Dhahabu Online TV

Dhahabu Online TV MAISHA SIRI

16/11/2025
09/10/2025

Gari iliyokuwa ikiongoza msafara wa Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto na Uokozi Zanzibar imepata ajali eneo la Kijichame Pemba kufuatia kugongana na Roli la Mchanga na kupekea kifo cha Askari Mmoja wa Zimamoto.

Akithibitisha tukio hilo Mkuu wa Kikosi cha Zimamoto Zanzibar Kanal Rashid Mzee Abdalla amesema msafara huo ulikuwa unalenga kutembelea maeneo ya vituo vya kikosi hicho ,hivyo katika ajali hiyo kikosi kimepata pigo kubwa la kupoteza askari wake mmoja (1) na majeruhi 6.

06/10/2025

Mgombea wa Urais wa Zanzibar kupitia Chama Cha Mapinduzi (CCM), Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema atahakikisha wanaendeleza ujenzi wa Skuli katika maeneo mbali mbali ya Unguja na Pemba ili kuhakikisha wanafunzi wasoma mkondo Mmoja jambo ambalo litasaidia kupata wakati mzuri wa kusoma elimu yao ya Dini

Dkt Mwinyi ameyaaleza hayo wakati akizungumza na viongozi wa dini na madhehebu mbalimbali katika ukumbi wa Utaani, Kaskazini Pemba, ambapo amesema tayari mafanikio hayo yameaaza kupatikana katika Mkoa wa Kusini Unguja kwa wanafunzi kuenda Skuli wakati wa Asubuhi pekee na jioni kuenda kujifunza katika masuala ya dini.

Akitaja mafanikio ya miaka mitano katika sekta ya elimu , Dk. Mwinyi alisema Serikali imetekeleza ujenzi wa madarasa 4,800 katika maeneo mbali mbali , jambo ambalo limevuka utekelezaji wa ilani ya Chama cha Mapindunzi ya mwaka 2020-2025 iliyoelekeza kujenga madarasa 1,500.

Aidha, Dk. Mwinyi amewaomba wananchi kukichagua Chama cha Mapindunzi ili Kuweza kuendeleza mazuri ambayo ikiwemo ujenzi wa Skuli ili kuweza kutimiza malengo ya wanafunzi kusoma mkondo mmoja pekee.

Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Kusini Unguja ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini U  ameshiriki katika mkutano wa Mkom...
03/10/2025

Mjumbe wa Kamati ya Siasa Mkoa wa Kusini Unguja ambae pia ni Mkuu wa Mkoa wa Kusini U ameshiriki katika mkutano wa Mkombea wa Chama cha Mapinduzi - CCM Dkt Hussein Ali Mwinyi uliofanyika Bumbwini Wilaya ya Kaskazini B Mkoa wa Kaskazini Ungujaa.

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewataka wananchi kupuuza kauli za baadhi ya viongozi wa...
03/10/2025

Mgombea urais wa Zanzibar kupitia CCM, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amewataka wananchi kupuuza kauli za baadhi ya viongozi wa vyama vya siasa wanaopinga kura ya mapema, akisisitiza kuwa ni utaratibu wa kisheria.

Akizungumza leo Oktoba 2 katika mkutano wa kampeni uliofanyika Uwanja wa Bubwini, Mkoa wa Kaskazini Unguja, Dk. Mwinyi amesema kura ya mapema ipo kwa mujibu wa Sheria ya Uchaguzi Zanzibar Namba 4 ya mwaka 2018, ambayo inawaelekeza wasimamizi wa uchaguzi kupiga kura siku moja kabla ya uchaguzi mkuu.

Amesisitiza kuwa wananchi waendelee kuhubiri amani kabla, wakati na baada ya uchaguzi mkuu ili taifa liendelee kudumu katika mshikamano na utulivu.

ALIYEKUA KIONGOZI WA ACT-WAZALENDO AELEZA MAALIM SEIF ALIVYOMUAMINI DKT MWINYI.Aliyekua Naibu Waziri Kivuli Utumishi wa ...
02/10/2025

ALIYEKUA KIONGOZI WA ACT-WAZALENDO AELEZA MAALIM SEIF ALIVYOMUAMINI DKT MWINYI.

Aliyekua Naibu Waziri Kivuli Utumishi wa Umma baraza kivuli la ACT-Wazalendo Halima Abbas ambae amehamia Chama cha Mapinduzi CCM amesema Marehemu Maalim Seif amekua akitoa kauli wakati wa uhai wake akionyesha kuwa na matumaini makubwa na Dkt Hussein Ali Mwinyi katika uongozi wake.

Halima ambae alitimikia chama cha Mapinduzi Miezi kadhaa iliyopita amepewa nafasi ya kuzungumza jukwaani wakati wa kampeni za Chama cha Mapinduzi CCM za kumnadi Mgombea wa nafasi ya Urais wa Zanzibar huko Bumwbini Mkoa wa Kaskazini Unguja

Amesema kauli za Marhemu Maalim Seif ziliashiria kumuunga mkono baada ya maono yake na matendo yake aliyoyafanya ya kuleta umoja na kuwaletea maendeleo wananchi wa Zanzibar

Amesema kazi kubwa iliyofanywa na Dkt Hussein Ali Mwinyi ni kielelezo kikubwa cha wananchi kuendelea kumuamini na kumpa ridhaa ya kuongeza tena Zanzibar katika uchaguzi mkuu wa Oktoba 2025

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hamida M***a Khamis  amefanya uzinduzi wa Madrasat Diin Islamiya  Kijundu Wilaya ya K...
26/09/2025

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hamida M***a Khamis amefanya uzinduzi wa Madrasat Diin Islamiya Kijundu Wilaya ya Kati iliyojengwa kwa ufadhili wa Nuru Yakin na Firdaus help foundation ya Uholanzi

Address

Fuoni Mambosasa
Zanzibar City

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dhahabu Online TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share