ASAM MEDIA

ASAM MEDIA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ASAM MEDIA, Media/News Company, KIJANGWANI, Zanzibar.

11/03/2026

Waswahili wanasema “fadhila si mali, bali ni moyo.” Na pale moyo unapoguswa na huruma ndipo utu wa kweli hujitokeza. Katika kuadhimisha International Women's Day, Tanzania Revenue Authority TRA Tanzania imeonesha mfano wa kuigwa kwa kugusa maisha ya wanawake waliopo katika mazingira magumu.

Kupitia ziara maalum ya kijamii, TRA ilitoa msaada wa vifaa mbalimbali na kuwatembelea wanawake wagonjwa wa akili pamoja na watoto na pia kuwafikia wafungwa wanawake, hatua iliyolenga kuwapa faraja, matumaini na kuwahakikishia kuwa jamii bado inawajali.

Hafla hiyo ilihudhuriwa na Naibu Spika wa Baraza la Wawakilishi Zanzibar, Mgeni Hassan Juma, aliyekuwa mgeni rasmi. Akizungumza katika hafla hiyo aliipongeza TRA kwa hatua hiyo, akisema jamii inahitaji zaidi vitendo vya huruma na mshik**ano k**a hivyo.

Amesema maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani hayapaswi kuwa sherehe pekee, bali pia ni fursa ya kutafakari nafasi ya mwanamke katika jamii na namna ya kumuinua zaidi. Alisisitiza kuwa mwanamke ni uti wa mgongo wa familia na jamii, na pale anapothaminiwa na kupewa nafasi, maendeleo ya taifa huimarika.

11/03/2026

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ, Mhe. Idrissa Kitwana Mustafa amesema mafanikio ya siku 100 za kipindi cha pili cha uongozi wa Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi yamezingatia miongozo na mikakati mbalimbali ya maendeleo ya taifa.

Mhe. Kitwana amesema utekelezaji huo umejikita katika kuzingatia Zanzibar Development Vision 2050, Ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) ya mwaka 2025–2030, hotuba ya Rais ya ufunguzi wa Baraza la 11 la Wawakilishi Zanzibar (2025–2030), pamoja na Mpango wa Maendeleo wa Zanzibar (ZADEP).

Aidha amesema mafanikio hayo pia yanatokana na utekelezaji wa ahadi za Rais pamoja na mipango mikakati ya taasisi zilizo chini ya Ofisi ya Rais – Tawala za Mikoa, Serikali za Mitaa na Idara Maalum za SMZ.

Ameeleza kuwa ofisi hiyo imefanikiwa kushirikiana kwa karibu na vyombo vya ulinzi na usalama katika kudumisha amani, utulivu na mshik**ano wa Zanzibar pamoja na wananchi wake.





11/03/2026
11/03/2026

Katibu Mkuu wa Wizara ya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Ndg. Abeida Rashid Abdallah amefungua mafunzo kwa watendaji wa wizara hiyo pamoja na maafisa wa serikali kwa lengo la kujenga uwezo kuhusu masuala ya jinsia.

Mafunzo hayo yamefanyika katika Hoteli ya Maru Maru Hotel, Mkoa wa Mjini Magharibi, na yamewakutanisha watendaji mbalimbali wa serikali wanaohusika na utekelezaji wa sera na mipango ya maendeleo ya jamii.

Akizungumza katika ufunguzi wa mafunzo hayo, Ndg. Abeida amesema lengo la mafunzo hayo ni kuwajengea uwezo watendaji wa wizara na maafisa wa serikali ili waweze kuelewa vyema masuala ya jinsia na kuyazingatia katika utekelezaji wa majukumu yao ya kila siku.

Ameongeza kuwa uelewa sahihi wa masuala ya jinsia utasaidia kuimarisha usawa, haki na maendeleo ya jamii kwa ujumla.





10/03/2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amesema Zanzibar imeandika historia ya kipekee kwa kuandaa tukio kubwa la Futari ya Kitaifa kwa mara ya kwanza lililowakutanisha maelfu ya waumini wa dini ya Kiislamu.

