96.9 Zenjfm Sauti ya Pwani

96.9 Zenjfm Sauti ya Pwani Huu ni ukurasa rasmi wa kituo cha radio 96.9zenj fm radio (sauti ya pwani) Tunasikika saa 24 Nyota Njema 6:30am.

Nakshnaksh za pwani 10:00am
02:00 Gigabyte
04:00 Mwangaza wa habari
07:00pm zenjsports
usisahau kusikiliza popo ulipo dunian kupitia Radio tadio

04/10/2025

🔥🔥 SIMULIZI: SIJAUWA MIMI – SEHEMU YA 18
✍️ Mtunzi: Mwenenu Binnassib
📞 WhatsApp: 0625995872

Asubuhi tulivu, upepo wa baridi ukivuma taratibu, lakini ndani ya moyo wa Konstebo Masoud kulikuwa na dhoruba.
Kila hatua aliyopiga kuelekea msibani, alikuwa akihisi macho kadhaa yakimfuatilia.
Simu ile ya jana usiku bado ilimtesa kichwani:

“Acha kuchunguza. Hii si kesi yako tena...”

Lakini moyo wake wa haki haukumruhusu kurudi nyuma.

Alipofika eneo la maziko, watu walikuwa wamejazana. Sauti za dua, machozi na simanzi vilitawala anga ya eneo hilo.
Bwana Ramadhan Mnyika, baba wa marehemu, alionekana amesimama mbele ya jeneza, macho yakiwa mekundu, sura ya majonzi.
Lakini Masoud, akiwa mbali kidogo, alihisi huzuni hiyo haikuwa ya kweli.

Aliyatazama kwa makini magari yaliyopaki pembezoni — yote ya kifahari, yenye namba zilizofanana, zenye ishara moja: DSV.

“Kila gari la kampuni yake... je, huu msiba ni wa kifamilia au wa kibiashara?” alijiuliza kimoyomoyo.

Wakati dua ikiendelea, macho ya Masoud yakagonga uso mmoja.
Malik!
Alikuwa amesimama mbali kidogo, akivaa miwani myeusi na kofia, akijaribu kujificha.
Masoud akamsogelea taratibu, hatua kwa hatua.

Lakini ghafla, Malik akaona harakati hizo — akageuka, akapanda kwenye gari moja, likatokomea kwa kasi.

Masoud akajaribu kumfuata, lakini kwa kuwa eneo lilikuwa na umati mkubwa, hakuweza.
Akasimama akihema, akisema:

“Huyu Malik anajua mengi. Kwa nini alikuwa hapa leo?”

Baada ya mazishi kumalizika, Bwana Ramadhan akasogea kwa waandishi wa habari, akasema kwa huzuni:

> “Ninachotaka ni haki kwa binti yangu. Namuamini Mungu na Jeshi la Polisi kufanya kazi yao kwa uadilifu.”

Maneno yake yalionekana ya ukweli, lakini Masoud alikuwa akijua kuna sura mbili nyuma ya uso huo.

Kabla hajaondoka, mzee mmoja wa zamani wa maskani alipomsogelea kwa hofu, akamwambia kwa sauti ya chini:

> “Kijana... usiendelee kuchimba sana. Wale watu hawana huruma. Yule binti alijaribu kusema, akapotea. Usije ukafuata njia yake.”

Masoud akamwangalia mzee yule, akasema:

“Nashukuru kwa onyo lako. Lakini haki ya marehemu lazima ijulikane.”

Mzee akatikisa kichwa taratibu, kisha akaondoka kwa kasi kana kwamba alikuwa anaogopa kitu.

Baadaye jioni, Masoud akiwa ofisini, akipitia picha za maziko zilizochukuliwa kwa siri na timu yake, aliona jambo la kushangaza.
Kwenye moja ya picha, nyuma ya msafara wa maziko, gari moja dogo lilionekana likifuata kwa umbali.
Namba zake zilikuwa zimefutwa kwa tope — lakini kwenye upande wa mbele, kamera ya CCTV ya barabarani ilikuwa imelik**ata vizuri.

Masoud alikuza picha hiyo kwa makini.
Kwenye kioo cha dereva, aliona uso wa mtu aliyemfahamu — Koplo Jafet.

Alitetemeka.

“Hapana... si Jafet wangu huyu!”

Akaongeza ukubwa wa picha — hakukuwa na makosa. Ilikuwa yeye.

Akahema kwa nguvu, akainuka taratibu, akijisemea kwa sauti ya chini:

“Ina maana... Jafet pia yumo ndani ya hii mchezo? Au alikuwa analinda msafara kwa siri?”

Simu yake ikalia tena.
Namba haikujulikana.
Akaipokea kwa tahadhari.

📞
“Masoud... tulikuonya. Umechimba sana. Sasa utalipa bei.”

Kabla hajajibu, mlango wa ofisi yake ukafunguliwa ghafla.
Risasi tatu zikapigwa!

