ASAM MEDIA

ASAM MEDIA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ASAM MEDIA, Media/News Company, KIJANGWANI, Zanzibar.

10/09/2025

Zanzibar: Mfumuko wa bei kwa bidhaa mbalimbali za chakula na zisizo za chakula umepungua katika mwezi wa Agosti 2025, ikilinganishwa na mwezi Julai mwaka huu.

#2025

10/09/2025

Afisa Habari wa Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Nishati na Maji Zanzibar (ZURA), Bi. Shara Chande Omar, amesema kuwa pamoja na kupungua kwa bei ya mafuta, matumizi ya nishati hiyo yameongezeka kuliko kawaida visiwani Zanzibar.

#2025

09/09/2025

Nyumba moja katika mtaa wa Mkele Juu imeteketea kwa moto hapo jana majira ya saa 8 mchana na kusababisha hasara kubwa kwa familia husika, baada ya mali mbalimbali ikiwemo vitanda na nguo kuteketezwa na moto huo.

#2025

09/09/2025

Harakati nyingi za Ofisini na Vyuo Vikuu zinahitaji Laptop kufanya kazi kiufanisi, lakini je 'Laptop' kwa Kiswahili fasaha huitwaje?

06/09/2025
05/09/2025

Ustadh Salim Juma Faki leo ametoa hotuba katika ibada ya Swala ya Ijumaa iliyofanyika katika Msikiti wa Raudhwa, Darajabovu, Wilaya ya Mjini Unguja.

Katika hotuba yake, Ustadh Salim amewakumbusha waumini na jamii kwa ujumla umuhimu wa kutunza amani, kudumisha uadilifu na kusimamia haki katika maisha ya kila siku.

Amesema amani ni nguzo ya maendeleo ya taifa, hivyo kila mmoja anapaswa kuwa mlinzi wa amani, huku haki na uadilifu vikipewa kipaumbele katika maisha ya kijamii na kitaifa.

05/09/2025

🏆⚔️ BAMMATA YAWASILI ZANZIBAR! 🏝️🎉
Mashindano ya Michezo ya Majeshi (BAMMATA) yanatarajiwa kufanyika visiwani Unguja, Zanzibar kuanzia 🗓️ 06 – 18 Septemba 2025.

🔹 Mashindano haya hufanyika kila mwaka katika mikoa mbalimbali ya Tanzania 🇹🇿.
🔹 Mwaka jana yalifanyika Morogoro, na mwaka huu Zanzibar imepewa heshima ya kuwa mwenyeji.
🔹 Lengo kuu ni kuimarisha mshikamano, nidhamu, ushirikiano na afya kwa wanajumuiya ya majeshi na jamii kwa ujumla 💪🤝.

🎥 Tazama taarifa kamili kupitia Asam Online TV 👉 https://youtu.be/zn-hHqVFy5A

⚽🏀🏐

04/09/2025

Mkurugenzi wa Asam Electrical Company Limited, Eng. Salum Haji Ali, amepongeza Chama cha TUCASA kwa kuandaa mafunzo ya kitaalamu yanayolenga kuwajengea uwezo wakandarasi na wadau katika kutekeleza majukumu yao kwa ufanisi.

#2025

04/09/2025

Bodi ya Usajili wa Wasanifu, Wahandisi na Wakadiriaji Majengo imeendesha mafunzo maalumu kwa wahandisi na wakadiriaji majengo, yakilenga kuongeza uelewa wa kitaaluma na masuala ya kimikataba katika utekelezaji wa majukumu yao.

#2025

04/09/2025

Mgombea Mwenza wa Urais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kupitia Chama cha ADA TADEA, Ali Makame Issa, amevitaka vyombo vinavyoshughulikia maadili ya vyama vya siasa ikiwemo Ofisi ya Msajili wa Vyama vya Siasa pamoja na vyombo vya ulinzi na usalama, kuchukua hatua dhidi ya wagombea wa urais wanaotoa kauli za uchochezi zinazoathiri amani na mshikamano wa kitaifa Visiwani Zanzibar.

#2025

04/09/2025

Leo tarehe 04 Septemba 2025, Rais Mwinyi amezindua rasmi Soko jipya la Wafanyabiashara Chuini, lililopo Wilaya ya Magharibi A, Mkoa wa Mjini Magharibi.

04/09/2025

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Makamu wa Pili wa Rais anayeshughulikia Sera, Uratibu na Baraza la Wawakilishi, Mhe. Hamza Hassan Juma, amewataka wagombea wa nafasi za udiwani, uwakilishi na ubunge pamoja na wafuasi wao, kuhakikisha wanaheshimu sheria na taratibu za usalama barabarani wakati wa kuelekea na kushiriki katika mikutano ya kampeni.

#2025

Address

KIJANGWANI
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ASAM MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share