LENZI Kipindi cha LENZI KAMILI ni kipindi cha Habari kitakacho kupa mfululizo wa Habari na Matukio mbalimbali toka Afrika Mashariki na Kati

Chama tawala nchini Botswana – ambacho kimekuwa uongozini kwa takriban miongo sita kinajaribu tena kutafuta ujanja wa ku...
10/27/2024

Chama tawala nchini Botswana – ambacho kimekuwa uongozini kwa takriban miongo sita kinajaribu tena kutafuta ujanja wa kushinda uchaguzi mkuu wa Jumatano wiki hii kwa kutumia tamko ambalo limehusishwa kwa muda mrefu na makundi ya upinzani.

Kwenye manifesto yake, chama cha kidemokrasia cha Botswana (BDP) kinataka “mabadiliko.”

“Tufanye mabadiliko pamoja na tujenge ufanisi kwa wote,” Rais Mokgweetsi Masis – ambaye amekuwa uongozini nchini humo tangu 2018 – ameyaandika kwenye utangulizi wake.

Ni utambulizi ambao unahitaji mambo kufanyika tofauti – upinzani unasema kwamba chama cha Rais hakina uwezo wa kutimiza hilo.

Japo wachambuzi wanasema kwamba matokeo ya uchaguzi huo ni magumu kutabiri wakati huu, chama cha BDP kimeshinda viti vingi bungeni mara 11 kwenye uchaguzi mbali mbali tangu taifa hilo kunyakuwa uhuru wake 1966.

Chama hicho kimewasaidia wagombea kiti cha Urais kuingia madarakani kila mara huku wabunge wanapomchagua kiongozi wa taifa hilo.

BDP imepongezwa kwa hatua ilizochukuwa kubadilisha maisha na hali ya Uchumi wa raia katika taifa la Botswana ambalo ni masikini, na lenya hali duni ya miundombinu k**a barabara chache za lami na kubadili hali ambapo maisha ya raia wa kawaida nchini humo ni ya juu kuliko kwengine kote barani Afrika.

Mojawapo ya rasilimali ambazo taifa hilo imetumia kuboresha Uchumi wake ni uchimbaji wa madini ya GEMSTONE, taifa hilo likiwa lenye kuchimba viwango vikubwa vya madini hayo kote ulimwenguni.

Na japo mambo hayako sawa.

Botswana inakabiliwa na changamoto za kiuchumi – sababu kuu ya tamko la Masisi kufanyike mabadiliko.

Kati ya watu wanne wenye uwezo wa kufanya kazi nchini humo, zaidi ya mmoja hana ajira, huku idadi kubwa ya kundi hilo likiwa vijana. Haya ni kwa mujibu wa Benki ya dunia.

Mhadhiri wa masuala ya kisiasa katika chuo kikuu cha Botswana Zibani Maundeni, ameitaja hali hiyo k**a, ‘Uchumi wa watu wasiokuwa na ajira.’

‘Tunawatoa waliofuzu kwenye chuo kikuu kila mwaka na Uchumi wetu hautoi nafasi za kutosha za ajira kuwafaa wote,’ aliiambia kitengo cha BBC Africa Daily Podcast.

Aidha, mali iliyomo nchini Botswana haijasambazwa kwa usawa miongoni mwa raia wake milioni 2.3.

Mkilala tunaamka hahaha
02/04/2024

Mkilala tunaamka hahaha

Black man in US
02/04/2024

Black man in US

Loading....
02/02/2024

Loading....

02/02/2024
Tunajichanga tukifanikiwa tutasema neno wewe  Tulia tu Saa ya Mungu ikifika utapata haja ya moyo wako
12/22/2023

Tunajichanga tukifanikiwa tutasema neno wewe Tulia tu Saa ya Mungu ikifika utapata haja ya moyo wako

Happy Birthday
12/22/2023

Happy Birthday

K**a sipo kumbe nipo  we are together.
12/17/2023

K**a sipo kumbe nipo we are together.

Maestro Diara 1st Goal Keeper in Africa
12/15/2023

Maestro Diara 1st Goal Keeper in Africa

Bado dakika chache sana
10/17/2023

Bado dakika chache sana

Sometimes in Afghanistan
10/14/2023

Sometimes in Afghanistan

Address

Houston, TX

Alerts

Be the first to know and let us send you an email when LENZI posts news and promotions. Your email address will not be used for any other purpose, and you can unsubscribe at any time.

Contact The Business

Send a message to LENZI:

Share