Dhahabu Online TV

Dhahabu Online TV MAISHA SIRI

Viongozi wa dini nchini wametakiwa kuendelea kuiombea nchi amani na mshik**ano hasa katika  kipindi hiki cha kuelekea uc...
14/09/2025

Viongozi wa dini nchini wametakiwa kuendelea kuiombea nchi amani na mshik**ano hasa katika kipindi hiki cha kuelekea uchaguzi Mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Oktoba mwaka huu.

Wito huo umetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Hamida M***a Khamis huko katika kanisa la Penticost Celebration Feroship Kidimni katika ibada maalum ya kuwaombea duwa Viongozi wakuu na Taifa kwa ujumla

Amesema jukumu la kuhakikisha nchi inabaki kuwa na utulivu ni la kila mwananchi, hivyo waumini wana wajibu wa kipekee kuendelea kuiombea nchi na viongozi wake walioko madarakani ili waweze kuendelea kuliongoza Taifa.

Ameelezakuwa Kila muumini anapaswa kuonyesha mfano wa upendo na kuvumiliana hata wanapokuwa na mitizamo tofauti ya kidini, kabila au siasa kwani Tanzania ni yetu sote hivyo tunawajibu wa kuhakikisha nchi inaendelea kubaki salama.

Akisalimia waumini wa kanisa hilo Mkuu wa Wilaya ya Kati Rajab Ali Rajab amewahimiza waumini kushiriki uchaguzi kwa amaniI na kutokubali kutumiwa k**a chombo cha kuchochea vurugu hususani katika kipindi cha Uchaguzi

Amesema jukumu la kuhakikisha nchi inabaki kuwa na utulivu ni la kila raia hivyo endapo atatokea mchungaji au waumini anahubiri maneno ya kuvunja amani basi waumini hawapaswi kumuunga Mkonoi

Awali akiongoza ibada ya sala Mwenyekiti wa Wachungaji Mkoa wa Kusini Unguja Bwana Edward Jackson Lenjima amesema atahakikisha waumini wao kutumia kipindi hiki kusimama katika maombi kwa kumuomba Mungu aendelee kuwalinda viongozi wakuu na nchi dhidi ya vurugu, migawanyiko na chuki za kisiasa.

Mjumbe wa Kamati ya siasa Mkoa  wa Kusini ā€˜u’ ambae pia ni Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Hamida M***a Khamis ameshiriki katika u...
13/09/2025

Mjumbe wa Kamati ya siasa Mkoa wa Kusini ā€˜u’ ambae pia ni Mkuu wa Mkoa huo Mhe. Hamida M***a Khamis ameshiriki katika ufunguzi wa kampeni za Chama cha Mapindunzi - CCM Zanzibar katika viwanja vya Mnazi mmoja

Tarehe 11.09.2025 Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Hamida M***a Khamis ameshiriki katika  hafla ya kuwaaga walimu wakuu...
12/09/2025

Tarehe 11.09.2025 Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Hamida M***a Khamis ameshiriki katika hafla ya kuwaaga walimu wakuu wastaafu wa Skuli ya Ukongoroni Bw. Hassan Haji Suleiman aliyekuwa Mwalimu Mkuu Sekondari na Bwana Mshimba Seif ali aliyekuwa Mwalimu Mkuu Msingi ambao wamemaliza utumishi wao rasmi baada ya kulitumikia taifa kwa zaidi ya miaka 30.

Tarehe  11 .09.2025 Mkuu wa Mkoa wa  wa Kusini Unguja Mhe. Hamida M***a Khamis ameshiriki katika Kongamano la Umoja  wa ...
12/09/2025

Tarehe 11 .09.2025 Mkuu wa Mkoa wa wa Kusini Unguja Mhe. Hamida M***a Khamis ameshiriki katika Kongamano la Umoja wa wanawake wa Kikristo na maendeleo Zanzibar hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Dkt Shein Tunguu Zanzibar.

