19/09/2020
Benki ya CRDB humu nchini leo imezindua huduma rafiki ya kimtandao ambayo itamuwezesha mteja wake kuweza kufikisha malalamiko na kupata majibu kwa muda mfupi zaidi kuwahi kushuhudiwa.
Akiitambulisha huduma hiyo meneja wa kanda ya mashariki wa benki hiyo nd; Badru Iddi amesema huduma hiyo ya kimtandao ni huduma rafiki kwa mteja na ni njia bora itakayosaidia kutatutua changamoto zitakazojitokeza baina ya mteja na miamala atakayoifanya kwa benki hiyo na ama huduma nyenginezo.
Mapema akizungumza kabla ya kumkaribisha mgeni rasmi meneja biashara wa benki hiyo bw; Gorge Yatera amesema huduma hiyo itafahamika k**a QR CORDE na ni njia rahisi zaidi ya kimawasiliano inayoweza kufanywa na wateja wote wanaotumia simu janja yaani smart phone.
Miongoni mwa wateja wakubwa wa benki hiyo na ambae siku ya leo ametunukiwa na kuwa mgeni rasmi wa shuhuli hiyo nd; Annur Mohammed amesema wao k**a wateja hawana budi kuishukuru benki hiyo kwa kuwafikishia huduma zao kisiwani Pemba, kwani amesema Pemba ni kisiwa kinachokuwa kibiashara kwa mwendo wa taratibu.
Hivyo amesema anaamini huduma iliyozinduliwa itaweza kuwasaidia wafanyabiashara ambao ni wateja wa benki hiyo kufanikisha biashara zao.
Aidha ameitaka benki hiyo kuzidi kutanua wigo na kuboresha huduma zao hasa za miamala ya fedha na mawakala sambamba na ATM kote kisiwani humo.
Hafla ya uzinduzi huo imefanyika mapema asubuhi ya leo huko katika jengo la benki hiyo lililopo Madungu Chake chake kisiwani pemba, huku wafanya biashara na wadau kadhaa wakishuhudia uzinduzi huo wa huduma hiyo mpya ya kibenki.