
07/07/2025
Sulaiman Al Rajhi, mmoja wa mabilionea wakubwa wa zamani duniani kutoka Saudi Arabia, kwa hiari yake mwenyewe amebadilisha mkondo wa maisha yake sasa si bilionea tena, si kwa sababu ya hasara ya kibiashara, bali kwa uamuzi wa moyo wa kugawa utajiri wake karibu wote kwa ajili ya ustawi wa binadamu.
Akiwa na umri wa miaka 95, Al Rajhi aligawa takribani dola bilioni 16 za Kimarekani (zaidi ya TZS trilioni 41), mojawapo ya michango mikubwa kabisa kuwahi kufanywa na mtu mmoja katika historia ya dunia.
Al Rajhi alizaliwa katika familia maskini, alianza maisha k**a mpagazi na mjumbe wa barua, kisha akajijenga hadi kuwa bilionea. Lakini hakusahau alipokuja na hatimaye, aliamua kurudisha alichopata kwa jamii kabla hajafunga ukurasa wa maisha.