ASAM MEDIA

ASAM MEDIA Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from ASAM MEDIA, Media/News Company, KIJANGWANI, Zanzibar.

Sulaiman Al Rajhi, mmoja wa mabilionea wakubwa wa zamani duniani kutoka Saudi Arabia, kwa hiari yake mwenyewe amebadilis...
07/07/2025

Sulaiman Al Rajhi, mmoja wa mabilionea wakubwa wa zamani duniani kutoka Saudi Arabia, kwa hiari yake mwenyewe amebadilisha mkondo wa maisha yake sasa si bilionea tena, si kwa sababu ya hasara ya kibiashara, bali kwa uamuzi wa moyo wa kugawa utajiri wake karibu wote kwa ajili ya ustawi wa binadamu.

Akiwa na umri wa miaka 95, Al Rajhi aligawa takribani dola bilioni 16 za Kimarekani (zaidi ya TZS trilioni 41), mojawapo ya michango mikubwa kabisa kuwahi kufanywa na mtu mmoja katika historia ya dunia.

Al Rajhi alizaliwa katika familia maskini, alianza maisha k**a mpagazi na mjumbe wa barua, kisha akajijenga hadi kuwa bilionea. Lakini hakusahau alipokuja na hatimaye, aliamua kurudisha alichopata kwa jamii kabla hajafunga ukurasa wa maisha.

07/07/2025
Leo tarehe 7 Julai 2025, Uingereza imeadhimisha miaka 20 tangu kutokea kwa mashambulizi ya kigaidi ya Julai 7, 2005 jiji...
07/07/2025

Leo tarehe 7 Julai 2025, Uingereza imeadhimisha miaka 20 tangu kutokea kwa mashambulizi ya kigaidi ya Julai 7, 2005 jijini London, ambapo watu 52 walipoteza maisha na mamia wengine kujeruhiwa katika mashambulizi ya mabomu kwenye usafiri wa umma.

Mfalme Charles III ameongoza taifa hilo katika kuwakumbuka wahanga wa tukio hilo, akisisitiza mshik**ano na nguvu ya umoja wa kitaifa ulioshuhudiwa baada ya janga hilo.

Katika tukio la kumbukizi lililofanyika Hyde Park saa 2:50 asubuhi — muda kamili ambao bomu la kwanza lililipuka — Waziri Mkuu Keir Starmer na Meya wa London Sadiq Khan waliweka maua katika eneo la kumbukumbu, wakiungana na manusura, familia za waathirika, familia ya kifalme na wahudumu wa dharura.




**ano

Kwa masikitiko makubwa tunatangaza kifo cha Mzee Ally Samatta, baba mzazi wa mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania M...
06/07/2025

Kwa masikitiko makubwa tunatangaza kifo cha Mzee Ally Samatta, baba mzazi wa mshambuliaji wa timu ya taifa ya Tanzania Mbwana Ally Samatta, ambaye amefariki dunia alfajiri ya leo katika makazi yake yaliyopo Mbagala Kuu, jijini Dar es Salaam.

Mzee Ally Samatta alikuwa mchezaji wa zamani wa timu ya taifa, akiitumikia kwa heshima akiwa amevalia jezi namba 10 ishara ya kipaji, heshima na mchango wake mkubwa kwa soka la Tanzania.

Inna Lillahi wa inna ilayhi raji’un
Hakika tumetoka kwa Mwenyezi Mungu na kwake tutarejea.

06/07/2025

Kijana mmoja wa kikundi cha burudani maarufu cha Makachu amejeruhiwa vibaya baada ya kuanguka kutoka sehemu ya juu wakati wa maonesho ya kuruka katika eneo la Forodhani, Mjini Zanzibar.

#2025

04/07/2025

Msanii wa Bongo Fleva na mchekeshaji anayejihusisha pia na siasa, Baba Levo, amejibu kauli ya kiongozi wa chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, aliyesema kwamba sasa siasa imevamiwa na wachekeshaji.
Kupitia video iliyosambaa mitandaoni, Baba Levo amesema:
“Zitto Kabwe ni chawa mkubwa tu. Mimi siyo mchekeshaji wa kuvamia siasa, mimi ni raia mwenye haki ya kuchangia maendeleo ya nchi k**a wengine wote.”
Kauli hiyo imeibua mijadala mikali mtandaoni, huku baadhi ya wafuasi wake wakimuunga mkono, wakisema wasanii nao wana mchango katika jamii na siasa, huku wengine wakitaka nidhamu zaidi katika mazungumzo ya kisiasa.
Mpaka sasa, Zitto Kabwe hajaonyesha dalili za kujibu tena kauli hiyo ya Baba Levo.

#2025

03/07/2025

Katika na mkutano na waandishi wa habari kuhusu Tamasha la Kizimkazi la 10, Mwenyekiti wa tamasha hilo Ndg. Mahfoudh Said Omar, ameeleza kuwa tamasha hilo limesogezwa mbele kutokana na kutokamilika kwa baadhi ya miradi muhimu.

Miradi hiyo ni pamoja na uwanja wa michezo wa Suluhu Sports Academy, kiwanja cha kufurahisha watoto, matawi ya CCM, pamoja na mradi wa maji endelevu.

Ndg. Mahfoudh amesema kuwa bila ya miradi hiyo kukamilika, tamasha haliwezi kufanikisha malengo yaliyokusudiwa, hivyo limeghairishwa hadi tarehe mpya itakapotangazwa rasmi.

Amesisitiza kuwa maendeleo ya Kizimkazi yanakwenda sambamba na tamasha hilo, na bila miradi hiyo, “Kizimkazi haiwezi kunoga.”

#2025

02/07/2025

Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi, Dk. Hussein Ali Mwinyi, amefanya mabadiliko ya uongozi katika ngazi ya mikoa na wilaya kwa lengo la kuimarisha utendaji na kuongeza ufanisi katika utoaji wa huduma kwa wananchi.

02/07/2025

Ajali ya moto imetokea katika Hoteli ya White Beach Villa iliyopo Mtoni, Wilaya ya Magharibi A, Zanzibar, na kusababisha hasara kubwa katika mali za wageni na miundombinu ya hoteli hiyo.

#2025

02/07/2025

Kumekuwepo na picha mjongeo zinazozagaa mitandaoni zikidai kuwa baadhi ya wafanyabiashara katika eneo la soko la Darajani, Zanzibar, wamechukuliwa na kupigwa na maafisa kutoka Mamlaka ya Uhifadhi na Uendeshaji Mji Mkongwe. Tuhuma hizo zimezua mjadala mkubwa na taharuki miongoni mwa wananchi na watumiaji wa mitandao ya kijamii.

#2025

01/07/2025

Waziri wa Utalii na Mambo ya Kale, Mheshimiwa Mudrik Ramadhan Soroga, ametoa tamko rasmi kufuatia taarifa zilizosambaa mitandaoni kuhusu madai ya baadhi ya wafanyabiashara wa Mji Mkongwe kupigwa au kugombana na maafisa wa Mamlaka ya Uhifadhi na Uendeshaji wa Mji Mkongwe.

01/07/2025

Katika Mtaa wa Kwahani, Unguja, kuna Madrasa yenye historia kubwa kwa vijana na watoto Madrasa ya Shuwar. Ni madrasa ambayo kwa miaka kadhaa imekuwa nguzo ya kuwalea watoto katika maadili na elimu ya dini ya Kiislamu.

Address

KIJANGWANI
Zanzibar

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when ASAM MEDIA posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share