
22/05/2024
KAMATI ya maandalizi ya siku ya uhuru wa habari duniani Zanzibar, imeeleza kuwa maadhimisho ya siku ya uhuru wa habari duniani yanategemewa kufanyika Mei 23, mwaka huu.
Taarifa iliyotolewa kwa niaba ya kamati ya maandalizi ya maadhimisho hayo inayoundwa na Baraza la habari Tanzania (MCT ) Ofisi ya Zanzibar , Chama cha Waandishi wa Habari Tanzania Zanzibar (TAMWA - ZNZ), Jumuiya ya Waandishi wa Habari za Maendeleo (WAHAMAZA) na Klabu ya Waandishi wa Wabari Zanzibar (ZPC), Makamu Mwenyekiti wa kamati hiyo, Dk. Mzuri Issa, alisema maadhimisho hayo yatafanyika ukumbi wa ZSSF Kariakoo Zanzibar.