Zanzibarleo Online

Zanzibarleo Online Pata habari za uhakika na kuaminika kutoka Gazeti namba 1 visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

๐’๐ž๐ซ๐ข๐ค๐š๐ฅ๐ข ๐Š๐ฎ๐ฐ๐ž๐ค๐š ๐Š๐ข๐ฉ๐š๐ฎ๐ฆ๐›๐ž๐ฅ๐ž ๐Š๐ฎ๐ค๐š๐ฆ๐ข๐ฅ๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐•๐ข๐ญ๐ฎ๐จ ๐ฏ๐ฒ๐š ๐€๐Ÿ๐ฒ๐š ๐•๐ข๐ง๐š๐ฏ๐ฒ๐จ๐ฃ๐ž๐ง๐ ๐ฐ๐šSerikali imesema itaendelea kuelekeza fedha katika ku...
11/06/2026

๐’๐ž๐ซ๐ข๐ค๐š๐ฅ๐ข ๐Š๐ฎ๐ฐ๐ž๐ค๐š ๐Š๐ข๐ฉ๐š๐ฎ๐ฆ๐›๐ž๐ฅ๐ž ๐Š๐ฎ๐ค๐š๐ฆ๐ข๐ฅ๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐•๐ข๐ญ๐ฎ๐จ ๐ฏ๐ฒ๐š ๐€๐Ÿ๐ฒ๐š ๐•๐ข๐ง๐š๐ฏ๐ฒ๐จ๐ฃ๐ž๐ง๐ ๐ฐ๐š

Serikali imesema itaendelea kuelekeza fedha katika kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya vituo vya afya 364 vinavyoendelea kujengwa nchini kabla ya kuanza miradi mipya katika kata zinazostahili kupata huduma hizo, ikiwemo Kata za Chawi na Mnima katika Halmashauri ya Mji wa Nanyamba.

Kauli hiyo imetolewa kufuatia swali la Mbunge wa Nanyamba, Abdallah Dadi Chikota, aliyetaka kujua ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya vya Chawi na Mnima ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi wa maeneo hayo.

Akijibu swali hilo Bungeni, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuuโ€“TAMISEMI, Dkt. Japhari Seif, amesema Serikali imeendelea kuwekeza katika sekta ya afya Nanyamba kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 2.7 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/22 hadi 2025/26 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya afya.

Aidha, amesema katika mwaka wa fedha 2026/27, Serikali imetenga shilingi milioni 300 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Nanyamba, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.

Na Saida Issa, Dodoma

Mbunge wa Tunduru Kaskazini na Katibu wa Chama cha ACT Wazalendo, Ado Shaibu, ameishauri Serikali kuendelea kuchukua hat...
11/06/2026

Mbunge wa Tunduru Kaskazini na Katibu wa Chama cha ACT Wazalendo, Ado Shaibu, ameishauri Serikali kuendelea kuchukua hatua zaidi za kudhibiti ongezeko la bei ya mafuta nchini ili kupunguza athari zinazowakabili wananchi kutokana na kupanda kwa gharama za maisha.

Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dodoma, Shaibu amesema Serikali imekuwa ikieleza dhamira yake ya kuhakikisha upatikanaji wa mafuta ya kutosha pamoja na kuweka mazingira yatakayosaidia bei za mafuta kuwa nafuu na himilivu kwa wananchi.

Ameeleza kuwa wananchi wengi bado wanatarajia kuona matokeo makubwa zaidi ya hatua hizo, hasa katika kupunguza gharama zinazotokana na matumizi ya mafuta, jambo ambalo lina mchango mkubwa katika shughuli za kiuchumi na kijamii.