Masoud akaruka upande wa meza, akajificha chini, akavuta bastola yake.
Lakini risasi ziliposimama, aliposimama taratibu, hakukuwa na mtu.
Madirisha yalikuwa wazi — risasi zilikuwa zimepigwa kutoka nje.

Akahema, akapiga simu kituo kikuu cha doria.

“Nahitaji ulinzi wa haraka, kuna mtu ananiandama!”

Usiku huo, akiwa chini ya ulinzi, Masoud alikaa kimya chumbani, akifikiria.
Aliandika katika daftari lake:

“Mchezo huu si wa kawaida. Malik, Jafet, na Mnyika — wote wanaunganishwa na jina moja: Joanita.”

Kisha akafunga daftari, akatazama dirishani.
Mbele ya nyumba, aliona kivuli cha mtu akipita kimya kimya.

Akasema kwa sauti ndogo, huku akibeba bastola yake:

“Haki haifi... hata k**a damu itamwagika.”

đź’Ą ITAENDELEA... đź’Ą

đź–¤ Usikose Sehemu ya 19.
đź’¬ Toa maoni yako hapa chini!





“Risasi tatu zilifyatuliwa... lakini lengo lilikuwa nani? Je, ni nani anayetaka kumzima mpelelezi Masoud kabla hajafichua siri ya Joanita?”

Aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Poul Makonda ameteuliwa na Halimashauri Kuumya Ccm kushika nafasi ya Katibu wa H...
22/10/2023

Aliyekuwa mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaam Poul Makonda ameteuliwa na Halimashauri Kuumya Ccm kushika nafasi ya Katibu wa Halimashauri kuu ya Ccm Taifa Itikadi na Uwenezi.

Makonda amechukua nafasi ya Sophia Edward.

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amefanya ziara ya Usiku  kukagua Miradi ya Ujenzi wa maso...
19/10/2023

Makamu wa Pili wa Rais wa Zanzibar Mhe. Hemed Suleiman Abdulla amefanya ziara ya Usiku kukagua Miradi ya Ujenzi wa masoko ya Mwanakwerekwe na Jumbi Wilaya ya Magharibi “B” kujionea maendeleo ya miradi hiyo.
Mhe. Hemed amesema hatua iliyofikia katika ujenzi wa masoko hayo ni ya kuridhisha ambapo amewataka wakandarasi na washauri elekezi kuongeza kasi ya ujenzi ili kukamilika kwa wakati uliopangwa na ubora wa hali ya juu .



Amesema mategemeo ya Rais Dkt. Hussein Ali Mwinyi kuwa masoko hayo yakamilike mwishoni mwa mwaka huu ili wafanyabiashara waweze kuyatumia kwa shughuli za kujipatia kipato cha kila siku.



Aidha amemshukuru Rais Dkt. Mwinyi kwa miongozo anayoitoa katika miradi hiyo pamoja na upatikanaji wa fedha kwa wakati bila ya ucheleweshaji hatua ambayo inawapa moyo wakandarasi kuwa na kasi ya ujenzi huo.

10/10/2023
Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita na Waziri wa Utamaduni ,Sanaa na Michezo Tanzan...
21/09/2023

Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita na Waziri wa Utamaduni ,Sanaa na Michezo Tanzania Bara Damas Ndumbaro wamesema Taifa Cup iwe ni chachu ya kuibua vipaji kwa vijana katika michezo yote shiriki.

Wakizungumza katika hafla ya ugawaji wa vifaa vya michezo kwa Mikoa ya Zanzibar kwa ajili ya Mashindano ya Taifa Cup,yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Wizara ya Habari,Vijana Utamaduni na Michezo Migombani.

Waziri Tabia alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuendeleza na kuimarisha sekta ya michezo nchini,lakini pia kuweka hamasa ya kununua magoli katika michezo imewapa ari viongozi katika kuwaamsha vijana katika michezo.

Alisema wataendeleza ushirikiano na Wizara ya Utamaduni,Sanaa na Michezo Tanzania bara katika kutekeleza majukumu yao kwa wakati ili kuzisaidia Serikali zote mbili lengo kupatikana maendeleo.

Nae Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Damas Ndumbaro alisema ni vyema mikoa kutafuta vipaji ngazi ya chini na hatimae watakapofika Taifa kuendelezwa vipaji hivyo bila ya kuviacha vipotee.

Alisema wana kila sababu ya kulinda,kudumisha na kusimamia Muungano na kuhakikisha atafanya kazi kwa ushirikiano na Waziri Tabia katika kulinda Muungano na kuimarisha michezo nchini.

“ Nampongeza Dk.Hussein Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kuiongoza vyema Zanzibar,lakini pia anaimarisha michezo na kudumisha Muungano wetu nampongeza sana Rais” alisema.

Hivyo aliwataka Maofisa Michezo Mikoa kuzilea timu na kuibua vipaji ili kuisaidia Tanzania iendelee kimichezo na kupata vijana imara wa kuweka historia.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab alisema Wizara itaendelea kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuibua vipaji kila Mikoa kwa ajili ya kuviendeleza.

Alimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuthamini na kutekeleza malengo ambayo yanawaletea mafanikio wananchi.

Kamisha wa Idara ya Michezo Zanzibar Ameir Makame Mohammed alisema mashindano hayo yamekuwa na ushindani mkubwa kwani zaid ya mikoa 25 inas

Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita na Waziri wa Utamaduni ,Sanaa na Michezo Tanzan...
21/09/2023

Waziri wa Habari,Vijana,Utamaduni na Michezo Zanzibar Tabia Maulid Mwita na Waziri wa Utamaduni ,Sanaa na Michezo Tanzania Bara Damas Ndumbaro wamesema Taifa Cup iwe ni chachu ya kuibua vipaji kwa vijana katika michezo yote shiriki.

Wakizungumza katika hafla ya ugawaji wa vifaa vya michezo kwa Mikoa ya Zanzibar kwa ajili ya Mashindano ya Taifa Cup,yaliyofanyika kwenye ukumbi wa Wizara ya Habari,Vijana Utamaduni na Michezo Migombani.

Waziri Tabia alimpongeza Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa ajili ya kuendeleza na kuimarisha sekta ya michezo nchini,lakini pia kuweka hamasa ya kununua magoli katika michezo imewapa ari viongozi katika kuwaamsha vijana katika michezo.

Alisema wataendeleza ushirikiano na Wizara ya Utamaduni,Sanaa na Michezo Tanzania bara katika kutekeleza majukumu yao kwa wakati ili kuzisaidia Serikali zote mbili lengo kupatikana maendeleo.

Nae Waziri wa Utamaduni,Sanaa na Michezo Damas Ndumbaro alisema ni vyema mikoa kutafuta vipaji ngazi ya chini na hatimae watakapofika Taifa kuendelezwa vipaji hivyo bila ya kuviacha vipotee.

Alisema wana kila sababu ya kulinda,kudumisha na kusimamia Muungano na kuhakikisha atafanya kazi kwa ushirikiano na Waziri Tabia katika kulinda Muungano na kuimarisha michezo nchini.

“ Nampongeza Dk.Hussein Mwinyi Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi kwa kuiongoza vyema Zanzibar,lakini pia anaimarisha michezo na kudumisha Muungano wetu nampongeza sana Rais” alisema.

Hivyo aliwataka Maofisa Michezo Mikoa kuzilea timu na kuibua vipaji ili kuisaidia Tanzania iendelee kimichezo na kupata vijana imara wa kuweka historia.

Katibu Mkuu Wizara ya Habari, Vijana,Utamaduni na Michezo Fatma Hamad Rajab alisema Wizara itaendelea kufanya kazi kwa bidii kwa lengo la kuibua vipaji kila Mikoa kwa ajili ya kuviendeleza.

Alimpongeza Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dk. Hussein Mwinyi pamoja na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Samia Suluhu Hassan kwa kuthamini na kutekeleza malengo ambayo yanawaletea mafanikio wananchi.

Kamisha wa Idara ya Michezo Zanzibar Ameir Makame Mohammed alisema mashindano hayo yamekuwa na ushindani mkubwa kwani zaid ya mikoa 25 inashiriki lengo kuibua vipaji na kuendeleza Muungano uliopo.

Alisema mashindano yaliyopita Mkoa wa Mjini walikuwa mabingwa mpira wa miguu na kwa upande wa Riadha Kusini Unguja ( Makunduchi) iliibuka bingwa na upande wa singeli na Sanaa walifanya vizuri.

Kamishna alisema waliokabidhiwa mipira Maofisa wa michezo ikiwemo Mkoa wa kasakazini Pemba, Mkoa wa Kusini Pemba, Mkoa wa Kaskazini Unguja,Mkoa wa Mjini Magharibi ,Pamoja na Mkoa wa Kusini Unguja.

Jumla ya mipira 270 iligawiwa kwa kila mkoa mipira 54 ,ikiwemo mpira wa miguu 18,mpira wa kikapu 18 pamoja na mpira wa wavu 18.

Madereva wa Bodaboda wamemlilia Raisi Dr Samia Suluhu Hassan kupanda bei ya MafutaBaadhi ya waendesha vyombo vya moto wa...
07/09/2023

Madereva wa Bodaboda wamemlilia Raisi Dr Samia Suluhu Hassan kupanda bei ya Mafuta

Baadhi ya waendesha vyombo vya moto wa Manespaa ya Bukoba Mkoani Kagera wameiomba serikal kuwapunguzia bei ya mafuta baada ya mamlaka ya udhibiti wa hufuma ya nishati na maji EWURA kutangaza bai mpyaa za Mafuta ya Petrol,Diseil pamoja na mafuta ya Taa

Address

Mombasa
Zanzibar

Telephone

+255715968968

Website

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when 96.9 Zenjfm Sauti ya Pwani posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to 96.9 Zenjfm Sauti ya Pwani:

Shortcuts

Share