Alhaji Dkt. Mwinyi ameyasema hayo Machi 7, 2026 alipotoa salamu zake kwa waumini wa dini ya Kiislamu waliohudhuria futari hiyo ya kitaifa iliyofanyika katika Uwanja wa New Amaan Complex, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Kwa upande wake, Naibu M***i wa Zanzibar, Sheikh Mahmud Kufutari M***a Wadi amesema tukio hilo la futari ya pamoja linaongeza mapenzi na upendo miongoni mwa waumini, huku likisaidia kuondoa chuki na kuimarisha umoja wa waumini wa makundi mbalimbali ya dini ya Kiislamu.

Naye Katibu Mtendaji wa Zanzibar Commission for Tourism, Ndg. Arif Abbas Manji amesema taasisi hiyo imetumia jukwaa la futari ya kitaifa k**a tukio muhimu la kuitangaza Zanzibar kimataifa katika juhudi za kuimarisha sekta ya utalii.





Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar,Mhe. Lela Muhamed M***a, amekutana na watendaji wa Kituo cha Walimu (TC) Du...
10/03/2026

Waziri wa Elimu na Mafunzo ya Amali Zanzibar,Mhe. Lela Muhamed M***a, amekutana na watendaji wa Kituo cha Walimu (TC) Dunga kujadili hatua za kuimarisha mageuzi ya elimu nchini

Amesema mageuzi ya elimu hayahusiani tu na ujenzi wa miundombinu au kuongeza walimu, bali yanahusisha pia kuimarisha taasisi zote zinazohusika na sekta hiyo

Akizungumza katika kituo hicho kilichopo Dunga, Mhe. Lela alisisitiza umuhimu wa vituo vya walimu kuwa sehemu ya taasisi za elimu ili kuongeza ufanisi katika utoaji wa mafunzo na utekelezaji wa majukumu yao.


***a

Taarifa zinasema kuwa beki wa kimataifa wa Argentina, Cristian Romero, anatarajiwa kuondoka katika klabu ya Tottenham Ho...
10/03/2026

Taarifa zinasema kuwa beki wa kimataifa wa Argentina, Cristian Romero, anatarajiwa kuondoka katika klabu ya Tottenham Hotspur mwishoni mwa msimu huu ,

Romero, ambaye ni mmoja wa mabeki muhimu wa Spurs, anaweza kuvutia vilabu vikubwa barani Ulaya vinavyotafuta kuimarisha safu yao ya ulinzi kabla ya kuanza kwa msimu mpya.




10/03/2026

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dkt. Hussein Ali Mwinyi amewasisitiza viongozi wakuu wa taasisi za umma kuzingatia upendo, uadilifu na haki katika kuwasimamia wanaowaongoza pamoja na utekelezaji wa majukumu yao.

Rais Dkt. Mwinyi ameyasema hayo leo Machi 8, 2026 katika Kongamano la Tatu la Kiimani kwa viongozi wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar lililoandaliwa na Office of the M***i of Zanzibar na kufanyika katika Ukumbi wa Sheikh Idrisa Abdulwakil uliopo Kikwajuni, Mkoa wa Mjini Magharibi.

Amesema kongamano hilo ni msingi muhimu wa kukumbushana umuhimu wa kuzingatia maadili katika utumishi wa umma pamoja na kuwa jukwaa la kujifunza namna ya kuleta uwiano wa kazi kwa kuzingatia misingi ya kiimani.

Aidha, Rais Mwinyi ameeleza kuwa kuzingatia misingi hiyo kutasaidia kuimarisha ufanisi katika utendaji wa taasisi za Serikali na kuchangia mafanikio makubwa katika utoaji wa huduma kwa wananchi.





Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuimarisha miundombinu ya uvuvi ili kukuza uvuvi wa bahari kuu na kuongeza ...
10/03/2026

Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar inaendelea kuimarisha miundombinu ya uvuvi ili kukuza uvuvi wa bahari kuu na kuongeza kiwango cha samaki wanaovuliwa nchini. Hayo yameelezwa na Waziri wa Uchumi wa Buluu na Uvuvi, Masoud Ali Mohamed, alipokuwa akizungumzia mafanikio ya siku 100 za uongozi wa Rais wa Zanzibar, Hussein Ali Mwinyi

Amesema Serikali ipo katika mchakato wa kununua meli moja kubwa ya uvuvi wa bahari kuu yenye urefu wa mita 25 pamoja na boti nne za uvuvi zenye urefu wa mita 18, sambamba na maandalizi ya ujenzi wa bandari ya uvuvi katika eneo la Ngalawa





Address

KIJANGWANI
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ASAM MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share