ( .jmagufuli ) na Wagombea wengine 30 kugombea Ubunge Viti Maalum kupitia kundi la UVCCM

Katibu wa Itikadi, Uenezi na Mafunzo wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Amos Makalla ametangaza majina hayo leo July 29,2025.

01/08/2025
01/08/2025

: Tume ya Huru ya Taifa ya Uchaguzi (INEC) imesema hakuna sheria inayoruhusu kura za mapema kupigwa kwa upande wa Tanzania bara katika uchaguzi mkuu utakaofanyika Oktoba 29 mwaka huu.

Kura hiyo ni ile ambayo itapigwa Zanzibar na baadhi ya watu, ambazo siku ya uchaguzi watakuwa na majukumu ya kusimamia uchaguzi mkuu huo.

Kauli hiyo meelezwa na Mwenyekiti wa INEC Jaji Mstaafu wa Mahak**a ya Rufaa Jackobs Mwambegele, wakati akizungumza na Wahariri wa vyombo vya Habari Jijini Dar es Salaam.

Amesema Zanzibar ilipitisha sheria ya kuruhusu upigwaji huo wa kura.

Mbali ya Hilo Jaji Mwambegele amesema raia wa Tanzania wanaoishi nje ya nchi hawataweza kupigakura kutokana na sheria kutaka zoezi kufanyika hapahapa nchini.

Tume huru ya taifa ya uchaguzi (INEC) inaendelea kukutana na makundi mbalimbali kuelezea maandalizi ya uchaguzi mkuu yalipofikia.


01/08/2025

Jeshi la Polisi Mkoani Mtwara limesema limemk**ata Anastanzia Exavery Mahatane (27), maarufu Ebitoke katika fukwe za Msanga Mkuu Mjini Mtwara akiwa katika hali inayoonekana kuwa amechanganyikiwa na wala hakuwa ametumbukizwa katika shimo wala kutekwa k**a ambavyo alivyokuwa ameeleza mitandaoni ambapo Polisi hao wamempeleka Ebitoke Hospitali ya Mkoa Mtwara kwa matibabu na limeomba Ndugu zake wafike Mtwara kumchukua.

Akiongea leo August 01,2025, Kamanda wa Polisi Mtwara Issa Suleiman amesema ““Mnamo July 30, 2025 Anastanzia Exavery Mahatane (27), maarufu Ebitoke ambaye ni Msanii wa comedy hapa Tanzania, Mkazi wa Dar es salaam, ambaye kwa sasa anaishi katika Kata na Kijiji cha Msanga Mkuu Wilaya ya Mtwara alichapisha taarifa katika akaunti zake za mitandao ya kijamii ikiwemo Instagram kuwa yeye kwa sasa yupo Mtwara na kwamba ametumbukizwa katika shimo huko katika fukwe za Msanga Mkuu na kwamba wapo Watu ambao aliwataja kwa majina kuwa wanataka kumuua”

“Kwakuwa Jeshi la Polisi jukumu lake la msingi ni kulinda raia na mali zao, Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara lilianza uchunguzi wa haraka sana ilikujua ukweli wa taarifa iliyotolewa na Anastanzia Mahatane, katika uchunguzi wa awali Jeshi la Polisi Mkoa wa Mtwara limebaini kwamba Ebitoke alifika Mtwara tangu
Aprili 2025 na kufikia katika hoteli moja iliyopo Msanga Mkuu na kuomba hifadhi kwa Watu waliokuwa wanafahamiana kabla ya maisha yake kumuendea vibaya huko alikokuwa”

“July 31, 2025 saa 11:00 jioni Jeshi la Polisi Mtwara lilimk**ata Ebitoke huko katika fukwe za Msanga Mkuu akiwa katika hali inayoonekana kuwa amechanganyikiwa na wala hakuwa ametumbukizwa katika shimo wala kutekwa k**a ambavyo alivyokuwa ameeleza katika mitandao hiyo ya kijamii, Ebitoke amefikishwa katika Hospitali ya Mkoa wa Mtwara kwa ajili ya matibabu na Jeshi la Polisi Mtwara linawaomba ndugu na jamaa wa Ebitoke kufika Mkoa wa Mtwara kutoa msaada au kumchukua ndugu yao”

28/06/2025
28/06/2025
11/09/2022

Bondia Mtanzania amesema begi lake ambalo lilipotea Airport, Amsterdam likiwa na viatu vyake na vifaa vingine, limepatikana, itakumbukwa usiku wa Septemba 3, 2022 Mwakinyo katika pambano dhidi ya Muingereza Liam Smith lililochezwa Liverpool, England alipoteza kwa TKO round ya 4 katika pambano la round 12 ambalo hata hivyo lilikuwa gumzo kutokana na jinsi lilivyomalizika kwa utata.