Kutokana na hali hiyo, Shaibu ameomba Serikali kutoa ufafanuzi kuhusu hatua zinazoendelea kuchukuliwa kudhibiti mabadiliko ya bei za mafuta na namna zitakavyosaidia kupunguza athari kwa wananchi pamoja na kuimarisha ustawi wa uchum

โœ๐Ÿฝ Saida Issa, Dodoma

Jesahi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limefanikiwa kuwakamata watu wanne, wanaotuhumiwa kuhusika katika mauaji...
11/06/2026

Jesahi la Polisi Kanda Maalum ya Dar es Salaam, limefanikiwa kuwakamata watu wanne, wanaotuhumiwa kuhusika katika mauaji ya raia wa China, Boazhang Ge, aliyekuwa mmiliki wa kiwanda cha kuchakata makopo cha Xin Lin, kilichopo Mabibo jijini Dar es Salaam.

Kamanda wa kanda hiyo, Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi, Jumanne Muliro, aliwaambia waandishi wa habari jana kwamba watuhumiwa hao walikiri kuhusika na mauaji hayo na kisha kukimbia na shilingi milioni tisa.

Alisema watuhumiwa hao walikamatwa baada ya uchunguzi wa kina uliofanywa kufuatia tukio hilo lililosababisha taharuki miongoni mwa ndugu, jamaa na wafanyakazi wa marehemu.

Alisema watuhumiwa wawili walinaswa Namanga wakiwa wamekimbilia eneo la mpakani huku wengine wawili wakikamatwa Mabibo, jijini Dar es Salaam walikokuwa wakijificha baada ya kutoroka baada ya tukio.

Bhaozang ambaye mwili wake ulichomwa moto Mei 24, 2026 katika eneo maalumu Makumbusho jijini Dar es Salaam na majivu yake kusafirishwa nchini China.

Wananchi wa Zanzibar leo wanatarajiwa kuelekeza macho na masikio yao kwa ajili ya kusikiliza Bajeti Kuu ya Serikali ya M...
11/06/2026

Wananchi wa Zanzibar leo wanatarajiwa kuelekeza macho na masikio yao kwa ajili ya kusikiliza Bajeti Kuu ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kwa mwaka wa fedha 2026/2027 itakayowailishwa katika ukumbi wa Baraza la Wawakilishi.

Bajeti hiyo inatarajiwa kuwasilishwa na Waziri Fedha na Mipango, Dk. Juma Malik Akil, mnamo majira ya 10 za alaasiri.

Dk. Akil atawasilisha bajeti kuu ya serikali kufuatia wajumbe wa Baraza hilo kupitisha makadirio ya matumizi na mapato kwa wizara za sekta zote za serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Wageni mbali mbali wanatajiwa kuhudhuria hafla hiyo ikiwa ni pamoja na viongozi wa serikali, wakiwemo Mawaziri, Makatibu Wakuu wa SMZ, Wakurugenzi, Mabalozi wa wadogo wanaoziwakilisha nchi zao hapa nchini, Jumuiya za Kimataifa, Wanasiasa pamoja na viongozi wa dini.

Tarehe 11 Juni, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝhttps...
11/06/2026

Tarehe 11 Juni, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.

Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ
https://epaper.smsz.co.tz/

| Kwa Ukweli na Uwazi

Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imewataka wakuu wa taasisi kuhakikisha wanawatumia madereva waliopangiwa kuendesha magari h...
10/06/2026

Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imewataka wakuu wa taasisi kuhakikisha wanawatumia madereva waliopangiwa kuendesha magari hayo, na sio wao wawe madereva na kusisitiza kuwa kinyume chake ni ukiukwaji wa taratibu.

Kauli hiyo ilitolewa na Naibu Waziri wa Wizara hiyo, Badria Attai Masoud, alipokuwa akijibu suali la Mwakilishi wa Jimbo la Tumbe, Mmanga Mohammed Hemed, aliyehoji muda na utaratibu wa matumizi ya magari hayo huko katika kikao cha Baraza la Wawakilishi Chukwani nje kidogo ya mji wa Zanzibar.

Naibu huyo alisema kumekuwa na tabia ya baadhi ya viongozi, kuendesha magari hayo jambo ambalo kikanuni za utumishi linakatazwa kwa vile madereva wanaohusika ndio wanaotakiwa kuendesha vyombo hivyo kupitia maofisa wao wausafiri.

