11/06/2026
๐๐๐ซ๐ข๐ค๐๐ฅ๐ข ๐๐ฎ๐ฐ๐๐ค๐ ๐๐ข๐ฉ๐๐ฎ๐ฆ๐๐๐ฅ๐ ๐๐ฎ๐ค๐๐ฆ๐ข๐ฅ๐ข๐ฌ๐ก๐ ๐๐ข๐ญ๐ฎ๐จ ๐ฏ๐ฒ๐ ๐๐๐ฒ๐ ๐๐ข๐ง๐๐ฏ๐ฒ๐จ๐ฃ๐๐ง๐ ๐ฐ๐
Serikali imesema itaendelea kuelekeza fedha katika kukamilisha ujenzi wa miundombinu ya vituo vya afya 364 vinavyoendelea kujengwa nchini kabla ya kuanza miradi mipya katika kata zinazostahili kupata huduma hizo, ikiwemo Kata za Chawi na Mnima katika Halmashauri ya Mji wa Nanyamba.
Kauli hiyo imetolewa kufuatia swali la Mbunge wa Nanyamba, Abdallah Dadi Chikota, aliyetaka kujua ni lini Serikali itatoa fedha kwa ajili ya ujenzi wa Vituo vya Afya vya Chawi na Mnima ili kuboresha huduma za afya kwa wananchi wa maeneo hayo.
Akijibu swali hilo Bungeni, Naibu Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri MkuuโTAMISEMI, Dkt. Japhari Seif, amesema Serikali imeendelea kuwekeza katika sekta ya afya Nanyamba kwa kutoa zaidi ya shilingi bilioni 2.7 katika kipindi cha mwaka wa fedha 2021/22 hadi 2025/26 kwa ajili ya utekelezaji wa miradi mbalimbali ya afya.
Aidha, amesema katika mwaka wa fedha 2026/27, Serikali imetenga shilingi milioni 300 kwa ajili ya kuendeleza ujenzi wa miundombinu ya Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Nanyamba, ikiwa ni sehemu ya jitihada za kuimarisha upatikanaji wa huduma bora za afya kwa wananchi.
Na Saida Issa, Dodoma