Zanzibarleo Online

Zanzibarleo Online Pata habari za uhakika na kuaminika kutoka Gazeti namba 1 visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Tarehe 15 Agosti, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: 👇🏽htt...
15/08/2026

Tarehe 15 Agosti, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.

Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: 👇🏽
https://epaper.smsz.co.tz/

| Kwa Ukweli na Uwazi

Tarehe 14 Agosti, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: 👇🏽htt...
14/08/2026

Tarehe 14 Agosti, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.

Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: 👇🏽
https://epaper.smsz.co.tz/

Zanzibar Leo | Kwa Ukweli na Uwazi

Halmashauri za Mkoa wa Mara zimetoa zabuni zenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 224 kupitia Mfumo wa NeST kwa makundi m...
13/08/2026

Halmashauri za Mkoa wa Mara zimetoa zabuni zenye thamani ya zaidi ya Sh. milioni 224 kupitia Mfumo wa NeST kwa makundi maalum ya vijana, wanawake, wazee na watu wenye ulemavu, ikiwa ni sehemu ya utekelezaji wa Sheria ya Ununuzi wa Umma ya mwaka 2023.

Meneja wa Mamlaka ya Udhibiti wa Ununuzi wa Umma (PPRA) Kanda ya Ziwa, Mhandisi Juma Mkobya, ametoa taarifa hiyo kwa Kiongozi wa Mbio za Mwenge wa Uhuru Kitaifa, Wazo Mwang’onda, wakati wa kuhitimisha mbio hizo Mkoa wa Mara, Agosti 9, 2026, katika Halmashauri ya Wilaya ya Bunda.

Kwa mujibu wa Mhandisi Mkobya, zabuni hizo zimetolewa na Halmashauri ya Manispaa ya Musoma (Sh. milioni 99), Rorya (Sh. milioni 7.4), Musoma (Sh. milioni 37.7), Tarime (Sh. milioni 55.6), Bunda (Sh. milioni 16.81) na Serengeti (Sh. milioni 8). Hata hivyo, halmashauri tatu hazikuwa zimetoa zabuni kwa makundi hayo hadi Agosti 9, 2026.

Amesema jumla ya vikundi 1,590 vya makundi maalum vimesajiliwa katika Mfumo wa NeST katika halmashauri zote za Mkoa wa Mara, vikiwemo vikundi 781 vya vijana, 650 vya wanawake, 91 vya wazee na 68 vya watu wenye ulemavu. Halmashauri ya Mji wa Bunda inaongoza kwa usajili ikiwa na vikundi 238.

Mwang’onda amewapongeza viongozi wa halmashauri za Mara na kuwataka kuongeza juhudi kuhakikisha makundi yaliyosajiliwa yanapata zabuni, akisema hatua hiyo inaendana na dhamira ya Serikali ya Awamu ya Sita ya kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Ameongeza kuwa usimamizi madhubuti wa PPRA na uzalendo wa watumishi wa umma utasaidia kujenga uchumi jumuishi na kufikia malengo ya Dira ya Taifa ya Maendeleo 2050.

Mwenge wa Uhuru ulikimbizwa Mara kuanzia Agosti 1 hadi 9, 2026, kabla ya kukabidhiwa Mkoa wa Mwanza, huku Kikundi cha Musoma Cleaners kikieleza kuwa zabuni kupitia NeST zimekuwa chachu ya ukombozi wa kiuchumi.

Meneja wa VETA Kanda ya Kaskazini, Monica Mbella, amemueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu ...
13/08/2026

Meneja wa VETA Kanda ya Kaskazini, Monica Mbella, amemueleza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, namna mafunzo ya ufundi stadi yanavyonufaisha makundi mbalimbali katika jamii.

Maelezo hayo yametolewa wakati Rais Samia alipotembelea banda la VETA katika Tamasha la Kizimkazi, linalofanyika katika Viwanja vya Dimbani, Mkoa wa Kusini Unguja, Zanzibar.

Tamasha hilo lenye kaulimbiu “Kizimkazi Kumenoga, Shangwe na Fursa” limezinduliwa Agosti 12, 2026, na Rais wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar, Dkt. Hussein Ally Mwinyi, likiwa na lengo la kuwakutanisha wananchi na wadau mbalimbali katika kujadili na kuibua fursa za maendeleo.

Tamasha la Kizimkazi linatarajiwa kuhitimishwa Agosti 14, 2026, likiwa limejikita katika kuhamasisha fursa na shughuli mbalimbali zenye manufaa kwa jamii, huku taasisi za elimu na mafunzo k**a VETA zikiendelea kutoa elimu kuhusu nafasi ya ujuzi wa ufundi katika kuwawezesha wananchi kiuchumi.

Tarehe 13 Agosti, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: 👇🏽htt...
13/08/2026

Tarehe 13 Agosti, 2026. Ukurasa wa mbele na nyuma wa gazeti la Zanzibar Leo.