Alisema Serikali imeweka miongozo maalumu ya matumizi ya magari ya
Serikali, ili kuhakikisha yanatumika kwa shughuli zilizokusudiwa pekee. Alisema kwa mujibu wa miongozo hiyo, magari ya Serikali yanapaswa kutumika katika saa za kazi, isipokuwa pale panapokuwa na kibali maalumu kwa kazi za dharura au majukumu ya nje ya muda wa kawaida wa kazi.

Alifafanua kuwa baada ya muda wa kazi, magari hayo yanapaswa kuegeshwa katika ofisi za Serikali au maeneo yaliyoidhinishwa.

Hata hivyo, alisema katika mazingira maalumu na kwa idhini ya viongozi husika, magari yanaweza kulazwa nje ya ofisi.

Aidha, alisema Serikali kupitia vitengo vya ukaguzi wa ndani na nje inaendelea kufanya tathmini za mara kwa mara kubaini matumizi yasiyo sahihi ya magari hayo, na hatua kali huchukuliwa kwa wanaokiuka taratibu.

MKUU wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania  , Mizengo Pinda, amesema chuo hicho kimejipanga kutanua huduma zake za elimu kwa ...
10/06/2026

MKUU wa Chuo Kikuu Huria cha Tanzania , Mizengo Pinda, amesema chuo hicho kimejipanga kutanua huduma zake za elimu kwa kuanzisha matawi katika kila mkoa nchini, ili kuwafikia wananchi wengi zaidi na kurahisisha upatikanaji wa elimu ya juu.

Pinda aliyasema hayo baada ya kuweka jiwe la msingi la ujenzi wa tawi la Chuo kikuu HuriaTanzania huko Pemba, akieleza kuwa mkakati huo unalenga kuwapatia Watanzania fursa sawa za elimu bila kujali maeneo wanayoishi.

Alisema mfumo wa elimu ya masafa unaotolewa na chuo hicho umeendelea kuwa suluhisho kwa watu wanaotaka kuendelea na masomo huku wakitekeleza majukumu yao ya kila siku.

โ€œLengo letu ni kuona kila Mtanzania mwenye sifa anapata nafasi ya kusoma kwa urahisi na kwa gharama nafuu. Kuanzishwa kwa matawi katika mikoa yote kutasaidia kufanikisha azma hiyo,โ€ alisema Pinda.

๐™๐’๐’๐… ๐ค๐ฎ๐ž๐ง๐๐ž๐ฅ๐ž๐ณ๐š ๐ฎ๐ฃ๐ž๐ง๐ณ๐ข ๐ง๐ฒ๐ฎ๐ฆ๐›๐š ๐ณ๐š ๐ค๐ข๐ฌ๐š๐ฌ๐š ๐Œ๐›๐ฐ๐ž๐ง๐ขMfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) itatekeleza mradi wa nyumba za k...
10/06/2026

๐™๐’๐’๐… ๐ค๐ฎ๐ž๐ง๐๐ž๐ฅ๐ž๐ณ๐š ๐ฎ๐ฃ๐ž๐ง๐ณ๐ข ๐ง๐ฒ๐ฎ๐ฆ๐›๐š ๐ณ๐š ๐ค๐ข๐ฌ๐š๐ฌ๐š ๐Œ๐›๐ฐ๐ž๐ง๐ข

Mfuko wa Hifadhi ya Jamii Zanzibar (ZSSF) itatekeleza mradi wa nyumba za kisasa za makaazi awamu ya pili katika eneo la Mbweni Mjini Unguja.

Akizungumza na Zanzibar Leo, katika ofisi za Mfuko huo Kilimani, Mkurugenzi Rasiliamli Watu na Utawala, Saleh Daud Makame, amesema katika mwaka wa fedha 2026/2027 mfuko utaendelea kuimarisha haiba ya mji na makaazi ya wananchi kupitia utekelezaji wa miradi wa nyumba za kisasa za maendeleo awamu ya pili.

