02/11/2021
Mgulani Primary School
Shule flani ya kiswahili iliyopo karibu na ushuani....imagine imezungukwa na Police Barracks, JKT Mgulani, JWTZ Twalipo, DUCE, Uhamiaji Kurasini, Railway na Bandari, Ukoo wa Rashid Matumla, TX Moshi William nk
Classmate mmoja kati ya wengi wanaoiwakilisha vyema ni Ramadhan Chombo ( Redondo)Achana na ..fundi flani wa mpira...unajua tuliyoiangalia Valencia kitambo tunaelewa maana halisi ya kuitwa Redondo, jina flani la kiungo kashata kwelikweli....yaani anaujua sana mpira halafu pia anaujua sana uhuni, so inategemea wewe unataka kumuona kwenye sura ipi....ni k**a tunakmuona Fei toto wa Sasa, kuna muda anaweza kuwa mhuni k**a Jonjo Shevley na kuna muda anajifanya Pirlo
Basi bwana pale Mgulani P/S chini ya Mwailafu na baadae Materu k**a Headmaster kulikuwa na Talent za kutosha kuanzia soka, ngoma, ngumi, basketball nk ...Leo kizazi kile kinasherehekea kumuona mmoja wa mafundi bora wa soka kuwahi kutokea akirejea timu ya Taifa.... Ramadhan Chombo
All the best mwana...kuitwa peke yake ni mafanikio tosha mzee wangu, kuhusu kucheza nafikiri mwalimu anabaki kuwa muamuzi wa mwisho kulingana na mfumo na aina ya mpinzani anayekutana nae...all the best Redondo