Mgeni rasmi katika hafla hiyo ni Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dkt Hussein Ali Mwiny

06/09/2025
03/09/2025

Mgombea Urais wa Zanzibar kupitia Chama cha AAFP Said Soud amesema kuwa chama chake kitakua cha kwanza kuridhia matokeo ya uchaguzi ya urais wa Zanzibar ya mgombea wa CCM Dk Hussein Ali Mwinyi.

Ameyasema hayo leo Septemba 3,2025 wakati akizungumza na waandishi wa habari katika Ofisi za Chama hicho Mwera nje ya mji wa Zanzibar.

Amesema vyama vya upinzani bila ya kuungana haitowezekana kukiondoa chama cha Mapinduzi madarakani kutokana na sera za chama hicho.

Amesema kuwa AAFP nayo inategemea nafasi ya umakamu wa kwanza wa Rais katika serikali na sio nafasi ya urais ambapo mgombea pekee anaweza kushinda ni Dk Hussein Ali Mwinyi.

Amesema akiingia katika serikali ya umoja wa kitaifa akiwa makamu wa kwanza atamshauri Rais Dk Mwinyi kuhalalisha kilimo cha bangi.

Baraza la Manispaa ya Wilaya ya  Kati imezindua rasmi Kampeni ya upandaji wa miti ya kivuli, matunda na bustani yenye le...
03/09/2025

Baraza la Manispaa ya Wilaya ya Kati imezindua rasmi Kampeni ya upandaji wa miti ya kivuli, matunda na bustani yenye lengo la kutunza mazingira na kukabiliana na mabadiliko ya tabianchi.

Akizundua kampeni hiyo huko Tunguu mbele ya Makamo Makuu ya Polisi iliyowashirikisha viongozi wa Serikali ya Mkoa, Wilaya, wafanyakazi na makundi ya hamasa Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe Hamida M***a Khamis amesema kampeni hiyo iliyopewa jina la Safisha, pendezesha wilaya ya kati ina lenga kupanda miti elfu tatu ikiwa ni sehemu ya juhudi ya Serikali ya kuhakikisha mazingira yanabaki salama na kuleta mabadiliko katika maeneo mbalimbali ya Wilaya hiyo.

Ameeleza kuwa viongozi wa manispaa hiyo wana wajibu wa kuhakikisha wanaimarisha usafi katika maeneo yote kwa kuweka vifaa vya kutosha vya kuhifadhia taka pembezoni mwa barabara ili kuona mji unakuwa msafi na wenye haiba nzuri sambamba na kuwa mfano wa kuigwa katika suala hilo na uhifadhi wa mazingira.

Kwa upande wake Mkurugenzi Manispaa Wilaya ya Kati Mwanaisha Ali Saidi amesema dhamira ya kuzindua kampeni hiyo ni kuchochea upandaji na kutunza miti ili kuboresha hali ya hewa, kuondosha uchafu na kubainisha kwamba mbali na zoezi hilo pia wataendelea kutoa elimu kwa jamii, maskulini na makundi mbalimbali ya vijana kuhusu umuhimu wa uhifadhi wa mazingira, utunzaji wa miti na mambo mengine ya maendeleo.

Nae Mkuu wa Wilaya ya Kati Rajab Ali Rajab amewataka wananchi kuendelea kushiriki katika masuala mbalimbali ya kitaifa na kimaendeleo na kuhakikisha miti iliyopandwa inatunzwa ili ifikie hatua ya kukomaa kwani miti hiyo imechaguliwa kwa kuzingatia hali ya hewa ya nchi na kutumika kwa matumizi mbalimbali k**a kivuli, urembo na mandhari ya mji.

Kampeni hiyo ya Safisha, pendezesha Wilaya ya Kati ilianzia kwa kufanyika maandamano ya vijana, wafanyakazi kutoka Jumbi Bango la Mkoa hadi Tunguu na ina lengo la kuelimisha jamii kuhusu umuhimu wa kuweka mazingira safi kwa afya, na maendeleo vijijini.