โ€œMradi huu utahusisha ujenzi wa nyumba za ghorofa nane zenye jumla ya nyumba 224, ambazo zinatarajiwa kukidhi mahitaji ya makazi kwa wananchi katika eneo hilo na maeneo jiraniโ€, alisema.

Saleh alifahamisha kuwa kati ya nyumba hizo nyumba 96 zitakuwa na vyumba viwili viwili na nyumba nyengine 96 zitakuwa za vyumba vitatu huku nyumba 32 za zitajengwa vyumba vinne.

Aidha alisema nyumba hizo zitakuwa za ghorofa nane kwa kila moja jambo ambalo linaolenga kuboresha mandhari ya mji, ustawi wa mazingira pamoja na kuongeza upatikanaji wa makaazi bora.

Sambamba na hilo, alisema mradi wa nyumba hizo utaimarishwa kwa vivutio mbalimbali ambavyo vitazingatia kuongeza ushawishi wa uwekezaji kwa wageni na wazawa ikiwemo maeneo ya kupumzikia, busatani, maduka ya kisasa pamoja na umeme wa jua.

โ€œGharama za ujenzi hadi kukamilika kwake zinakadiriwa kufikia shilingi bilioni 75.4 na kwa kuanzia kiasi cha shilingi bilioni 37.7 zimeshatengwa na hivi sasa tuko hatua za mwisho kuanza kwa ujenzi huoโ€, alisema.

Tarehe 10 Juni, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝhttps...
10/06/2026

Tarehe 10 Juni, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.

Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: ๐Ÿ‘‡๐Ÿฝ
https://epaper.smsz.co.tz/

Zanzibarleo | Kwa Ukweli na Uwazi

๐’๐ž๐ซ๐ข๐ค๐š๐ฅ๐ข ๐ค๐ฎ๐š๐ง๐ณ๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐›๐ž๐ง๐ค๐ข ๐ฒ๐š ๐ฎ๐ฐ๐ž๐ค๐ž๐ณ๐š๐ฃ๐ข, ๐ฌ๐จ๐ค๐จ ๐ฅ๐š ๐ก๐ข๐ฌ๐šSerikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Nchi, Ofisi ya Ra...
09/06/2026

๐’๐ž๐ซ๐ข๐ค๐š๐ฅ๐ข ๐ค๐ฎ๐š๐ง๐ณ๐ข๐ฌ๐ก๐š ๐›๐ž๐ง๐ค๐ข ๐ฒ๐š ๐ฎ๐ฐ๐ž๐ค๐ž๐ณ๐š๐ฃ๐ข, ๐ฌ๐จ๐ค๐จ ๐ฅ๐š ๐ก๐ข๐ฌ๐š

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar kupitia Wizara ya Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, imepanga kuanzisha Benki ya Uwekezaji ya Zanzibar (Zanzibar Investment Bank โ€“ ZIB) pamoja na Soko la Hisa la Zanzibar (Zanzibar Stock Market), katika mwaka wa fedha 2026/2027, ikiwa ni hatua ya kuimarisha sekta ya fedha na kukuza uchumi wa visiwa hivyo.

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, Fedha na Mipango, Dk. Juma Malik Akili, aliliambia Baraza la Wawakilishi kuwa hatua hiyo inalenga kuongeza fursa za uwekezaji, kuimarisha upatikanaji wa mitaji kwa wawekezaji wa ndani na nje, na kuchochea ushiriki wa sekta binafsi katika maendeleo ya uchumi wa Zanzibar.

Alisema kuanzishwa kwa taasisi hizo mbili kutasaidia kuongeza ushindani katika sekta ya fedha, kupanua huduma za uwekezaji na kuwezesha upatikanaji wa rasilimali za kifedha kwa ajili ya miradi ya maendeleo.

Address

Maisara
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zanzibarleo Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zanzibarleo Online:

Share