Soma gazeti kupitia mtandao, Tembelea: 👇🏽
https://epaper.smsz.co.tz/

| Kwa Ukweli na Uwazi

BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali na wadau mbalimba...
12/08/2026

BENKI ya Taifa ya Biashara (NBC) imesisitiza dhamira yake ya kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali na wadau mbalimbali katika kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia, kuhifadhi mazingira, kukuza utalii na kuendeleza ubunifu wa vijana.

Dhamira hiyo ilibainishwa jana na Mkurugenzi Mtendaji wa NBC, Theobald Sabi, wakati wa hafla maalum ya mnada wa sanaa za picha iliyoongozwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dkt. Samia Suluhu Hassan, katika Hoteli ya Kwanza, Kizimkazi, Zanzibar.

Hafla hiyo iliandaliwa na Mwanamke Initiative Foundation (MIF) kwa kushirikiana na kampuni ya ubunifu ya Waba Group, ikiwa na lengo la kutumia sanaa ya upigaji picha kuhamasisha uhifadhi wa mazingira, nishati safi ya kupikia na utalii.

Picha zilizopigwa katika maeneo mbalimbali ya Zanzibar zilionesha mandhari, utamaduni, maisha ya jamii, utalii na urithi wa asili wa visiwa hivyo.

Akizungumza katika hafla hiyo, Rais Samia aliwataka wadau wa sanaa ya upigaji picha, hususan vijana, kutumia ubunifu wao katika kuitangaza Tanzania na vivutio vyake vya utalii.

Alisema sekta hiyo ina fursa kubwa za kibiashara na inaweza kuwa chanzo cha ajira na kipato kwa vijana.

Rais Samia pia alieleza kuvutiwa na baadhi ya picha zilizowasilishwa, zikiwemo za pomboo chini ya bahari, wanawake wakilima mwani na mandhari mbalimbali za Zanzibar.

Alisema kazi hizo zinaweza kutumika kuitangaza Tanzania, utamaduni wake na vivutio vyake katika soko la ndani na kimataifa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Mwanamke Initiative Foundation, Wanu Hafidh Ameir, alisema fedha zitakazopatikana kupitia mnada huo zitaelekezwa katika kuunga mkono jitihada za kukuza matumizi ya nishati safi ya kupikia na kupunguza utegemezi wa nishati zinazochangia ukataji wa misitu.

Akizungumzia nafasi ya NBC katika agenda ya nishati safi ya kupikia, Sabi alisema benki hiyo iko tayari kushirikiana na wadau mbalimbali kuwezesha mnyororo mzima wa nishati hiyo, kuanzia uzalishaji hadi matumizi.

Katika hafla hiyo, NBC ilitunukiwa tuzo maalum na Rais Samia kwa kutambua mchango wake katika kufanikisha tukio hilo na kuunga mkono ajenda ya maendeleo endelevu, ikiwemo nishati safi ya kupikia na uhifadhi wa mazingira.

Taasisi za Ukaguzi wa Hesabu za Serikali (SAIs) barani Afrika, zimehimizwa kutumia Akili Bandia (AI), Sayansi ya Data na...
11/08/2026

Taasisi za Ukaguzi wa Hesabu za Serikali (SAIs) barani Afrika, zimehimizwa kutumia Akili Bandia (AI), Sayansi ya Data na teknolojia za usalama wa mitandao katika ukaguzi wa fedha za umma ili kubaini mianya ya ubadhirifu, udanganyifu na matumizi yasiyo sahihi ya rasilimali za wananchi.

Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Charles Kichere, alitoa kauli hiyo wakati akifungua mafunzo ya wiki mbili ya kimataifa ya ukaguzi wa akili bandia, sayansi ya data na usalama wa mitandao huko katika Taasisi ya Teknolojia ya India (IIT) Madras Zanzibar.

Alisema matumizi ya teknolojia hizo yanapaswa kuwa sehemu ya msingi ya taaluma ya ukaguzi kutokana na kasi kubwa ya serikali kuelekea mifumo ya kidijitali.

Aidha Kichere alisema mabadiliko hayo si jambo la siku zijazo, bali tayari yanaendelea katika taasisi mbalimbali za serikali zinazotumia mifumo ya kidijitali katika ukusanyaji wa mapato, utoaji wa huduma na usimamizi wa rasilimali za umma.

Alifahamisha kuwa matumizi ya AI yanaweza kuisaidia sekta ya ukaguzi kuchunguza miamala yote badala ya kutegemea sampuli ndogo k**a ilivyokuwa katika mifumo ya ukaguzi wa kawaida.

Charles alibainisha kuwa teknolojia hiyo inaweza kubaini malipo yaliyorudiwa, akaunti za wazabuni, pamoja na taarifa za benki za watumishi wa serikali.

“Mfumo huo unaweza kutambua ankara zinazowekwa chini kidogo ya viwango vilivyowekwa, hali ambayo inaweza kuashiria nia ya kukwepa taratibu zinazohitaji idhini ya ziada”, alisema.

