Asobola's Lattest LUV Updates

Asobola's Lattest LUV Updates Contact information, map and directions, contact form, opening hours, services, ratings, photos, videos and announcements from Asobola's Lattest LUV Updates, Publisher, 27 Ben kiwanuka Road, Kampala.

This page'z major intention of creation is to share,sort, &discuss matters concerning with love and relationship hop u'll cooperate 2 share fun & solve Poole's scandals

Baba alinisisitizia kuchukua likizo kazini nirudi nyumbani nikamuone. Na alitaka nikae huko mwezi mmoja. Nilikua na mamb...
06/05/2024

Baba alinisisitizia kuchukua likizo kazini nirudi nyumbani nikamuone. Na alitaka nikae huko mwezi mmoja. Nilikua na mambo mengi sana kazini na nikamwambia sitaweza kupumzika kazi mwezi mzima. Lakini aliniambia mwezi mmoja wa kung'ang'ania kazi naweza kuujutia maisha yangu yote.

Kwa namna alivyokua anaongea niliogopa. Baba yangu hakua mtu wa kudekadeka. Mara nyingi alijifanya 'mgumu' hata alipokua anaumia sana. Nilipomsikia anaongea vile nilijua nahitajika kwenda kumuona. Nikachukua likizo nikaenda.

Nilifika nyumbani nikamkuta yupo hoi kitandani. Kweli alikua anaumwa, alikua kaisha, alikua kakonda, afya imedhoofu na alikua hawezi hata kunyanyuka. Alikua mpole, anaongea taratibu na mnyonge sana. Kwa mtu aliyekua anamfahamu angemuonea huruma na hata kutoa machozi. Nilimuangalia kwa huruma lakini alilazimisha tabasamu, hakutaka kuonekana mnyonge.

Aliniambia "Wewe ndiye mtoto wangu wa kwanza. Una wadogo zako sita. Wa k**e wawili na wa kiume wanne. Kuna kitu nataka nikufundishe kabla sijafa ili uje kuwa baba bora kwa wanao na si kuwa k**a mimi"

Nilimuitikia nikidhani kuwa kuna kitu ataniambia, lakini mpaka likizo inaisha hakuniambia kitu chochote. Nilishangaa na kumuuliza mbona kaniahidi kuniambia kitu lakini hajaniambia na likizo inaisha natakiwa kurudi kazini?

Alitabasmau na kuniambia kuwa ameshaniambia. Nilifikiria sana nikijaribu kukumbuka k**a kuna kitu labda aliniambia nikakisahau lakini sikukumbuka. Nilifikiri sana sikukumbuka chochote. Nikamwambia Baba mbona sikumbuki chochote. Alitabasamu tena, huku akiongea kwa shida, kisha akaniuliza nimekaa pale siku ngapi? Niilimuambia siku 23. Akaniuliza tena wewe una shangazi wangapi? Nikamuambia wawili. Akaniuliza na Baba wadogo? nikamuambia watatu.

Akaniuliza tangu nikae hapo walishakuja mara ngapi? Nilimuambia Shangazi mmoja alikuja mara tatu, kuna mwingine kila baada ya siku mbili anakuja. Baba wadogo aliyekuja ni mmoja tu, naye alikuja mara moja kwani wote wapo mjini na familia zao.

Alitabasamu tena na kuniuliza vipi mama yako tangu uje hapa yeye kaja mara ngapi? Nilishanga ana nikadhani Baba ameanza kuchanganyikiwa.

Inaendelea Part 2..!

Address

27 Ben Kiwanuka Road
Kampala

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when Asobola's Lattest LUV Updates posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Share

Category