Baada ya pambano hilo Mwakinyo akasema “Hujuma ambayo imetokea juzi wakati nafika Airport Watu wote walipata mabegi Mimi langu sikulipata karibu masaa matatu nimelisubiri baadaye wakaniambia begi langu limesahauliwa Amsterdam kwahiyo nikae pale masaa matano walilete au nitoe anuani ya napokaa watalituma baada ya siku mbili"

"Niliwasiliana na Promota akaniambia njoo uendelee na mambo mengine sisi tutashughulikia masuala ya begi lako, begi halijakuja juzi, jana na leo siku ya pambano wamenipa vifaa vingine vyao, viatu ambavyo nimevaa sijawahi kuvaa kupigania kuna muda nilipiga goti nikamwambia Refa nimepata ankle akaniambia unaweza kuendelea nikasema naweza kuendelea"

"Mara ya pili nikasikia ankle inakuja tena, nikatema mouth guard chini, sheria ukitema mouth guard Refa anatakiwa amrudishe nyuma Boxer unayepigana nae akuulize kuna tatizo gani au akuhesabia nikamwambia nina ankle ak**aliza pambano"

Bondia Mtanzania Mwakinyo amesema kutokana na Refa wa pambano hilo kuwa ‘unfair’ kwake, Promota Benjamin Shalom amekubali pambano hilo lirudiwe January 2023 vs Liam Smith.

11/09/2022

Waziri Mkuu Kassim Majaliwa akiwa ziarani katika Wilaya ya Uyui Mkoani Tabora amekagua ujenzi wa Chuo kipya cha Ufundi Stadi VETA ambapo ameonesha kutoridhishwa na gharama za ujenzi wa kibanda cha mlinzi ambacho gharama za ujenzi wake zimetajwa kuwa ni Tsh. Milioni 11.

Waziri Mkuu ameiagiza TAKUKURU Mkoa wa Tabora kuingilia kati na kuchunguza gharama za ujenzi wa kibanda hicho.

11/09/2022

Mahak**a ya Hakimu Mkazi Kiteto Mkoani Manyara imemuhukumu kifungo cha miaka 30 Jela, Yerenia Chidaka, Mkazi wa Kijiji cha Dongo Wilayani Kiteto, baada ya kufanya ngono na kumtia mimba Mtoto wake wa miaka 16.

Mtuhumiwa amekiri kosa hilo mbele ya Hakimu Mkazi Mosi Sasy, na kusema hataki kuisumbua Mahak**a na kusema aliamua kumpa mimba Mtoto wake huyo ili asiolewe na Mwanaume wa Kabila la Wakamba.

Imeelezwa kuwa Baba huyo alipomuuliza Mke wake juu ya suala la kutotaka Mtoto wao aolewe na Wakamba, Mkewe alimjibu kwa dhihaka kwamba k**a hataki aolewe basi amuoe yeye na ndipo alipoamua kumpa ujauzito.

Alipotakiwa kujitetea, Mtuhumiwa aliiomba Mahak**a impunguzie adhabu kwakuwa shetani alimpitia kutenda kosa hilo, huku Mwendesha Mashtaka wa Polisi Mahak**ani hapo Inspekta Wilfred Mollel, akisema Jeshi la Polisi halina taarifa k**a Mtuhumiwa aliwahi kufanya kosa zaidi ya hilo na kumwomba Hakimu kumpa adhabu inayostahiki.

11/09/2022

Malkia wa Uingereza Elizabeth II amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 96, Kasiri la Buckingham limethibitisha kifo chake na kusema amefariki akiwa chini ya uangalizi wa matibabu huko Balmoral baada ya Madaktari kuwa na wasiwasi juu ya afya yake.

11/09/2022

Mwanafunzi wa Chuo Kikuu cha St. John Dodoma, Winfrida Michael (24), aliyekuwa anasoma Diploma ya Medical Laboratory amefariki dunia baada ya kushambuliwa kwa kuchomwa kisu na Mpenzi wake, Julius Gervas (26), RPC Dodoma Martin Otieno amethibitisha .

Winfrida alifariki wakati anapelekwa Hospitali baada ya kuwa amevuja damu nyingi na Julius baada ya kufanya tukio hilo alijaribu kujichoma kisu tumboni lakini Watu walimuwahi na kumchukua kisha kumpeleka Hospitalini ambako anaendelea na matibabu chini ya ulinzi.

Inaelezwa kuwa Winfrida alikuwa amepanga nje ya Chuo na alikuwa na mahusiano na Kijana huyo kwa muda fulani lakini walikuwa wameachana na Kijana alikuwa anamsumbua Msichama hivyo alimuahidi kuwa akimaliza mtihani atamjulisha.

Juzi Msichana alikuwa amemaliza mtihani wake wa mwisho na kwa mujibu wa Mama mwenye nyumba walikutana wakaongea sana pale ndani na ilipofika saa nne na nusu walitoka nje akawa anamsindikiza ndio lilipotokea tukio la kuchomwa kisu na akawa anaomba msaada na walimchukua na kumpeleka Hospitali lakini akawa amefariki, mwili wa Marehemu umeagwa na kusafirishwa kwenda Ukerewe kwa mazishi.

11/09/2022

Address

Usa River

Telephone

+255752243648

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Taarifa ZOTE posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share