Alifahamisha kuwa alama hizo mara nyingi ni vigumu kubainika kwa macho ya mkaguzi, lakini zinaweza kuonekana kwa urahisi kupitia mifumo ya kiteknolojia iliyofundishwa kuchambua taarifa kwa kina.

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imeendelea kuweka msukumo mkubwa katika kuboresha miundombinu ya usafiri Pemba, huku i...
11/08/2026

SERIKALI ya Mapinduzi ya Zanzibar imeendelea kuweka msukumo mkubwa katika kuboresha miundombinu ya usafiri Pemba, huku ikitangaza kuwa ujenzi wa barabara ya Mkoani–Chake Chake unatarajiwa kuanza ndani ya mwaka 2026.

Hayo yamesemwa na Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar, Hemed Suleiman Abdulla, wakati akielezea tathmini yake baada ya ziara ya kukagua miradi mbalimbali ya maendeleo katika Kisiwa cha Pemba hivi karibuni.

Makamu wa Pili wa Rais alisema maandalizi ya kuanza kwa ujenzi wa barabara hiyo yamefikia hatua nzuri, akiwataka wananchi wa Pemba kuwa na matumaini na kujiandaa kwa kuanza kwa utekelezaji wa mradi huo muhimu.

Alisema mradi huo, inatekelezwa kwa ufadhili wa kifedha uliowezeshwa na taasisi ya Serikali ya Uingereza kupitia mfumo wa mikopo, UK Export Finance (UKEF), kwa Serikali ya Zanzibar na ni sehemu ya juhudi pana za Serikali, katika kuimarisha miundombinu ya usafiri na kuchochea shughuli za kiuchumi visiwani.

Kwa mujibu wa Makamu wa Pili wa Rais, mradi huo utaenda sambamba na miradi mingine mikubwa ya kimkakati, ikiwemo ujenzi wa barabara ya Tunguu-Makunduchi pamoja na ujenzi wa Uwanja wa Ndege wa Pemba, ambao tayari umeanza kufanyika.

Akizungumzia umuhimu wa barabara hiyo, Hemed alisema barabara ya Mkoani–Chake Chake ni kiunganishi muhimu cha miundombinu ya usafiri na maeneo mbalimbali ya Pemba.

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali imeamua kufunga kamera z...
11/08/2026

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali imeamua kufunga kamera za usalama barabarani ili kudhibiti ongezeko la ajali zinazotokana na uvunjifu wa sheria za barabarani.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo alipokutana na Kamati ya Baraza la Wawakilishi ya Kusimamia Viongozi Wakuu wa Kitaifa, iliyofika Ikulu jana na kuonana naye kwa mazungumzo, ikiongozwa na Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Machano Othman Said.

Alisema dhamira ni kurudisha nidhamu barabarani, kufuatwa kwa sheria na kumfanya kila mtumiaji wa barabara kuwa katika mazingira salama wakati wote, wakiwemo madereva na watembea kwa miguu.

Alisema serikali itaendelea kuimarisha mfumo wa kamera za barabarani katika maeneo yote mjini na vijijini, baada ya kuanza utekelezaji katika Mkoa wa Mjini Magharibi na kuwasisitiza wananchi kuunga mkono dhamira hiyo ya serikali.

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ipo katika hatua za mwisho za kuandaa mpango wa kuimarisha hifadhi ya chakula kwa kuwe...
11/08/2026

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar ipo katika hatua za mwisho za kuandaa mpango wa kuimarisha hifadhi ya chakula kwa kuwekeza katika uzalishaji wa mchele Tanzania Bara.

Hatua hiyo inalenga kuhakikisha upatikanaji wa chakula cha kutosha kwa wakazi wa visiwa hivyo.

Hayo yalisemwa na Ofisa Uchumi kutoka Tume ya Mipango Zanzibar, Kombo Haji Makame, wakati akitoa ufafanuzi kuhusu mpango wa hifadhi ya chakula katika mkutano wa takwimu uliofanyika Ofisi ya Mtakwimu Mkuu wa Serikali, Mazizini Unguja.

Makame alisema serikali inaendelea na mchakato wa kuandaa mpango wa kuagiza na kuhifadhi mchele kutoka Tanzania Bara, ambapo tayari andiko la mradi limeandaliwa na tafiti zimefanyika katika mikoa ya Morogoro na Mbeya.

Alisema matokeo ya utafiti yanaonesha kuwa Mkoa wa Morogoro una uwezo mkubwa wa kuzalisha chakula cha kutosha kuikidhi Zanzibar kwa zaidi ya miaka mitatu.

Kutokana na uwezo huo, alisema SMZ imeanza mazungumzo ya awali kuhusu uwezekano wa kuwekeza katika shughuli za kilimo mkoani Morogoro ili kuhakikisha upatikanaji wa chakula cha uhakika.

Address

Maisara
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zanzibarleo Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zanzibarleo Online:

Shortcuts

Share