ASAM MEDIA

ASAM MEDIA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ASAM MEDIA, Media/News Company, Zanzibar City.

24/07/2025

Tabia ya baadhi ya vijana kujisaidia haja ndogo kwenye chupa na kuzitupa ovyo mitaani imeibua hasira kwa wakazi wa mtaa wa Mpendae, Zanzibar.

Asam Online TV imeshuhudia mazingira hayo duni na kuzungumza na wananchi wakiwemo kina mama wa mtaa huo, wakiongozwa na Binti Amrani, ambao wamesema hali hiyo si tu ni uchafuzi wa mazingira bali pia ni tishio kwa afya ya jamii.

24/07/2025

🔥 GHALA LATEKETEA KWA MOTO MKUBWA – MNZI MMOJA, ZANZIBAR 🔥
Hasara kubwa imeripotiwa kufuatia moto uliolipuka ghafla katika Mtaa wa Kibokoni, Shehia ya Mnazi Mmoja, na kuteketeza ghala lililokuwa likihifadhi rangi.

🗣 Mmiliki wa ghala hilo amesema bado hajafahamu chanzo cha moto huo, huku akieleza maumivu makubwa ya kiuchumi aliyoyapata. Ametoa shukrani kwa Kikosi cha Zimamoto kwa juhudi zao za haraka kuuzima moto kabla haujasambaa zaidi.

🚒 Jeshi la Zimamoto linaendelea na uchunguzi wa kiini cha tukio hilo, na limehimiza umuhimu wa vifaa vya kuzimia moto kwa maeneo yote ya biashara.

🎥 Tazama tukio hili kwa undani kupitia Asam Online TV:
👉 https://youtu.be/t9ooalG2w5o

⚠️ Tahadhari: Usalama wa moto ni jukumu la kila mmoja. Chukua hatua mapema!

24/07/2025

Katika jitihada za kuendeleza haiba ya kihistoria na kuvutia watalii, Mamlaka ya Uhifadhi na Uendeshaji wa Mji Mkongwe imeanzisha kampeni kabambe ya kuhamasisha usafi na nidhamu ya mazingira kwa wakazi wa eneo hilo maarufu duniani.

#2025

19/07/2025

Mamlaka ya Uhifadhi na Uendeshaji Mji Mkongwe imewataka wananchi na watumiaji wa mitandao ya kijamii kufuata sheria na kanuni zilizowekwa katika kulinda hadhi, haiba na vivutio vya kihistoria vilivyopo ndani ya Mji Mkongwe wa Zanzibar, kwa maslahi ya taifa na vizazi vijavyo.

#2025

18/07/2025

Kwa jamii ya Hadzabe, wawindaji na wakusanyaji wa asili wanaoishi pembezoni mwa Ziwa Eyasi, kifo hakionekani k**a mwisho wa maisha bali ni mwanzo wa safari ya roho kuelekea kwa mababu.

#2025

18/07/2025

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea na juhudi kubwa za kuboresha miundombinu ya nchi, ikiwa ni sehemu ya ajenda yake ya kuimarisha huduma za kijamii na kuleta ustawi wa kiuchumi kwa wananchi. Miongoni mwa miradi mikubwa inayotekelezwa kwa sasa ni ujenzi wa daraja la juu (flyover) katika eneo la Amani, mradi wa kimkakati unaolenga kupunguza msongamano mkubwa wa magari katika makutano hayo muhimu ya barabara.

17/07/2025

Makunduchi si tu jina la mji bali ni moyo wa utamaduni wa Kizanzibari, eneo lenye historia ya kipekee, utajiri wa mila na desturi, na misingi imara ya maisha ya kijamii. Wakazi wa kijiji hiki wameendelea kuenzi urithi wao kwa vizazi, wakiheshimu utamaduni wa kuwasiliana na mizimu kwa ajili ya kutafuta msaada wa kimazingira, kiafya, au kijamii.

17/07/2025

Katika kuendeleza na kuenzi mila na desturi za Wamakunduchi, watoto wameonekana kushiriki kikamilifu katika sherehe za Mwaka Kogwa mwaka huu, wakifurahia michezo, mavazi ya kitamaduni na nyimbo za asili, huku wakijifunza historia ya jamii yao.

17/07/2025

Mwaka Kogwa ni mojawapo ya sherehe maarufu na za kipekee zinazofanyika kila mwaka katika kijiji cha Makunduchi, kusini mwa kisiwa cha Unguja, Zanzibar. Sherehe hizi hufanyika mwanzoni mwa mwezi wa Julai, Asili ya sherehe hii inahusishwa moja kwa moja na tamaduni za Wamakunduchi wa asili ya Kiajemi waliowahi kuhamia Zanzibar karne nyingi zilizopita.

#2025

16/07/2025

Watuhumiwa sita wa kesi ya mauaji ya Sheikh Jabir Haidar Jabir wataendelea kubaki rumande baada ya kesi yao kuahirishwa tena leo, Julai 16, 2025, katika Mahak**a Kuu ya Zanzibar iliyopo Tunguu, mbele ya Jaji Khadija Shamte Mzee. Kesi hiyo ilipangwa kutajwa lakini imeahirishwa kutokana na kutokamilika kwa upelelezi.

#2025

16/07/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Mheshimiwa Dkt. Hussein Ali Mwinyi, amezindua rasmi Jengo jipya na la kisasa la Afisi Kuu ya Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC) lililopo Maisara, Mkoa wa Mjini Magharibi. Uzinduzi huo ni sehemu ya juhudi za Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kuimarisha mazingira bora ya utendaji wa taasisi hiyo muhimu kwa kuendeleza demokrasia nchini.

#2025

16/07/2025

Leo tunazungumzia neno linalopenya kila kona ya muziki "MELODY".
Unalisikia kwenye nyimbo, linatajwa kwenye mitandao, wasanii wanalitamka kwa mbwembwe, lakini je, unafahamu kweli maana yake?

Address

Zanzibar City

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ASAM MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share