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hamida M***a Khamis amewasihi Wakuu wa Wilaya za Unguja na Pemba kuendeleza Mashiriki...
03/09/2025

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hamida M***a Khamis amewasihi Wakuu wa Wilaya za Unguja na Pemba kuendeleza Mashirikiano ya pamoja kati yao ili kuhakikisha wanatekeleza jukumu la kumsaidia Mhe. Rais katika Wilaya wanazosimamia .

Akizungumza katika kikao cha kuwaaga na kufanya uchaguzi wa Viongozi wa Umoja wa Wakuu wa Wilaya wa Zanzibar kilichofanyika katika Hoteli ya ZanBreeze iliyopo Kikungwi Mkoa wa Kusini Unguja amewashukuru wakuu wa Wilaya kwa kumpa mashirikiano katika kipindi chote alichokuwa Mwenyekiti wa Wakuu wa Wilaya, hivyo amesisitiza kumpa mashirikiano Mwenyekiti mpya na viongozi wengine walio wachagua.

Ameeleza kuwa umoja huo wa Wakuu wa Wilaya umeweza kumsaidia kwa kiasi kikubwa katika kipindi chote cha nafasi yake ya Mkuu wa Wilaya kupitia utaratibu ambao waliojiwekea wa kufanya vikao vya pamoja mara kwa mara kuweza akutathmini utekelezaji wa majukumu yao katika wilaya wanazozisimamia,

Baadhi ya Wakuu wa Wilaya wamemshukuru Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja kwa kipindi chote alichokuwa akiwaongoza katika Umoja wa Wakuu wa Wilaya pamoja na kuwapatia miongozo mbali mbali na ushauri katika utekelezaji wa majukumu yao.

Kwa Upande wake Mkuu wa Wilaya ya Micheweni ambae ndie Mwenyekiti mpya wa Umoja wa Wakuu wa Wilaya za Zanzibar Khatib Juma Mjaja amewashukuru wakuu wa Wilaya kwa kumchagua kushika nafasi hiyo , hivyo amewaomba kushirikiana kwa pamoja ili kuhakikisha wanatekeleza majukumu yao ikiwemo ulinzi na Usalama wa wananchi katika Wilaya Zao hususani katika kipindi hiki cha kuelekea Uchaguzi Mkuu.

Katika kikao hicho cha kumuaga Mwenyejiti wa Wakuu wa Wilaya ayekuwa Mkuu wa Wilaya ya Magharibi B pamoja na kufanya uchaguzi wa mwenyekiti mpya kimemchagua Mkuu wa Wilaya ya Micheweni Khatib Juma Mjaja kuwa Mwenyekiti Mpya , nafasi ya Makamo Mwenyekiti Mkuu wa Wilaya ya Kaskazini B Sururu Juma Sururu pamoja na Mkuu wa Wilya ya Kusini Unguja Othman Ali Maulid kuwa katibu wa Umoja huo.

MWISHO

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hamida M***a Khamis  ameshiriki hafla ya kukabidhi hati ya kupandishwa hadhi kwa  bar...
19/08/2025

Mkuu wa Mkoa wa Kusini Unguja Mhe. Hamida M***a Khamis ameshiriki hafla ya kukabidhi hati ya kupandishwa hadhi kwa baraza la mji kati kua Manispaa na Halmashauri ya wilaya kusini kua Baraza la Mji hafla iliyofanyika katika Ukumbi wa Dkt Shein Tunguu ambapo Mgeni Rasmi katika tukio hilo ni Waziri wa Nchi Ofisi ya Raisi Tawala za Mikoa Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ Mhe. Masoud Ali Mohammed

Address

Fuoni Mambosasa
Zanzibar City

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Dhahabu Online TV posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share