Zanzibarleo Online

Zanzibarleo Online Pata habari za uhakika na kuaminika kutoka Gazeti namba 1 visiwani Zanzibar na Tanzania kwa ujumla.

Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Hamad Rashid Mohamed amesema end...
21/10/2025

Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Alliance for Democratic Change (ADC), Hamad Rashid Mohamed amesema endapo atapata ridhaa atawalipia deni la mikopo ya Bodi ya Mikopo ya Elimu Juu, waliokopeshwa kwa ajili ya kusomea.

Mgombea huyo aliyasema hayo kwakati akiwahutubia wananchi ikiwa ni muendelezo wa mikutano yake ya kampeni ulifanyika Mjimbini Mkoani mkoa wa Kusini Pemba.

Alieleza waajiriwa wengi wamekuwa wakiishi maisha duni, kutokana na mishahara yao kukatwa na kulipa deni la mikopo ya elimu ya juu.

Alisema sera ya chama chake ni kuwepo kwa elimu bure kuanzia msingi hadi chuo kikuu, hivyo akiingia madarakani atawalipia madeni kwa wote ambao wanadaiwa na Bodi ya mikopo, waondokane na hali ngumu za maisha.

.smsz.co.tz

Waislam wenye kuishi na baadhi ya maradhi hawatoruhusiwa kuingia nchini Saudi Arabia kwenda kutekeleza ibada ya hijja kw...
21/10/2025

Waislam wenye kuishi na baadhi ya maradhi hawatoruhusiwa kuingia nchini Saudi Arabia kwenda kutekeleza ibada ya hijja kwa mwaka 2026.

Daktari dhamana wa afya za mahujaji, Naufal Kassim Mohammed, ameeleza hayo alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari katika msikiti Jamii Zinjibar uliopo Kiembe Samaki.

Aliyataja maradhi hayo ni pamoja na figo linalohitaji kufanyiwa usafishaji, moyo, mapafu yanayohitaji matumizi ya oksijini, maradhi ya ini na uti wa mgongo unaomzuia mgonjwa kufanya shughuli za kawaida.

Maradhi mengine ni mishipa ya fahamu inayosababisha ulemavu wa viungo, uzee, shida ya akili, ujauzito, maradhi ya miguu yanayosababisha mtu kushindwa kutembea kwa masafa na waliopo kwenye matibabu ya saratani.

Alisema kuwa maelekezo hayo wameyapokea kutoka kwa mamlaka inayosimamia ibada ya Hijja kutoka nchini Saudi Arabia, hatua ambayo inalenga kulinda afya za wenye nia ya kwenda kutekeleza ibada hiyo.

Dk. Naufal alikumbushia kuwa miongozo inayotakiwa kufuatwa kwa kila taasisi zinazosimamia mahujaji ni kuhakikisha wanapima afya za mahujaji watarajiwa wakati wa kujiandikisha.

Miongozo mengine kwa taasisi inayochukua mahujaji wa jinsia ya k**e na kiume inatakiwa kuwa na madaktari angalau wawili, mmoja kutoka kila jinsia.

Soma zaidi: 𝐳𝐚𝐧𝐳𝐢𝐛𝐚𝐫𝐥𝐞𝐨.𝐜𝐨.𝐭𝐳

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema mageuzi ya uchumi na fedha yaliyo...
21/10/2025

RAIS wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema mageuzi ya uchumi na fedha yaliyoanzishwa nchini, yamekuwa msingi muhimu katika kuijenga Zanzibar.

Dk. Mwinyi aliyasema hayo katika hafla ya kupongezwa kwa mageuzi ya uchumi na fedha, utoaji wa gawio kwa wawekezaji wa hati fungani ya Zanzibar inayofuata misingi ya kiislam (SUKUK) na uzinduzi wa skimu ya hifadhi ya jamii yenye kufuata misingi ya kislam.

Katika hafla hiyo iliyofanyika ikulu mjini Zanzibar, Dk. Mwinyi alisema mageuzi ya kiuchumi na kifedha yaliyokwenda sambamba na ushirikishwaji wa wananchi kikamilifu yameifanya Zanzibar kupiga hatua za maendeleo.

Alifahamisha kuwa utekelezwaji wa mageuzi hayo uliambatana na uwekaji wa sera za utekelezwaji na mifumo imara ya kisasa ya usimamizi wa fedha za umma.

Dk. Mwinyi alisema Zanzibar inashuhudia matokeo chanya kwenye nyanja mbalimbali ikiwa pamoja na ukuaji wa uchumi ambao umefikiza zaidi ya asilimia 7.2 kwa mwaka.

Soma zaidi: 𝐳𝐚𝐧𝐳𝐢𝐛𝐚𝐫𝐥𝐞𝐨.𝐜𝐨.𝐭𝐳

Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali ya CCM itaendelea ...
17/10/2025

Mgombea urais wa Zanzibar kwa tiketi ya Chama cha Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amesema serikali ya CCM itaendelea kuimarisha mazingira ya kibiashara na kulifanya eneo la Darajani kuwa eneo la kibiashara.

Dk. Mwinyi ameyasema hayo wakati akizungumza na wafanyabiashara wa Darajani ikiwa ni muendelezo wa kampeni zake za kuomba kura kwa wananchi, ambapo alisema hatua hiyo inalenga kukuza uchumi kupitia sekta ya biashara na kuongeza mvuto wa utalii kwa visiwa vya Zanzibar.

Alisema serikali inataka kuona Zanzibar inaendelea kuvutia wageni kwani ikiboresha mazingira ya
wafanyabiashara, si tu kuwasaidia wao bali hata kuzifanya shughuli zao kuwa bora zaidi.

Dk. Mwinyi ameridhishwa na hali ya ufanyaji biashara katika eneo la Darajani Souk, kwani awali eneo hilo
halikuwa katika mazingira mazuri ya kufanyia biashara na lilikuwa eneo dogo ukilinganisha na mazingira ya sasa.

Dk. Mwinyi alisema serikali itaendelea na utaratibu wa kujenga maduka zaidi kwani bado kuna idadi kubwa ya wafanyabiashara wanaoweka biashara zao pembeni kwenye kuta jambo ambalo halikubaliki.

Soma zaidi katika gazeti la Zanzibarleo, tembelea: 𝗲𝗽𝗮𝗽𝗲𝗿.𝘀𝗺𝘀.𝗰𝗼.𝘁𝘇

Address

Maisara
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Zanzibarleo Online posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to Zanzibarleo Online:

Share